Hamad Rashid ni mtaji maalum

Nionavyo mm, bara tunasapoti muungano kuliko wa visiwa.......hawaonyeshi kuujali ukilinganisha na huku, sasa wachache Kama hr wakijitokeza tuuu.....wanakua maadui hukoo kwao, hoja moja kubwa aliyoisema Hamad r. Ni ile ya maalim kutofanya kazi bara, although yy ni katibu mkuu wa taifa, sasa amekua sumu.....na problem nyingine ninayoiona Ni kwa wapmb wakishamuamini mtu baaasi wanaona hauwezi kukosea na wengi wao washaweka imani kwa maalim seif baaaasi!! Hawageuki hao.....
 
Hamada Rashid hawezi kamwe kuwa mtaji wa vita kandamizi dhidi ya uislamu. Ila najua ni mkakati maalumu wa kuigawanya pemba ikose nguvu ya cuf na hapo ndio utakuwa ni mwisho wa nguvu ya CUf Pemba. Chama kipya cha Hamad kitakuwa na nguvu kubwa katika..... lakini bado ana fursa ya kuhamia chadema kama nilivyodokeza awali...
 
Ni kazi nzito kujua na kuweza kusema kwa uhakika Kati ya Seif Sharif Hamad na Hamad Rashid nani anaongoza kwa uchu wa madaraka


Wote ni waroho wa madaraka hawana lolote Waislam watupu akina Barubaru hovyooooooooooooo
 
Uasi wa Hamad Rashid ndani ya CUF umepata uungwaji mkono usio wa kawaida katika vyombo vya habari Tanzania kama kwamba tukio kama hilo halijapata kutokea kwa vyama vyengine au ni mara ya mwanzo katika CUF.

Zaidi ya uungwaji mkono huo, sasa msajili wa vyama bwana Tendwa na Jaji Werema nao wameingilia kati kuonesha kutoridhishwa kwao na uamuzi madhubuti uliochukuliwa na uongozi wa CUF. Haipendezi kwa wanasheria hao kushikilia habari za mahakama ilhali viongozi wa CUF wameshasema hawakupokea amri ya mahakama.

Ukweli ambao wanasiasa na wanaJF hawapendi kuusema ni kuwa Hamad ni mtaji maalum wa kukivuruga CUF. Na kwanini iwe CUF? Ni mkakati wa kuimeza Zanzibar.Kwa upande mwengine CUF si chama cha kiislamu lakini kwa vile kimeasisiwa Zanzibar waislamu ni wengi na hii imekuwa nongwa. Katika mtazamo uliompana huu ni mwendelezo wa kuzima ushiriki wa waislamu katika siasa na hii ni vita ya kimataifa dhidi ya uislamu.

Huu mkorogo hata sielewi ni nini? Any way hiyo avatar yako tu inajitosha kufikisha ujumbe
 
Jamani acheni kusema sema bila kufikiria..Kwani Maalim Seif kuambiwa ukweli na kiongozi mwenzie ni kosa?? Kwani CUF kinakuja juu au kinazamaa??
Yeye Maalim kama mtendaji mkuu wa chama na Makamu wa kwanza wa Rais atatekelezaje shughulli za kichama??
Angalieni mbele na nyuma..i like this HR..ni kawa mwazi kuliko vita ya chini chini..Aliutaka ukatibu mkuu na akasema live..Sasa mtu kutoa mawazo yake anafukuzwa?? Ina Maana mwanachama haruhusiwi kushika wadhifa fulani kwenye chama zaidi ya mtu mwingine????

Some Signature yangu Chini..
 
Uasi wa Hamad Rashid ndani ya CUF umepata uungwaji mkono usio wa kawaida katika vyombo vya habari Tanzania kama kwamba tukio kama hilo halijapata kutokea kwa vyama vyengine au ni mara ya mwanzo katika CUF.

