Hawa funza wametoka wapi?

Hawa funza wametoka wapi?

Maiti aliyefukiwa asipoguswa na nzi hatatoa funza nijuzeni

Iron Lady,jibu ni ndio maiti atakayefukiwa na kukingwa kabisa na inzi wasiweze kutaga mayai juu yake basi haitatoa funza(maggots).Si maiti tu hata kwa chakula ama nyama inayooza ikiwa protected vema kutokana na flies haitozalisha funza kamwe.
 
Mkuu hii sayansi naikumbuka kwa mbali.... labda tu kuwa pamoja... ina maana wale funza wa chooni kama vyoo vya shuleni baadae (saint Kanumba) wanageuka kuwa nzi wakifika stage ya 4?

Mkuu kuna species mbalimbali za flies wanaoishi na kutaga mayai mazingira tofauti tofauti,funza wa vyooni hutokana na aina mbili za flies ambao ni housefly(Musa domestica) na Blowfly,hawa upenda kutaga mayai sehemu zenye uozo(wa mimea na wanyama)na kwenye vinyesi,mayai yatabadilika kuwa maggots(larva stage) ambao ndio funza na kama watapata nutrients wakikamilisha stage zilizobaki uwa inzi ingawa si funza wote wa chooni hubadilika kuwa inzi kuna baadhi hufa.
 
Iron Lady,jibu ni ndio maiti atakayefukiwa na kukingwa kabisa na inzi wasiweze kutaga mayai juu yake basi haitatoa funza(maggots).Si maiti tu hata kwa chakula ama nyama inayooza ikiwa protected vema kutokana na flies haitozalisha funza kamwe.
maembe . unakuta umenunua embe unaona nje zuri ndani ukikata lina funza sasa huyu nzi katua saa ngapi ndani ya embe nijuzeni na hapa.
 
maembe . unakuta umenunua embe unaona nje zuri ndani ukikata lina funza sasa huyu nzi katua saa ngapi ndani ya embe nijuzeni na hapa.

Iron lady, hao ni inzi wa embe kitaalamu huitwa Bactrocera dorsalis hufanana sana na manyigu na wana alama ya T mgongoni wanazishambulia embe kwa kuzimeng'enya zikiwa katika hatua za mwanzo za ukuaji na kuingia ndani yake wanapoingia ndani inzi hawa hutaga mayai mengi sana ambayo yatabadilika na kuwa funza,funza hawa mara nyingi hula nyama za ndani za embe na kupelekea embe kuharibika ama kuoza kabisa,na hata kama embe itafanikiwa kuiva na kuonekana nzuri kwa nje bado ndani yake si nzuri kutokana na uwepo wa hao funza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom