JICHO LA TATU
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 306
- 49
Habari wajameni nina kaka yangu mmoja hivi sasa yeye anatatizo linalomsumbua.Alikuwa na uhusiano na binti mmoja wa Kiarabu katika mahusiano yao binti akapata mimba hivyo akazaa naye mtoto, kwenye maisha yao yote binti alikuwa akiishi kwao kwani wazazi wake walikuwa hawako tayari kuona binti yao anaolewa na mtu wa dini tofauti isitoshe wametofautiana kwa mengi sana binti kwao hali nzuri kaka yangu mie kawaida tu. Sasa jana amepata habari binti amempigia simu anamwambia kuwa wazazi wao wamemtafutia mchumba ambaye ni Mwarabu mwenzao hakuwahi kuwaza kitu kama hicho na huyo mtu walomtafutia hamjui na wamemwambia sio jukumu lake kumjua kinachotakiwa ni ndoa tu, hivyo binti analia amechanganyikiwa, ndoa ni siku yoyote kuanzia wiki ijayo sasa my bro hajui afanye nini, tafadhali naombeni msaada wa mawazo yenu.