Zaidi ya uungwaji mkono huo, sasa msajili wa vyama bwana Tendwa na Jaji Werema nao wameingilia kati kuonesha kutoridhishwa kwao na uamuzi madhubuti uliochukuliwa na uongozi wa CUF. Haipendezi kwa wanasheria hao kushikilia habari za mahakama ilhali viongozi wa CUF wameshasema hawakupokea amri ya mahakama.

Ukweli ambao wanasiasa na wanaJF hawapendi kuusema ni kuwa Hamad ni mtaji maalum wa kukivuruga CUF. Na kwanini iwe CUF? Ni mkakati wa kuimeza Zanzibar.Kwa upande mwengine CUF si chama cha kiislamu lakini kwa vile kimeasisiwa Zanzibar waislamu ni wengi na hii imekuwa nongwa. Katika mtazamo uliompana huu ni mwendelezo wa kuzima ushiriki wa waislamu katika siasa na hii ni vita ya kimataifa dhidi ya uislamu.

Uh, mtizamo wako haujatulia. Umekaa kiudini zaidi. Swali inamaana waliomfukuza mwenzao majority si waislamu? Vita ipo wapi hapo dhidi ya uislamu? Acha hizo!
 
kila kitu udini kila kitu mpaka mchomekee udini..
hivi seif ni budha? wajumbe waliomuondoa ni mapentekoste?
ukweli kilichomponza ni uchu na tamaa ya madaraka ambao upo huko cuf!!!!
si hamad peke yake hata wajumbe waliopo humo cuf wana uchu wa madaraka.

Mimi nashangaa sana wa Zanzibar wapo kimya na wamefurahia kufukuzwa kwa Hamad Rashid. Kwanini Bara mnawaingilia.

Je ni nongwa kwa pandikizi lenu kufukuzwa?
Mbona Chadema walimuengua Zitto kabwe katika kinyang'anyiro cha kugombea uenyekiti wa Chadema taifa kwa kutumia mizengwe na watu hawakusema.

Mbona wamefukuza madiwani wao Arusha, lakini hakuna aliyesema?

Kwanini iwe nongwa kwa CUF.

Tunasikia Mpaka maaskofu Akina Kilaini wanalisemea hilo.
Hii inajionyesha kulikuwa na namna kati ya hamad Rashid na maaskofu na chadema pia.

Ok all in all amefukuzwa na hatakiwi na kama nyie mnamtaka mchukueni basi kuliko kuleta zogo hapo.

Kwa CUF hilo sio tena tulufu bali ni Galasa. kama mnamuona tulufu mchukueni.

 
  • Thanks
Reactions: Ami
Wakati HR anamdhihaki Mbowe kuhusu kambi rasmi ya upinzani bungeni kina Ami mlimpa support ya nguvu huku mkijua anachofanya ni uhuni tu.

Mlipanda na sasa mnavuna vumilieni maana mvumilivu hula mbivu!
 
hamada rashid hawezi kamwe kuwa mtaji wa vita kandamizi dhidi ya uislamu. Ila najua ni mkakati maalumu wa kuigawanya pemba ikose nguvu ya cuf na hapo ndio utakuwa ni mwisho wa nguvu ya cuf pemba. Chama kipya cha hamad kitakuwa na nguvu kubwa katika..... Lakini bado ana fursa ya kuhamia chadema kama nilivyodokeza awali...

yaani chadema kazi zao ni kungojea wanasiasa waliotemwa ndipo waombe kujiunga nao! Ushauri wangu wa bure kwa cdm nendeni kwa wananchi mkatafute wanachama kwa kutumia sera zenu na acheni kutafuta wananchama kwa njia za mkato! Kwa kungojea waasi wa vyama vingine!!

Hembu jiulizeni, lwakatare, akwilombe na waasi wengine toka vyama vya kisiasa wameisaidia nini cdm? Na hata hamad rashid akijiunga nanyi atawasaidia nini? Hamadi rashid anadhamira ya kuupata ukatibu mkuu, jee, slaa yuko tayari kugombea nae? Na akiukosa ukatibu na uenyekiti atautaka! Jee, mbowe nae yuko tayari kuachia ngazi?

