Hamad Rashid aomba radhi...

Hili galasa la cuf linatakiwa kwenda Cdm, maana cdm inapenda kuchukuwa magalasa wa vyama vingine mfano prof Safari. Ni galasa alieshindwa uchaguzi wa mwenyekiti wa cuf.
 
kuna nini ktk siasa za bongo?
prof safari alivyotangaza nia ya kugombea uenyekiti tunajua yalomkuta'
zitto alivyotangaza kugombea uraisi tunakumbuka pia sakata lake mpaka sasa chamani
kafulila pia mwelekeo ni kama huo,
hamadi rashidi ukatibu imekuwa nongwa,
ccm wajisemee wenyewe,
na wengine sikumbuki. napata taabu kujua kama kuna demokrasia ya kweli, naona kama maigizo tu.....
 
Kuna tetesi za kuaminika kwamba Hamad hataki Jusa achukue Ukatibu Mkuu maana yeye si MPEMBA
 
huyu ni wa kufukuza tu ..nilikuwa namheshimu sana kumbe ana tamaa sana ya madaraka ..nonsense


tamaa huwa inaisha ana LAANA YA MADAARAKA NA NJAAA ALISHAWAHI KUMWAMBIA MJOMBA WANGU MMOJA KIPINDI WANAKIMBIZANA NA MBOWE KUHUSU MKUU WA UPINZANI AKAAPA HATOMWACHIA KIRAHISI NA YUKO RADHI KWENDA MAHAKAMANI HUYU NDIE HAMA RASHID LOH
 
kuna nini ktk siasa za bongo.....
zitto alivyotangaza kugombea uraisi tunakumbuka pia ....napata taabu kujua kama kuna demokrasia ya kweli, naona kama maigizo tu.....

Zitto alitaka kubombea urais wa nini, TFF? Kama urais wa Tz basi yaonekana hata hujui matakwa ya katiba ya sasa juu ya umri wa mgombea....
 
huyu ni wa kufukuza tu ..nilikuwa namheshimu sana kumbe ana tamaa sana ya madaraka ..nonsense
It goes bothways.
Cross examine Maalim Sharif hicho unachomhukumia Hamad naye yuko guilty.
Kumbuka Maalim wa "Ngangari kinoma" na Maalim Makamu wa rais zenji.
 
huyu ni wa kufukuza tu ..nilikuwa namheshimu sana kumbe ana tamaa sana ya madaraka ..nonsense

wabongo bwana..hivi kati ya Hamad Rashid na Seif Sharrif nani hasa mwenye tamaa ya madaraka?

Hamad anadai chama kimedorora chini ya uongozi wa Seif Sharif na kwamba kunahitajika mabadiliko ya uongozi na yeye anaamini ni katika watu wanaweza kuleta hayo mabadililko hiyo ni tamaa ya madaraka??? tujaalie jibu ni ndiyo, je kitendo cha Seif Shariff kung'ang'ania madaraka hata ushahidi wa wazi ukionyesha kwamba chama kimedorora na kukosa mvuto chini yake ambayo inamaanisha kushindwa uongozi nalo liitweje, siyo tamaa ya madaraka?????

mi nadhani CUF wakubali kwamba chama chao kinakufa na kinahitaji mtu wa kukihuisha, si Seif wala Lipumba wataweza kazi hiyo, kwangu Hamad has a point katika madai yake na nadhani aachwe atumie haki yake ya kidemokrasi ingawa uzoefu unaonyesha kuwa atashindwa na si ajabu akafukuzwa chamani lakini ikiwa CUF watafikia hapo basi watakuwa wamejizika rasmi.
 
Acheni uchochezi.

ya ng'oswe aachiwe ng'oswe mwenyewe. Kwani naamini kuna taratibu na utamaduni wa kujadili mambo pasi na kupiga kelele nje.

aya mambo ya watanzania yanakuhusu nini wewe mu-Oman??nyie ndio mnataka kuleta machafuko kama kwenu uko.
 
Tukitala kuishinda ccm lazima kuwe na mageuzi makubwa ndani ya vyama vyetu vya siasa, viongozi wengi wa vyama hivi wamekuwa madarakani kwa muda mrefu, na wameshindwa kutufikisha watanzania tunapo pataka, wametengeneza safu za utawala ambao unawazuia wengine kuwapinga na kuweka changamoto.

Lengo la chama chochote cha upinzani ni kutawala nchi, lakini inapofikia viongozi wa vyama hivyo wanausaidia chama tawala kuendelea kutawala, inakuwa hakuna haja tena ya kuwa na vyama vya upinzani. Kama wakatokea watu ndani ya vyama vyetu, wakataka mabadiliko wanaoneka ni waasi, bado tunaunga mkono kuwajibishwa kwao kwa kisingizio kuwa vyama vinalinda katiba, wakati ukweli ni kuwa viongozi wanalinda masilahi yao binafsi.

Kwa suala la David na la Rashidi, tumekuwa tukitoa mchango kiushabiki zaidi, badala kuangalia ukweli wa mambo, kukubali na kunyamaza kimya si utii bali ni uoga, wale wanao mshauri Davidi kuomba msamaha kwa viongozi wake ni sawa na kumfundisha uoga, haitasaidia kitu kama akiomba msamaha kwa kuwa moyo wake unataka mabadiliko.

