Hadithi : Suprise Ya Ajabu

Hadithi : Suprise Ya Ajabu

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,638
Image may contain: one or more people, close-up and text

HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 01
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

Mazoea kwa kweli ni ugonjwa pamoja na kuwa na kila kitu katika maisha yangu hakuna nilicho kikosa. Nilikuwa na maisha mazuri watoto wangu wote wana maisha mazuri, lakini tabia zangu mbaya ambazo nilishindwa kuziacha ndizo zilizonifikisha hapa. Nilitamani dunia ipasuke kwani ilikuwa aibu ya mwaka mbele ya watoto wangu. Pamoja na kufanya za Siri lakini leo nimeumbuka mbele ya wanangu, nasema Mimi tena basi.
****
Simu iliendelea kulia Martin aliacha gazeti na kuichua, alipoangalia namba zilikuwa za mdogo wake anayeishi Canada aliipokea
"Haloo Edna lete story mdogo wangu."
"Shikamoo kaka."
"Marahaba, za Otawa?"
"Nzuri, sijui za huko Bongo?"
"Za huku safi, mbona kimya?"
"Si mimi au ninyi, nyie ndiyo uliye nisusa."
"Tuachane na hayo siku zote upigapo simu huwa una jipya."
"Ni kweli kaka"
"Ehe lete story."
"Kaka ni hivi jana nimempigia asimu mama lakini sikumpata nilitaka nimualifu yeye kwanza ndio niwataalifu nyinyi kaka zangu, vipi na Moses hajambo?"
"Mmh! Yule kaka yako mtu wa safari si mnajua kazi za serikali kila kukicha anazunguruka na mheshimiwa."
"Basi ina maana hata kwa mama hamjaenda muda mrefu?"
"Ni kweli, kwa upande wangu nina mwezi sasa."
"Aah! Jamani mama yetu ni mmoja inatakiwa tuwe tunamtembelea hasa nyinyi uliye karibu."
"Ni kweli, shughuli zimetubana lakini nilipanga wiki ijayo niende kwa bi mkubwa."
"Sasa ni hivi mimi nilikuwa nipo njiani kuja huko."
"He! Mbona ghafla kuna nini?"
"Aah! Kaka kuja nyumbani mpaka pawepo na kitu, kwa mama yetu ni muhimu hata kila siku kumuona. Nampenda sana mama yangu na nikiolewa naondoka naye."
"Yaani wewe ndiye mwenye mapenzi kuliko watoto wake wote?"
"Ninyi mpo karibu lakini mwezi unapita bila kumtembelea bi mkubwa."
"Edna tuachane na hayo ulikuwa unasemaje mdogo wangu?"
"Ni hivi kaka yangu, huku nimepata mchumba ambaye yupo tayari kufunga ndoa na mimi."
"Hongera, ni raia wa nchi gani?"
"Ni Mkanada mwenye asili ya Afrika."
"Mmh! Haya, sasa ulikuwa unasemaje?"
"Tumekubaliana mimi nitangulie kuwajulisha kisha yeye atafuata, sijui kwa hilo mnasemaje kaka yangu?"
"Siyo baya sasa unakuja lini?"
"Wiki ijayo."
"Itakuwa vizuri maana nina imani tutakutana kwa mama."
"Basi mjulishe na kaka Moses."
"Basi unganisha mawasiliano ya watu watatu ili tulizungumze kwa pamoja."
Edna aliunganmisha mawasiliano ya watu watatu na kuanza kuzungumza na kaka yake Moses ambaye anamfuata kwa mara ya pili ambaye alikuwa katibu mkuu ofisi ya Rais.
"Haloo kaka."
"Ooh! Bibie za Canada?"
"Nzuri tu kaka, shikamoo”
“Marahaba, naona leo umenikumbuka mdogo wangu.”
“Nitafanya nini na ninyi mmenisusa.”
“Hapana mdogo wangu kazi za serikali nimenibana ila nitatulia tu.”
“Haya kaka, za misafara maana nasikia kila alipo rais na wewe upo."
"Nitafanyaje na mimi nimeichagua hii kazi."
"Vipi upo wapi kwa sasa?"
"Nipo Denmark."
"Mmh!" Edna aliguna.
"Mbona una guna ulikuwa unasemaje?"
Edna anamueleza yote kama aliyomueleza kaka yake mkubwa Martin na jinsi walivyo panga kukutana kwa mama yao wiki ijayo.
"Kumbe ni hivyo, hakijaharibika kitu mdogo wangu, wiki ijayo nitakuwa Tanzania na nitakuwa na mapumziko marefu ya wiki tatu kwa hiyo safari ya kwenda kwa mama tutakuwa pamoja."
"Wawooo, itakuwa bonge la Surprise," Edna alifurahishwa na maneno ya kaka yake.
"Sasa ni hivi tusimjulishe mama tumzukie bila yeye kujua akiamka asubuhi atukute mlangoni kwake hiyo unasemaje?"
"Si mchezo ni Bonge la Surprise," Edna aliunga mkono.
"Kwa hiyo wote tukutane kwa bwana mkubwa Arusha siku moja kabla ya kwenda kwa mama."
Walikubaliana wote watatu ambao ni watoto wa mama mmoja lakini hawakubahatika kumuona baba yao. Baada ya kuelezwa na mama yao kuwa baba yao alimkimbia na kumuachia watoto. Mama yao ambaye aliwalea watoto wake na kufaniwa kuwasomesha iliyo ya juu, ambao baada ya masomo kila mmoja alipata kazi nzuri.
Historia ya maisha ya mama yao iliyowafikisha pale, iliwafanya watoto wake wamlee mama yao kama mboni ya macho yao. Kuonesha wanamjali mama yao walimjengea jumba la kifahari sehemu za Mbezi na kumwekea wafanyazi pamoja na magari ya kutembelea.
Kila mmoja alikuwa na hamu ya kukaa na mama yake, lakini aliwakatalia kwa kusema kila mtu aishi maisha yake ili mwenye hamu afunge safari kumfuata.
Walikuwa watoto watatu wawili wa kiume na mmoja wa kike, wa kiume mmoja alikuwa mfanya biashara mkubwa wa madini ambaye pamoja na elimu yake aliyoipata Marekani aliamua kujikita kwenye biashara ya madini na kuweza kumiliki migodi miwili. Biashara ile ilimuingizia pesa sana na kumnfanya kuwa mtu maarufu wenye kutikisa jiji la Arusha.
Wa pili yeye ni katibu mkuu ofisi ya Rais ambaye na yeye alikuwa na maisha mazuri, alikuwa na majumba na magari ya kifahari na wa mwisho alikuwa msichana ambaye yeye alibahatika kupata kazi katika shirika moja la utangazaji nchini Canada.
Baada ya kukubaliana wote walipanga siku ya kukutana jiji Arusha tayari kwenda jiji Dar kwa mama yao bila kumjulisha kwa kumshtukiza. Kwa Upande wa Edna alikuwa na furaha isiyo na kifani kukutana na ndugu zake kwa mama yao na kuweza kuwaeleza kupata kwake mchumba.
Aliomba siku ile ifike upesi ili wamfanyie mama yao surprise ya ajabu kwa watoto wake kukutana kwa pamoja asubuhi baada kufungua mlango awakute mlangoni.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 02
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500
...ILIPOISHIA:
Baada ya kukubaliana wote walipanga siku ya kukutana jiji Arusha tayari kwenda jiji Dar kwa mama yao bila kumjulisha kwa kumshtukiza. Kwa Upande wa Edna alikuwa na furaha isiyo na kifani kukutana na ndugu zake kwa mama yao na kuweza kuwaeleza kupata kwake mchumba.
Aliomba siku ile ifike upesi ili wamfanyie mama yao surprise ya ajabu kwa watoto wake kukutana kwa pamoja asubuhi baada kufungua mlango awakute mlangoni.
SASA ENDELEA...
*******
Mipango ya ndugu watatu ilikwenda kama walivyotaka na siku ilipotimu walikutana wote jiji Arusha kwa mkubwa wao Moses. Kila mmoja walifurahia kumuona ndugu yake walikuwa wakipenda kwa kujifananisha na Masii eti wamezaliwa bila baba.
“Jamani kaka Mose shavu dodo.”
“Mbona humsemi Martin.”
“Yeye sitii neno kwa vile yupo kwenye mihela.”
“Hata wewe mdogo wetu Canada imekukubali,”
“Basi wote tumshukuru Mungu kutupa afya bora.”
“Lakini kaka zangu fanyeni mazoezi kidogo mwili huo una madhara.”
“Tumekuelewa.”
“Jamani safari yetu kesho alfajiri nimeisha kodi ndege.”
“Yaani sijui mama yetu atafurahije kutoana wanaye watatu tena alfajiri kabla ya kuamka.”
“Litakuwa bonge la surprise.”
“Natamani kesho ifike upesi tukanyonye kwa mama.”
Siku ile walikesha sebuleni wakizungumza mambo mengi, alfajiri iliwakuta palepale. Alfajiri ilipofika walielekea uwanja wa ndege na kuondoka na ndege ya kukodi.
Waliwasili jijini Dar majira ya saa kumi na mbili asubuhi asubuhi, baada ya kuteremka kwenye ndege walikodi gari na kwenda moja kwa moja hadi Mbezi walipomjengea kwa mama yao. Walisimamisha gari mbele ya lango, kwa vile hawakutaka kumshtua mama yao, waliingia waliteremka kwenye gari na kwenda kugonga geti ambalo lilifunguliwa na mlinzi.
Alipowaona alitaka kupiga kelele za furaha walimzuia kwani hawakutaka mama yao ajue kitu mpaka atakapofungua mlango na kuwaona wanaye watatu wamesimama mbele yake. Baada ya kuingia ndani walikwenda moja kwa moja mlangoni.
Mlango wa nyumba kubwa ulikuwa umefungwa kuonesha ndani bado wamelala. Walipofika kwenye mlango walibonyeza kengere zaidi ya mara tatu. Baada ya muda walisikia sauti ya mtu kutembea. Wote walikaa mkao wa kusema kwa sauti neno la” Surprise mamaaa.”
Mara mlango ulifunguliwa wakati wanajiandaa kusema surprise mama, walishangaa kumuona aliyefungua ni msichana wao wa kazi. Alipotaka kupayuka kwa furaha baada ya kuwaona, walimuonyesha ishara ya kidole mdomoni kuwa asipige kelele na yeye alifanya kama alivyoagizwa,
"Vipi mama amelala?" aliuliza Edna.
"Mama?” Ajabu Eliza msichana wa kazi badala ya kujibu na yeye akauliza swali.
“Eliza kwani nimekuuliza nani?”
"Ha..ha..yupo.”
“Hayupo! Amesafiri?"
"Ha..ha..pana.”
“Hapana! Sasa yupo wapi?”
“Jana alitoka hajarudi," Eliza alijibu huku akitafuna vidole kitu kilichowashtua na kutaka kujua kuna nini.
"Hajarudi? amekwenda wapi"
"Kwa kweli sijui aliniaga tu anatoka."
"Jamani maswali huku tumesimama sio mazuri tuingie ndani," Moses alishauri.
Kabla hawajaingia ndani msichana wa kazi aliponyanyua macho baada ya kusikia geti likifunguliwa alipiga ukelele.
"Ha!"
Kauli ile ya mshangao iliwafanya wote waligeuka nyuma na kukutana na sura ya mama yao akiwa kwenye hali ya umajeruhi. Kila mmoja alitaharuki mama yao alikuwa na bandeji kubwa kichwani na mkononi na mdomo ulikuwa umevimba.
Kilichowashangaza zaidi kilikuwa mavazi ya ajabu ya nusu uchi aliyokuwa amevaa manma yao. Yalikuwa ya aibu kila mtoto wa kiume aliangalia pembeni ili mama yao aingie ndani kwanza ili ajistiri mwili wake.
Edna alijikuta akibubujikwa na machozi kutokana na hali aliyokuwa nayo mama yake, hakujari mavazi yake zaidi ya majeraha aliyokuwa nayo. Wakati huo mama yao alikuwa amepigwa na butwaa kwa kuumbuka mbele ya wanaye na kujisemea moyoni "Mungu wa ajabu."
Baada ya kuingiza ndani na kubadili nguo kwa kuvaa nguo za heshima zilizoufichwa mwili wake. Edna aliwaita kaka zake wakati huo mama yao ambaye hakutegemea kuwakuta wanaye maeneo yale kibaya zaidi wote watatu. Mama alijikuta akiangua kilio huku kujiuliza atawambia nini wanaye kwa hali ile waliyomuona nayo kuwa anatoka wapi
Edna alimfuata mama yake huku akibubujikwa na machozi.
“Mama umeumia sana.”
Mama yake hakusema kitu aliendelea kulia akiwa amejiinamia.
“Mama kama umeumia sana twende hospitali, kina kaka tumpelekeni mama hospitali.”
“Kachukue funguo za gari tumuwahishe hospitali.”
“Wanangu siimwi kama mnavyofikiria.”
“Sasa mama unalia nini?”
“Wanangu nimeumbuka mchana kweupe.”
"Mama umepatwa na nini?" mama yao hakujibu kitu zaidi ya kuangalia chini huku machozi yakiendelea kumtoka.
"Mama au unasikia maumivu makali?"
Ilikuwa kitu tofauti na jinsi walivyomzoea mama yao kwa ucheshi na uchangamfu hasa anapokutana na wanaye. Walitegemea angefurahi kuwaona wanaye lakini imekuwa tofauti na walivyo fikiria zaidi ya kuona kilio cha mama yao ambacho toka wazaliwe hawajawahi kukiona.
Wote watatu walijikuta wakianza kulia, lakini Edna yeye ndiye aliyelia kwa sauti ya juu akiwa amepiga magoti mbele ya mama yake.
"Mama tatizo nini? Mbona unatuacha njia pana mama ni bahati gani kuwaona wanao wote. Tueleze umepatwa na nini ili tujue tukusaidieje. Mama umepatwa na nini mama yetu?"
Mama yao huku akilia alimpapasa mwanaye mgongoni kwa mkono mzima na kusema kwa sauti ya kilio.
"Wanangu silii kwa maumivu bali kwa majuto, Mungu kaniumbua."
"Majuto ya nini tena mama? Mungu kakuumbua nini?"
"Si waongo waliosema siku ya kwenda uchi ndiyo siku ya kukutana na mkweo."
"Mama mbona hatukuelewi?"
"Kilichopo mbele yangu najua ni mipango ya Mungu ili kuniumbua mama yenu."
"Mama bado hatujakuelewa akuumbue kwa lipi?"
"Ilikuwa siri ambayo ndiyo iliyobeba maisha yenu kwa ujumla."
"Ni siri! Iliyobeba maisha yetu. Ni siri gani hiyo mama?"
"Ni siri chafu ambayo hamkupaswa kuijua, nina imani Mungu kayafanya haya ili kuniumbua sina budi kuiweka bayana ili munielewe mama yenu najua kama nitakaa kimya nitawatesa wanangu mpaka mnakufa."
Watoto wake wote walitazamana kisha kila mmoja alirudisha macho kwa mama yake na kuendelea kumsikiliza kutaka kujua mama yao ana siri gani. Pia kutaka kujua ile hali aliyonayo mama yao imetokana na nini?
Mama yao akiwa bado ameinama alinyanyua macho na kuwatazama wanaye kila mmoja kisha alijitengeneza vizuri kitini na kusema:

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 03
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Sawa na mvuta sigara hawezi kulala bila kupata angalau mkupuo mmoja na mimi mama yenu hivyohivyo."
"Ni nini hicho, hebu mama kiweke wazi kwa vile umeamua kutueleza." Moses ambaye muda mwingi alikuwa kimya alimueleza mama yake.
Mama yao akiwa mwingi wa aibu waliwatazama watoto wake kwa zamu kwa mara nyingine kisha alisema:
SASA ENDELEA....

"Wanangu naweza sema maisha yangu mpaka kufikia hapa nimepitia mambo mengi machafu na magumu ambayo ukimuhadithia mtu ataona ni uongo," alivuta pumzi huku alitengeneza vizuri ushungi wake uliokuwa umemteremka.
"Basi wanangu maisha haya ingekuwa yanaonekana jinsi mwanadamu anavyoishi unaweza kumuonea huruma au kumdharau kama si kumchukia kabisa.
"Wanangu mnaweza kuona leo mama yenu naishi maisha mazuri hakuna nilichokikosa maishani kwa sasa, mmenijengea nyumba nzuri, gari zuri na kunipatia mahitaji yote muhimu. Ni kweli, lakini historia nzima ya maisha yangu inanihukumu.
“Sikupenda wanangu mjue maisha yenu yamepitia wapi mpaka leo mpo kwenye hali hii. Wanangu sikupenda lakini leo sina jinsi, bila hivyo hali mlionikuta nayo hamtanielewa kama nitawaeleza nusu nusu. Historia yangu mimi mama yenu inaanzia miaka thelathini na tatu iliyopita kabla sijayajua maisha ni nini.
MIAKA THELATHINI NA TATU ILIYOPITA
Nikiwa ni mtoto wa tatu katika familia ya watoto wanne, wa kiume watatu na wa kike mmoja, ambaye ndiye mimi mama yenu niliyekuwa kiziwanda. Kwa kweli baba yangu alikuwa akinipenda sana hasa tukizingatia ni mimi pekee mtoto wa kike na mama yangu hakuwa na uwezo wa kuzaa tena.
Nilipewa upendeleo ambao hata kaka zangu uliwaudhi, lakini hakuna kilichowabadilisha baba na mama yangu. Nilipofika hatua ya kwenda shule, nilitafutiwa shule ya kimataifa, tofauti na kaka zangu ambao wao japokuwa walisoma za kulipia, lakini hazikuwa na gharama kubwa kama yangu.
Kitu kingine kilichofanya wazazi wangu wasijutie uamuzi wao wa kunipeleka shule ya gharama ni akili yangu. Nilifanya vizuri katika masomo yangu na kushika nafasi za juu shuleni. Baba aliniahidi nikimaliza kidato cha sita atanipeleka Marekani kusoma.
Kama mjuavyo nilijikuta nabweteka na mapenzi ya wazazi wangu na kujua sitachukuliwa hatua yoyote kwa lolote nitakalo lifanya. Nikiwa kidato cha tano ambapo nilisomea Uganda, chuoni nilikutana na kijana mmoja ambaye ni Mtanzania mwenzangu, ambaye alinivuta kwenye mambo ya mapenzi.
Nilijikuta nafanya starehe kwa fujo bila kuogopa kitendo kile kitawaudhi wazazi wangu. Wakati huo yule kijana ambaye alikuwa mwaka wa mwisho, katika uhusiano wetu wa mapenzi kwa bahati mbaya nilishika ujauzito.
Nilifikiria kuutoa lakini nilihofia kwa kuambiwa kuwa pale shuleni kuna wasichana wawili walikufa kwa ajiri ya kutoa mimba. Habari zile zilinishtua sana na kunifanya niogope kutoa kwa kuhofia maisha yangu.
Katika uchunguzi wa afya za wanafunzi niligundulika mjamzito na kurudishwa nyumbani. Wakati huo bwana aliyenipa ujauzito alikuwa ameshaondoka na kurudi Tanzania. Sikuwa na jinsi zaidi ya kurudi nyumbani Arusha ambako ndipo nilipozaliwa.
Nilipofika nyumbani baba hakuwepo alikuwa amesafiri, nilimkuta mama ambaye alishangaa kuniona muda ule. Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa kupendwa na wazazi wangu, sikuhofia chochote nilimweleza yote.
Mmh! Kauli ile ilimshtua sana mama na kuniomba bora tuitoe ile mimba kabla baba hajarudi. Nilimkatalia kwa kuhofua maisha yangu.
"Mama mimba inaweza kuondoka na maisha yangu!"
"Hapana mwanangu hii ndiyo njia pekee ya kukuponya kwa baba yako."
"Mama, baba ananipenda hawezi kufanya lolote."
"Mwanagu humjui baba yako, mimi namjua vizuri hawezi kukubaliana na hili japo anakupenda sana."
"Wasiwasi wako tumsubiri uone."
"Hapana baba yako alimfukuza mdogo wake ambaye alikuwa akimpenda tena alikabidhiwa na wazazi wake amtunze na kumsomesha. Na yeye alifanya upuuzi kama wako baba yako alipojua mapenzi yote yaliisha na kumfukuza kama mbwa na hakutaka kumuona mpaka leo hii tunavyoongea anasema hataki kumuona"
"Mama yule alikuwa ni mdogo wake lakini mimi ni mwanaye," bado nilikuwa mbishi.
"Mwanangu usiwe mbishi, heri nusu shari kuliko shari kamili," mama aliendelea kunibembeleza.
Sikuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na mama kwenda kuitoa mimba kabla baba hajarudi ikiwezekana awahi kunirudisha shuleni. Mama alinipeleka hadi kwa daktari mmoja maarufu sana jijini Arusha.
Baada ya kukutana na daktari alikubaliana na mama gharama za kunitoa ujauzito. Mama alilipa na kupelekwa chumba cha kutolea mimba, niliingizwa chumba cha kutolea mimba. Nilifanyiwa vipimo kabla ya kunitoa, lakini mambo yalikuwa kinyume.
Ujauzito wangu ulikuwa umekaa vibaya ambao usingiweza kutoka kama wangeutoa, ungetoka na roho yangu. Hapo mama alichanganyikiwa na kushindwa kujua atatumia njia gani kuificha siri ile. Hakuamini kauli ya daktari yule tulikwenda hospitali zaidi ya nne jibu lilikuwa lile ile, kuwa mimba haiwezi kutoka.
Mama hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokeo na kuamua kumsubiri baba na yeye ana uamuzi gani. Japokuwa mama alionekana mwenye wasiwasi, kwa upande wangu sikuwa na hofu yoyote kwa baba hasa nikizingatia mapenzi yake kwangu yalikuwa makubwa sana.
Baada ya siku tatu baba alirudi kutoka safari zake za nje ya nchi, tulimpokea kwa furaha na bashasha. Aliponiona alishtuka kuniona nipo nyumbani siku za shule. Mama alimtuliza kwa kumwambia
"Poa kwanza, hata hujatulia na safari."
"Mke wangu nitulie kwa uchovu gani, hasa kwenye tatizo wakati mwenetu alikuwa shule leo yupo nyumbani tena siku za shule kama anaumwa atibiwe awahi shule na kama kuna tatizo lingine litatuliwe haraka huu si muda wa kucheza na elimu."
"Si umefika utayasikia, haraka ya nini kuna mtu anaondoka," mama alizidi kumtuliza baba.
Kauli ile ilimfanya baba anyamaze na kuendelea na mambo mengine. Japokuwa nilikuwa na uhakika baba hawezi kufanya lolote kutokana na kisanga changu, lakini hofu kidogo ilinitawala kutokana na maneno yake juu ya kucheza na elimu.
Nikiwa nimejilaza chumbani kwangu baada ya chakula cha usiku, nilisikia mlango ukigongwa kwa nguvu kama ameingia askari. Nilinyanyuka na kwenda kufungua mlango. Baada ya kufungua, mlango ulifunguliwa kwa nguvu kitu kilichonitisha.
Baba kwa hasira alinifokea kwa sauti ya juu kitu ambacho hakuwahi kukifanya toka nizaliwe. Mara nyingi mama aliponifokea baba ndiye aliye kuwa mtetezi wangu. Kwa hali ile hofu ilinijaa moyoni, kwa hasira baba aliniuliza huku akiwa ameshikilia ile barua niliyopewa shuleni.
"We Moureen hiki ni nini?" alisema huku akinitupia ile karatasi.
"Bahati mbaya baba," nilijibu huku nikiwa nimepoteza ujasiri na kuanza kutetemeka.
"Mmh! Bahati mbaya eeeh," aliongea kwa sauti ya chini.
"Ndi.ndi.yoo...ba.aba."
"Bahati mbaya," aliongea kwa sauti ya juu ikifuatiwa na kofi zito lililotua kwenye shavu la kushoto na kunirusha kwa nyuma mpaka chini, haja ndogo ilinitoka bila kupenda. Nikajua siku hiyo patakuwa hapatoshi. Niliikumbuka hofu ya mama juu ya hali atakayokuwa nayo baba baada ya kusikia ujinga wangu.
"Wewe nguruwe nasema hivi kuanzia sasa hivi nenda kwa nguruwe mwenzio aliyekubebesha uchafu huo."

