Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

1466631354457-jpg.359148


Mbetini,
Kwanza nakushukuru kwa kuileta picha hii hadharani.
Mimi ndiye mtu wa kwanza kuiona picha hii nje ya wenyewe.

Hii picha nilipewa na watoto wa Sheikh Abdallah Chaurembo
katika miaka ya 1980 na mimi nnilifanya mipango ipatikane nakala
yenye ubora na hilo lilifanyika.

Picha hii ilipigwa 1956 shambani kwa Sheikh Abdallah Chaurembo
Mtoni Dar es Salaam.

Ukoo wa Chaurembo una kawaida ya kufanya hawli kila mwaka na hii
inaendelea hadi leo

Katika hawali ya mwaka ule Mwalimu Nyerere alialikwa.
Pamoja na Nyerere kuna watu wengi maarufu katika picha hiyo.

Nyerere amekaa katika ya Liwali Ahmed Saleh kushoto na Sheikh
Bilal Mshoro
kulia.

Yupo Rajab Diwani, Liwali Ahmed Saleh, Sheikh Bilal Mshoro
kutoka Tabora, Sheikh Ramadhani Abbas, Saleh Muhsin huyu alikuwa
TANU kisha akatoka pamoja na Zuberi Mtemvu kuunda Tanganyika
African Congress (ANC) mwaka wa 1958 kufuatia Uchaguzi wa Kura Tatu,
katika watoto waliokaa chini yuko Said Mahfoudh mmoja wa vijana wa
kwanza kuingia Chuo Kikuucha Dar es Salaam katika miaka ya awali ya
1960.

Hii picha ilipotea kwa miaka zaid ya 20 hata wenyewe akina Chaurembo
wakawa hawana nakala ya picha hii.

Nimefurahi kuiona tena hii picha.
Alhamdulilah.

Nimeiweka picha hii katika blog yangu:
Mohamed Said: KUTOKA JF: HAKUNA PICHA INAYOELEZA HISTORIA YA WAISLAM NA MWALIMU NYERERE KAMA HII
Ahlan wasaala....

CC: Yericko Nyerere
 
Maalim wangu Mohamed Said.
Mimi ndiyo wa kukushukuru wewe,kwa kifupi baada ya kusoma utambuzi wa kwenye hiyo picha nimetoka machozi sijui kwanini wallahi, Sheikh Chaurembo wanae nafahamiana nao sana sikujua kama hii picha walikupa wewe kusema kweli nilipoipata ni Studio ya picha maeneo ya kisutu na nilipewa baada ya kushindwa kuwatambua waliopiga hiyo picha nikaomba nipewe ili kutafuta nani atawatambua na bahati kitandawili umekifumbua ahsante sana. Alhamdulillahi
Maalim Sheikh Bilali Mshoro wa Tabora ni Mzee wangu mmoja wa watoto wake Amefariki
Mwaka huu Mwezi March Marehemu Salehe Mshoro alikuwa Mkurugenzi wa fedha TRA tumesoma wote Tabora,kaka yake ni Prof. Mshoro yupo chuo cha ardhi.
Kingine Said Mahfoudh ni mjomba wangu na nitamtafuta kupata habari zaidi.

Maalim Faiza alisema hii picha “inaongea maneno Milioni" hakika she is absolutely right.
Maalim mi nipo tayari kuitoa kwako hii Amana iliyopotea zaidi ya miaka ishirini uitunze isije kupotea tena.
Mtebetini,
Nakuomba pia mtafute kaka Idd Churembo lazima atawajua
waliokuwa kwenye picha.

Mimi pia nikimfahamu Sheikh Bilal Mshoro na kitu kimoja Allah
alichomjaaliwa ni kuwa na watoto wenye akili nzuri sana darasani.

Alikuwapo mwanae mmoja Idara ya Uchumi Chuo Kikuu Mlimani
na yeye sasa ni marehemu.

Said Mahfoudh hata mimi namfahamu toka utoto wangu.

Yeye ni mpwa wa Mwalimu Adam aliyekuwa akisomesha Al Jamiatul
Islamiyya Muslim School.

Kwa hisani yako ukipata hizo taarifa tafadhali tuletee hapa Majlis na sisi
tufaidi.
 
1466631354457-jpg.359148


Mbetini,
Kwanza nakushukuru kwa kuileta picha hii hadharani.
Mimi ndiye mtu wa kwanza kuiona picha hii nje ya wenyewe.

