Hatimaye nimefika Tanzania. Haya ndio niliyojionea mpaka dakika hii

Habari za muda huu Jamii forum na poleni sana kwa mihangaiko ya hapa na pale ya kutafuta maisha.

Nakumbuka siku mbili tatu za nyuma nilikuwa na mawazo ya kuja Tanzania kutafuta opportunities za maisha kwani nimekaa Kenya muda mrefu na nikaona sio mbaya kama nikija nchi za karibu napo kuangalia opportunities zingine.

Kiufupi ni kwamba niliishi Tanzania kidogo sana nakumbuka tuliondoka wakati nipo mdogo sana wakati bado sina uelewa na tumekuwa tukiishi kenya maeneo ya kilifi. Sasa baada ya siku mbili tatu hizi kuangaika na kuweka sawa ishu za documents hatimaye nimefanikiwa kusafiri na kuja rasmi Tanzania kuja kutafuta opportunities za maisha na kiufupi ni kwamba majuzi nimefanikiwa kufika Tanga ambapo nipo hapa kwa siku ya tatu sasa na malengo yangu ni kufika dar es salaam ndani ya siku mbili hizi.

Hakika niliyojionea hapa tanga ni ya kipekee sana kwani watu wa huku ni wakarimu sana na wanapenda kuwa karibu na watu kwani tangu nifike hapa sijajisikia mpweke kwakweli. Vile vile utamaduni wa watu wa huku kwenye mambo ya ngoma zao pia nimevutiwa sana na mazingira ya huku nimeyapenda kwakweli.

Nimepita kwenye fukwe kwakweli panapendeza na vilevile mabinti wa huku ni wazuri sana na wakarimu hasa kwa mtu mgeni. Nilipanga kukaa siku mbili tu lakini ningependa kuongeza siku nyingine mbili zaidi.

Hizi ni baadhi ya picha za sehemu nilipotembelea na ningependa nishare hapa kwenye jukwaa.

View attachment 1508529View attachment 1508530View attachment 1508531View attachment 1508532View attachment 1508533
Kuwa makini na hao mabinti watakula nauli yako ushindwe kwenda dar wala kurudi kilifi
 
Mambo ya tanga
IMG_20200717_222245_0.jpeg
 
Mbona hakuna sentensi inayosema kiswahili nimejifunza kilifi.. ishu ni kwamba kiswahili kiuongeaji na kimaandishi nakimudu vizuri sana kwanza nilishawahi kuishi huku pindi mtoto kingine kule kenya nilikuwa naishi maeneo ya pwani ambapo kiswahili pia sio tatizo sana
Hata kama,kuna ile misemo misemo bhana,kama kuita kande gadheli sijui demu kuita nin sijui vitu kama hivyo bhana we mkenya niaje wew em tuchanganyie changanyie mzee
 
Kulala Katikati Kuna Faida Zake Unapata Ya Dar es salaam Na Dodoma
Watani Zangu Sina Maana Katikati Hiyo. Morogoro
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Tanga tena! ww jiandae kuongeza zaidi ya hizo siku mbili ulizopanga..ngoja ukamatwe na mdigo uwekwe kende kwenye kisosi safari ya Dar es salaam lazima uisahau tu
Huyu nu ke mkuu huoni picha yake 1 ametuma yupo kwenye ..sasa mwanamke ana kende ?
 
Kama mnabisha kwamba huyo sio mkenya ni mtanzania mwenzenu mm nitakua wawapi jamani maana kiswahili mataifa mengi wanazungumza tena vizuri tu,ila Tanzania hata mm napapenda sana hasa maeneo ya buza
 
~ Mbona hausaundi kama watu wa pwani ya kenya?Au umekulia Kenya ya Tanganyika bars?

Karibu sana ila usikaribie bora urudi kweni ....uchaguzi unavurugu uje baadae!
 
Back
Top Bottom