Watetezi wa haki za Binadamu chini ya Mwamvuli wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDs),1 kwa ushirikiano na wadau wengine tunapinga vikali kufungiwa kwa gazeti la MwanaHalisi na Serikali mnamo tarehe 30th Julai 2012 kwa kutumia Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 Sura ya 229. Tunatambua kwamba Mwanahalisi ni gazeti la kujitegemea na la kichunguzi hapa
Tanzania.
Kwa pamoja, tumeona kuwa kufungiwa kwa Gazeti hili kunaonesha dhahiri nia ya serikali kuleta hofu na kuwanyamazisha wapigania haki za binadamu, vyombo vya habari, na watetezi wa haki za binadamu. Gazeti hili la MwanaHalisi limekuwa likitoa taarifa kwa umma kuhusu nani wahusika kwenye sakata la kutoweka na kuteswa kwa Dr Ulimboka, baada ya kuona serikali imelifumbia macho swala hili Mwahalisi limekuwa likifanya taarifa za kichunguzi ambazo zimekuwa zikitolewa kwenye mfululizo wa matoleo ya magazeti ya Mwanahalisi.
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDs) tumeguswa na swala hili na tumeona kuwa hii ni nia dhahiri ya Serikali kuvizuia vyombo vingine kutokuzungumzia masuala nyeti yenye maslahi ya umma Tunahofia kuiona Serikali inatumia sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976 Sura ya 229, ambayo ni moja ya sheria mbovu na isiyo na misingi ya haki za binadamu. Sheria hii kwa miaka mingi imekuwa ikipigiwa kelele na ni sheria kandamizi, pia na ni sheria ambayo inapingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
<<<HABARI KAMILI>>>
Tanzania.
Kwa pamoja, tumeona kuwa kufungiwa kwa Gazeti hili kunaonesha dhahiri nia ya serikali kuleta hofu na kuwanyamazisha wapigania haki za binadamu, vyombo vya habari, na watetezi wa haki za binadamu. Gazeti hili la MwanaHalisi limekuwa likitoa taarifa kwa umma kuhusu nani wahusika kwenye sakata la kutoweka na kuteswa kwa Dr Ulimboka, baada ya kuona serikali imelifumbia macho swala hili Mwahalisi limekuwa likifanya taarifa za kichunguzi ambazo zimekuwa zikitolewa kwenye mfululizo wa matoleo ya magazeti ya Mwanahalisi.
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDs) tumeguswa na swala hili na tumeona kuwa hii ni nia dhahiri ya Serikali kuvizuia vyombo vingine kutokuzungumzia masuala nyeti yenye maslahi ya umma Tunahofia kuiona Serikali inatumia sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976 Sura ya 229, ambayo ni moja ya sheria mbovu na isiyo na misingi ya haki za binadamu. Sheria hii kwa miaka mingi imekuwa ikipigiwa kelele na ni sheria kandamizi, pia na ni sheria ambayo inapingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
<<<HABARI KAMILI>>>