Hadithi: Raha Yenye Maumivu

Hadithi: Raha Yenye Maumivu

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,662
Image may contain: text


HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 01
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.


RAHA YENYE MAUMIVU

Hali ya hewa katika mji wa Arusha ilikuwa ya ubaridi kila mmoja alikuwa na nguo nzito za kukabiliana na hali ya hewa. Ila kwa wenyeji wa mkoa huu walikuwa na nguo za kawaida kwao ile hali ya ubaridi kwao ilikuwa ya kawaida hata nguo walizovaa zilikuwa nyepesi tofauti na mgeni wa mkoa huo.
Katika hotel ya New Arusha kila mmoja alikuwa bize na unywaji wa pombe na utafunaji wa nyama choma. Mmoja ya waliokuwa wakipata moja moto moja baridi alikuwepo mama mmoja ambaye umri wake ulikuwa umekwenda kidogo lakini kutokana na uwezo wake wa kipesa alionekana bado.
Yule mama mmoja ya wafanya biashara wakubwa pia alikuwa wanawake wenye pesa nyingi. Pale Arusha alikuwepo kibiashara akiwa safarini nchi za Ulaya. Ni mkazi wa jiji la kila aina ya maraha jiji la Mheshimiwa Rukuvi hapo mwanzo lilijulikana kama jij la Muheshimiwa Kandolo.
Katika maisha yake alibahatika kupata mtoto mmoja wa kike ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 19 ambaye alikuwa yupo kidato cha tano moja ya shule za gharama nchini.
Kwa muda huo hakuwa na mume baada ya kuachana na mume wake, kwa jeuri ya pesa ilimpelekea kuachana na mumewe kwa kuona maisha ya ndoa ni utumwa ambao yalikuwa yakimwekea mipaka ya kazi zake.
Toka aachane na mumewe hakuwa na haja ya kuolewa tena na mwanaume zaidi ya akili yake kuielekeza kwenye biashara ambayo ilimfanya awe na uwezo mkubwa kipesa na kuwa na uwezo wa kufanya lolote atakalo.
Biashara zake zilivuka mipaka mpaka nje ya nchi alijikuta muda mwingi aliutumia kusafiri kwa ajili ya biashara zake hata jina lake lilikuwa moja na watu wenye uwezo wa kifedha jijini. Kitu kilichomfanya asiwe na wazo la kuolewa tena na kuchukulia mwanaume ni kitu cha starehe kwake.
Kutokana kuwa na pesa nyingi alipokuwa akishikwa na haja za kimapenzi alimhonga mwanaume yoyote amtakaye na amalizapo kumstarehesha huupa ujira ambao alijua lazima utamfurahisha hakuwa na bwana maalumu kwa kuogopa kuoneana wivu. Kitu kilichomfanya kuwa na uhuru wa kufanya mambo yake bila kuingiliwa na mtu.
Mam’ kubwa kama jina lake maarufu jijini Dar, akiwa jijini Arusha ambako alipita kufuatilia madeni yake akiwa njiani kwenda Uingereza baada ya kukusanya madeni yake alipanga kwenye Hotel ya new Arusha. Majira ya saa moja usiku alijumuika sehemu ya vinywaji kupata moja moto moja baridi.
Akiwa ametafuta meza ya pembeni aliagiza bia yake ya castle ya kopo na kunywa taratibu huku akifikiria safari yake ya asubuhi katika uwanja wa ndege wa KIA alikuwa amepanga kuondoka na ndege ya saa kumi na mbili asubuhi ya shirika la Gurf Air.
Pombe zilivyo kuwa zikimzidi kumpanda alijikuta akipata hamu ya kuwa na mwanaume kama kawaida yake alivutiwa na kijana mmoja aliyekuwa mhudumu upande wa uchomaji wa nyama. Kijana ambaye alikuwa akimletea nyama, wakati akiendelea kukata maji taratibu kama mamba mzee kwenye bwawa.
Wakati yule kijana akimletea maji ya kunawa alijikuta anamuuliza kwa sauti ya kilevi kidogo.
"Samahani kijana sijui unatoka kazini saa ngapi?"
"Muda si mrefu kuanzia sasa wanaokuja kutupokea wameisha ingia hapa najiandaa kwenda kuoga."
"Mmmmh sawa," alijibu huku akichukua kopo la bia na kupeleka kinywani.
"Kwani vipi?"
"Hapa Arusha una kaa wapi?" Alimuuliza baada ya kumeza funda ya pombe.
"Unga limited."
"Umeoa?"
"Maisha ya kuoa yapo wapi ma’ mkubwa, hela ninayo pata hailingani na hali halisi ya maisha. Mwenyewe tu maisha yananipeleka mchakamchaka huyo mwanamke nitamlisha hewa."
"Mmmh pole sana...Sasa ni hivi naomba kabla ya kuondoka tuonane shika na hii hela njoo na vinywaji nipo chumba namba 033 ...sawa."
"Sawa mama," yule kijana aliondoka kwenda kujiandaa kukabidhi kazi kwa wenzake, wakati huo mam’ kubwa alimsindikiza kwa macho alijua kijana kaisha nasa kwenye mtego wake.
Mam’ kubwa alibeba kinywaji chake kilichobakia na kwenda nacho chumbani kwake kusubiri mtego wake kama utanasa japo alikuwa na imani kwa asilimia 99%. Alipofika chumbani kwake alikwenda bafuni kuoga harakaharaka na kuvaa nguo nyepesi ya kulalia na nguo moja ya ndani.
Alipulizia mafuta yenye harufu nzuri na kukaa mkao wa mamba majini wa kumvizia mwanadamu. Akiwa anamalizia kinywaji chake alisikia mlango ukigongwa moyo ulimpasuka alimkaribisha.
"Pita mlango upo wazi," mlango ulifunguliwa na kuingia mkusudiwa alipomuona aliachia tabasamu pana.
"Oooh karibu sana."
"Asante," alikuwa ameshikia vinywaji alivyo agizwa.
"Karibu jisikie uhuru wa lolote utakalo nina imani usiku wa leo utakuwa pamoja nami," Mam’ Kubwa alisema huku akiachia tabasamu la jisikie huru.
"Hamna tabu mama."
"Usiniite mama niite Sweet."
"Hamna tabu Sweet."
"Ukinifurahisha na wewe nitakufurahisha, hutanisahau kama vile utavyonifanya nisilisahau penzi lako."
Kijana hakuwa nyuma waliendelea kupata vinjwaji huku wakipapasana hapa na pale kila mmoja akijitahidi kumfurahisha mwenzake. Muda ulipotimu kijana alitumia ujuzi wake wote kuhakiki anamkata jimama kiu.
Mtinange ulikuwa mzito uliomfanya kijana wa watu awe hoi kama dume la bata na kujikuta akipitiwa usingizi mzito. Penzi alilopewa jimama lilimrusha akili kama isingekuwa safari angeongeza siku za kuwepo Arusha ili kuendelea kukatwa kiu na kijana. Penzi ambalo anakumbuka alilipata wakati anavujwa ungo.
Jimama aliamka alfajiri ili kuwahi safari yake wakati huo kijana alikuwa bado amelala hajitambui. Hakutaka kumsumbua aliamua kumuachia pesa ambayo alijua itamsaidia maishani mwake na kumuachia ujumbe mfupi uliosema:
Mpenzi..Tino nina imani jana ilikuwa siku yangu ambayo itakuwa ya kuikumbuka maishani mwangu. Penzi ulilonipa sijui kama nitalipata tena.
Kama nilivyokuahidi nami sina budi kukupa zawadi ambayo itakusaidia kusogezea siku. Bakia salama Mungu akijalia tutaonana ni mimi mama Teddy.
Alikiweka kile kikalatasi na shilingi laki saba kwenye mfuko wa suruali wa kijana Augustino Tamilway kisha alimpiga busu kwenye shavu na kuondoka kuwahi usafiri wa ndege uwanja wa ndege wa kimatafa wa Kilimanjaro (KIA)
Aliwasiri kiwanjani nusu saa kabla ndege haijaondoka na kufuata taratibu zote zilizomwezesha kukamilisha taratibu za usafiri na saa kumi na mbili juu ya alama Mam’ kubwa au mama Teddy aliiaga anga ya Tanzania.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 02
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Alikiweka kile kikalatasi na shilingi laki saba kwenye mfuko wa suruali wa kijana Augustino Tamilway kisha alimpiga busu kwenye shavu na kuondoka kuwahi usafiri wa ndege uwanja wa ndege wa kimatafa wa Kilimanjaro (KIA)
Aliwasiri kiwanjani nusu saa kabla ndege haijaondoka na kufuata taratibu zote zilizomwezesha kukamilisha taratibu za usafiri na saa kumi na mbili juu ya alama Mam’ kubwa au mama Teddy aliiaga anga ya Tanzania.
SASA ENDELEA…
******
Kijana Augustino Tamilway au kama wengi wapendavyo kumwita Tino aliposhtuka usingizini alijishangaa kujikuta yupo peke yake kitandani. Alipepesa macho yake akijua labda jimama amekwenda kuoga lakini alikumbuka jana alimweleza ana safari alfajiri.
Aliona yule mama alimdanganya na kumkimbia hata bila ya kumuasha, lakini alijipa moyo kuwa kuna chenji ambazo hakumrudishia Mam’ Kubwa wakati akimtuma pombe ambazo si chini ya elfu nane alijua zitamtoa kwa asubuhi.
Lakini wazo lilimjia huenda yule jimama amezichukua zile hela zitazomfanya aone siku ngumu kwake wazo lake la kwanza ni kwenda kuziangalia zile hela zake kama zimo au la.
Alinyanyuka hadi sehemu aliyoweka suruali yake kitu kingine kilichomtia hofu ni ile hali ya suruali ilivyo kuwa ni tofauti na yeye alivyoiweka. Aliichukua suruali na kuingiza mkono mfuko alishangaa mkono kukutana na uzito alishika vizuri kilichokuwemo na kukitoa hakuamini macho yake zilikuwa pesa nyingi zilizo zungurushiwa kalatasi ndogo nyeupe.
Alizirudisha zile pesa mfukoni na kukisoma kile kikalatasi kilichokuwa na maneno matamu ambayo yalimfanya azitoe zile hela na kuzihesabu zilikuwa laki saba. Tino alishukuru Mungu kweli unaweza kulala maskini na ukaamka tajiri ule usemi ulijidhihirisha kwake.
Katika kitu alichokuwa akikitafuta maishani mwake ni kupata mtaji ambao utamsaidia maishani yeye katika kuhangaika aliomba siku moja apate laki moja ya mtaji lakini siku ile amepata laki saba. Alijua huo ndio mwisho wa kufanya kazi za kuajiliwa alipanga kukimbila jijini Dar kuanzisha biashara ya mitumba.
*****
Augustino Tamilway baada ya kupata kiasi kile kikubwa cha pesa hakuwa na haja ya kupoteza muda aliamua siku ya pili kukimbilia jijini Dar bila kuwaaga watu zaidi ya rafiki yake mkubwa Dani kuwa anakwenda Dar kujaribu maisha. Lakini hakumweleza kuwa ana pesa za kumfanya asiyumbe kimaisha katika jiji linalo aminika ndilo linaloongoza kwa matumizi ya pesa kila kitu kinanunuliwa mpaka uchafu.
Aliondoka jijini Arusha majira ya saa kumi na mbili na basi la Dar express na kuwasiri jijini majira ya saa tisa mchana hakuwa mgeni wa jiji alikwenda kwa rafiki yake Flibert aliyekuwa anakaa Keko Mwanga.
Kwa bahati alimkuta rafiki yake ambaye alikuwa akifanya kazi kampuni ya Plasitic. Hapo ndipo Tamilway alipoanza maisha yake kwa kuulizia biashara gani zinazofaa alielekezwa na kuanza na biashara ya kutandaza chini mtaa wa Kongo .
Alijikuta akipata faida kila kukicha na kufikia hatua ya kusajili watu kumuuzia biashara zake. Alijikuta akipata pesa zilizomfanya aongeze biashara zingine ikiwa pamoja na kununua fremu ya kuuzia biashara zake zilizompa utajiri wa haraka sana.
Wakati huo alikuwa ameishahama kwa rafiki yake Filbert na kupanga chumba chake mwenyewe maeneo ya Temeke Wailes.
********
MIEZI MITATU BAADAYE JIJINI LONDON UINGEREZA

Mabadiliko ya hali ya mam’ kubwa au mama Teddy yalimtia wasiwasi baada ya kupoteza siku zake kwa muda wa miezi miwili kitu kilichomtia wasiwasi na kumfanya aende hospital kuangalia afya yake ajue ile hali ya kutokuziona siku zake inatokana na nini.
Baada ya vipimo vyote ilionekana Mam’ kubwa ni mjamzito wa miezi miwili kitu kilicho mshtua na kuuliza mara mbilimbili.
"Ni kweli usemayo dokta?"
"Kwa nini nikudanganye wewe ni ujamzito wa miezi miwili."
Baada ya kusikia taarifa ile ilimfanya arudishe kumbukumbu zake nyuma na kujiuliza ni mwanaume gani aliye kutana naye miezi mitatu nyuma. Jibu lilikuwa ni Tino kwani ndiye anayekumbuka alikutana naye siku za hatari lakini hakuwa na wasiwasi kwa kujua muda ule hawezi kuzaa tena.
Toka afike jijini London akuwahi kutembea na mwanaume kwa kupindi cha mwezi mzima, kwa kuwa alikuwa bize ma masuala ya biashara. Mara nyingi alipenda kufanya starehe baada ya kumaliza pilikapilika zake za biashara.
Kama ujauzito ungekuwa wa mwezi mmoja angejua ameupatia pale lakini wa miezi miwili lazima alijua ameupatia Tanzania tena jijini Arusha na aliyempatia si mwingine ni Tamilway yule muhudumu wa hotel ya New Arusha.
Pamoja na kupata mshituko haukuwa wa kujuta bali wa furaha kwani ni baada ya miaka 19 toka ajifungue mtoto wake wa kike ambaye kwa sasa anakimbilia miaka 20. Japo alikuwa na hamu ya kupata mtoto mwingine lakini hakubahatika pamoja na kumsaka kwa udi na uvumba lakini aliambulia patupu.
Alitumia dawa za mwanga na kiza zote zilidunda pamoja na kujitahidi kubadilisha wanaume kila kukicha. Alijua Mungu alimpa mtoto mmoja wa kike hata hivyo alimshukuru Mungu kwa kumpatia mtoto wa kike kwani wapo waliokosa kabisa.
Ilikuwa ni furaha isiyo na kifani baada ya kupata uhakika kuwa ana ujauzito wa miezi miwili. Aliamua kubakia Uingereza ambako alipanga angekaa kwa muda na kutimkia Marekani ambako angeendelea kuutunza ujauzito wake karibu na hospitali kubwa duniani ili kuhakikisha hampotezi mwanaye.
Aliogopa kurudi Afrika kwa kuwa wanawake walio wengi upoteza watoto kwa sababu za kizembe. Hata mwanaye anayesoma Hi-lavel alimwagiza amalizapo mtihani wa kidato cha sita amfuate mama yake ulaya.

