Hatari: Nimenusurika kifo

Hatari: Nimenusurika kifo

KikulachoChako

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2013
Posts
19,759
Reaction score
39,496
Habari wakuu.

Jana mwanajamii mwenzenu ilibaki kidogo tu ni rest in peace kutoka kwa wananchi wenye hasira Kali. Ilikuwa kwenye daladala...kama mnavyojua wana JF usafiri wa umma tabu zake hasa nyakati za asubuhi.

Basi baada ya daladala kuingia kituoni watu tukaanza kugombania..hatimaye nikafanikiwa kuingia..lakini sikufanikiwa kupata siti....nilisimama na mdada Fulani hivi pembeni yangu huku akiwa amening'iniza mkoba wake upande Wangu..wakati tunaendelea na safari na hizi barabara zetu zilizo kwenye marekebisho. Ule mkoba ukawa unaning'inia kuniegemea mimi.

Sasa kuna mtu alikuwa anashuka kituo kinachofuata ikanilazimu kusogea mbele kidogo ili kumpisha mshukaji..kwa bahati mbaya wakati nampisha Yule mshukaji mabega yetu yakawa kama yanauvuta ule mkoba wa yule dada.

Kasheshe likaanzia hapo baada kunihisi mimi ndiye niliyekuwa nauvuta ule mkoba kwa makusudio ya kuiba..akaanza kunipigia makelele ya wizi.

Jambo ambalo liliwapa hamaki abiria wengine wakaanza kunishambulia hadi konda alipoanza kunitetea kwa kuwa alilishuhudia. Na ukijumlisha na personality ...abiria wakaanza kunielewa kwamba sikuwa mwizi.

Ikanibidi nishukie kituo kinachofuata ili kuondoa nuksi...duh..kweli si kila anayekufa kwa wizi basi kaiba kweli..wengine wanasingiziwa tu...tuweni tunaposhambulia wezi.
 
Uwege unaenda kanisani walau mara moja moja mkuu.
 
Lakini pole sana, maana sipati picha moyo ulivyokua unakwenda kasi kama magari ya langa langa.,
 
Sasa sisi tutajuaje kama sio mwizi kweli?Kwani mwizi ana rangi gani?
 
Da pole sana kaka mi ilinitokea Sinza siku moja kwenye lodge moja hivi. Nilikuwa na Shem wenu ndani ya chumba tukagombana coz ma gal alikuwa anawivu sana.

Baada ya kugombana nikabidi mi nisepe zangu nikaona hamna dalili ya kupata mzigo hapa but kipindi naondoka Shem wenu alikuwa yupo anaoga.. Mi nipo njiani nakaribia pale meeda nikaona kundi kubwa la watu km 10 hivi wananifata na kuita mwizi mwizi mi nikashangaa vp. Ghafla namuona mlinzi wa lodge anasema kuna demu mmoja Anasema umemwibia pochi yenye laki 2..watu baada ya kusikia hivyo wakaanza kunipiga mdogo mdogo kwamba lazima tukuchome wewe, watu wakawa wanaongezeka na kipondo kinaongezeka yani sipati hata muda wa kujitetea.

Mara gafla akatokea jamaa mmoja tulipiga naye mzumbe chuo amani Mimi mtu huyu namjua twendeni turudi lodge Kwa huyo binti aliyeibiwa, basi tukarudi watu kama 20 ivi hapo nishapigwa sana jamani.. Tukafika guest house pale, Dada wa reception akasema yule msichana kaondoka sasa hivi kafatwa na mwanaume akiwa na gari..kuhusu pochi kumbe kaiona ilikuwa chini ya mto. Sitoisahau that day
 
pole sana... But hilo jina lako hilo....
 
Mimi yalishawahi kunikuta mwaka 2008, natoka kwenye tamasha la kampuni flani ya simu mida ya saa moja jioni(ilikua ufukwe mmoja maarufu dsm) nashangaa kundi la vijana kama kumi hivi wanakuja mbio huku wakiniuliza " simu uliyoiba iko wapi"

Kabla sijapata hata muda wa kujitetea tayari nilishapigwa ngumi mfululizo za tumbo na uso mpaka macho yamevimba kiasi cha kutokuona vizuri,
Walipoanza kunisachi nikawa kama nazuia kwa kuweka mikono mfukoni, nilipigwa visu vya mikono, uso, mgongoni na mkononi mpaka leo nina makovu makubwa ya kutosha.