Hii picha nilipewa na watoto wa Sheikh Abdallah Chaurembo
katika miaka ya 1980 na mimi nnilifanya mipango ipatikane nakala
yenye ubora na hilo lilifanyika.

Picha hii ilipigwa 1956 shambani kwa Sheikh Abdallah Chaurembo
Mtoni Dar es Salaam.

Ukoo wa Chaurembo una kawaida ya kufanya hawli kila mwaka na hii
inaendelea hadi leo

Katika hawali ya mwaka ule Mwalimu Nyerere alialikwa.
Pamoja na Nyerere kuna watu wengi maarufu katika picha hiyo.

Nyerere amekaa katika ya Liwali Ahmed Saleh kushoto na Sheikh
Bilal Mshoro
kulia.

Yupo Rajab Diwani, Liwali Ahmed Saleh, Sheikh Bilal Mshoro
kutoka Tabora, Sheikh Ramadhani Abbas, Saleh Muhsin huyu alikuwa
TANU kisha akatoka pamoja na Zuberi Mtemvu kuunda Tanganyika
African Congress (ANC) mwaka wa 1958 kufuatia Uchaguzi wa Kura Tatu,
katika watoto waliokaa chini yuko Said Mahfoudh mmoja wa vijana wa
kwanza kuingia Chuo Kikuucha Dar es Salaam katika miaka ya awali ya
1960.

Hii picha ilipotea kwa miaka zaid ya 20 hata wenyewe akina Chaurembo
wakawa hawana nakala ya picha hii.

Nimefurahi kuiona tena hii picha.
Alhamdulilah.

Nimeiweka picha hii katika blog yangu:
Mohamed Said: KUTOKA JF: HAKUNA PICHA INAYOELEZA HISTORIA YA WAISLAM NA MWALIMU NYERERE KAMA HII
Wanamajlis,
Naomba mtazame hii video hapo chini kipindi nilichofanya na Azam TV
Nyerere Day 2015:

<iframe width="560" height="315" src="" frameborder="0" allowfullscreen></iframe>
 
Mzee wangu Mohamed Said shikamoo
Darsa unazotoa hapa majlis ni za hali ya juu sana.
Unanikumbusha darsa ya tafsiri ya sheikh Hemed Bin jumaa bin Hemed
wakati alipokuwa akitafsiri surati yusuf.
Hakika masikio yangu yalikuwa yakisikia kitu kipya ambacho
sikuwahi kusikia kabla.
Ndivyo unavyoweka mambo hapa majlis.
Ni fadhaa na ugeni wayasikiyapo uyaelezayo
ndipo taharuki, hamaki na sintofahamu inapowajaa.
Lakini wataelewa inshallah.
Mungu akulipe kheri umeacha athari kubwa sana
kwa vizazi na vizazi kwa siku za usoni.
Nguruvi3,
Mtu wa kwanza kuitangaza TANU hakuwa Nyerere.

TANU ilitangazwa na Ramadhani Mashado Plantan
kupitia gazeti lake, ''Zuhra.''

Hadharani mtu wa kuitangaza TANU alikuwa Bi. Titi.

Mkutano huu ulifanyika Mnazi Mmoja na Nyerere
hakuweko alikuwa Musoma.
 
View attachment 359174
Wazee wa Dar es Salaam katika Baraza la Wazee wa TANU na Mwalimu Julius Nyererekatika Uchaguzi Mkuu wa 1962. Masikitiko ni kuwa mashujaa hawa hadi leo nchi haijawatambua isipokuwa Nyerere peke yake. Kushoto ni Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana, Julius Nyerere na Mshume Kiyate, picha ilipigwa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 1962.

Mashujaa kwa lipi!? Inawezekana walikuwa wacheza bao nje ya ofisi za TANU, au wakereketwa tu, kama walivyo manyumbu wengine wa vyama vya siasa.....!

Hawana mchango wowote zaidi ya ushabiki, hivyo kutokea kwenye picha haina maana kuwa ulichangia chochote katika harakati za ukombozi...! Hata wewe unaweza kuingia kwenye kundi la wachezaji wa Yanga kushangilia ushindi, ukatokea kwenye picha! Hiana maana kuwa na wewe ulikuwa uwanjani.!
 
Mashujaa kwa lipi!? Inawezekana walikuwa wacheza bao nje ya ofisi za TANU, au wakereketwa tu, kama walivyo manyumbu wengine wa vyama vya siasa.....!

