LOVINTAH GYM
JF-Expert Member
- Oct 22, 2015
- 459
- 643
DIS-ECONOMIES OF SCALE
Hiki ni kinyume cha economies of scale.
Ni kitendo cha gharama za uzalishaji kuongezeka kadri unavyoongeza uzalishaji wa bidhaa.
Mfano:
Una fuso lako la kusafirisha mizigo, mwanzoni ukaona hulitendei haki kwa kubeba mizigo michache, ukaamua kuongeza mizigo.
Kitendo cha mizigo kuwa mingi kikasababisha wewe kukamatwa na TANROAD na kulipishwa fine ambayo inakurudisha nyuma kimaendeleo.
Mfano 2:
Una kijana mmoja wa kazi wa kukusaidia kazi zako za ndani, ukaona uajiri mfanya kazi mwengine ili wasaidizane kufanya usafi.
Kitendo cha kuongeza mfanyakazi mwengine pia umeongeza gharama kama mshahara, vijana wote wanakula kwako, wakiumwa wote utahitaji kuwatibia. Kwahiyo lengo lako la kufanya nyumba iongezeke usafi gharama zimekuwa kubwa.
Mfano 3:
Una bakery, umeajiri mpishi unamlipa 400,000 na ana uwezo wa kutengeneza mikate 100 kwa siku, bei ya mkate 1 ni 1,000.
Kila siku mikate yote inauzika na bado kuna wateja 10 na zaidi wakija kuulizia wanakuta mikate imeisha.
Kwasiku 1 Mauzo yako ni = mikate 100 x bei 1,000 = 100,000
Kwahiyo una uwezo wa kuuza 100,000 kwa siku.
Kwa mwezi una uwezo wa kuuza = 100,000 x 30 = 3,000,000
Ukitoa gharama ya kumlipa mpishi mshahara
= 3,000,000 - 400,000 =2,600,000
Ukaona basi ni kheri uajiri mpishi mwengine ambaye nae utamlipa 400,000 ili atengeneze mikate 10 ya wateja wanaokosa.
Mauzo kwa siku = mkate 110 x bei 1,000 = 110,000
Mauzo kwa mwezi = 110,000 x 30 = 3,300,000
ukitoa mishahara ya wapishi =400,000 x wapishi 2 = 800,000
mauzo - mishahara = 3,300,000- 800,000 =2,500,000
Kwahiyo kwa kuongeza uzalishaji wa mikate 10 na kuongeza kumuajiri mtu mwengine kumekupunguzia kipato kwa 100,000
Na hapo hatujapigia ongezeko la gharama nyingine kama mafuta, unga, amira, umeme, maji, mifuko nk.
Tume assume gharama yako ni mshahara tu, kwahiyo kuna bidhaa nyingine unavyojitahidi kutengeneza nyingi basi gharama huongezeka maradufu
Kama mnakumbuka law of diminishing marginal return kwamba kuna sehemu ikifika hata ukiongeza kitu flani uzalishaji hautoongezeka badala yake utapungua.
Basi diseconomies of scale nayo ni ile sehemu ambayo kadri unavyoongeza uzalishaji gharama inakuwa kubwa sana.
Mfanano wa hizi theories ni kwamba, ni rahisi mfanya biashara kupata hasara akiwa katika hii position.
TOFAUTI YA DIMINISHING MARGINAL RETURN NA DISECONOMIES OF SCALE NI HIZI:
DIMINISHING MARGINAL RETURN
1.Hutokea biashara itakapoongeza kitu kimoja na kuacha kuongeza vitu vyengine ambavyo ni muhimu katika ukuaji wa biashara.
2.Hii ni rahisi kutokea katika mda mfupi kweye biashara
DISECONOMIES OF SCALE
1. Hutokea gharama za uzalishaji kuongezeka kadri unavyojitahidi kuongeza idadi ya bidhaa.
2.Hii hutokea kadri biashara inavyozidi kuwa kubwa
Mara nyengine Diseconomies of scale husababisha bei ya bidhaa kuongozeka ili mfanya biashara aweze kupata faida.
Bei ya bidhaa ikipanda inamaana itasaidia kulipa zile gharama za uzalishaji zilizoongezeka.
