Mfiaukweli
JF-Expert Member
- Aug 30, 2018
- 5,636
- 8,774
Juzi Jumatano ilinyesha mvua iliyoambatana na upepo mkali sana ulisababisha miti na nguzo za umeme kuanguka katika maeneo kadhaa hapa Arusha. Moja ya maeneo hayo ni estate moja inayomilikiwa na moja ya mashirika ya umma.
Jana vijana fulani wakaanza kukata miti (ili kuitoa miti iliyoanguka na kuziba barabara na pia kujipatia kuni). Hakuna malipo yoyote waliyopewa au kutegemea kulipwa.
Vijana hao walikamatwa kwa amri ya estate manager. Kuna mwendesha bodaboda mmoja alimuuliza huyo estate manager: "hivi barabara zitakaa hivi hivi zikiwa zimefungwa na miti iliyoanguka hadi lini?"
Meneja akamjibu: "nimeombea fungu la kuwalipa watakaoikata na kuiondoa miti. Kuweni na subira wakati tunashughulikia hilo jambo."
Jana vijana fulani wakaanza kukata miti (ili kuitoa miti iliyoanguka na kuziba barabara na pia kujipatia kuni). Hakuna malipo yoyote waliyopewa au kutegemea kulipwa.
Vijana hao walikamatwa kwa amri ya estate manager. Kuna mwendesha bodaboda mmoja alimuuliza huyo estate manager: "hivi barabara zitakaa hivi hivi zikiwa zimefungwa na miti iliyoanguka hadi lini?"
Meneja akamjibu: "nimeombea fungu la kuwalipa watakaoikata na kuiondoa miti. Kuweni na subira wakati tunashughulikia hilo jambo."