Hawa ndio aina ya Makandarasi wetu

Hawa ndio aina ya Makandarasi wetu

miku

Senior Member
Joined
Oct 24, 2011
Posts
148
Reaction score
190
Mimi ni kati ya Watanzania waliokuwa wakitetea sana Wahandisi wazawa kupewa kazi mbalimbali nchini lakini baada ya kuona picha hizi nimesikitika sana!
attachment.php
 

Attachments

  • P1010596.JPG
    P1010596.JPG
    48.1 KB · Views: 4,707
  • P1010597.JPG
    P1010597.JPG
    76.2 KB · Views: 1,449
dah kazi ipo, hamna wakaguzi wa miradi, mkaguzi nae akikuta kosa au mapungufu ni hongo itatumika kufunika kombe.
 
Tatizo ni mawasiliano. Mjenzi wa barabara alijenga barabara yake akakuta Tanesco tayari ameshasimika nguzo pale. Ufumbuzi ni kuwa Tanesco ahamishe nguzo yake lakini wa kugharamia hiyo kazi ni mwenye barabara (sio mkandarasi). Sasa utakuta mwenye barabara hana kasma ya pesa ya kufanya hiyo kazi ya kuhamisha hiyo nguzo.

Kwa hiyo asilaumu mkandarasi mlaumu mwenye barabara kwa sababu alipokuwa akifanya upembuzi yakinifu alipaswa aione hiyo nguzo na aweke hela ya kuihamisha kwenye bajeti yake ya kuijenga bararbara hiyo. Hapo hakuna cha hongo wala rushwa ni upeo tu umepungua kwenye kuona mambo!
 
wakandarasi uchwala wasio na weledi, wanadhalilisha taaluma yao. Kazi kwa crb kuwafutia usajili
 
Na mji huo una mainjinia wa mji au tanroad na mipango mji wapo?. Isitoshe wameshakabidhiwa hiyo kazi kwa kufunguliwa na mkimbiza mwenge au waziri mkuu. Hivi ikitokea ajali hapo nani wa kulaumiwa? Tuwe serious wakati mwingine bwana tuache masihara na kodi za wananchi. Diwani wa eneo husika jiuzulu kwa msisitizo.
 
Halafu kesho utasikia rais au makamu wake anakuja kufanya uzinduzi wa barabara, wenye kuisifia kazi watasifia na kupiga makofi na vigelegele kadhalika mwenye kukata utepe atakata bila kuhoji usalama wa watumiaji wa hiyo barabara na hasa nyakati za usiku, hivi tujiulize je hapo kungekuwa na call box wangeizunguka kama walivyo fanya kwa nguzo? Haya mambo ya ubabaishaji yatakwisha lini?
 
Tatizo ni mawasiliano. Mjenzi wa barabara alijenga barabara yake akakuta Tanesco tayari ameshasimika nguzo pale. Ufumbuzi ni kuwa Tanesco ahamishe nguzo yake lakini wa kugharamia hiyo kazi ni mwenye barabara (sio mkandarasi). Sasa utakuta mwenye barabara hana kasma ya pesa ya kufanya hiyo kazi ya kuhamisha hiyo nguzo. Kwa hiyo asilaumu mkandarasi mlaumu mwenye barabara kwa sababu alipokuwa akifanya upembuzi yakinifu alipaswa aione hiyo nguzo na aweke hela ya kuihamisha kwenye bajeti yake ya kuijenga bararbara hiyo. Hapo hakuna cha hongo wala rushwa ni upeo tu umepungua kwenye kuona mambo!
Pamoja na maelezo yako lakini bado kuna mushkeli...Huoni ni hatari sana sana sana tena sana kwa hali ya namna hiyo? Busara zaidi ilibidi kutumika!
 
Mkuu naona kama hapo ni Mbeya au Iringa kutokana na miti ya Jacaranda.
Watu wengi huwa hawaelewi kuwa tatizo hapo ni Halmashauri zetu ambazo idara zao za Ujenzi huwa ni very poorly equiped and staffed.
Idara hizi zina wahandisi wachanga mno wasioweza kutayarisha kimipango utekelezaji wa miradi ya ujenzi.
Vile vile huwa hawana staff wa kutosha kutengeneza designs , BOQ(mahesabu ya gharama ya kazi), na hata wasimamizi wa kazi yenyewe huko site.