Bila shaka yatamkuta yaliyomkuta zitto kabwe alipotaka kugombea uenyekiti ambao ni hati mili ya watu maalum ndani ya cdm!!
 
kwa mtazamo wangu Hamad ni mtendaji kazi mzuri, na mwelekeo wa uchangiaji wake mada bungeni unaegemia utaifa zaidi ya uchama na 'ushabiki'. Kutaka madaraka si dhambi, na ili kuleta mabadiliko wakati mwingine kuwa na madaraka ni muhimu. Mgogoro uliopo ni kiashiria cha demokrasia 'legevu' ndani ya CUF, wenye madaraka hawako tayari kuyaachia, Hamadi amethubutu kuongea and he 's paying the price..!<br><br>
 
Sawa sawa amijei,za mchambawima? Au siku hizi umeamia skuli ya chanjan-jawiri? Wape salamu zangu yakhe mimi nipo jambiani
 
Ukweli ambao wanasiasa na wanaJF hawapendi kuusema ni kuwa Hamad ni mtaji maalum wa kukivuruga CUF. Na kwanini iwe CUF? Ni mkakati wa kuimeza Zanzibar.Kwa upande mwengine CUF si chama cha kiislamu lakini kwa vile kimeasisiwa Zanzibar waislamu ni wengi na hii imekuwa nongwa. Katika mtazamo uliompana huu ni mwendelezo wa kuzima ushiriki wa waislamu katika siasa na hii ni vita ya kimataifa dhidi ya uislamu.

Kwa mtiririko huu wa ujengaji hoja unapaswa kujifua zaidi katika logic. Hisia zimekuongoza zaidi ya hoja madhubuti. Kwa hiyo wataka kusema:
A) CUF ni chama cha waislamu ama ni chombo pekee ambacho kwacho ushiriki wa waislamu katika siasa hufanyika?

B) Hamad Rashid ni wakala wa upinga uislam?
C) uliambatanisha pia hoja kuwa kwa kitendo cha msajili wa vyama na mwanasheria mkuu kuonesha kutofurahishwa na kufukuzwa uanachama kwa Hamad ni "mpango wa kuimeza Zanzibar", kivipi? CUF=Zanzibar?
 
HAmad Rashid ana uchu wa madaraka.

Sio kweli Hamad Rashid ni mmoja wa waasisi wa Cuf lakini hakuna na wadhifa wowote mkubwa zaidi ya kuwa mbunge,Maalim Seif ndio mwenye uchu wa Madaraka tena kwa kiwango cha juu kabisa,toka chAma kianze yeye kawa Katibu Mkuu utadhani Papa mpaka afe ndio warithi waje,yeye na Lipumba ndio walafi wa madarka,
 
Uasi wa Hamad Rashid ndani ya CUF umepata uungwaji mkono usio wa kawaida katika vyombo vya habari Tanzania kama kwamba tukio kama hilo halijapata kutokea kwa vyama vyengine au ni mara ya mwanzo katika CUF.

Zaidi ya uungwaji mkono huo, sasa msajili wa vyama bwana Tendwa na Jaji Werema nao wameingilia kati kuonesha kutoridhishwa kwao na uamuzi madhubuti uliochukuliwa na uongozi wa CUF..., Katika mtazamo uliompana huu ni mwendelezo wa kuzima ushiriki wa waislamu katika siasa na hii ni vita ya kimataifa dhidi ya uislamu.

Huu ni udhaifu wa uelewa wako Ami, ama sivyo bange la Tarime limekolea vibaya. Hamad Rashid ni Muislamu safi aliyefukuzwa na CUF si kwa sababu ya dini yake bali kakiuka katiba ya chama. Hapa udini unakujaje maana hata akina Tendwa hawakuwa wanamtetea kwa kigezo cha udini bali ukiukwaji wa sheria!

