Hatari: Nimenusurika kifo

Hatari: Nimenusurika kifo

MUNGU amlaze marehem mahali pema peponi inahuzunisha sana jaman! polen sana! Naomba kuwaleteeni hiki kisa cha kusikitisha; ilikuwa mwaka jana jamaa yangu na rafiki yangu tulisoma naye o'level huko mara katika harakati za maisha alikuja dsm sasa huo mwaka jana alikuwa na biashara ya butcher na kijana mmoja katika kukosa uaminifu wakadhurumiana na mdhumiwa akiwa rafiku yangu anaitwa frenk warioba. Sasa mkakati ukaundwa na huyo mshirika wake akaitwa na rafiki yake maeneo ya ving'ung'uti kuwa akamlipe pesa yake aliondoka tabata akamuaga mke wak
 
pole sana mkuu, ila hilo jina lako linashabiiana na yalokutkea
 
Da pole sana kaka mi ilinitokea Sinza siku moja kwenye lodge moja hivi. Nilikuwa na Shem wenu ndani ya chumba tukagombana coz ma gal alikuwa anawivu sana.

Baada ya kugombana nikabidi mi nisepe zangu nikaona hamna dalili ya kupata mzigo hapa but kipindi naondoka Shem wenu alikuwa yupo anaoga.. Mi nipo njiani nakaribia pale meeda nikaona kundi kubwa la watu km 10 hivi wananifata na kuita mwizi mwizi mi nikashangaa vp. Ghafla namuona mlinzi wa lodge anasema kuna demu mmoja Anasema umemwibia pochi yenye laki 2..watu baada ya kusikia hivyo wakaanza kunipiga mdogo mdogo kwamba lazima tukuchome wewe, watu wakawa wanaongezeka na kipondo kinaongezeka yani sipati hata muda wa kujitetea.

Mara gafla akatokea jamaa mmoja tulipiga naye mzumbe chuo amani Mimi mtu huyu namjua twendeni turudi lodge Kwa huyo binti aliyeibiwa, basi tukarudi watu kama 20 ivi hapo nishapigwa sana jamani.. Tukafika guest house pale, Dada wa reception akasema yule msichana kaondoka sasa hivi kafatwa na mwanaume akiwa na gari..kuhusu pochi kumbe kaiona ilikuwa chini ya mto. Sitoisahau that day

pole sana chipa
 
Habari wakuu...
Jana mwanajamii mwenzenu ilibaki kidogo tu ni rest in peace kutoka kwa wananchi wenye hasira Kali. Ilikuwa kwenye daladala...kama mnavyojua wana JF usafiri wa umma tabu zake hasa nyakati za asubuhi.

Basi baada ya daladala kuingia kituoni watu tukaanza kugombania..hatimaye nikafanikiwa kuingia..lakini sikufanikiwa kupata siti....nilisimama na mdada Fulani hivi pembeni yangu huku akiwa amening'iniza mkoba wake upande Wangu..wakati tunaendelea na safari na hizi barabara zetu zilizo kwenye marekebisho. Ule mkoba ukawa unaning'inia kuniegemea mimi.

Sasa kuna mtu alikuwa anashuka kituo kinachofuata ikanilazimu kusogea mbele kidogo ili kumpisha mshukaji..kwa bahati mbaya wakati nampisha Yule mshukaji mabega yetu yakawa kama yanauvuta ule mkoba wa yule dada.

Kasheshe likaanzia hapo baada kunihisi mimi ndiye niliyekuwa nauvuta ule mkoba kwa makusudio ya kuiba..akaanza kunipigia makelele ya wizi. Jambo ambalo liliwapa hamaki abiria wengine wakaanza kunishambulia hadi konda alipoanza kunitetea kwa kuwa alilishuhudia. Na ukijumlisha na personality ...abiria wakaanza kunielewa kwamba sikuwa mwizi.

Ikanibidi nishukie kituo kinachofuata ili kuondoa nuksi...duh..kweli si kila anayekufa kwa wizi basi kaiba kweli..wengine wanasingiziwa tu...tuweni tunaposhambulia wezi....

Pole sana Ndugu

Huu ujinga ulibatizwa jina la kizaramo Mob Justice unadhihirisha ni jinsi gani nchi zetu za kiafrika zilivyo na uongozi dhaifu na hazifuati sheria za nchi kiasi wananchi wanashindwa kuziamini mamlaka na kuanza kujichukulia sheria mkononi.