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 04
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

"Bahati mbaya," aliongea kwa sauti ya juu ikifuatiwa na kofi zito lililotua kwenye shavu la kushoto na kunirusha kwa nyuma mpaka chini, haja ndogo ilinitoka bila kupenda. Nikajua siku hiyo patakuwa hapatoshi. Niliikumbuka hofu ya mama juu ya hali atakayokuwa nayo baba baada ya kusikia ujinga wangu.
"Wewe nguruwe nasema hivi kuanzia sasa hivi nenda kwa nguruwe mwenzio aliyekubebesha uchafu huo."
Mmh! niliona mambo mazito, nilipiga magoti mbele ya baba kuomba msamaha.
"Baba naomba unisamehe."
"Nikusamehe kwa lipi?"
"Kwa hii hali niliyokuwa nayo."
"Sikiliza mwanangu kwa vile umekuwa mtu mzima, sina budi kukuruhusu ukaishi na umpendaye kwa vile kuwa kwenu unaona unachelewa."
"Baba simjui anapoishi."
"Atii nini?" kauli yangu ilimuudhi baba.
"Ni kweli baba ni bahati mbaya ilikuwa kama ajali, tena alinibaka mi nilikuwa sitaki," nilijaribu kujitetea.
"Nasema hivi naomba uondoke machoni kwangu, usiku huu na tusionane mpaka mauti yatakapo tuchukua."
Ilikuwa kauli nzito ambayo sikuitegemea kuisikia toka kinywani kwa baba yangu kipenzi. Siku hiyo nililia sana, mama alinisaidia kumuomba msamaha lakini hakuwa tayari kunisamehe hata yeye alitishiwa kufukuzwa kama ataendelea kuninitetea.
Kwa mara ya kwanza mapenzi ya baba yangu yaliyeyuka kama donge la mafuta kwenye kikaango cha moto. Baba alikuwa mbogo alinifukuza usiku ule. Sikuwa na jinsi nilikwenda kwa rafiki yangu ambaye alikuwa amepangiwa chumba na rafiki yake wa kiume. Alinipokea na kunipa hifadhi ya kulala mpaka siku ya pili.
Asubuhi shoga yangu alinieleza:
“Moureen zile ni hasira za baba yako lakini leo ukirudi atakusamehe.”
“Mmh! Siamini kama baba atabadilika.”
“Inawezekana hata yeye anajilaumu kukufukuza pengine usiku alikutafuta.”
“Eti eeh!”
“Shoga rudi kwani baba yako anajua utaishi vipi?”
Nilijifikiria na kukubaliana na shoga yangu kurudi siku ile kuomba msamaha. Niliamini kabisa alichozungumza baba yangu ilikuwa ni hasira za ghafla, lakini nikirudi kumuomba msamaha atanisamehe kwa kujua mimi ndiye mtoto wake sina pa kwenda.
Nilikubaliana na wazo la rafiki yangu baada ya kupata kifungua kinywa ambacho kilinishinda, niliamua kurudi nyumbani kuomba msamaha.
Niliwasili nyumbani na kubahatika kuwakuta wazazi wangu wote wawili waliokuwa wamekaa sebuleni wakijadili jambo. Mama alikuwa wa kwanza kuniona, alinikaribisha.
"Karibu mwanangu," kauli ile ilimfanya baba ageuke kuangalia nani aliye karibishwa. Aliponiona mimi kwa sauti ya juu yenye kila aina ya ghadhabu alisema:
"We shetani mwanamke umefuata nini?"
"Baba Moureen msamehe mtoto," mama aliniombea msamaha kwa baba
"Nimsamehe eeh, subiri uone nitakavyo msamehe," baba alisema yale huku akisimama na kuelekea chumbani.
Nikiwa bado nimesimama karibu kabisa na mlango wa kuingilia sebuleni. Nilishtushwa na sauti ya mama:
"Moureen mwanangu kimbiaaaa," nilipotupa macho baba alikuwa na bunduki mkononi, lakini mama kwa ujasiri mkubwa alifanikiwa kumdaka na kuanguka naye chini. Wakati huo mama alikuwa akiendelea kupiga kelele.
"Moureen mwanangu kimbia baba yako atakuua."
Baba naye alijitahidi kunyanyuka lakini mama alikuwa amemshikilia madhubuti.
"Niache mama Moureen nimuulie mbali shetani huyu, bora nikanyongwe kuliko aibu hii," nilijikuta nimeshindwa nifanye nini miguu ilinitetemeka.
"Moureeeen kimbiaaaa," mama alizidi kusisitiza.
Wakati huo baba alikuwa ameamka, bunduki ikiwa imedondoka mbali, muda wote nilikua bado nimepigwa butwaa. Baba aliponyanyuka ili aiwahi bunduki hapo ndipo nilipojua kilichokuwa mbele yangu si maigizo bali kweli nilitimua mbio huku nyuma nilimsikia baba akifoka kwa hasira:
"Bahati yako ningekufumua kichwa mwana haramu mkubwa."
Nilikimbia bila kuangalia nyuma mpaka kwa shoga yangu nilikuta mlango upo wazi niliingia ndani bila kupiga hodi nilipofika tu nilianguka chini na kupoteza fahamu.
Rafiki yangu alinipatia huduma ya kwanza, kisha alitaka kujua yaliyojili nilipokwenda, Nilimweleza yote.
"Utani huo Moureen!" shoga yangu alishangaa.
"Bila mama leo ningekuwa marehemu."
"Mmh! Kama imefikia hivyo kuna umuhimu kumtafuta baba mwenye mimba, hii hakuna njia nyingine kwa hatua hiyo sidhani kuna suluhu," shoga yangu alinishauri.
Rafiki yangu aliniombea nauli ya kuja Dar kwa mpenzi wake ambaye alinipa na pesa za matumizi. Kesho yake nilifunga safari hadi Dar, jiji ambalo toka nizaliwe nililiona kwenye r runinga tu. Nilikumbuka aliniambia Dar anakaa Mikocheni nyuma ya jengo la Super Market ya Shorpers Plaza.
Alinieleza nikivuka bar moja wanayouza kiti moto nihesabu nyumba mbili kuna mtaa unaingia kulia, mbele kuna muuza chipsi nikate kushoto na kuifuata njia ya moja kwa moja kuna fundi viatu nyumba hiyo ndiyo anayoishi.
Niliwasiri Dar majira ya saa tisa alasiri na kukodi gari hadi Mikocheni. Nilimuomba aniteremshe pale Shorpers Plaza ili nisiipoteze ramani yangu, niliteremshwa Shopers Plaza na kuangalia ramani yangu haikuwa tofauti na maelezo aliyonipa.
Niliifuata njia aliyonielekeza, muda ule ulikuwa ni saa kumi na moja kasoro. Kuchelewa kote ilitokana na foleni kubwa ya magari ambayo ilikuwa ni ajabu kwa sisi watu wa mikoani kwenye uchache wa magari.
Nilifanikiwa kufika kwenye ile Bar ambayo kweli niliona kiti moto kikiuzwa. Nilihesabu nyumba mbili na kutokea kwenye njia iliyoingia kulia, mbele nilikutana na banda la chipsi. Nilikata kushoto, huwezi amini japo kuna mitaa na vichochoro ramani ilikuwa haipotezi wala haina haja ya kumuliza mtu.
Nilifuata kijinjia kidogo hadi mbele ambapo nilimkuta mshona viatu. Nilipo muona kwanza nilishusha pumzi na kumshukuru Mungu kwa kufika bila kupotea.Nilisabahi yule kaka
"Za saizi kaka."
"Nzuri karibu."
"Asante, shikamoo."
"Marahaba."
"Sijui kaka hapa ndipo anapokaa Shauri Kati au Shaka Zuru?"
"Wewe ni nani?" yule mkaka aliniuliza huku akinitazama nilivyo.
"Mmh! Mimi ni rafiki yake tulikuwa tunasoma pamoja Uganda."
"Ooh! Umefika, ndio hapa."
"Yupo?"
"Kwa sasa hayupo hapa amehama."
"Mungu wangu! Amehamia wapi?" nilishtuka.
"Usihofu ni karibu tu."
"Ooh! Afadhali, nilishtuka."
Yule kaka alimuachia mtu kazi yake na kunipeleka anapoishi Shauri, hapakuwa mbali kama nyumba ya sita kutoka kwao. Tulipofika aligonga mlango, mlango ulifunguliwa na Shauri alitoka aliwa kifua wazi amevalia bukta.
Aliponiona alishtuka na kusema:
"Aah! Moureen!"
"Ni mimi Shaka," nilijikuta nikitabasamu kumuona kipenzi changu Shaka.
"Karibu sana."
"Asante," nilijibu huku nikiingia ndani, kumbe Shaka alikua ‘Artisit’ Mchoraji. Kumbe muda ule alikuwa akichora. Baada ya kukaa na kuniagizia soda alitaka kujua mbona nipo pale wakati wenzangu wanaendelea na masomo.
“Moureen mbona huku kipindi cha masomo?”

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 05
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
"Ni mimi Shaka," nilijikuta nikitabasamu kumuona kipenzi changu Shaka.
"Karibu sana."
"Asante," nilijibu huku nikiingia ndani, kumbe Shaka alikua ‘Artisit’ Mchoraji. Kumbe muda ule alikuwa akichora. Baada ya kukaa na kuniagizia soda alitaka kujua mbona nipo pale wakati wenzangu wanaendelea na masomo.
“Moureen mbona huku kipindi cha masomo?”
SASA ENDELEA...

Nilimueleza nia na madhumuni ya kuniona mbele yake, nilimuona akishtuka na kuuliza.
"Moureen utani huo!"
"Kweli kabisa na sina pa kukimbilia."
"Moureen tafuta mwingine wa kumbambikia mimba hiyo sio mimi?" He! Shaka naye aliniruka.
"Shaka hii mimba mwenyewe ni wewe, naomba unipokee nitakuwa mgeni wa nani na wewe ukinikataa," nilijikuta nikichanganyikiwa mtoto wa kike.
"Moureen naomba unielewe sina msaada mwingine zaidi ya kukupa hifadhi ya leo, kesho nakupa nauli urudi kwenu."
Ngoma ilikuwa nzito Shaka naye alinitolea nje, niliona dunia imenigeuka hata mwenye mzigo kanikataa.Nilipojaribu kumlazimisha niliambulia kipigo, mmh nikaona hakuna haja ya kulazimisha maisha mjinga mimi. Wazo la kujiua nililikataa na kuwa tayari kupambana na maisha.
Siku ya pili hapakuwa na mabadiliko yoyote zaidi ya kupewa nauli ya kurudi Arusha. Nilijiuliza Arusha nitarudi kwa nani, niliamua kubaki Dar liwalo na liwe. Hapo ndipo nilipo ingia kwenye ukahaba nikiwa na ujauzito wangu kwa kulala ovyo.”
Kauli ile iliwafanya watoto wake kutokwa na machozi, lakini mama yao aliendelea na mkasa mzito wa kusikitisha.
“Basi katika zungukazunguka yangu nilipata shoga ambaye alinikaribisha kwake, tukawa wote usiku tunatoka kutafuta wanaume. Mungu hamtupi mja wake nilijikuta nayaendesha maisha yangu bila matatizo.
Muda ulipofika ndipo nilipo jifungua mtoto wangu wa kwanza ambaye ni wewe Martin. Nilimlea mwanangu kwa kazi yangu ya ukahaba, Mwanangu kwa kweli alikuwa kwenye mazingira magumu kwa kumuacha peke yake chumbani na mimi mama yake kwenda kwenye ukahaba.
Mungu naye alimjalia alikuwa bila tatizo lolote kama maradhi ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Ile kazi ilinisaidia kuweza kupanga chumba changu na kuweza kuwa na vitu vyote muhimu chumbani kwangu. Aliyeingia chumbani kwangu alijua ni mfanya biashara mwenye pesa.
Sikuchukua muda mrefu mwanangu Martin alipofikisha umri wa mwaka mmoja na nusu, nilishika ujauzito mwingine. Kwa kweli sikujua ile mimba ni ya nani kwa kuwa nilikuwa nakutana na wanaume wengi wengine wabishi kutumia Kondomu. Kwa vile nilihitaji pesa yao sina budi kukubaliana nao.
Niilea ile mimba ambayo baba yake sikumjua mpaka nilipofanikiwa kujifungua salama mtoto wa pili ambaye ni wewe Moses.
Wakati huo kidogo pesa nilikuwa nazo. Mwanangu alipata huduma nzuri kwa kuwa na mhudumu ambaye alimhudumia kipindi nikiwa sipo.
Niliendelea na kazi yangu ya ukahaba ambayo iliendeleza kupunguza makali ya maisha. Siku moja nikiwa katika mawindo yangu nilichukuliwa na wazungu. Siku zote kazi yetu tulipenda tukutane na wazungu ambao dau lao lilikuwa kubwa tofauti na waswahili hawachelewi kukukopa.
Lakini siku hiyo haikuwa kama nilivyo fikiria, waliniuliza kwa wote ni shilingi ngapi. Walikuwa wanne, niliwajibu kwa wote watanipa dola mia nne. Walikubali na kunipa zote taslimu ambazo nilimuachia shoga yangu kwa kuhofia kudhulumiwa.
Niliingia kwenye gari na kuondoka nao kuelekea nisipo pajua, siku zote kazi zetu tulimwachia Mungu kulinda maisha yetu. Nilipofika kwao kumbe haikuwa hivyo walikuwa wamepanga kunifanyisha mapenzi na mbwa wao wawili kwa nguvu.
Nilipokataa walinilazimisha kwa kunitishia na bastora, hata hivyo sikuwa tayari walinipiga na kunifunga kamba kisha waliwachukua mbwa wao na kuniingilia kimwili huku nikisikia maumivu makali. Siku hiyo nilijuta kufanya ukahaba kwa kuingiliwa kinyume na maumbile na wanyama wale.
Mpaka wananiachia nilikuwa hoi sijiwezi, walinichukua na kwenda kunitupa kwenye mtaro. Niliokotwa na watu nikiwa sina kitu mwilini, walinichukua na kunipeleka hospitali.
Nilipata fahamu siku ya pili jioni, wakati huo nilikuwa nimeshapatiwa matibabu ya hali ya juu ikiwa pamoja kupigwa bomba. Kabla ya kutoka polisi walifika kuchukua maelezo. Kwa vile sikuwajua vizuri ila nilikuwa nawafahamu nilitoa maelezo nao waliahidi kuwasaka mpaka kuwatia nguvuni.
Baada ya wiki mbili walifanikiwa kuwakamata baada ya kutega mtego sehemu tunayofanya biashara ya miili. Kitu cha ajabu baada ya kukamatwa wale Wazungu waliandika maelezo na kuwekwa ndani kisha nikaelezwa nirudi siku ya pili.
Nilikwenda nyumbani na siku ya pili nilirudi polisi nikiwa na ushahidi wa shoga zangu waliokuwepo siku nilipochukuliwa. Kila kitu kilikuwepo ikiwemo taarifa ya daktari vilionesha kweli niliingiliwa na mbwa, kilichotakiwa ni kuwafikisha mahakamani na kufunguliwa mashtaka
Usitaajabu ya Musa utayaona ya Filauni, siku ile nilipofika kibao kikanigeukia mimi eti kumbe wale Wazungu walikuwa na RB yangu alikuwa nayo aliyofungua muda mrefu ya kuwaibia dola laki moja na walikuwa wakinitafuta. Basi wanangu mimi ndiye niliye ingizwa hatiani na kufikishwa mahakamani mara moja na kufungwa mwaka mmoja baada ya kujitetea nina watoto wadogo. Hebu wanangu ona jinsi uonevu ulivyo fanywa juu yangu kwa vile nilikuwa mnyonge sina kitu.
Nilikubali matokeo lakini moyoni nilijiapiza nitakapotoka kila aliyehusika hastahili kuishi duniani. Basi sikuwa na jinsi nilitumikia mwaka gerezani.
Nilipotoka nilianza msako wa kuwasaka wabaya wangu, wanangu nilimuua mmoja mmoja kila kukicha. Kwa wale wazungu niliua mpaka mlinzi na mbwa wao. Nilipomaliza kumuua mkuu wa polisi aliyeshiriki kubadilisha kesi yangu ndipo nilipotorokea Mwanza.
“Uliwauaje wote hao bila kushikwa?” Edna alijikaza na kumuuliza mama yake.
“Mnajua wale wazungu walikuwa ma x-part waliokuwa wakisimamia miradi mingi nchini na walikuwa wakilindwa na serikali. Kesi kama ile haikuwa kwangu tu kumbe mchezo ule tulifanyiwa wanawake wengi waliokuwa wakifanya biashara kama yangu.
Ilionesha mkuu wa polisi niliyemuua alikuwa akihongwa na kuwageuzia makosa wote waliokwenda kushtaki na kuwafanya wasichana wengi wakitendewa unyama kukaa kimya.
Baada ya kutoka gerezani nikiwa na hasira na wote walionitenda kuanzia mkuu wa polisi hakimu na hao wazungu ambao waliendelea na tabia za kutudhalilisha wanawake.”
“Mama wakati unafungwa kina kaka walikuwa wapi?” Edna aliuliza tena kwani kaka zake walikuwa wamepigwa na bumbuwazi na kuona kama aliyokuwa akiyasema mama yao ni hadithi ya ndotoni.
“Kuna shoga yangu mmoja aliwachukua na kukaa nao, bahati nzuri nilikuwa na fedha ya kutosha katika akaunti yangu, hivyo niliamini hata ningefungwa miaka miwili ingeweza kuwasaidia. Basi baada ya kurudi nilitembelea sehemu zangu kuendeleza kazi yangu ya ukahaba kuendelea kujipatia riziki baada ya akiba yangu kukuta imebakia kidogo kwa vile sikuwa na kazi nyingine niliamini kazi ile ndiyo mkombozi wangu.
Kwanza niliwauliza mashoga zangu kuhusu mchezo wa wale wazungu kuwafanyisha mapenzi na mbwa. Niliambiwa mzungu mmoja alifukuzwa nchini baada ya kesi kumkalia vibaya baada ya msichana mmoja kumpata mtu wa kumsimamia kwenye kesi yake na kulipwa fedha nyingi lakini na yeye kazi ya ukahaba ilikuwa kwenye damu hakuacha japo alipunguza na kuchagua wanaume wenye fedha kwani alikuwa akija kazini na gari lake.
Nilielezwa wakati narudi walikuwa wakiwachukua wanawake na kukubali kufanya nao mapenzi wote watatu. Japokuwa wanasema ulitaka ule ushibe lakini ulikuwa ukitoka na fedha nzuri. Baada ya kuelezwa vile niliendelea kuwawinda kwa siri bila mashoga zangu kujua dhamira yangu ni nini kwa washenzi wale. Nilitembea na dawa ya kulevya ya kupaka kwenye matiti ambayo huitumia kama unataka kumwibia mtu pia kisu nilichokificha kwenye mkoba wangu.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 06
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Nilielezwa wakati narudi walikuwa wakiwachukua wanawake na kukubali kufanya nao mapenzi wote watatu. Japokuwa wanasema ulitaka ule ushibe lakini ulikuwa ukitoka na fedha nzuri. Baada ya kuelezwa vile niliendelea kuwawinda kwa siri bila mashoga zangu kujua dhamira yangu ni nini kwa washenzi wale. Nilitembea na dawa ya kulevya ya kupaka kwenye matiti ambayo huitumia kama unataka kumwibia mtu pia kisu nilichokificha kwenye mkoba wangu.
SASA ENDELEA...

