adui mwingine huyu hapa!
#Unalipwa 600,000 Ukatwe kodi ya PAYE 18% ya
mshahara
600,000-108000= 492000
Ukatwe 18% mkopo wa boom
ulioupata chuo
492000-108,000=384,000
Kodi ya nyumba
384,000-100,000=284,000
NSSF wakate hapo
284,000-80,000=204,000
Bili ya umeme
204,000-20,000= 184,000
Dala dala kwenda kazini kurudi
home
800*30=24,000
184,000-24,000=160,000
Bili ya maji =10,000
160,000-10,000=150,000
Chakula mchana uwapo kazini
2000*30=60,000.
150,000-60,000= 90,000
Chakula cha usiku
2000*30=60,000
90,000-60,000=30,000
Chai 1000*30= 30,000
30,000-30,000=0
Hapo vocha ya 500*30=15,000
0-15,000= -15,000
Ulijisahau ukanywa soda
kwenye pita pita zako 600 -15,000-600=-15,600
Usivae
Ukivaa unakuza deni lako
Na hapo ni hesabu za mshahara
wa kima cha chini
kikiwa 600,000 Huna mke wala mtoto wala
tegemezi ya aina
yoyote
Kwa sasa mshahara kima cha
chini hakija fika
315,000 hali ikoje kwa watumishi wa serikalini kada
ya chini.
#Elimu bure itampunguzia masikini mzigo mkubwa #Bima za afya zitawapunguzia maskini mzigo
mkubwa
#kupunguza kodi na iwe katika level ya kimataifa
itampunguzia mfanya kazi
mzigo. #tafakari chukua hatua Usifanye makosa uchaguzi huu
leta mabadiliko
tumia kura yako.
.......halafu unakuta mjinga anashabikia ccm ....inakuwa ni akili zilizopigwa strock.....katika maisha uthubutu ni kitu cha mhimu sana!! mwaka huu tumedhamiria kuthubutu kubadili mfumo!!!!
Jamaa yangu usidanganyike mabadiliko kupitia CCM ni ndoto ya mchana kweupe.. mi mwenyewe mwana CCM lakini kura yangu ni kwa Lowasa... ikiwa CCM ilifutilia mbali maoni ya wananchi ktk katiba ni dhahiri kwamba CCM haitakuwa/haipo tayari kufanya mabadiliko yatakayoiumiza.
Maana ili ufanye mabadiliko ni lazima CCM iumie kwani CCM inauroho wa madaraka sana...na vigogo na watoto wao wachache wa CCM ndio wanaomiliki uchumi wa nchi na raslimali.
Usishangae jamaa yangu ni kwamba watanzania wameamua kwa dhati na kwa ujumla wao kuiadhibu CCM kutokana na mfumo wake wa kulindana na kuongeza maadui 2 zaidi Ufisadi na rushwa na kimsingi ukitazama kwa makini Lowassa kaachia ngazi za kiserikali toka 2007 miaka 8 takribani lakini ufisadi umeongezeka maradufu kumbe tatizo sio Lowassa ni mfumo CCM.