Sasa wanapakutana na kizungumkuti cha idara nyingine kama TANESCO au DAWASA hapo inakuwa kimbemne cha idara na wadau wenye uozo aawa katika miradi.

Na hii ni kwa sababu huwa fedha inayoitwa RELOCATION FUNDS huwa haipo, na mkandarasi kupewa site hivo hivi.

Hiyo picha uliyoonyesha ni cha mtoto, tembea uone madudu zaidi.
 
Na mji huo una mainjinia wa mji au tanroad na mipango mji wapo?. Isitoshe wameshakabidhiwa hiyo kazi kwa kufunguliwa na mkimbiza mwenge au waziri mkuu. Hivi ikitokea ajali hapo nani wa kulaumiwa? Tuwe serious wakati mwingine bwana tuache masihara na kodi za wananchi. Diwani wa eneo husika jiuzulu kwa msisitizo.

Sasa kodi hapo inahusikaje? Relocation ya services kama njia za umeme, simu au maji vinafanywa na wahusika kama Tanesco, ttcl etc hapo huenda Tanesco walitoa gharama kubwa na Client akashindwa. Mkandarasi au mhandisi hahusiki na uhamishaji wa miundo mbinu mingine zaidi ya ile inayomuhusu

Pia tujaribu kutofautisha kati ya mhandisi(Engineer) na mkandarasi(Contractor)
 
wakandarasi uchwala wasio na weledi, wanadhalilisha taaluma yao. Kazi kwa crb kuwafutia usajili


Na mji huo una mainjinia wa mji au tanroad na mipango mji wapo?. Isitoshe wameshakabidhiwa hiyo kazi kwa kufunguliwa na mkimbiza mwenge au waziri mkuu. Hivi ikitokea ajali hapo nani wa kulaumiwa? Tuwe serious wakati mwingine bwana tuache masihara na kodi za wananchi. Diwani wa eneo husika jiuzulu kwa msisitizo.
Swali limejijibu.
Mkandarasi huwa anajenga kitu alicho amriwa na mktaba kujenga.
Na kazi inakaguliwa kabla ya malipo.
Hicho unachokiona ni kile mlipaji , yaani Halmashauri, ndicho ilitaka kijengwe.
Mkandarasi ni punda ambaye atakwenda tu kule mwenye punda anataka aende.
 
Tatizo ni mawasiliano. Mjenzi wa barabara alijenga barabara yake akakuta Tanesco tayari ameshasimika nguzo pale. Ufumbuzi ni kuwa Tanesco ahamishe nguzo yake lakini wa kugharamia hiyo kazi ni mwenye barabara (sio mkandarasi). Sasa utakuta mwenye barabara hana kasma ya pesa ya kufanya hiyo kazi ya kuhamisha hiyo nguzo. Kwa hiyo asilaumu mkandarasi mlaumu mwenye barabara kwa sababu alipokuwa akifanya upembuzi yakinifu alipaswa aione hiyo nguzo na aweke hela ya kuihamisha kwenye bajeti yake ya kuijenga bararbara hiyo. Hapo hakuna cha hongo wala rushwa ni upeo tu umepungua kwenye kuona mambo!

hivi unajua kwanini upanuzi wa barabara ya ali hassan mwinyi kutoka morocco hadi mwenge unachelewa???!!! ni kwasababu tanesco na dawasco wanachelewa kuhamisha nguzo na mabomba....sasa KONOIKE wangekuwa na akili kama huyo mkandarasi unaemtetea sasa hivi tungeona hicho kituko zaidi ya mara 20 kutoka mwenge mpaka morocco. KONOIKE wanajua kazi yao ndio maana hawaanzi ujenzi hadi maandalizi yatimie. huyo mkandarasi unaemtetea alikuwa ana haki zote kuto kujenga na kusema nguzo ziondolewe kwani ni hatari sio kwake tu ila kwa kila mtu.
 
