Hakuna Ufiisadi kwa Dr. Slaa?

Noboka

JF-Expert Member
Nov 12, 2011
1,246
626
Ni mnafiki peke yake ndiye ambaye hawezi kukubali kuwa Dr. Slaa anaendelea kutoa mchango mkubwa kwenye ustawi wa maendeleo hapa Tanzania. Kwakuwa ufisadi ulioripotiwa na CAG umezigusa kwa kiasi kikubwa H/wilaya ambako fedha nyingi hupelekwa na serikali, sasa je huko H/wilaya ya Karatu hali ikoje? hakuna ufisadi kwenye hiyo H/Wilaya?, je kuna hati safi au chafu?
Nauliza hilo kwa maana kuwa ndiko anakotoka Dr. Slaa na wakati huo alikuwa ni mbunge tena M/kiti wa hesabu za serikali za mitaa, na hiyo H/W imekuwa chini ya uongozi wa CDM.
Mwenye taarifa atujuze.
 
Unataka majibu gani kama umesema CAG alishatoa ripoti? C ukasome hiyo ripoti sasa uone ili uje na nguvu ya hoja hapa badala ya kuleta blaa blaa zako hapa? Kwan CAG katoa ripot ya mwaka 2010? coz muda huo ndo Dr alikua Mbuge, we hukusoma taarifa za CAG wakati huo? Au umetuma? Unapokuja kwa watu makini, uje na taarifa za uhakika bana, jifunze kwa Dr. Slaa, kua na visibitisho sio unaleta hoja zako za kushinikiza! KAJIPANGE UMPYA
 
hakuna ufisadi karatu hati za almashauri ni safi nani angethubutu kula kwa vuvuzela,inamaana hajipendi?
 
Ni mnafiki peke yake ndiye ambaye hawezi kukubali kuwa Dr. Slaa anaendelea kutoa mchango mkubwa kwenye ustawi wa maendeleo hapa Tanzania. Kwakuwa ufisadi ulioripotiwa na CAG umezigusa kwa kiasi kikubwa H/wilaya ambako fedha nyingi hupelekwa na serikali, sasa je huko H/wilaya ya Karatu hali ikoje? hakuna ufisadi kwenye hiyo H/Wilaya?, je kuna hati safi au chafu?
Nauliza hilo kwa maana kuwa ndiko anakotoka Dr. Slaa na wakati huo alikuwa ni mbunge tena M/kiti wa hesabu za serikali za mitaa, na hiyo H/W imekuwa chini ya uongozi wa CDM.
Mwenye taarifa atujuze.

Nini maana ya ufisadi? Fisadi ni nani?
319813_10150823416927387_673232386_12280169_997406907_n.jpg haya ndo mambo ya kujadili haya. usitutoe kwenye mada na kutuletea utapeli wa kisiasa.
 
Unataka majibu gani kama umesema CAG alishatoa ripoti? C ukasome hiyo ripoti sasa uone ili uje na nguvu ya hoja hapa badala ya kuleta blaa blaa zako hapa? Kwan CAG katoa ripot ya mwaka 2010? coz muda huo ndo Dr alikua Mbuge, we hukusoma taarifa za CAG wakati huo? Au umetuma? Unapokuja kwa watu makini, uje na taarifa za uhakika bana, jifunze kwa Dr. Slaa, kua na visibitisho sio unaleta hoja zako za kushinikiza! KAJIPANGE UMPYA

Wewe ni mtu makini hiyo ripoti ya CAG ni ya mwaka gani wa fedha? usije ukawa unakurupuka tu kwa kuvutwa na upepo kumbe hata hiyo ripoti yenyewe hujasoma
 
Baada ya kuona ripoti yako, ikabidi niingie website ya NAO ili kujua yaliyojiri kwa mwaka ulioisha June 2011. Nimesoma na nimeona ripoti yao haikua mbaya ingawa ina mapungufu kidogo kwa kitaalamu Karatu wamepewa "Unqualified opinion". Hii inaonesha kuwa inasimamiwa vizuri ingawa nimeona pia kuna fedha nyingi zilipelekwa ila hazikutumika bila sababu ya msingi.