Kisha wakachukua kila kitu huku wakiendelea kunishambulia kwa kelele za mwiziiiiii mwiziiii, hapo sasa raia wenye hasira zao wakamalizia hasira zao kwangu(ninachoshukuru ilikua beach hakukua na mawe wala tofali, hivyo kilikua kipigo cha ngumi, mateke na makuti,) nakumbuka mpaka nililishwa mchanga kama adhabu,
Kwa kweli Mungu ni mkubwa, kilichoniokoa hata siamini mpaka leo.

Nikipata muda nitarudi kuwapa mkasa mzima ni wa kuumiza sana.
Asubuhi njema wakuu.
 
habari wakuu...jana mwanajamii mwenzenu ilibaki kidogo tu ni rest in peace kutoka kwa wananchi wenye hasira kali...ilikuwa kwenye daladala...kama mnavyojua wana jf usafiri wa umma tabu zake hasa nyakati za asubuhi...basi baada ya daladala kuingia kituoni watu tukaanza kugombania..hatimaye nikafanikiwa kuingia..lakini sikufanikiwa kupata siti....nilisimama na mdada fulani hivi pembeni yangu huku akiwa amening'iniza mkoba wake upande wangu..wakati tunaendelea na safari na hizi barabara zetu zilizo kwenye marekebisho.

ule mkoba ukawa unaning'inia kuniegemea mimi....sasa kuna mtu alikuwa anashuka kituo kinachofuata ikanilazimu kusogea mbele kidogo ili kumpisha mshukaji..kwa bahati mbaya wakati nampisha yule mshukaji mabega yetu yakawa kama yanauvuta ule mkoba wa yule dada..kasheshe likaanzia hapo baada kunihisi mimi ndiye niliyekuwa nauvuta ule mkoba kwa makusudio ya kuiba.

akaanza kunipigia makelele ya wizi..jambo ambalo liliwwapa hamaki abiria wengine wakaanza kunishambulia hadi konda alipoanza kunitetea kwa kuwa alilishuhudia...na ukijumlisha na personality ...abiria wakaanza kunielewa kwamba sikuwa mwizi...ikanibidi nishukie kituo kinachofuata ili kuondoa nuksi...duh..kweli si kila anayekufa kwa wizi basi kaiba kweli..wengine wanasingiziwa tu...tuweni tunaposhambulia wezi....

poleni sana! Naomba kuwaleteeni hiki kisa cha kusikitisha; ilikuwa mwaka jana jamaa yangu na rafiki yangu tulisoma naye o'level huko mara katika harakati za maisha alikuja dsm sasa huo mwaka jana alikuwa na biashara ya butcher na kijana mmoja katika kukosa uaminifu wakadhurumiana na mdhumiwa akiwa rafiku yangu anaitwa frenk warioba.

Sasa mkakati ukaundwa na huyo mshirika wake akaitwa na rafiki yake maeneo ya ving'ung'uti kuwa akamlipe pesa yake aliondoka tabata akamuaga mke wake ambaye ana mtoto mmoja. Kumbe mdaiwa wake alikuwa ameandaa raia kuwa kuna jambazi sugu anakuja kufanya uharifu kwa hiyo atamuita na wasifanye kosa zaidi ya kumuua.

Mara akapigiwa simu akaenda mara kufika tu maeneo aliyoelekezwa akavamiwa na watu kuanza kumpiga huku wakimwitia jambazi!jambazi! Alipigwa mpaka akawa ameishiwa nguvu.

Mwisho akapewa simu aongee na ndugu yeyote ndo akampigia simu mama yake aliye kuwepo musoma mara akamwambia mama nauliwa mimi mwanao nimepaziwa mwizi...! Mama yake huku akisikia makelele mara wakamnyanganya simu jamaa wakamfunga mataili ya magari wakamwagia petroli wakamchoma moto akiwa hai. Nasimulia kama hadithi but it happened hapa dsm mwaka jana.

