masai dada
JF-Expert Member
- Dec 29, 2013
- 16,707
- 16,422
Wapendwa, kwanza poleni sana na msiba.
Kwa upande wangu, naona kabisa kama niko kwenye majaribu makubwa.
Nimejaliwa watoto wangu wawili, na nikahisi wananitosha kabisa.
Hapo nikachukua uamuzi wa kuweka kipandikizi mkononi.
Baada ya mwaka mmoja kupita, kile kipandikizi kikaniletea maudhi mengi, hivyo nikakitoa miezi mitatu iliyopita.
Miongoni mwa maudhi hayo ilikuwa kupotea kabisa kwa hamu ya mambo ya ndoa. Baada ya kukitoa, mwezi wa kwanza sikuona mabadiliko yoyote.
Lakini mwezi wa pili… mambo yakaanza kubadilika ghafla.
Wakati wa ovulation nilijikuta napata hisia kali sana.
Hadi nikajikuta nashindwa kuelewa kinachoendelea hamu imekuwa kali mno. Leo ndiyo nimekaa na kutafakari vizuri ndipo nikagundua kuwa chanzo kinawezekana ni mabadiliko ya homoni baada ya kutoa kipandikizi.
Aisee ndugu zangu, mpaka nimeongea na Mungu leo… sijui nifanye nini. Najisikia vibaya sana, kwa sababu nilishafunga kabisa mlango wa mambo ya watu wazima kwa kifupi nimekuwa nikiishi bila kufanya tendo la ndoa.
Baba wa watoto tumeachana kimkoa kutokana na kazi, ingawa tunalea watoto pamoja. Kwa hiyo muda mwingi niko “dry sell” tu.
Sihitaji kutenda dhambi, lakini majaribu yamekuwa makubwa kweli.
Naomba ushauri wenu.
Ninategemea kuanza mazoezi ya gym mapema mwakani, ili niachwe nikiwa nimechoka na kutofikiria mambo hayo.
Lakini kwa sasa nikiwa nimeshughulika sana mchana, nikilala au kupumzika kidogo tu hisia zinaongezeka.
Hali hii sikuwa nayo kabla ya kipandikizi, hivyo nahisi bado homoni hazijajibuana vizuri.
Naombeni ushauri jamani, maana hali inanipa hofu na kunitia wasiwasi.
Kwa upande wangu, naona kabisa kama niko kwenye majaribu makubwa.
Nimejaliwa watoto wangu wawili, na nikahisi wananitosha kabisa.
Hapo nikachukua uamuzi wa kuweka kipandikizi mkononi.
Baada ya mwaka mmoja kupita, kile kipandikizi kikaniletea maudhi mengi, hivyo nikakitoa miezi mitatu iliyopita.
Miongoni mwa maudhi hayo ilikuwa kupotea kabisa kwa hamu ya mambo ya ndoa. Baada ya kukitoa, mwezi wa kwanza sikuona mabadiliko yoyote.
Lakini mwezi wa pili… mambo yakaanza kubadilika ghafla.
Wakati wa ovulation nilijikuta napata hisia kali sana.
Hadi nikajikuta nashindwa kuelewa kinachoendelea hamu imekuwa kali mno. Leo ndiyo nimekaa na kutafakari vizuri ndipo nikagundua kuwa chanzo kinawezekana ni mabadiliko ya homoni baada ya kutoa kipandikizi.
Aisee ndugu zangu, mpaka nimeongea na Mungu leo… sijui nifanye nini. Najisikia vibaya sana, kwa sababu nilishafunga kabisa mlango wa mambo ya watu wazima kwa kifupi nimekuwa nikiishi bila kufanya tendo la ndoa.
Baba wa watoto tumeachana kimkoa kutokana na kazi, ingawa tunalea watoto pamoja. Kwa hiyo muda mwingi niko “dry sell” tu.
Sihitaji kutenda dhambi, lakini majaribu yamekuwa makubwa kweli.
Naomba ushauri wenu.
Ninategemea kuanza mazoezi ya gym mapema mwakani, ili niachwe nikiwa nimechoka na kutofikiria mambo hayo.
Lakini kwa sasa nikiwa nimeshughulika sana mchana, nikilala au kupumzika kidogo tu hisia zinaongezeka.
Hali hii sikuwa nayo kabla ya kipandikizi, hivyo nahisi bado homoni hazijajibuana vizuri.
Naombeni ushauri jamani, maana hali inanipa hofu na kunitia wasiwasi.