Tatizo ni mawasiliano. Mjenzi wa barabara alijenga barabara yake akakuta Tanesco tayari ameshasimika nguzo pale. Ufumbuzi ni kuwa Tanesco ahamishe nguzo yake lakini wa kugharamia hiyo kazi ni mwenye barabara (sio mkandarasi). Sasa utakuta mwenye barabara hana kasma ya pesa ya kufanya hiyo kazi ya kuhamisha hiyo nguzo. Kwa hiyo asilaumu mkandarasi mlaumu mwenye barabara kwa sababu alipokuwa akifanya upembuzi yakinifu alipaswa aione hiyo nguzo na aweke hela ya kuihamisha kwenye bajeti yake ya kuijenga bararbara hiyo. Hapo hakuna cha hongo wala rushwa ni upeo tu umepungua kwenye kuona mambo!
Nope.

Miji yote ina ramani na wapanga Miji wanaelewa hilo. Hivyo, Tanesco kabla ya kuweka hizo Nguzo walitakiwa waende kwenye wizara husika na kupata Ramani kamili ya wapi kuna Barabara, wapi ni njia za maji taka nk.

Hivyo, kuwatetea Tanesco kuwa hawakujua ndio kosa lenyewe, maana kama wangetaka kujua wapi kuna Barabara na wapi kuna njia ya maji taka nk, wangefanya hivyo.

Kosa ni Tanesco na Wapanga miji kuachia Tanesco wafanya huo utovu wa nidhamu.
 
Swali limejijibu.
Mkandarasi huwa anajenga kitu alicho amriwa na mktaba kujenga.
Na kazi inakaguliwa kabla ya malipo.
Hicho unachokiona ni kile mlipaji , yaani Halmashauri, ndicho ilitaka kijengwe.
Mkandarasi ni punda ambaye atakwenda tu kule mwenye punda anataka aende.

kwahio kwenye mkataba ameambiwa weka lami hata ukikuta nguzo katikati??!!
 
hivi unajua kwanini upanuzi wa barabara ya ali hassan mwinyi kutoka morocco hadi mwenge unachelewa???!!! ni kwasababu tanesco na dawasco wanachelewa kuhamisha nguzo na mabomba....sasa KONOIKE wangekuwa na akili kama huyo mkandarasi unaemtetea sasa hivi tungeona hicho kituko zaidi ya mara 20 kutoka mwenge mpaka morocco. KONOIKE wanajua kazi yao ndio maana hawaanzi ujenzi hadi maandalizi yatimie. huyo mkandarasi unaemtetea alikuwa ana haki zote kuto kujenga na kusema nguzo ziondolewe kwani ni hatari sio kwake tu ila kwa kila mtu.

Mkuu RRONDO kuna kitu kinaitwa compensation maana mkandarasi yupo site hajakabidhiwa site 100% hapo hao konoike wanahesabu gharama tu mwisho wa siku utakuta gharama halisi ya kazi ni say, 10b lakini mkandarasi kalipwa 16b hiyo 6b ni hasara yetu walipa kodi
 
Last edited by a moderator:
Mkuu RRONDO kuna kitu kinaitwa compensation maana mkandarasi yupo site hajakabidhiwa site 100% hapo hao konoike wanahesabu gharama tu mwisho wa siku utakuta gharama halisi ya kazi ni say, 10b lakini mkandarasi kalipwa 16b hiyo 6b ni hasara yetu walipa kodi

exactly...sasa mkandarasi anaejua kazi yake atafika site na kusema haijawa tayari kuanza kazi kwasababu 1,2,3 mpaka zikamilike ndio anaanza kazi na sio huyu anaejenga barabara wakati nguzo ipo ndani ya barabara.
 
kwahio kwenye mkataba ameambiwa weka lami hata ukikuta nguzo katikati??!!

Mkuu kama unaijua mikataba basi unafanya kile kitu tu ulichoelekezwa.
Na mkandarasi ana lipwa tu kile kilichomo kwenye mkataba.
Hata hivyo hapa naona mtoa kazi na mlipiaji wa kazi yenyewe amesepa gharama za kuhamisha nguzo.
 
Back
Top Bottom