Hawana mchango wowote zaidi ya ushabiki, hivyo kutokea kwenye picha haina maana kuwa ulichangia chochote katika harakati za ukombozi...! Hata wewe unaweza kuingia kwenye kundi la wachezaji wa Yanga kushangilia ushindi, ukatokea kwenye picha! Hiana maana kuwa na wewe ulikuwa uwanjani.!
Ndakilawe,
Ni bahati mbaya una kibri.
Kibri kinatia ujinga na kinaangamiza.

Kibri kinatoa adabu.

Ukitaka kuamini maneno yangu mpe mtu asome maneno yako
uliyoandika kisha muulize.

Lakini mimi siamini kama mama yangu hakukupa malezi mema.
Hao wazee ndiyo waliompeleka Nyerere UNO mwaka wa 1955.

Naamini hili hukuwa unalijua kabla ya leo ndiyo maana ukaja na
matusi na kejeli.
 
Mzee wangu Mohamed Said shikamoo
Darsa unazotoa hapa majlis ni za hali ya juu sana.
Unanikumbusha darsa ya tafsiri ya sheikh Hemed Bin jumaa bin Hemed
wakati alipokuwa akitafsiri surati yusuf.
Hakika masikio yangu yalikuwa yakisikia kitu kipya ambacho
sikuwahi kusikia kabla.
Ndivyo unavyoweka mambo hapa majlis.
Ni fadhaa na ugeni wayasikiyapo uyaelezayo
ndipo taharuki, hamaki na sintofahamu inapowajaa.
Lakini wataelewa inshallah.
Mungu akulipe kheri umeacha athari kubwa sana
kwa vizazi na vizazi kwa siku za usoni.
Dos Santos,
Allahuma Amin ndugu yangu.
 
Ndakilawe,
Ni bahati mbaya una kibri.
Kibri kinatia ujinga na kinaangamiza.

Kibri kinatoa adabu.

Ukitaka kuamini maneno yangu mpe mtu asome maneno yako
uliyoandika kisha muulize.

Lakini mimi siamini kama mama yangu hakukupa malezi mema.
Hao wazee ndiyo waliompeleka Nyerere UNO mwaka wa 1955.

Naamini hili hukuwa unalijua kabla ya leo ndiyo maana ukaja na
matusi na kejeli.
Walimpeleka kwa nini, na kwann hawakwenda wao!

Jibu ni raisi, kwa sababu ya upeo wao mdogo, wasingeweza kuzungumza chochote
 
Mashujaa kwa lipi!? Inawezekana walikuwa wacheza bao nje ya ofisi za TANU, au wakereketwa tu, kama walivyo manyumbu wengine wa vyama vya siasa.....!

Hawana mchango wowote zaidi ya ushabiki, hivyo kutokea kwenye picha haina maana kuwa ulichangia chochote katika harakati za ukombozi...! Hata wewe unaweza kuingia kwenye kundi la wachezaji wa Yanga kushangilia ushindi, ukatokea kwenye picha! Hiana maana kuwa na wewe ulikuwa uwanjani.!
Mara nyingi ukikaa kimya huwa ni njia sahihi kuficha ujinga.
Laiti hapa usinge tomboka kama hivi wala tusinge jua ujinga wako.
Kaa kimya ufiche ujunga wako.
 
Walimpeleka kwa nini, na kwann hawakwenda wao!

Jibu ni raisi, kwa sababu ya upeo wao mdogo, wasingeweza kuzungumza chochote
Wewe kweli mweupe katika historia.. Walishaenda1950 lakini kwasababu walikuwa na imani mmoja walikataliwa kwahivyo wakarudi kujipanga.

Alipokuja mwalimu nyerere ndo akakaribishwa katika chama kwa kuangalia uzalendo zaidi.

Hata lile kusudio lililosomwa kule UNO na mwalimu nyerere lilikuwa tayari limeandikwa na wazee wetu..!
 
Wewe kweli mweupe katika historia.. Walishaenda1950 lakini kwasababu walikuwa na imani mmoja walikataliwa kwahivyo wakarudi kujipanga.

Alipokuja mwalimu nyerere ndo akakaribishwa katika chama kwa kuangalia uzalendo zaidi.

Hata lile kusudio lililosomwa kule UNO na mwalimu nyerere lilikuwa tayari limeandikwa na wazee wetu..!

Hao wazee wako waliandika kwa Elimu ipi, wakati hata kuandiaka a e i o u walikuwa hawajui? Mbona mnapenda sana kupotosha jamii..

Hayo ndio mnayofundishwa kwenye mijumuiko yenu, angali mkijua ni uongo kabisa. Na ukiangalia vitabu vyote mnavyodai ni historia nzuri, vimendikwa na hao hao wanaopinga watu wengine.

