DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Nzega Vijijini (CCM) Dkt. Hamis Kigwangalla ameshauri kutafutwa kwa namna itakayowezesha kufutwa kwa kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu
Katika machapisho yake ya septemba 30.2025 aliyoweka kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram Kigwangalla ameandika, "Tena kama mkifikiria vizuri zaidi mtatekeleza dira ya Mama Samia Suluhu Hassan ya 4R's (Maridhiano, Mabadiliko, Kujenga upya na uvumilivu) na slogan yake ya 'Kazi na Utu' kwa kutafuta kifungu kitakachoisaidia Mahakama kuifuta kesi inayomkabili ndugu Tundu Antipas Mughwai Lissu"
Katika hatua nyingine, Kigwangalla ambeye pia ni Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii amesisitiza kutopuuzwa kwa sauti za wananchi juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea nchini
“Watanzania wamechimba mkwara (kuhusu madai ya kutaka kuandamana na kuzuia uchaguzi), sote tunajua hawawezi kuandamana, lakini sauti yao imesikika, wamesema na tumewasikia, tusiwapuuze, tutoe uongozi, tuunganishe Taifa, tujenge" -Kigwangalla
Katika machapisho yake ya septemba 30.2025 aliyoweka kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram Kigwangalla ameandika, "Tena kama mkifikiria vizuri zaidi mtatekeleza dira ya Mama Samia Suluhu Hassan ya 4R's (Maridhiano, Mabadiliko, Kujenga upya na uvumilivu) na slogan yake ya 'Kazi na Utu' kwa kutafuta kifungu kitakachoisaidia Mahakama kuifuta kesi inayomkabili ndugu Tundu Antipas Mughwai Lissu"
Katika hatua nyingine, Kigwangalla ambeye pia ni Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii amesisitiza kutopuuzwa kwa sauti za wananchi juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea nchini
“Watanzania wamechimba mkwara (kuhusu madai ya kutaka kuandamana na kuzuia uchaguzi), sote tunajua hawawezi kuandamana, lakini sauti yao imesikika, wamesema na tumewasikia, tusiwapuuze, tutoe uongozi, tuunganishe Taifa, tujenge" -Kigwangalla