#law #diseconomiesofscale #diminishingmarginalreturn #opportunitycost #economics #averagecost #swahili
Hiki ni kinyume cha economies of scale.
Ni kitendo cha gharama za uzalishaji kuongezeka kadri unavyoongeza uzalishaji wa bidhaa.
Mfano:
Una fuso lako la kusafirisha mizigo, mwanzoni ukaona hulitendei haki kwa kubeba mizigo michache, ukaamua kuongeza mizigo.
Kitendo cha mizigo kuwa mingi kikasababisha wewe kukamatwa na TANROAD na kulipishwa fine ambayo inakurudisha nyuma kimaendeleo.
Mfano 2:
Una kijana mmoja wa kazi wa kukusaidia kazi zako za ndani, ukaona uajiri mfanya kazi mwengine ili wasaidizane kufanya usafi.
Kitendo cha kuongeza mfanyakazi mwengine pia umeongeza gharama kama mshahara, vijana wote wanakula kwako, wakiumwa wote utahitaji kuwatibia. Kwahiyo lengo lako la kufanya nyumba iongezeke usafi gharama zimekuwa kubwa.
Mfano 3:
Una bakery, umeajiri mpishi unamlipa 400,000 na ana uwezo wa kutengeneza mikate 100 kwa siku, bei ya mkate 1 ni 1,000.
Kila siku mikate yote inauzika na bado kuna wateja 10 na zaidi wakija kuulizia wanakuta mikate imeisha.
Kwasiku 1 Mauzo yako ni = mikate 100 x bei 1,000 = 100,000
Kwahiyo una uwezo wa kuuza 100,000 kwa siku.
Kwa mwezi una uwezo wa kuuza = 100,000 x 30 = 3,000,000
Ukitoa gharama ya kumlipa mpishi mshahara
= 3,000,000 - 400,000 =2,600,000
Ukaona basi ni kheri uajiri mpishi mwengine ambaye nae utamlipa 400,000 ili atengeneze mikate 10 ya wateja wanaokosa.
Mauzo kwa siku = mkate 110 x bei 1,000 = 110,000
Mauzo kwa mwezi = 110,000 x 30 = 3,300,000
ukitoa mishahara ya wapishi =400,000 x wapishi 2 = 800,000
mauzo - mishahara = 3,300,000- 800,000 =2,500,000
Kwahiyo kwa kuongeza uzalishaji wa mikate 10 na kuongeza kumuajiri mtu mwengine kumekupunguzia kipato kwa 100,000
Na hapo hatujapigia ongezeko la gharama nyingine kama mafuta, unga, amira, umeme, maji, mifuko nk.
Tume assume gharama yako ni mshahara tu, kwahiyo kuna bidhaa nyingine unavyojitahidi kutengeneza nyingi basi gharama huongezeka maradufu
Kama mnakumbuka law of diminishing marginal return kwamba kuna sehemu ikifika hata ukiongeza kitu flani uzalishaji hautoongezeka badala yake utapungua.
Basi diseconomies of scale nayo ni ile sehemu ambayo kadri unavyoongeza uzalishaji gharama inakuwa kubwa sana.
Mfanano wa hizi theories ni kwamba, ni rahisi mfanya biashara kupata hasara akiwa katika hii position.
TOFAUTI YA DIMINISHING MARGINAL RETURN NA DISECONOMIES OF SCALE NI HIZI:
DIMINISHING MARGINAL RETURN
1.Hutokea biashara itakapoongeza kitu kimoja na kuacha kuongeza vitu vyengine ambavyo ni muhimu katika ukuaji wa biashara.
2.Hii ni rahisi kutokea katika mda mfupi kweye biashara
DISECONOMIES OF SCALE
1. Hutokea gharama za uzalishaji kuongezeka kadri unavyojitahidi kuongeza idadi ya bidhaa.
2.Hii hutokea kadri biashara inavyozidi kuwa kubwa
Mara nyengine Diseconomies of scale husababisha bei ya bidhaa kuongozeka ili mfanya biashara aweze kupata faida.
Bei ya bidhaa ikipanda inamaana itasaidia kulipa zile gharama za uzalishaji zilizoongezeka.
#law #diseconomiesofscale #diminishingmarginalreturn #opportunitycost #economics #averagecost #swahili