Hausigali ana masharti wajameni!!!

Hausigali ana masharti wajameni!!!

Kama hana matatizo kwa mkeo na watoto wanapata malezi hana shida. Kuhusu mbwa na watoto, binafsi siafiki watoto kuzoena na mbwa hasa kutokana na aina ya mbwa na malezi yake ya kibongobongo.......Ushauri wangu usitumie mazingira ya nje kumhukumu huyu HG kwani nae anatafuta riziki ya kupambana na ugumu wa maisha. Hili la Kitifire nalo halina mshiko kwani ukiwa na midadi unaweza kwenda kujipatia kwenye centers fulani fulani. Note that ni kazi ngumu kupata perfect HG, huyu anaweza kuwa afadhali kwa ajaye.
Acha kutetea ujinga hapa.
Nyumba ni yake na bado awekewe masharti!!!
Hili halikubaliki kabisa. House girl hana mamlaka ya kubadili mfumo wa maisha ya nyumbani kwake kwa amri.
Jamaa kasema;
1/Anapenda kula kitimoto nyumbani kwake na familia yake tena kikiwa kumeandaliwa na house girl wake.

2/Anapenda mbwa na anapenda watoto wake wafurahi kucheza na mbwa wake.

3/Anapenda kurudi nyumbani usiku sana na atataka house girl awajibike kumfungulia nyumba na kumpokea.

4/Jamaa hakubali mfumo wa ibada wa swala tano nyumbani kwake.

*Ni jukumu la House girl kukubali mfumo huo wa maisha ya huyo jamaa, na kama hawezi asepe zake.
 
Ukiendelea na umburula wa kuendelea kukaa na huyo housegirl, usishangae kesho huyo housegirl anakupa masharti mengine kama haya

1/Usilale tena na mke wako
maana wewe ni Kafir.

2/Hawezi tena kuwapikia chakula kwa kuwa yupo kwenye mfungo wa mwezi mtuku.....
 
Hivi unapoajiriwa na kukubaliana na bosi wako unampa masharti???

Kwa nini nyumba yako igeuke jela? Mrudishe tafuta mwengine
 
chunguza mke, chunguza wakwe, chukua hatua mara moja; na hatua yenyewe ni moja tu..., kufukuza tu watoto kama hawajafikia kwenda shule peleka day care zipo zinazotoa huduma kwa watu wasio na walezi wa kuwaachia watoto nyumbani...

Ukichelewa kuchukua hatua utakuja hapa hapa na habari nyingine tena ya ajabu kumhusu huyo housegirl wako
 
Huyu jamaa asije akawa alipewa "SHEMEJI" amsaidie, sasa anatafuta gia ya kumtimua!
sijapata conection kati ya House Gal, Wakwe na Hofu ya huyu "NdegeMtu"!
...Hebu afunguke vizuri!
NB. Mbwa wa siku hizi siyo wa kuachwa na watoto..utakuta wamewapelekea yale mambo..hasa hawa wanaonyimwa uhuru wa kujitafutia malavidavi..nafuu wangekuwa koko.:nod:
 
Mbwa hawana shida. Mmoja tulikuwa naye toka watoto wote hawajazaliwa. Tatizo langu ni housegal, yupo yapata wiki ya pili sasa. Ni mtu mzima kunishinda, so nahisi mwanzoni alipoletwa alihisi kazi yake nyingine ni kulea baba na mama mwenye nyumba. Kabla yake nilishatimua watatu, wawili wakiwa toka huko huko ukweni. Niliwakilisha hapa ili nipate mchango wa wana jamii. Ushauri sasa: Usithubutu katu, kukubali hata kwa bure, msichana wa kazi mhaya. Mke ama mme,hiyo ni topic tofauti kabisa, ila not hausegal.
 
unakoelekea atakukalisha chini na mkeo akuambie maneo haya
1.''hawa watoto wamefuatana sana sasa mtoto mwingine nisimuona humu ndani hadi MAY 2017"
2.''nimechoka kumona mke anakuita babe maana hilo ni katazo kwa imani yangu''
3.la tatu nitamalizia kesho mmesikia?
 
sometimes ukauzu muhimu mkuu..ukiwa fair kila kitu matokea yake ndo hayo. mimi kama mimi case km hiyo may be in her dreams!!!!!!!!!!!
 
