We jidanganye tu hadi ushushiwe gunia la mkaa ndio utajuaWakati mwingine mtu ni mbaya ukiwa naye; siku akiondoka ndo utayaona mazuri yake ambayo hukuwahi kuyaona kabla. Huyo mke mbaya kwako; ndo mama mwema na mzuri kwa watoto wake (wenu). Itakuuma kuona watoto wako wamemkosa mama kwenye malezi, kwenye hatua zao za kimaisha etc. Watakapolia utaumia tu na kulia nao. Wewe na wema wako wote, huwezi kuwa mama kwa watoto wako regardless utajitahidi vipi kuziba hilo pengo; kuna kitu tu kitamiss. Wakati mwingine kwenye maisha hauhitaji mtu wa kukufanyia makubwaa: but mtu tu wa kumuita "baba au mama au dada au kaka, mke, mume n.k; ........wa kumuita tu
Kuna hii familia; baba alikuwa anarudi usiku amelewa, anakimbiza nyumba nzima na panga;yaani ilikuwa tafrani. Ikatokea yule baba akafa; yule mama analia hadi leo anasema bora hata mumewe angekuwepo tu pamoja na tabu zote alizokuwa anawapa. Alikuwa na matatizo yake; but angalau familia ilikuwa na uhakika wa kula; watoto kwenda shule, mahali pa kulala, kutibiwa etc. Pumzi ni kitu cha thamani sana