Try to be a lillte bit Meticulous
 
Mara nyingi ukikaa kimya huwa ni njia sahihi kuficha ujinga.
Laiti hapa usinge tomboka kama hivi wala tusinge jua ujinga wako.
Kaa kimya ufiche ujunga wako.
Tumia akili kidogo, sio kila unachoambiwa unameza tu! Hata wewe una uwezo kufikiri na kuamua
 
Hao wazee wako waliandika kwa Elimu ipi, wakati hata kuandiaka a e i o u walikuwa hawajui? Mbona mnapenda sana kupotosha jamii..

Hayo ndio mnayofundishwa kwenye mijumuiko yenu, angali mkijua ni uongo kabisa. Na ukiangalia vitabu vyote mnavyodai ni historia nzuri, vimendikwa na hao hao wanaopinga watu wengine.

Try to be a lillte bit Meticulous
Na chama cha TAA hadi TANU walianzisha na elimu ipi..?
 
Walimpeleka kwa nini, na kwann hawakwenda wao!

Jibu ni raisi, kwa sababu ya upeo wao mdogo, wasingeweza kuzungumza chochote
Ndakilawe,
Hiki ni kisa cha kweli.

Kapita mtu mbele ya watu wanaojiona wao kwa kibri chao wanajiona
ni bora dharau imewajaa wakamuita yule mpita njia kwa dharau na
kumbwambia kuwa wanataka kumuuliza swali.

Kwa kejeli, kibri na dharau kama unavyoonyesha wewe wakamuuliza
swali hili, ''Tuambie ni kitu gani bora duniani?''

Yule mja muungwana akawaambia,''Mbona mmekosea kuuliza swali
lenu?''

Pale pale wale watu kwa kibri wakashtuka vipi huyu mtu dhalili anaweza
kutusahihisha sisi?

Wakamuuliza,''Tumekosea vipi?''
Akawaambia,''Mlitakiwa muulize hivi ni kitu gani bora duniani na akhera?''

Wale nduguzo watu wa kibri wakawa hawana pa kutokea isipokuwa kuuliza
swali lao kama walivyofunzwa.

Wakauliza kama walivyosomeshwa na mja mwema.

Mja mwema akawaambia, ''Mnataka nikujibuni kishariri au kwa lugha ya
kawaida?''

Ahlal kibri hapa wakawa sasa hamaki zimewapanda wakamwambia tujibu
upendavyo.

Mja mwema akawaambia, ''Kitu bora duniani na akhera ni tabia njema
duniani watu watakupenda na kesho akhera Mungu atakulipa mema.''

Huyu aliyeniifunza haya ni Maalim wangu Sheikh Haruna.
 
Hao wazee wako waliandika kwa Elimu ipi, wakati hata kuandiaka a e i o u walikuwa hawajui? Mbona mnapenda sana kupotosha jamii..

Hayo ndio mnayofundishwa kwenye mijumuiko yenu, angali mkijua ni uongo kabisa. Na ukiangalia vitabu vyote mnavyodai ni historia nzuri, vimendikwa na hao hao wanaopinga watu wengine.

Try to be a lillte bit Meticulous
Ndakilawe,
Nakuhurumia kwa kuwa nakusoma hadi ndani ya nafsi yako.
Nimekuonya nimekwambia kibri kinaleta ujinga na huangamiza.

Nakuona unakuja na Kiingereza sasa.

Mimi nimaekuandikia nina First Class Merit Pass English Oral
Cambridge 1970.

Nimekuwa katika mradi wa Oxford University Press wa kusomesha
lugha ya Kiingereza na nimeandika katika mradi huo vitabu viwili.

Nilitiwa vile vile katika mradi wa Oxford University Press New York
na Harvard wa kuandika Dictionary of African Biography.

Mradi umekamilka 2011 na hizo kamusi volume 6 zimechapwa.

Sikuambii haya kujisifu ila nataka kukutanabaisha.
Jitulize tufanya mjadala wa staha.

Labda nikuulize kuhusu ilm.
Unauliza wazee wetu waliandika kwa elimu ipi.

Kwani ilm ina umbo na rangi ipi kiasi kuwa iweze kupendeza kwa
watu wapi na kwa kuchukulika kwa mbeleko ipi?

Hivi unajua kuwa Johan Krapf alipofika Vuga kwa Chief Kimweri
mwakawa 1848 alimkuta yeye na wanae wote wanajua kuandika
na kusoma na ni Waislam?

