Melki Wamatukio
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 6,360
- 11,588
Mtaani tayari kumeshachangamka. Kwetu sie tunaokaa uswahilini, wimbi la watoto limetaraadadi, ni mwendo wa vumbi madirishani jumlisha na kelele za ule wimbo wa kifaransa wa "Cheche Kule", ni mateso kwa kweli, walimu wana kazi ya ziada aisee
Mbali na mitaani, pia mitandaoni kumeanza kupambazuka, mtandao wa facebook uliosahaulika hatimaye umeanza kupata washirika, watoto wa shule wameuvagaa kama nyuki, hivyo post zisizo na mashiko zimeanza kutaraadadi
Sio tu facebook, hata humu JF tutegemee kukutana na nyuzi za ovyo kama vile "Kuna mdada nampenda, nifanyeje?", "Nilimuingiza magetoni nikapiga mabao ishilini hadi akataja jina la ukoo wao". Pia uzi wa kimasihara utaanza kusonga mbele kwa kasi ya ajabu. Maneno ya dhihaka kama vile "Chai" yatafufuka kuliko kawaida
Pia vile vitisho vya "Unajua unajibishana na nani?" vitaongezeka kwa kasi mpya. Tutashuhudia mengi kwa kweli
Ukiachana na mitandao, nyumba za kulala wageni zimeanza kufurika watu, ikiwa ni pamoja na wanafunzi waliokuwa bweni wakijaribu kutuliza upwipwi waliokuwa nao kwa muda mrefu sana, pia ndoa za ghafla bin vuu a.k.a ndoa za mikeka zitaenea kwa kasi ya wifi ya ZTE. Mambo yatakuwa mpwito mpwito
Wanafunzi karibuni mtaani, mje kutusumbua. Karibuni jukwaa la Love Connect mje mtuenjoy kutafuta wake na waume. Karibuni sana, ruksa kutengeneza IDs za kike mtupige pesa zetu za nauli
Mbali na mitaani, pia mitandaoni kumeanza kupambazuka, mtandao wa facebook uliosahaulika hatimaye umeanza kupata washirika, watoto wa shule wameuvagaa kama nyuki, hivyo post zisizo na mashiko zimeanza kutaraadadi
Sio tu facebook, hata humu JF tutegemee kukutana na nyuzi za ovyo kama vile "Kuna mdada nampenda, nifanyeje?", "Nilimuingiza magetoni nikapiga mabao ishilini hadi akataja jina la ukoo wao". Pia uzi wa kimasihara utaanza kusonga mbele kwa kasi ya ajabu. Maneno ya dhihaka kama vile "Chai" yatafufuka kuliko kawaida
Pia vile vitisho vya "Unajua unajibishana na nani?" vitaongezeka kwa kasi mpya. Tutashuhudia mengi kwa kweli
Ukiachana na mitandao, nyumba za kulala wageni zimeanza kufurika watu, ikiwa ni pamoja na wanafunzi waliokuwa bweni wakijaribu kutuliza upwipwi waliokuwa nao kwa muda mrefu sana, pia ndoa za ghafla bin vuu a.k.a ndoa za mikeka zitaenea kwa kasi ya wifi ya ZTE. Mambo yatakuwa mpwito mpwito
Wanafunzi karibuni mtaani, mje kutusumbua. Karibuni jukwaa la Love Connect mje mtuenjoy kutafuta wake na waume. Karibuni sana, ruksa kutengeneza IDs za kike mtupige pesa zetu za nauli