Hatuachani na China! Ruto aijibu Marekani

Hatuachani na China! Ruto aijibu Marekani

The Zanzibar Echo

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2025
Posts
490
Reaction score
836
Rais wa Kenya, William Ruto, amejibu hatua ya Marekani ya kutaka kupitia tena hadhi ya nchi yake ya mshirika mkuu asiye mwanachama wa NATO, akisema kuwa machaguo yake ya sera za masuala ya mambo ya nje yanazingatia kile ambacho kinafaa zaidi kwa Kenya.

Akizungumza na sekta za kibinafsi, Ruto alitetea ukuaji wa kibiashara na nchi kama China, akisema kuwa lengo la utawala wake ni kunufaisha wazalishaji wa Kenya na kurekebisha kile ambacho hakijakuwa sawa kwa muda mrefu.

Rais Ruto alikiri kuwa baadhi ya washirika wake wanahoji ukuaji wa kibiashara kati ya Kenya na China, lakini akasisitiza kuwa maamuzi ya hatua hizo yanashinikizwa na mahitaji ya Kenya kiuchumi.

“Baadhi ya marafiki zetu wanalalamika kwamba tunafanya biashara nyingi na China. Wakati nilikutana na Rais Xi Jinping, nilimwambia Kenya inaingiza bidhaa za Sh600 bilioni kutoka China, lakini tunasafirisha tu labda 5%. Usawa huo wa kibiashara ni mbaya,” Ruto alisema.

Ruto aliongeza kuwa China imekubali kufungua soko lake kwa bidhaa za kilimo za Kenya.

“Wamekubali kufanya mabadiliko ya usawa wa kibiashara kati ya Kenya na China. Wamekubali kuondoa ushuru wote kwa chai yetu, kahawa, parachichi, na bidhaa zote za kilimo tunazouza nje ya nchi.

Tunaendeleza mazungumzo na India. Tuna uhusiano mzuri na Uturuki na Canada,” Ruto alisema.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge juu ya Masuala ya Ulinzi nchini Kenya, Nelson Koech, amemwandikia mwenzake, Seneta wa Marekani, Jim Risch, akisema:

“...Namuomba mwenzangu wa Marekani, Seneta Jim Risch, Mwenyekiti wa Masuala ya Mambo ya Nje, kufikiria upya mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Uidhinishaji wa Kitaifa wa Ulinzi (NDAA) ya Mwaka 2026 kwa maslahi bora ya mataifa yetu mawili ya kirafiki.

Mapitio yaliyopendekezwa na Seneta Risch, ikiwa yataidhinishwa, yatajumuisha tathmini ya sera za kigeni na za kidiplomasia za Kenya, kama vile kujifungamanisha na Marekani na ushirikiano wake na China, Urusi, na Iran, pamoja na makubaliano yanayowezekana ya Kenya, uhusiano wa kisiasa au kifedha na wanamgambo wenye silaha kama vile al-Shabaab na Rapid Support Forces (RSF), na mengineyo.”
 
Kenya wiki hii wamepokea M1117 armoured personnel carriers kadhaa kutoka Marekani, mwaka jana wameahidiwa idadi jumla 150.

Hivi karibuni pia walipokea light attack helicopter moja kutoka US, watapata mbili. Vilevile wamenunua MRAPs kutoka Afrika Kusini.

Marekani wanatoa msaada wa kijeshi kujishikanisha na Kenya, kitu ambacho sikipendi hasa ukiweka akilini ofisi za UN zinazohamia Nairobi. Ukizingatia uwepo wa majeshi ya US na UK hapo Kenya basi nchi inatumika kwa maslahi ya Western.
 
Kenya wiki hii wamepokea M1117 armoured personnel carriers kadhaa kutoka Marekani, mwaka jana wameahidiwa idadi jumla 150.

Hivi karibuni pia walipokea light attack helicopter moja kutoka US, watapata mbili. Vilevile wamenunua MRAPs kutoka Afrika Kusini.

Marekani wanatoa msaada wa kijeshi kujishikanisha na Kenya, kitu ambacho sikipendi hasa ukiweka akilini ofisi za UN zinazohamia Nairobi. Ukizingatia uwepo wa majeshi ya US na UK hapo Kenya basi nchi inatumika kwa maslahi ya Western.
Kwani wameanza leo?😁
Si support Ruto lakini Kwa hili swalha, aendelee kushikilia papo hapo hadi kieleweke. Tukiendeleza hivyo ipo siku tutakuja kua na nguvu za kidiplomasia kiasi cha kwamba tutakua tunaeza kufanya uhusiano na yeyote iwe east au west bila kutishiwa au kupewa onyo na yeyote...



------

Iran, Kenya set $1 billion annual trade target: agri. min​

Iran, Kenya set $1 billion annual trade target: agri. min

TEHRAN, Aug. 13 (MNA) – Iranian minister of agriculture says that Tehran and Nairobi have set for the annual $1 billion trade target.
Gholamreza Nouri Ghezeljeh made the remarks at the 7th Session of the Kenya-Iran Joint Commission for Cooperation, held in Nairobi, emphasizing the strategic geographical situation of the Republic of Kenya in eastern Africa.
The economic capacities of this African country have prepared a suitable ground for the development of trade-economic relations between the two countries, Ghezeljeh stated.
Iran’s agriculture minister has described Kenya as the country’s gateway to East Africa, stressing that the two nations should boost their currently “unsatisfactory” level of trade.
He expressed hope that, by tapping into both countries’ industrial, agricultural, and logistical capacities, bilateral trade could rise to several billion dollars.
The minister underlined Iran’s readiness to swiftly remove trade barriers, and encouraged Kenyan partners to address banking and barter trade issues to facilitate business.
Iranian delegation includes major companies in pharmaceuticals, industry, agriculture, and technology, reflecting Kenya’s importance in Iran’s Africa strategy, the agriculture minister added.
The current value of trade between the two countries stands at over $300 million, but it is expected to exceed $1 billion in the near future if obstacles are resolved.
The minister and his accompanying delegation are in Nairobi to attend the two-day Joint Economic Cooperation Commission meeting that kicked off on Tuesday.
 
Asijelia tu mbele ya safari...
Yes, marekani sio nchi ya kukosewa bila mpango. Ruto asiwe kama wengine. Anyamaze na kufanya mambo kimya kimya, vile alivyofanya alipoenda China ilikua anajitafitia shida tupu. Aliambia Xi eti China ndo, "New World Order". Hilo tamko ndo limekasirisha marekani, manake hata hao marekani wanahofia China ndo itakua kiongozi wa Dunia huko mbeleni. Sasa nchi ndogo kama Kenya ikianza ku confirm mapema hivi, hio ni tishio Kwa marekani.
 
Yes, marekani sio nchi ya kukosewa bila mpango. Ruto asiwe kama wengine. Anyamaze na kufanya mambo kimya kimya, vile alivyofanya alipoenda China ilikua anajitafitia shida tupu. Aliambia Xi eti China ndo, "New World Order". Hilo tamko ndo limekasirisha marekani, manake hata hao marekani wanahofia China ndo itakua kiongozi wa Dunia huko mbeleni. Sasa nchi ndogo kama Kenya ikianza ku confirm mapema hivi, hio ni tishio Kwa marekani.

Gachagua aliyemtosa Uvice yupo Marekani miezi sasa hajui anapika mangapi kule so akili kichwani kwake!
 
Back
Top Bottom