Hata Mimi Ukiniimba Kwa Kunichafua - Nakupiga

Tata Maestro

Senior Member
Jan 8, 2017
169
175
Nimejaribu kuusikiliza ule wimbo wa msanii wenu pendwa nimesikitika sana. Kama yeye msanii pendwa sikujua nini kimemsukuma na kujiingiza kwenye utetezi wa anaetuhumiwa kuwa hana vyeti. Kama yeye alikuwa anataka kumsaidia angeimba certification ya vyeti vyake maana hawa watu tunahasira nao sana , walitunyanyasa sana wakati wa ukaguzi wa vyeti tunashinda halmashauri siku 2 kabisa tunasubiri kukaguliwa ,kumbe wanaotukagua hawana vyeti. Mwenye wimbo anaweza akaona jinsi gani , inavyo uma watu wengi? Unashinda umesimama ili ukaguliwe kumbe anaekukagua hana vyeti? Aseee inauma sana. Kwa kugesi tu ,huyu msanii muda si mrefu anageuka chukizo kwa wengi maana watu wamenyanyasika sana na wanashida sana.

Askofu wangu pendwa na mpongeza sana, kwa ku - react immediately otherwise unapokaa kimya kwa nyimbo au vitu vya ajabu - ajabu kama hivi na kuviacha vi-sounds kwenye vichwa vya watu, watu wanaamini na image yao kwako inabadilika so unatakiwa ku-react immediately ili waaumini wako waendelee kuwa na imani na wewe, muumini humwamini sana mchungaji wake na anposikia kitu kibaya juu ya mchungaji wake ,huwa anatamani kuupata ukweli juu ya issue tata. Sasa mchungaji unaelengwa unapokaa kimya unatengeneza sintofahamu kubwa sana kwa waumini wako na jamii kwa ujumla. Mchungaji wa kweli ni yule anaetolea ufafanuzi kuhusu maswala tata yaliyo tolewa kwenye media yakimuhusu yeye na siyo akae kmya harafu atuache njia panda.

Wote wanaompanda askofu wangu pendwa either hamiijui Biblia au wanaijua kwa mapokeo. Aliyesema asiye fanya kazi na asile ndiye Yuleyule aliyesema msiisumbukie kesho, kuwa mtakula nini au mtavaa nini na tafuteni kwanza ufalme wa mbinguni. Na ni Yuleyule aliyesema hakuja kuibadilisha torati bali kuitimiza na kumbukeni torati ilikuwa jino kwa jino , na jicho kwa jicho. Na msipende kuwafananisha watumishi wa Mungu especially maasikofu au wachungaji moja kwa moja na Yesu. Biblia inamtaja Yesu kuwa ni Mungu 100% maana Yesu yeye mwenyewe anawaambia wanafunzi wake amuonae yeye ameona Baba yake ambae ni Mungu. So Wachungaji/Maasikofu ni binadamu 100% pamoja kuwa wanamuwakilisha Kiristo. Na wengi wenu munajua maana ya kuwakilisha sitaki kufafanua sana. So as Binadamu ukisingiziwa kuwa umebaka mke wa mtu ni lazima ujibu shutuma usikae kimya ukaona ndo utakatifu, No unapotea, watu wataamini na utajiletea sifa mbaya kwenye jamii. Kama uongo ukisemwa sana na mara kwa mara watu huamini kuwa ni kweli. So anaetuhumiwa kuwa hana vyeti ajitokeze nae a-react tuyapime maneno yake. Au atoe vyeti kabisa siyo kuja na vijinyimbo hapa, yeye vipi?

It is true, zero on the paper represents zero in planning. Even aliyetoa kiji-nyimbo yawezekana nae ana zero on the paper, kama siyo kwanini akubali kutumika ki-zero zero ivi. Mimi binafsi nimemu rate kwenye zero, kuminya sauti siyo issue. Issue ni una zero on the paper au hauna?
Mwisho, Hata mimi ningekuwa na cheo kibwa kanisani kuliko hata uasikofu , ukinichafua kwa vijinyimbo vya nama hii na mimi nakupiga. Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Ha Mtapigwa sana mwaka huu na askofu wetu pendwa nyie jichanganyeni tu.
 
Wanamaombi tuendelee kumuombea masihi wa Bwana bishop Gwajima... Mungu azidi atukuzwa kupitia huduma yake ya uchungaji
 
"Mimi wananipiga lakini nikirudisha mapigo wanaanza kusema eeh mchungaji punguza mapigo mbona hawakuwaambia wapunguze kunipiga mimi?"
- pr. Gwajima
 
Back
Top Bottom