Wandugu hawa Jamaa wanafanya haya kwa sababu wamepewa vikwazo vya kiuchumi, ni story ndefu turisha liongelea humu,issue ilianzia kuzalisha umeme kwa nuclear na ikaendelea NK kurutubisha miozi sasa kurutubisha miozi hawa wakubwa hawataki kwa sababu ukiyarutubisha zaidi ndio miozi hatari ya nuclear ya kuangamiza kizazi hadi vizazi kama hutasimamia vizuri isiingie kwa magaidi,Mfano kwa Tanzania tunayo hayo madini ya Uranium yapo kusini Kule na tukanunua kinu kutoka Urusi tukarutubisha hayo madini tukapata miozi ya kuzalisha umeme,kwanza bei tutalipa hata sh.10 kwa Unit,pili tutazalisha umeme mwingi na tutauza nje ya nchi tatu viwanda vitapata unafuu kuzalisha bidhaa,hasara ni pale inapotekea janga kama Japan vinu vingi vilitawanya sumu,tukitaka tuwe kama NK tuanzishe hayo mambo bila ruhusa ya wakubwa wa dunia.