Krapf alipigwa na mshtuko kwani huko alikotoka aliambiwa unakwenda
katika nchi ya washenzi.

Kafika Usambaa kapokewa na watu walioavaa vyema na wanajua kusoma
na kuandika.

Uislam hauendi pamoja na ujinga.
Uislam unaambatana na elimu.

Ilm Tanganyika haikuja na wamishionari.
Ilm Tanganyika iliingia na Uislam.

Wazee wetu walikuwa wasomi wazuri sana.
Maalim wangu Sheikh Haruna ni kati ya wasomi wa sifa.

Punguza kibri na kudhani unajua ujifunze.
 
Ndakilawe,
Nakuhurumia kwa kuwa nakusoma hadi ndani ya nafsi yako.
Nimekuonya nimekwambia kibri kinaleta ujinga na huangamiza.

Nakuona unakuja na Kiingereza sasa.

Mimi nimaekuandikia nina First Class Merit Pass English Oral
Cambridge 1970.

Nimekuwa katika mradi wa Oxford University Press wa kusomesha
lugha ya Kiingereza na nimeandika katika mradi huo vitabu viwili.

Nilitiwa vile vile katika mradi wa Oxford University Press New York
na Harvard wa kuandika Dictionary of African Biography.

Mradi umekamilka 2011 na hizo kamusi volume 6 zimechapwa.

Sikuambii haya kujisifu ila nataka kukutanabaisha.
Jitulize tufanya mjadala wa staha.

Labda nikuulize kuhusu ilm.
Unauliza wazee wetu waliandika kwa elimu ipi.

Kwani ilm ina umbo na rangi ipi kiasi kuwa iweze kupendeza kwa
watu wapi na kwa kuchukulika kwa mbeleko ipi?

Hivi unajua kuwa Johan Krapf alipofika Vuga kwa Chief Kimweri
mwakawa 1848 alimkuta yeye na wanae wote wanajua kuandika
na kusoma na ni Waislam?

Krapf alipigwa na mshtuko kwani huko alikotoka aliambiwa unakwenda
katika nchi ya washenzi.

Kafika Usambaa kapokewa na watu walioavaa vyema na wanajua kusoma
na kuandika.

Uislam hauendi pamoja na ujinga.
Uislam unaambatana na elimu.

Ilm Tanganyika haikuja na wamishionari.
Ilm Tanganyika iliingia na Uislam.

Wazee wetu walikuwa wasomi wazuri sana.
Maalim wangu Sheikh Haruna ni kati ya wasomi wa sifa.

Punguza kibri na kudhani unajua ujifunze.
Sheikh Muhamed huyu Ndakilawe atakusumbuwa sana huyu ni mtu asie jua na hajui kama hajui.
Mtu wa aina hii labda umuyayushe umtengeneze upya kitu kisicho wezekana maana huyu ni kiumbe sio chombo.
Huyu niwakumpuuza au kama unataka kumsaidia basi muombee dua.
 
Sheikh Muhamed huyu Ndakilawe atakusumbuwa sana huyu ni mtu asie jua na hajui kama hajui.
Mtu wa aina hii labda umuyayushe umtengeneze upya kitu kisicho wezekana maana huyu ni kiumbe sio chombo.
Huyu niwakumpuuza au kama unataka kumsaidia basi muombee dua.
Sahimtz,
Marehemu mama yangu alikuwa na msemo wake akipenda kuutumia,
''Dua tufanye na mchele mkononi.''

Maana yake ni sawa na ile hadith ya kumfunga ngamia kisha uombe
dua.

Tuna wajibu wa kuwasomesha watu kama hawa kwa sababu kwa miaka
mingi walikuwa katika kiza hawaijui historia ya nchi yao wenyewe.

Hizi kejeli unazoziona hapa ni matokeo ya mshtuko uliowapiga baada ya
ukweli kuwadhihirikia.
 
Mashujaa kwa lipi!? Inawezekana walikuwa wacheza bao nje ya ofisi za TANU, au wakereketwa tu, kama walivyo manyumbu wengine wa vyama vya siasa.....!

Hawana mchango wowote zaidi ya ushabiki, hivyo kutokea kwenye picha haina maana kuwa ulichangia chochote katika harakati za ukombozi...! Hata wewe unaweza kuingia kwenye kundi la wachezaji wa Yanga kushangilia ushindi, ukatokea kwenye picha! Hiana maana kuwa na wewe ulikuwa uwanjani.!
Unajipunja bure kwa umri wako unatakiwa utulizane ujifunze historia ya Tanganyika.
 
Back
Top Bottom