Sababu za kupata 'Unqualified opinion' ni;

  • Missing Payment Vouchers Shs.7,211,820
  • Improperly Vouched Expenditure Shs.63,988,179
  • Payables were understated by Shs.242,593,184
  • There were unadjusted stale cheques of Shs 41,522,125
 
hakuna ufisadi karatu hati za almashauri ni safi nani angethubutu kula kwa vuvuzela,inamaana hajipendi?

Ni kweli lakini kumbuka kuwa siku hizi hofu ya kuiba haipo, hata Bagamoyo kwa JK, watendaji walifisadi, unakumbuka sakata la Jerry Muro? Ni jambo jema huko Karatu, kama ni hivyo kuna kila sababu ya H/W zinazoongozwa na CDM kujifunza namna Karatu inavyoendeshwa, ikumbukwe watendaji ni wa serikali si wa CDM, wakiiba kwenye hizo H/W zilizoko chini ya CDM mtaulizwa kulikoni?
 
Mwezi wa April nilikwenda Karatu kuwaona ndugu na jamaa zangu..... kwa kweli Karatu ni somo kubwa na mfano mzuri kwa Halmashauri zote.... Nilikuwa nikifuatilia utekelezaji wa miradi yao.... ukianza na jengo la Halmashauri na la DC yamejengwa kwa ubora wa hali ya juu..... utadhani ni majengo yaliyojengwa zamani enzi za mwalimu ambapo hakukuwa na uchakachuaji... ni imara na madhubuti mithiri ya majengo ya shule zangu za zamani za Songea Boys na Mazengo...

Ukija madarasa ya shule za kata ndo usiseme....... yamesukwa vilivyo, hakuna darasa ambalo lina nyufa kama tunavyoshuhudia sehemu nyingine, na pia kata zote zina shule za kata.... na sasa wanampango wa kuchagua baadhi ya shule kuzipanua kuwa na madarasa ya kidatu cha sita na pia kuanzisha shule za ufundi.... miradi iko murwa, kila kijiji kina maji ya bomba...
 
Baada ya kuona ripoti yako, ikabidi niingie website ya NAO ili kujua yaliyojiri kwa mwaka ulioisha June 2011. Nimesoma na nimeona ripoti yao haikua mbaya ingawa ina mapungufu kidogo kwa kitaalamu Karatu wamepewa "Unqualified opinion". Hii inaonesha kuwa inasimamiwa vizuri ingawa nimeona pia kuna fedha nyingi zilipelekwa ila hazikutumika bila sababu ya msingi

Nashukuru kwa taarifa, hayo ni mapungufu ambayo kiukweli inabidi yafanyiwe maboresho na iwe angalizo kwa H/W zingine hususan zilizoko chini ya CDM, kwani huko kwingine watu wanashindana kuiba tu!
 
Mwezi wa April nilikwenda kuwaona ndugu na jamaa zangu..... kwa kweli Karatu ni somo kubwa na mfano mzuri kwa Halmashauri zote.... Nilikuwa nikifuatilia utekelezaji wa miradi yao.... ukianza na jengo la Halmashauri na la DC yamejengwa kwa ubora wa hali ya juu..... utadhani ni majengo yaliyojengwa zamani enzi za mwalimu ambapo hakukuwa na uchakachuaji... ni imara na madhubuti mithiri ya majengo ya shule zangu za zamani za Songea Boys na Mazengo...

Ukija madarasa ya shule za kata ndo usiseme....... yamesukwa vilivyo, hakuna darasa ambalo lina nyufa kama tunavyoshuhudia sehemu nyingine, na pia kata zote zina shule za kata.... na sasa wanampango wa kuchagua baadhi ya shule kuzipanua kuwa na madarasa ya kidatu cha sita na pia kuanzisha shule za ufundi.... miradi iko murwa, kila kijiji kina maji ya bomba...

Mtawatambua kwa matendo yao, kama ameweza hayo huko Karatu ni vema anasema anachotenda.
 
Uhusianishaji wako wa mambo hauna mantiki kabisa. Jitahidi sana kuweka vitu logically. In fact, when you have decided to give out your opinion, make sure you sit down and first think of how you can give correlation of issues.
 
Back
Top Bottom