MIEZI TISA BAADAYE

Muda wa kulipo timu aljifungua salama mtoto wa kiume aliye kuwa na afya njema, aliyempa jina la baba yake mzazi Malon. Baada ya miezi sita ndipo alipoamua kurudi jiji Dar, siku aliyofika hakupumzika alikwea ndege hadi jijini Arusha kumtafuta kijana Tamilway ambaye alimuona anamfaa kuwa mumewe japo kijana mdogo kwa sababu penzi halichagui umri.
Mam’ kubwa au kwa sasa analipenda aitwe mama Malon aliwasiri Arusha majira ya saa kumi jioni na kwenda moja kwa moja Hotel ya New Afrika na kumuulizia Tamilway. Kutokana na muda mrefu kupita aliwakuta wafanyakazi wageni, walisema hawamjui lakini alijaribu kutafuta wenyeji ambao nao walimjulisha kuwa hayupo hata uondokaji wake ulikuwa wa ghafla hivyo hawajui yupo wapi kwa muda ule.
Majibu yalimkatisha tamaa na kuamua kurudi jijini akiwa amelowa na kujiona kama mtu aliyepotelewa koti lake wakati wa baridi kali. Alijua huo ndiyo muda wake wa kutulia baada ya kupata mtoto na kumfanya mume mwanaume aliyemzalisha.
Kauli ya mwanaye siku zote ilimuumiza sana pale alipomuonya mama yake tabia ya kuchanganya wanaume vijana na wazee bora atafute mtu mmoja atulie naye tena anayejiheshimu kuliko kurukaruka ipo siku watachangia mwanaume watashindwa kutazamana.
Baada ya kupata ujauzito ule alijua jawabu ya kilio cha mwanaye limepatika lakini siku zote wa moja havai mbili. Alirudi Dar akiwa amechoka aliamua kumlea mwanaye kwanza hata baadhi ya biashara zake alizimamisha kwa ajili ya kumlea mwanaye ambaye alijua ndiye kichwa cha familia.
Malon alipo fikisha miaka miwili alipelekwa shule ya kulelea watoto iliyo nchini Marekani ambako alimpeleka ili yeye aendelee na biashara zake pamoja na kulipa hela nyingi lakini alijua ndiyo sehemu iliyo salama ambako mtoto hupata malezi na elimu ya hali ya juu.
Nini Kitaendelea ili kuyajua yote endelea kufuatulia.
Bado naendelea na usajili katika Whatsapp Group kwa Ths 2500 kwa mwezi. Baada ya mwezi wa Ramadhani Chombezo mtakalolichagua linaanza baada ya hapo sitapokea mtu tena kwa vile nimetoa muda wa kutosha.
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 03
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Baada ya kupata ujauzito ule alijua jawabu ya kilio cha mwanaye limepatika lakini siku zote wa moja havai mbili. Alirudi Dar akiwa amechoka aliamua kumlea mwanaye kwanza hata baadhi ya biashara zake alizimamisha kwa ajili ya kumlea mwanaye ambaye alijua ndiye kichwa cha familia.
Malon alipo fikisha miaka miwili alipelekwa shule ya kulelea watoto iliyo nchini Marekani ambako alimpeleka ili yeye aendelee na biashara zake pamoja na kulipa hela nyingi lakini alijua ndiyo sehemu iliyo salama ambako mtoto hupata malezi na elimu ya hali ya juu.
SASA ENDELEA…

JIJINI DAR
Kijana Tino Tamilway akiwa hana habari kuna neema inamtafuta ya kukabidhiwa utajiri na mam’ kubwa baada ya kuutafuna mfupa ulio washinda wengi. Naye kwa upande wake mambo yalizidi kumnyookea kwa muda wa mwaka na nusu alikuwa tayari ameisha jenga nyumba mbili na kununua gari la kutembelea hakuwa yule mhudumu wa nyama choma bali mtu maarufu jijini kwa kuwa na maduka ya kuleta vitu vya kisasa.
Kila kukicha alibuni mradi mpya ambao ulimuongezea kipato na kujikuta naye anamiliki magari ya kusafirisha mizigo mikoani jina lake lilijengeka kila kukicha wengi walimwita Tell me way sio tena Tamilway. Pamoja na utajiri aliokuwa nao hakuwa na mwanamke kwa kuogopa kuvurugwa akili na wanawake ambao siku zote aliwaona viumbe wenye vituko.
Alipanga mambo yake yakishatulia hapo ndipo atapotafuta mwanamke atakaye mpenda yeye kama yeye na sio utajiri wake.

CHUO KIKUU MLIMANI JIJINI DAR

Msichana Gift alikuwa na mawazo tele juu ya tabia ya kijana Kanuth kumng'ang'ania kimapenzi pamoja na kumkatalia alikuwa akimnyima raha kwa kumng'ang'ania kutaka urafiki naye. Kama sio tabia zake chafu zilizoenea chuoni za kubadili wanawake kama nguo angemkubali, kwani hata yeye alimpenda kutokana na kuwa na umbile la mvuto kwa kiumbe yoyote wa kike.
Kutokana na upendeleo aliopewa na Mungu Kanuth kila msichana alimtaka yeye pale chuoni. Alikuwa ameisha tembea na wasichana zaidi ya kumi tena wote wanajuana miongoni mwao ni rafiki zake wa karibu pamoja na kumkatalia bado aliendeleza kumfuatafuata kitu kilichomnyima raha.
Gift tatizo lile alimfikishia rafiki wake wa karibu Eliza juu ya kero za Kanuth, Eliza alimpa jibu jepesi kuwa ampe masharti kama kweli anampenda aende akapime HIV na kama yupo safi basi ampe sharti la kutokuwa na msichana mwingine pale chuoni.
"Unafikiri Gift lazima atatoa nje, hapo ndio utakuwa mwisho wa kukusumbua."
"Mmh, kweli wacha nifanye hivyo."
Kama kawaida Kanuth hakuchoka kumfuata Gift cha ajabu mara nyingi anapo mwita huwa hasimami lakini alishangaa kumwona Gift akisimama kumsikiliza. Alijua huo ndio muda muafaka kwani alijiamini kumpata msichana yoyote atayekubali kusikiliza sera zake. Baada ya kufika alimsalimia.
"Za saizi msichana mrembo."
"Nzuri tu mvulana hand some," kauli ile ilimfanya Kanuth ajione kuwa ushindi umekuwa mwepesi tofauti na alivyotegemea alijua pangechimbika kutokana na msimamo wa Gift.
"Za masomo?"
"Nzuri sijui zako?"
"Mmh, kwa kuwa nipo mbele na msichana mrembo kama wewe lazima ziwe nzuri."
"Mmh, nieleze ulichonisimamishia naona umeanza nahau."
"Unajua Gift unautesa moyo wangu kila siku hasa pale unapokataa hata kusikiliza kilio changu," Kanuth kama kawaida akaanza tenzi zake.
"Hicho kilio umewalilia wangapi?" Gift alimuuliza huku akimpandisha na kumshusha.
"Unajua Gift sifa yangu imekuwa mbaya hapa chuoni kutokana na tabia za watu kunipakazia, mazoea na wasichana imekuwa nongwa unajua nina damu ya kupatana na watoto wa kike."
"Haya tuachane na hayo, ulikuwa unasemaje?"
"Hilo ndilo swali ulitakiwa kuniuliza mapema, Gift nina imani sote tupo mwaka wa tatu bado mwaka mmoja tumalize masomo yetu na baada ya hapa kila mmoja anatakiwa kupata kazi kwa watakaojaaliwa kwa upande wangu suala la kazi silifikilii sana kwa kuwa wazazi wangu wana kila aina ya utajiri ninacho fikiria ni kujenga familia ya kuwa na mke mwema ili anizalie watoto watakao fuata maadili mema ya wazazi wao.
"Nina imani ombi langu kama utalipokea kwa mikono miwili na kunipa jibu litakalo upa moyo faraja la milele sijui mtoto mrembo unasemaje?"
"Nasikia hayo maneno ameyanukuu kila mwanamke unaye kutananaye unamueleza hivyo."
"Aah, ni nani niliyemweleza maneno kama hayo?"
"Mwaija."
"Ni kweli nilikuwa nina nia kweli ya kumuoa lakini hakuwa muaminifu kitu kilichopelekea tuachane najua ndiye mbaya wangu anayeeneza maneno ya uongo ili kunichafulia jina lakini si kweli sina sifa hizo," Kanuth alizidi kujitetea.
"Pamoja na maneno yako lakini bado sikuamini."
"Nifanye nini ili uniamini."
"Ukapime HIV."
"Haa! ili iweje?"
"Ndio nikuamini."
"Ina maana nikukuletea cheti ndio utanikubali?"
"Ndio jibu jepesi."
"Basi tegemea jibu jioni ya leo."
"Sawa."
Waliagana kila mmoja alishika hamsini zake, Taarifa zile alimfikishia rafiki yake Eliza.
"Nimemweleza kama ulivyo nieleza."
"Ehe, alisemaje?"
"Kwanza alishtuka kisha akasema eti cheti atanileleta jioni ya leo."
"Thubutu atawahi unafikili ni kwenda kupima maralia, alikuwa anatafuta njia ya kuondokea najua umemkata maini hakufuati tena."
"Mmh, kama ni hivyo nitashukuru maana alikuwa kero, ya nini kuniua na UKIMWI mwana wa mwenzie akafie mbele na haohao vichangudoa vyake vyenye tamaa sina tamaa ndogondogo sina ninachokikosa kwa mzazi wangu na vile nipo peke yangu mtoto wa kike kama jicho nini nikitake nikikose."
*****
Majira ya saa mbili usiku baada ya chakula cha usiku Gift akiwa na Eliza alisikia sauti ya Kanuth ikimwita alipogeuka walikutana uso kwa uso.
"Vipi Kay?"
"Ule mzigo huu hapa," alisema huku akimkabidhi bahasha.
"Mzigo gani?"
"Kwani asubuhi tuliongea nini nilifanyie kazi maneno yako na majibu ni haya."
"Ina maana ulienda kupima?" Kauli ile ilimshtua Gift
"Gift nilitaka kukuonyesha maneno yote uliyosikia ni kunipakazina tu."
"Mmh, majibu yanasemaje?"
"Nenda kasome mwenye nina imani kesho utanipa jibu zuri," Gift aliipokea ile bahasha na kuelekea nacho chumbani mwake ili akakisome, alijikuta amepagawa hata kumpita shoga yake Eliza aliyekuwa akimsubiri pembeni.
"Shosti mbona unanipita kuna nini tena?"
"Kaniletea majibu."
"Yanasemaje?"
"Kanipa nikayasome mwenyewe."
"Atakuwa muongo kanunua tu cheti atawahi hivi unafikili kupima mchezo akose umeme kicheche kama yule."
Walikwenda hadi chumbani na kukisoma kile cheti kilicho onyesha yupo safi alichopima ANGAZA.
"Sasa itakuwaje?"
"Mwambie humuamini ikiwezekana muende wote."
"Mmh, na tukienda wote na akaonekana yupo safi itakuwaje?"
"Nakuhakikishia hawezi," Eliza alimtia moyo Gift.
"Mmh, nitajaribu."
Waliagana kila mmoja alijiandaa na masomo ya usiku lakini Gift hakuhudhulia aliamua kulala.

Nini Kitaendelea ili kuyajua yote endelea kufuatulia.
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 04
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Walikwenda hadi chumbani na kukisoma kile cheti kilicho onyesha yupo safi alichopima ANGAZA.
"Sasa itakuwaje?"
"Mwambie humuamini ikiwezekana muende wote."
"Mmh, na tukienda wote na akaonekana yupo safi itakuwaje?"
"Nakuhakikishia hawezi," Eliza alimtia moyo Gift.
"Mmh, nitajaribu."
Waliagana kila mmoja alijiandaa na masomo ya usiku lakini Gift hakuhudhulia aliamua kulala.
SASA ENDELEA…