Mie nimewahi kuibiwa i know how it pain, ila sishabikii, sipendi, na siwezi kukuta mwizi anapigwa nikajumuika kumpiga na kumtoa uhai, Japo police wanashabikia kwani ukitoa taarifa wanakuuliza wanampiga kwani ameshakufa?

Naomba tubadilike ili kuepusha kuuwa ndugu zetu wasio na hatia kwa kisingizio cha mwizi, ilihali katika wale wote wanaompiga hakuna hata mmoja anaweza kudhibitisha kwamba anayepigwa amemuibia.
 
Am really sorry for the Man, bcoz he has got embarrased with his wife but at the other point, amejua ukweli pia.

Acha mkuu inaumiza sana ila damu isiyo na hatia lazima Mungu ailipie jamaa mpanga njama naskia amekuwa kama chizi ivi....!
 
Si mjui aliyefanya kitendo hicho ila kuna rafiki yangu aliyekuwa karibu sana na jamaa huyo. Ila wakati wa mkasa unatokea yeye alikuwa bagamoyo kikazi. Mimi nilisimuliwa mwaka huu mwezi wa nne kuwa frenk alisha kufa kwa kupakaziwa wizi. Ila aliniambia aliyefanya hivyi sasa hivi amekuwa kama chizi hivi aluchanganyikiwa ivi. Kaka inauma sana.
POLE SANA
ila Marehemu alitakiwa awaambie wale wanaompiga kuwa mbaya wake ni fulani na ANAMDAI HELA YA MAUZO YA NYAMA
naona Wasamaria wema wangemuelewa.
Lakini mara zote Marehemu huwa ana makosa
Haya mambo yapo
(Kuna jamaa mmoja yangu Ismail Kyarumbika R.I.P.alifanyiwa hivyo huko Mombasa alipoenda kumdai kinguvu mdaiwa wake)
 
POLE SANA
ila Marehemu alitakiwa awaambie wale wanaompiga kuwa mbaya wake ni fulani na ANAMDAI HELA YA MAUZO YA NYAMA
naona Wasamaria wema wangemuelewa.
Lakini mara zote Marehemu huwa ana makosa

Kaka usiongee kama ujui matukio ya kumkamata jambazi huwa hana nafasi ya kujitetea kweny snerio kana hiyo ingawa yeye ikuwa jambazi fake!

Unajua kwa mjibu wa sura ya tukio maeneo hayi kulikuwepo na tukio la ujambazi, mpaka leo watu wengi wanaamini walimuua jambazi hakuna ata mtu aliyefuatilia mama yake mzee sana. Mke wake ndiyo hawa wasichana wetu wa mjini kuona jamaa kafa kaamua kurudi alikotoka make ata kwao na jamaa apajui.

Ni shida sana.
 
Ni wiki sasa imepita kuna kijana wa miaka 17 kauawa huku kimara mwisho njia ya bonyokwa millenium. Huyu kijana alijiingiza kwenye ufundi wa bodaboda baada ya wazazi wake kushindwa kumlipia ada. Siku ya idd tar 29/7/2014 marehemu aitwae lawrance alishinda nyumbani kwao tu maeneo ya mavurunza kimara, ilipofika saa kumi kuna kijana aitwae john alifika nyumbani kwa akina lawrance kwa lengo la kumuomba akamtebgenezee bodaboda. ilipofika saa moja jioni wakaanza safari kuelekea mahali bodaboda ilipo, kufika kule kijana lawrance akafanikiwa kutengeneza ile pikipiki sasa ile aijaribu akiwa amempakia john na kijana mwingine ambaye hakufahamika hatua chache mbele wakasikia mwizi mwizi, john na yule kijana mwingine wakafanikiwa kuruka na kutokomea, lawrance kwa vile alikuwa hajui chochote akabaki ameduwaa ndipo walipoanza kumshambulia, akafanikiwa kuwachomoka akaingia kwenye nyumba moja bodaboda wakaizunguka ile nyumba kwa vitisho kuwa mwenye nyumba asipomtoa watachoma nyumba, wakaanza kuvuta mafuta toka kwa bodaboda zao, mwenye nyumba akaingia woga ikabidi lawrance atolewe wa bodaboda wakamtia mikononi kila alimshambulia anavyotaka mpaka mauti yalipomfika kila mtu akakimbia zake, baada ya uchunguzi ikagundulika kuwa john ndie aliyeiba bodaboda na wamemuua lawrance asiekuwa na hatia

Mbaya Sana hii!! Rushwa iliyokithiri kwenye mamlaka za serikali esp Polisi ndo imetufikisha hapa!