Kama tukisema David au Rashidi wamevunja katiba ya vyama vyao, mbona sisi viongozi wengi tu waupinzani tunavunja katika ya nchi katika mambo mengi, lakini kwa kuwa lengo letu ni moja, kuleta mabadiliko ndo maana tunakuwa na moyo wa kiujasiri, kama MB David kavunja katiba ya chama chake akafukuzwa, basi na wale wabunge wanovunja katiba ya nchi kwa madai ya kudai haki itabidi wafungwe kabisa.

Katiba zote zimeandika na kutungwa na watu kwa lengo la kulinda masilahi ya kiuongozi na kiutawala, ukitaka mabadiliko lazima kwanza uivunje hiyo katiba.

Kwa kumalizia, katika mfumo huu tulio nao katika vyama vyetu vya siasa, itakuwa ngumu sana ku defeat CCM. CCM ni chama kikongwe, kina mikakati mingi sana na hila nyingi za kuendelea kutawala, hata kuweka mapandikizi na kuwanunua baadhi ya wanasiasa wa upinzan, ili kuweza ku defeat CCM inabidi kwanza kufanya mapinduzi makubwa katika mifumo yetu ndani ya vyama vyetu vya upinzani, lengo letu wote liwe ni moja, kufanya mabadiliko katika nchi na sio kutaka madaraka.
 
Zitto alitaka kubombea urais wa nini, TFF? Kama urais wa Tz basi yaonekana hata hujui matakwa ya katiba ya sasa juu ya umri wa mgombea....

kwahiyo yeye alivyodai kuwa atagombea uraisi 2015 hakujua hiyo katiba ama hajui umri wake?
 

Labda ni wakati muafaka kwa Sharif kustaafu siasa...

Tuwe na utamadhuni wa kuachia ngazi baada ya kupata fursa ya kutawala kwa muda fulani. Na ukistaafu, ustaafu kweli kweli, siyo kuja kutawala kwa remote controll.
 
Ngojeni niwape ukweli huyu hamad rashid ni mbinafsi na tamaa sana,kwanza jimboni kwake hakupita katika kura za maoni alitokea mtu wa tatu lakini maalim seif akampigia kifua akapita kwa kujua umuhimu wake bungeni ,alipoingia bungeni akakosa nafasi ya kuwa kiongozi bungeni akaanza bifu kwani alishazoea sana posho akaanza sasa kuwa karibu na viongozi wa juu wa serikali na baadhi ya vyama hasimu na cuf. tamaa yake imemponza mungu hamfichi mnafiki mitego yake ikagundulika ,kwa ushauri wangu kwa viongozi wa cuf hichi ni kirusi au kensa ambayo inasambaa mwilini ,kwa vile wamegundua mapema kateni kiongo chochote cha mwili ili muokoe maisha ya mgonjwa,nina maana piga chini wapo zaidi yake yeye wenye uwezo na nidhamu wa kukamata nafasi yake ,na kama hili halitofanyika kwa kweli muelekeo wa cuf mbele ya wanachama wake utakuwa dhaifu kwa siku za baadae.
 
ukweli ni kwamba chama cha cuf kwa upande wa zanzibar bado hakijadororo kabisa na kinazidi kuwa na nguvu kadri siku zinavyokwenda chini ya uongozi wa maalim seif na siku akiondoka huyu ndo siku chama kitakavyopata pigo sna,mara zote katika chaguzi zote za zbar maalim anashinda na tena kwa ushindi wa kishindo nani asiyejua hata mtoto mdogo ,kwa sababu tuu ya mabavu yanayotumika anaporwa ushindi wake naye kwa sababu ya uungwana wake na kuogopa kumwaga damu ya wanachi wake anakubali kudhalilika kuepusha maafa ,huyu ni kuongozi shupavu asiye mchoyo wa madaraka ,angalia mfano wa kongo marais wawili wamejiapisha,watu wanauana ,kwa upande wa znz chaguzi nne zimepita zote maalim kashinda lakinii kaporwa kwa nguvu ,iko siku mungu atawafunga macho na masikio na atawakosesha nguvu wote wenye kutumia mabavu dhidi ya znz,kama ilivyotokea nchi nyengine .kwa kumalizia suala sio kubadilisha uongozi au kiongozi ,suala ni jee aliyepo ana uwezo? jibu ni ndio maalim bado ana uwezo na ataendelea kudumu manake naamini wazanzibar walio wengi wanampenda sana .sisi wabara hatujui sana siasa za zanzibar ila mimi nazifatilia sana kwani nimekaa sana znz
 
CUF hawamwezi huyu mkongwe wa siasa na ukizingatia sio jumbe huyu labda atajiuzulu tu.

Katika ngazi ya Parliamentary huyu mkongwe wa siasa kakipa sana popularity chama hiki cha CUF sasa wakitaka kukosa hata kura moja 2015 wamwage huyu mkongwe wa siasa.
 
CUF hawamwezi huyu mkongwe wa siasa na ukizingatia sio jumbe huyu labda atajiuzulu tu.

Katika ngazi ya Parliamentary huyu mkongwe wa siasa kakipa sana popularity chama hiki cha CUF sasa wakitaka kukosa hata kura moja 2015 wamwage huyu mkongwe wa siasa.
kabla ya 2015 kuna mambo mengi sana yatatokea katika nchi hii katika tasnia ya politiki- na hii ni dalili njema ya ukombozi wa taifa hili linalodhalilika kimataifa.
 
Back
Top Bottom