Asubuhi kama kawaida walikutana Kanuth alimchanulia Gift tabasamu pana
"Ooh, mrembo nina imani amelala njozi tamu zilizo kufanya usisikie uchovu ulipo amka asubuhi."
"Si kweli mawazo yako."
"Nini tatizo?"
"Kwa nini umenidanganya Kanuth kwa kugushi cheti ili uonekane mzima kwa nini unataka kuniua kosa langu nini kwani mapenzi lazima," Gift alianza kuporomosha machozi.
"Nafikiri baada ya muumba ni mimi ninaye yajali maisha yako, kama huniamini tuongozane na wewe mguu kwa mguu popote unapo paamini ili uthibitishe watu hawanitakii mema."
"Kweli upo tayari twende sasa hivi?"
"Nipo tayari popote unapo paamini na daktari unaye muamini ili kuthibitisha nipo safi na nina nia ya kweli na wewe."
Kauli ule ilikuwa kama kisu chenye moto kwenye siagi kwenye moyo wa Gift na kuona huenda yote aliyo sikia ni uongo kwa jinsi kila aliloambiwa na Eliza lilikuwa kinyume.
Alijikuta akimkubalia kwa sharti la penzi lao liwe siri mpaka hapo watakapo maliza shule na kuutangaza uchumba wao kabisa, naye Kanuth alikubali kuilinda siri ya mapenzi kwa kulifanya penzi lao kuwa la siri.
Tokea siku ile Gift na Kanuth walikuwa wapenzi mwanzo kweli lilikuwa penzi la siri, lakini siku zote mapenzi kikohozi kuyaficha huyawezi. Ilikuwa siri mwishowe ikawa bayana kila mmoja alijua penzi la Kanuth na Gift.
Siku zote jasiri haachi asiri siku moja Gift alipigiwa simu na mtu mmoja asiye mjua na kumuomba aende maeneo ya Sinza kwenye hote mpya iliyo karibu na Legho ameonekana Kanuth akiwa na rafiki yake mpenzi kipenzi Eliza.
Presha ikiwa juu alikodi gari hadi kwenye ile hoteli na kwenda moja kwa moja chumba alichoelekezwa, alipofika alitaka kugonga lakini akili nyingine ilimwambia ajaribu kufungua mlango alizungusha kitasa mlango ulitii amri na kufunguka.
Alijitoma ndani, picha aliyoikuta ilimfanya asiamini macho yake alikuwa kweli Kanuth na shoga yake kipenzi Eliza wakivunja amri ya sita. Cha ajabu pamoja na kumwona waliendelea kufanya mchezo wao mchafu bila kuhofu jambo lolote kitu kilicho mfanya Gift kushikwa na kizunguzungu na kuanguka chini nakupoteza fahamu.
****
Gift alipozinduka alijikuta akiwa amelala chini peke yake ndani ya chumba cha guest hapakuwepo Kanuth wala shoga yake Eliza. Alijinyanyua na kukaa kitako akiwaza nini kilichomtokea hapo ndipo kumbukumbu zilipomrudia alianza kulia kilio cha sauti ya chini na kujilaumu kwa kukubali kuwa mpenzi wa mtu aliyemjua tabia zake japo alikuwa hajawahi kumuona, lakini sifa zake pale chuoni zilikuwa mbaya.
Kweli aliamini wanaume wana lugha tamu za ushawishi ambazo huwa kama kisu cha moto kwenye bonge la mafuta ambacho hukata bila tabu wala kutumia nguvu. Pamoja na kweli Kanuth kuwa malaya wa kiume kilichomuuma ni ile hali ya kumkuta na shoga yake ambaye alimsisitiza asimkubali kuwa mpenzi wa Kanuth kwa kusema huenda ni muathirika wa UKIMWI, lakini ajabu ni yeye huyohuyo amemkuta akiwa na huyo aliyemwita muathirika.
Alijikuta akijishangaa kuendelea kuwepo pale tena kuendelea kulia ni heri aondoke ili arudi chuoni kuliko kuendelea kuwepo pale. Alijinyanyua pale chini ili aondoke mule ndani ya chumba cha nyumba ya wageni.
Gift alitoka ndani ya guet ya Rombo akiwa amechanganyikiwa alikuwa akitembea lakini hakuwa yeye, alijiuliza ni nani aliyempigia simu na alikuwa na maana gani kumpigia simu ile. Bila kujielewa alijikuta akitembea katikati ya barabara bila kujua kama yupo katikati barabara.
Agustino Tamilway a.k.a "Tell me why" akiwa katika mwendo wa kasi huku akiongea na simu yake kiganjani katika maongezi ambayo yalimfanya akili yake ihamie kwenye maongezi ndani ya simu.
Aliponyanyua macho hamadi! Mbele yake alikuwepo msichana ambaye alionyesha wazi amechanganyikiwa. Alijikuta akitumia uwezo wake wote kumkwepa yule msichana ambaye alionekana amechanganyikiwa. Alijikuta anafunga breki huku akiuma meno mpaka tairi za gali zilinuka kwa kujiburuza.
Alifanikiwa kufunga breki lakini gari liliseleleka kutokana na mwendo makali na kumpiga kikumbo Gift na kumtupa mbali kidogo. Tell me why alitereka kwenye gari na kumkimbilia Gift ambaye alikuwa ameanguka chini damu zikimtoka kichwani na alikuwa amepoteza fahamu.
Alimchukuwa harakaharaka kabla watu hawajakuwa wengi na kumuingiza kwenye gari lake, kwa haraka aligeuza gari na kumwahisha hospitali ya TMJ iliyopo Mikoche ambayo ndiyo anayotibiwa yeye. Alipomfikisha harakaharaka alichukuliwa na wauguzi na kukimbiziwa hodini tayari kwa huduma.
Tell me Why alikutana na daktali Eliud na kumwelezea sababu ya ajali
"Ina maana mgonjwa hakuwa na jamaa au ndugu?" Dakta aliuliza.
"Kwa kweli sijui kwa sababu baada ya kujitahidi kumkwepa na kukumba na bodi ya gari nilichojua ni kumwahisha hospitali ili kuokoa maisha yake zaidi ya hapo sijui."
"Pole sana, ni hali ya kawaida ambayo huwakuta watu wengi lakini wewe umeonyesha moyo wa ujasiri na huruma, mara nyingi watu wanapotokewa na tukio kama hili hukimbia na kumwacha mgonjwa bila kujua nini hatma yake.”
"Unajua nini Mr Eliud mara nyingi sababu ya madereva kukimbia husababishwa na wananchi wanaojiita raia wenye hasira kali, wao wanachojua kila ajali ni uzembe wa dereva. Baada ya ajali humuangushia kipigo dereva bila kujua ni yeye huyo mwenye usafiri anayeweza kuokoa maisha ya huyo mgonjwa kwa kumuwahisha hospitali."
"Ni kweli lakini nimegundua wengi ni wezi ambao hutumia nafasi ile kumuibia dereva chochote kilichomo kwenye gari...Sasa Mr Tell me why wacha nimshughulikie mgonjwa kwa sababu nimewaachia kazi ya kuchukua vipimo vya awali ili kujua ameumia kwa kiasi gani."
Dakta Eliud alikwenda kumuangalia mgonjwa na kuangalia vipimo, na kumuacha Mr Tell me why akiwa amejiinamia kwa mawazo na kujiuliza maswali mengi juu ya mgonjwa na hali yake. Alijikuta akijiuliza alikuwa anatoka wapi na kwa nini alikuwa akitembea katikati ya barabara ilionyesha alikuwa amechanganyikiwa.
Alimuomba Mungu amponyeshe upesi na majeraha yake yasiwe makubwa aliamini kikumbo kilichompata huenda maumivu yake yasiwe makubwa sana. Akiwa ameinama alishtushwa na sauti ya Dakta Eliud
"Mr tell me..vipi naona tukio limekuchanganya sana?"
Sauti ile ilimfanya anyanyuke kwa haraka kutaka kujua hali ya mgonjwa.
"Vipi Doctor hali ya mgonjwa ikoje?"
" Tuliza munkali Mr."
"Dakta ni vigumu kutulia kutoka roho ya mtu bila kutegemea lazima uchanganyikiwe...Vipi hali yake?"
"Tuliza munkali hali ya mgonjwa sio mbaya."
"Ooh, asante Mungu ningekuwa mgeni wa nani kibaya zaidi hata ndugu zake siwajui."
"Ila..."
"Oooh doctor ila nini tena?"
"Punguza munkali Mr tell me, kila kitu kitakuwa sawa ila nilitaka kukueleza kuwa hali yake si mbaya ni majeraha madogo siyo makubwa ya kutisha japo la kichwani ni kubwa kidogo lakini halihitaji kushonwa bali kufungwa dawa tu."
"Ooh afadhali," Mr Tell me why alishusha pumzi ndefu kisha alisema.
"Mr Eliud naweza kwenda kumuona mgonjwa wangu?"
"Mmh mara hii ameisha kuwa mgonjwa wako wakati umemuokota njiani?"
"Hapana kwa sasa ni mgonjwa wangu mpaka hapo nitakapo mkabidhi kwa familia yake."

Nini Kitaendelea? Ili kuyajua yote endelea kufuatulia.
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 05
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
"Punguza munkali Mr tell me, kila kitu kitakuwa sawa ila nilitaka kukueleza kuwa hali yake si mbaya ni majeraha madogo siyo makubwa ya kutisha japo la kichwani ni kubwa kidogo lakini halihitaji kushonwa bali kufungwa dawa tu."
"Ooh afadhali," Mr Tell me why alishusha pumzi ndefu kisha alisema.
"Mr Eliud naweza kwenda kumuona mgonjwa wangu?"
"Mmh mara hii ameisha kuwa mgonjwa wako wakati umemuokota njiani?"
"Hapana kwa sasa ni mgonjwa wangu mpaka hapo nitakapo mkabidhi kwa familia yake."
SASA ENDELEA…

"Ni kweli unaonyesha jinsi gani ulivyo na utu wa kuwajali wanadamu wenzio."
"Sasa naweza kwenda kumuona?"
"Hapana kwa leo itakuwa ngumu kwa kuwa muda huu amelala baada ya kumpatia dawa za maumivu zilizompa usingizi ili kumfanya apumzike hata atakapo amka atakuwa hana maumivu makali."
"Kwa hiyo mimi mnaniambiaje?"
"Wewe nenda ukaendelee na shuguli zako kama kawaida ila kesho nina imani ukija utamkuta nina imani kama hatakuwa na tatizo lingine tutamruhusu kesho."
"Daktari mbona haraka si unajua ajali kuna mambo hujificha kwa nini asikae hata wiki ili kuiangalia afya yake kwa umakini mkubwa."
"Ni kweli lakini kuna gharama zingine hazina umuhimu bora akauguzie maumivu nyumbani kwao kama atajisikia vibaya anaweza kurudi."
"Mr Eliud pesa kwangu sio tatizo la muhimu ni hali ya mgonjwa vilevile hatujui hali yake kimaisha huenda kwao hali ya kimaisha sio nzuri ambayo itasababisha apate shida ya kujitibu huoni kama tutakuwa tumemuongezea mzigo?"
"Mimi sina neno nakusikiliza wewe."
"Kama nilivyo kueleza atulie kwa muda wa wiki nzima."
"Ok, basi kesho kama kuna mabadiliko nitakujulisha kwa njia ya simu."
Waliagana na doctor Eliud na kuendelea na mambo mengine hata safari yake ya Kibaha aliiahilisha na kurudi nyumbani kwa mapumziko. Aliona mbele kuna mkosi.
****
TMJ HOSPITALI MIKOCHENI

Gift baada ya kuzinduka alishangaa kujikuta akiwa hospitali amelazwa kitandani, alijiuliza pale amefikaje na alipojaribu kujigeuza alihisi maumivu makali sehemu za mbavu na mwili wote ulikuwa ukimuuma. Alipopeleka mkono kichwani alikutana na jeraha lililokuwa limefungwa.
Gift alitahayali na kujiuliza nini kilichomsibu mpaka kuwa pale katika hali ile, alipojaribu kurudisha kumbukumbu alikumbuka kitendo alichotendewa na Kanuth na shoga yake mpenzi Eliza cha kumsaliti.
Lakini kumbukumbu zake zilimjulisha kuwa baada ya tukio lile alidondoka chini na kilichoendelea hakujua na alipozinduka alijikuta akiwa chumbani peke yake na wasaliti wake hakuwaona walikuwa wameisha ondoka na kumwacha ndani peke yake.
Lakini baada ya hapo hakumbuki nini kilichoendelea mpaka kujikuta pale.
Wazo lilimuijia huenda Kanuth alimpigaa.
"Mmh, huenda nilifanya fujo zilizopelekea wanipige...Mmh, lakini mbona sikumbuki kama nilifanya fujo zilizopelekea mimi kupigwa au..haa.. pana... lakini... hapana, nina uhakika sikufanya lolote zaidi ya mimi kuanguka chini au nilipata nguvu kuamka tena na kuanzisha fujo ...ni jambo la ajabu sijawahi wala sintawahi kupigania mapenzi japokuwa huwa naumia moyoni...basi itakuwa mara yangu ya kwanza...
"Mmh, na.. na.. nani aliye nileta hosipitali na hii ni hospitali gani ...ooh TMJ," alisema vile baada ya kuona nembo yake kwenye pazia za madirishani.
Akiwa katikati ya lindi la mawazo alishtushwa na sauti ya mlango wa chumba alicholazwa ukifunguliwa na kuingia muuguzi akiwa na trey iliyokuwa na dawa, aliachia tabasamu pana baada ya kuona mgonjwa amepata fahamu alimsogelea na kumjulia hali.
"Pole sana dada."
"Asante," Gift alijibu kwa sauti ya chini.
"Unaendeleaje?"
"Mmh, bado."
"Pole sana, lakini una mabadiliko makubwa na ulipoletwa."
"Kwani nilikuwa kwenye hali gani?"
"Ulikuwa hujitambui na damu zilikuwa ni nyingi zilizotushtua lakini baada ya kukupa matibabu ya haraka na vipimo vya awali ilionyesha hukuwana jeraha kubwa na vipimo vilionyesha ujaumia sana."
"Dada yangu sijaumia sana wakati mwili wote unaniuma kama kidonda?"
"Huo ni msukumo wa gari una bahati hukugongwa na gari bali ni msukumo. Inavyoonesha dereva alijitahidi kufunga breki lakini kwa vile ilikuwa kwenye kasi utelezi ulisababisha gari likukumbe na kukutupa kwenye mtalo."
"Yaani nesi unataka kuniambia nimegongwa na gari?" Gift alishtuka.
"Ina maana hukujua kilichokuleta hapa?"
"Hata moja sina nashangaa kujiona nipo hapa."
"Kwani wewe ulikuwa wapi mpaka ajali hii inakupata?"
"Sikumbuki ila...Oooh wacha aina muhimu...Ni nani aliyenileta hapa?"
"Kuna kaka mmoja mfanya biashara maarufu jijini ndiye aliye kugonga na ndiye aliyekuleta."
"Yeye yupo wapi lazima nimshtaki."
"Unachekesha yaani badala ya kumshukuru mtu kukugonga na kukukimbizia hospitali tena ya gharama. Tofauti na madereva wengi wakishagonga hukimbia au hukupeleka hospitali ya wilaya na kukuacha lakini kaka huyo.
"Alionyesha kuchanganyikiwa na hakuwa tayari kuondoka mpaka ajue hatma ya hali yako. Mpaka alipoelezwa kuwa unaendelea vizuri ndipo aliporuhusiwa kuondoka na kuelezwa arudi kesho."
"Simu yangu ipo wapi?"
"Kwa kweli hatujui tulikupokea hukuwa na kitu chochote."
"Inawezekana aliyenigonga ameniibia?"
"Sidhani mtu mwenyewe hujamuona sio mtu wa njaa hawezi kuchukua simu yako."
"Simu yenyewe unaijua nimeinunua milioni moja na nusu."
"Hata tatu si kwa Tell me why."
"Tell me why una maana gani?"
"Ndio jina la mfanya biashara huyo ni maarufu nashangaa wewe humjui."
" Una simu?"
"Ndio."
"Naomba nimtaarifu mama."
"Kwani mama yako ni nani?"
"Mama Tedy au mam’ kubwa."
"Yule mfanya biashara maarufu?"
"Ndiye huyohuyo."
"Ok, simu hii mpigie," Gift aliipokea ile simu na kumpigia mama yake.
"Haloo mama nipo hospitali nimepata ajali."
"My God hospitali gani...una hali gani mwanagu?" Mam’ kubwa alichanganyikiwa.
"Mama punguza presha nipo TMJ lakini hali yangu sio mbaya ni majeraha madogo madogo."
"Ok, nakuja sasa hivi," mama Teddy alikata simu.
"Asante anti kwa msaada wako," Gift alimshukuru muuguzi kwa msaada wa simu.
"Ni kawaida yetu wanadamu kusaidiana usihofu kwa hilo."
“Nashukuru.”
"Naomba basi nikuchome sindano."
Gift alijitayalisha kuchomwa sindano baada ya kuchomwa sindano muuguzi aliondoka ili kumuacha apumzike. Kabla hajapumzisha mwili baada ya kundungwa sindano mama yake aliingia huku akitweta.
"Vipi mwanangu upo salama?"
"Nipo salama mama."
"Ilikuwaje?"
"Ni ajali kama ajali zingine hata kuelezea nashindwa lakini namsifu dereva kwa kujitahidi kuokoa maisha yangu.Vilevile kuwa na roho ya kibinaadamu ya kunikimbiza hospitali."
"Huyo dereva yupo wapi?"
"Ukweli mama sijamuona ila nimeambiwa baada ya kunileta hakuondoka mpaka alipoelezwa hali yangu inaendelea vizuri lakini nasikia ameahidi kuja leo kunijulia hali yangu."