IMANI IMETOWEKA.
 
Mimi yalishawahi kunikuta mwaka 2008, natoka kwenye tamasha la kampuni flani ya simu mida ya saa moja jioni(ilikua ufukwe mmoja maarufu dsm) nashangaa kundi la vijana kama kumi hivi wanakuja mbio huku wakiniuliza " simu uliyoiba iko wapi" .
Kabla sijapata hata muda wa kujitetea tayari nilishapigwa ngumi mfululizo za tumbo na uso mpaka macho yamevimba kiasi cha kutokuona vizuri,
Walipoanza kunisachi nikawa kama nazuia kwa kuweka mikono mfukoni, nilipigwa visu vya mikono, uso, mgongoni na mkononi mpaka leo nina makovu makubwa ya kutosha.
Kisha wakachukua kila kitu huku wakiendelea kunishambulia kwa kelele za mwiziiiiii mwiziiii, hapo sasa raia wenye hasira zao wakamalizia hasira zao kwangu(ninachoshukuru ilikua beach hakukua na mawe wala tofali, hivyo kilikua kipigo cha ngumi, mateke na makuti,) nakumbuka mpaka nililishwa mchanga kama adhabu,
Kwa kweli Mungu ni mkubwa, kilichoniokoa hata siamini mpaka leo.
Nikipata muda nitarudi kuwapa mkasa mzima ni wa kuumiza sana.
Asubuhi njema wakuu.

Mnyenz nausubiria kesho mkasa wenyewe naomba na picha uweke za makovu...... alafu kama ulikuwa na mpenzi wakati huo alisemaje? je ndugu jamaa na marafiki walisemaje? asante na wewe pia
 
Pole sana Mkuu ila Mwizi hana alama alafu siku hizi wezi wanavaa smart sana ni ngumu kuwatambua.
 
Poleni sana sana,ilinitokea Kunduchi mwaka 2005,tupo bar flani hivi watu wengi kwelikweli tunaangalia mpira,ile niweke mguu vizuri jamamaa akaniitia mwizi kwamba nataka kumchomolea simu,acha bwana watu wakaanza kupanic,nilichofanya ni kutoa fungu nililokuwa nalo mfukoni pamoja na simu yangu,nikamuonesha jamaa na kuanza kumkolomea.Wananchi walinielewa hawakunigusa.
 
Dah.Ni hatar sana sana.Ni hivi TZ huwa kuna hili kundi linalojulikana kama 'WANANCHI WENYE HASIRA ' inabidi kushukuru kwa kutoka salama . Hili kundi mainly huwa ni watu wenye hasira na maisha magumu ingawa ndo waliochagua chama tawala na stress nyingine.Hasira zao huwa wanazitolea popote pale penye kaloop hole ingawa kwenye ballot za uchaguzi huwa hawazitolei huko
 
Pole sana mkuu,nadhani kuna haja ya wananchi kuyachunguza kwanza matukio ya kuchukua sheria mkononi kabla ya kuchukua hatua ili kunusuru maisha ya watu wasio na hatia...
 
Ni Hatari kuchukua sheria mkokoni.

BR,
~Amalinze The Cat.
 
Mimi ilinitokea nilikua safar kibiashara eneo nilipokua jirani kulikua na duka nikaenda kununua vocha tukakutana na mama momoja mm mfukoni nilikua na sh. 9000 nikatoa sh 2000 nikanunua vocha ya buku ile chenj alionipa nikachanganya na zile nyingine ikabak elf nane.

Sasa yule mama nae sijui ni kitu gan alinunua akawa anadai chenj yake mwenye duka ambayo ni sh elfu nane mwenye duka akasema we mama bado ujatoa pesa akakataa akasema umetoa akamwambia mwenye duka umetoa ila huyu kaka amechukua, mwenye duka akatoka nje nakuanza kuniambia toa pesa kabla sijakuchinja nikasachiwa huku nimekunjwa ikakutwa hiyo elfu 8 akasema pesa hii apa mwizi mkubwa nikapigwa makof shat langu likachanika nikaomba msamaa wakaniachia nikaondoka iliniuma sana baada ya siku3 ilikuandio safar nikapita pale kununua maji nikamkuta yule jamaa akaniambia samahan ulipondoka yule mama aliiona pesa yake kwenye sidiria amekutafuta sana akuombe msamaa nikamwambia we ndio ulie nipiga chukua wewe.

Kweli sio wote wanauwawa wameiba tuwe makin.
 
Back
Top Bottom