Nilifanya kazi kwa taadhari kubwa ili nisirudie kosa la awali, sikuwa tayari kwenda na mtu mwenye gari bali kufanya mapenzi ya papo hapo na kumalizana. Niliendelea na kazi yangu huku nikifanya mawindo ya watu wangu. Sikutaka kuanza na mkuu wa polisi wala hakimu kwa vile nilijua wale ni watu wa kumalizia.
Siku moja nikiwa lindoni mwangu, lilikuja gari na kushangaa kuona mashoga zangu hawalikimbilii, nilijiuliza kuna nini. Nilipouliza niliambiwa:
“Shoga leo hatutaki wale wazungu wana mchezo mbaya, leo hawapati mtu tumewaambia kama kwenda na mmoja sawa lakini wote watatu hatutaki.”
Kauli ile ilinifanya nichekelee moyoni, nilijisogeza mbele hadi kwenye lile gari waliponiona walinieleza kama nitakubali watu watatu sawa ilionesha wamenisahau.
Nilikubali kuwa nipo tayari, niliongozana hadi kwao, moyoni nilikuwa na dhamira mbaya kila nikikumbuka moyo unanitetemeka na kumuomba Mungu anisamehe.
Tulipofika niliwaeleza nitafanya mapenzi na wote lakini kwanza na mmoja mmoja kisha baadaye nitafanya na wote kwa pamoja. Tena niliwaeleza kwanza nitafanya mapenzi kwa kila mmoja kuwa chumbani kwake. Bila kujua nimedhamiria nini, walikubali. Basi nilianza kwa kuingia kwenye chumba cha mmoja na kuondoa nguo zote nikijifanya nimepandwa maruhani ya mapenzi.
Wakati wa kuandaana nilipaka dawa yangu kwenye matiti bila kujua kisha nilimwambia anyonye ili kunipandisha mdadi, bila kujua alifanya nilivyotaka. Haikuchukua muda alinyonya kisha nilimuona akilegea na kujilaza pembeni.
Nilichukua mto na kumziba pumzi usoni, sikuutoa mpaka alipotulia nikijua nimemaliza kazi kisha nilimlaza vizuri.
Nilijipaka dawa yangu tena kwenye nyonyo na kutoka bila kitu mwilini na kwenda chumba cha mzungu mwingine aliyekuwa akinisubiri kwa hamu sana.
Kama kawaida baada ya kupanda kitandani nilimuomba anyonye matiti na yeye alinyonya baada ya muda alilegea na kummaliza kama mwenzake.
Kumbe wakati nammalizia yule mzungu wa pili mzungu wa tatu sijui alishtukia vipi nilimuona akija huku akimwita mwenzake kwa sauti ya juu.
“Mr Rich kuwa makini Mr Rich kuwa makini.”
Kwa haraka niliteremka kitandani na kujificha nyuma ya mlango, aliingia na bastora mkononi akili yake ikiwa kwa mwenzake ambaye nilikuwa nimeisha msafirisha kuzimu. Nilijua nimekufa kwa vile sikuwa na ujanja wowote wa kujiokoa kwa mzungu yule aliyekuwa na silaha mkono, pili hata mwili wake kama ngenikamata basi ningefia mikononi kwake.
Nikiwa natetemeka mpaka haja ndogo ilinitoka baada ya kuona akimpima mwenzake mapigo ya moyo. Niliona ile ndiyo nafasi yangu ya kutoka mbio, nilikurupuka nyuma ya mlango na yeye alimuacha mwenzake na kunifuata. Kwa vile nilijua mlango umefungwa nilijitahidi kuufunga ule mlango ili nimfungie ndani. Wakati huo yule mzungu alikuwa akija mbio, nilifanikiwa kuufunga ule mlango na kumfanya ajigonge mlangoni na kuanguka chini.
Alianguka kwa kishindo, nilifunga mlango kwa komeo kwa nje kisha nilichungulia ndani na kumuona amelala chini damu zikimtoka kichwani. Nilikwenda mpaka jikoni na kufanikiwa kupata kisu kikubwa ambacho nilirudi nacho na kuufungua mlango wakati huo roho ya damu ilinijaa.
Nilimfuata chini alipolala huku nikiwa na hasira niliteremsha mapigo mfululizo ya kifuani mpaka alipotulia. Nilinyanyuka na kujifuta damu kisha nilivaa nguo zangu. Nilianza kupekua kila kona na kufanikiwa kupata dola laki nne, nilizifunga vizuri kisha nilichukua bastora hadi kwenye banda la mbwa na kuwaua mbwa wote na kwenda kwenye moja la gari lao na kutoka nalo.
Mlinzi alipoangalia ndani ya gari na kuniona mimi alishtuka na kunihoji:
“Vipi mbona unatoka na gari?”
“Siyo juu yako fungua geti,” nilimjibu kwa sauti ya ukali.
“Kazi yangu ni ulinzi nina haki ya kuuliza,” mlinzi naye alikuwa mbishi.
“Sikiliza we kidampa hebu fungua geti kabla sijakupoteza!” nilimtisha afungue mlango.
“Siwezi mpaka nipate ruhusa ya mabosi wangu.”
Niliona kama ananichelewesha nilichukua bastora iliyokuwa pembeni yangu na kumshuti. Niliteremka haraka na kwenda kufungua geti kisha nilirudi kwenye gari na kuliondoa kwa kasi.
Nilitembea huku moyo wangu ukiwa na hasira ya kunywa damu ya mtu. Nilikwenda na gari hadi mjini ambako nililiacha njiani na kuchukua teksi iliyonipeleka nyumbani. Kwa wasiwasi wa kukamatwa sikutoka ndani kwa siku tatu huku nikisikiliza taarifa kwenye vyombo vya habari ambavyo viliripoti vifo vya wazungu watatu na mlinzi wao waliouawa kinyama na mtu asiyejulikana.
Nilitulia kwa muda wa mwezi mzima nikiwa mtu wa kujificha ikiwemo kuhama nilipokuwa nakaa na kuhamia nje ya mji. Baada ya hali kutulia nilianza msako wa mkuu wa polisi na hakimu. Nilifuatilia nyendo zao na kujua kila mmoja anakunywa wapi.
Pia niliona kuwapata siyo kazi kutokana na tabia zao za unywaji na kupenda wanawake. Niliona nianze na hakimu kwa kujua polisi msako wake ni mkubwa kuliko wa hakimu. Hakimu alikuwa akikaa maeneo ya Mikocheni na alikuwa akipenda kunywa kwenye baa moja maarufu iliyopo Kinondoni.
Niliamua kumfuatilia nyendo zake ambazo nilizielewa, siku moja nilimkuta kwenye baa hiyo akiwa amekaa peke yake akinywa bia yake huku akichati na simu. Kwa vile nilikuwa nimevaa kiutata niliamini kila mwanaume alitamani kuwa na mimi. Nilisogelea meza yake na kumsalimia:
“Habari za saizi?”
Kabla ya kuitikia alinyanyua uso na kunitazama kisha alishusha pumzi ndefu na kusema:
“Ooh! Sorry, karibu mrembo.”
“Hapana nakusalimia,” nililegeza sauti.
“Ooh! Nzuri mrembo karibu.”
“Asante, vipi una mtu hapa?”
“Nipo peke yangu karibu mtoto mzuri.”
Nilikaa na kujifanya natoa simu kwenye mkoba na kujifanya nasoma kitu kumbe ilikuwa kumlia pozi.
“Mmh! Binti unatumia kinywaji gani? Aliniuliza baada ya uhudumu kuja kusimama mbele ya meza yetu.
“Heinken.”
“Na nini mrembo?”
“Kwanza hiyo inatosha kwanza mi si mnywaji sana.”
Baada ya vinywaji kuletwa nilitulia na kunywa kistaarabu, kitu kilichomfanya hakimu kutaka kunijua zaidi.
“We ni mgeni?”
“Si sana.”
“Mwenyeji wa wapi?”
“Arusha.”
“Ooh! Nimefurahi kuwa na wewe nina imani leo tutakuwa pamoja.”
“Mmh! Na mkeo?” nilijifanya kulia wivu.
“Mke wangu nikirudi kwangu, sasa hivi mimi nipo na wewe mtoto mzuri.”
“Mmh! Kama hivyo basi wewe tu,” nilijifanya kulegea.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 07
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
“Mwenyeji wa wapi?”
“Arusha.”
“Ooh! Nimefurahi kuwa na wewe nina imani leo tutakuwa pamoja.”
“Mmh! Na mkeo?” nilijifanya kulia wivu.
“Mke wangu nikirudi kwangu, sasa hivi mimi nipo na wewe mtoto mzuri.”
“Mmh! Kama hivyo basi wewe tu,” nilijifanya kulegea.
SASA ENDELEA...

Baada ya chakula tulikubaliana kwenda nyumba ya wageni kwa kulala kwa mapenzi ya muda mfupi kwa kisingizio nipo kwa baba yangu mdogo siruhusiwi kulala nje. Tulitoka pamoja kwenye gari lake na kuingia, nilipata wazo la haraka la kumuulia ndani ya gari ili kufuta ushahidi.
Baada ya kutoka eneo la baa niliacha gari liende mbele kidogo na kumuomba alisimamishe pembeni.
“Kuna nini sweet?”
“Nina hamu mpenzi naomba uninyonye matiti kidogo uzipunguze.”
“Vumilia nitazishusha sasa hivi.”
“Hapana ninyonye,” nilisema huku nikizitoa nyonyo zangu ambazo zilimbabaisha na kukubali kupaki gari pembeni na kuanza kuzinyonya. Japokuwa alinipandisha mzuka lakini lengo langu lilikuwa roho yake.
Aliendelea kulinyonya kwa ufundi mkubwa sana mpaka nikajikuta namaliza haja zangu bila kupenda, lakini lengo langu kwa siku ile halikuwa hilo zaidi ya roho yake. Baada ya kunyonya kwa muda nilimuona akianza kulegea na kuliachia ziwa kisha alijilaza pembeni.
Nilimtikisa na kugundua amelegea nilichukua mto mdogo ndani ya gari na kumziba nao usoni kwa kumkandamiza kwa nguvu. Kwa vile hakuwa na nguvu hakuweza kunizuia nilimbana mpaka alipopoteza uhai nilimlaza pembeni na kuteremka kwenye gari, nilifunga mlango na kuondoka zangu.
Nilitembea haraka mpaka mbele na kukodi bodaboda mpaka Magomeni ambako nilikodi teksi mpaka nyumbani. Nilitulia ndani kusikilizia kwenye vyombo vya habari vitaripoti vipi kifo kile. Taarifa ya asubuhi kwenye radio zote zilielezea Hakimu Kiondo alivyokutwa amekufa kwenye gari lake.
Vyanzo vya habari vilisema alionekana ameongozana na mwanamke mmoja mrembo na kwenda kwenye gari lake na baadaye gari lake kuonekana hatua chache na baa aliyokuwa akinywa.
Polisi walisema wanamsaka mwanamke aliyetoka naye japo ilikuwa vigumu kunigundua kwa vile hakuna hata mmoja aliyekuwa akinifahamu pia alikuwa mgeni maeneo yale. Baada kufanikisha kifo cha Hakimu nilitulia kwa miezi mingine miwili kujipanga kwa ajili ya kummaliza mkuu ya kituo ambaye wakati huo alikuwa OCD katika wilaya moja mkoani Morogoro.
Mwanamke baada ya kujipanga nilifunga safari mpaka Morogoro na kupanga kwenye hoteli moja yenye hadhi mkoni Morogoro. Nilianza kumfuatilia OCD Mzizire kwa siku tatu na kugundua bado ana tabia zilezile za kunywa kwenye baa kubwa pia kupenda watoto wazuri.
Baada ya kujua baa anayokunywa nilikwenda siku moja kwenye ile baa na kutafuta siti ya karibu na alipokuwa amekaa na wapambe wake wakinywa. Nilimwita mhudumu.
“Habari dada.”
“Nzuri, karibu.”
“Asante, samahani dada yangu.”
“Bila samahani.”
”Eti mzee Mzizire anakunywa kinywaji gani?”
“Serengeti.”
“Na wenzake?”
“Kuna anayetumia ndovu, konyagi na Tusker.”
“Kila mmoja mpe tatutatu mwambie mzee Mzizire ofa yangu kwake.”
“Sawa.”
“Shilingi ngapi?”
“Usiwe na wasi nitakwambia baada ya kuhudumia, wewe je, huagizi?”
“Mi niletee Heinken moja.”
“Baridi, moto?”
“Moto hali ya hapa ni baridi.”
“Dada baridi ipo wapi wewe mgeni?”
“Si sana.”
Yule msichana aliondoka na kunifanya niendelee kumtazama kwa uchu mzee Mzizire, kila nilipokumbuka alivyonifanyia, moyo uliniuma na sikutaka kumsamehe hata kidogo, kwa tabia zake za kuwakandamiza wanawake na kuwatetea wazungu waliowafanya vibaya wanawake kwa kuwafanyisha mapenzi na mbwa na mwisho wa siku wanafungwa wao bila kosa.
Baada ya muda nilimuona yule mhudumu akiweka tlei la vinywaji kwenye meza. Nilimuona akiuliza, mhudumu alinionesha mimi ambaye alimpokea kwa tabasamu kali. Niliwaona wote wakinishuku kwa kushika vifuani vyao nami nilijibu kwa kushika changu kuonesha nikubali.
Alipotoka pale aliniletea heinken yangu na kunifungulia na kutaka kuniwekea kwenye glasi, nilimkataza na kujiwekea mwenyewe na kupiga funda moja na kutulia. Nilifanya kuangalia chini ili niwape nafasi ya kuusanifu uzuri wangu ambao ulinifanya nijiamini muda wote.
Siku zote huwa naamini wakubwa ndiyo wanapenda kujipendelea kizuri lazima wakitake wao. Baada ya muda yule dada alikuja na bia nne na kutaka kuziweka juu ya meza yangu.
“Vipi dada?” nilimuuliza.
”Mzee amesema nikuhudumie, nikupe chochote unachokitaka.”
“Mwambie asante, leo sijisikii kunywa sana, sina uhakika hata kama bia hii moja nitamaliza.”
“Dada si ungechukua hata kama hunywi ungenipa mimi mdogo wako.”
“Usiwe na wasiwasi we rudisha nitakupa elfu kumi ya matumizi unasemaje?”
“Duh! Dada yangu utaokoa maana leo hali ni mbaya.”
Nilifungua mkoba wangu na kuchukua noti ya elfu kumi na kumpa.
“Hii ya nini?”
“Yako.”
“Na bili?”
“Hujaniambia kiasi gani pia hujawaongezea bia nyingine.”
“Kwa hiyo niwaambiaje kuhusu bia hizi?”
“Mwambie kama nilivyokwambia kuwa sijisikii kunywa bia leo, labda kesho nitaungana nao.”
“Haya dada, asante sana.”
Yule mhudumu aliondoka na kuniacha nikiibembeleza bia yangu ambayo niliiweka kuzugia tu kwa siku ile sikuwa mnywaji kabisa zaidi ya kumtamani Mr Mzizire kama Simba mwenye njaa aliyemuona Swala
akinywa maji pembeni yake.
Baada ya muda yule mhudumu alinifuata na kuniletea kimemo toka kwa Mr Mzizire.
Sorry mrembo tunaweza kuwa pamoja leo?
Baada ya kukisoma nilitabasamu kumfanya aliyeleta ujumbe ambaye nilijua alikuwa akinifuatilia kujua nitaupokeaje. Tabasamu langu lilikuwa la kwanza kumpa matumaini.
Baada ya kusoma nilimuomba kalamu mhudumu na kunipa na kugeuza karatasi kwa nyuma na kuandika.
Kwa leo au kwa siku zote?
Nilimpa mhudumu aliyempelekea baada ya kusoma naye aliandika kikaratasi kingine.
Nimekupenda sana, nina imani itakuwa siku zote.
Nilipoletewa nilisoma na kumjibu.
Sawa, lakini sipendi kuchezewa na wanaume! Nilijifanya kutoa onyo.
Mhudumu alichukua ujumbe ule na kumpelekea baada ya kuusoma alijibu:
Nimekuelewa, naomba tuzungumze faragha.
Baada ya kuletewa niliusoma na kumjibu:
Hakuna tatizo.
Baada ya kupelekewa jibu langu, niliona akijadiliana na mpambe wake baada ya muda nilimuona yule mpambe akija nilipokuwa nimekaa na kuniinamia.
“Samahani naomba unifuate.”

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 08
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Sawa, lakini sipendi kuchezewa na wanaume! Nilijifanya kutoa onyo.
Mhudumu alichukua ujumbe ule na kumpelekea baada ya kuusoma alijibu:
Nimekuelewa, naomba tuzungumze faragha.
Baada ya kuletewa niliusoma na kumjibu:
Hakuna tatizo.
Baada ya kupelekewa jibu langu, niliona akijadiliana na mpambe wake baada ya muda nilimuona yule mpambe akija nilipokuwa nimekaa na kuniinamia.
“Samahani naomba unifuate.”
SASA ENDELEA...

“Sawa ngoja nilipe kwanza.”
“Hapana mzee atalipa.”
“Hapana, vinywaji hivi nimeagiza mimi.”
Baada ya kulipa nilitoka na yule mpambe aliyenipeleka mpaka kwenye hoteli moja iliyokuwa nje kidogo ya mji. Moyo wangu ulijawa furaha baada ya kuona mtego wangu umenasa kirahisi tofauti na nilivyofikiria. Jamaa baada ya kunifikisha chumbani aliniacha na kuondoka.
Baada ya kuondoka nilibakia chumbani peke yangu nikiwa katika wakati mgumu wa kutimiza nilicho dhamiria. Wasiwasi wangu ulikuwa kujulikana mimi ndiye muuaji hivyo kunifanya nishikwe mara moja na kukamatwa kabla sijafika mbali.
Nilijikuta nikiingiwa wasiwasi kuhusiana na mpango wangu kwa vile kama ningemuua, basi ningekamatwa mara moja. Wazo la kumuua siku ile sikutaka kulitekeleza kwa vile mazingira yalikuwa tata kwa kujua wapambe wake hawakuwa mbali. Niliamini baada ya kuonekana natoka lazima watamfuatilia na wakimkuta amekufa msako wake ungekuwa mkubwa na mimi nisingefika mbali, lazima wangenikamata.
Siku zote niliamini mpango mzuri ni kati yangu na adui yangu asiwepo wa tatu mwenye kujua mpango ule ambaye anaweza kuwa shahidi wa kuweza kunitia hatiani. Nilikubali siku ile nifanye mapenzi tu bila kuingiza kitu chochote huku nikiapa kujituma ili kumfanya aombe tukutane siku nyingine.
Nikiwa katikati ya mawazo, mkuu wa polisi wa wilaya (OCD) mzee Mzizire aliingia na kuja moja kwa moja nilipokuwa nimejilaza kwenye kochi.
“Niambie mpenzi wangu?”
“Mmh! Nakusikiliza wewe.”
“Mimi ninalo zaidi ya kuhitaji mapenzi yako.”
“Lakini kweli unanipenda au unanitamani?” nilijifanya kujibalaguza huku nimelegeza macho na sauti.
“Siyo siri mrembo, sijawahi kumpenda mtu kwa haraka hivi kama nilivyokupenda wewe.”
“Muongo! Unanidanganya unataka kunichelea tu leo kisha uniache,” nilijifanya kudeka.
“Kweli kabisa nakupenda kwa dhati wala si kukuchezea.”
“Kweli?”
“Kweli kabisa, unataka nikufanyie kitu gani uamini nakupenda?”
“Unipende tu wala sitaki kitu kingine.”
“Wewe ni mgeni hapa?”
“Ndiyo.”
“Unatokea wapi?”
“ Arusha.”
“Ooh! Vizuri na hapa Morogoro umefikia wapi?”
“Nipo katika mapumziko tu.”
“Unafanya kazi?”
“Ndiyo.”
“Ipi?”
“Kwenye kampuni ya utalii.”
“Upo likizo?”
“Ndiyo, leo ni siku ya tano, ila kesho nitakuwa Dar ambako nitakaa siku mbili na kwenda Zanzibar kidogo kisha nitaenda Mwanza na kurudi Arusha, kidogo nitakuwa nimeosha macho.”
“Duh! Inaonekana utalii umekukaa sana.”
“Upo ndani ya damu yangu.”
“Kwa nini usimalize likizo yako hapa ili tuwe pamoja, nitakupangia kwenye hoteli hii kwa muda wote utaokuwa hapa.”
“Asante, kwa vile nimeishapanga ratiba zangu, nitakutafutia nafasi yako hata ya kusema uongo kazini kuwa nauguliwa, hivyo nitakuja unifiche unifaidi.”
“Basi ondoka kesho kutwa.”
“Hapana, naomba kesho uniache niondoke, naweza kuacha kwenda Mwanza nikarudi kwako niache niende Dar na Zanzibar.”
“Mmh! Sawa.”
Baada ya kukubaliana tuliondoana nguo zetu kwa kupeana msaada kisha tulikwenda kuoga na kurudi kitandani ambako nilimpa raha kamili zilizompagawisha mzee wa watu. Kwa vile nilikuwa mzoefu wa kukutana na wanaume pia nilijua kuitaka hela ya mwanaume ambaye alikuwa akiitoa bila kusita hata tuliyokubaliana lazima uiongeze kwa penzi ninalompa.
“Mpenzi kwa nini kesho usihahirishe safari yako, kwa penzi unalonipa sijawahi kupewa, sema unataka nikupe nini ili usiondoke.”
Nilitaka kumwambia naitaka roho yake, lakini ilibakia siri yangu ambayo niliijua mimi na Mungu wangu.
Niliendelea kumpa vitu vipya mtoto wa kike huku nikikataa kila alichotaka kunipa kujifanya sina tamaa kumbe naitaka roho yake.
“Mpenzi sihitaji chochote bali penzi lako.”
“Penzi umepata, nakuahidi kukujengea nyumba na kukununulia gari hata kesho.”
“Nimekuelewa mpenzi wangu ila nina ombi moja kwako.”
“Ombi gani mpenzi wangu?”
“Kwa vile kesho nitakuwa Dar, naomba uje hata jioni tuwe pamoja, nimefurahia penzi lako naomba niwe nyumba yako ndogo,” nilizidi kumtia ujinga.
“Umeipata hata ukitaka nimfukuze mke wangu nipo radhi.”
“Hapana mkeo usimfukuze bali mimi nipo radhi kuwa nyumba ndogo lakini naomba uniheshimu tu.”
“Nakuhahidi kukuheshimu zaidi ya heshima hata ukitaka nikupikie na kukufulia.”
“Hapana sivyo hivyo, nataka utambue mimi kuanzia leo ni mpenzi wako.”
“Jamani bebi au nipige kelele kuonesha nimekubali.”
“Basi nimekuelewa lakini hujajibu ombi langu.”
“Lipi bebi?”
“La mimi na wewe kuwa kesho Dar.”
“Kumbe hilo, usiwe na wasi nakuahidi mpaka saa kumi na mbili jioni nitakuwa Dar, unataka tuwe hoteli gani?”
“Sea Cliff.”
“Hakuna tatizo mpenzi wangu.”
“Nimefurahi kusikia hivyo, naomba fedha ya hoteli nilipe mimi.”
“Naomba mpenzi wangu nilipe mimi.”
Sikutaka kulazimisha nilimkubalia na kunieleza asubuhi kabla ya mimi kuondoka atakodi yeye chumba ili nikifika nifikie kwenye hicho chumba.
Siku ile tulilala mpaka siku ya pili alfajiri aliponiaga anakwenda nyumbani kuvaa sare ya kazi ili aingie kazini na saa tisa alasiri ataondoka Moro kuja Dar.
Kabla ya kuondoka alibuku chumba Sea Cliff hoteli na kuniuliza aandike jina la nani.
Ili kupoteza ushahidi nilimwambia aandike jina lake, baada ya kupata chumba namba 215 kwa jina Kaka Mkubwa aliondoka na kuniacha nimejilaza kitandani ili kujiandaa kurudi Dar huku nikifurahia mpango wangu umekwenda vizuri. Nilitamani kupige vigelegele vya furaha. Moyo mwingine uliingia huruma kumuua mzee kama yule aliyekuwa na familia nilijikuta kwenye wakati mgumu wa maamuzi yangu.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 09
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Kabla ya kuondoka alibuku chumba Sea Cliff hoteli na kuniuliza aandike jina la nani.
Ili kupoteza ushahidi nilimwambia aandike jina lake, baada ya kupata chumba namba 215 kwa jina Kaka Mkubwa aliondoka na kuniacha nimejilaza kitandani ili kujiandaa kurudi Dar huku nikifurahia mpango wangu umekwenda vizuri. Nilitamani kupige vigelegele vya furaha. Moyo mwingine uliingia huruma kumuua mzee kama yule aliyekuwa na familia nilijikuta kwenye wakati mgumu wa maamuzi yangu.
SASA ENDELEA...