Nini Kitaendelea?
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 05
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
"Punguza munkali Mr tell me, kila kitu kitakuwa sawa ila nilitaka kukueleza kuwa hali yake si mbaya ni majeraha madogo siyo makubwa ya kutisha japo la kichwani ni kubwa kidogo lakini halihitaji kushonwa bali kufungwa dawa tu."
"Ooh afadhali," Mr Tell me why alishusha pumzi ndefu kisha alisema.
"Mr Eliud naweza kwenda kumuona mgonjwa wangu?"
"Mmh mara hii ameisha kuwa mgonjwa wako wakati umemuokota njiani?"
"Hapana kwa sasa ni mgonjwa wangu mpaka hapo nitakapo mkabidhi kwa familia yake."
SASA ENDELEA…

"Ni kweli unaonyesha jinsi gani ulivyo na utu wa kuwajali wanadamu wenzio."
"Sasa naweza kwenda kumuona?"
"Hapana kwa leo itakuwa ngumu kwa kuwa muda huu amelala baada ya kumpatia dawa za maumivu zilizompa usingizi ili kumfanya apumzike hata atakapo amka atakuwa hana maumivu makali."
"Kwa hiyo mimi mnaniambiaje?"
"Wewe nenda ukaendelee na shuguli zako kama kawaida ila kesho nina imani ukija utamkuta nina imani kama hatakuwa na tatizo lingine tutamruhusu kesho."
"Daktari mbona haraka si unajua ajali kuna mambo hujificha kwa nini asikae hata wiki ili kuiangalia afya yake kwa umakini mkubwa."
"Ni kweli lakini kuna gharama zingine hazina umuhimu bora akauguzie maumivu nyumbani kwao kama atajisikia vibaya anaweza kurudi."
"Mr Eliud pesa kwangu sio tatizo la muhimu ni hali ya mgonjwa vilevile hatujui hali yake kimaisha huenda kwao hali ya kimaisha sio nzuri ambayo itasababisha apate shida ya kujitibu huoni kama tutakuwa tumemuongezea mzigo?"
"Mimi sina neno nakusikiliza wewe."
"Kama nilivyo kueleza atulie kwa muda wa wiki nzima."
"Ok, basi kesho kama kuna mabadiliko nitakujulisha kwa njia ya simu."
Waliagana na doctor Eliud na kuendelea na mambo mengine hata safari yake ya Kibaha aliiahilisha na kurudi nyumbani kwa mapumziko. Aliona mbele kuna mkosi.
****
TMJ HOSPITALI MIKOCHENI

Gift baada ya kuzinduka alishangaa kujikuta akiwa hospitali amelazwa kitandani, alijiuliza pale amefikaje na alipojaribu kujigeuza alihisi maumivu makali sehemu za mbavu na mwili wote ulikuwa ukimuuma. Alipopeleka mkono kichwani alikutana na jeraha lililokuwa limefungwa.
Gift alitahayali na kujiuliza nini kilichomsibu mpaka kuwa pale katika hali ile, alipojaribu kurudisha kumbukumbu alikumbuka kitendo alichotendewa na Kanuth na shoga yake mpenzi Eliza cha kumsaliti.
Lakini kumbukumbu zake zilimjulisha kuwa baada ya tukio lile alidondoka chini na kilichoendelea hakujua na alipozinduka alijikuta akiwa chumbani peke yake na wasaliti wake hakuwaona walikuwa wameisha ondoka na kumwacha ndani peke yake.
Lakini baada ya hapo hakumbuki nini kilichoendelea mpaka kujikuta pale.
Wazo lilimuijia huenda Kanuth alimpigaa.
"Mmh, huenda nilifanya fujo zilizopelekea wanipige...Mmh, lakini mbona sikumbuki kama nilifanya fujo zilizopelekea mimi kupigwa au..haa.. pana... lakini... hapana, nina uhakika sikufanya lolote zaidi ya mimi kuanguka chini au nilipata nguvu kuamka tena na kuanzisha fujo ...ni jambo la ajabu sijawahi wala sintawahi kupigania mapenzi japokuwa huwa naumia moyoni...basi itakuwa mara yangu ya kwanza...
"Mmh, na.. na.. nani aliye nileta hosipitali na hii ni hospitali gani ...ooh TMJ," alisema vile baada ya kuona nembo yake kwenye pazia za madirishani.
Akiwa katikati ya lindi la mawazo alishtushwa na sauti ya mlango wa chumba alicholazwa ukifunguliwa na kuingia muuguzi akiwa na trey iliyokuwa na dawa, aliachia tabasamu pana baada ya kuona mgonjwa amepata fahamu alimsogelea na kumjulia hali.
"Pole sana dada."
"Asante," Gift alijibu kwa sauti ya chini.
"Unaendeleaje?"
"Mmh, bado."
"Pole sana, lakini una mabadiliko makubwa na ulipoletwa."
"Kwani nilikuwa kwenye hali gani?"
"Ulikuwa hujitambui na damu zilikuwa ni nyingi zilizotushtua lakini baada ya kukupa matibabu ya haraka na vipimo vya awali ilionyesha hukuwana jeraha kubwa na vipimo vilionyesha ujaumia sana."
"Dada yangu sijaumia sana wakati mwili wote unaniuma kama kidonda?"
"Huo ni msukumo wa gari una bahati hukugongwa na gari bali ni msukumo. Inavyoonesha dereva alijitahidi kufunga breki lakini kwa vile ilikuwa kwenye kasi utelezi ulisababisha gari likukumbe na kukutupa kwenye mtalo."
"Yaani nesi unataka kuniambia nimegongwa na gari?" Gift alishtuka.
"Ina maana hukujua kilichokuleta hapa?"
"Hata moja sina nashangaa kujiona nipo hapa."
"Kwani wewe ulikuwa wapi mpaka ajali hii inakupata?"
"Sikumbuki ila...Oooh wacha aina muhimu...Ni nani aliyenileta hapa?"
"Kuna kaka mmoja mfanya biashara maarufu jijini ndiye aliye kugonga na ndiye aliyekuleta."
"Yeye yupo wapi lazima nimshtaki."
"Unachekesha yaani badala ya kumshukuru mtu kukugonga na kukukimbizia hospitali tena ya gharama. Tofauti na madereva wengi wakishagonga hukimbia au hukupeleka hospitali ya wilaya na kukuacha lakini kaka huyo.
"Alionyesha kuchanganyikiwa na hakuwa tayari kuondoka mpaka ajue hatma ya hali yako. Mpaka alipoelezwa kuwa unaendelea vizuri ndipo aliporuhusiwa kuondoka na kuelezwa arudi kesho."
"Simu yangu ipo wapi?"
"Kwa kweli hatujui tulikupokea hukuwa na kitu chochote."
"Inawezekana aliyenigonga ameniibia?"
"Sidhani mtu mwenyewe hujamuona sio mtu wa njaa hawezi kuchukua simu yako."
"Simu yenyewe unaijua nimeinunua milioni moja na nusu."
"Hata tatu si kwa Tell me why."
"Tell me why una maana gani?"
"Ndio jina la mfanya biashara huyo ni maarufu nashangaa wewe humjui."
" Una simu?"
"Ndio."
"Naomba nimtaarifu mama."
"Kwani mama yako ni nani?"
"Mama Tedy au mam’ kubwa."
"Yule mfanya biashara maarufu?"
"Ndiye huyohuyo."
"Ok, simu hii mpigie," Gift aliipokea ile simu na kumpigia mama yake.
"Haloo mama nipo hospitali nimepata ajali."
"My God hospitali gani...una hali gani mwanagu?" Mam’ kubwa alichanganyikiwa.
"Mama punguza presha nipo TMJ lakini hali yangu sio mbaya ni majeraha madogo madogo."
"Ok, nakuja sasa hivi," mama Teddy alikata simu.
"Asante anti kwa msaada wako," Gift alimshukuru muuguzi kwa msaada wa simu.
"Ni kawaida yetu wanadamu kusaidiana usihofu kwa hilo."
“Nashukuru.”
"Naomba basi nikuchome sindano."
Gift alijitayalisha kuchomwa sindano baada ya kuchomwa sindano muuguzi aliondoka ili kumuacha apumzike. Kabla hajapumzisha mwili baada ya kundungwa sindano mama yake aliingia huku akitweta.
"Vipi mwanangu upo salama?"
"Nipo salama mama."
"Ilikuwaje?"
"Ni ajali kama ajali zingine hata kuelezea nashindwa lakini namsifu dereva kwa kujitahidi kuokoa maisha yangu.Vilevile kuwa na roho ya kibinaadamu ya kunikimbiza hospitali."
"Huyo dereva yupo wapi?"
"Ukweli mama sijamuona ila nimeambiwa baada ya kunileta hakuondoka mpaka alipoelezwa hali yangu inaendelea vizuri lakini nasikia ameahidi kuja leo kunijulia hali yangu."

Nini Kitaendelea?

Ndo tunasubilia
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 06
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
"Ni ajali kama ajali zingine hata kuelezea nashindwa lakini namsifu dereva kwa kujitahidi kuokoa maisha yangu.Vilevile kuwa na roho ya kibinaadamu ya kunikimbiza hospitali."
"Huyo dereva yupo wapi?"
"Ukweli mama sijamuona ila nimeambiwa baada ya kunileta hakuondoka mpaka alipoelezwa hali yangu inaendelea vizuri lakini nasikia ameahidi kuja leo kunijulia hali yangu."
SASA ENDELEA…

"Chuoni umewajulisha amepata ajali?"
"Niwajulishe wapi simu sina."
"Na kweli simu yako ipo wapi?"
"Hata sielewi ndio namsubiri huyo kaka labda ameniwekea."
"Basi wacha niwapigie simu chuoni kwenu ili wajue upo kwenye hali gani."
"Sawa mama."
Mama Gift alimpigia simu mkuu wa chuo kumjulisha matatizo yaliyomkumba mwanaye naye mkuu wa chuo alisema atawajulisha wote. Aliamua kwenda kumuona daktari mkuu Mr Eliud ili ajue hali ya mwanaye.
Mama kubwa au mama Teddy ukipenda mwite mama Gift baada ya kutoka kwa mwanaye na kuelekea kwa daktari alipishana mlangoni na kijana mtanashati aliyekuwa amepakatia mfuko uliokuwa na vitu vingi pamoja na kadi na ua mkononi.
Hakumjali alielekea kwa daktari, yule kijana aliingia kwenye chumba cha Gift na kumkuta Gift akiwa anakula ndizi alizoletewa na mama yake. Alipomuona kijana mtanashati akiingia na chumba chote kubadilika harufu ya ndani na kunukia manukato ya gharama ambayo aliyakumbuka aliishawahi kutumia mama yake siku za nyuma na kumwambia ni matukato ya gharama nchi za Afrika hayapatikani ni wachache wa kuyanunua.
"Karibu kaka."
"Asante...nina imani wewe ni mgonjwa wangu?"
"Kwani wewe ndiye uliyenigonga?" Gift aliacha kula na kumtazama yule kujana aliyekuwa amepeneza mavazi nywele zake muonekano wake mbele za watu. Shingoni alikuwa na mkufu mnene wa dhahabu.
"Hapana sijakugonga bali gari lilikusukuma kidogo."
"Ndiyo mimi, karibu tunakula."
"Asante, kwanza pole sana, vipi hali yako?"
"Kiasi sijambo sio kama jana."
"Inaonekana jana ulikuwa umechanganyikiwa shemeji alikuwa amekuudhi nini?"
"Walaaa, matatizo ya dunia."
"Umeolewa?"
"Hapana nasoma."
"Wapi?"
"Chuo kikuu Mlimani."
"Ooh, kumbe naongea na msomi."
"Mmh,"Gift aliguna tu.
"Sasa mrembo nina imani familia yako imeshapata taarifa?"
"Ndiyo..tena mama yupo."
"Oooh kumbe mama mkwe ameisha kuja vizuri..Sasa ni hivi wacha niwahi ila kesho nitakuja na kujua nini cha muhimu ili kuhakikisha unarudi katika hali yako ya kawaida."
"Mmh, sidhani kuwepo hadi kesho nasubiri mama atakuja kuniambiaje."
"Sio mbaya chukua hii kadi yangu ya shughuli zangu tutawasiliana sawa au nitakuja kukutafuta chuoni, nakaribishwa?"
"Karibu, lakini naomba umsubiri mama akuone."
"Hapana...nani kweli?"
"Gift."
"Oooh, una jina zuri inaweza kuwa zawadi yangu," Gift hakujibu alitabasamu tu.
"Ok, Gift tutaonana msalimie sana mama kwa vile una kadi yangu nitafika nyumbani au chuoni kukujulia hali..Huna simu msomi?"
Kauli ile ilimshtua Gift wakati yeye alikuwa akijipanga kuulizia simu yake ilibidi ajibu.
"Nilitegemea labda wewe jana uliichukua hivi nilikuwa najiandaa kukuuliza."
"Oooh pole, sana inawezekana watu waliichukua baada ya ajali."
"Simu yangu ilikuwa ya gharama kubwa."
"Kwani ilikuwa shilingi ngapi?"
"Milioni moja na nusu."
"Milioni moja na nusu zote unanunua simu?"
"Alininunulia mama alipokwenda nje kibiashara."
"Usihofu nitakupa pesa sasa hivi ili akija umpe akakununulie."
Tell me alimpa Gift Milioni mbili taslimu na kumuaga huku Gift akisisitiza amsubiri mama yake arudi iliamuone. Lakini Tell me alimuomba radhi siku nyingine. Aliondoka na kumuacha nyuma Gift akimsindikiza kwa macho.
***

Gift alikuwa anaona kama njozi ya mchana na kuona watu wana pesa za mchezo mtu kumwambia kiasi kikubwa cha pesa kiasi kile lakini hakuteteleka wala kuguna. Alijiona mpumbavu pale alipomkisia kamchulia simu yake. Akiwa bado akizihakiki zile pesa mara mama yake aliingia na kumkuta akiwa bado amezishikilia mkononi alishangaa kazitoa wapi ulibidi amhoji mwanaye.
"He! Mwenzetu pesa zote hizo umezitoa wapi?"
"Kanipa yule kaka aliyenigonga."
"Za nini?"
"Za simu yangu."
"Ulimdai?"
"Hapana ila alipokuja aliniuliza kama nina simu ili tuweze kuwasiliana kujua hali yangu, ndipo nilipomweleza kuwa simu yangu imepotea siku ya ajali."
"Ehe ikawaje?"
"Basi aliniuliza simu ya aina gani na dukani unauzwa kiasi gani? Nilimwambia milioni moja na nusu nilishangaa anafungua mkoba wake na kunipa hela hii."
"Kwa nini usiikatae?"
"Mama kuna mtu anakataa pesa wewe hutulii nyumbani kwa ajili ya pesa, tena siyo ananihonga bali ananilipa simu yangu."
"Sio hivyo mwanangu unajua mtu aliyejitolea kuokoa maisha yako kukuleta hospitali ya gharama kama hii.Kitu kingine cha ajabu bado amekuja kukujulia hali na kadi ya pole na maua amekuletea pamoja na matunda....pesa nini mwanangu kwani mimi ningeshindwa kukunulia simu nyingine?" Mama Gift hakufurahishwa na kitendo cha mwanaye kumlipisha simu.
"Lakini mama mimi sikimdai amenipa mwenyewe."
"Oooh, tuachane na hayo, haya huyo kijana yupo wapi?"
"Nina imani umepishana naye alikuwa na haraka amepigiwa simu."
"Kwa nini hukuniita nikaja kumjua inaonyesha ni kijana mwema mwenye roho ya huruma."
"Mama nimemsihi akusubiri alikubali lakini kuna simu amemfanya aondoke haraka lakini kanipa bussines card kama nikinunua simu nimjulishe."
"Itakuwa vizuri nitamualika chakula cha jioni utakapotoka hospitali."
"Itakuwa vizuri mama yule kijana wa ajabu sana ni mpole na mcheshi vilevile nimeambiwa ni mmoja wa wafabiashara maarufu."
"Pesa sio kigezo tabia ni moyo wa mtu...," mama Teddy alikatishwa na hodi iliyokuwa ikigongwa.
"Karibu ingia." mama Teddy alikaribisha, mlango ulifunguliwa alikuwa ni Mkuu wa chuo aliyeongozana na baadhi ya wanafunzi miongoni ya wanafunzi alikuwepo shoga yake Eliza.
Gift alipomuona moyo ulimpasuka alitamani ammeze kwa kumuona ni adui yake namba moja. Lakini aliificha hasira yake angekuwa peke yake angemfukuza kama mbwa mwizi. Lakini ndiyo hivyo yupo mbele ya mkuu wa chuo na mama yake na wanafunzi wenzie pia hakutaka siri yao kila mtu aijue.
Baada ya kumpa pole Mkuu wa chuo na wanafunzi waliaga na kuondoka na kumwacha mama Gift na mwanaye. Naye mama Gift aliingia mjini kwa ajili ya shughuli zake za kibiashara na kumwacha mwanaye akiwa amepumzika.
Gift akiwa amefura kwa hasira baada ya Eliza kuja kumsanifu alijikuta akijiapiza moyoni kuwa akitoka salama atahakikisha anamshikisha adabu. Akiwa katikati ya mawazo mlango uligongwa aliacha kuwaza kukalibisha.
"Pita ndani"
Mlango ulifunguliwa aliyeingia alimfanya Gift azidishe hasira na kujikuta akibwata kwa hasira kwa sauti ya juu.
"We mbwa umerudi kufanya nini?" Alimfokea Eliza aliyerudi kuomba msamaha.

