Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
- Thread starter
- #21
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 20
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500
ILIPOISHIA:
Mmh! Mtoto wa kike nilianza kuamini kauli za Side Butamu kwamba yeye kaumwa kwa viungo vyote vitamu duniani. Japokuwa niliinjoi mapenzi kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu. Lakini niliona fedheha kushindwa na kinyangarakata kama Side ambacho hata mkononi hakijai. Mpaka tunakwenda mapumziko Side alikuwa anaongoza tena kwa pointi nyingi.
SASA ENDELEA...
Niliamini nilimdharau na tamaa zangu za mwili ndizo zilizofanya nifanye mapenzi na mtu asiye na hadhi kama Side Butamu kama alivyojinadi. Kwanza alikuwa maskini pili alikuwa mlemavu wa miguu iliyolemaa na kutembea kwa kujivuta kwa makalio.
Nilimuangalia Side Butamu aliyekuwa amejilaza pembeni yangu kama kifurushi cha mzigo akiangalia juu kwenye dali bila wasi kuonesha hakubahatisha.
“Side ni kweli au umenibahatisha?”
“Mara nyingi ukisema kilicho ndani ya uwezo wangu, siwezi kukuhonga pesa ila nina uwezo wa kukupa penzi la kweli. Na leo ni woga kama tupo sehemu tulivu mbona leo ungeomba talaka kwa mumeo,” Side alijitapa.
“Utani huo Side?”
“We mwenyewe si umeuona muziki usio zima kwa umeme wa mgao?”
Mmh! Side jamani alinitisha kwa majingambo yake, lakini sikuwa wa kukubali kushindwa kirahisi. Baada ya mapumziko mafupi tulirudi kwenye ungwe ya pili. Kama kawaida Side alianza kwa kasi ile ile ya mwanzo na kuzidi kuniweka katika wakati mgumu.
Nami sikutaka kurudi nyuma tukakutana wote katikati ya uwanja ikawa piganikupige, Side alikuja juu nami nilimfuata hukohuko. Nilijikuta nikimwaga chozi mtoto wa kike kwa penzi tamu la Side Butamu. Mtoto wa kike wazimu wa mapenzi ulinipanda na kujituma vilivyo kulinda hadhi yangu.
Sikuamini mtu kama yule mlemavu asiye na hadhi yoyote kunipeleka puta kama gari kwenye njia mbovu. Katika ya mpambayo nilishangaa kumuona Side akitulia na kuanza kutokwa povu zito mdomoni. Macho yalimbadilika na kutazama juu kama ugonjwa wa kifafa.
Mungu wangu! Nilijua nimeishaua kumzidishia dozi kaka wa watu, yeye mapenzi starehe mwenzie sehemu ya maisha yangu kama kuvuta pumzi.
Nilishtuka na kuruka pembeni na kuanza kumwita.
“Side...Side.. Side Buta..”
Side hakuitikia zaidi ya kukoroma huku povu likimtoka, tumbo lilikuwa limerudi ndani kidogo likutane na mgongo. Wakati nimepagawa nafikiria jinsi ya kumsaidia Side, mlango uligongwa kwa nje. Sauti ya mume wangu ilizidi kunichanya na kujiona nimekwisha mtoto wa kike.
Nilijiuliza imeanza lini mume wangu kurudi bila kunijulisha, niliona nimeumbuka mchana kweupe. Talaka niliiona mbele ya sura yangu, wazo la haraka lilinituma nikamfiche Side bafuni. nilimbeba kama furushi na kwenda kumbwaga bafuni kisha nguo zake nilizificha chini ya uvungu.
Muda wote huo mume wangu alikuwa akigonga mlango huku akiniita kwa jina langu.
Nilijifuta jasho lililokuwa likimwagika kama maji, kisha nilifungua mlango na kukutana na mume wangu aliyekuwa amefura kwa hasira.
“Imeanza lini kujifungia mlango kwa ndani?” mzee Kupe alifoka.
“Nawe imeanza lini kurudi bila kunijulisha?” badala ya kumjibu nami nilimbana kwa swali.
“Nimekupigia simu hupokei, nimetuma mtu hufungui ulitaka nisifanye kazi zangu, nimeamua kuja mwenyewe. Mbona kama ulikuwa una...!!” Moyo ulipasuka pa! nikajua nimeumbuka mtoto wa kike, lakini niliwahi kumkata kauli.
“Nafanya nini? si nilikuwa nimelala.”
“Mbona mwili unatoka jasho?” akiniuliza huku akinichunguza.
“Niliota ndoto mbaya sana.”
“Ndo utoke jasho namna hiyo kama ulikuwa unacheza mieleka?”
