Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema hawautambui mkutano huo kwa sababu una zuio la Mahakama Kuu.
Akizungumza na Mwananchi Jumanne Machi 12, 2019, Maalim Seif amesema, sisi hatuna uwezo wa kuuzuia lakini kama jeshi la polisi likitaka linao uwezo huo.
“Ni kama mchezo wa kuigiza kuhusu suala hili, kama polisi ina nia ya dhati ya kuzuia wale hawawezi kufanya lolote lile. Utafanyaje mkutano wakati kuna zuio tena la Mahakama Kuu? Alihoji Maalim Seif.
“Siyo mantiki yoyote kwa polisi kuanza kuzungumza na viongozi wa CUF wa upande ule wakati suala lipo wazi kabisa. Nawaambia msimamo wetu upo pale pale mkutano huu hatuutambui kabisa kwa sababu ni haramu,” amesema Maalim Seif.
CUF upande wa Profesa Ibrahim Lipumba unafanya mkutano mkuu jijini Dar es Salaam ambapo polisi wa Ilala umeuzuia mkutano huo lakini agizo hilo halikutekelezwa na mkutano uliendelea.
Akizungumza na Mwananchi Jumanne Machi 12, 2019, Maalim Seif amesema, sisi hatuna uwezo wa kuuzuia lakini kama jeshi la polisi likitaka linao uwezo huo.
“Ni kama mchezo wa kuigiza kuhusu suala hili, kama polisi ina nia ya dhati ya kuzuia wale hawawezi kufanya lolote lile. Utafanyaje mkutano wakati kuna zuio tena la Mahakama Kuu? Alihoji Maalim Seif.
“Siyo mantiki yoyote kwa polisi kuanza kuzungumza na viongozi wa CUF wa upande ule wakati suala lipo wazi kabisa. Nawaambia msimamo wetu upo pale pale mkutano huu hatuutambui kabisa kwa sababu ni haramu,” amesema Maalim Seif.
CUF upande wa Profesa Ibrahim Lipumba unafanya mkutano mkuu jijini Dar es Salaam ambapo polisi wa Ilala umeuzuia mkutano huo lakini agizo hilo halikutekelezwa na mkutano uliendelea.