Haki na amani: Mifano inayotolewa haifanani na hali halisi

Haki na amani: Mifano inayotolewa haifanani na hali halisi

Zawadini

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2012
Posts
2,937
Reaction score
2,149
Wanajamvi; nimeamka nikaona niseme kidogo. Kumekuwa na matukio mawili ambayo yamekuwa yakielezwa kama kigezo cha taswira njema kwa yaliyotokea nchini mwetu wakati na baada ya uchaguzi. Matukio hayo mawili ni fainali za AFCON25 na uchaguzi wa Uganda.

1. Katika fainali za AFCON, watu humu wamempongeza kocha wa Senegal kwa kuitoa uwanjani timu yake kwa kutoridhishwa na uamuzi wa mwamuzi kuipa penalti Morocco. Ila kwa kutumia uzoefu na hekima za mchezo alizonazo kimataifa, Sadio Mane akairejesha timu uwanjani, penalti ikapigwa na mchezo ukaendelea. Hivi leo yule kocha kamiminiwa lawama na huenda akaadhibiwa. Kama si busara na weledi wa Sadio Mane timu ya Senegal huenda ingekuwa inakabiliwa na adhabu. Sasa yale madai kuwa Senegal imefuata nyayo za chama fulani, huenda si nyayo sahihi.

2. Kuhusu uchaguzi nchini Uganda, tumeoma humu watu wakisema kwenye uchaguzi hule, Museveni hakuua ie hakukuwa na mauaji. Hili ni sahihi, ila pia kwenye uchaguzi hule chama kikuu cha upinzani hakikususia uchaguzi na zaidi kilisimamisha mgombea - Bobby Wine. Aidha hakuna mtu alimzuia mtu kuenda kupiga kura seuze kumpiga kwa kuamua kutumia haki yake ya kupiga kura. Sikuona wala kusikia kulikuwa na maandamano seuze uharibifu au wizi. Hivyo basi, ulinganishaji wa matukio haya mawili na yale ya kwetu, nayaona hayafanani.

Karibuni kwa michango. Sijatukana na kwa hivyo sitarajii matusi. Ada ya mja kunena muungwana ni vitendo.
 
Matusi yanajulikana mkuu.
Inaonekana ufanano kwako ni hadi wafanane rangi ya jezi. Kufanana sio lazima iwe 100% bali ni uwiano fulani. Ww ni wale ukisikia baba anafanana na binti yake utasema wanafananaje wakati binti ni ke, na baba ni me?
 
Kabla ya kuchangia hebu tuambie matusi kwako ni yepi ili tusije tukatoa maoni yetu ukasema tumekutukana.
Matusi yanajulikana mkuu
Inaonekana ufanano kwako ni hadi wafanane rangi ya jezi. Kufanana sio lazima iwe 100% bali ni uwiano fulani. Ww ni wale ukisikia baba anafanana na binti yake utasema wanafananaje wakati binti ni ke, na baba ni me?
Mkuu; sio lazima wafanane rangi ila wafanane kiuhalisia.
 
Matusi yanajulikana mkuu

Mkuu; sio lazima wafanane rangi ila wafanane kiuhalisia.
Sasa ww umepewa mifano unataka kila kitu kifanane, sasa huko ni kufanana gani?
 
Sasa ww umepewa mifano unataka kila kitu kifanane, sasa huko ni kufanana gani?
Sijataka kifanane kila kitu ila kifanane kiuhalisia. Mifano niliyoisemea ni AFCON na Uganda ambayo maelezo hayaendani na yaliyotokea.
 
Back
Top Bottom