Nini Kitaendelea? Ili kuyajua yote endelea kufuatulia
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 07
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Baada ya kusema yale Eliza alianza kulia kitu kilichofanya Gift anyanyuke kitandani na kwenda kumbembeleza.
“Pole sana rafiki yangu.”
“Gift inauma umasikini huu utaendelea kutudhalilisha mpaka lini?”
“Najua nakuahidi kukusaidia rafiki yangu najua mimi nimeumia lakini wewe umeumia mara mbili kwa vile hukufanya kwa ridhaa yako tofauti na mimi.”
Gift alisahau yake na kumtia moyo Eliza aliyekuwa akilia kwa majuto.
SASA ENDELEA…
***************

Ilikuwa siku ya jumapili Gift akiwa na shoga yake ambaye shuleni wapambe waliwabatika kama wake wenza kwa ajili ya kutembea na mwanaume mmoja. Kwa vile msimamo wao ulikuwa mmoja wa kumkomoa Kanuth hilo halikuwashtua walikuwa na siri yao nzito.
Wakiwa wanajisomea chini ya mti kwa mbali lilisimama gari moja la kifahari aina ya Lange lover Vogue ya rangi ya nyeusi. Hawakuijali baada ya kuisifia tu kuwa gari zuri waliendelea na masomo yao. Sauti ya juu iliyokuwa ikimwita Gift ilimfabya aache kusoma na kuangalia ni nani.
"Gift mgeni wako huyo," Eliza alisema huku alimuangalia vizuri mgeni wa kiume ambaye alikuwa mgeni machoni mwake.
Kila alivyokuwa akisogea naye alimwangalia vizuri, alikuwa kijana mmoja mtanashati aliyekuwa kwenye suti nzito alijiuza ni nani. Macho yalipotulia alimkumbuka lakini jina alikuwa amemsahau.
Bila kijielewa alijikuta ametupa vitabu na kukimbia kumpokea kwa kumkumbatia.
"Oooh! Kaka karibu."
"Asante, upo sawa?"
"Kama chuma si unaniona!"
"Vizuri, mrembo hujambo?" alimgeukia Eliza aliyekuwa bado amepigwa butwaa.
"Sijambo shemeji."
"Eliza tabia gani mtu hujatambulishwa unapayuka."
"Samahani shoga...karibu kaka..nani sijui?"
"Gift atakutambulisha."
"Huwezi amini jina lako nimelisahau.. hebu ngoja nikumbuke Mr listen kama sikosei..oooh nimekumbuka talk to me."
"Ngoja nikukumbushe naitwa Niambie kwa nini umelisahau jina langu wakati hata kadi nilikupa."
"Oooh nimekumbuka Tell me why....Oooh karibu sana kaka tell me why ni kweli nilikuwa na kadi ambayo nilimpa mama ili siku nitayotoka tukualike tujumuike pamoja kwa chakula cha usiku mama alikuwa na hamu ya kukuona.
"Lakini aliondoka siku moja baada ya mimi kutoka hospitali na kupanga tutakualika, kibaya hata kadi yako aliondoka nayo na mimi sikuwa nimeiandika pembeni. Nilikuwa na hamu ya kukuona lakini ndivyo hivyo ilibidi namsubiri mpaka mama arudi."
"Mmh! Tuachane na hayo, vipi hali yako unajua sikujisikia vizuri kutokujua maendeleo yako kibaya zaidi msomi ambaye ni tegemeo la taifa," Tell me alisema huku akichanua tabasamu mwanana.
"Tegemeo wapi kila kukicha tunanyanyapaliwa na serikali."
"Lakini si mambo yametulia."
"Sawa yametulia lakini jasho limetutoka kila siku mpaka mishipa ya shingo itusimame. Wao mbona huwa hawaandamani kuongezana posho wamesahau na wao wamesoma bure lakini wenzao ndio watukamue."
"Hata nyinyi mkifika juu mtakuwa hivyohivyo, wangapi walisema lakini wamepata wamesahau ahadi zao njaa mbaya ukiwa na njaa utatoa ahadi za ajabu hata kuvuta meli kwa mkono ili upate chakula ukishiba unawageuka kwa kuwauliza ni nani mwenye uwezo wa kuvuta meli kwa mkono wewe atakuwa wa pili."
"Mr Tell me why mbona unatetea au una mpango wa kugombania Ubunge?"
"Siku zote kweli utafutiwa sababu ili kuonekana si kweli."
"Umeshinda, tuachane na hayo karibu kazini kwetu hapa ndipo tunapo itafuta sembe."
"Ninashukuru huwezi kuamini kukaa kwangu kote jijini sijawahi kufika chuoni hapa."
"Muongo mtu maarufu kama wewe usifike sehemu kama hii."
"Gift yaweza kuwa kweli pengine hana shida napo aje afanye nini?" Eliza alimuunga mkono Mr Tell me.
"Kwanza mimi si maarufu kama anavyosema, ningekuwa maarufu angepoteza kadi yangu na kushindwa kunipata."
"Mmh! Tell me imekuwa sababu..basi nisamehe leo simu ninayo najua sasa kesi itaisha."
"Kuwa na simu siyo sababu muhimu mawasiliano."
"Sasa utanichoka usijesema karaha au kumuudhi wifi."
"Ni hapo nitakapokuwa naye....Sasa Gift nina imani kidogo moyo wangu utaridhika au kutulia baada ya kupata kujua hali yako. Nimefarijika sana kukuta mzima wa afya tena ukibukua."
"Hata mimi nimefurahi huwezi kuamini siri ipo moyoni mwangu ipo siku nitakwambia. Tell me why kila dakika unanifanya niwe mwanafunzi wako wa kujifunza tabia za watu na kufuta dhana kuwa baadhi ya viumbe si wabaya ila kiumbe mmoja ndiye anayeweza kutia doa na kusababisha kuona wote ni wabaya....wewe ni mfano wa kuigwa."
"Kwa nini unasema hivyo?"
"Ni vigumu kuamini japo ni muda mrefu nashangaa kuona kama nilikuwa nawe siku zote na kujiona mpweke pale utakapo niaga na kujuta kwa nini nimekufahamu."
"Gift una maana gani?" Maneno ya Gift yalimchanganya kidogo Tell me.
"Ni vigumu kuwa wakili wa moyo wako, hasa sisi wanawake pale moyo unapoingia gerezani pasipo kosa wakati mtetezi yupo ambaye ni muoga kuutetea moyo ambao huteseka bila kosa."
"Ninaweza kuwa nimekuelewa lakini huenda vilevile sijakuelewa hebu niweke wazi una maana gani kama sivyo nifikiliavyo?" Maneno ya mafumbo yalizidi kumwweka njia panda.
"Sio siri kila muda kila dakika kila nikikufikiria nakosa jibu kuwa wewe ni kiumbe wa aina gani hata mama yangu mzazi alikusifia kwa yote uliyonitendea nashindwa nikilipe nini...ili isiweze kukupoteza ili nami uuone ukarimu wangu."
"Sihitaji malipo yoyote kutoka kwako...ilikuwa ni wajibu wangu kama mwanadamu kuonyesha ubinaadamu hasa pale unaposababisha maumivu kwa mwenzio japo ilikuwa bahati mbaya."
"Lakini elewa Tell me why siku zote hesabu huanzia moja, lakini kwa upande wangu naomba ifike kumi na moja nina imani unaijua hesabu hii hutumika hasa kanisani, moja na moja huwa moja kibinaadamu huwa kumi na moja naomba hesabu yetu iende kikanisa ili tupate moja."
"Nimekuelewa kuliko ulivyozungumza nipe muda."
"Umenielewa nini Tell me why?"
"Nina imani mzigo ulionipa umeufunga hukutaka kila mtu aujue kwa mimi muungwana nimekuelewa kwa hiyo wacha nikauangalie kama unapendeza hauna kipingamizi."
"Nitafurahi kama kile nilichokiota mchana kinakuwa kweli nimeamini unaweza kuota huku ukiwa macho."
"Umeota nini tena Gift?"
"Nimeota moja na moja ni moja wala si mbili wala kumi na moja."
"Mmmh kweli wewe msomi unayeongea kwa mifano isiyoonekana kwa macho wala kwa akili nyepesi bali kwa yule aliyezama chini ya maji ndiye hugusa mchanga mweupe."
"Hakika kila asimamae kwa ajili ya nafsi yake huiokoa nafsi yake."
Tell me why alimuaga Gift ambaye alimsindikiza hadi kwenye gari lake aliwaaga na kuondoka huku akimuacha Gift kwenye mtihani mzito wa moyo wake na kujiuliza ni kweli turufu aliyoitupa ni kubwa kuliko ya mpinzani wake au ndio imemezwa na kubwa zaidi kama samaki mdogo kuliwa na mkubwa.