Niliondoka Morogoro na basi majira ya saa moja kasoro asubuhi na kufika Dar saa tatu na kukodi teksi hadi kwangu. Nilipofika nilijipumzisha kwa kuoga na kujilaza, majira ya saa kumi na mbili niliamka na kuoga ili kujiandaa kwenda Hoteli ya Sea Cliff kumsubiri mtu wangu ili nimalize kazi iliyobaki ili kufanya mambo mengine.
Baada ya kujiandaa na kuchukua vifaa vyangu vya kazi nilikodi teksi hadi Sea Cliff , nilifika majira ya saa moja na nusu tofauti na muda tuliokubaliana wa saa kumi na mbili kasoro. Kwa vile mzee Mzizire alikuwa amesha chukua chumba nilikwenda moja kwa moja mapokezi na kuomba funguo, nilimkuta dada mmoja mrembo.
“Habari dada?”
“Nzuri, karibu.”
“Asante, naomba ufunguo wa chumba namba 215.”
Yule msichana alipekua kitabu na kuniuliza.
“Samahani dada mbona chumba hiki kimechukuliwa na mtu anayeitwa Kaka Mkubwa?”
“Ndiye mpenzi wangu, chumba hiki tumechukua kwa kubuku kwa simu alfajiri ya leo.”
“Ooh! Mpenzi ndo unafika,” sauti nyuma ilinishtua ilikuwa ya mzee Mzizire.
Niligeuka mzimamzima na kwenda kujitupa kifuani kwake, kwa usanii niliokuwa natumia hata ungekuwa na moyo mgumu kiasi gani angekubali nampenda sana.
Kwangu hakikuwa kitu kigeni kwa vile ile ndiyo kazi yangu iliyokuwa ikinipatia kipato, hivyo nilikuwa najua jinsi na kumpumbaza mwanaume na kuamini nampenda kumbe nina yangu.
“Waaawooo mpenzi,” nilijifanya kuchanganyikiwa.
“Waaawoo.”
“Yaani ndo nafika na kukutana na maswali kama polisi,” nilijifanya kudeka.
“Jamani dada yangu sasa ningetoa chumba bila kuwa na uhakika?” msichana wa mapokezi alijitetea.
“Basi mpenzi, vipi umefika zamani?”
“Kama ningefika zamani si ningeumbuka.”
“Basi yameisha, tunaomba ufunguo,” mzee Mzizire alisema.
Tulipewa ufunguo na kuelekea kwenye vyumba tukiwa tumekumbatiana mtoto wa kike nilideka kuonesha nimemmisi sana. Tulikwenda mpaka chumbani na kujilaza kitandani kabla ya kwenda kuoga. Wakati mwenzangu akiwaza mapenzi, mimi nilikuwa naitamani roho yake ambayo niliamini sehemu ile ilikuwa nzuri sana isiyo na ushahidi.
Tulipotoka kuoga sikuhitaji auchezee mwili wangu tena kwa vile pale nilikuwa na kazi moja naye. Baada ya kutoka kuoga nilipaka dawa yangu kwenye matiti na kumuomba anyonye.
“Mpenzi..mpenzi naomba uninyonye matiti nisikie raha.”
Mzee wa watu zikiwa zimempanda alivamia nyonyo zangu na kunyonya kama mtoto aliyelikosa ziwa la mama yake toka asubuhi. Kutokana na kuipaka dawa nyingi hakuchukua muda mzee mzima alilegea. Kama kawaida nilichukua mto na kumziba pumzi sikumuachia mpaka alipotulia.
Baada ya kupata uhakika nimemaliza kazi, nilinyanyuka na kuvaa nguo zangu na kutoka. Niliuacha ufunguo kwa ndani kwa kuamini hakuna mtu wa kuingia kwa siku ile mpaka siku ya pili. Nilitoka na kutembea kwa haraka kuelekea barabara ya Salenda Bridge.
Kwa vile ilikuwa giza hakuna aliyeniona, ilipita teksi niliyoipiga mkono baada ya kusimama nilikwenda nayo mpaka Kinondoni kwa Manyanya na kuchukua nyingine mpaka nyumbani.
Kama kawaida yangu baada ya tukio nilikaa ndani kusikilizia nini kitaendelea, mpaka kunakucha hakukuwa na taarifa yoyote kutoka katika vyombo vya habari kuhusiana na niliyoyafanya. Niliamini mwili wa mzee Mzizire utagundulika siku ya pili kwa mfanya usafi atakapoingia ndani.
Asubuhi ilikuwa tulivu hakukuwa na taarifa yoyote muda mwingi niliutumia kuangalia na kusikiliza taarifa za habari kwenye redio na tivii. Majira ya saa sita vyombo vya habari vya redio na tivii vilitoa taarifa iliyoitwa ya kushtusha pale waliposema Mkuu wa Polisi wilaya ya Morogoro, Bwana Mzizire amekutwa amekufa kwenye Hoteli ya Sea Cliff katika chumba namba 215.
Taarifa iliendelea kusema kwa mujibu wa maelezo ya mhudumu wa hoteli ile aliyekuwa zamu alisema majira ya saa moja na nusu waliingia marehemu na mwanamke mmoja aliyeonekana ni mpenzi wake. Lakini majira ya saa nne asubuhi siku ya pili wakati wa kufanya usafi ndipo ilipogundulika hali ile iliyowashtua na kutoa taarifa polisi.
Baada ya maelezo msichana wa mapokezi aliyeonekana kuchanganyikiwa alifuata mkuu wa upelelezi wa mkoa kusema kuwa watafanya uchunguzi wa kifo kile ikiwa pamoja na kumtafuta mwanamke yule aliyefanya mauaji yale.
Moyoni nilifurahia kusikia wabaya wangu wote nimewamaliza.
Niliamini muda ule ulikuwa muafaka kuondoka jijini Dar na kwenda kuishi mkoa wowote. Sikutaka kurudi Arusha niliamua kwenda mbele kwa mbele. Wazo la haraka lilikuwa kwenda kujificha mkoani Mwanza jiji ambalo lilikuwa limechangamka hata mtu kukutilia mashaka ni vigumu tofauti na mikoa mingine ukiingia mgeni unajulikana haraka.
Sikutaka kukurupuka kwa siku zile nilitulia kwa wiki huku nikifanya mambo yangu ikiwa ni pamoja na kuwakabidhi wanangu kwa shoga yangu ambaye nilimuachia kiasi kikubwa cha fedha cha kuwatunza. Baada ya kila kitu kwenda vizuri niliondoka bila kumjulisha nakwenda wapi ila nilimweleza nitamjulisha baada ya kufika ninapokwenda.
Niliondoka na ndege ya jioni na kufika Mwanza saa mbili usiku, kwa vile nilikuwa mgeni, nilimuomba dereva anipeleke kwenye hoteli nzuri iliyo nje kidogo ya mji. Kama jiji Dar basi iwe maeneo ya Temeke siyo Mbagala au Kibamba.
“Dada wewe mgeni?” dereva aliniuliza.
“Kaka nimekueleza nitafutie hoteli, maswali ya nini?” sikupenda maswali yake.
“Lazima nikuulize ili nijue hoteli gani inakufaa.”
“Yoyote nzuri lakini isiwe nje kidogo ya mji.”
“Kwani Mwanza hujawahi kufika?”
“Zamani sana, baba yangu aliondoka nina miaka kumi,” nilimdanganya.
“Mmh! Zamani sana, ulikuwa unakaa wapi?”
Mmh! Lile kidogo lilikuwa gumu kidogo na kunifanya ninyamaze kidogo kukumbuka maeneo ya Jiji la Mwanza. Baadhi ya maeneo niliyakumbuka nilipokuwa Dar niliwahi kuzisikia kama Igoma, Ilemela kwenye kituo cha Redio Free Africa na Star TV, Mabatini na Isamilo. Nilitafuta jina moja na kulitamka.
“Tulikuwa tunakaa Isamilo.”
“Mmh! Inaonekana mlikuwa nayo!”
“Baba yangu alikuwa mkuu wa polisi.”
“Ndiyo maana, vipi umekuja kibiashara?”
“Kaka yangu mbona maswali kama natafuta pasipoti?”
“Basi dada, nitakupeleka kwenye hoteli nzuri pia nitakupa namba yangu, ukiwa na shida nijulishe.”
“Hakuna tatizo,” nilimjibu kwa mkato kwa vile nilikuwa tayari nimechoka na maswali yake kama mpelelezi.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 10
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
“Mmh! Inaonekana mlikuwa nayo!”
“Baba yangu alikuwa mkuu wa polisi.”
“Ndiyo maana, vipi umekuja kibiashara?”
“Kaka yangu mbona maswali kama natafuta pasipoti?”
“Basi dada, nitakupeleka kwenye hoteli nzuri pia nitakupa namba yangu, ukiwa na shida nijulishe.”
“Hakuna tatizo,” nilimjibu kwa mkato kwa vile nilikuwa tayari nimechoka na maswali yake kama mpelelezi.
SASA ENDELEA...

Kwa vile ulikuwa usiku hata mandhari ya Jiji la Mwanza kutoka Uwanja wa Ndege sikuyaona japokuwa ilionesha jiji lilikuwa limejengeka sana. Baada ya muda alisimamisha gari mbele ya hoteli moja iliyokuwa na gharofa tatu lakini ilikuwa ipo katika hali nzuri na kunifanya nipapende hata kabla ya kukaa.
Niliingia na kukodi chumba kisha nilimlipa hela yake na asante nilimuongezea elfu ishirini. Alinishukuru na kuniachia namba yake ya simu ili niwapo na shida nimjulishe. Niliagana naye na kuingia ndani ya chumba changu kilichokuwa kwenye hali nzuri kilichokuwa ghorofa ya kwanza na kujilaza kwanza kabla ya kuoga na kutafuta chakula.
Baada ya kula niliagiza pombe kali na kunywa nusu chupa, nilijikuta nilewa na kupitiwa usingizi bila kujua mpaka siku ya pili. Kwa vile nilikuwa mgeni siku hiyo nilishinda ndani nikiangalia picha kwenye tivii.
Jioni nilitoka na kukaa sehemu ya bar iliyokuwa palepale kwenye ile hoteli ambayo ilikuwa na watu wengi majira ya kuanzia jioni. Nilikaa nje mpaka saa nne usiku niliporudi ndani kulala.
Katika hoteli ile ilikuwa na wapangaji wengi, mmojawapo dada mmoja wa kizungu ambaye alitokea kunizoea haraka. Muda mwingi nilikuwa naye kitu kilichofanya tuwe mtu na shogaye.
Japokuwa alikuwa mzungu alikuwa amechangamka sana kama mswahili, akikueleza kazaliwa Tanzania tena uswahilini, ungekubali kutokana na kuyajua mambo ya kiswahili na lugha ya kiswahili aliizungumza vizuri sana.
Kwa kweli kupata rafiki yule ambaye alinipunguzia upweke, kila jioni alinipeleka kumbi za starehe kama Delux, Kapili Kabana na kumbi nyingi za Jiji la Mwanza, ambazo nazo zilikuwa zimekucha.
Kama ujuavyo Mungu alivyonipendelea kila kona wanaume walinitolea macho, kila mmoja alitangaza dau nene ili kunikamata. Wengi walipitia kwa shoga yangu Carloliner. Japokuwa nami niyatamani maisha ya kujimwaga na kumpata mtu wa kunikata kiu yangu ya mapenzi.
Lakini sikuwa tayari kujiingiza kwenye shimo jingine la kifo baada kuponea tundu la sindano. Nilitamani maisha ya utulivu kwa muda mrefu ili kujipanga kimaisha ikiwezekana niichukue familia yangu niishi Mwanza baada ya kuufurahia mji huo ambao ulikuwa na pilikapilika kama Dar.
Ili kujiweka mbali na wanaume, waliomtuma Callo niliwadanganya kuwa mimi ni mke wa mtu, nipo pale kwa ajili ya kumsubiri mume wangu.
Wapo walioomba kufanya mapenzi na mimi hata kwa dakika moja ili wanihonge milioni. Nilijua nikikubali dakika hiyohiyo moja inaweza kunipeleka kaburini.
Pia ilionesha wanaume wengi walinitamani ili kutaka kujua ndani ya mwili wangu kuna nini kimefichwa kwenye umbile lenye utata.

Baada ya mwezi Callo aliondoka na kuniaga kuwa anasafiri kidogo na kuniacha peke yangu lakini baadhi ya wafanyakazi wa hoteli ile tayari nilikuwa nimeisha jenga nao urafiki kwa kuwatembelea maeneo waliokuwa wakikaa.
Wengine walikuwa wakikaa Igogo, Igoma Nyakato, Mabatini, Mkuyuni na Pasiansi.

Kwa kweli nilijikuta nikifurahia maisha ya Mwanza na kusahau ya Dar japokuwa moyo uliniuma kukaa mbali na familia yangu.
Nilijikuta nikipata wazo la haraka kwa nini nisiwasiliane na shoga yangu aniletee wanangu Mwanza ili niweze kuyaanza maisha mapya.
Lakini siku zote bandubandu humaliza gogo, ndani ya miezi tisa niliyokaa Mwanza pesa ilianza kunikatikia kutokana na matumizi bila mahesabu.
Hapo ndipo nilipojikuta kwenye wakati mgumu
na kushindwa nianzie wapi maisha kutokana kutokuwa na mradi wowote. Lakini bahati nzuri wakati huo rafiki yangu Callo alikuwa amerudi akiwa na pesa nyingi sana.
Alinieleza nisiwe na wasi atanisaidia, kwa kweli Callo alinisaidia vitu vingi ikiwepo kunipa pesa za matumizi na kunilipia pesa ya hotel kwa miezi miwili zaidi.
Nilimshukuru sana lakini siku zote Callo sikujua kazi zake japokuwa mawazo yangu huenda ni mfanyakazi wa mashirika ya kujitolea kusaidia umaskini Afrika.
********
Nakumbuka siku moja ambayo kulikuwa na sherehe ambayo tulikunywa sana, japokuwa nakumbuka sikunywa kinywaji kikali sana kutokana na kutokuwa na mzoefu na maeneo yale.
Siku ya pili nilipoamka nilijikuta nipo sehemu ambayo ilikuwa siijui, lakini ilionesha ni nyumba ya wageni. Nilipoangalia pembeni yangu nilishangaa kumuona mwanaume amelala usingizi mzito akikoroma.
Nikiwa bado nimo kwenye shuka ya hoteli ile iliyokuwa na jina la Aspen. Moyo ulinilipuka baada ya kuona kondomu zaidi ya tatu zilizokuwa zimetumika. Nilijikuta nikinyanyuka kitandani huku nikiitupa shuka pembeni.
Sikuamini kujikuta nikiwa mtupu bila nguo yoyote, moyo uliniuma na kujiuliza pale nimefikaje. Nilichukua nguo zangu haraka na kuzivaa ili niondoke.
Kabla ya kumaliza kuvaa sauti ya yule mwanaume ilinishtua:
"Mrembo mbona haraka subiri haki yako."
"Pumbavu unikome," nilimtukana huku nikimalizia kuvaa nguo zangu.
"Sikiliza mrembo umbile na kauli yako ni vitu tofauti, japokuwa pesa niliishampa Zungu lakini mahaba yako motomoto lazima nikuongezee ya asante."
Kauli ile ilinifanya nisite kuvaa nguo na kushtuka huku nikiweka mkono mdomoni kwa mshangao. Kauli ile ilionyesha jinsi gani Callo alivyo nifanyia biashara bila mwenyewe kujua. Wakati huo yule bwana alikuwa ameisha amka na kutoa pesa mfukoni na kunihesabia wekundu watano.
Kutokana na hasira nilimpiga nazo usoni pesa zake na kutoka kwa hasira huku nikimalizia kuvaa vizuri nje ya chumba kwenye korido. Japokuwa sikuwa na pesa muda ule ambao ulikuwa ni saa moja asubuhi, sikuwa na haja ya gari nilitembea kwa miguu huku nikiapa Callo atanitambua kwa kitendo alichonifanyia.
Nilijiuliza kwa nini hakunishirikisha akajua nitasemaje na mimi. Nilipofika hotelini nilikwenda moja kwa moja chumbani kwa Callo, sikumkuta.
Wafanyakazi wa hotelini walinieleza kuwa tangu tulipotoka pamoja jana yake hajarudi. Nilikwenda kuoga huku nikimsubiri kwa hamu kubwa.
Baada ya kupata supu ya nguvu nilijilaza kitandani kutokana na uchovu usingizi haukuchelewa, kunichukua.
****
Mkono wa mtu kunitikisa begani ulinifanya nifumbue macho. Hakuwa mwingine zaidi ya Callo.
"Vipi Shosti mbona umelala umerudi saa ngapi?" aliniuliza huku akitabasamu bila kujua ameniudhi sana.
Nijikuta nikijaa kifua na kushindwa nimjibu nini, nilimpandisha na kumshusha nisipate jibu.
"Sikiliza Suzy kwa vile wewe ni rafiki yangu kipato cha jana sichukui hata senti tano, hela zako hizi hapa."
Callo alisema huku akihesabu elfu 50 na kunikabidhi. Kabla ya kuzipokea nilimuuliza.
"Za nini?"
"Suzy kutokana na kazi ya jana, kwenye pati kuna mtu alijipendekeza nami sikuwa na jinsi kwa vile najua hata shemeji akirudi haipungui utamu hiyo."
Mmh! Maneno ya Callo yalinikata makali nilimuangalia nisimmalize kwa sauti ya chini nilimuuliza:
"Callo kwa nini usiniambie mapema ili nami nikajindaa?"
"Suzy japokuwa sasa hivi mambo yako si mazuri lakini umekuwa mtu mwenye msimamo. Kwa vile hata mimi kazi inayoniweka mjini ni hii, ndiyo maana nimeamua kukushirikisha ili mambo yako yakiwa mazuri utajua jinsi ya kujipanga huenda mumeo ameingia mitini.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 10
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
“Mmh! Inaonekana mlikuwa nayo!”
“Baba yangu alikuwa mkuu wa polisi.”
“Ndiyo maana, vipi umekuja kibiashara?”
“Kaka yangu mbona maswali kama natafuta pasipoti?”
“Basi dada, nitakupeleka kwenye hoteli nzuri pia nitakupa namba yangu, ukiwa na shida nijulishe.”
“Hakuna tatizo,” nilimjibu kwa mkato kwa vile nilikuwa tayari nimechoka na maswali yake kama mpelelezi.
SASA ENDELEA...

Kwa vile ulikuwa usiku hata mandhari ya Jiji la Mwanza kutoka Uwanja wa Ndege sikuyaona japokuwa ilionesha jiji lilikuwa limejengeka sana. Baada ya muda alisimamisha gari mbele ya hoteli moja iliyokuwa na gharofa tatu lakini ilikuwa ipo katika hali nzuri na kunifanya nipapende hata kabla ya kukaa.
Niliingia na kukodi chumba kisha nilimlipa hela yake na asante nilimuongezea elfu ishirini. Alinishukuru na kuniachia namba yake ya simu ili niwapo na shida nimjulishe. Niliagana naye na kuingia ndani ya chumba changu kilichokuwa kwenye hali nzuri kilichokuwa ghorofa ya kwanza na kujilaza kwanza kabla ya kuoga na kutafuta chakula.
Baada ya kula niliagiza pombe kali na kunywa nusu chupa, nilijikuta nilewa na kupitiwa usingizi bila kujua mpaka siku ya pili. Kwa vile nilikuwa mgeni siku hiyo nilishinda ndani nikiangalia picha kwenye tivii.
Jioni nilitoka na kukaa sehemu ya bar iliyokuwa palepale kwenye ile hoteli ambayo ilikuwa na watu wengi majira ya kuanzia jioni. Nilikaa nje mpaka saa nne usiku niliporudi ndani kulala.
Katika hoteli ile ilikuwa na wapangaji wengi, mmojawapo dada mmoja wa kizungu ambaye alitokea kunizoea haraka. Muda mwingi nilikuwa naye kitu kilichofanya tuwe mtu na shogaye.
Japokuwa alikuwa mzungu alikuwa amechangamka sana kama mswahili, akikueleza kazaliwa Tanzania tena uswahilini, ungekubali kutokana na kuyajua mambo ya kiswahili na lugha ya kiswahili aliizungumza vizuri sana.
Kwa kweli kupata rafiki yule ambaye alinipunguzia upweke, kila jioni alinipeleka kumbi za starehe kama Delux, Kapili Kabana na kumbi nyingi za Jiji la Mwanza, ambazo nazo zilikuwa zimekucha.
Kama ujuavyo Mungu alivyonipendelea kila kona wanaume walinitolea macho, kila mmoja alitangaza dau nene ili kunikamata. Wengi walipitia kwa shoga yangu Carloliner. Japokuwa nami niyatamani maisha ya kujimwaga na kumpata mtu wa kunikata kiu yangu ya mapenzi.
Lakini sikuwa tayari kujiingiza kwenye shimo jingine la kifo baada kuponea tundu la sindano. Nilitamani maisha ya utulivu kwa muda mrefu ili kujipanga kimaisha ikiwezekana niichukue familia yangu niishi Mwanza baada ya kuufurahia mji huo ambao ulikuwa na pilikapilika kama Dar.
Ili kujiweka mbali na wanaume, waliomtuma Callo niliwadanganya kuwa mimi ni mke wa mtu, nipo pale kwa ajili ya kumsubiri mume wangu.
Wapo walioomba kufanya mapenzi na mimi hata kwa dakika moja ili wanihonge milioni. Nilijua nikikubali dakika hiyohiyo moja inaweza kunipeleka kaburini.
Pia ilionesha wanaume wengi walinitamani ili kutaka kujua ndani ya mwili wangu kuna nini kimefichwa kwenye umbile lenye utata.

