Kwa ujumla halmashauri zetu nyingi ni uozo wa ajabu, huwezi kuamini.Fedha nyingi sana zinazopelekwa kwenye halmashauri hizi zinaishia kwenye mifuko ya watendaji sio miradi, rushwa imekithiri,siasa za ovyo, uelewa mdogo wa wafanyakazi wa halmashauri,madiwani wengi mbumbumbu,halmashauri nyingi hazina vision na wakurugenzi wengi wa halmashauri sio wabunifu na hawana vision. Kweli halmashauri kama zinapata wakurugenzi wazuri wenye vision, madiwani wazuri waliosoma na wenye vision, wenyeviti na mayors wenye elimu na vision, halmashauri zingekuwa ni kitivo cha maendeleo, lakini ni balaa, zimegeuka sehemu ya watu kujineemesha.Nafikiri kuna haja ya kuangalia upya mfumo wa halmashauri zetu, na nafikiri mkurugenzi iwe nafasi ya kupigiwa kura badala ya kuteuliwa kwa kuwa ndio injini ya maendeleo ila wengi wao wapowapo tu hawana vision japo wengi wanaelimu nzuri.