Nini Kitaendelea?
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 08
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
"Hakika kila asimamae kwa ajili ya nafsi yake huiokoa nafsi yake."
Tell me why alimuaga Gift ambaye alimsindikiza hadi kwenye gari lake aliwaaga na kuondoka huku akimuacha Gift kwenye mtihani mzito wa moyo wake na kujiuliza ni kweli turufu aliyoitupa ni kubwa kuliko ya mpinzani wake au ndio imemezwa na kubwa zaidi kama samaki mdogo kuliwa na mkubwa.
SASA ENDELEA…
*****
Huo ndio ukawa mwanzo wa mahusiano ya karibu kati ya Tell me why na Gift. Tabia ya Gift ya msimamo na kupenda kujua mambo na muda wote alipenda kuwa muwazi. Ilimvutia Tell me why na kumuona ni msichana anayefaa kumuoa. Alimsubiri amalize masomo yake ili waweze kuwa karibu zaidi, kwa vile muda uliokuwa umebaki ni wa mtihani wa mwisho.
Alipomaliza tu mtihani alijiachia na muda wote kuwa karibu ya Tell me why.
Tabia za Gift kila dakika zilimvutia Tell me na kuamini kabisa mwanamke wa ndoto yake ni Gift. Siku moja Tell me why alimueleza ukweli Gift juu ya kuvutiwa kwake na tabia zake na kila alichokitaka kwake alikuwa nacho na zaidi.
Alimjulisha kuwa anataka kukamilisha ile hesabu ya moja na moja.
Gift aliona kama miujiza ile ndoto yake inakaribia kutimia alimuomba Mungu itimie kweli. Tell me alimuomba ndoa yake ifanyike upesi upesi kwa kuwa alikuwa na shughuli nyingi.
Kwa kuwa mama yake alikuwa nje kikazi Gift alimuomba waiahirishe mpaka hapo atakuapo rudi mama yake, kauli ile ilimfanya Tell me ahoji..
"Ina maana mzazi wako wa kiume amekwisha kufa?"
"Hapana."
"Kwani yeye hawezi kusimamia ndoa yako?"
"Anaweza lakini aliachana na mama kila mtu yupo kivyake."
"Hata kama wapo kivyao, lakini baba yako bado ana nguvu ya kusimamia ndoa yako."
"Mama lazima atakasirika ikiwezekana hata kuivunja ndoa yetu."
"Kwani akivunja wanawake wamekwisha?"
"Sivyo hivyo, nitakuwa nimeathirika mimi."
"Kauli yako imenifanya nihoji ni nani aliyevunja ndoa ya wazazi wako wawili?"
"Ni mama."
"Nilijua, kwa nini?"
"Toka alipopata pesa kwenye biashara zake na baba kumwekea mipaka hapo ndipo alipo lazimisha talaka. Japo baba alikuwa hapendi kumwacha, mama alimpeleka baba mahakamani kumdai talaka ambayo ilitolewa mbele ya Hakimu."
"Baba yako ana kazi gani?"
"Ni mtumishi wa umma aliyesitaafu."
"Ana shughuli gani?"
"Ana mashine ya kusagia unga na Heace mbili."
"Unamuheshimu baba yako?"
"Tena sana, kitendo cha mama cha kumwacha baba na kumliza mzee mzima mahakamani akimlilia mama, kiliniumiza moyo na baba aliapa hataoa maishani mwake mpaka anakufa. Japo mama yeye anapenda ujana humchukua mwanaume yoyote amtakaye kwa gharama yoyote. Kitu kinachonitisha na kama hivyo amezaa na kijana mmoja Arusha ambaye hamjui jina wala sura hamkumbuki japo amesema mdogo wangu anafanana na baba yake copy right, unajua nini Tell me kwa mfano.
"Wewe ni kijana bado unadai vilevile una matamanio ya kimwili na mama yangu ni mtu mzima anayekwenda na wakati kwa bahati mbaya wewe nawe mwanadamu unaweza kukutana naye bila kumjua kama mkweo katika biashara zenu na kumchombeza unarudi nyumbani nakutambulisha kuwa huyu ndiyo mkweo sijui hapo kutakuwa na picha gani?"
"Itakuwa mbaya tutashindwa kutazamana usoni tumuombe Mungu ayaepushe haya."
"Ndiyo maana nikaitafuta hesabu ya moja kwa moja yenye jibu ya moja yaani ndoa ya watu wawili huzaa mwili mmoja."
"Naomba twende kwa baba yako mpe heshima kama inavyo sitahili."
"Wacha niwasiliane na mama kama ataweza kuwahi ili wajumuike wazazi wangu wote."
"Itakuwa vizuri basi tuonane baadaye kujua umefikia wapi...sitaki uifute shauku ya moyo wangu, elewa wewe ndiye uliye ushawishi naogopa usije uudhi."
Waliagana Tell me why na Gift, jioni ya siku ile aliwasiliana na mama yake ambaye alimjulisha atachelewa kurudi na kuomba radhi kwa kuwa tayari kulipa gharama yote ya harusi. Alimuomba baba yake awe msimamizi wake, lakini mama yake alikataa katakata kwa kusema gharama za maisha ya Gift anazijua yeye umiliki wa Gift uliishia pale walipoachana tu siku alipotoa talaka mahakamani.
Gift alijua kama atamweleza Tell me why, yale aliyoongea na mama yake mume atamkosa. Aliamua kutunga uongo pale alipokutana na Tell me why kwa kumwambia kuwa mama yake amekubali baba yake awe msimamizi wake. Kauli ile ilimfanya Tell me why afurahi sana na kupanga siku ya pili kwenda kwa baba yake mzee Edgar Bilikila
Siku ya pili waliongozana hadi kwa mzee Bilikila ambako walipokelewa kwa furaha na bashasha. Gift baada ya kumtambulisha mchumba wake alieleza sababu kubwa iliyowapeleka pale. Mzee Bilikila alishangaa na kuhoji.
“Leo mtoto wa mama umekuja mimi baba yako maskini nikuoze na mama yako je?"
"Mama hayuko ila amesema wewe uendelee na shughuli zote bado mizunguko yake haijaisha."
"Sipendi kuongea mengi kwa vile wewe mwanangu upo peke yako nilikuwa na haki ya kukataa. Lakini nitakuwa sikukutendea haki, kingine ni mtoto uliyeonyesha mapenzi ya dhati kwa mimi baba yako pamoja na mama yako kukukataza."
"Baba wewe ndiye baba yangu sina mwingine, baba huwa najisikia uchungu kwa kitendo cha mama cha kukuacha kwa ajili ya pesa namuomba Mungu nisifuate nyayo za mama ili niwe mtiifu kwa mume wangu nimpende kwa shida na raha kwa kuwa fedha ni matokeo fedha zinaweza kukupa sifa pia hizohizo zikakudhalilisha."
"Ni kweli mwanangu kauli yako inaonyesha ni kiasi gani ulivyopevuka na pesa si msingi wa maisha pale unapozitumia vibaya...mwanangu ninakupa baraka zote ili uolewe na mumeo. Na wewe baba nakuomba uwe mume mwema lakini uwe makini kwa hawa wanawake japo mwanangu sipendi awe na tabia kama za mama yake."
"Nashukuru kwa nasaha zako baba namuomba Mungu ampe mke wangu mtalajiwa akili na upendo ili ndoa yetu itenganishwe na kifo."
"Amen."
Baada ya kupata idhini ya kumuoa Gift Tell me alirudi mjini kufanya taratibu zote za ndoa ambazo nazo zilikwenda kwa haraka sana. Ndani ya wiki mbili ndoa ilifungwa rasmi na Gift kuwa mke wa Tell me why.
Gift alikuwa na siri moyoni juu ya kauli ya mama yake alijua akirudi lazima kutakuwa na matatizo hata kufikia hatua ya kutoitambua ndoa yao. Lakini alijipanga kwa ajili ya kukabiliana na mama yake na kuwa tayari kwa lolote, wala hakumtaarifu kuwa ameisha funga ndoa.
***
Tell me why alianza maisha kwa mafanikio makubwa na kujilaumu kwa kuchelewa kuoa, lakini alijua kama angewahi kuoa asingepata mwanamke kama Gift alijua ni zawadi aliyopewa na Mungu. Ndani ya wiki mbili alikuwa tayari ameisha cheka na nyavu, mwezi ulikatika Gift akiwa mjamzito. Mimba nayo ilimpenda alizidi kunawili na kupendeza. Wakiwa wamekaa sebuleni Gift alimtania Tell me.
"Mmh sikuwezi."
"Kwa vipi mpenzi?"
"Yaani kugusa tu bao.”
"Siku zote biashara mapema na mshambuliaji mzuri si mpiga cheka bali mpiga mabao.”
"Siyo unizalishe kama mlea kambi ya yatima."
"Wanne wanatosha."
"Mmh! Wengi wawili tu."
"Lazima wawe wanne yaani wawili kwenu na wawili kwetu."
"Mmh, haya kazi kwako kulima kwa bidii."
Mara simu ililia wote walishtuka kwa uchovu Gift aliichukua na kuongeam ilikuwa inatoka kwa mama yake.

Nini Kitaendelea?
 
SEHEMU: 09
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
"Mmh! Wengi wawili tu."
"Lazima wawe wanne yaani wawili kwenu na wawili kwetu."
"Mmh, haya kazi kwako kulima kwa bidii."
Mara simu ililia wote walishtuka kwa uchovu Gift aliichukua na kuongea ilikuwa inatoka kwa mama yake.
SASA ENDELEA…
"Haloo mama Shikamoo."
“Marahaba.”
“Leo umetukumbuka, za siku?”
"Nzuri vipi hali yako?"
"Mimi sijambo sijui wewe?"
"Kwa kweli mimi mzima wa afya japo mambo yangu ni mengi lakini nakuja mara moja wiki ijayo kusimamia harusi ili nirudi kwenye shughuli zangu."
"Hamna tatizo mama."
Gift alimficha mama kuwa amekwisha olewa na sasa hivi ni mke wa mtu. Aliogopa malumbano ya ndani ya simu, vile vile mama yake angeweza kughaili kuja Tanzania. Aliamua amuache ili aje ajionee mwenyewe mkwewe ambaye anashida naye ya kumuona kama mwanga kwa kipofu.
Baada ya mazungumzo Gift alimgeukia mumewe.
"Honey mama anakuja wiki ijayo."
"Oooh vizuri hata mimi nina hamu naye."
WIKI MOJA BAADAYE
Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu J.K.Nyerere majira ya saa nne Gift akiwa na mumewe waliwasiri uwanja pake kumsubiri mama Gift ambaye alikuwa akiwasiri siku ile. Waliwahi nusu saa kabla ndege ya shirika la ndege la Swiss air kuwasiri. Wakiwa wametulia sehemu ya kupokelewa wageni tangazo liliwajulisha kuwa wakati wowote ndege ya shirika la Swiss air itawasiri.
Wote waliokuja kupokea wageni wao walikaa tayari kuwapokea wageni wao. Gift na mumewe Tell me why nao walijitayalisha kumpokea mgeni. Saa nne juu ya alama ndege iliwasiri na abiria walianza kushuka mmoja mmoja. Kila aliyekuja kupokea mgeni wake alipepesa macho ili amuone.
Gift alipepesa macho kwenye foleni ya wageni waliokuwa wakitoka kwenye msafara mmoja. Mara alimuona mama yake alijikuta akipiga ukelele
“Mamaaa.”
"Wawooooo mwanangu."
Mama yake na yeye alijikuta akiachia kigari cha mizigo na kumkumbatia mwanaye.
"Jamani mwanangu."
Wakiwa wamekumbatiana Tell me why alikuwa pembeni akiangalia furaha ya mama na mtoto, baada ya kuachiana Gift alimtambulisha mumewe kwa mama yake.
"Mama kutana na mkweo ambaye ulikuwa na hamu ya kumuona lakini sasa ni mume wangu."
"Oooh baba nimefurahi kukuona," alisema huku akijitoa kwa Gift na kumkumbatia.
"Hata mimi."
Waliongozana hadi kwenye gari na kurudi mjini, wakiwa njiani mama Gift alitaka kujua ile hali ya mwanaye kuwa katika ujauzito bila kufunga ndoa.
"Haya mama tutayaongelea nyumbani humu sio pahala pake."
Mama Gift hakutaka kuongeza neno akilini mwake alijua mwanaye bado hajafunga ndoa na haikuwa vizuri mtu akiwa akisubiri ndoa akubali kubeba mimba.
Baada ya kufika nyumbani walimwacha mama yao ajipumzishe ili jioni wapate muda wa kuongea naye. Kwa upande wa mama Gift alikuwa amempotea kabisa Tell me why kwa kuwa hata kimawazo asingeamini mchoma nyama kuwa tajiri mkubwa namna ile.
Hata Tell me naye hakumtilia maanani mama Gift siku waliyokutana kwa mara ya kwanza kwa hiyo sura yake haikuwa kwenye kumbukumbu kabisa alimwona mtu kama mtu. Na kwa muda ule alimchukulia kama mama mkwe.
Jioni walikwenda kwa mama Gift kwa mazungumzo ya safari na mipangilio aliyokuja nayo mama Gift. Ilikuwa baada ya chakula cha usiku majira ya saa tatu na nusu wakiwa sebuleni Mama Gift alitaka kujua mpaka sasa matayalisho ya harusi yamefikia wapi.
Tell me alishtuka kusikia kauli ile ilibidi amgeukie Gift kwa kumuuliza kwa macho kuwa mama ana maana gani.
"Mama sina budi kwanza nikuombe msamaha kwa kukiuka kauli yako, pili kusema uongo kwa baba nilikuwa sina jinsi. Ukweli nimeisha olewa huu ni mwezi wa pili na sasa hivi mimi ni mzazi mtarajiwa."
"Atiii..unasemaje Gift umeolewa kwa idhini ya nani?"
"Ya baba."
"Nilikwambiaje?"
"Kumbuka mimi ni mtoto wa pande mbili na mwenye madaraka ni baba yangu siwezi kumdharau baba yangu bila yeye mimi nisingekuwepo," Gift alijibu kwa kujiamini.
"Baba yako ni nani mbona mdogo wako amepatikana bila baba yako hata wewe ungepatikana bila yeye. Kwanza nilifanya makosa kuolewa na mtu maskini kama yule."
"Mama bila baba nisingezaliwa mimi, angezaliwa mwingine kaa ukielewa namheshimu baba na nitaendelea kumheshimu sioni kosa lake kwako zaidi ya kumdhalilisha kwa umasikini wake."
"Gift unanivunjia adabu mbele ya mumeo lakini amini ndoa mliyofunga ni batili mimi siitambui."
"Kama huitambui sio juu yako mimi sasa hivi ni mke wa mtu na baba yangu ndiye msimamizi mkuu."
"Na huyo baba yako atanitambua atatoaje idhini anajua gharama za malezi yako?"
"Hakushindwa bali ulining'ang'ania," Gift alimpasulia mama yake.
"Gift leo umenigeuka?"
"Kwa mtindo huo sipo pamoja nawe," Tell me aliyekuwa kimya ilibidi aingilie kati.
"Samahanini japo sijui kwa undani, sidhani kama mmeachana ifikie hatua ya kuchukiana kiasi hicho. Siku zote kiunganisho cha familia ni watoto nakuomba mama mkwe tuliza munkari, tumieni ndoa yetu ili kurudisha mahusiano."
"Itakuwa ngumu."
"Hata kama kwako ni ngumu lakini baba yangu nampenda tena kwa taarifa yako kila siku ilikuwa lazima nionane naye mawazo yake ndiyo leo yamenipa muongozo na kuwa mke mwema kwa mume wangu. Kama ningefuata tabia zako siwezi kukaa na mwanaume.
“Mama tabia yako hainifurahishi naogopa kuishi maisha unayoishi ni madhara makubwa wala hayana mafunzo kwetu sisi wanao. Nikikufuata siwezi kujenga nyumba yangu pesa si kitu kama utu wa mtu," Gift alizungumza huku akilia kwa kutoa machungu ya muda mrefu ya tabia ya mama yake.
"Nini kilichopunguka kwangu?" Mama Gift alihoji.
"Hukioni mdogo wangu baba yake ni nani?"
"Baba siyo muhimu, cha muhimu malezi anawazidi hata hao wenye baba."
"Siku akimtaka baba yake utamwambia nini?"
"Gift hujakuwa,wewe huwezi kunihikumu."
"Nikuhukumu kwa lipi zaidi ya kukueleza ukweli, isifikiri nafurahia kitendo cha kumuacha baba roho inaniuma. Umasikini sio sababu ya kumuacha mtu, mangapi baba alikufanyia mpaka ukawa hapo na chanzo chote cha baba kuwa kwenye hali ile ni wewe kwa kumtapeli pesa zake," Gigt kwa uchungu aliamua kumvua nguo mama yake mbele ya mumewe.
"Gift hapa sio wakati wake," Tell me aliingilia kati kwa kuona marumbano yamekuwa makubwa na mwelekeo wake ni mbaya.

Nini kitaendelea?
 
SEHEMU:10
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
.ILIPOISHIA:
"Gift hapa sio wakati wake," Tell me aliingilia kati kwa kuona marumbano yamekuwa makubwa na mwelekeo wake ni mbaya.
SASA ENDELEA…

