Habari zenu wapendwa, Jamani naomba mnisaidie nina tatizo dogo tu ambalo kadri siku zinavoenda naona linanikwaza, mume wangu kila nikirudi home kutoka job au popote tu lazima atavizia handbag yangu ataipekua, nimeshamkutia karibia mara 15 sikumuuliza wala sikuchukia, juzi nimemkutia tena na hafanyi hivo mbele yangu anapekua kwa usiri hivo ata kumkutia inakuwa ni bahati tu, hiyo ya juzi nilikuwa nimetoka chuo nikaenda kuweka handbag room, nimerudi sitting room nimekaa kama dakika 5 tu akaja nayeye alikuwa chumbani, akachungulia pale sitting room kaniona niko busy na mtoto akarudi tena chumbani, namie hapohapo nikaingia chumbani nikamkuta tena busy anachambua handbag yangu, jamani ata kama kuna kitu anatafuta kwa mara hizo zote angekuwa ameshakipata, mimi binafsi nachukia na nilishawai kumwambia karibuni tu kama mara ya 13 hivi kuwa kwanini unapenda kufungua handbag yangu, unatafuta nin nikamuuliza vipi mimi nikiwa nakagua mifuko yako ya suruali kila ukirudi utajisikiaje maana wanaume hawabebi handbag, nikamwambia naomba uwe na imani na mimi hili jambo kwakweli linanikwaza, tangia nimemwambia hiyo juzi kaninunia mpaka leo hii eid imepita kimyakimya tu, jamani nisaidieni nifanye nini ili huyu mtu awe na imani namm au anatafuta sababu?
Shosti huyo hajiamini kama yuko peke yake.lakini kwakweli nitabia mbaya sana mwanamme kufungua Handbag ya mkewe
malezi gani hayo alolelewa? tena usimcheke bora ajue kama hupendi na usichoke kusema,ama sivyo ukimuachia atataka akupekua mpaka kwenye chupi ajue kama umelala namwengine au laa.
we mstaarabu mi wa kwangu nikirudi nikiwa nimeutwika ananisachi wakati nakoroma.. kumbe hajui watakatifu tuko wachacheNaiman tupo wengi tunaokerwa na hali hii ,mimi mume wangu ana the same tabia mimi sijawahi kumwuliza ila naona nitaanza kwani mimi sijawahi hata kugusa pochi yake unless kama natafuta kitu na awe amenituma
Jiwe nimesahau tu kukujulisha ya simu, anaanzaga katika handbag anamalizia katika simu, tena simu ndio never miss, na wakati huohuo ana password ya yahoomail yangu, na anapassword ya fb pia, kwaiyo anapita huko kote daily japo sikwaziki katika hivo maana password nimempa mwenyewe
Jiwe nimesahau tu kukujulisha ya simu, anaanzaga katika handbag anamalizia katika simu, tena simu ndio never miss, na wakati huohuo ana password ya yahoomail yangu, na anapassword ya fb pia, kwaiyo anapita huko kote daily japo sikwaziki katika hivo maana password nimempa mwenyewe
Ok pole maadam ushamwambia ukweli mwache nafikiri kuna kitu anahisi juu yako ndio anatafuta ukweli jitahidi kumvumilia atachoka kufwatilia mwenyewe ataacha. password ya huku hujampa? tusije kuPM kumbe ni yeye tukakuharibia!!
hizi ni zangu changanya na za kwakoDuh hii kiboko kabisa, asante kwa ushauri amsterdam
Mpitanjia, naona huyu mtu kwa hali hii aliyojiwekea inawezekana ata akikaa offisini ananiwazia mabaya tu mda wote, sasa hii hali itakuja kumuathiri bila sababu ya msingi
Nawe mwombe password zake za simu, emails zote uone kama utapewa.... huyo mumeo anawivu ambao mie nauita ni wa kitoto kwanini hajiamini yaelekea anayoyafanya yeye huko nje wewe huyajui anadhani nawe unayafanya na ndio maana kutwa kiroho chake kiko juu kwa kukuwazia mabaya.... mkanye na usichoke kumkanya kwani anakuja kuathhirika kisaikolojia kwa kuhofia vitu ama mambo amabayo hayawazii kuyafanya.
iko siku ukitaka kutoka ama akiwa anatoka atakagua chupi uliovaa asubui ndio atakayo kukuta nayo jioni ukitaka kuoga lazima uombe ruhusa maana ukioga kubadilisha kabla hajrudi kosa....