Emmanuel_DWSS
Verified User
- May 30, 2023
- 2
- 11
Hali ya huduma ya Maji safi Dodoma.
Kufuatia ongezeko la watu katika jiji la Dodoma lililosababishwa na Serikali kuhamia Dodoma, mahitaji ya maji yaliongezeka kutoka Lita Milion 44 kwa siku mwaka 2017 hadi Lita Milion 133 kwa siku mwaka 2023. Vyanzo vyote vya maji vilivyopo Dodoma vina uwezo wa kuzalisha Lita Milion 67.8 kwa siku (takribani 50% ya mahitaji kwa kwa siku).
Ili kukabiriana na ongezeko hili, Serikali Ilitenga kiasi cha 7.8bn kwaajili ya hatua za muda mfupi za kupunguza tatizo hili. Hatua hizo ni uchimbaji wa Visima virefu na kuviendeleza katika maeneo ya Mzakwe, Ihumwa, Nala, Ntyuka Chimalaa, Bahi, Kongwa na Chamwino.
Hatua hizi zimetupa matokea yafuatayo:-
1.0 DUWASA imeongeza Uzalishaji kutoka Lita Milion 61.5 hadi 67.8 kwa siku Mjini Dodoma.
2.0 Bahi imeongeza upatikanaji wa maji kutoka asilimia 37 hadi 95.
3.0 Chamwino imeongeza upatikanaji wa Maji kutoka asilimia 42 hadi 87.
4.0 Kongwa imeongeza upatikanaji wa Maji kutoka asilimia 44 hadi 88.
Aidha Serikali imetenga fedha kiasi cha Tsh. 23.8 bn kwaajili ya kuendelea kutekeleza kazi za muda mfupi za kuendelea kupunguza uhaba wa maji katika jiji la Dodoma hususani katika maeneno ya NZUGUNI, BIHAWANA na ZUZU.
Hatua za muda Muda wa kati na Muda mrefu
1.0 Ujenzi wa Bwawa la Farkwa.
- litatoa maji lita Milion 130 kwa siku
-Fedha za kuaza kujenga Bwawa na Mtambo wa kutibu maji zimepatikana - Dola Mil. 125.3 (phase 1). Kwasasa tayari wahandisi washauri (consultant) kwa ajili ya design review, catchment protection na panel of experts wamepatikana.
-Mradi utachukuwa muda wa miaka kati ya 5-7.
2.0 Mradi wa kuchukuwa maji kotoka Ziwa Victoria.
- Mradi huu upo katika hatua ya kumpata Mshauri (Consultant)
Hatua za Dharula
1.0 Mradi wa kuchukuwa maji kutoka katika Bwawa la Mtera.
- Mradi unalenga kuchukuwa maji lita Mil. 130 kwa siku
-Una umbali wa mita 131 kutoka Dodoma mjini.
- Unaweza kukamilisha ndani ya miaka mitatu
-Gharama yake ni Dola Mil 170.
-Mhandisi Mshauri (Consultant) yupo kazini na na anategemea kuwasilisha taarifa yake ya mwisho mwezi Juni tarehe 10 2023.
Tutaendelea kuwahabarisha hatua mbalimbali kadri zinavyotokea na kutekelezwa.
Asante
Eng. Emmanuel Mwakabole
DWSS-DUWASA
DODOMA
Kufuatia ongezeko la watu katika jiji la Dodoma lililosababishwa na Serikali kuhamia Dodoma, mahitaji ya maji yaliongezeka kutoka Lita Milion 44 kwa siku mwaka 2017 hadi Lita Milion 133 kwa siku mwaka 2023. Vyanzo vyote vya maji vilivyopo Dodoma vina uwezo wa kuzalisha Lita Milion 67.8 kwa siku (takribani 50% ya mahitaji kwa kwa siku).
Ili kukabiriana na ongezeko hili, Serikali Ilitenga kiasi cha 7.8bn kwaajili ya hatua za muda mfupi za kupunguza tatizo hili. Hatua hizo ni uchimbaji wa Visima virefu na kuviendeleza katika maeneo ya Mzakwe, Ihumwa, Nala, Ntyuka Chimalaa, Bahi, Kongwa na Chamwino.
Hatua hizi zimetupa matokea yafuatayo:-
1.0 DUWASA imeongeza Uzalishaji kutoka Lita Milion 61.5 hadi 67.8 kwa siku Mjini Dodoma.
2.0 Bahi imeongeza upatikanaji wa maji kutoka asilimia 37 hadi 95.
3.0 Chamwino imeongeza upatikanaji wa Maji kutoka asilimia 42 hadi 87.
4.0 Kongwa imeongeza upatikanaji wa Maji kutoka asilimia 44 hadi 88.
Aidha Serikali imetenga fedha kiasi cha Tsh. 23.8 bn kwaajili ya kuendelea kutekeleza kazi za muda mfupi za kuendelea kupunguza uhaba wa maji katika jiji la Dodoma hususani katika maeneno ya NZUGUNI, BIHAWANA na ZUZU.
Hatua za muda Muda wa kati na Muda mrefu
1.0 Ujenzi wa Bwawa la Farkwa.
- litatoa maji lita Milion 130 kwa siku
-Fedha za kuaza kujenga Bwawa na Mtambo wa kutibu maji zimepatikana - Dola Mil. 125.3 (phase 1). Kwasasa tayari wahandisi washauri (consultant) kwa ajili ya design review, catchment protection na panel of experts wamepatikana.
-Mradi utachukuwa muda wa miaka kati ya 5-7.
2.0 Mradi wa kuchukuwa maji kotoka Ziwa Victoria.
- Mradi huu upo katika hatua ya kumpata Mshauri (Consultant)
Hatua za Dharula
1.0 Mradi wa kuchukuwa maji kutoka katika Bwawa la Mtera.
- Mradi unalenga kuchukuwa maji lita Mil. 130 kwa siku
-Una umbali wa mita 131 kutoka Dodoma mjini.
- Unaweza kukamilisha ndani ya miaka mitatu
-Gharama yake ni Dola Mil 170.
-Mhandisi Mshauri (Consultant) yupo kazini na na anategemea kuwasilisha taarifa yake ya mwisho mwezi Juni tarehe 10 2023.
Tutaendelea kuwahabarisha hatua mbalimbali kadri zinavyotokea na kutekelezwa.
Asante
Eng. Emmanuel Mwakabole
DWSS-DUWASA
DODOMA