Uchaguzi 2020 Haihitajiki Kampeni kwa Lissu kushinda urais

PSEUDOPODIA

JF-Expert Member
Aug 9, 2020
376
735
Jana nilikuwa kijiwe kimoja hivi cha madalali wa nyumba na viwanja hapa Dar es Salaam.

Watu walikuwa wanajadili kwa kina maswala ya usajili ya vilabu vya simba na Yanga.

Ghafla mada ikabafilika ghafla baada ya mzee mmoja niliekuwa nnamfahamu ambaye ana bint yake aliyefaulu form 4 kwenda form 5.

Mada ilibafilika baada ya Mimi kumuuliza mzee bint yako alipangiwa kombi gani, mzee kwa kulalamika akajibu kuwa alifaulu sayansi ila wakampanhia HKL .

Mara jamaa mmoja akadakia, duuh anza kumtafutia mtaji kabisa akimaliza chuo aanze biashara. Maana siku hizi ajira hakuna. Mada ikakolea baada ya watu kuanza kumuhesabia magufuli miaka aliyobakiza hata kama atashinda tena. Ikaonekana yule mtoto paka amalize chuo magufuli atakuwa kashaondoka madarakani.

Fundi ujenzi mmoja akadakia kuwa, Huyu bwana safari hii hapiti, Amefanya maisha yamekuwa magumu kwelikweli. Kipindi cha Nyuma kazi zilikuwa nyingi paka tunazikimbia, leo zunguka mji wote huu utakuta sehemu zinazojengwa hazizidi hata tatu. Mimi 2015 nlimpigia kura ila mwaka huu simpigii.

Madalali nao wakadakia kuwa hata kwao hali ni hiyohiyo. Yaani huyu jamaa wakiskia ameshindwa watafurahi sana.

Nlichokiona Jana kwa hili kundi na makundi mengine ya Bodaboda, Mamantilie, Wajasiriamali wadogowadogo ni kuwa karibu wote wanata Magufuli aondoke. Yaani hata itokee tume ya uchaguzi waseme Uchaguzi ni kesho na hakuna kampeni Basi Magu anashindwa vibaya sana ingawa yeye kafanya kampeni karibu miaka mitano na bado zinafanyika juhudi za kutosha ili Lisu asisikike. Nilichokiona ni kuwa Lisu haitaji Kampeni wala habari zake ziwafikie watu. Ila watu wenyewe wapo tayari kumchagua bila hata kumsikia.

Ni hayo tu.
 
Sioni Magufuli akipata hata 30% ya kura. Atapata kura za akina Makonda na ndugu zake wa Chatto anaowapa uteuzi kila siku.

Wa Tanzania wote au wenyewe au ndugu zao amewaathiri kimaisha kwa maamuzi haya:-
-Kuwaondoa wanafunzi wa UDOM waliokuwa wanasoma ualimu wa sayansi
- Kufuta wafanyakazi wa vyeti feki
- Kuwatumbua wafanyakazi bila kufuata sheria
- Kutopandisha mshahara na madaraja
- Kutotoa ajira kwa wahitimu wa vyuo
- Kuvunja nyumba za Kimara na kuachia za Mwanza
- Kubagua maendeleo majimbo ya wapinzani kama Kilwa
- Kuzuia wanafunzi wenye mimba wasiendelee na masomo
- Kumtimua CAG makini kwa vile kuulizia ufisadi wa Tsh 1.5 Trilion
-Kuua wakosoaji kama BenSaa Nane na Azory Gwanda
- Kutumia vibaya fedha za Serikali kama ujenzi wa kiwanja cha Ndege Chato na mbuga ya Burigi
- Kuwaweka rumande wafanyabiashara kwa makosa ya kubambikiza kama Rugemalira
-Kuwabambikiza makosa wakosoaji kama Kabendera
- Kutunga sheria kandamizi
-Kutawala kwa kidikteta
- Kuvuruga wafanyabiashara kama Yusuf Manji
 
Kuna watu mnajua kijifariji duuu mungu azidi kuwatia nguvu hasa kwenye maisha binafsi mzidi kuwa na mioyo zaidi ya hiyo
 
Kuna watu mnajua kijifariji duuu mungu azidi kuwatia nguvu hasa kwenye maisha binafsi mzidi kuwa na mioyo zaidi ya hiyo
Mapinduzi duniani huwa hayafanywi na watu wote bali hufanywa na wachache waliojitoa kwa ajili ya watu wote.

Fidel Castro au Che Guevara waliongoza mapinduzi kuwatoa watawala madikteta ili wananchi walio wengi waweze kuishi maisha yenye uhuru na maendeleo.

Waoga kama wewe mtoa post endleeni kukaa makwenu, waachieni akina Lissu wafanya kazi waliyojitolea.
 
Lisu ana viunzi viwili tu, cha tarehe 25 August mbele ya Jaji Kaijage, na kingine ni ujuzi wa IT.
 
Kuna watu mnajua kijifariji duuu mungu azidi kuwatia nguvu hasa kwenye maisha binafsi mzidi kuwa na mioyo zaidi ya hiyo


Wewe subiri pesa ya rushwa kama huyu mwenzako aliyejificha na pesa kwenye kofia

pesa ndani ya kofia.jpeg
 
Back
Top Bottom