Baada ya mwezi Callo aliondoka na kuniaga kuwa anasafiri kidogo na kuniacha peke yangu lakini baadhi ya wafanyakazi wa hoteli ile tayari nilikuwa nimeisha jenga nao urafiki kwa kuwatembelea maeneo waliokuwa wakikaa.
Wengine walikuwa wakikaa Igogo, Igoma Nyakato, Mabatini, Mkuyuni na Pasiansi.

Kwa kweli nilijikuta nikifurahia maisha ya Mwanza na kusahau ya Dar japokuwa moyo uliniuma kukaa mbali na familia yangu.
Nilijikuta nikipata wazo la haraka kwa nini nisiwasiliane na shoga yangu aniletee wanangu Mwanza ili niweze kuyaanza maisha mapya.
Lakini siku zote bandubandu humaliza gogo, ndani ya miezi tisa niliyokaa Mwanza pesa ilianza kunikatikia kutokana na matumizi bila mahesabu.
Hapo ndipo nilipojikuta kwenye wakati mgumu
na kushindwa nianzie wapi maisha kutokana kutokuwa na mradi wowote. Lakini bahati nzuri wakati huo rafiki yangu Callo alikuwa amerudi akiwa na pesa nyingi sana.
Alinieleza nisiwe na wasi atanisaidia, kwa kweli Callo alinisaidia vitu vingi ikiwepo kunipa pesa za matumizi na kunilipia pesa ya hotel kwa miezi miwili zaidi.
Nilimshukuru sana lakini siku zote Callo sikujua kazi zake japokuwa mawazo yangu huenda ni mfanyakazi wa mashirika ya kujitolea kusaidia umaskini Afrika.
********
Nakumbuka siku moja ambayo kulikuwa na sherehe ambayo tulikunywa sana, japokuwa nakumbuka sikunywa kinywaji kikali sana kutokana na kutokuwa na mzoefu na maeneo yale.
Siku ya pili nilipoamka nilijikuta nipo sehemu ambayo ilikuwa siijui, lakini ilionesha ni nyumba ya wageni. Nilipoangalia pembeni yangu nilishangaa kumuona mwanaume amelala usingizi mzito akikoroma.
Nikiwa bado nimo kwenye shuka ya hoteli ile iliyokuwa na jina la Aspen. Moyo ulinilipuka baada ya kuona kondomu zaidi ya tatu zilizokuwa zimetumika. Nilijikuta nikinyanyuka kitandani huku nikiitupa shuka pembeni.
Sikuamini kujikuta nikiwa mtupu bila nguo yoyote, moyo uliniuma na kujiuliza pale nimefikaje. Nilichukua nguo zangu haraka na kuzivaa ili niondoke.
Kabla ya kumaliza kuvaa sauti ya yule mwanaume ilinishtua:
"Mrembo mbona haraka subiri haki yako."
"Pumbavu unikome," nilimtukana huku nikimalizia kuvaa nguo zangu.
"Sikiliza mrembo umbile na kauli yako ni vitu tofauti, japokuwa pesa niliishampa Zungu lakini mahaba yako motomoto lazima nikuongezee ya asante."
Kauli ile ilinifanya nisite kuvaa nguo na kushtuka huku nikiweka mkono mdomoni kwa mshangao. Kauli ile ilionyesha jinsi gani Callo alivyo nifanyia biashara bila mwenyewe kujua. Wakati huo yule bwana alikuwa ameisha amka na kutoa pesa mfukoni na kunihesabia wekundu watano.
Kutokana na hasira nilimpiga nazo usoni pesa zake na kutoka kwa hasira huku nikimalizia kuvaa vizuri nje ya chumba kwenye korido. Japokuwa sikuwa na pesa muda ule ambao ulikuwa ni saa moja asubuhi, sikuwa na haja ya gari nilitembea kwa miguu huku nikiapa Callo atanitambua kwa kitendo alichonifanyia.
Nilijiuliza kwa nini hakunishirikisha akajua nitasemaje na mimi. Nilipofika hotelini nilikwenda moja kwa moja chumbani kwa Callo, sikumkuta.
Wafanyakazi wa hotelini walinieleza kuwa tangu tulipotoka pamoja jana yake hajarudi. Nilikwenda kuoga huku nikimsubiri kwa hamu kubwa.
Baada ya kupata supu ya nguvu nilijilaza kitandani kutokana na uchovu usingizi haukuchelewa, kunichukua.
****
Mkono wa mtu kunitikisa begani ulinifanya nifumbue macho. Hakuwa mwingine zaidi ya Callo.
"Vipi Shosti mbona umelala umerudi saa ngapi?" aliniuliza huku akitabasamu bila kujua ameniudhi sana.
Nijikuta nikijaa kifua na kushindwa nimjibu nini, nilimpandisha na kumshusha nisipate jibu.
"Sikiliza Suzy kwa vile wewe ni rafiki yangu kipato cha jana sichukui hata senti tano, hela zako hizi hapa."
Callo alisema huku akihesabu elfu 50 na kunikabidhi. Kabla ya kuzipokea nilimuuliza.
"Za nini?"
"Suzy kutokana na kazi ya jana, kwenye pati kuna mtu alijipendekeza nami sikuwa na jinsi kwa vile najua hata shemeji akirudi haipungui utamu hiyo."
Mmh! Maneno ya Callo yalinikata makali nilimuangalia nisimmalize kwa sauti ya chini nilimuuliza:
"Callo kwa nini usiniambie mapema ili nami nikajindaa?"
"Suzy japokuwa sasa hivi mambo yako si mazuri lakini umekuwa mtu mwenye msimamo. Kwa vile hata mimi kazi inayoniweka mjini ni hii, ndiyo maana nimeamua kukushirikisha ili mambo yako yakiwa mazuri utajua jinsi ya kujipanga huenda mumeo ameingia mitini.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 11
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
"Suzy kutokana na kazi ya jana, kwenye pati kuna mtu alijipendekeza nami sikuwa na jinsi kwa vile najua hata shemeji akirudi haipungui utamu hiyo."
Mmh! Maneno ya Callo yalinikata makali nilimuangalia nisimmalize kwa sauti ya chini nilimuuliza:
"Callo kwa nini usiniambie mapema ili nami nikajindaa?"
"Suzy japokuwa sasa hivi mambo yako si mazuri lakini umekuwa mtu mwenye msimamo. Kwa vile hata mimi kazi inayoniweka mjini ni hii, ndiyo maana nimeamua kukushirikisha ili mambo yako yakiwa mazuri utajua jinsi ya kujipanga huenda mumeo ameingia mitini.
SASA ENDELEA...

Huyo mwanaume gani asiyejua mkewe mwaka sasa unakatika haonekani wala kukutumia pesa za matumizi, yeye anajua unakula mawe?"
"Sawa, lakini ulitakiwa kunijulisha mapema."
"Lazima ungekataa," alizungumza huku akinikabidhi elfu 50 ambazo sikuwa na jinsi zaidi ya kuzipokea na kujilaumi kuzikataa zile elfu 50 zingine nilizopewa hotelini asubuhi.
"Suzy kwa sura na umbile lako ndani ya mwaka utajenga nyumba na kupata usafiri wa kutembelea. Mimi napata pesa kwa uzoefu tu, lakini ningekuwa kama wewe mbona ningenunua hata ndege," Callo alinimwagia sifa.
Bila kutegemea nilijikuta nikirudi kulekule nilipotoka kazi ya uchangudoa. Sikuwa na jinsi zaidi ya kuifanya ili kujikomboa maana mambo yalivyokuwa yakielekea yalinitisha nisijue hatma yangu.
Niliingia kilingeni rasmi na changudoa mzoefu Callo ambaye alinipa mbinu za kimataifa ambazo yeye ilizitumia kufanya mapenzi na wanaume wengi bila kuchoka. Ikiwa pamoja na kutumia madawa ya kuongeza nguvu ili kukabiliana na wanaume wengi.

Kwa kweli kazi yangu haikuwa ngumu kutokana na kupata wateja kwenye hoteli zote kubwa za Jiji la Mwanza. Kutokana na upendeleo niliopewa na Mungu na maelekezo ya kuifanya kazi ile kimataifa, niliweza kutengeneza pesa kama sina akili nzuri.
Kazi ile ya ukahaba ilikuwa ina tofauti kubwa na ile tuliyokuwa tukiifanya Dar. Hatukuwa tukienda kujiuza barabarani na kujinadi uchi kama mnadani. Kule ilikuwa ni kujipamba na kuingia hotel kubwa na kutafuta meza ya pembeni huku ukiagiza kinywaji cha bei kubwa kwani hata mwanaume itakaye jigonga kwako lazima atakujua wewe ni mtu wa matawi ya juu.
Hata akikutaka dau lake lazima litakuwa la juu tu. Sio unaingia hotelini unaagiza soda moja na kuinywa zaidi ya masaa zaidi ya matatu au matano.
Hata mwanaume ukiwa pembeni akikufuatilia atakujua wewe mtu wa hadhi ya chini. Siku zote ukitaka kukamata samaki mkubwa lazima uweke chambo mkubwa ama sio utaendelea kukamata vidagaa vya maji mafupi.
Na dau lake sanasana atakupa elfu kumi akizidi sana kumi na tano au ukopwe kabisa. Ukitaka faida ya biashara yako lazima uingie gharama ya matangazo. Wahindi wanasema weka mingi upate mingi, siku nyingine naweza kutumia hata elfu 30 na ukatoka kapa.
Lakini mambo yakiwa mazuri mpaka asubuhi unaweza kutoka na laki mbili mpaka tatu kama siku kijiwe kimekubali, lakini pesa ya chini ilikuwa elfu hamsini.
Tulikuwa tukipata pesa nyingi, kazi tulikuwa tukiifanya mara tatu kwa wiki Jumatano Jumamosi na Jumapili, siku nyingine tulikuwa tukipumzika.
Nilijikuta nikiyafurahia maisha ya Mwanza ambayo nilitengeneza pesa ambazo baada ya mwezi nilikuwa nimeisha fungua akanti mpya na kuweza kuweka milioni moja na laki tano ambazo zilikuwa hazina kazi kwa muda ule. Niliweza kusafiri miji mbalimbali kama Machimboni ambako kwa kweli tulitengeneza pesa sana. Kule watu walitoa pesa bila kuifikiria, kwa kweli Machimboni nilikuwa nikitembea na wanaume zaidi ya saba kwa siku.
Mwanzo nilipata shida kwa kutembea na wanaume watatu au wanne, kila nilipomaliza nilikuwa nipo hoi na kushindwa kujitambua. Kuna siku nilitembea na wanaume watano japo nilipata fedha ya maana, lakini siku hiyo nilipoteza fahamu na ilibidi nikimbizwe hospitali. Kitu kilichonifanya nipumzike kazi kwa miezi miwili.
Baada ya kupona ndipo shoga yangu Callo aliponifundisha kutumia dawa za kuongeza nguvu ambazo tulizinunua kwa bei kubwa. Nilizitumia kwa muda na kuona faida yake kwa kuweza kufanya mapenzi na wanaume shababi zaidi ya kumi bila kuchoka.
Biashara ilikuwa nzuri iliyotuongezea kipato na kuweza kufikisha milioni saba kwa miezi sita. Callo alipingana na wazo langu la kutafuta chumba kupanga kwani alinieleza kazi ile haitaki bughuza.
Nilikubaliana naye kutokana na kipato tulichokipata kiliweza kutupatia pesa ya kulipia chumba na matumizi ya kawaida pamoja na pesa ya kuweka benki.
Niliweza kwenda naye baadhi ya mikoa na nje ya nchi za kama Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi mpaka Zaire ambako tulitengeneza pesa za kumwaga. Callo alikuwa mzoefu wa kazi ile alinifundisha njia nyingine ya kujiongezea kipato ambayo kwa njia nyingine ilikuwa ya hatari.
Alinifundisha kuwaibia watu pesa kwa mtindo wa kuwawekea dawa za kulevya kisha kuwaibia wakiwa wamelala fofofo hawajitambui kwa kuleweshwa na dawa. Hapo unamsachi na kuchukua pesa zake na kutimka usiku uleule.
Kwa mlevi tulikuwa tukimwekea kwenye kinywaji, kwa asiye mlevi tulikuwa tukimpakia dawa kwenye matiti na katikati ya mapenzi, unamuomba akunyonge matiti ili kukupandisha mzuka. Akijidanganya tu kunyonya anakwenda na maji na kufanya vitu vyetu.
Ile haikuwa ngeni kwangu ndiyo njia niliyotumia kulipizia kisasi, ila shoga yangu alikuwa mtaalamu sana kuliko mimi. Huwezi kuamini safari zetu tulikuwa tukirudi na pesa zaidi ya milioni tano kwa wiki.
Japokuwa tulipata pesa lakini tulikuwa tukiishi maisha ya kujificha tunapokuwa tupo nje ya nchi. Lakini tulipokuwa tukirudi tulijiachia kisawasawa.
Callo kila nililokuwa nikilitaka kulifanya kwa wakati ule alinikataza. Kama kununua nyumba au gari la kutembelea. Alinieleza pesa niliyokuwa nayo zaidi ya milioni kumi na tano zilikuwa kidogo sana alipenda nipate wazo lile nitakapokuwa na zaidi ya milion 50 mpaka 100.
Kwa biashara ile nilikuwa nikiamini ndani ya mwaka mzima ningekuwa nimefikisha, kwani wakuja walikuwa ni wengi ambao tuliwaingiza mjini. Pia tulijichanganya kwenye magulio ya ng'ombe ambako tuliwaokota wakuja kama hatuna akili nzuri.
Callo alikuwa jasusi la kimapenzi ilifikia hatua ya kunifundisha hata kuua japokuwa kitu kile hakikuwa kigeni kwangu lakini nilifanya mchezo ule katika kulipa kisasi si katika uchangudoa.
Kitendo kile tulikifanya kwenye Machimbo ya almasi na dhahabu Jamhuri ya Kongo. Kule tulitoka na pesa zaidi ya milioni 50.
Taratibu nilianza kuvutika na kufika hatua ya mimi kuwaza kuua pale mtu atakapoingia kwenye anga zangu. Mimi na Callo tulikuwa kama mapacha hasa Callo alinitumia kutengeneza pesa nyingi kutokana na mimi kukubalika sana kwa wanaume.
Tulijikuta tukiingia katika kazi ya ujambazi kuwaibia watu waliokuja kununua dhahabu kwa kuwapulizia dawa za kulevya na kuchukua fedha zote kisha tulitoroka usiku huo na kurudi Mwanza.
Lakini kila kizuri kina ubaya wake, siku moja tukiwa tupo Geita kwenye machimbo tukiwa tumepanga gesti moja na mtu mmoja aliyekuwa na pesa za manunuzi ya dhahabu. Callo kwa uzoefu wake alimgundua.
Yule bwana pamoja na kumtega, aliruka vihunzi lakini Callo aliniambia nimuache kwani alijua angemfanya nini.
Siku ile Callo alinikataza kuchukuliwa na mwanaume yeyote hata kama angenihonga milioni.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 12
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Lakini kila kizuri kina ubaya wake, siku moja tukiwa tupo Geita kwenye machimbo tukiwa tumepanga guest moja na mtu mmoja aliyekuwa na pesa za manunuzi ya dhahabu. Callo kwa uzoefu wake alimgundua.
Yule bwana pamoja na kumtega aliruka vihunzi lakini Callo aliniambia nimuache kwani alijua angemfanya nini.
Siku ile Callo alinikataza kuchukuliwa na mwanaume yoyote hata kama angenihonga milioni.
SASA ENDELEA...

“ Moureen leo hatufanyi biashara ya mwili.”
“Kwa nini?”
“Kuna kazi moja ina hela kuliko hata kulala na wanaume saba.”
“Hakuna tatizo.”
Nikiwa nimelala chumbani kwangu
Callo alinishtua usiku wa manane na kuniomba tuondoke pale. Niliniamka na kutoka, kutokana na kunijulisha nilale kama nipo kwenye lindo yaani nilale na nguo zangu.
Nilipoamka nimkuta Callo ana begi lilionyesha amelichukua kwa yule mwanaume.Tuliondoka Geita usiku uleule na kuingia Mwanza Alfajiri. Tulipofika tuliteremkia mjini na kukodi gari jingine hadi hotelini kwetu. Tulipofika tulikwenda moja kwa moja hadi chumbani kwake na kulifungua lile begi lililokuwa na pesa nyingi.
Kwa vile tulikuwa tumechoka sana kila mmoja alipumzika chumbani kwake ili baadaye tuweze kuzihesabu na kugawana. Nilikwenda chumbani kwangu na kujimwagia maji ili nijilaze kutokana kulala usingizi wa machugamachuga. Baada ya kuoga na kupanda kitandani na kulipitiwa na usingizi mzito.
*****
Sauti kali ya mlango kugongwa ilinishtua katika usingizi mzito nilijikuta nikifoka kwa ukali
"Ni ustaarabu gani huo?"
Sauti kali ya juu toka nje uliniamuru nifungue mlango:
"Fungua!"
Nikiwa nimejifunga taulo tu nilikwenda hadi mlangoni na kufungua, nilishangaa kuona askari wenye bunduki wakiwa na mhudumu wa hoteli wakiwa mlangoni kwangu, nilishangaa na kuwauliza:
"Jamani kuna nini?" niliuliza kwa woga kidogo.
"Mwenzio amekwenda wapi?" askari aliyekuwa mbele aliniuliza.
"Mwenzangu nani?"
"Muuaji mwenzio."
Kauli ile ilinishtua na kujikuta nikibakia kinywa wazi na kukumbuka safari yetu ya usiku Callo alifanya mambo yake.
"Tunakuuliza muuaji mwenzako amekwenda wapi?"
"Kwa kweli sijui lolote wala mimi sio muuaji na sijui lolote kuhusiana na huyo mnayemtafuta."
Nilijitahidi kujitetea lakini hawakunielewa na kuamliwa nichukuliwe na kupelekwa polisi tayari kufunguliwa mashtaka la mauaji baada ya kuonekana Callo amekimbia na mimi kuwa naye siku ya tukio.
*************
Nilichukuliwa na kupelekwa polisi ambako nilifunguliwa mashtaka ya mauaji, pamoja na kujitetea hakuna aliyenielewa. Nilikaa ndani miaka miwili bila kuhukumiwa, Wakati naingia gerezani kumbe nilikuwa na ujauzito wa mwezi mmoja wa mwanangu wa mwisho. Nilijikuta mtoto wa kike kujiingiza kwenye kesi mbaya ya wizi na uuaji. Kibaya sijukua wanangu wanaishi maisha gani japokuwa niliacha fedha nyingi ya matunzo.
Nilimshukuru Mungu nilijifungua salama na mwanangu kukua katika hali nzuri kipindi chote nilichokuwa gerezani.
Siku zote nilijiuliza Callo alitakuwa amekwenda wapi na kwa nini alikimbia na kuniacha bila kunijulisha hatari ile. Mungu mkubwa baada ya kusota gerezani kwa miaka miwili. Nilitoka kwa msamaha wa Rais baada ya kukosekana ushahidi wa kutosha wa kunitia hatiani.
Nilitoka kwenye gereza la Butimba na kurudi hadi mjini na kwenda moja kwa moja benki angalau nichukue pesa kidogo za matumizi ili nijipange upya. Namshukuru Mungu nilikuta fedha zangu zaidi ya milioni 35. Niliona ndicho kipindi changu cha kurudi Dar kuungana na familia yangu.
Nilirudi Dar na kumshukuru shoga yangu kunitunzia wanangu kipindi chote nikiwa mbali naye. Nilifurahi kuwakuta wanangu wapo katika hali nzuri, nilimshukuru sana Mungu.
Fedha niliyokuwa nayo nilinunua nyumba kisha nilijifikiria kuanzisha biashara ya salon ili kujiingizia kipato. Kwa vile sikujua hali yangu ya mbele niliwapeleka watoto wangu shule ya kulipia ya kulala hukohuko kwa miaka mitatu ili nijipanga kwa kuamini mpaka ada ya miaka mitatu.
Niliamini mpaka ada inakwisha nitakuwa nimepata fedha nyingine.
*****
Baada ya kupumzika nilijikuta nikipata hamu ya kurudi kwenye kazi yangu japo sikuwa na shida ya kimaisha. Kwa vile jasiri haachi asili kukaa hivihivi nilishindwa nikajikuta nakuwa na hamu ya kuingia kwenye kazi yangu ya asili. Kwa kweli nilirudi kijiweni na kuendelea na kazi yangu kwa vile sikufanya kwa shida nilifanya biashara kwa kuchagua wateja.
Niliwapenda wateja wa ndani ya gari kuliko kwenda kulala naye, kwa kweli ile ilinisaidia kufanya mapenzi mepesi pia kupata malipo mazuri na kulala nyumbani.
Kwa kweli kazi niliifanya kwa kupenda huku ikiniongezea fedha ya matumizi ambayo ilinifanya nisitumie fedha zangu. Kwa vile nilikuwa peke yangu kwa kweli fedha niliyopata kila nilipotoka ilinitosha na nyingine kuweka ndani. Maisha yalikwenda vizuri huku nikifurahia mpangilio wangu wa biashara.
Siku moja nikiwa kijiweni lilikuja gari la kifahari na kusimama mbele yetu, kwa vile nilikuwa kibiashara ya kuchagua na si kukimbilia kama wenzangu. Kutokana na kujiamini na kutofanya kazi kwa njaa nilisimama nyuma yao, lakini mwenye gari alinitaka mimi. Nilipita mbele yao na kuonana na mzee aliyekuwemo kwenye gari ambaye alikuwa amevaa kofia ya pana.
“Ingia mrembo.”
Niliingia bila kusema kitu na kukaa siti ya mbele, baada ya kukaa mzee yule alinisamilia.
“Habari mrembo?”
“Nzuri.”
Japokuwa alikuwa mtu wa mzima umri wa baba yangu kwenye biashara yetu hakukuwa na shikamoo, akitaka kuamkiwa aende kwa watoto wake.
“Nikupatie shilingi ngapi?”
“Elfu hamsini.”
“Mpaka asubuhi?”
“Hapana huwa silali kwa mtu pia ukitaka mapenzi na mimi tunamalizana kwenye gari siku hizi wanaume haaminiki.”
“Kwa nini?”
“Wengi wamekuwa na tabia mbaya anakupeleka guest na kukulewesha kisha anakufanyia mchezo mbaya.”
“Aah! Binti mimi mtu wa heshima siwezi kufanya hivyo.”
“Wengi walisema hivyo, lakini mwisho wake nilijuta.”
“Sasa mapenzi ndani ya gari yana raha gani?”
“Hujawahi kufanyiwa?”
“Bado, napenda sana kitandani.”
“Basi leo jaribu kesho utanitafuta.”
“Poa ngoja nijaribu leo, lakini mbona gharama kubwa.”
“Hata huduma yake ni kubwa.”
Mzee mzima alipaki gari pembeni na kuteremsha suruali nusu mlingoti na kuanza kumpatia huduma ambayo ilimpagawawisha na kuniomba twende hotelini ili nimpe raha zaidi.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 13
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
“Sasa mapenzi ndani ya gari yana raha gani?”
“Hujawahi kufanyiwa?”
“Bado, napenda sana kitandani.”
“Basi leo jaribu kesho utanitafuta.”
“Poa ngoja nijaribu leo, lakini mbona gharama kubwa.”
“Hata huduma yake ni kubwa.”
Mzee mzima alipaki gari pembeni na kuteremsha suruali nusu mlingoti na kuanza kumpatia huduma ambayo ilimpagawawisha na kuniomba twende hotelini ili nimpe raha zaidi.
SASA ENDELEA...

