Hatimae TZ UK yapata Viongozi wapya lakini.........

Hatimae TZ UK yapata Viongozi wapya lakini.........

alibaba

Senior Member
Joined
Jun 24, 2009
Posts
185
Reaction score
43
Ilimchukua Mwanabalozi wetu ambae pia ni mlezi wa jumuiya ya Watanzania waishio Uigereza(TA UK), mama Mwanaidi Maajar kuonyesha ufundi wake wa Kidiplomasia, Hekima, Busara na Nguvu za ushawishi, Kuwakubalisha zaidi ya Watanzania 200 Kuukubali mfumo wa uchaguzi uliowekwa mbele yao na Kamati maalum (Task Force) na hivyo uchaguzi kufanyika na kuwapata viongozi wa jumuiya hiyo watakaoongoza kwa kipindi cha miaka miwili. Malumbano na Mdahalo mkali vilizuka pale Watanzania walioshiriki wakitegemea hatimae wangepiga kura kuchagua viongozi wao, walipoambiwa kuwa haki hiyo iko kwa Wawakilishi wa Mikoa 12 tu ambayo imetuma timu ya watu 5 kila mkoa. Karibu wapingaji wengi wa mfumo/utaratibu walioyesha kukasirishwa na kutoamini kuwa Kikundi hicho cha watu 60 ndio kingewaamulia Uongozi wao. Pamoja na majibu ya Kamati Maalum kuwa faida ya mfumo huo ni kujenga nguvu za jumuiya kuanzia Chini (Grassroots) Bado hali ilikuwa mbaya kiasi cha kutishia kutowezekana kuwepo kwa uchaguzi.
Ndipo Shujaa wetu alipopanda Mimbari Na kwa ustadi mkubwa
Akalirudisha Jahazi lililokuwa tayari limeenda Mrama katika njia sahihi. (Pongezi mama Mwanaidi) Balozi aliwaasa Watanzani wakubali Mageuzi na wasiwe wapotezaji wakati, kwani kuahirisha uchaguzi huu ni gharama na wakumbuke kuwa uongozi uliokuwepo umeshajiuzulu na kuwa Serekali inawategemea sana katika mradi huu wa Mtu kwao (Dispora) na haitakuwa rahisi kuuendesha ikiwa hamtakuwa na uongzi.
Baada ya hutuba yake ukumbi ulisimama kumpongeza na baada ya hapo mfumo mpya ulitumika kuwapata vingozi na Bw. John Lusingu aliekuwa katibu mkuu wa chombo hicho alichaguliwa kuwa Mwenyekiti. kuna mjumbe mwengine mmoja toka timu ya zamani na wengine wote kumi ni wapya.
Kwa tafsiri yeyote ushindi wa leo ni wa Mh. mama Balozi.
 
Kafanya maamuzi KICCM CCM ili kuinyima demokrasi kufanya kazi yake. Duhhh! kazi kweli kweli!
 
Abubakar Faraji ndiye mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Uingereza na kukiongoza chama hicho kwa miaka miwili.

Uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Asian Community Centre uliopo katikati ya mji wa Wembley mwezi uliopita uliofuatia baada ya kamati ya muda iliyokuwa na Bi Nora Sumari kumaliza muda wake.

Faraji alifanikiwa kuibuka mshindi baada ya kupata kura 37 dhidi ya Said Yakubu aliyepata kura 27, wakati Suzani Mzee alipata kura 22 katika ya kura 86 zilizopigwa, nafasi ya Makamu Mwenyekiti imekwenda kwa Bi Zubeda Mahugu.

Katika nafasi ya Katibu Mkuu, Bw.John Lusingu aliibuka mshindi dhidi ya Bi Nunu Chondoma, wakati Bw. Juma Pinto alichaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa jumuiya hiyo kwa kumshinda Bw. Yahaya Kiomoni. Bi Lucy Shegikile alipita bila ya kupigwa baada ya kukosa mpinzani katika nafasi yake ya uhazini na wajumbe saba waliochaguliwa ni Bw.Gerald Lusingu,Bw.Almas Kasongo, Bw.Dessa Makoko, Bw.Haruna Mbeyu, Bw.Rehani Ellofy, Bi Zeyana Amour na Bi. Nora Sumari.
Hii habari niya miaka miwili iliyopita..jaribu kuirekebisha inaweza kuchanganya watu.
 
