Hatimaye Subhash Patel amvaa Reginald Mengi

Kama hao Papa wanakupandisha hasira je Nyangumi?
 
Ni vyema kama wanajivalisha kitanzi taratibu, tutafika tu!
 

10 Billion?

Sisi Watanzania tunataka fidia ya hela zote za EPA!

Subhash naye apewe siku saba...arudishe hela zetu!
 
 
No no no no no hapana huyu bwana hajapata kuwa mweka hazina wa mtandao hata siku moja ila ni rafiki mkubwa wa tangu utotoni wa muungwana.

Ni kweli huyu ni rafiki yake toka utotoni, actually huyu Subashi ndiye aliyekodishiwa kwa mkataba wenye Utata jengo la UVCCM Makao makuu pale Lumumba na Kampuni yake ya Ujenzi inayoitwa ESTEEM ndiyo inajenga jengo hilo la vijana, jengo la iliyokuwa Gogo hotel, Upanuzi wa barabara ya Ali Hassan Mwinyi kwenda Tegeta na wanajenga nyumba za mwenyekiti hapo migombani street na Kijiji cha Muungwana katika vijilima vya Msoga.

Wakati wa mtandao alichangia kiasi kikubwa cha fedha lakini hakuwa mweka hazina.. mweka hazina alikuwa Rostam na msaidizi alikuwa Karamagi(what a team). Vifaa vyote vya kampeni ya CCM vinakaa kwenye magodowns ya Subash pale Mwenge MM STEEL na taarifa za karibuni wameshaleta kofia na T shirt kwa ajili ya 2010 na vyote viko pale.
 
Huyu ni mtu wa muungwana na alishaahidiwa kuwa atapewa mchuchuma na ndio maana kila Mkuu wa Mkoa anayepelekwa Iringa tangu muungwana aingie madarakani lazima awe mtu wa karibu kulinda maslahi ya JK[ Except mama Kasungu ambaye ilibidi wamuondoe] Kunzia Jaka Mwambi, Amina Said na sasa amempeleka afisa wa usalama wa Taifa kutoka Tanga. Kuna umuhimu kwa wananchi kumsaidia Mengi katika vita hii dhidi ya hawa mafisadi papa ama sivyo mali zetu zote zitakombwa.
 
Last edited:
Kama ni hivyo basi ni aibu kubwa sana kwa `mwenyenchi! Kuwa rafiki na fisadi ni kuwa fisadi! Hivi kweli itawezekana kuwashughulikia hawa jamaa kama mwenye hatamu ni mtu wao? Wadau nisaidieni...!
 
Jamani mchuchuma dingi yangu alifukuzia sana dili lile na ni mzalendo mweusi nashangaa dili limedondokea kwa huyu Gabacholi mtume tumekwisha.
 
Like the son like the father! Yule kachukua Kiwira huyu ataondoka na Mchuchuma!!
Watanzania, it is too much; hivi hamna watu wakawaonyesha mfano watu kama hawa? Kiburi yao ni kubwa sana; wanajua tutasema halafu tutalala; sheria zetu wala hazina maana! What next?
 

Umegusa penyewe!
Kuna watu humu nadhani hawamjui subash...urafiki wake na JK ni kimaslahi... just like urafiki wake na officials TRA, NSSF, PPF, defence, ministry of finance, tourism, BOT na kadhalika.. uliza wangapi walikuwa karibu yake enzi za Mwinyi na Mkapa.. saizi hawako serikalini kawatema...

Kila mzee serikalini akiulizwa uhusiano wake na hawa wahindi jibu walisoma wote au wametokea kijiji kimoja.. na mitoto yao inakubali ...hahahahahaha
 
Hii series inabidi tuipe jina kwani michezo inaendelea tunapiga kelele zinaishia hewani wao hawaguswi na sisi pesa zetu zinazidi kupotelea kwenye accounts zao huko mbele, think of the name of the series............ Tanzania and the fiadis' na hii ni season 1 episode 8. Tulianza na richmond, Kiwira, Kagoda, Mramba and Yona, EPA, Liyumba and now Mengi and them.