Tell me alimuondoa mkewe ambaye alionekana kughadhibika na tabia za mama yake. Alimuondoa huku Gift akiwa analia na mama yake akiwa amepingwa na bumbuwazi asiamini aliyokuwa akizungumza mwanaye na kujiuliza ujasili ule kautoa wapi.
Hata walipofika nyumbani Gift alikuwa bado analia kitu kilichomfanya Tell me aingie kazi ya kumbembeleza mkewe.
"Basi Honey yameisha si tumeisharudi?"
"Yaani wewe hujui basi tu mama yangu amenizaa lakini sina haja naye kwanza malezi gani anayonilea muda mwingi yupo kwenye biashara zake bila baba sijui ningekuwa kwenye hali gani?"
"Kwani nini kilichofanya mama na baba yako watengane?"
"Ni hadithi ndefu, mama yangu kabla ya kuolewa na baba alikuwa akifanya biashara ndogo ndogo. Wakati huo baba alikuwa ni mfanyakazi serikalini. Sielewi kama mama wakati ule alimkubali baba kwa kuwa alikuwa na pesa nyingi.
“Kwa maelezo ya baba, mama alipewa kila alichotaka kwa vile baba alikuwa akimpenda sana mama alijikuta akiiba vitu vingi na kuviuza na pesa zote alimpa mama. Baba alikiri ndoa yao ulitawaliwa na matumizi makubwa yaliyofanya baba awe na kazi ya ziada kuhakikisha nyumba haiteteleki.
“Lakini kama hujuavyo kila kitu chenye mwanzo hakikosi mwisho, serikali iliposhtuka mirija ya pesa ya baba ilizibwa na kujikuta akitegemea mshahara tu. Hapo ndio ukawa mwanzo wa matatizo ya mama kutaka vitu vya bei ya juu na matumizi makubwa wakati akijua hali ya baba...
“Hapo ndiyo ukawa mwanzo wa dharau na kujiamulia vitu anavyotaka, baada ya baba kustaafu alilipwa malipo yake hapo mama aliomba nusu ya malipo ili afanyie biashara. Pamoja na dharau baba bado alikuwa na mapenzi na mama alimpa kiasi anachotaka.
“Mama alianza biashara za nje ya mkoa ambazo siku nyingine zilitumia wiki hadi mwezi. Kumbe mama alikuwa na biashara mbili ya kununua vitu na kuuza na ya mwili. Kwa muda mfupi mama alijulikana na kuwa na pesa nyingi kwa kuwa alihujumu ndoa yake na matajiri.
“Hapo ndipo alipoanza biashara za kusafiri nje ya nchi, wingi wa pesa uliongeza kiburi na dharau kwa baba wakati huo baba hela yake ilikuwa ndogo kwa kutegemea mashine yake ya kusaga na gari zake mbili za kubeba abiria. Taarifa za mama kutokuwa muaminifu kwenye ndoa yake ilimfanya baba ampige marufuku kufanya biashara ile.
Hapo ndipo mama alipoota mapembe na kulazimisha talaka baba alipokataa mama alifungua kesi mahakamani na kufanikiwa kuivunja ndoa yake bila malipo yoyote. Wakati huo nilikuwa na miaka kumi na tano mama alinichukua na kunikataza nisiende kwa baba. Jambo ambalo kwangu lilikuwa gumu baba yangu nilikuwa nampenda muda mwingi nilikuwa naye karibu.
“Nilimkubalia mama kwa mdomo lakini muda mwingi mama akiwa hayupo nilikwenda kwa baba na kushinda siku nyingine hulala huko huko. Toka mama aachane na baba amekuwa na tabia mbaya ambazo kwa upande wangu sikupaswa kuziona wala kuzisikia lakini kwa mama yangu aliona ni jambo la kawaida.
“Tabia mbaya ambayo ilibidi hata mimi mwanaye nimkemee ni tabia ya kukosa ustaarabu kwa kutembea ovyo na wanaume bila kijali lika wala umri. Kibaya zaidi toka awe na pesa amekuwa akiwahonga wanaume nilimweleza mama kuwa tabia kama ile ni mbaya sana anaweza kuchangia mwanaume na mimi mwanaye tutaangalianaje.
Nilimuomba atafute mwanaume mmoja ambaye atamfaa na kuwa mumewe japo nilimuomba amrudie baba bila mafanikio kwa upande wa baba kutokana na mapenzi na mama alikubali wakati wowote. Ninachoshukuru kitu kama hicho hakijatokea nimeweza kuolewa bila kutokewa na kitu cha aibu. Hebu fikiria mama yangu kila sehemu akifika anatafuta bwana kwa hela zake.
Kibaya hata aogopi gonjwa la ukimwi ukimuuliza anasema anajali kama angekuwa anajali mtoto amempataje.
"Kingine kibaya hata aliyempa mimba amemsahau alikutana naye siku moja usiku akiwa kwenye safari zake na hata alipomfuata alikuta ameacha kazi."
"Ni wapi huko?" Tell me aliuliza.
"Hata najua, ukimuhoji sana unaonekana umekosa adabu."
Kwa kuwa muda ulikuwa umekwenda waliamua kupumzika na kulala mpaka siku ya pili.
****
Mama Gift hakuamini maneno ya mwanaye yaliyokuwa na ukweli mtupu. Aliamua siku ya pili kwenda kwa mwanaye kumuomba msamaha na kuwaacha ndoa waendelee yao.
Aliwasiri kwa mwanaye majira ya saa nne asubuhi na kuwakuta Gift na mumewe akiwa wametulia sebuleni, Gift akiwa amemwegemea mumewe kifuani kwenye sofa.Walipomuona walimkaribisha kwa furaha kama jana hapakuwa na malumbano yoyote.
Mama Gift akiwa ameongozana na Mwanaye ambaye alifanana sana na Tell me Why, lakini hakuwa na wazo kuwa atakuwa baba yake hakuamini kama mchoma nyama anaweza kuwa siku moja tajiri mkubwa.
Tell me alimpokea shemeji yake na kukaa naye karibu, naye mama Gift alitumia muda ule kumuomba msamaha mwanaye na kukubaliana na kile kilichotokea bila idhini yake.
"Mama mimi sina kinyongo na wewe kwa kuwa nilichokifanya nilikuwa na haki kufanya vile."
"Nimefurahi kusikia hivyo la muhimu ni kurudisha mapenzi yetu ya awali."
"Mama kama nilivyokueleza mimi sina kinyongo na wewe jisikie amani moyoni mwako."
Wakati wakiongea Gift aliponyanyua macho alikuta na kitu ambacho kilimfanya aongee kwa sauti.
"Mume wangu yaani mlivyofanana na mdogo wangu mtu akiingia atajua wewe ndiye baba yake."
"Duniani wawili wawili huenda baba yake tunafanana."
Kauli ile ilimfanya mama Gift kunyanyua macho kuangalia kile alichokuwa akikisema mwanaye. Alimwangalia mwanaye kisha Tell me ilijikuta moyo ukimshtuka baada ya kugundua mwanaye anafana sana na Tell me kwa kiwango kikubwa.
Picha ya Tell me ilionekana si ngeni kwenye ubongo wa mama Gitf, alijikuta akimuuliza Tell me labda anaweza kuwa na mahusiano na mtu ambaye ni mzazi mwenzie.
"Samahani baba sijui umeishawahi kukaa Arusha?"
"Ndiko nilipozaliwa."
"Mmh! Hotel ya New Arusha Hotel unaijua?"
"Aah, mbona pale nimefanya kazi sana."
"Kipindi gani?"
"Mwaka wa tano sasa."
"Wa tano?" Mama Gift aliuliza kwa mshangao.
"Ndio mama."
"Ulikuwa unafanya kazi gani?"
"Unajua mama maisha haya huwezi kuamini hatua mtu alizopitia hata leo kuwa kwenye maisha haya. Hata mke wangu niilisha mweleza kuwa siku zote mwanadamu usikate tama, hujui Mungu mbele amekupangia nini. Maisha niliyokuwa nikiishi siamini.
“Lakini ukweli utabakia pale pale yalikuwa maisha ya kubahatisha, pale nilikuwa nafanya kazi upande wa jikoni nilikuwa mtaalamu wa kuchoma nyama. Mshahara tuliokuwa tukipata mdogo sana ilikuwa laki moja kwa mwezi.
“Lakini siku zote malengo ndio njia pekee ya kukukomboa pale upatapo kidogo. Nilipanga kama nitapata pesa basi ningekuja hapa jijini kufanya kazi ya kuuza mitumba rafiki yangu mmoja alinieleza nitafute laki moja. Lakini siku moja nilipata zali la kupata laki tano. Nikaona nasubiri nini? Kesho yake nikatimkia Dar. Mungu akaniangazia mpaka leo hii nipo hivi."
Ilikuwa simulizi iliyoushitua moyo wa mama Gift na kujikuta akitafuta ukweli zaidi kwa kumchimba Tell me.
"Kwa hiyo baba ulipoondoka hukuwaaga wenzako?"
"Sikumuaga yoyote sikupenda mtu ajue mipango yangu, labda rafiki yangu mmoja wa karibu ambaye kwa sasa ni marehemu."

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU:11
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Ilikuwa simulizi iliyoushitua moyo wa mama Gift na kujikuta akitafuta ukweli zaidi kwa kumchimba Tell me.
"Kwa hiyo baba ulipoondoka hukuwaaga wenzako?"
"Sikumuaga yoyote sikupenda mtu ajue mipango yangu, labda rafiki yangu mmoja wa karibu ambaye kwa sasa ni marehemu."
SASA ENDELEA

"Mmh! Unajua baba simulizi yako haina tofauti na ya shoga yangu, pale Arusha hotel na yeye alikutana na kijana mmoja mchoma nyama ambaye alitembea naye na kumuachia pesa laki tano na yeye kuondoka."
"Huyo shoga yako yupo wapi?"
"Ni Muda mrefu tumepotezana."
"Lazima niseme ukweli hili hata mke wangu nilimueleza kuwa pesa za utajiri wangu nilivyozipata. Ni kweli, basi huyo shoga yako ndiye aliyenipa huu utajiri na kama nitamuona leo nitampa zawadi kubwa."
Kauli ile ilikuwa kama mshale moyoni kwa mama Gift kwa mara ya kwanza kauli ya mwanaye inatimia alijikuta akipiga ukulele:
"Ooh! Mungu wangu nimekwisha," baada ya kauli ile walishangaa kumuona mtu akiseleleka kwenye kochi alilokuwa amekaa na kuanguka chini kitu kilicho washtua Gift na mumewe.
"Maskini mama yangu," Gift alipiga kelele baada ya kumuona mama yake amelegea kwenye zuria.
"Hiki nini tena?" Tell me aliuliza.
"Hata sijui tumuwahishe hospitali."
"Ina maana huwa ana matatizo haya?"
"Sijawahi kuyaona."
Tell me alimbeba juujuu hadi kwenye gari na kumuwahisha TMJ Mikocheni. Alipokelewa haraka haraka na kupata huduma ya kwanza ambayo ulimrudisha katika hali yake ya kawaida. Baada ya huduma ya kwanza na kuchukua maelezo na vipimo ilionyesha ni mshtuko tu wala hakukuwa na tatizo kubwa.
Mama gift alipata mapumziko kuangalia hali yake, akiwa katika chumba cha mapumziko alimuomba daktari asimruhusu mtu yoyote aingie ndani kwa sababu hakupenda kuonana na mtu kwa wakati ule.
Daktari alikubali na kuwaeleza Gift na mumewe waliokuwa wakisubiri kujua hali ya mgonjwa
"Samahanini naomba kwa sasa mwende nyumbani mgonjwa atakuwa kwenye mapumziko mafupi kwa hiyo njooni jioni."
"Lakini hali yake inaendeleaje?" Gift aliuliza.
"Ni mshtuko tu lakini yupo sawa ni mapumziko ya matazamio."
"Daktari hebu tueleze ukweli kama amezidiwa usinifiche mimi ndiye mtoto wake wa pekee."
"Kama kungekuwa na tatizo ningekujulisha yupo sawa ni mapumziko ya kawaida tu."
"Sawa daktari tutarudi hiyo jioni, sasa hata hatujui aletewe chakula gani?"
"Suala la chakula lisikusumbueni kila kitu tutamaliza hapahapa jioni njooni tu mumuone na pengine kuondoka naye."
Gift na mumewe waliondoka kurudi nyumbani kila mmoja akiwaza yake juu ya tukio lililotokea la mshtuko wa gafla wa mama Gift.
"Ni nini kilichofanya mama awe kwenye hali ile?"
"Hata mimi sijui la muhimu tumsubiri mwenyewe ndiye anayejua hasa tukizingati ni jana tu amerudi."
"Au labda ni kutokana na ugomvi wa jana?"
"Sidhani lakini si mlisameheana na yakaisha"
"Maskini sijui nini kimemsibu mama yangu," Gift alisema huku akilia.
"La muhimu tumuombee kwa Mungu atoke salama"
*****
Mama gift akiwa chumbani peke yake alijikuta akiyakumbuka maneno ya mwanaye Gift, kuwa tabia ya kutembea ovyo na wanaume ipo siku watatembea na mwanaume mmoja sijui wataangalianaje?
Aliamini mdomo ndio unaonuka ila kauli hainuki, wala si kauli ya mkubwa hata ya mtoto nao usipoifuata lazima yatakukuta ya kukukuta
"Maskini mie nitaiweka wapi sura yangu, heri ningetembea na mwanaume mmoja na mwanangu, lazima hii itakuwa laana ya mume wangu baba Gift ya kumtelekeza....Sijui mwanangu atamwitaje Tell me why na dada yake? Mbona nimeleta kitendawili cha mwaka sijui nani wa kukitegua.
“Hii aibu nitauweka wapi uso wangu, najua wanangu wanataka kujua nini kilichonisibu, lakini sina jinsi lazima niwe muwazi sijui mkwe na wanangu watanitazama vipi na akikuwa nitamueleza nini pia jamii itanielewa vipi.
“Hakuna njia nyingine ni kuuacha ukweli na mimi nitangulie mbele ya Mungu ili nisubiri hukumu yangu," mama Gift alikuwa akiongea huku machozi yakimtoka kama maji, alikuwa amepiga magoti pembeni ya kitanda na kuendelea kulia kilio cha majuto.
"Kweli Mungu akitaka kukuumbua hukuumbua kwa dhalilisho zito, mbona nimefanya kioja cha mwaka, sistahili kuishi bora nife."
Mama Gift alifuta machozi na kutoka mpaka nje ya wodi na kuagiza kalamu na kalatasi, baada ya kuletewa. Akiwa amepiga magoti kalatasi ilikuwa juu ya kitanda, aliandika ujumbe ambao alitaka apewe mwanaye atayekuja jioni.
Machozi yakiwa yanamwagika kama maji alianza kuandika ujumbe kwa mwanaye Gift:
Mwanangu Gift, najua uamuzi wangu utakushtua na kukuumiza kwa namna moja au nyingine. Lakini siyo mapenzi yangu, sina jinsi lazima nifanye hivi.
Kauli yako mwanangu haikwenda mbali, siku zote malipo ya ubaya huwa hapa hapa duniani. Ulilosema ambalo uliliogopa katika maisha yako limetimia, nashindwa sijui nitauweka wapi uso wangu, wewe na mumeo mtanielewaje. Mdogo wako nitamueleza nini anielewe na jamii itanielewaje. Nakubaliana na usemi wako, japo niliuona wa kitoto wa mtu asiye jua lolote, lakini leo umenifanya nijute na kuijutia nafsi yangu. Kweli pesa iliyonipa sifa lakini leo imenidhalilisha na kunifanya niwe kituko mbele ya jamii.
Najua nimezunguka sana kuusema ukweli, lazima nikuweke wazi wewe na mumeo. Kama ulikuwa ukifuatilia mazungumzo yangu na mumeo najua hakuna aliyejua kuna kitu gani kimepatikana kwenye yale mazungumzo si wewe wala mumeo.
Huu ndio ukweli, mdogo wako Malon baba yake mzazi ni Tell me why ambaye wakati ule alikuwa akitumia jina la Tamilway na ndiye niliyetembea naye pale Arusha hotel. Na ndiye niliyempa laki tano ambazo anadai ndizo zilizompa utajiri.
Hebu angalia ni aibu gani uliyoingia kwenye familia, mdogo wako atakuitaje ikiwa lazima Tell me amwite baba mzazi. Hiki ni kitendawili sijui kama kitapata mfumbuzi. Mwanao ambaye ni mgeni mtalajiwa atamwitaje Malon, mbona mwanangu nimefanya vioja vya mwaka na kufanya simulizi midomoni mwa watu.
Uamuzi niliochukua ndio haki yangu sina njia nyingine, nimeamua kujiua ili kujiepusha na aibu hii ambayo haina tofauti na kujipaka mavi mbele ya kadamnasi. Najua nimekukosea, najua nimemkosea baba yako najua nimemkosea mwanangu Malon.
Lakini naomba wote mnisamehe naomba uniombee msamaha kwa baba yako nimemkwaza kwa mambo mengi. Mwisho naomba mnilelee mwanangu Malon Mungu akipenda tutaonana. Nakuombeeni maisha marefu yenye upendo na furaha.
Buriani mwanangu nakupendeni sana mimi mama yako Thereza.