“Binti unajua, sijawahi kufanyiwa mchezo kama huu toka nizaliwe.”
“Mzee punguza mapepe leo hamu zako zote zitaishia humuhumu ndani ya gari.”
Niliendelea kumpa huduma mzee iliyompagawisha na kuniomba kesho tena nionane naye.
“Mrembo kazi unaijua badala ya elfu hamsini ninakupa laki mbili.”
“Asante mzee wangu, kwenye gari hivi kitandani si ungehonga nyumba.”
“Binti fedha ninayo na uzee wangu fedha niliyonayo nakula raha tu.”
“Na mama nyumbani?”
“Mama kachoka kawa kama mti uliokauka, unatia mapengo panga langu, lakini wewe binti laiini hata kwa wembe unakatika.”
“Kwa hiyo nikija mchana utanipa shilingi ngapi?”
“Japokuwa nilikuwa nataka kuondoka kesho lakini kwa ajili yako nitakupa milioni.”
“Weweee acha utani!” macho ya tamaa yalinitoka pima.
Tamaa iliniingia na kuitamani ile fedha lakini niliamini huduma niliyompa kwa usiku ule na malipo ya laki mbili si haba. Niliamini sikuwa na haja ya kurudi kijiweni baada ya kutoka kwa babu ningekodi gari na kurudi nyumbani.
“Kweli binti, raha nilizopata sikuwa kupata katika ujana wangu na wenzako wengi wanajali fedha kuliko huduma.”
“Kwa hiyo upo hoteli gani?”
“Serena.”
“Kesho nije saa ngapi?”
“Kuanzia saa nne asubuhi nitakusubiri wewe tu.”
“Poa, wacha niwahi home.”
“Kwa jinsi ulivyonifurahisha nitakuongezea laki ya nauli ya kukupeleka nyumbani na nyingine ya kukuleta hotelini.”
“Asante mzee wangu.”
Kabla ya kuondoka mzee yule alinipa business card, ili kesho nikifika nimpigie simu kama yumo ndani. Niliichukua na kukodi teksi hadi kwangu huku nikifurahi siku ile kuwa yenye bahati. Nilipofika nilioga na kula kisha nilichukua pombe kali kwenye friji na kunywa, kisha nilijilaza kuitafuta siku ya pili.
****
Asubuhi niliamka na kujiandaa kwa ajili ya kwenda kuonana na mteja wangu huku nikijiandaa kumpa penzi takatifu mteja wangu ili niendelee kula zaidi vitu vya yule mzee aliyekuwa akipata mapenzi ya kulipua. Siku hiyo nilijipamba kwa nguo nzuri yenye mvuto ambayo nilipoivaa kila mwanaume alinimezea mate.
Baada kuhakikisha nipo sawa nilichukua business card na kuitazama, jicho langu lilishtuka kukuta jina kama la baba yangu mzazi.
“Mmh! Ina maana majina yana fanana? Hapana labda siyo yeye ngoja nikamuone. Baba yangu hawezi kufanya vitu kama hivi.”
Nilijikuta nikiwaza hivyo, lakini akili
nyingine iliniambia nisiende moja kwa moja, nikifika nikae sehemu ili kumuona atakaye tokea isiwe baba yangu mzazi kikawa kizaazaa.

Baada ya kuamini nipo sawa nilitoka na kukodi gari mpaka Serena Hoteli kuonana na mwanaume wangu ambaye nilimchanganya kwa mapenzi. Moyoni nikipanga kumfanyia mambo makubwa mwanaume ambaye alionekana mgeni katika medani ya mapenzi. Pamoja na kupanga yale bado moyo wangu ulikuwa na wasiwasi na jina la yule mwanaume kufanana na la baba yangu mzazi, japokuwa tayari nilikuwa nimeshafanya naye mapenzi.
Nilipofika hotelini niliteremka na kuingia hadi mapokezi kisha nilipiga simu. Niliamini kwa jinsi nilivyokuwa nimevaa wigi na miwani isingekuwa rahisi kunitambua.
Baada kuketi kwenye kochi nilipiga simu ambayo iliita kidogo na kupokelewa mara moja kuonesha alikuwa ameishikilia mkononi.
“Haloo.”
“Haloo bebi,” nilijibu kwa pozi.
“Vipi umefika?”
“Ndiyo.”
“Basi njoo ndani chumba namba 220.”
“Hapana bebi nifuate sijawahi kuingia, naogopa.”
“Basi ingia mpaka mapokezi.”
“Noo, bebi naogopa njoo nipo nje ya hoteli.”
“Haya nakuja umevaaje?”
“Jamani bebi jana tu umenipotea?” nilijishauwa mtoto wa kike.
“Si unajua ilikuwa usiku sikukutazama usoni.”
“Mi mbona nakukumbuka, nikukuona tu nakufuata.”
“Hakuna tabu nakuja.”
Baada ya kukata simu nilitulia huku nikiitengeneza vizuri miwani yangu kuhakikisha nampoteza atakayetoka kunifuata. Kilichonifurahisha zaidi kilikuwa kutonifahamu usiku ule, ile ilikuwa nafasi ya kumtambua kama ni baba au la, japokuwa niliamini baba yangu hawezi kuwa na tabia chafu kama zile.
Niliwa nimeinama nikisoma ujumbe kwenye simu, nilishtuliwa na sauti.
“Samahani binti.”
“Bila samahani,” nilijibu huku nikinyanyua uso wangu.
Moyo ulishtuka kidogo usimame, aliyekuwa amesimama mbele yangu ni baba yangu mzazi mzee Hans Mouses. Nilijitahidi kuficha hofu yangu na kumtazama kupitia msaada wa miwani.
“Mgeni wangu?” baba aliniuliza bila kujua niliyekaa pale ni mwanaye wa kumzaa.
“Hapana,” nilikataa huku nikitikisa kichwa kwa msisitizo.
“Ok, samahani.”
“Bila samahani.”
Mzee Hans Mouses aliyekuwa amevaa penzi ya maua na flana kwa juu na chini alivaa sandoz aliondoka kuelekea nje. Hapo ndipo nilipoamini kumbe jana yake nilitembea na baba yangu mzazi.
Lakini nilitaka kupata ukweli, baada ya kunipa mgongo akielekea nje niliipiga simu yake.
Baada ya kuita nilimuona akipokea huku akitokomea.
“Haloo mpenzi upo wapi?” aliniuliza.
“Wee upo wapi?”
“Mi ndo’ natoka nje ya hoteli.”
“Nikwambie kitu mpenzi?”
“Niambie tu.”
“Lakini naomba usikasilike.”
“Siwezi, niambie tu.”
“Nimeondoka nyumbani kwa haraka ya kukuwahi nimeondoka na ufunguo wa geti, hivyo nimepigiwa nirudishe funguo ili baba atoe gari,” nilitengeneza uongo.
“Ooh! Kwani unakaa na nani?”
“Na wazazi.”
“Kwa hiyo?”
“Naomba nifikisha ufunguo nyumbani na kurudi mara moja.”
“Basi haina tatizo, leo nipo kwa ajili yako.”
“Poa ila samahani kwa kuonekana mswahili.”
“Usihofu bebi wahi basi.”
“Ok.”
Nilikata simu na kutulia huku macho yangu nikiyaelekeza mlango wa kutokea nje. Baada ya muda nilimuona baba akirudi kuonesha anaamini kabisa mpenzi wake amerudi nyumbani.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 14
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Nilikata simu na kutulia huku macho yangu nikiyaelekeza mlango wa kutokea nje. Baada ya muda nilimuona baba akirudi kuonesha anaamini kabisa mpenzi wake amerudi nyumbani.
SASA ENDELEA...

Baada ya kunipita na kuelekea chumbani nilinyanyuka na kuelekea nje. Nilipofika nje nilikodi gari hadi nyumbani, nilipofika nilijilaza kitandani kichwa kikiwa kinaniuma baada ya kugundua nimefanya mapenzi na baba yangu mzazi kwa sababu ya kufanya mapenzi gizani. Nilijiuliza kama asingenipa busness card ingekuwaje pale ambapo ningekwenda moja kwa moja chumbani na kumkuta baba amejaa tele.
Nilijikuta nikipata wazo lingine na kujinga kwa kujilaumu kuondoka, nilitakiwa kwenda chumbani kwake ili aone faida ya kunifukuza kwake.
Lakini wazo kama lile sikukubaliana nalo, niliamini nilitakiwa kumuheshimu mzazi wangu kwa vile kosa lilikuwa langu na tukio la jana yake litabaki kama bahati mbaya.
Sikutaka kujilaumu kwa kitendo kilichotokea kwa vile niliamini ilikuwa ajali kazini.
Nilijikuta nikijawa na mawazo kuhusu baba yangu kujiingiza kwenye tabia ya kutembea na machangudoa hasa nikizingatia alikuwa akiwalaani watoto wa watu waliokuwa wakijiuza.
Nilikumbuka jinsi nilivyokuwa naye jana yake ilionesha tabia ile ni mtindo wake kila alipokuja Dar na hakupata mwanamke anayejua mapenzi kama mwanaye aliyefanya naye mapenzi bila kujua.
Moyo ulinituma lazima nimpigie simu baba na kumueleza kitendo chake cha kunifukuza na ushahidi wa kutembea na mwanaye kwenye gari lake. Nilijua atashtuka lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kuusema ukweli.
Kutokana na kichwa kuchanganyikiwa nilikwenda kwenye friji na kuchukua pombe kali na kunywa kwa fujo kisha nilijilaza kwenye kochi kwa vile niliamini siku ile ilikuwa ni nuksi kwangu.
***
Nilishtuka saa moja usiku, njaa ikiniuma kama kidonda, nilikwenda kwenye bar ya jirani na kuchukua mchemsho, kisha nilirudi ndani na kuushambulia wote kutokana na njaa ya tokea asubuhi.
Baada kushiba nilikwenda kuoga kisha nilijilaza kwenye kochi na kuwasha tivii kuangalia vipindi huku nikichukua simu yangu niliyokuwa nimeiacha juu ya kochi.
Nilikuta missed calls zaidi ya ishirini na SMS zaidi ya tano, zote zikuwa za baba.
Nilifungua upande wa ujumbe mfupi na kukutana na ujumbe wa lawama wa kwanza ulisema:
Bebi mbona kimya, kwa nini hupokei simu?
Wa pili ulisema: Vipi, kuna tatizo?
Wa tatu: Nijulishe basi mpenzi ili nijue umepatwa na nini?
Nilipotaka kuufungua wa nne simu iliingia nilipoangalia kwenye kioo alikuwa baba Mzee Hans Mouses. Nilijiuliza nikiipokea nitamjibu nini.
Lakini niliamini lazima nimpe makavu live kisha sionani naye tena. Niliamini ukweli nitakaompa ataondoka akijua kabisa kitendo alichonifanyia cha kunifukuza kama mbwa ni cha kinyama na matokeo yake tukafanya mapenzi bila kujuana.
Wakati nikiwaza yale simu ilikatika, niliichukua na kuitazama huku nikiwa na mambo mawili nimpigie au niache. Kabla sijapata jibu simu iliita tena. Nilibofya kwenye kitufe cha kupokelea na kuweka simu sikioni.
“Haloo.”
“Haloo, bebi umefanya nini? Yaani hapa nimeshindwa kuondoka kwa ajili yako umepatwa na nini mpenzi?” baba aliuliza kwa shauku ya kujua.
“Kuna tatizo,” nilimjibu.
“Tatizo gani?”
“Kuhusu wewe.”
“Mimi?” alionesha kushtuka.
“Ndiyo.”
“Tatizo gani?”
“Samahani wewe ni kweli unaitwa Mzee Hans Mouses?”
“Bebi swali gani hilo ikiwa business card nilikupa, kuna tatizo?”
“Naomba ujibu swali langu kama lilivyokuja.”
“Ndiyo.”
“Unakaa Arusha?”
“Ndiyo bebi, mbona unaniuliza hivyo?”
“Utajua tu, Moureen unamjua?”
“Moureen gani?”
“Moureen Hans Mouses.”
“Si..si..simjui,” alipata kigugumizi kidogo.
“Mbona kama unasita?” nilimuuliza.
“Hapana nilijitahidi kumkumbuka lakini kumbukumbu haiji.”
“Mouses Hans Mouses naye humfahamu?”
“Huyo namfahamu.”
“Unamfahamu kivipi?”
“Mwanangu wa kwanza.”
“Yupo Marekani?”
“Ndiyo, umejuaje?”
“Si kujuaje bali kukushangaa kumjua mkubwa mdogo usimjue.”
“Ooh! Kumbe Moureen aliyekuwa binti yangu?”
“Ndiyo.”
“Namfahamu, kafanya nini?”
“Kwa sasa yupo wapi?”
“Sijui.”
“Kwa nini ujue mkubwa tena mtoto wa kiume usijue mdogo ambaye ni mwanamke anayetakiwa kulindwa.”
“Alifanya upuuzi wake nikamfukuza.”
“Akirudi leo kukuomba msamaha utamsamehe?”
“Kama amekutuma mwambie sitaki kuona hata kivuli chake.”
“Ukimuona utamkumbuka?”
“Sina shida ya kuonana naye.”
“Sasa naomba unisikilize vizuri, nina imani simu yako imejaa salio hivyo unisikilize kwa kituo ili mwisho tujue tutafanya nini?”
“Hakuna tatizo.”
Nilianza kumpa historia yangu yote tangu aliponifukuza mpaka siku nilipofanya naye mapenzi bila kujua na kushtuka baada ya kuisoma business card yake aliyonipa usiku.
Niliendelea kumueleza aliponiuliza aliponikuta mapokezi na kumkatalia huku wasiwasi wangu juu ya kutembea na mzazi wangu ukijidhihili.
“Hata siamini siwezi kutembea na mwanangu ,” baba aling’aka.
“Ndiyo umeisha tembea naye, najua ningekuja chumbani kwako ungeweza kupata presha bure na kuonekana nimeua.”
“Hapana siwezi kutembea na mwanangu.”
“Ndo umetembea naye kazi yangu ya kuuza utamu wa mwili kipi unaona ajabu?”
“Mungu wangu, basi naomba tuonane.”
“Ili?”
“Sitaki jambo hili lifike mbali.”
“Mbali wapi?”
“Jamii ikijua nitaonekana sina maana.”
“Umesema hutaki kuona hata kivuli changu, tuonane ili iweje?”
“Kwa kilichotokea lazima tuonane, tujue tufanye nini kuiziba siri hii ya aibu.”
“Katu sitaonana na wewe mpaka nakufa.”
“Moureen najua umekasirika mama, naomba tuonane nipo tayari urudi nyumbani na kukusamehe.”

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 15
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
“Umesema hutaki kuona hata kivuli changu, tuonane ili iweje?”
“Kwa kilichotokea lazima tuonane, tujue tufanye nini kuiziba siri hii ya aibu.”
“Katu sitaonana na wewe mpaka nakufa.”
“Moureen najua umekasirika mama, naomba tuonane nipo tayari urudi nyumbani na kukusamehe.”
SASA ENDELEA...

“Sasa hivi na maisha yangu na familia yangu, sihitaji msaada wa mtu.”
“Nakuahidi kukupatia kiasi chochote ili siri isimfikie mama yako.”
“Nimwambie ili iweje, nilitaka kukueleza unyama ulionifanyia matokeo yake Mungu amekulani na kujikuta ukifanya uchafu na binti yako wa kumzaa.”
“Nisamehe mwanangu mbona najuta.”
“Nina imani umelewa, kwa hiyo naomba kuanzia leo usinipigie wala usinijue, ukaribu wetu uliisha toka uliponifukuza kwako kama mbwa.”
“Hapana tunaweza kukaa tukayamaliza.”
“Na nani, kwanza sasa hivi si mtoto bali mwanamke wako wa kujipozea ukiwa nje ya Dar najua unataka kuniulia mama yangu kwa kulitafuta gonjwa.”
“Usifike huko mwanangu.”
“Nina imani nimeeleweka, naomba tuishie hapa ukija nitakuhudumia kama mteja na si baba yangu.”
“Nakuahidi kuanzia leo sitatoka nje ya ndoa yangu nimekoma.”
“Hayanihusu.”
Sikutaka mazungumzo mengi nilikata simu na kuizima kabisa kisha nilikwenda kwenye friji na kuchukua pombe kali na kunywa mpaka nikapoteza kumbukumbu.
***
Baada ya tukio lile la aibu, niliamua kupumzika kazi ile kwa muda na kuendelea na shughuli zangu. Lakini siku zote nilizoamua kupumzika nyumbani sikujisikia raha kabisa nilikuwa kama mvuta sigara. Nilikuta nikipata hamu za kurudi tena kijiweni hata nimpate mwanaume wa kumpa bure ili tu nijisikie raha.
Niliamua kutoka siku mojamoja kwa hamu, sikuwa nikitoka kwa shida. Pamoja na kutoka kwa hamu sikutaka nitoke kapa bali nipate hata mtu mmoja ambaye angekidhi haja zangu na kufanya siku yangu iishe vizuri.
Siku moja nikiwa kijiweni siku ambayo ilikuwa kigumu, hakuna aliyepata mpaka tukajiuliza labda serikali imepiga marufuku.
Majira ya saa sita na nusu iliingia, ngoma ilikuwa nzito na kibaridi kilikuwa kikali kilichotuingia mpaka kwenye mifupa. Tukiwa tunapanga jinsi ya kurudi nyumbani, gari aina ya Toyota Land Cruser lilisimama pembeni yetu na kushushwa kioo na sauti ilitoka ndani.
"Hei, njoo mara moja."
"Nani, mimi?" tuliuliza kwa pamoja kila mmoja alijishika kifuani kwake.
"Wewe."
"Nani?" tuliuliza kwa pamoja.
"Wewe mwenye gauni jekundu," hakuwa mwingine ila nilikuwa mimi.
Nilichepua mwendo na kuingia kwenye gari kwani mlango tayari ulikuwa umefunguliwa. Baada ya kuingia alitaka kuondoa gari nilimuuliza.
“Mbona unaondoka bila kuelewana?”
"Unataka kiasi gani mrembo?"
"Unataka huduma gani?" nilimuuliza.
"Nataka unitoe chozi lisilo na kilio."
"Elfu 30," nilipunguza ili nipate cha kulalia.
"Punguza nyingi."
"Tena nimekupunguzia hata sijui una shetani gani, hebu angalia mtu kama mimi utanipa kiasi gani?"
Nilisema kwa sauti ya kubana huku nikinyanyua gauni langu fupi na kuuweka mwili wangu nje, kufanya vile lilikuwa pigo mujarabu lililomfanya mzee wa watu mimacho imtoke na kumeza mate ya uchu.
Baada ya kukubaliana, alitoa elfu thelathini keshi na kulisogeza gari sehemu nzuri. Mtoto wa kike niliteremsha suruali nusu mlingoti na kumpa huduma sitahiki iliyomfanya mzee wa watu atatalike juu ya kiti kama kakalia siafu. Baada ya kumliza chozi lisilo na msiba, alichanganyikiwa na kuniuliza:
"Sasa mrembo una kondom ili angalau unipige funda moja ya maji ya dafu, itakuwa kiasi gani?"
Kweli samaki alikuwa kameza chambo na ndoana, mzee alimeza vyote kwa mpigo na kumshika tumboni, Baada ya kilio kisicho na msiba na kuchanganyikiwa na umbile langu. akabadili anataka funda moja ya maji ya dafu. Sikutaka kumlazia damu niliongeza bei.
"Utaongeza kama ile."
"Okay, nipe huduma ili niwahi kulala."
"Basi ongeza kiyoyozi nikupe raha," nilimueleza huku nikimkata jicho la kuumaliza, kwa kazi ile nilikuwa changudoa wa kimataifa.
Aliongeza kiyoyozi na kufanya ubaridi ndani ya gari kuongezeka, mzee wa watu baada ya kuchimba udongo muhogo ilionekana na kukaa mkao wa ‘mimi tayari kazi kwako.’
Kama ilivyokuwa kawaida yangu, nilitaka kumliza mzee mzima ili aelewe kote alipopita alikuwa amekosea. Nilianza kuwajibika mtoto wa kike, mpaka tunapumzika mzee wa watu alikuwa hoi, nimuona akiniangalia kama kaniona nina tofauti na wengine aliowahi kuwaona.
“Mmh! Mrembo unajua.”
“Hujawahi nini kukutana na machejo adimu?”
"Sijawahi, mrembo laki inakutosha?" mzee wa watu alipagawa na kuropoka.
"Mmh ongeza kidogo," japo tulikuwa tumekubaliana aongeze elfu 30 lakini huduma niliyompa nilijua atajinyonga mwenyewe nami nilijifanya haitoshi.
"Basi nitakupa laki na nusu, kesho nitakata kitu kamili nakuomba usiende na mtu yoyote unisubiri sawa mrembo?" mzee alichanganyikiwa.
Alisema huku akinichezea mashavu yangu laini na kunipa laki na nusu kisha aliniongezea elfu 20 za nauli ya kurudia nyumbani.
"Mrembo usisahau basi inaonekana u mtaalamu wa kutikisa minazi na kufanya madafu kuanguka na kupasukia kichwa bila maumivu na kukufanya usikie utamu usio kikomo."
"Wewe tu, hapa ukigusa hutoki yaani gusa unite."
Niliangana naye kwa kukubaliana tukutane kesho pale pale, aliponikuta majira ya saa nne usiku.
Nilitereka kwenye gari na kuwafuata wenzangu ambao walikuwa wamepigwa baridi ya sheria yake. Kwa vile walikuwa wameliwa na mbu bure niliwapa elfu arobaini wagawane ili wapate nauli ya kurudi nyumbani. Nilikodi teksi na kurudi nyumbani.
Niliamini mwenye nazo ziku zote anaongezewa, wenzangu waliokwenda kwa njaa alitoka kapa tofauti na mimi niliyekwenda kwa hobi zangu nilipata tena fedha ya kutembea na wanaume zaidi ya watano lakini niliipata kwa muda mfupi.
***
Siku ya pili ilikuwa lazima nipumzike, lakini nilikuwa na mawazo mengi juu ya mwaliko wa babu wa kwenda kuonana naye. Niliamini ile ni kazi nyepesi yenye malipo mazuri tena ya mteja mmoja maalumu. Niliamua niende nikaonene naye. Kwa vile tulikubaliana tukutane saa nne usiku nilitoka nyumbani saa tatu usiku na kukodi teksi mpaka eneo la tukio.
Nilifika eneo la kazi na kukuta shoga zangu wakiwa katika hinyahinya ya kukimbizana na wateja. Waliponiona alinishangaa.
“Shoga za jana zilikuwa nyingi nini! Zikakufanya usahau shambani?’
“Walaa nina oda special.”
“Wewee!” walishtuka wote.
Kabla sijajibu kitu gari la mzee wangu lilisimama mbele yetu na kufanya shoga zangu walikimbilie. Sikusumbuka naona nilisogea mlangoni na kuwaeleza wenzangu:
“Jamani vitu vya watu hivi.”
Nilifungua mlango na kuingia ndani ya gari, baada ya kufunga babu aliondoa gari. Nilishangaa gari kuondoa bila makubaliano . Gari lilikata mitaa na kuliona gari likiendelea Mikocheni. Ile ilinitisha na kujiuliza babu yule ananipeleka wapi.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 16
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Kabla sijajibu kitu gari la mzee wangu lilisimama mbele yetu na kufanya shoga zangu walikimbilie. Sikusumbuka naona nilisogea mlangoni na kuwaeleza wenzangu:
“Jamani vitu vya watu hivi.”
Nilifungua mlango na kuingia ndani ya gari, baada ya kufunga babu aliondoa gari. Nilishangaa gari kuondoa bila makubaliano . Gari lilikata mitaa na kuliona gari likiendelea Mikocheni. Ile ilinitisha na kujiuliza babu yule ananipeleka wapi.
SASA ENDELEA...