Acha kutetea ujinga hapa.
Nyumba ni yake na bado awekewe masharti!!!
Hili halikubaliki kabisa. House girl hana mamlaka ya kubadili mfumo wa maisha ya nyumbani kwake kwa amri.
Jamaa kasema;
1/Anapenda kula kitimoto nyumbani kwake na familia yake tena kikiwa kumeandaliwa na house girl wake.

2/Anapenda mbwa na anapenda watoto wake wafurahi kucheza na mbwa wake.

3/Anapenda kurudi nyumbani usiku sana na atataka house girl awajibike kumfungulia nyumba na kumpokea.

4/Jamaa hakubali mfumo wa ibada wa swala tano nyumbani kwake.

*Ni jukumu la House girl kukubali mfumo huo wa maisha ya huyo jamaa, na kama hawezi asepe zake.
Note "Mjinga akierevuka ........ yupo mashakani" umeniambia natetea ujinga atieeeeeeeeeeeee
Back to mada....unafikiri huyu jamaa siyo mjingaaaaaa, kama alikuwa na udini kiasi hiki mbona hakuweka vigezo katika HG anayemtaka? Wenzie wenye akili wanawaagiza watafutaji wazingatie dini, kabila, rangi, umbo, umri, uzuri, elimu, etc ndipo wanafanikiwa kupata wa aina yao. Sasa basi jaribu nawe umshauri huyu.
 
Nimeipenda hii, nilikuwa sijacheka leo, ahsante smile kwa kunichekesha

tena muondoshe na mkongoto wa nguvu...nyambafuuu...aiseee kuna wasichana pasua kichwa
 
hapo hakuna cha beki tatu wala mama mwenye nyumba
wote ni matatizo
simama kama baba mwenye nyumba lakini.
 
Haswaaaa, hapo hapo Singida type, wanakerajee!!! Pia kuna ushirikina ndani yao, usipokuwa makini ataivuruga nyumba na familia yako nzima.
Nilikaa nae wiki moja masharti yakanishinda, nikatimua.

ha ha naimani keshaanza madogoli mpaka kidume kinakuja humu kinalia lia ujue dawa zishaanza we Birdman we endeleakuja kulia lia kule dawa zinazidi kupulizwa
 
Last edited by a moderator:
ni h/girl au mkeo wa pili!,, ni mkeo bwanaa acha kutuzugaa!
 
hapana lazima atakua mhaya

umepatia best ahaaa ila kweli jeuri misifa iko kwenye damu hawa watu.
Kuna mmoja alikuwa anafanya kwa sister khaaaa eti naenda kutembea ananipangia job nikamwambia wewe kichaa kweli nimekuja kupumzika huku baada ya misukosuko unanipangia kazi??
Tena usinizoee nitakukung'uta sasa hivi nitafanya napojisikia na ninapoweza afuuu dizaini kama sister anamtetemekea ha ha ha madogoli hapa au?
 
Huyu jamaa anatu enjoy.tangu lini mfanyakazi awe na amri kwa bosi wake.
ukiona mtu kabanwa na housegirl ujue kaishagegeda.
Asimsingizie eti kaletwa na mama mkwe.
Baba mwenye nyumba ukishajishusha kwa binti wa kazi ni bora u-handle over madaraka kwa mkeo, na wewe usubiri kuongozwa tu.
na usipoangalia, kuna siku wife atakuta dada kakaa sebuleni anaangalia TV, wewe ndiyo uko jikoni unapika.
 
Back
Top Bottom