Halima Mdee hastahili 'kutendwa' vile

Halima Mdee hastahili 'kutendwa' vile

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Hata kama ni mambo ya kisiasa,twende taratibu. Jana, Mbunge wa Kawe (CHADEMA) na Mwenyekiti wa BAWACHA Halima Mdee alikosa dhamana na kuswekwa rumande. Ikatolewa sababu kuwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana. Sasa, hebu twende hatua kwa hatua.

Kwanza Halima Mdee alikamatwa. Pili Halima Mdee akaachiwa kwa dhamana ya Polisi. Tatu Halima Mdee alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka yake. Nne, upande wa Mashtaka haukuwa na pingamizi juu ya dhamana ya Halima Mdee wala wenzake. Tano,Hakimu akatoa masharti ya dhamana. Sita, washtakiwa wote walikuwa tayari kuyatekeleza na kuachiwa kwa dhamana. Saba, upande wa Mashtaka ukataka kwenda kuhakiki wadhamini wa Halima Mdee na wenzake.

Umepagundua penye tatizo? Ni hapo pa kuhakiki wadhamini. Halima Mdee anajulikana. Wadhamini wake, ambao wengi ni Wabunge na Maafisa wa CHADEMA Makao Makuu wanajulikana. Kuhakiki kulikujaje? Wengine mbona hawafanyiwi hivyo? Kibaya zaidi,wahakiki hawakuenda mahali popote hadi Halima Mdee alipopandishwa karandinga na kwenda mahabusu. Wahakiki walitokomea kusikojulikana. Why?........Kwanini?

Nitoe rai kwa wahusika wote kufanikisha dhamana ya Halima Mdee. Ingawa si wa chama changu, hastahili kombolela lililochezwa jana. Hakuna haja ya 'kuipaisha' CHADEMA na viongozi wake kupitia Mahakama. We are suffering from that;it must end! Pole sana Halima Mdee.


Updates....
Halima Mdee na wenzae 8 wamepata dhamana. Ni jambo jema
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Last edited by a moderator:
Wanamjengea ujasiri , a natakiwa kuzoea mikikimikiki kama hiyo , wanamuandaa, wanamtengenezea ufuasi wa kutosha ..........
 
Kaka umeongea maneno mazito sana,kama utakuwa ni dada nisamehe kwa kutumia neno kaka. Ktk hilo hakuna neno umeacha la kuongeza. Barikiwa sana kwa kusema ukweli, tusifike mahali kuchezeana fitina namna hii.
 
Wenye kuangalia mbali walijua mapema kuwa polisi wanatumiwa na ccm wenye akili ndogo wakabisha.
pia wenye akili wakesema mahakama zetu zinatumiwa na wanasiasa (ccm) wenye upeo mdogo wakabisha.
Sasa kwa hili la Halima Mdee nina hakik hata wale wasioelewa kabisa kitu sasa watajua matatizo ya hizi taasisi zetu!
 
Mkuu utashangaa walicheza huo mchezo mchafu kesho wakapandishwa vyeo ha ha ha ha hii ndio Tanzania bana wafanyakazi wa serekali wamekubali kuwa misukule ya chama tawala.
 
Kaka umeongea maneno mazito sana,kama utakuwa ni dada nisamehe kwa kutumia neno kaka. Ktk hilo hakuna neno umeacha la kuongeza. Barikiwa sana kwa kusema ukweli, tusifike mahali kuchezeana fitina namna hii.

Mkuu,uko sahihi.Mimi ni me

Mzee Tupatupa
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Mkuu utashangaa walicheza huo mchezo mchafu kesho wakapandishwa vyeo ha ha ha ha hii ndio Tanzania bana wafanyakazi wa serekali wamekubali kuwa misukule ya chama tawala.
reff. kamuhanda na mauaji ya Mwangosi. Mdee anaumia ila ni advantage kwa chama chake!
 
Iko siku nitakuwa tayari kufanya jambo lolote b@ya ili kuwalinda wanyonge!
 
Kuhakiki ni utaratibu wa kawaida kwa mahaka,
inawezekn mjia tu yameandwa lkini hawakuwa na tarifa kuwa wao ni wadhamini,
Acha upotoshaji
 
Hawa Polisi watu wa ajabu sana. JK si alimkaribisha Ikulu sasa wao walimkamatia nini?


jkkk.jpg
 
Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.. pia lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho.
 
Hakika mzee nakupa hongera sana kwa uchamburi mahili lati kama wenzako wangekuwa kama wewe hakika tanzania sasa tungekuwa tunafikiria vitu vingine na si hivi vya kupelekana segarea
 
Umepagundua penye tatizo? Ni hapo pa kuhakiki wadhamini. Halima Mdee anajulikana. Wadhamini wake, ambao wengi ni Wabunge na Maafisa wa CHADEMA Makao Makuu wanajulikana. Kuhakiki kulikujaje? Wengine mbona hawafanyiwi hivyo? Kibaya zaidi,wahakiki hawakuenda mahali popote hadi Halima Mdee alipopandishwa karandinga na kwenda mahabusu. Wahakiki walitokomea kusikojulikana. Why?........Kwanini?

Nitoe rai kwa wahusika wote kufanikishadhamana ya Halima Mdee. Ingawa si wachama changu, hastahili kombolela lililochezwa jana. Hakuna haja ya 'kuipaisha' CHADEMA na viongozi wake kupitia Mahakama. We are suffering from that;it must end! Pole sana Halima Mdee.

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Hili huwa naliamini! Polisi na CCM yao,wanadhani kwenda Mahabusu ni dhambi!

Viongozi wetu wa Kisiasa wa upinzani walitambue hilo ,kuwa kutafuata hakibinafsi au ya Umma mpana,suala la kwenda sero ni sehemu ya Maisha,na Mhe.Godbless lema aliwaonyesha mfano.

Ukiacha mfano huo mifano ya aina hiyo iko mingi na historia inatupa mwanga kuwa wengi wao walifanikiwa ,katika kufikisha ujumbe kwa Umma na mwisho Umma ukajitambua na ukachukua hatua dhidi ya Watawala dhalimu kama hawa wa CCM.

Hivyo Mhe.Halima huko uliko chonde chond usikae kimya ,bila shaka huko sero wapo akina mama wanyonge walioporwa haki yao kwa nguvu za cheo na Pesa kama walivyokufanyia kwa hatua ya kupata dhamana.Mungu akujaze nguvu ya kuendeleza Mapambano.
 
Mkuu utashangaa walicheza huo mchezo mchafu kesho wakapandishwa vyeo ha ha ha ha hii ndio Tanzania bana wafanyakazi wa serekali wamekubali kuwa misukule ya chama tawala.
hili linawezekana ndani ya serikali ya ccm
 
Hapo wanampaisha Mbunge wetu na Mwenyekiti wa Balaza la Wanawake CHADEMA - tupo pamoja kamanda!!
 
Wanamjengea ujasiri , a natakiwa kuzoea mikikimikiki kama hiyo , wanamuandaa, wanamtengenezea ufuasi wa kutosha ..........

umenikumbusha kaul ya Che Guovar Alivyosema Hawezi Maisha Bila Misukosuko Hatimae Akauwawa Kinyama Na Wa Bolovia
 
Back
Top Bottom