Lakini mpaka kieleweke, waende mahakamani ili ukweli upatikane
 
Inasikitisha na kuuma sana, kwamba tunashindwa umakini na nchi ndogo kama Malawi ambao wameamua kuweka kipaumbele kwenye uchimbaji wa uranium badala ya makaa ya mawe kutokana na mabadiliko ya haraka ya teknolojia.

Lakini kikubwa ni kwamba kabla ya kuanza uchimbaji wa madini hayo waliomba ushauri benki ya dunia, jumuiya ya madola na International Atom Agency. Sisi tunafanya maamuzi yetu kwa utashi wa mtu aliyepo pale magogoni kwa wakati huo, matokeo yake ndito hayo ya miradi mikubwa kama huo wa Mchuchuma na Liganga kupewa mtu asiye na teknolojia ya kuuendeleza.

Watanzania tuamke kulinda rasilimali zetu kwa nguvu zetu zote, Malawi walifanya hivyo na ni pale matakwa ya NGOs yalipokubaliwa ndipo mradi wa uchimbaji uranium ulipoanza. Wenzetu walisimama kidete kuona madini hayo yanawanufaisha wamalawi, sisi ni kulalamika tu huku watawala wakiendelea na unyang'au wao.
 

Nakubaliana na wewe sisi wakati baba (hakuwa serikalini) yetu yupo hai, wahindi walikuwa wakituona tu zawadi haziishi .....
kabla hajafa alipata stroke kwa hiyo alikuwa nyumbani kwa muda mrefu karibu miaka mitano nakwambia wale wahindi walikua hawaji nyumbani hata siku moja hata kumuangalia.....
Ukikutana nao hata ukiwaamkia hawajibu shikamoo yako.....
 
Subhash Patel nadhani si sahihi awe kwenye chungu cha mapapa. Namfahamu huyu bwana kwa miaka mingi kama mhangaikaji/mjasiriamali asiyecheza faulo.

Kasome ripoti ya Kamati ya bUNGE ILIYOWASILISHWA MWAKA 1992 YA aYILA UTAJUA HUYU NI NANI AKIWA NA cHAVDA.
 
.Anawataka waombe radhi ndani ya siku saba na wamlipe fidia ya shs bilioni kumi

- Yaaani fisadi papa aombwe radhi na wananchi kwa kuwa na ushahidi wa ufisadi wake? Hawawezi kweli wana kiburi sana hawa, hivi wanakitoa wapi hiki kiburi?

FMES!
 
- Yaaani fisadi papa aombwe radhi na wananchi kwa kuwa na ushaidi wa ufisadi wake? Hawa wezi kweli wana kiburi sana hawa, hivi wanakitoa wapi hiki kiburi?

FMES!

Kiburi ni kuwa wanajua inawezekana kuwahonga baadhi ya majaji wa hapa Tanzania, HIVYO WANAAMINI HAKUNA KILICHO ZAIDI YA PESA.
 
Kiburi ni kuwa wanajua inawezekana kuwahonga baadhi ya majaji wa hapa Tz, HIVYO WANAAMINI HAKUNA KILICHO ZAIDI YA PESA.


Kipo kimoja tu, hata uwe na mipesa kama mlima Kilimanjaro.....kupuuufwuuuuzzzz!!!
 
- Yaaani fisadi papa aombwe radhi na wananchi kwa kuwa na ushaidi wa ufisadi wake? Hawa wezi kweli wana kiburi sana hawa, hivi wanakitoa wapi hiki kiburi?

FMES!

Nadhani watakuwa wanakitoa jikoni pale magogoni!!!!!!!
 
Kutishia kwenda mahakamani ndio zao hawa mafisadi wote wa CCM; mnakumbuka hata Nchimbi nae aliwahi kulitisha gazeti la MWANAHALISI pale alipohusishwa na kifo cha Amina Chifupa! Mpaka leo ziiiiiiiiiiiiiiiiiiii hajaenda kwa mjumbe wa nyumba kumi wala kwa sheha!! Hawa mafisadi wamepatwa na mapepo hawajui watendalo!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…