“Mume wangu hata sijui ni nini, kama jinamizi lilinikaba na kuteseka kwa muda huku jasho likinitoka. Yaani kugonga kwako mlango ndio kumenitoa kwenye ndoto hiyo sijui ungechelewa ingekuwaje labda ungekuta mkeo nimekufa,” nilitengeneza uongo huku nikijifuta jasho ambalo bado liliendelea kutoka japo chumba kilikuwa na kiyoyozi.
Mume wangu alinipita na kuelekea msalani, nilitaka kumzuia lakini nilijiuliza atanielewaje ikiwa sijawahi kufanya kitendo kama kile hata siku moja. Nilijikuta nikisimama kama sanamu na kumsindikiza kwa macho. Nilijiuliza mlango wa bafuni niliufunga au la, niliamini kwa mchecheto niliokuwa nao sikukumbuka kuufunga.
Nilimuomba Mungu asimuone kwani ilikuwa aibu kubwa kukutwa na mwanaume nikifanya mapenzi wenye kitanda chake kibaya zaidi mlemavu. Nikiwa naomba dua kimoyomoyo, haikuzuia chochote. Dua langu halikufika popote nilisikia sauti kali ya mume wangu ikiniita.
“Mooreen hiki nini?”
Mara alitoka na Side akimburuza kwa kukishika kiguu chake kimoja.
“Moureen mke wangu ni uchafu gani unafanya? Unadiliki kufanya mapenzi na mlemavu, ni aibu gani hii?” Mzee Kupe alianza kulia.
“Nisamehe mume wangu ni shetani tu kanipitia,” nilijitetea huku nikipiga magoti mbele yake.
“Sawa kakupitia, lakini si kwa mlemavu kama huyu mke wangu aibu gani hii. Umelazimisha tumpe nafasi afanye kazi kumbe mwanaume wako?” Mzee Kupe alisema kwa hasira.
Mume wangu angejua wala asingesema kauli ile, Side alikuwa zaidi ya wale wanaovaa masuti na miili mikubwa ya mazoezi. Kwangu Side ndiye niliyemuoina mwanaume wangu wa shoka.
“Kweli ni mlemavu, lakini yote umeyataka wewe,” mtoto wa kike baada ya kuona maji yapo shingoni nilimtolea uvivu kwa kumwaga mchele mbele ya kuku.
“Yapi hayo?” nilimuona akishtuka macho yamemtoka pima.
“Unikidhi haja zangu muhimu umekuwa ukinipaka shombo tu kila siku.”
“Kwa mtindo huo utaniua kwa ukimwi.”
“Kwa hiyo unaamua nini?” Nilimuuliza nikiwa nimemshikia kiuno nilijua kama mbwai, mbwai tu.
“Kila mtu achukue chake, nitaendelea kuchukua Changudoa kama zamani nijue moja kuliko kufuga changudoa mama huruma.”
“Vyovyote vile, hata mimi nimechoka kupakwa shombo, mwili huu unatakiwa kutumiwa na wanaume wenye nguvu sio wewe kibabu. Kwanza shukuru nimekuvumilia muda wote lakini nimekuwa nikiteseka kila kukicha,” nilijua chakula hakiliki tena kwa vile Mzee Kupe alikuwa amemwaga ugali nami nikamalizia kwa kumwaga mboga.
“Kabla ya yote uondoe uchafu wako mbele ya macho yangu.”
Muda huo Side alikuwa amerudiwa na hali yake ya kawaida, kutokana na woga uliomtawala haja ilimtoka pale chini. Nilimtolea nguo zake chini ya uvungu na kumpa, kutokana na kuchanganyikiwa Side alijikuta akivaa kaptula yake kichwani.
Nilijikuta nikitaka kucheka, lakini nilimuonea huruma nilimsaidia kuvaa nguo zake na kumruhusu aondoke. Niliamini Side hakuamini jinsi alivyoachwa bila kuguswa. Baada ya kuondoka vita ikabakia kwangu, mume wangu aliamua tuachane.
“Mi nafikiri tumeshindwana, siwezi kutunza uchafu ndani mwangu.”
“Nami siwezi kukaa na mwanaume mchelemchele.”
“Ndiyo nini, unanitukana?”
“Sikutukani, ukweli ndiyo huo.”
“Sawa hata ukinitukana, lakini kama nilivyosema kila mtu achukue ustaarabu wake kwa vile wewe ni kunguru hufugiki.”
“Poa, mi’ kunguru nawe nyoka mtembelea tumbo unayetaka kukimbia wakati miguu huna, unataka wanawake vijana wakati mwenyewe nguvu za kupepea, utaliwa mali zako kila siku.”
Nini kitaendelea?
