Mwendabure
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 2,138
- 1,045
Mapenzi ni ugonjwa mbaya sana!!
Wtu wanaipenda CCM....hadi wakuwa wajinga..!! Egypt kulikuwa na Dikteta akatolewa kwa nguvu ya umma..kaingia dikteta naye sasa hivi anashugulikiwa kwa nguvu ya umma pia!
Huoni sisi tulimtoa mkoloni mwingereza....Alieingia TANU/CCM katugeuka nae tuna mchenjia....akija CDM akaja kuboronga nae anachenjiwa tu.....
Mapambano huwa hayaishi........nani alikuambia duniani kuna kupumzika!!!???
kwa kauli hii, umesema ukweli ila tatizo walio madarakani wanadhani wao pekkee ndiyo wana sifa kamili ya kuwa WATANZANIA. WANACHOTAKIWA KUFANYA NI KUBADILI MTAZAMO WAO TU, NA KUPAMBANA NA UOVU, NAPO KTK HILI SHIDA INAKUJA PALE AMBAPO NAO NI WAOVU WA KUFA MTU. ILA UMESEMA UKWELI NAKUPONGEZA TENA WENGINE WAKE ZAO WALIpewa leso, fulana, chumvi, kofia kisha wakatoa ulaji kwa wenye meno. sasa wanaliwa wanalalamika.ila kama habasri hizi ni za kweli basi tunakoenda ni kubaya kuliko maelezo, walio madarakani wafahamu dhuruma haisimami daima ila haki ndio husimama daima na kudumuCcm mliiweka madarakani wenyewe!!!!!!!! Sasa malalamiko ya nini?
Jf imeingiliwa na watoto sasa ambao wanataka ku practice english kwa zile tuishen za mchikichini
Spika anatoka njombe mkuu na siyo masasi.
Walipokuwa Dodoma,Chadema tried to invent trouble,tried to put trouble where there was no trouble. Now someone is bothering them without a reason.
Ah,Masasi ndio nyumbani kwake Spika. I can understand why Chadema does not have many friends in Masasi.
mbinu na hila za ccm zimekwisha hiyo ndio njia ya kutupa nguvu na hoja kwa chadema ,makamanda wavumilie ukombozi huko karibu kikija kikosi cha makamanda wote watatoka na nguvu mpyaPamoja na Waziri Mkuu kuamuru kuwa wale wote waliokamatwa kwa uchochezi wa matukio ya vurugu Mtwara waachiwe hali ni kinyume kabisa kwani kila siku watu wanakamatwa hovyo. Kwa sasa watu wanakamatwa kwa kosa la kuwa wananchama wa CHADEMA. Jana huko Lulindi kata ya Namalenga kijiji cha Mitesa mwenyekiti wa kijiji hicho kupitia CHADEMA aitwaye GHADAFI amekamatwa saa 6 usiku na polisi wa Masasi. Alikamatwa pamoja na kaimu mtendaji wa kijiji hicho.
Jana hiyo hiyo yapata Mahabusu 110 walifikishwa mbele ya hakimu wa mahakama ya mwanzo. Kwa kuwa mahakama ya mwanzo ilichomwa moto hakimu alilazimika kuwasomea mashitaka yao katika chumba cha hakimu mkazi. Kosa kubwa linalowagharimu viongozi na wanachama wa CHADEMA ni kukutwa na kadi ya CDM. Kwa sasa imewalazimu wananchi kutembea na kadi za CCM kama njia pekee ya kunusurika na kukamatwa na polisi ambao wengi wao wametoka Tunduru na Songea.
Askari hawa wakija kukamata watu wanapora vitu mbalimbali vya ndani. Ukikutwa una TV unadaiwa risiti kama huna wanaichukua. Viongozi wote wa mashina wa CDM wamekamatwa. Kwa kweli hali ni mbaya sana. Hakuna chombo cha habari hata kimoja kinachotoa taarifa ya mambo yanayotokea huku. Wananchi wanadai kwamba vyombo vya habari vimenyamazishwa.
Viongozi kadhaa wa CHADEMA wa Masasi na karibu mkoa wote wa Mtwara wako katika wakati mgumu sana. Baadhi wamekimbia majumbani mwao na sasa wengine inasemekana kwamba wameenda DSM kujificha.
CCM wameamua kutumia jeshi la polisi kuhakikisha kwamba wapenzi, wanachama,viongozi na mashabiki wa CHADEMA wananywea na kuogopa kabisa kujitambulisha na chama chao. Hii sasa ni nchi ya vitisho. Sioni kama tutafika tuendako. Hali ni tete sana huko Mtwara.