Alibaba,
Nilikuwepo na moto ulikuwa mkali, kunaaliedai kuwa ndio mana Watanzania hatuendelei. Kuna aliedai kuwa tunaonekana kama Wavichaa vile. dada aliejitambulisha kwa jina la Lulu toka Reading Alidai kuwa Fomu za uwakilishi huko kwao zilipitishwa kwa mlano wa uwani na pia kuna ngvu ya kanisa inayodai kuwa wao wametumwa na Mungu, je sisi tusio na Mungu nani atatuwakilisha aliuliza da Lulu na kuifanya kadamnasi imshangilie kwa Nderemo.
Kwa kifupi naona kuliuwa na mafanikio na tunaonyesha Uwezo wetu wa kukabili mijadala na kusema unachokusudia bila Hofu. Mwisho niungane nawe kumpongeza mama Balozi alifanya kilichostahili.
 
mama balozi ndio ameshiriki kubaka demokrasia
huu sio uongozi wa TZ uk bali ni wa CCM UK
 
Ati ndie balozi wetu mtarajiwa marekani mwambien awafanyie ujinga uko huko akiletaa mambo yake us tunamrudisha kusimamia kampuni yake
 
Mh kwa maandishi hayo hapo juu na mtazamo wangu inaelekea hizi jumuiya hazina natija kwa watanzania zaidi ya kuwa kijiwe cha majungu na lawama kila la kheri wengine wacha tuwakalie mbali
 
TZA yapata viongozi wapya



Chama cha watanzania nchini Uingereza leo jumamosi ya tarehe 27 mwezi wa tatu kimechagua viongozi wapya watakao kiongoza chama hicho kwa muda wa miaka miwili. Akizungumza kwenye mkutano huo Mwenyekiti mpya wa chama hicho Bw. Lusingu amesema atashirikia na watanzania wote ili kuweza kufanikiwa kukiendelendeleza chama hicho. Katika uchaguzi huo Bw. John Lusingu amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Bi. Nellie Nsemwa amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Msaidizi, Bw. Hassan Hafidh amechaguliwa kuwa Katibu, D Makoko amechaguliwa kuwa kuwa Katibu Msaidizi, Bw. Goodluck Mbuya amechaguliwa kuwa Katibu Mwenezi na Dr. Evans Mella amechaguliwa kuwa Mweka Hazina.










Posted by Ally Muhdin at 02:48 0 comments



Subscribe to: Posts (Atom)

 
TZA yapata viongozi wapya



Chama cha watanzania nchini Uingereza leo jumamosi ya tarehe 27 mwezi wa tatu kimechagua viongozi wapya watakao kiongoza chama hicho kwa muda wa miaka miwili. Akizungumza kwenye mkutano huo Mwenyekiti mpya wa chama hicho Bw. Lusingu amesema atashirikia na watanzania wote ili kuweza kufanikiwa kukiendelendeleza chama hicho. Katika uchaguzi huo Bw. John Lusingu amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Bi. Nellie Nsemwa amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Msaidizi, Bw. Hassan Hafidh amechaguliwa kuwa Katibu, D Makoko amechaguliwa kuwa kuwa Katibu Msaidizi, Bw. Goodluck Mbuya amechaguliwa kuwa Katibu Mwenezi na Dr. Evans Mella amechaguliwa kuwa Mweka Hazina.










Posted by Ally Muhdin at 02:48 0 comments



Subscribe to: Posts (Atom)


Halafu mkishajulishwa viongozi wa kitanzania je wanamanufaa gani zaidi ya diaspora? Nadhani it is about time people should questions the benefit of diasporas.
 
Back
Top Bottom