SEHEMU: 20
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500
ILIPOISHIA:
Mmh! Mtoto wa kike nilianza kuamini kauli za Side Butamu kwamba yeye kaumwa kwa viungo vyote vitamu duniani. Japokuwa niliinjoi mapenzi kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu. Lakini niliona fedheha kushindwa na kinyangarakata kama Side ambacho hata mkononi hakijai. Mpaka tunakwenda mapumziko Side alikuwa anaongoza tena kwa pointi nyingi.
SASA ENDELEA...
Niliamini nilimdharau na tamaa zangu za mwili ndizo zilizofanya nifanye mapenzi na mtu asiye na hadhi kama Side Butamu kama alivyojinadi. Kwanza alikuwa maskini pili alikuwa mlemavu wa miguu iliyolemaa na kutembea kwa kujivuta kwa makalio.
Nilimuangalia Side Butamu aliyekuwa amejilaza pembeni yangu kama kifurushi cha mzigo akiangalia juu kwenye dali bila wasi kuonesha hakubahatisha.
“Side ni kweli au umenibahatisha?”
“Mara nyingi ukisema kilicho ndani ya uwezo wangu, siwezi kukuhonga pesa ila nina uwezo wa kukupa penzi la kweli. Na leo ni woga kama tupo sehemu tulivu mbona leo ungeomba talaka kwa mumeo,” Side alijitapa.
“Utani huo Side?”
“We mwenyewe si umeuona muziki usio zima kwa umeme wa mgao?”
Mmh! Side jamani alinitisha kwa majingambo yake, lakini sikuwa wa kukubali kushindwa kirahisi. Baada ya mapumziko mafupi tulirudi kwenye ungwe ya pili. Kama kawaida Side alianza kwa kasi ile ile ya mwanzo na kuzidi kuniweka katika wakati mgumu.
Nami sikutaka kurudi nyuma tukakutana wote katikati ya uwanja ikawa piganikupige, Side alikuja juu nami nilimfuata hukohuko. Nilijikuta nikimwaga chozi mtoto wa kike kwa penzi tamu la Side Butamu. Mtoto wa kike wazimu wa mapenzi ulinipanda na kujituma vilivyo kulinda hadhi yangu.
Sikuamini mtu kama yule mlemavu asiye na hadhi yoyote kunipeleka puta kama gari kwenye njia mbovu. Katika ya mpambayo nilishangaa kumuona Side akitulia na kuanza kutokwa povu zito mdomoni. Macho yalimbadilika na kutazama juu kama ugonjwa wa kifafa.
Mungu wangu! Nilijua nimeishaua kumzidishia dozi kaka wa watu, yeye mapenzi starehe mwenzie sehemu ya maisha yangu kama kuvuta pumzi.
Nilishtuka na kuruka pembeni na kuanza kumwita.
“Side...Side.. Side Buta..”
Side hakuitikia zaidi ya kukoroma huku povu likimtoka, tumbo lilikuwa limerudi ndani kidogo likutane na mgongo. Wakati nimepagawa nafikiria jinsi ya kumsaidia Side, mlango uligongwa kwa nje. Sauti ya mume wangu ilizidi kunichanya na kujiona nimekwisha mtoto wa kike.
Nilijiuliza imeanza lini mume wangu kurudi bila kunijulisha, niliona nimeumbuka mchana kweupe. Talaka niliiona mbele ya sura yangu, wazo la haraka lilinituma nikamfiche Side bafuni. nilimbeba kama furushi na kwenda kumbwaga bafuni kisha nguo zake nilizificha chini ya uvungu.
Muda wote huo mume wangu alikuwa akigonga mlango huku akiniita kwa jina langu.
Nilijifuta jasho lililokuwa likimwagika kama maji, kisha nilifungua mlango na kukutana na mume wangu aliyekuwa amefura kwa hasira.
“Imeanza lini kujifungia mlango kwa ndani?” mzee Kupe alifoka.
“Nawe imeanza lini kurudi bila kunijulisha?” badala ya kumjibu nami nilimbana kwa swali.
“Nimekupigia simu hupokei, nimetuma mtu hufungui ulitaka nisifanye kazi zangu, nimeamua kuja mwenyewe. Mbona kama ulikuwa una...!!” Moyo ulipasuka pa! nikajua nimeumbuka mtoto wa kike, lakini niliwahi kumkata kauli.
“Nafanya nini? si nilikuwa nimelala.”
“Mbona mwili unatoka jasho?” akiniuliza huku akinichunguza.
“Niliota ndoto mbaya sana.”
“Ndo utoke jasho namna hiyo kama ulikuwa unacheza mieleka?”
