Hali ya maisha ikoje mahali uliko?

Hali ya maisha ikoje mahali uliko?

Los técnicos

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2014
Posts
3,015
Reaction score
2,645
Katika wiki kadhaa zilizopita tumeshuhudia bei za baadhi ya bidhaa kama nyanya na gesi kupanda.

Ongezeko hili bila shaka linagusa vipato vyetu vya kila siku. Lengo la uzi huu ni kujua kama kuna bidhaa nyingine zilizopanda bei na kama zimepanda ni kwa kiasi gani?

Hii inaweza pia ikatutengenezea fursa za kibiashara kwa wajasiliamali lakini pia kujua kiasi gani viongozi wetu wamefanikiwa kuboresha maisha ya watanzania kwa kubalance uchumi.

Lakini pia kubaini vyanzo vya ongezeko hilo ni nini hasa?

Naomba tudondoshe hapa aina ya bidhaa yoyote iliyopanda na bei yake? Na mwenye kujua sababu atanabaishe.

Tukianza na Mahindi, Unga, Gesi, Nyanya, sukari n.k



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bei ya nyanya imeathiriwa na hali ya hewa kwa kiasi kikubwa, lakini pia Bei za vyakula kwa msimu huu kikawaida huwa inapanda mpaka wakati Wa mavuno.
Bei ya vitu vya viwandani kama mabati, simenti, n.k ina sababu nyingi za kupanda ikiwemo kuongezeka kwa gharama za uzalishaji utaokanao na sababu mbalimbali.
Bei ya gas na petrol hiyo inaratibiwa na huko yatokako
Tuendelee kupambana tu maisha hayashuki yanazidi kupanda siku hadi siku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo Hapa Kigamboni Tunafungua Majengo Ya Wilaya
Sasa Yule Mwekezaji Anayewazuia Wananchi Kupita Eti Amefunga Njia Afungue Haraka. Naweza Kufuta Hati Ya Ardhi Anayomiliki Halafu Tuone

Halafu Anazuia Mpaka Watu Kupita Kwenda Kuzika, Ajue Naye Atakufa Atazikwa Humo Humo
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania


😅😄😃🤣😂😁
 
Back
Top Bottom