Kibaya zaidi yeye alikuwa mtoto peke yake kwa mama yake ambaye ni mjane. Na kingine mjane huyo akufanya lolote maana ana uwezo wa kufuatilia kifo cha mtoto wake mmoja ili haki itendeke... Kiukweli nilipoambiwa maswaubu ya kifo cha rafiki yangu iliniuma sana na nikamuhurumia na mama mjane na mzee aliyempoteza mtoto wake mmoja na pekee.

Kama ugushwa na mkasa huu sema amina kwa marehemu na mama huyu mjane mwenye uchungu mkubwa moyoni mwaje.
 
poleni sana! Naomba kuwaleteeni hiki kisa cha kusikitisha; ilikuwa mwaka jana jamaa yangu na rafiki yangu tulisoma naye o'level huko mara katika harakati za maisha alikuja dsm sasa huo mwaka jana alikuwa na biashara ya butcher na kijana mmoja katika kukosa uaminifu wakadhurumiana na mdhumiwa akiwa rafiku yangu anaitwa frenk warioba. Sasa mkakati ukaundwa na huyo mshirika wake akaitwa na rafiki yake maeneo ya ving'ung'uti kuwa akamlipe pesa yake aliondoka tabata akamuaga mke wake ambaye ana mtoto mmoja. Kumbe mdaiwa wake alikuwa ameandaa raia kuwa kuna jambazi sugu anakuja kufanya uharifu kwa hiyo atamuita na wasifanye kosa zaidi ya kumuua. Mara akapigiwa simu akaenda mara kufika tu maeneo aliyoelekezwa akavamiwa na watu kuanza kumpiga huku wakimwitia jambazi!jambazi! Alipigwa mpaka akawa ameishiwa nguvu. Mwisho akapewa simu aongee na ndugu yeyote ndo akampigia simu mama yake aliye kuwepo musoma mara akamwambia mama nauliwa mimi mwanao nimepaziwa mwizi...! Mama yake huku akisikia makelele mara wakamnyanganya simu jamaa wakamfunga mataili ya magari wakamwagia petroli wakamchoma moto akiwa hai. Nasimulia kama hadithi but it happened hapa dsm mwaka jana. Kibaya zaidi yeye alikuwa mtoto peke yake kwa mama yake ambaye ni mjane. Na kingine mjane huyo akufanya lolote maana ana uwezo wa kufuatilia kifo cha mtoto wake mmoja ili haki itendeke... Kiukweli nilipoambiwa maswaubu ya kifo cha rafiki yangu iliniuma sana na nikamuhurumia na mama mjane na mzee aliyempoteza mtoto wake mmoja na pekee. Kama ugushwa na mkasa huu sema amina kwa marehemu na mama huyu mjane mwenye uchungu mkubwa moyoni mwaje.

Mkuu kisa chako kinasikitisha huu n mkasa ambao huwezi kuuepuka, je huyo jamaa unamfaham aliefanya hayo? Kma c ww je mke wake?

Najarb kuona jinsi ambavyo dunia ilivyo katili
 
Mkuu kisa chako kinasikitisha huu n mkasa ambao huwezi kuuepuka, je huyo jamaa unamfaham aliefanya hayo? Kma c ww je mke wake?

Najarb kuona jinsi ambavyo dunia ilivyo katili

Si mjui aliyefanya kitendo hicho ila kuna rafiki yangu aliyekuwa karibu sana na jamaa huyo. Ila wakati wa mkasa unatokea yeye alikuwa bagamoyo kikazi.

Mimi nilisimuliwa mwaka huu mwezi wa nne kuwa frenk alisha kufa kwa kupakaziwa wizi. Ila aliniambia aliyefanya hivyi sasa hivi amekuwa kama chizi hivi aluchanganyikiwa ivi. Kaka inauma sana.
 
Pole sana mkuu siku nyingine ukisimama na wadada wenye vimkoba waambie waweke kwa mbele maana unaweza kosa wakukutetea ukala vipondo vikaleeeeeee
 
Wabongo ovyo kabisa yalishanikuta kitu km hicho kwenye daladala huko moshi.usijelogwa kumsaidia mtu mzigo wake daladalan
 
Ingekuwa nchi za watu huyo mwanamke aliyekuzushia yote hayo angelikuwa anatoa maelezo kituo cha Polisi sasa kwa makosa kadhaa...

Hapa kwetu sheria kama hizi ni ngumu kuzitekeleza ingawaje zipo...
 
Back
Top Bottom