Wazo langu la haraka lilikuwa labda ananipeleka guest ili nikampe huduma kutokana na makubaliano ya siku ya jana. Sikutaka kumsemesha lolote zaidi ya kusubiri kitakacho tokea kwa kuamini hata bila mapatano nilijua nitapata malipo manono. Baada ya mwendo wa robo saa gari lilisimama mbele ya geti la rangi nyekundu.
Baada ya kupiga hodi geti lilifunguliwa na gari liliingia ndani kwenye jumba moja la kifahari.
Mzee Yule alilisimamisha gari na kuteremka kisha alizunguka upande wangu na kunifungulia mlango kama Muheshimiwa.
"Mjukuu karibu."
"Asante babu."
Niliteremka kwenye gari na kuongozana naye moja kwa moja ndani ya nyumba ambako nililakiwa na sebule ya nguvu iliyokuwa na kila kitu. Japo kwa upande wangu sikuwa mgeni wa sehemu kama zile ilikuwa kitu cha kawaida kwangu.
Kilichonishangaza sehemu ile kuwa tofauti na hoteli nilizozizoea ilikuwa kama nyumbani kwa mtu.
Baada ya kuingia sikutaka kukaa mapema kwa vile sikujua pale ni wapi, Mzee aliponiona nimesimama bila kukaa aliniuliza.
"Vipi mjukuu mbona hukai?"
"Kwanza hapa wapi?" nilimuuliza sikutaka kukaa kichwakichwa, ,siyo unaingia nyumba ya mtu hujui anakaa na nani unajiweka kama kwako utajikuta unakobolewa na maji ya moto cha mtu mavi.
"Aah mjukuu hapa ni kwangu."
"Na mkeo yupo wapi?"
"Ningekuwa naye ningekuleta hapa?"
"Ni mara ngapi nimeona wanaume wanawapeleka mahawala wao majumbani kwao na kumteremsha mkewe kitandani?"
"Siyo mimi, sina mke."
"Muongo babu! Mtu mzima kama wewe tena mwenye pesa ukose mke?"
"Ni kweli nilikuwa na mke ambaye alifariki miaka mitano iliyopita."
"Nini kilichomuua?"
"Ajali ya gari aligongwa akiendesha."
"Ooh! Pole sana, kwa nini muda huo hujaoa?"
"Nimejitahidi kutafuta mwanamke wa mfano wake wengi wamekuwa wana tamaa ya mali yangu si mapenzi ya kweli."
"Na wote uliwaleta kwako?"
"Hapana wewe ni wa kwanza."
"Kwa nini umenileta mimi?"
"Una tofauti kubwa na wanawake wengi una tabia ya tafauti kubwa, ni msikivu mwenye huruma mwenye uelewa."
"Kwa hiyo umenileta hapa ili iweje?"
"Kukuleta hapa ni heshima kubwa kwako vile vile ni kulilinda penzi lako ambalo kwa kipindi hiki kwangu ni muhimu sana."
"Kwa hiyo unataka kunioa?"
"Ndiyo maana yake."
Mmh! Kauli ile ilinifanya nijiulize nini kinachofuata kwani siku zote upatapo neema lazima kuna balaa linakuja mbele.

***********
Kama kawaida yangu nilijikuta nikiangukia mikononi mwa mikono ya mzee Kupe. Kuanzia hapo ile kazi ya kulinda usiku niliachana nayo na kuwa mke mtarajiwa wa mzee Kupe aliyekuwa na ana kila kitu kwa maisha ya mwanadamu.
Kutokana na utajiri ya yule mzee na mihangaiko yangu ya kuhatarisha maisha yangu katika biashara ya ukahaba nilikubali kuolewa. Mzee Kupe hakutaka makubwa alinioa baada ya miezi miwili na kuwa mkewe wa halali kwa sherehe uliyohudhuliwa na watu wasiopungua hamsini.
Niliyaanza maisha kama malkia kwa kupata kila kitu nilichokikosa katika maisha yangu. Pamoja na pesa na utajiri wa mzee Kupe niligundua alikuwa na mapungufu makubwa kitandani. Alikuwa mtu wa kunywa dafu moja, zaidi ya hapo hulala kama gogo hata jogoo huwa amelala wakati ndiyo kwanza kumekucha.
Nilijikuta kila siku kila mnilipokutana na mzee Kupe ilikuwa sana na kuchambia pilipili kutokana kuacha njiani kila siku. Mtoto wa kike nilikuwa napata taabu kwa kukasa usingizi kufikia hatua ya kujikanda na maji ya moto kama nimetoka kujifungua.
Mzee Kupe alijitahidi kunipa kila nilichokitaka lakini kwenye majambozi alikuwa mchovu wa kutupa. Nilijikuta nikipata taabu kila siku kwa kuachwa njiani wakati mwenzie mambo ndiyo kwanza yalikuwa yakianza.
Mateso yalipozidi nilijikuta nikipata wazo la kutafuta mtu wa nje kunipunguzia mateso. Kutokana na kuwa na uwezo niliona ni upumbavu kuendelea kuumia kukosa chakula cha nafsi.
Niliamini kupitia pesa nilizopewa na mume wangu ningepata kijana mmoja shababi ambaye angenikamua vilivyo na kumlipa pesa zake. Kama kawaida nikiwa kwenye gari langu la kifahari nilisimamisha kwenye kijiwe ambacho vijana wengi hukaa kwa ajili ya kupiga porojo bila kazi yoyote. Nilipofika pale kijiweni nilisimamisha gari na klumtafuta kijana aliyeonekana mtanashati.
Baada ya kuridhika na kijana mmoja niliteremsha kioo na kupiga honi, waliopogeuka niliita wote waliuliza
"Nani?"
"Huyo mwenye mkanda nje," nilimchagua kijana mmoja.
Kijana mmoja alikuja hadi kwenye gari alipofika nilimfungulia mlango. Naye bila ubishi aliingia kwenye gari.
"Naomba ufunge mlango," nilimwambia.
Yule kijana alifanya kama nilivyo muelekeza nami nilikanyaga mafuta.
"Samahani unafanya kazi gani?"
"Sifanyi kazi yoyote" alinijibu akinitazama usoni.
"Mbona umependeza hela unapata wapi?"
"Napewa na wazazi."
"Sasa sikiliza kuna kazi moja nataka kukupa ya muda mfupi ukifanya vizuri nitakupa pesa nyingi ambayo itakufanya uachane na kuwategemea wazazi wako."
"Ni kazi gani?"
"Utaiona si tupo pamoja."
Wakati huo nilikuwa napiga honi kwenye geti la nyumbani kwangu. Baada ya kufunguliwa na mlinzi Mmasai, niliingiza gari mpaka sehemu ya kuegeshea magari niliteremka na yule kijana ambaye alionekana hajiamini.
"Ondoa hofu jisikie kama upo nyumbani" nilimuondoa hofu
"Hakuna tatizo sister."
Nilimkaribisha sebuleni na kumuuliza kinywaji gani anatumia, sikuwa na wasi kutokana na mzee wangu kunijulisha atakuwa na kikao kitakachomfanya arudi usiku. Hakuwa mtu muongo wa kusema uongo akisema atarudi saa fulani basi muda ule ule hurudia au kukupigia simu kukujulisha dharula yoyote.
Siku zote si wanaume ambao hutege tetele kwa kumwaga mtama mwingi ili kunasa kwa urahisi. Akiwa anapata kinywaji nilimuuliza:
"Hivi katika maisha yako ya kila siku lini ulipata pesa nyingi?"
"Mmh hata sikumbuki."
"Kiasi gani?"
"Mmh kama elfu 50."
"Kwa kazi gani?"
"Kwa kazi za kupewa na dingi."
"Sasa mimi leo nina kazi ndogo ambayo naimani utaifanya kwa masaa mawili hata moja kama utaifanya vizuri na malipo yake ni laki moja."
"Ha! kwa kazi gani hiyo?" alishtuka.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 17
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500
...ILIPOISHIA:
Siku zote si wanaume ambao hutege tetele kwa kumwaga mtama mwingi ili kunasa kwa urahisi. Akiwa anapata kinywaji nilimuuliza:
"Hivi katika maisha yako ya kila siku lini ulipata pesa nyingi?"
"Mmh hata sikumbuki."
"Kiasi gani?"
"Mmh kama elfu 50."
"Kwa kazi gani?"
"Kwa kazi za kupewa na dingi."
"Sasa mimi leo nina kazi ndogo ambayo naimani utaifanya kwa masaa mawili hata moja kama utaifanya vizuri na malipo yake ni laki moja."
"Ha! kwa kazi gani hiyo?" alishtuka.
SASA ENDELEA...
"Naomba unifuate."
Niliongozana naye hadi chumba cha wageni, baada ya kuingia chumbani nilivua nguo zote na kubakia mtupu mbele ya yule kijana ambaye alionekana kunishangaa. Mkononi nilikuwa nimeshikilia laki moja taslimu na kumkabidhi.
Akiwa bado ameshangaa nilianza kumvua nguo, niliyasikia mapigo ya moyo ya yule kijana yakifuatiwa na jasho jingi. Kutokana na kuwa na uzoefu nilijua kijana alipoteza uwezo wa kujiamini.
Huenda ulitokana na kuamini mwanamke mzuri kama mimi ni chakula cha watu wenye pesa na kuisahau mwanamke yoyote ni nyama kwa mwanaume mwenye kisu kikali. Japokuwa kisu cha mume wangu kilikuwa butu kama utachinja mnyama basi lazima utakula kibudu.
Kwa sauti iliyohitaji huduma ya haraka ambayo ingeokoa maisha yangu nilisema
"Naomba unikate kiu nitakuongezea zaidi ya hizi."
Mtoto wa kiume hakuwa na muda wa maandalizi aliudandia mnazi kama mwizi aliyevamia shamba la mtu kuogopa kukamatwa.
Alianza kuutikisa mnazi ambao haukuchelewa kuangusha dafu lililoniangukia kichwani na kunifanya niamini nilichokitafuta ndicho chenyewe. Nami kama kawaida sikuwa nyuma nilikwenda naye sambamba.
******
Kila dakika zilivyozidi kwenda nilitamani kulia kwa raha kutokana na yule kijana kuonekana kunimudu vilivyo. Maruhani yangu yalianza kupanda na kutakiwa yateremshwe, lakini ajabu kijana wa watu ndio kwanza alianza kupunguza kasi na kunifanya nifoke kwa sauti
"Pumbavu utaniuzi jitahidi unifikishe angalau safari moja nyingine."
"Sister nimechoka," alisema kwa sauti ya mtu aliyebeba mzigo mzito.
"Kwa hiyo unataka kuniambia nini?" nilimuuliza kwa hasira.
"Kwa leo inatosha."
"Nooo! Haiwezekana kama ulijua huwezi kuniukuna kwa nini umenichambia upupu, sikwezi kukuruhusu uondoke lazima unikune," nilisema kwa hasira.
"Labda kesho, hapa nilipo siwezi kuendelea zaidi ya hapa hata leo nimejitahidi, mimi mwisho madafu matatu lakini leo nimeangusha madafu matano."
"Madafu gani hayo si vidaka dafu gani halina maji, ili tuelewane naomba unisindikize nami nimwage trip moja ya mchanga."
"Siwezi utanisamehe kama hela yako baki nayo."
Mmh! mtoto wa kike mimi ndio naanza kuchanganya mwenzangu kamaliza na kuendelea hawezi tena. Nilijitahidi kumbembeleza huku nikimlilia. Najua mtacheka au kuniona mtu wa ajabu.
Nilimpigia magoti abadili msimamo wake na kumuahidi kumuongezea laki nyingine
"Sio kwamba sitaki siwezi tena kuendelea naomba niondoke."
Nilijitahidi kumrudisha kwenye hali ya kawaida kwa kutumia ujanja wangu wote na ujuzi wangu kwa kuweza kumgusa sehemu zenye msisimko. Mtoto wa kike nilihaha huku jasho likinitoka kama maji nikijitahidi kumtoa nyoka pangoni alipogoma kutoka.
Simu yangu ya mkononi ililia niliichukua nikiwa sina nguo yoyote mwili labda ingeamsha hisia za kuutamani mnazi wangu ambao ulikuwa na kila sifa ya kupandwa na mkwezi mzuri.
Nilipoangalia namba zilikuwa za mume wangu, moyo ulinishtuka kidogo. Nilitoa hofu na kujirudisha kwenye hali ya kawaida kabla ya kuipokea
"Hallo honey"
"Ooh! My Sweet vipi upo nyumbani?"
"Nisiwepo nyumbani niende wapi mpenzi wangu, upo wapi?"
"Sipo mbali na nyumbani nipo hapa jirani kwenye super market, nikuletee nini mpenzi wangu."
Kauli ile nusra simu iniponyoke kwa mshtuko na kujikuta nikiuliza tena ili nimuelewe vizuri."
"Nipo hapa jirani na nyumbani au nikufuate uje uchague ukitakacho?"
"Mmh! Hebu subiri," nilikata simu na kumuomba yule kijana avae haraka na kutoka.
Baada ya kuvaa nilimtoa hadi mlangoni na kumuomba atoke, naye alifanya vile na mimi kukimbilia bafuni kuoga. Nilioga haraka na kurudi hadi ndani ambako nilivaa gauni langu jepesi la usiku na kutoka kuelekea super market.
Nilimkuta akiwa amekasilika akijitayalisha kutoka ndani ya super market. Aliponiona aliniuliza kwa sauti ya juu kidogo.
"Mpenzi muda wote ulikuwa wapi au haukuwepo nyumbani?"
"Mmh! Mpenzi muda unanipigia nilikuwa nimelala, hivyo nisingeweza kuja bila kujimwagia maji ili kuondoa uchovu."
"Mbona hukunijulisha?"
"Nilifanya vile ili kukuwahi nisamehe mpenzi wangu kama nimekuudhi," nilijifanya kuomba msamaha.
Tuliyamaliza na kununua vya kununua na kurudi ndani mwetu, mtoto wa kike japokuwa nilijua safari nusu niliyokwenda haitafika kamili zaidi ya kuniongezea robo.
Usiku mambo yalikuwa yale yale na kunifanya nizidi kuwa kwenye wakati mgumu na kujuta kuolewa na mzee kama yule.
****

Siku ya pili kama kawaida yangu baada ya mume wangu kwenda kwenye mihahaiko yake nilitinga tena kijiweni kumfuata kijana mwingine na kuondoka naye hadi kwangu.
Mmh! Si ya kusema yaani nilijuta kumchukua ilikuwa sawa na kunichambia pilipili. Sijui niseme nini ili mnielewe, yaani mwenzie nikiwa na kimuhemuhe cha kupandishwa juu ya mnazi.
Sikuamini yaani wakati ndio najiandaa kupandisha mashetani ili ayapunge vizuri, mwenzangu ndio kwanza alikuwa akimwaga mzigo na kutulia.
Kibaya zaidi baada ya kumwaga mzigo mnazi ulilala dolo, mwanzo nilidhania labda ni kupasha mwili nguvu kumbe mwenzangu ndio kamaliza kila kitu.
Kila niliponyanyua mdomo na kifaru ili kinipige lakini wapi mkonga ulikuwa umelala chini na haukuwa na dalili zozote za kunyanyuka.
Mtoto wa kike sikukubali kirahisi kupakwa shombo nilimchezea niwezavyo kwa mikono na mdomo wapi niliishia kunyonya mafuta lakini gari liligoma kuwaka. Nilihangaika kwa kila mtindo nilijua hata wa kugusanisha positivu na negativu labda umeme ungeshtua lakini wapi.
Wakati huo nilikuwa kwenye hali mbaya kwani maji yalikuwa yamejaa kisimani mpaka yanamwagika na kuweka michirizi kwenye mapaja. Nilijikuta nikilia peke yangu huku nimekaa pembeni ya yule kijana ambaye naye aliangalia chini kwa aibu.
Baada ya kuhangaika bila mafanikio kumuamsha jogoo aliyegoma kuwika kwa zaidi ya masaa matatu. Nilikata tamaa na kukubali matokeo kwa kujiona mwanamke nimeingia choo cha juu cha kiume nitajisaidia vipi?
Nilimuamuru avae na kuondoka kwa vile hakuwa na faida kama mti wa mpapai dume ambao hauzai matunda haufai kwa kuni haufai hata kwa kivuli.
**********
Nilijikuta nikijiingiza kwenye tabia ya kuwa mama huruma kwa kutafuta vijana mtaani kugawa uroga kwa kuwapa pesa ili kuhakikisha nakidhi haja zangu. Lakini nilikuwa sawa na kubeba maji kwenye gunia, kila niliyemgusa alishindwa kuniridhisha kikamilifu.
Lakini kidogo njia ile ilinisaidia kupunguza maumivu ya wadudu wadogo wadogo. Najua mwenzangu kila ninachokisema unakunja uso na kunionea huruma eti mwanamke kama mimi mwenye uzuri wa kusifika pia kazi naijua ya kumtoa kamasi mwanaume.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 18
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Nilijikuta nikijiingiza kwenye tabia ya kuwa mama huruma kwa kutafuta vijana mtaani kugawa uroga kwa kuwapa pesa ili kuhakikisha nakidhi haja zangu. Lakini nilikuwa sawa na kubeba maji kwenye gunia, kila niliyemgusa alishindwa kuniridhisha kikamilifu.
Lakini kidogo njia ile ilinisaidia kupunguza maumivu ya wadudu wadogo wadogo. Najua mwenzangu kila ninachokisema unakunja uso na kunionea huruma eti mwanamke kama mimi mwenye uzuri wa kusifika pia kazi naijua ya kumtoa kamasi mwanaume.
SASA ENDELEA...

