Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,210
- 829,208
Kilicho trend last week ni ishu ya aliyekuwa mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahim Haruna Lipumba kutengua uamuzi wake wa kujiuzulu nafasi hiyo na kupata msaada wa dola kwenda kuvunja makufuli ya iliyokuwa ofisi yake ya chama na kuamua kuishi hapo usiku na mchana huku akiwa na walinzi lukuki
Hili lilitanguliwa na viongozi wenzake kumtuhumu kwa uwazi kabisa kuwa katumwa na chama tawala kuivuruga CUF huku wakiweka wazi kiasi alichopewa na vitu alivyonunua.
Post hazikuwa haba hapa jukwaani na kwengineko za kumkosoa kumtusi kumkashifu na kukubaliana naye zote zilikuwepo, kwa ufupi tunaweza kuuita WIKI YA LIPUMBA, kwakuwa hata ishu ya waziri mkuu kuhamia Dodoma haikuwa habari kivile.
Wote kwa ujumla wetu tulobebwa na jina Lipumba na yale aliyoyafanya...! Akibezwa mpaka kiwango chake cha elimu na jinsi alivyodhalilisha nafasi ta uprofesa
Mimi nachukua nafasi hii kuwa na mtazamo tofauti kidogo.
Kwanza ni ukweli usiopingika kuwa Lipumba ni msomi mchumi aliyefanya mengi kuliko wengi wetu kitaifa na hata kimataifa, anatambulika na kufahamika kwenye mengi.
Kilichomtokea yeye si bahati mbaya bali ni mipango ya muda mrefu iliyosukwa kwa ustadi na ushawishi mkubwa...hapo ahadi ya pesa nyingi ulinzi na hata cheo vilitumika sana.
Nani asiyependa ulinzi wa dola wa kipekee kutoka kitengo?
Nani asiyependa cheo na nafasi serikalini?
Nani asiyependa pesa nyingi zisizo za kuhangaikia sana? Hata mwendawazimu anajua hii ni pesa asiitupe.
Inahitaji moyo mgumu wenye uthubutu wa kipekee kuweza kuruka viunzi vya ushawishi wa namna hii.
Kitengo kilipewa special task ya kusambaratika muunganiko fulani. hapo waliangaliwa nani ambao wana ushawishi lakini ambao wanaweza kulainika kama shekeli nk vikitumika, list ilikuwa ndefu..tumeona yaliyotokea. Prof naye alikuwa mmojawapo.
Pesa ya kitengo ni nyingi ni tamu na haikatwi kodi na unapewa yote kwa mpigo kama ni kwa istallment haziwezi kuzidi mbili...halafu haina kelele
Wajanja wanapoichukia ile pesa na kufanya kazi ya awali hukimbia nchi kwakuwa ukibaki, itabidi uendelee kuitumikia ile pesa ya watu kwa matakwa ya waliokulipa.
Hapa ndio penye shida kubwa
Hapa ndio watu hufanya mambo tofauti na kawaida
Hapa ndio watu huweka taaluma pembeni na kukubali kutumika
Hapa ndio utu heshima na hekima ya mtu hugoma na kugota kufanya kazi bali kupokea maagizo kutoka gizani, maagizo yasiyohojiwa.
Lipumba yuko kwenye mtanziko huo kwasasa na hana jinsi bali kutii
Tumbeze kumdhihaki na kumcheka lakini hata kama ni wewe ungekuwa kama prof Ibrahim Haruna Lipumba
Hili lilitanguliwa na viongozi wenzake kumtuhumu kwa uwazi kabisa kuwa katumwa na chama tawala kuivuruga CUF huku wakiweka wazi kiasi alichopewa na vitu alivyonunua.
Post hazikuwa haba hapa jukwaani na kwengineko za kumkosoa kumtusi kumkashifu na kukubaliana naye zote zilikuwepo, kwa ufupi tunaweza kuuita WIKI YA LIPUMBA, kwakuwa hata ishu ya waziri mkuu kuhamia Dodoma haikuwa habari kivile.
Wote kwa ujumla wetu tulobebwa na jina Lipumba na yale aliyoyafanya...! Akibezwa mpaka kiwango chake cha elimu na jinsi alivyodhalilisha nafasi ta uprofesa
Mimi nachukua nafasi hii kuwa na mtazamo tofauti kidogo.
Kwanza ni ukweli usiopingika kuwa Lipumba ni msomi mchumi aliyefanya mengi kuliko wengi wetu kitaifa na hata kimataifa, anatambulika na kufahamika kwenye mengi.
Kilichomtokea yeye si bahati mbaya bali ni mipango ya muda mrefu iliyosukwa kwa ustadi na ushawishi mkubwa...hapo ahadi ya pesa nyingi ulinzi na hata cheo vilitumika sana.
Nani asiyependa ulinzi wa dola wa kipekee kutoka kitengo?
Nani asiyependa cheo na nafasi serikalini?
Nani asiyependa pesa nyingi zisizo za kuhangaikia sana? Hata mwendawazimu anajua hii ni pesa asiitupe.
Inahitaji moyo mgumu wenye uthubutu wa kipekee kuweza kuruka viunzi vya ushawishi wa namna hii.
Kitengo kilipewa special task ya kusambaratika muunganiko fulani. hapo waliangaliwa nani ambao wana ushawishi lakini ambao wanaweza kulainika kama shekeli nk vikitumika, list ilikuwa ndefu..tumeona yaliyotokea. Prof naye alikuwa mmojawapo.
Pesa ya kitengo ni nyingi ni tamu na haikatwi kodi na unapewa yote kwa mpigo kama ni kwa istallment haziwezi kuzidi mbili...halafu haina kelele
Wajanja wanapoichukia ile pesa na kufanya kazi ya awali hukimbia nchi kwakuwa ukibaki, itabidi uendelee kuitumikia ile pesa ya watu kwa matakwa ya waliokulipa.
Hapa ndio penye shida kubwa
Hapa ndio watu hufanya mambo tofauti na kawaida
Hapa ndio watu huweka taaluma pembeni na kukubali kutumika
Hapa ndio utu heshima na hekima ya mtu hugoma na kugota kufanya kazi bali kupokea maagizo kutoka gizani, maagizo yasiyohojiwa.
Lipumba yuko kwenye mtanziko huo kwasasa na hana jinsi bali kutii
Tumbeze kumdhihaki na kumcheka lakini hata kama ni wewe ungekuwa kama prof Ibrahim Haruna Lipumba