Hapo uislamu unapigwaje vita? Waliomtimua HR wote ni waislamu, hata huyo "Julius" Mtatiro ana sigda kubwa kama tochi naye ni walewale, utasemaje kuna udini hapo?
 
kwa mtazamo wangu Hamad ni mtendaji kazi mzuri, na mwelekeo wa uchangiaji wake mada bungeni unaegemia utaifa zaidi ya uchama na 'ushabiki'. Kutaka madaraka si dhambi, na ili kuleta mabadiliko wakati mwingine kuwa na madaraka ni muhimu. Mgogoro uliopo ni kiashiria cha demokrasia 'legevu' ndani ya CUF, wenye madaraka hawako tayari kuyaachia, Hamadi amethubutu kuongea and he 's paying the price..!<br><br>


Mtendaji mzuri ni yule anayefuata sheria na kaanun za chama chake katika kupata uongozi mpya au hata katika kutatua migogoro yake ya ndani.

Hamad Rashid ana pupa na uchu wa uongozi kiasi cha kutaka kuvunja katiba na kanuni walizojiwekea katika kupata viongozi wao.

Kwake njia sahihi ni kuongea na wanahabari na sio kuwasilisha malalamiko yake kufuata taratibu za chama chake.

Na tunamfahamu Hamad Rashid unaona kabisa ametumwa na kupata maslahi katika kutaka kuleta mtafaruk kwenye chama chake.

lakin haki sawa kwa wote naye yamemkuta.

Agombee tu kupitia chadema jimbo la Temeke.
 
Barabara inayoelekea Cuf sio njia yangu. Lakini napita tu, kwa kusema kuwa HR. Ndio anayoimaliza Cuf na itatoweka
katika macho ya Watanzania, Ukitaka kujua kama hao watu ni wanafiki wakupindukia ndio hapo sasa, HR ambaye
kesha chukua hesabu yake kwa kazi hiyo maalum, kutoka huko kunakoeleweka na wote. Madhumuni kuivunja Cuf na
kumuondoa Sharif Hamad katika serikali ya mseto. Tunaelewa yote na sasa hivi sisi ni wasikilizaji na waangaliaji wa
mchezo huo wa Tamaa.
 
Kwa mtiririko huu wa ujengaji hoja unapaswa kujifua zaidi katika logic. Hisia zimekuongoza zaidi ya hoja madhubuti. Kwa hiyo wataka kusema:
A) CUF ni chama cha waislamu ama ni chombo pekee ambacho kwacho ushiriki wa waislamu katika siasa hufanyika?

B) Hamad Rashid ni wakala wa upinga uislam?
C) uliambatanisha pia hoja kuwa kwa kitendo cha msajili wa vyama na mwanasheria mkuu kuonesha kutofurahishwa na kufukuzwa uanachama kwa Hamad ni "mpango wa kuimeza Zanzibar", kivipi? CUF=Zanzibar?
Siasa za miaka hii hakuna demokrasia wala nini.Kila kundi linaangalia maslahi yake na huwa wamekaa kimtego mtego kutumia fursa inayopatikana.Ukweli pekee aliousema Seif jana kati ya mengi aliyonayo moyoni ndio uhalisia wenyewe.Kwamba kuna watu wengi hawakupenda muafaka uliofikiwa Zanzibar.Kwa uhakika kati ya hao ni wakristo popote walipo Tanzania.
Inasemekana HR anatumiwa,yawezekana kwa udhaifu wake anatumika bila kujijua.Wakristo walipoona hali yake walitumai sana kazi itakuwa nyepesi.Lakini CUF ni chama madhubuti sana katika kushughulika na watu wa aina ya Hamada.Aliposhughulikiwa wakristo wamechanganyikiwa.Bila aibu wanaropokwa na kumtetea mhalifu.
Maelezo yangu ya juu yanajibu a na b.Hiyo c ni kuwa hawa watu wapo kama watendaji wa serikali lakini kwa ndani ni watekelezaji wa malengo yaliyo kinyume cha katiba kwa faida za hapo a na b.Nitashangaa ukinipinga kwa hili wakati vitu kama Chama cha wanajeshi wakristo ndani ya majeshi yetu bado havijajibiwa.
 