Pia nina mwanaume mwenye uwezo wa pesa ambazo ninaweza kuzila mpaka nakufa na wajukuu zangu wasingeweza kuzimaliza. Lakini lazima niwe mkweli toka moyoni mwangu kuwa nimekuwa mtumwa wa ngono kutokana na kuifanya biashara ya ukahaba kwa muda mrefu.
Lakini kibaya zaidi kilichonifanya niwe mtumwa wa ngono ilitokana na kutumia wa dawa za kuongeza nguvu kitu kilichonipelekea kutaka kukutana na mwanaume aliyeshiba na si mzee kama mume wangu.
Ni kweli mume wangu ana uwezo wa kipesa lakini alikuwa hana kitu muhimu ambacho ndiyo ugonjwa wangu. Mzee Kupe alikuwa kama bata akigusa hanyanyuki tena na kunipa mateso kila nilipokutana naye na kunilazimisha nijikande na maji ya moto kama nimejifungua.
Kwa upande wangu uamuzi wangu niliuona una maana kubwa kwangu kwani kama shamba lilimshinda babu Kupe wapo vijana shababi wenye nguvu za kuweza kumsaidia kupitia pesa zake mwenyewe.
Kwa maisha niliyo yazoea hata mwanaume asiwe na kitu lakini akinishika nikashikika moyo wangu unajaa furaha na kujiona nina raha kuliko kiumbe chochote nikikohoa naitikiwa.
Niende wapi zaidi ya kumlinda mume wangu kwa kumpa mahaba motomoto ambayo yatamchanganya akili kwa kujituma muda wote wa mchezo huku nikimpa maneno matamu ya kumtoa nyoka pangoni.
Nilijiona sawa na gari zuri lililokosa dereva mwenye kujua kulikimbiza bila huruma wakati barabara inaruhusu. Sikuwa na njia nyingine ya kutoka nje ya ndoa ili kukidhi haja zangu.
Na haya nisemayo ni yangu peke yangu unisifuate kwani ndoa ni muhimu ndugu yangu.
****
Siku moja mume wangu alirudi nyumbani akionyesha kuna kitu kinamsumbua akilini mwake, lakini kila nilipomuuliza alisema yupo kwenye hali ya kawaida japokuwa niliamini hakuwa kwenye hali yake ya kawaida.
Sikutaka kujisumbua kwa kuuliza kitu kisicho nihusu kwa kuamini huenda ni kwenye shughuli zake. Japokuwa nilitakiwa mkewe kujua na kumliwaza, lakini kwa vile nilijitahidi kumuuliza kwa kumbembeleza lakini alikataa ningemfanyaje nami nilitulia tuli kwa kujua nitampata sehemu gani.
Nilipanga wakati wa kuukwea mnazi wangu akifika karibia na madafu hapo ndipo nitakapohoji kitu gani kinachomsumbua lazima asema kuanguka juu ya mnazi mchezo. Baada ya chakula ambacho vile vile hakula vizuri.
Wasi wasi wangu huenda anaumwa vilevile nilipomuuliza alisema haumwi. Nilijiuliza mume wangu ana tatizo gani ambalo lilianza kunitia wasiwasi na kunikosesha raha.
Nilianza kujiliza nami kususa kula na kuanza kulia na kukimbilia chumbani kitu kilichomfanya mume wangu anifuate na kuniuliza:
"Sweet una lina nini?"
Sikumjibu nilijilaza kitandani huku nikilia kikweli kitu kilichomshtua mume wangu.
"Mpenzi unalia nini?" aliniuliza huku akinipapasa mgongoni.
"Moureen mpenzi hebu nyamaza mpenzi uniambie nini kinakuliza?"
"Hunipendi bora niondoke," mtoto wa kike nilitishia.
"Mbona umefikia mbali mpenzi wangu kwani tatizo nini?"
"Nikuulize wewe kama unaona sina umuhimu kwako kwa nini kunipotezea muda."
"Unajua mpenzi kuna maneno juu yako yameniumiza moyo wangu nisiamini kama ni kweli," mwanaume alianza kufunguka.
Kauli ile ilimshtua moyo wangu na kujua mtoto wa kike nimeumbuka, lakini sikutaka kujihukumu niligeuka huku macho yakiwa yamejaa machozi na kuuliza.
"Ni habari gani hizo mume wangu?"
"Eti umekuwa jamvi la wageni mama huruma hapa mtaani, Moureen kitu gani ambacho umekosa hapa ndani kufikia hatua ya kunidhalilisha mtu mzima kama mimi mwenye pesa na mwenye heshima kubwa mbele za jamii.
“Siamini kama umekuwa ukiugawa mwili wako kama pipi kwa kweli jambo hilo siwezi kulifumbia macho wala kulivumilia kweli kunguru hafugiki."
Mmh! Kauli ile ilinishtua na kujua nimeula wa chuya kwa uvivu wa kuchangua. Moyo ulinilipuka na kujua kama nitafukuzwa na mzee Kupe nitauelezeaje umma. Hata mashoga zangu ambao kwa namna moja ama nyingine walipata unafuu wa maisha, niliamini kwa kauli ile lazima amefikiria kuniacha.
Leo hii nirudi kijiweni na kuanza tena maisha ya kuwinda kwa kupigwa na baridi na kuliwa na mbu. Niliamini nimeumia lakini sikukubali kufa kikondoo japo moyo ulikuwa umekufa ganzi.
Nilinyanyuka kitandani kama nguruwe aliyekurupushwa shambani na kusimama huku nikimuuliza kwa sauti kavu:
"Mume wangu ni maneno gani ya kuniambia, kama umenichoka we nipe talaka yangu sio kutafuta kisingizio au kwa vile umenikuta nauza mwili. Kwa taarifa yako wewe ndiye mwanaume wa kwanza na nilikwenda kwa shinikizo lakini kazi ile sikuzoea.
“ Hivi huu mwili unauonaje yaani nimepungukiwa nini mpaka nifikie hatua ya kuugawa nje nini nakikosa kwako?" Nilisema vile ili kulinda ndoa yangu lakini kipo nilichokikosa. Pia nilipanda juu ya kitanda nikiwa mtupu na kujizungusha kila kona kuuonyesha mwili wangu kama mlimbwende anajinadi mbele ya majaji.
"Sikiliza Kupe usipoteze muda wako kutunga uongo mwili huu ni ghali tofauti na unavyo fikiria wewe niache tu wala usitafute sababu."
Baada ya kusema yale niliondoka hadi kwenye kabati la nguo na kuanza kukusanya nguo zangu na kuziweka kwenye begi ili niondoke. Mkwala wangu ulisaidia kwa mume wangu kunifuata na kunipigia magoti.
"Moureen mke wangu ni uamuzi gani huo?"
"We si hauna shida na mimi na ulinichukua kimakosa," alizungumza huku nikiendelea kulia.
"Sio mimi mke wangu ni watu ndio wamesema wamekuona ukifanya uchafu huo."
"Kama una waamini endelea nao mimi naondoka, kama ingekuwa kweli kwa nini wasikuite ili unikamate?"
"Lakini mke wangu mimi naamini huo uongo wewe huwezi kufanya kitu kama hicho kwani umepungukiwa na nini,” mzee Kupe aliniomba msamaha.
"Ndio unajua sasa, nashukuru wacha tu niondoke ili wapate nafasi labda wanaona nafaidi," mtoto wa kike kesi niliigeuza mshitaki kuwa mshtakiwa mbona uwanja ulikuwa wangu kwa kudeka nikijua ushindi ni wangu.
Mzee wa watu alimaliza maneno yote kuniahidi vitu vikubwa kuhakikisha siondoki.
“Basi mpenzi nisamehe sema chochote utakacho ili unisamehe.”
Nilijifanya kubadili uamuzi kwa kutaka kujengewa nyumba na kununuliwa gari vitu vilivyotimia ndani ya miezi miwili.
Mzee wa watu fedha kwake haikuwa tatizo ndani ya muda huo nilipata vitu vyote nilivyotaka. Baada ya kuponea kwenye tundu la sindano niliachana na mchezo wangu ule mchafu na kutafuta njia nyingine wa kupunguza shombo nililokuwa napakwa na mzee Kupe.
Wakati nikitafuta njia muafaka niliamua kutulia kwa muda ili kumfanya mume wangu aamini ule ni uongo. Ili kurudisha imani kwangu hata kutembea nilikuwa sitaki zaidi ya kukaa ndani na nilitoka kwa taarifa kitu kilichoongeza mapenzi kwa mume wangu na kuamini yote aliyoambiwa ni uongo.
***
Nakumbuka siku moja kabla ya kuelekea mjini nilipeleka viatu vyangu kwa shoe shine Mlemavu wa miguu aliyekuwa nje ya uzio wa nyumba yetu. Na yule mlemavu ni mimi niliye mkingia kifua baada ya mume wangu kusema kuwa eti ni uchafu kuwepo kwenye ukuta wa uzio wa nyumba yetu.
Lakini nilimweleza mume wangu na kunielewa na kumuacha afanye kazi pale nje ya uzio wa nyumba yetu. Kwa upande mwingine alinisaidia kunisafishia viatu vyangu ambavyo awali nilikuwa nikienda mjini nilisafishia hukohuko.
Japo kutokana na ukarimu wangu alipenda anisafishie viatu bure lakini nilimkatalia kwa kujua ile ndiyo kazi yake na sisi ndio tunaotakiwa kumsaidia kimaisha. Japokuwa alikuwa akinisafishia viatu kwa shilingi mia tatu mimi nilikuwa nampa kila kiatu elfu moja.
Kwa kweli kwa muda mfupi nilizoeana naye na yeye alipenda kuniita mchumba nami nilimkubalia ili naye asijione kuwa mlemavu wa miguu hana haki ya kupata upendo kwa watu hasa wanawake wazuri kama mimi.
Kutokana na ukaribu na mazoea siku nyingine huacha viatu kila nilitoka mjini na yeye alikuwa akinisafishia kumtuma mfanyakazi anifuatie. Siku hiyo nakumbuka vizuri kabla ya kutoka kwenda mjini nilitoka nje kupeleka viatu vyangu visafishwe na kupigwa dawa.
Nilipokaribia kijiweni kwake hakuniona kutokana na kunipa mgongo, alikuwa akisafisha viatu vya mmoja wa mteja wake. Kwenye benchi kulikuwa na vijana watano wa kijiweni. Mazungumzo yake yalinifanya nisimame nyuma yake bila kuzungumza ili nisimkatishe kwa kujitokeza.
Nilimsikia akiwaambia wateja wake juu ya uwezo wake wa kufanya mapenzi na wanawake.
"Hivi mnajua kwa nini naitwa Side Butamu?"
"Hatujui" mmoja alijibu.
"Maana yake ni jinsi mtoto wa kiume nilivyo mtamu kitu kilichosababisha wake za watu niwaone nuksi."
"Nuksi kivipi."
"Hivi ndugu yangu Side mimi na viguu hivi kama vijiko leo hii lizuke vagi nitaanzaje kukimbia?"
"Acha uongo umeisha onja mke wa mtu?"
"Kaka kila aliyeonja alitangaza kuachana na mume wake na kuomba nimuoe."
Kauli ile iliwafanya wote waliokuwa pale waangue kicheko pamoja na mimi nilicheka kwa kushika mdomo ili sauti isitoke na kukatisha utamu.
"Side utani huo," mmoja wa vijana walisema.
"Kama utani nipe mkeo nimuonje kisha jibu utapata kama hakuomba talaka. Wengine wapenzi tunafanyia kazi sio starehe, sio ukigusa kidogo kama bata hupandi tena.
“Basi nikipanda juu nakuwa mdogo kama kidumu cha lita tano hapo mwanamke atamaliza maneno yote. Wengi hujiuliza nimeungwa kwa viungo gani asali si asali, sukari si sukari. Kibaya zaidi nikiwakoleza huvinyonya viguu vyangu kama nimevipaka sukari."
Kauli ile nilinifanya nicheke kwa kushika mdomo, huku nikiangalia viguu vyake vidogo.
"Side mbona huna mke?" mmoja alimuuliza.
"Toka nifike hapa sitaki wanawake nitakaye muonja lazima atawahadithia wenzake na kuwafanya wanikimbilie kama mzinga wa nyuki. Mi mtamu bwana utafikiri nimetolewa kwenye pipa la asali."
Maneno ya Side yalinifanya nicheke kwa sauti na kumfanya agundue nipo nyuma yake. Alipogeuka aliona aibu na kuniomba msamaha kutokana na kuheshimiana sana.
"Ooh! Mchumba samahani sikukuona, si unajua nipo na wahuni."
"Aah! Side ya kawaida, nifanyie chapuchapu nawahi mjini."
Nilimuachia viatu na kurudi ndani huku nikichekea moyoni kila nilipokumbuka maneno ya Side Butamu kama apendavyo kujiita. Nilijikuta nikijiuliza swali juu ya yale yote aliyokuwa akiyazungumza kama ni kweli au ni porojo.
Nilijikuta nikipata wazo la kutaka kufanya naye mpenzi uhakikiwa wa maneno ya Side Butamu yana ukweli gani. Baada ya kunisafishia viatu vyangu nilielekea mjini huku mawazo makubwa yakitawala kichwani kuhusiana na maneno ya Side Butamu.
Kweli ugonjwa wa ngono ulikuwa ukinisumbua kila nilipokumbuka maneno ya Side Butamu nilihisi kuwa na hamu ya kufanya naye mapenzi na kutaka kuthibitisha kwa vitendo. Nilijikuta nikimtamani Side Butamu kufanya naye mapenzi japo mlemavu.
Akili yangu ilinituma kama kweli asemayo nitayakuta basi nilipanga kuyabadili yaisha yake kwa kumuhamisha mji na kumpangia nje ya mji na kumpatia huduma zote muhimu.
Pia nilipanga kumnunulia gari ya Automatic gear ambalo atalitumia kuijia mjini. Lakini nilijiuliza nitaweza kumuingiza ndani bila mtu yeyote kujua, baada ya kupanga na kuwazua nilipata jibu la kufanya.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Surprise ya Aibu
SEHEMU: 19
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Kweli ugonjwa wa ngono ulikuwa ukinisumbua kila nilipokumbuka maneno ya Side Butamu nilihisi kuwa na hamu ya kufanya naye mapenzi na kutaka kuthibitisha kwa vitendo. Nilijikuta nikimtamani Side Butamu kufanya naye mapenzi japo mlemavu.
Akili yangu ilinituma kama kweli asemayo nitayakuta basi nilipanga kuyabadili yaisha yake kwa kumuhamisha mji na kumpangia nje ya mji na kumpatia huduma zote muhimu.
Pia nilipanga kumnunulia gari ya Automatic gear ambalo atalitumia kuijia mjini. Lakini nilijiuliza nitaweza kumuingiza ndani bila mtu yeyote kujua, baada ya kupanga na kuwazua nilipata jibu la kufanya.
SASA ENDELEA...
****
Siku ya pili mume alinijulisha kuwa mchana anaweza kuchelewa kutokana na kubanwa na mkutano muhimu ofisini. Ilikuwa kawaida yake panapotokea mabadiliko yoyote lazima anijulishe.
Niliamini siku ile ndiyo ya kudhihilisha kauli ya Side Butamu kama ina ukweli. Majira ya saa nne nilitoka hadi nje ya geti na kumkuta Side akisafisha viatu juu ya benchi kulikuwepo mtu mmoja tu.
Side aliponiona alidaka juu juu:
"Ooh! mchumba wangu huyo!"
"Ni mimi mpenzi wangu Side Butamu."
Kauli yangu ilimfanya aone aibu lakini sikutaka kumkosesha raha nilimweleza kilicho nieleka pale.
"Sasa Side nilikuwa naomba ukimaliza kazi hii usipokee kazi ya mtu yeyote njoo ndani kuna kazi kusafisha mikoba yangu."
"Mingapi?"
"Ipo mingi sidhani kama leo utaimaliza naona itakuwa kazi yako ya kutwa nzima," nilitengeneza uongo wa kuingiza ndani bila yeye kujua.
"Poa mchumba nakuja."
Baada ya kukubaliana na Side nilirudi hadi chumbani na kutandika kitanda vizuri kuliko siku zote. Kisha nilikwenda bafuni kuoga ikiwa kuufanyia usafi uwanja utakaotumiwa katika mechi.
Mtoto wa kike nilisimama mbele ya kioo nikiwa mtupu na kuuangalia mwili wangu na kugeuka huku na kule huku nikurusharusha makalio yangu yaliyokuwa laini kama mchicha pori.
Nilijipamba nikapambika na kujipulizia utuli ambao hata mtu angepumua ungemeza uvundo wote. Nilijifunga kanga moja nyepesi bila nguo ndani na kukaa mkao wa kumsubiri huyo Side butamu aliyejisifia mtamu zaidi ya vitamu. Baada ya muda mfanyakazi wangu wa ndani alinifuata chumbani kwangu.
“Dada Mou.”
“Judy vipi?”
“Dada Side amekuja.”
“Mwambie apite ndani.”
Nilisubiri kwa muda bila kumuona kitu kilichonifanya nitoke kumfuata. Nilimkuta bado yupo sebuleni akiwa kwenye zulia.
“Vipi Side?”
“Mchumba niletee hapahapa.”
“Mchumba utaniuzi umesikia nakula watu?”
“Basi hakuna tatizo tangulia nakuja.”
Nilitangulia chumbani, baada ya muda Side aligonga mlango, nilitoka hadi mlangoni na kufungua, kweli alikuwa Side Butamu kama alivyojiita. Mtoto wa kike nilipomuona nilikuwa na shauku kama mwenye kiu aliyeona dimbwi la maji.
Pamoja na kujisifu bado nilikuwa na wasiwasi wa kunikata kiu yangu iliyokuwa ikinitesa kila kukicha.
“Side mpenzi pita ndani.”
“Noma mchumba babu ataniua akinikuta,” Side aliingia wasiwasi.
“Akukute ili iweje?”
“Si unajua mazingira,” Side alijitetea.
“Side hebu ingia ndani umalize kazi uliyoitiwa mara moja uwahi kazi zako, kumbuka nje wateja wanakusubiri,” nilimuhimiza aingie ndani ili anipe alichokinadi mbele za watu kuwa mtamu kama katumbukizwa kwenye pipa la asali.
Side aliingia chumbani kwa woga baada ya kuingia niliufunga mlango kwa komeo. Side kuona vile alishtuka na kuhoji.
“He! Mchumba mbona unanitisha?”
“Acha woga kipi cha ajabu?”
“Nyumbani kwa mtu hapa usinitoe sadaka nikakatwa masikio.”
“Walaa, hofu yako kwani na mimi sijipendi?”
“Mmh! Haya hebu nipe hiyo kazi niifanye maana sehemu hii si salama kabisa hasa mtoto kama wewe umbile na vazi alilovaa ni mtihani mzito kwangu.”
“Ukizidiwa nitakupa wala usihofu, mtoto wa kike nyama isiyo na mfupa kwa mwanaume.”
“Mmh! Mtihani huo, lakini nipe kazi maana nisije fanya kazi isiyo nihusu ukamsahau mzee wako bure.”
Mmh, Side bila kujua alikuwa akiingia kwenye mtego mwenyewe, sikutaka kuipoteza nafasi ile. Khanga moja niliyokuwa nimejifunga niliidondosha makusudi, jicho la Side lilipotua mwilini mwangu alishtuka na kuangalia chini.
Niiokota kanga kwa pozi kujifunga kisha nilimsogelea pale chini alipokuwa amekaa na kukaa pembeni yake.
“Side,” nilimwita kwa sauti ya uchokozi.
“Mmh,” maskini Side aliingiwa na aibu kama mwari.
“Side unajua kazi niliyokuitia?”
“Ya kusafisha mikoba.”
“Hapana, kumbe hukusikia vizuri,” nilifanya kama hakusikia vizuri.
“Mbona nilisikia kusafisha mikoba,” Side alijitetea.
“Kuna kazi nyingine kabisa ukiifanya vizuri nakuhakikishia umasikini utakutoka utasahau kusafisha viatu vya wanaume wenzako.”
“Kazi gani hiyo?” aliuliza macho yamemtoka pima.
“Nataka unipe ulichokinadi kwa wanaume wenzako huko nje.”
“Kipi hicho mchumba?”
“Nataka unipe ule utamu iliouahidi kuwa ukimpata mke wa mtu anachanganyikiwa.”
“Hakuna mchumba nilikuwa nawatania tu.”
“Muongo Side usiniogope.”
“Kweli mchumba zile porojo tu,” kauli ya Side kidogo initoe machozi.
“Side hebu nionee huruma mpaka kukuleta huku kuna kitu nakitaka kwako.”
“Lakini humu ndani noma, mchumba unataka babu aniue.”
“Side babu mwanaume jina hana lolote nakaa naye kwa vile ana pesa lakini nikimpata mtu wa kuzimaliza haja zangu haki ya nani nakununulia nyumba na gari,” mtoto wa kike hamu zilinipanda na kujikuta nikitoa siri ya ndani huku nikitangaza bingo.
“Siwezi kukataa ofa nono kama hiyo, lakini mazingira yenyewe hayaruhusu. Unafikiri mumeo akinifuma ndani kuna kupona kweli?”
“Side mume wangu huwa harudi bila kunijulisha na pia huwa harudi mchana.”
“Tufanye kesho mchumba popote tofauti na hapa,” Side alikuwa na maneno mengi kiasi cha kuanza kunirusha stimu.
“Side nionee huruma mtoto wa mwenzako, siwezi kuvumilia hali ni mbaya nione jinsi ninavyo teseka mpaka kisima kimejaa maji ya kumwaga bondeni. Hata mwili wangu umebadilika rangi na kuwa mwekundu kama nyoka mwenye sumu kali hebu nionee huruma mwana wa mwenzio,” nilijitetea kwa Side baada ya hali kuwa mbaya.
Nilizungumza sauti ambayo hata mlokole asingeweza kuruka, huku nikiitambaza mikono yangu laini kuelekea kwenye shamba la muhogo. Side taratibu alianza kulainikia, kama umeme nilimbeba kama kifurushi na kumuhamishia kitandani. Sikumchelewesha muda mfupi wote tulikuwa salesale maua.
Mtoto wa kike zilikuwa zimenipanda kila kona niliyoguswa nilihisi msisimko wa ajabu. Mmh! Side alinitisha na mtindo wake wa kuniandaa aliouita mboga saba. Kila kona ya mwili aliyonigusa aliigusa kwa ufasaha na kunifanya nisikie raha ya ugwadu usiojulikana ni tamu au chachu.
Baada ya mtoto wa kike kulainika kama mchicha pori, ngoma iliwekwa uwanjani. Side alianza kwa mkwala mzito kama katika ngumi alishambulia bila kupumzika kitu kilichonifanya nijihami muda wote huku nikienda wavuni zaidi ya mara mbili mfululizo.
Mmh! Mtoto wa kike nilianza kuamini kauli za Side Butamu kwamba yeye kaumwa kwa viungo vyote vitamu duniani. Japokuwa niliinjoi mapenzi kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu. Lakini niliona fedheha kushindwa na kinyangarakata kama Side ambacho hata mkononi hakijai. Mpaka tunakwenda mapumziko Side alikuwa anaongoza tena kwa pointi nyingi.

Nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom