Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikiendelea kukumbwa na mtikisiko wa ndani, mamia ya wanachama wake wanaripotiwa kujivua uanachama, huku wakihusishwa na mpango wa kujiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), kikiwa miongoni mwa vyama 19 vilivyosajiliwa rasmi nchini.
Licha ya wanachama hao kutotangaza hadharani chama wanachokusudia kujiunga nacho, duru za siasa zimeelekeza vidole kwa CHAUMMA kuwa ndiyo chaguo lao jipya, kutokana na historia ya wazi ya kupokea wanachama kutoka vyama vingine.
Kwa mujibu wa tovuti ya Mwananchi, Mwenyekiti wa CHAUMMA, Hashim Rungwe, amesema mpaka sasa bado hajapokea rasmi wanachama hao, lakini amesisitiza kuwa milango ya chama chake iko wazi kwa Watanzania wote.
"Wana uhuru kujiunga na chama chochote. Hadi sasa hawajaja CHAUMMA, nami nasikia kwenye vyombo vya habari tu. Tukikutana nao tutawaeleza bayana," amesema Rungwe.
Ameongeza kuwa vyama vya siasa ni mali ya wananchi na si mali binafsi ya viongozi, hivyo mtu yeyote ana uhuru wa kuhama kutoka chama kimoja kwenda kingine bila lawama.
"Hiki chama si changu, ni cha wananchi. Hakuna mwenye mamlaka ya kumzuia Mtanzania kuhamia chama kingine," amesisitiza.
Rungwe pia ameeleza kuwa mchakato wa ndani wa kupata wagombea wa nafasi mbalimbali katika chama hicho umeanza, lakini mkutano mkuu uliopangwa kufanyika Mei 11-12, uliahirishwa hadi Juni 27-28, 2025, kutokana na changamoto ya kifedha.
Anasema mkutano huo utakuwa wa kihistoria kwa kuwa utafanya uteuzi rasmi wa mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kwa tiketi ya CHAUMMA.
Akizungumzia msimamo wa chama chake kuelekea uchaguzi mkuu ujao, Rungwe amesema CHAUMMA haitasusia uchaguzi kama vyama vingine vinavyolalamikia mfumo wa uchaguzi, bali itaendelea kushiriki na kutoa maoni ya marekebisho ya sheria na kanuni kwa njia za kisheria.
"Sheria zina matatizo, lakini haziwezi kutufanya tusishiriki uchaguzi. Tutalalamika kwa utaratibu, lakini hatujawahi kususia uchaguzi," amesema Rungwe.
Akijibu kauli kwamba amekaa muda mrefu kwenye uongozi wa chama hicho, Rungwe amesema: “Wengine wanasema nimekaa sana, lakini Nyerere alikaa miaka 25 na hakuna aliyelalamika hadi alipoamua kuondoka mwenyewe.
Licha ya wanachama hao kutotangaza hadharani chama wanachokusudia kujiunga nacho, duru za siasa zimeelekeza vidole kwa CHAUMMA kuwa ndiyo chaguo lao jipya, kutokana na historia ya wazi ya kupokea wanachama kutoka vyama vingine.
"Wana uhuru kujiunga na chama chochote. Hadi sasa hawajaja CHAUMMA, nami nasikia kwenye vyombo vya habari tu. Tukikutana nao tutawaeleza bayana," amesema Rungwe.
Ameongeza kuwa vyama vya siasa ni mali ya wananchi na si mali binafsi ya viongozi, hivyo mtu yeyote ana uhuru wa kuhama kutoka chama kimoja kwenda kingine bila lawama.
"Hiki chama si changu, ni cha wananchi. Hakuna mwenye mamlaka ya kumzuia Mtanzania kuhamia chama kingine," amesisitiza.
Rungwe pia ameeleza kuwa mchakato wa ndani wa kupata wagombea wa nafasi mbalimbali katika chama hicho umeanza, lakini mkutano mkuu uliopangwa kufanyika Mei 11-12, uliahirishwa hadi Juni 27-28, 2025, kutokana na changamoto ya kifedha.
Anasema mkutano huo utakuwa wa kihistoria kwa kuwa utafanya uteuzi rasmi wa mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kwa tiketi ya CHAUMMA.
Akizungumzia msimamo wa chama chake kuelekea uchaguzi mkuu ujao, Rungwe amesema CHAUMMA haitasusia uchaguzi kama vyama vingine vinavyolalamikia mfumo wa uchaguzi, bali itaendelea kushiriki na kutoa maoni ya marekebisho ya sheria na kanuni kwa njia za kisheria.
"Sheria zina matatizo, lakini haziwezi kutufanya tusishiriki uchaguzi. Tutalalamika kwa utaratibu, lakini hatujawahi kususia uchaguzi," amesema Rungwe.
Akijibu kauli kwamba amekaa muda mrefu kwenye uongozi wa chama hicho, Rungwe amesema: “Wengine wanasema nimekaa sana, lakini Nyerere alikaa miaka 25 na hakuna aliyelalamika hadi alipoamua kuondoka mwenyewe.