“Mume wangu hata sijui ni nini, kama jinamizi lilinikaba na kuteseka kwa muda huku jasho likinitoka. Yaani kugonga kwako mlango ndio kumenitoa kwenye ndoto hiyo sijui ungechelewa ingekuwaje labda ungekuta mkeo nimekufa,” nilitengeneza uongo huku nikijifuta jasho ambalo bado liliendelea kutoka japo chumba kilikuwa na kiyoyozi.
Mume wangu alinipita na kuelekea msalani, nilitaka kumzuia lakini nilijiuliza atanielewaje ikiwa sijawahi kufanya kitendo kama kile hata siku moja. Nilijikuta nikisimama kama sanamu na kumsindikiza kwa macho. Nilijiuliza mlango wa bafuni niliufunga au la, niliamini kwa mchecheto niliokuwa nao sikukumbuka kuufunga.
Nilimuomba Mungu asimuone kwani ilikuwa aibu kubwa kukutwa na mwanaume nikifanya mapenzi wenye kitanda chake kibaya zaidi mlemavu. Nikiwa naomba dua kimoyomoyo, haikuzuia chochote. Dua langu halikufika popote nilisikia sauti kali ya mume wangu ikiniita.
“Mooreen hiki nini?”
Mara alitoka na Side akimburuza kwa kukishika kiguu chake kimoja.
“Moureen mke wangu ni uchafu gani unafanya? Unadiliki kufanya mapenzi na mlemavu, ni aibu gani hii?” Mzee Kupe alianza kulia.
“Nisamehe mume wangu ni shetani tu kanipitia,” nilijitetea huku nikipiga magoti mbele yake.
“Sawa kakupitia, lakini si kwa mlemavu kama huyu mke wangu aibu gani hii. Umelazimisha tumpe nafasi afanye kazi kumbe mwanaume wako?” Mzee Kupe alisema kwa hasira.
Mume wangu angejua wala asingesema kauli ile, Side alikuwa zaidi ya wale wanaovaa masuti na miili mikubwa ya mazoezi. Kwangu Side ndiye niliyemuoina mwanaume wangu wa shoka.
“Kweli ni mlemavu, lakini yote umeyataka wewe,” mtoto wa kike baada ya kuona maji yapo shingoni nilimtolea uvivu kwa kumwaga mchele mbele ya kuku.
“Yapi hayo?” nilimuona akishtuka macho yamemtoka pima.
“Unikidhi haja zangu muhimu umekuwa ukinipaka shombo tu kila siku.”
“Kwa mtindo huo utaniua kwa ukimwi.”
“Kwa hiyo unaamua nini?” Nilimuuliza nikiwa nimemshikia kiuno nilijua kama mbwai, mbwai tu.
“Kila mtu achukue chake, nitaendelea kuchukua Changudoa kama zamani nijue moja kuliko kufuga changudoa mama huruma.”
“Vyovyote vile, hata mimi nimechoka kupakwa shombo, mwili huu unatakiwa kutumiwa na wanaume wenye nguvu sio wewe kibabu. Kwanza shukuru nimekuvumilia muda wote lakini nimekuwa nikiteseka kila kukicha,” nilijua chakula hakiliki tena kwa vile Mzee Kupe alikuwa amemwaga ugali nami nikamalizia kwa kumwaga mboga.
“Kabla ya yote uondoe uchafu wako mbele ya macho yangu.”
Muda huo Side alikuwa amerudiwa na hali yake ya kawaida, kutokana na woga uliomtawala haja ilimtoka pale chini. Nilimtolea nguo zake chini ya uvungu na kumpa, kutokana na kuchanganyikiwa Side alijikuta akivaa kaptula yake kichwani.
Nilijikuta nikitaka kucheka, lakini nilimuonea huruma nilimsaidia kuvaa nguo zake na kumruhusu aondoke. Niliamini Side hakuamini jinsi alivyoachwa bila kuguswa. Baada ya kuondoka vita ikabakia kwangu, mume wangu aliamua tuachane.
“Mi nafikiri tumeshindwana, siwezi kutunza uchafu ndani mwangu.”
“Nami siwezi kukaa na mwanaume mchelemchele.”
“Ndiyo nini, unanitukana?”
“Sikutukani, ukweli ndiyo huo.”
“Sawa hata ukinitukana, lakini kama nilivyosema kila mtu achukue ustaarabu wake kwa vile wewe ni kunguru hufugiki.”
“Poa, mi’ kunguru nawe nyoka mtembelea tumbo unayetaka kukimbia wakati miguu huna, unataka wanawake vijana wakati mwenyewe nguvu za kupepea, utaliwa mali zako kila siku.”
Nini kitaendelea?