Halima Mdee Unachemka

Halima Mdee Unachemka

Una funza kwenye ubongo, mdee anakusanya kodi yako?

Anakula kodi zetu kwenye mshahara, posho na marupurupu ndio maana tunataka awe responsible.

To whom much is given much should be expected
 
Acheni longolongo ccm wamekalia hilo jimbo yangu Uhuru hawajajenga hiyo barabara kwa 50yrs unataka mdee ajenge kwa 3.5 yes how come?

ccm acheni unafiki.
 
Sijui kwanini hata kwenye kudiscuss jambo watu wanachangia kichama chama...
 
Offcoz sisi hatutaki msaada wake yeye anatakiwa atu mobilize tu tufanye wenyewe.

wewe michael acha upuuzi wako, nini maana ya kumteuwa au kumchagua mbunge anayeweza kuleta maendeleo ktk eneo husika? vipi na wewe umeanza kuwaza kwa kutumia tigo? acha ushamba wa posta
 
Hi Mh. Halima Mdee, ujue 2015 ndio hiyoo inakuja na sisi wananchi wa jimboni kwako tunakuangalia tu na promise zako ambazo unashindwa tekeleza. vitu vidogo vidogo tu vinakushinda sasa ukikosa hili jimbo lako utatulaumu?

Mwaka Jana mwezi kama wa Nne hivi kama si kosei tulikuita sisi wananchi wa Boko eneo la Magereza tena umekuja baada ya kukuita bila mafanikio kwa mara mingi, siku hiyo nakumbuka ukaja tukakutana na wewe pale Pommy Hill Club tukaongelea swala la Barabara yetu huku boko magereza. kwa Nyodo nyingi sana ukijifanya utashughulikia swala hilo na katika kile kikao ukawa mkali mkali tu,kikao kimeisha ukasema baada ya mwezi utarudi ilikutane na wamiliki wa magari yanayo beba mawe maana wao ndio wanao haribu barabara. na siku ile kuna mtu alisema wewe utuachie azimio kama baada ya huo mwezi hakuna lililofanyika tufunge barabara kwa magari makubwa ukakataa na ukasema utarudi yule mtu akarudia kusema " Nawajua wana siasa maneno mengi sana, naambia huyu harudi tena huku" na kweli alio yasema ndio yalio tokea.

Sasa angalia picha za barabara uliosema utarudi baada ya mwezi na sasa ni mwaka hatujakuona.
View attachment 147831 View attachment 147832

Mimi napenda Mageuzi sana lakini jinsi hii itabidi CDM watupe mgombea mwingine jimbo hili wewe unachemka sana. una issue kama kumi hivi ushachemka sana kama CDM hawaoni basi hili Jimbo tutalikosa wakikusimamisha wewe tena.

Asante sana.

Poleni sana Makamanda.
 
Yeye si ametususa sawa tutaona 2015 sijui atapita barabara gani, sisi ni watu wa mageuzi na action..tumejichangisha wenyewe 10,000 kwa kila mtu, na huku kuna vichwa kama 700 hivi na tumetengeneza sehemu zote hatarishi now barabara inapitika, nilikuwa nataka aone Jinsi gani sisi tunauwezo wa kutafakari na kuchukua Hatua na kutoa feedback. yeye alikuja akatafakari..akaingia mitini na hakuna feedback, Asanteni sana mlio changia Uzi huu kwa mawazo yenu. nita post Picha za marekebisho tuliofanya pamoja na nakara ya kuchangishana ili kutengeneza barabara maana ilikuwa hatari, itokee kuna mgonjwa anatakiwa hospital haraka kwa kweli angeweza fia njiani. Ukiangalia swala hili unaliona kama mzamaha lakini lina mambo mengi sana. nitapost picha kesho za vielelezo. Asanteni.
 
Hi Mh. Halima Mdee, ujue 2015 ndio hiyoo inakuja na sisi wananchi wa jimboni kwako tunakuangalia tu na promise zako ambazo unashindwa tekeleza. vitu vidogo vidogo tu vinakushinda sasa ukikosa hili jimbo lako utatulaumu?

Mwaka Jana mwezi kama wa Nne hivi kama si kosei tulikuita sisi wananchi wa Boko eneo la Magereza tena umekuja baada ya kukuita bila mafanikio kwa mara mingi, siku hiyo nakumbuka ukaja tukakutana na wewe pale Pommy Hill Club tukaongelea swala la Barabara yetu huku boko magereza. kwa Nyodo nyingi sana ukijifanya utashughulikia swala hilo na katika kile kikao ukawa mkali mkali tu,kikao kimeisha ukasema baada ya mwezi utarudi ilikutane na wamiliki wa magari yanayo beba mawe maana wao ndio wanao haribu barabara. na siku ile kuna mtu alisema wewe utuachie azimio kama baada ya huo mwezi hakuna lililofanyika tufunge barabara kwa magari makubwa ukakataa na ukasema utarudi yule mtu akarudia kusema " Nawajua wana siasa maneno mengi sana, naambia huyu harudi tena huku" na kweli alio yasema ndio yalio tokea.

Sasa angalia picha za barabara uliosema utarudi baada ya mwezi na sasa ni mwaka hatujakuona.
View attachment 147831 View attachment 147832

Mimi napenda Mageuzi sana lakini jinsi hii itabidi CDM watupe mgombea mwingine jimbo hili wewe unachemka sana. una issue kama kumi hivi ushachemka sana kama CDM hawaoni basi hili Jimbo tutalikosa wakikusimamisha wewe tena.

Asante sana.

hapa nisawa na kumtuhumu monita kwa kutosahihishwa kwa daftari wakati msahihishaji ni mwalimu
 
Ingawa CDM magumashi lakini hapa kama mnamuonea huyu dada, kwanza ujenzi ama ukarabati wa barabara unatokana na fedha zinazotengwa na serikali kuu ama zipo kwenye mkakati wa taifa.

Hizo hela Mdee hana uamuzi ziende wapi ni jukumu la serikali mitaa na manispaa sasa yeye afanyaje zaidi ya kuomba tu wazibe hayo mashimo na alikadhalika hawezi ingilia priority zao, atleast hata madiwani wanakaa kwenye budget hizi lakini mmbunge sijui anasaidia vipi labda atumie hela zake mwenyewe.

Kuna viongozi wengi sana ambao ni wabunge na wanauwezo wa ku-influence wizara na budget ambao wamearibu dhana ya uwakilishi kwa kupeleka vitu kwao kama hongo kutokana na nafasi zao za juu kiupendeleo upendeleo. Hili lazima lieleweke kwasababu si wabunge wote wanauwezo huo wengine sanasana inabidi wakumbushie au waponde sera lakini kutegemea mmbunge aone shule zimejengwa, barabara zimekuwa bora, sijui ulinzi umeimarika huko ni kupotoka yeye hana control na hizo budget wala priority za serikali ya mitaa, let alone sera za serikali kuu.
 
Back
Top Bottom