mkalamo
JF-Expert Member
- Sep 7, 2013
- 324
- 347
CCM MAHMUMU, CHALIII KIFO CHA MENDEEEE;
Ameandika Malisa J.
Tunapotafuta madaraka ya kisiasa tunatumia mbinu mbalimbali, lakini ni muhimu kutumia mbinu ambazo hazitaharibu mahusoano yetu na Mungu wala hazitadhalilisha imani ya wengine.
Mzee wangu Harrison Mwakyembe hiki unachokifanya Kyela kutumia makanisa kama "platform" ya kufanya vikao vya chama chako si sahihi hata kidogo. Sikemei kwa kuwa wewe ni CCM, hasha! Hata Mbowe angefanya hivi ningekemea pia. Tena kwa nguvu kubwa zaidi.
Mimi kama Mkristo nimefundishwa kuheshimu hekalu la BWANA. Hata Yesu alipokuta watu wanafanya biashara hekaluni alipindua meza zao na kumwaga bidhaa zao chini. Akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi (Mathayo 21:13).
_
Sasa wewe umegeuza kanisa kuwa kijiwe cha siasa. Hadi eneo la madhabahu umegeuza "high table" ya viongozi kukaa na kuzungumza na wanachama wenu? Vitambaa vya kupamba madhabahu vimeondolewa na kuwekwa vitambaa vya chama chako. Mzee wangu umelinajisi kanisa. Mbaya zaidi wewe ni Mkristo tena uliyeokoka. Tukueleweje?
Kuna maeneo mengi hapo Kyela mngeweza kukutana na kupanga mipango yenu si lazima kuipangia kanisani. Mngeweza kukodi ukumbi au mkatumia kumbi za mashuleni (sekondari na vyuo) ambazo mngeweza kuziomba na kupanga mipango yenu badala ya njia hii ya kulinajisi kanisa. Tafadhali tubu, na tafuta njia nyingine ya kukutana na watu wako. Usilazimishe hasira ya Mungu ikawaka juu yako.!
As written by Malisa J.
Ameandika Malisa J.
Tunapotafuta madaraka ya kisiasa tunatumia mbinu mbalimbali, lakini ni muhimu kutumia mbinu ambazo hazitaharibu mahusoano yetu na Mungu wala hazitadhalilisha imani ya wengine.
Mzee wangu Harrison Mwakyembe hiki unachokifanya Kyela kutumia makanisa kama "platform" ya kufanya vikao vya chama chako si sahihi hata kidogo. Sikemei kwa kuwa wewe ni CCM, hasha! Hata Mbowe angefanya hivi ningekemea pia. Tena kwa nguvu kubwa zaidi.
Mimi kama Mkristo nimefundishwa kuheshimu hekalu la BWANA. Hata Yesu alipokuta watu wanafanya biashara hekaluni alipindua meza zao na kumwaga bidhaa zao chini. Akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi (Mathayo 21:13).
_
Sasa wewe umegeuza kanisa kuwa kijiwe cha siasa. Hadi eneo la madhabahu umegeuza "high table" ya viongozi kukaa na kuzungumza na wanachama wenu? Vitambaa vya kupamba madhabahu vimeondolewa na kuwekwa vitambaa vya chama chako. Mzee wangu umelinajisi kanisa. Mbaya zaidi wewe ni Mkristo tena uliyeokoka. Tukueleweje?
Kuna maeneo mengi hapo Kyela mngeweza kukutana na kupanga mipango yenu si lazima kuipangia kanisani. Mngeweza kukodi ukumbi au mkatumia kumbi za mashuleni (sekondari na vyuo) ambazo mngeweza kuziomba na kupanga mipango yenu badala ya njia hii ya kulinajisi kanisa. Tafadhali tubu, na tafuta njia nyingine ya kukutana na watu wako. Usilazimishe hasira ya Mungu ikawaka juu yako.!
As written by Malisa J.