Harusi kama hizi ndizo zinatuvunja Moyo Sisi wengine hata Kufikiria kama siyo Kuthubutu Kuoa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,548
108,879
Kuna Harusi moja nimeiona imefanyika nchi Jirani tu hapo ambapo Kwanza wakati Bwana Harusi anaenda Kupeleka Mahari kwa Wakwe zake alikodi Helikopta. Siku ya Harusi yenyewe ilifanyika ndani ya Ziwa Victoria ambapo kuna Meli maalum ilikodiwa na ikarembwa ambapo Wageni waalikwa wote waliingia humo Kula, Kunywa na Kusaza.

Hiyo ikiwa ni Tisa ambapo Kumi yake sasa ilikuwa ni wakati wa Kutoa Zawadi Siku ya Harusi ambapo Zawadi ndogo ambayo ilitolewa kwa Wanandoa hao ni ya Gari aina ya IST ambayo aliyoitoa alisema iwe ni ya Wafanyakazi Wao kuitumia kwenda Kufanya Manunuzi yao Sokoni au kwenda Kujazia Majiko yao ya Gesi pale ikipungua.

Harusi ilipomalizika tu Wanandoa haraka sana waliwahishwa Uwanja wa Ndege kwenda Fungate ( Honeymoon ) yao huko nchini Ufaransa katika Kisiwa kimoja maarufu na chenye Gharama sana Kutembelewa na wengi wanaotembea huko ni wale Binadamu Matajiri kuliko wengine ulimwenguni.

Najuta hata Kuisoma hii taarifa kwani imeshanivunja kabisa Moyo wa Mimi kuendelea na Mchakato mzima wa Kupeleka Mahari na Kujiandaa na Harusi kwani nina uhakika haya yaliyofanyika katika hiyo Harusi ya Kitajiri ( Kifahari ) hapo juu sina ubavu nayo na yangu itakuwa ni ya Kimasikini zaidi.

Wanaume wenzangu tujitahidi tutafute Hela Kwanza ili nasi tuwe na Jeuri kama ya huyo Mwanaume mwenzetu wa nchi jirani. Sijui Sisi wengine tumekosea au tumechelewa wapi na Sisi ama Kuzaliwa na Wazazi Matajiri au kupitiwa pembeni na Pesa ambazo Wenzetu hawa wanazo.

Tujadili.
 
Mkuu, Ndoa za hivyo baada ya wiki 4 tu utasikia mke kafumaniwa na ndoa inavunjika.

Uko sahihi Kiongozi kwani ipo moja ya Mtoto wake Tajiri Mzee Rupia yaliyotokea kama haya ila yenyewe sababu haikuwa ni Usaliti bali Mwanamke ( Mke ) alikataa Kutekeleza Jukumu alilopewa na Mwanaume ( Mumewe ) na akishinikiza kuwa Yeye hana Hadhi hiyo bali Dada wa Kazi ndiyo alipaswa Kuyafanya yote hayo. Huyo Binti alikuwa ni wa Yule Waziri ambaye miaka kadhaa iliyopita aliionja Jela ya Segerea na sasa yupo Uraiani ( Huru )
 
Sasa ndugu huo si ubinafsi unakusumbua kweli? Wewe si ufanye ya staili yako, huyo anakukatishaje tamaa? Shida ya waafrika wengi ni kuongozwa na jamii kuliko wewe binafsi. Wewe ukitaka kataa kuongozwa na wanajamii, fanya kile unataka. Hii si kwa ndoa tu, hata masuala mengine ya maisha.

Vijana wengi wakitaka kuoa wanakimbizwa kweli, wanakubali kuumia ama kuumiza wengine kiuchumi kisha wanaachwa hawana kitu zaidi ya suti na shela walilonunuliwa siku ya harusi.Unafanyaje harusi ya milioni 10, halafu baada ya miezi michache mkeo anakwenda kujifungua unakopa hela kwa shiiida, unakopa hela ya kodi ya nyumba kwa shiiida? Cha kushangaza wakati huo huchangiwi tena!

Waafrika tukitukanwa na kina Trump tunakasirika bure, tuna shida.
 
Usipate tabu Mara nyingi ndoa za hivyo hazidumu. Lakini muhimu zaidi Fanya kile uwezo wako unaruhusu,ukisubiri na wewe ufanyie harusi ndani ya ziwa Victoria hutooa mana hujui huyo mpaka ameweza amepitia wapi na ni nini kilichomuwezesha kufanikisha hilo
 
Jamaa anaitwa Jared Otieno.Ni mmoja wa waliomuuzia ndugu yake mfalme wa Saud Arabia Fake Gold .na mpaka sasa yupo Lokapu .So lets not discuss him kwani hizo mbwembwe zote ni pesa za wizi na utapeli.Nyumba yake moja wapo na magari na mkewe see below pictures
 

Attachments

  • c5fbf954802d8780.jpg
    c5fbf954802d8780.jpg
    49.7 KB · Views: 38
  • 6fb359f97da02174.jpg
    6fb359f97da02174.jpg
    59 KB · Views: 29
  • b69902e08445bea2.jpg
    b69902e08445bea2.jpg
    59.5 KB · Views: 32
  • images (13).jpeg
    images (13).jpeg
    35.7 KB · Views: 34
  • images (15).jpeg
    images (15).jpeg
    26.9 KB · Views: 31
  • images (16).jpeg
    images (16).jpeg
    18.5 KB · Views: 30
  • 6778-696x522.jpg
    6778-696x522.jpg
    44.2 KB · Views: 34
  • 12991006_10209482641282563_53979047552470136_n (1).jpg
    12991006_10209482641282563_53979047552470136_n (1).jpg
    52.3 KB · Views: 29
  • images (14).jpeg
    images (14).jpeg
    23.8 KB · Views: 32
Sasa ndugu huo si ubinafsi unakusumbua kweli? Wewe si ufanye ya staili yako, huyo anakukatishaje tamaa? Shida ya waafrika wengi ni kuongozwa na jamii kuliko wewe binafsi. Wewe ukitaka kataa kuongozwa na wanajamii, fanya kile unataka. Hii si kwa ndoa tu, hata masuala mengine ya maisha.

Vijana wengi wakitaka kuoa wanakimbizwa kweli, wanakubali kuumia ama kuumiza wengine kiuchumi kisha wanaachwa hawana kitu zaidi ya suti na shela walilonunuliwa siku ya harusi.Unafanyaje harusi ya milioni 10, halafu baada ya miezi michache mkeo anakwenda kujifungua unakopa hela kwa shiiida, unakopa hela ya kodi ya nyumba kwa shiiida? Cha kushangaza wakati huo huchangiwi tena!

Waafrika tukitukanwa na kina Trump tunakasirika bure, tuna shida.

Kiongozi hadi Mtu anapewa Gari aina ya IST kuwa iwe tu ya Wafanyakazi wake wa Ndani wakati Sisi wengine hata uwezo tu wa Kuinunua hiyo IST ili tutambe nayo Mtaani hatuwezi huoni kama hii ni dharau na huku ni kuvunjana Moyo?
 
Mwisho wa siku mwanamke anableed kama kawaida.

Makubwa! Kwani kuna Mwanaume / Binadamu asiyejua kuwa Kimaumbile na Kiumbwaji kila Mwanamke anapa Hedhi ( Bleed / Menstruation ) ndani ya Mwezi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom