Hamad Rashidi ndiye aliyeisaliti Zanzibar

Hamad Rashidi ndiye aliyeisaliti Zanzibar

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,288
Reaction score
38,908
Kura mbili za rasimu zimepatikana kutoka kwa Hamad Rashidi mbunge wa Wawi imefahamika mjini Dodoma leo.

Katika hali ya kushangaza, Hamad Rashidi ndiye aliyepewa jukumu la kuwanunua wabunge wawili wa CUF (majina yanahifadhiwa) ili kukidhi akidi iliyotakiwa.

Wabunge hao ambao walikuwa wajumbe wa bunge maalum la katiba kabla ya kususia waliahidiwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania kila mmoja ili kufanikisha mpango huo. Aidha Hamad ndiye aliyepewa jukumu hilo la kuwashawishi huku wale waliopiga kura za siri za 'HAPANA' wakiwekwa kitako na Pinda pamoja na Seif Idd ili kukamilisha mpango huo.

Hamad Rashidi kwa sasa ndiye mtu anayejadiliwa zaidi hapa Dodoma kwa sasa kutokana na tukio hilo.

Updates...........
Hamadi Rashidi katika mahojiano na MWANANCHI JUMAPILI amekiri kuwashawishi wajumbe hao ili waipitishe rasimu ila amekana kuwanunua "Ni ushawishi wangu tu ili kuwakomoa CUF" alijigamba Rashidi.

Ila ukweli ni kuwa wajumbe hao waliahidiwa kiwango hicho cha fedha.

Pia wapo wa kura za siri waliopiga kura za 'HAPANA' takribani wajumbe 17 ingawa Hamadi Rashidi anatudanganya kuwa ni yeye aliwashawishi wapige kura za siri na wote walipiga za 'NDIYO' na anadai eti baada ya kupiga walikuwa wakimuonyesha ili athibitishe! Huu ni uongo wa wazi kabisa!!!!!
 
SASA kwanini usiyataje hayo majina, unayaficha ili iweje. kama huweki majina habari yako ni kipofu.
 
Huyu jamaa hafai hata chembe. Rushwa hadi kwenye katiba. Watanzania tunakataa upuuzi huu.
 
duuuuh 250m au kuweka taifa rehani..zaidi ya watu 40million walikuwa wanasubiri matokeo ya hyo kaatiba ila watu wameingia na tamaa ya pesa na kuharibu kabsa,hii style ya ufisadi itazidi kuitafuna taifa karne hadi karne kwa kweli tutabaki kuwa maskini na wachache kuwa matajiri kwa werevu wao mdogo ambao hata maskini angaata hiyo bahati angetajirika...watanzania tuna amani ya uwoga period
 
Kama ushahidi huo upo nenda mahakamani watanzania tuna penda sana propaganda bila kufahamu si afya kwenye jamii ambayo tunataka kuwa na mafanikio kiuchumi,afya na elimu ukweli ndio jambo la msingi na lenye nguvu
 
Yule mbunge wa mahakama? Isije mwataka kumuua kisiasa! ACT
 
Millioni 250 kwa maisha ya watanzania wa sasa kuzikataa ingekuwa ni jaribu gumu kwa wengi. Najua wengi tutabeza tu na kuonyesha uchungu tulionao kwa taifa letu ila usiombe yakukute ndugu yangu. Afu kukomesha unakuta jamaa washa andaa milioni 125 zipo kwenye mabox au mifuko ya Rambo wanakwambia chukua hizi nusu afu kesho kutwa nusu Nyingine. Ndugu Zangu kuzikataa inahitaji moyo. Kuna vitu inabidi umuombe Mungu kabla ya kufanya uamuzi kwa hizi akili za kibinadamu kawaida tu yataka moyo.
 
Kura mbili za rasimu zimepatikana kutoka kwa Hamad Rashidi mbunge wa Wawi imefahamika mjini Dodoma leo.

Katika hali ya kushangaza, Hamad Rashidi ndiye aliyepewa jukumu la kuwanunua wabunge wawili wa CUF (majina yanahifadhiwa) ili kukidhi akidi iliyotakiwa.

Wabunge hao ambao walikuwa wajumbe wa bunge maalum la katiba kabla ya kususia waliahidiwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania kila mmoja ili kufanikisha mpango huo. Aidha Hamad ndiye aliyepewa jukumu hilo la kuwashawishi huku wale waliopiga kura za siri za 'HAPANA' wakiwekwa kitako na Pinda pamoja na Seif Idd ili kukamilisha mpango huo.

Hamad Rashidi kwa sasa ndiye mtu anayejadiliwa zaidi hapa Dodoma kwa sasa kutokana na tukio hilo.

Una maanisha Hamadi Rashi huyu huyu mbunge wa mahakama ya Wawi ni mjuaye mimi???
 

Attachments

  • RASHID.jpg
    RASHID.jpg
    21.4 KB · Views: 561
baada ya kufukuzwa uanachama sasa ameanza kusaliti alikozaliwa,hajui kwamba laana hiyo itakiandama kizazi chake chote na amesahau kwamba kwa sasa ccm wamemtumia kama kondom NA hawana haja nae tena
 
Wadau hebu tutafute namna Hamadi alivyokaa siku ya upigaji kura kama kweli angeweza kufanya haya anayojigamba nayo leo..Simple logic ni kuwa hata yeye Hamadi angepiga kura ya siri!! Ila kwenye kununua wabunge wa CUD ni kweli alifanya hivyo!!
 
Halafu Huyu jamaa inaonekana ana interest zake nyingi sana huku bara na kila mara anakuwa huku Dar anarandaranda na Benz ML yake.....inawezekana kabisa kapewa hela....ana nyumba yake kubwa pale Kawe inatizamana na ya Basil Mramba na zote zilikuwa zimekodishwa na kampuni ya kitapeli ya mawasiliano ya voice and data Tantel cjui kama sijakosea.
 
Akidi haijatimia kwa sababu wajumbe kutoka Zanzibar ni 212 lakini kura zilizopigwa zinaonyeshwa zilikuwa 219, hizi kura 7 za hewa zilitoka wapi? Kuna wajumbe 7 waliochaguliwa kinyemela ili kuhakikisha akidi inatimia? Ofisi ya Bunge na Sitta mbona wako kimya kuhusu hizi kura 7 ambazo hazijulikani zimetoka wapi?
 
Halafu Huyu jamaa inaonekana ana interest zake nyingi sana huku bara na kila mara anakuwa huku Dar anarandaranda na Benz ML yake.....inawezekana kabisa kapewa hela....ana nyumba yake kubwa pale Kawe inatizamana na ya Basil Mramba na zote zilikuwa zimekodishwa na kampuni ya kitapeli ya mawasiliano ya voice and data Tantel cjui kama sijakosea.

Voice and Data Communication mbona nijuavyo mimi ni mtandao fulani maarufu wa simu za kiganjani hapa Tz, inahusika vp na hilo? Naomba utujuze vizuri.
 
Nimesoma habar yake kwenye mwananchi yani jamaa hana kitu kichwan kabisaaa…!!! Anakubali kuwa kwel kafanya hvo alafu anajipongeza kama kazi ilikuwa ngumu sana ila anashukhuru mungu kwa kukamilisha…!! Alafu mwakan atajiunga na ADC na atagombea huko…!!!, sasa mtu kama huyu unamkaribisha kwwnye chama chako wann? Kumbe wakina MM wakowengi jamani…………!!!
 
Kura mbili za rasimu zimepatikana kutoka kwa Hamad Rashidi mbunge wa Wawi imefahamika mjini Dodoma leo.

Katika hali ya kushangaza, Hamad Rashidi ndiye aliyepewa jukumu la kuwanunua wabunge wawili wa CUF (majina yanahifadhiwa) ili kukidhi akidi iliyotakiwa.

Wabunge hao ambao walikuwa wajumbe wa bunge maalum la katiba kabla ya kususia waliahidiwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania kila mmoja ili kufanikisha mpango huo. Aidha Hamad ndiye aliyepewa jukumu hilo la kuwashawishi huku wale waliopiga kura za siri za 'HAPANA' wakiwekwa kitako na Pinda pamoja na Seif Idd ili kukamilisha mpango huo.

Hamad Rashidi kwa sasa ndiye mtu anayejadiliwa zaidi hapa Dodoma kwa sasa kutokana na tukio hilo.

Updates...........
Hamadi Rashidi katika mahojiano na MWANANCHI JUMAPILI amekiri kuwashawishi wajumbe hao ili waipitishe rasimu ila amekana kuwanunua "Ni ushawishi wangu tu ili kuwakomoa CUF" alijigamba Rashidi.

Ila ukweli ni kuwa wajumbe hao waliahidiwa kiwango hicho cha fedha.

Pia wapo wa kura za siri waliopiga kura za 'HAPANA' takribani wajumbe 17 ingawa Hamadi Rashidi anatudanganya kuwa ni yeye aliwashawishi wapige kura za siri na wote walipiga za 'NDIYO' na anadai eti baada ya kupiga walikuwa wakimuonyesha ili athibitishe! Huu ni uongo wa wazi kabisa!!!!!

Unahonga hicho kiasi ili kuwakomoa CUF? Kwani katiba inayopendekezwa ni ya CUF? Hiyo ni katiba ya CCM.
Kama Hamad Rashid aliwashawishi hao walipwe 250m na ccm.Je,yeye aliahidiwa sh ngapi?
 
Back
Top Bottom