kadovela
JF-Expert Member
- Jan 31, 2016
- 471
- 679
Katika rukaruka za ujana nishawahi kutembea na wanawake ambao kuna watu wanawahisi ni waathirika wa HIV, hii kitu ilinifanya nijihisi mfu ninaetembea na nikawa muoga sana kwenda kupima, lakini katika kipindi hicho chote utendaji wangu katika lile tendo ulikuwa mzuri japo nilikuwa nahisi kama nawaambukiza mabinti wa watu bila hatia maana mimi si mfuasi wa condom.
Zoezi la kutoa damu kwa mtu muhimu kwangu lilinifanya nisiwe na namna ya kukwepa kupima, baada ya kupima na kugundulika mzima nikatoa damu kwa mtu muhimu, lakini ile hali ya kujua ni salama imenifanya kuwa na hofu na kufanya mapenzi kiasi cha kukosa hamu kabisa.
Wataalamu wa saikolojia na wenye uzoefu juu ya hali hii naomba msaada wa kujinasua katika hili maana hata mpenzi wangu kaanza kunihisi vibaya.
Zoezi la kutoa damu kwa mtu muhimu kwangu lilinifanya nisiwe na namna ya kukwepa kupima, baada ya kupima na kugundulika mzima nikatoa damu kwa mtu muhimu, lakini ile hali ya kujua ni salama imenifanya kuwa na hofu na kufanya mapenzi kiasi cha kukosa hamu kabisa.
Wataalamu wa saikolojia na wenye uzoefu juu ya hali hii naomba msaada wa kujinasua katika hili maana hata mpenzi wangu kaanza kunihisi vibaya.