Siasa za miaka hii hakuna demokrasia wala nini.Kila kundi linaangalia maslahi yake na huwa wamekaa kimtego mtego kutumia fursa inayopatikana.Ukweli pekee aliousema Seif jana kati ya mengi aliyonayo moyoni ndio uhalisia wenyewe.Kwamba kuna watu wengi hawakupenda muafaka uliofikiwa Zanzibar.Kwa uhakika kati ya hao ni wakristo popote walipo Tanzania.
Inasemekana HR anatumiwa,yawezekana kwa udhaifu wake anatumika bila kujijua.Wakristo walipoona hali yake walitumai sana kazi itakuwa nyepesi.Lakini CUF ni chama madhubuti sana katika kushughulika na watu wa aina ya Hamada.Aliposhughulikiwa wakristo wamechanganyikiwa.Bila aibu wanaropokwa na kumtetea mhalifu.
Maelezo yangu ya juu yanajibu a na b.Hiyo c ni kuwa hawa watu wapo kama watendaji wa serikali lakini kwa ndani ni watekelezaji wa malengo yaliyo kinyume cha katiba kwa faida za hapo a na b.Nitashangaa ukinipinga kwa hili wakati vitu kama Chama cha wanajeshi wakristo ndani ya majeshi yetu bado havijajibiwa.
.

Kweli kabisa. Lakini bila kumung'unya maneno kwa kuwa anajulikana kwa kupenda ukubwa. CHADEMA wanamtaka kuwa mgombea mwenza au mgombea wa urais kupitia chama cha Chadema kwa kiti cha Zanzibar.

Ni pandikizi lililo jidhihirisha na kwa kudra za Mola limejulikana na kugundulika na ndio maana watetezi wake wote wapo BARA na sio Znz alipokuwa anawakilisha.
 
Uasi wa Hamad Rashid ndani ya CUF umepata uungwaji mkono usio wa kawaida katika vyombo vya habari Tanzania kama kwamba tukio kama hilo halijapata kutokea kwa vyama vyengine au ni mara ya mwanzo katika CUF.

Zaidi ya uungwaji mkono huo, sasa msajili wa vyama bwana Tendwa na Jaji Werema nao wameingilia kati kuonesha kutoridhishwa kwao na uamuzi madhubuti uliochukuliwa na uongozi wa CUF. Haipendezi kwa wanasheria hao kushikilia habari za mahakama ilhali viongozi wa CUF wameshasema hawakupokea amri ya mahakama.

Ukweli ambao wanasiasa na wanaJF hawapendi kuusema ni kuwa Hamad ni mtaji maalum wa kukivuruga CUF. Na kwanini iwe CUF? Ni mkakati wa kuimeza Zanzibar.Kwa upande mwengine CUF si chama cha kiislamu lakini kwa vile kimeasisiwa Zanzibar waislamu ni wengi na hii imekuwa nongwa. Katika mtazamo uliompana huu ni mwendelezo wa kuzima ushiriki wa waislamu katika siasa na hii ni vita ya kimataifa dhidi ya uislamu.

Sidhani kma ni swala la uisalamu kwa maoni yangu nadhani wanawasiwasi muafaka unaweza ukawatumbukia nyongo serikali ya umoja wa kitaifa unaweza kuingia dosari kama Kufukuzwa kwa Hamad kunaweza kupenyeza chuki baina ya wanachama wa CUF Zanzibar hawa viongozi wa serikali wanalinda serikali ya mufuaka wa kimataifa manake ikitisika itakuwa Political suicide Kwa CCM Zanzibar vivyo CCM Tanganyika
 
nilitaka kukusifu kwa kupangilia hoja yako paragraph za mwanzo, lkn naungana na mwenzangu mwingine kwamba umeharibu ulipoanza kuzungunzia udini! Lala salama usiku mwema na heri kwa mwaka mpya!
 
Back
Top Bottom