Aliirudia ile barua zaidi ya mara mbili huku machozi yakimmiminika kama maji. Alijifuta machozi kisha alitoka mpaka kwenye ofisi ya wauguzi na kuwakabidhi ile bahasha aliyokuwa ameiandika jina la mwanae Gift.
"Samahanini naomba akija mwanangu kama nitakuwa nimepitiwa na usingizi mumpe. Ila sipendi nionane naye kwa leo, akija mwambie tuonane kesho."
"Sawa mama," wauguzi aliipokea ile barua na kuendelea na shughuli zao hawakumtilia maanani.

Nini kitaendelea?
 
SEHEMU:12
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
...ILIPOISHIA:
Aliirudia ile barua zaidi ya mara mbili huku machozi yakimmiminika kama maji. Alijifuta machozi kisha alitoka mpaka kwenye ofisi ya wauguzi na kuwakabidhi ile bahasha aliyokuwa ameiandika jina la mwanae Gift.
"Samahanini naomba akija mwanangu kama nitakuwa nimepitiwa na usingizi mumpe. Ila sipendi nionane naye kwa leo, akija mwambie tuonane kesho."
"Sawa mama," wauguzi aliipokea ile barua na kuendelea na shughuli zao hawakumtilia maanani.
SASA ENDELEA…

Mama Gift baada kuwapa ile barua alirudi hadi chumbani kwake na kuichukua shuka ambayo aliitengeneza kama kitanzi na kuifunga juu kwenye pangaboi. Baada ya kuifunga vizuri ile shuka alijifunga shingoni na kujifyatua kwenye kitanda.
Mmoja wa wauguzi pamoja alikuwa bize aligundua kitu fulani usoni kwa mama Gift, uso wake ulikuwa umevimba uikionyesha alikuwa akilia kitu kilichomfanya ashtuke. Baada ya kuondoka mama Gift aliwauliza wenzake.
"Jamani mmemuona yule mama?"
"Hata kwani ana nini?"
"Yaani mnajifanya mpo bize kama sio kwa ajili ya wagonjwa, ubize huo mgeupata wapi?"
"Mbona maneno mengi kwani yule mama ana nini?"
"Mnajua mimi nawashangaa sana, mgonjwa anakuja hata hamumuangalii usoni ninyi mnaendelea na porojo, bila kujua yupo vipi halafu kitu kingine kilichonishtua ni sauti yake inaonyesha ana tatizo."
"Sasa sisi tumfanyaje?" Mmoja alijibu huku akipaka rangi kwenye kucha.
"Haya ngoja yatokee, hizi porojo mtazipigia nyumbani, jamani kazi mbaya ukiwanayo."
"Zinduna kwani umegundua nini?"
"Wakati yule mama akija hapa mimi nilikuwa najaza ripoti ya dawa, lakini sauti yake ilinifanya ninyanyue macho, kuna kitu nimekiona usoni kwake si cha kawaida huenda yule mama amezidiwa hali yake si nzuri ni jambo ambalo linatakiwa tulijue sisi kama wauguzi, hivi aje daktari tutamwambia nini, tushukuru Mungu hapajatokea tatizo, lakini tabia yetu ya kuingia mpaka tunatoka hatuendi kumuangalia mgojwa sio nzuri."
"Ni kweli Zinduna, sasa unatushauri nini?"
"Kwa vile mimi najaza ripoti mmoja wetu akamjulie hali ya yule mama."
Mmoja wa wauguzi alinyanyuka na kuelekea chumba alicholazwa mama Gift. Alikwenda kwa kujivuta huku kama mtu aliyelazimishwa, mlango ulikuwa umerudishwa kwa kuegeshwa, alifika moja kwa moja na kuusukuma mlango.
Tukio aliloliona mbele yake lilimfanya apige kelele za woga pale alipomuona mama Gift akipapalika kwenye kitanzi cha shuka. Wauguzi wengine walikuja mbio na kumkuta mama Gift ameninginia juu.
Kwa ujasiri mkubwa walifanikiwa kuikata ile shuka na mama Gift kuanguka chini akiwa amelegea. Alikuwa amepoteza fahamu lakini mapigo ya moyo yalikuwa mbali sana ambayo yalifanya maisha yake yawe kwenye hatihati.
Walimkimbilia daktari ambaye alifanya kazi ya ziada lakini kila dakika mapigo ya moyo yalikuwa yakipungua kupiga. Ilibidi awekewe mashine ya kumsaidia kupumua hali yake ilikuwa mbaya sana.
Daktari Eliud alichanganyikiwa na kujiuliza yule mama alikuwa na siri gani? Kwanza alikataa familia yake isimuone, pili ameamua kujitoa uhai kuna siri gani? Mama Gift alikuwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi akipumua kwa kutumia mashine.
*******
Gift akiwa na mumewe waliwasiri hospitali ya TMJ na kuelekea moja kwa moja kwenye chumba alicholazwa mama yake. Wakati anapita maeneo ya ofisi ya wauguzi dada mmoja ambaye si mgeni na Gift alimkimbilia.
"Da’ Gift kuna mzigo wako."
"Nani kakupa."
"Mama yako aliuleta ofisi ili tukupe ukija."
"Ina maana ameisha toka?"
"Ha.ha..apa.na," alijibu kwa kubabaika.
"Hata hivyo wewe si mjibuji kwa vile yupo mwenyewe atajibu."
Baada ya kuipokea ile barua aligeuka ili aondoke
"Samahani da Gift kabla ya kwenda chumba cha mgonjwa daktari alisema mpitie kwake kwanza."
"Kuna nini? Mbona mambo ya hapa yananichanganya."
"Yanakuchanganya nini, we twende kwa daktari hatujui anataka kutuambia nini tukitoka tunakwenda kumuona mama," Tell me alimwambia mkewe.
Waliongozana wote hadi kwenye ofisi ya daktari. Walimkuta akiwa amesimama akifuta jasho na kufungua friji ndogo kutoa maji baridi. Alipowaona waliwakaribisha.
"Oooh Mr and Mrs Tell me karibuni sana."
"Asante," walijibu kwa pamoja wakiwa wamesimama.
"Chukueni viti," walikaa kwa pamoja.
Daktari walikunywa yale maji kwa mkupuo alishupa pumzi nzito kisha alikaa kwenye kiti chake. Kabla ya kuongea alichukua cheti kilichokuwa juu ya meza yake kama anakisoma, kumbe alikuwea akitafuta neno la kuongea ili aeleweke.
Baada ya kupata la kuanzia alikohoa kidogo japo hakuwa na kikohozi na kusema:
"Samahanini jamani."
"Bila samahani."
"Sasa jamani nimewaiteni ili..." walikatishwa na sauti ya muuguzi ambaye aliingia huku akipiga kelele.
"Dokta mashine imezimika."
"Oooh Mungu wangu! Samahanini nakuja mara moja," Dokta alipitia koti lake na kutoka kwa mwendo wa kasi, kitu kilichofanya Gift na mumewe watazamane na Tell me kunyanyua mabega juu.
Wakiwa wamebakia peke yao kwenye ofisi ya daktari zaidi ya masaa robo saa Gift alimwambia mumewe.
"Mpenzi kwa nini tusiende kwanza kumuona mgojwa ili akirudi akute na sisi tumeisha mjulia hali mgojwa?"
"We subiri hujui kwa nini ametuita huku kabla ka kuonana na mgonjwa, najua madaktari pengine wanataka kukuuliza chanzo cha tatizo."
"Mbona jana tulimwambia."
"Huenda alikuwa amechanganyikiwa kwa ajili ya kuokoa maisha ya mgonjwa, pengine alikusikia lakini hakukuelewa."
"Haya wacha tumsuburi"
Wakiwa wametulia kumsubiri daktari, Gift aliamua kuisoma barua aliyopewa na muuguzi ajue imeandikwa nini? Aliifungua ile barua na kuanza kuisoma wakati huo mdogo wake Malon alikuwa amepakatwa na Tell me .
Aliisoma ile barua taratibu kila alivyokuwa akisoma ndivyo mapigo ya moyo yalivyokuwa yakipanda na joto kuongezeka mwilini. Aliisoma hadi mwisho alijikuta akisema.
"Hapana..Hapana...Ooooh maskini mama yanguuuu," Gift aliteleza toka juu ya kiti akiwa amelegea na kupoteza fahamu. Lilikuwa tukio la pili lililofanana la watu wawili, moja la mama Gift na la sasa ni la Gift mwenyewe.
Tell me alijikuta akichanganyikiwa na kushindwa kuelewa kwa nini mkewe yupo kwenye hali ile. Alimuwahi kabla hajaanguka chini toka juu ya kiti na kumlaza. Wakati huo Malon na yeye alianza kulia kitu kilichozidi kumchanganya Tell me.
Alishindwa aanzie wapi kumuhudumia mkewe na Malon shemeji yake ambaye ni mwanaye na yeye alikuwa akilia. Bahati nzuri daktari aliingia na kukuta tukio lingine kitu kilichomshangaza.
"Tell me vipi tena shemeji?"
"Ndugu yangu yaani hata sijui alikuwa akisoma hii barua akiwa kimya mara alianza kupayuka hapana..hapana kisha alisema maskini mama yangu na kupoteza fahamu."
"Mmh shughuli ipo, wewe mwanaume jikaze mambo ni mazito."
"Kwa nini daktari?"
"Kila tukio ni zito."
"Una maana gani?"
"Ngoja kwanza tumuhudumie shemeji."
Gift alipewa huduma ya kwanza na kurudiwa na fahamu, alipopata fahamu aliangua kilio cha sauti ya juu.
"Oooh maskini mama yangu...kwa nini umechukua uamuzi huo, japo kila baya malipo yake ni mabaya…mama hukutakiwa kujihukumu."

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: ... RAHA YENYE MAUMIVU
SEHEMU: 07
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Baada ya kusema yale Eliza alianza kulia kitu kilichofanya Gift anyanyuke kitandani na kwenda kumbembeleza.
“Pole sana rafiki yangu.”
“Gift inauma umasikini huu utaendelea kutudhalilisha mpaka lini?”
“Najua nakuahidi kukusaidia rafiki yangu najua mimi nimeumia lakini wewe umeumia mara mbili kwa vile hukufanya kwa ridhaa yako tofauti na mimi.”
Gift alisahau yake na kumtia moyo Eliza aliyekuwa akilia kwa majuto.
SASA ENDELEA…
***************

Ilikuwa siku ya jumapili Gift akiwa na shoga yake ambaye shuleni wapambe waliwabatika kama wake wenza kwa ajili ya kutembea na mwanaume mmoja. Kwa vile msimamo wao ulikuwa mmoja wa kumkomoa Kanuth hilo halikuwashtua walikuwa na siri yao nzito.
Wakiwa wanajisomea chini ya mti kwa mbali lilisimama gari moja la kifahari aina ya Lange lover Vogue ya rangi ya nyeusi. Hawakuijali baada ya kuisifia tu kuwa gari zuri waliendelea na masomo yao. Sauti ya juu iliyokuwa ikimwita Gift ilimfabya aache kusoma na kuangalia ni nani.
"Gift mgeni wako huyo," Eliza alisema huku alimuangalia vizuri mgeni wa kiume ambaye alikuwa mgeni machoni mwake.
Kila alivyokuwa akisogea naye alimwangalia vizuri, alikuwa kijana mmoja mtanashati aliyekuwa kwenye suti nzito alijiuza ni nani. Macho yalipotulia alimkumbuka lakini jina alikuwa amemsahau.
Bila kijielewa alijikuta ametupa vitabu na kukimbia kumpokea kwa kumkumbatia.
"Oooh! Kaka karibu."
"Asante, upo sawa?"
"Kama chuma si unaniona!"
"Vizuri, mrembo hujambo?" alimgeukia Eliza aliyekuwa bado amepigwa butwaa.
"Sijambo shemeji."
"Eliza tabia gani mtu hujatambulishwa unapayuka."
"Samahani shoga...karibu kaka..nani sijui?"
"Gift atakutambulisha."
"Huwezi amini jina lako nimelisahau.. hebu ngoja nikumbuke Mr listen kama sikosei..oooh nimekumbuka talk to me."
"Ngoja nikukumbushe naitwa Niambie kwa nini umelisahau jina langu wakati hata kadi nilikupa."
"Oooh nimekumbuka Tell me why....Oooh karibu sana kaka tell me why ni kweli nilikuwa na kadi ambayo nilimpa mama ili siku nitayotoka tukualike tujumuike pamoja kwa chakula cha usiku mama alikuwa na hamu ya kukuona.
"Lakini aliondoka siku moja baada ya mimi kutoka hospitali na kupanga tutakualika, kibaya hata kadi yako aliondoka nayo na mimi sikuwa nimeiandika pembeni. Nilikuwa na hamu ya kukuona lakini ndivyo hivyo ilibidi namsubiri mpaka mama arudi."
"Mmh! Tuachane na hayo, vipi hali yako unajua sikujisikia vizuri kutokujua maendeleo yako kibaya zaidi msomi ambaye ni tegemeo la taifa," Tell me alisema huku akichanua tabasamu mwanana.
"Tegemeo wapi kila kukicha tunanyanyapaliwa na serikali."
"Lakini si mambo yametulia."
"Sawa yametulia lakini jasho limetutoka kila siku mpaka mishipa ya shingo itusimame. Wao mbona huwa hawaandamani kuongezana posho wamesahau na wao wamesoma bure lakini wenzao ndio watukamue."
"Hata nyinyi mkifika juu mtakuwa hivyohivyo, wangapi walisema lakini wamepata wamesahau ahadi zao njaa mbaya ukiwa na njaa utatoa ahadi za ajabu hata kuvuta meli kwa mkono ili upate chakula ukishiba unawageuka kwa kuwauliza ni nani mwenye uwezo wa kuvuta meli kwa mkono wewe atakuwa wa pili."
"Mr Tell me why mbona unatetea au una mpango wa kugombania Ubunge?"
"Siku zote kweli utafutiwa sababu ili kuonekana si kweli."
"Umeshinda, tuachane na hayo karibu kazini kwetu hapa ndipo tunapo itafuta sembe."
"Ninashukuru huwezi kuamini kukaa kwangu kote jijini sijawahi kufika chuoni hapa."
"Muongo mtu maarufu kama wewe usifike sehemu kama hii."
"Gift yaweza kuwa kweli pengine hana shida napo aje afanye nini?" Eliza alimuunga mkono Mr Tell me.
"Kwanza mimi si maarufu kama anavyosema, ningekuwa maarufu angepoteza kadi yangu na kushindwa kunipata."
"Mmh! Tell me imekuwa sababu..basi nisamehe leo simu ninayo najua sasa kesi itaisha."
"Kuwa na simu siyo sababu muhimu mawasiliano."
"Sasa utanichoka usijesema karaha au kumuudhi wifi."
"Ni hapo nitakapokuwa naye....Sasa Gift nina imani kidogo moyo wangu utaridhika au kutulia baada ya kupata kujua hali yako. Nimefarijika sana kukuta mzima wa afya tena ukibukua."
"Hata mimi nimefurahi huwezi kuamini siri ipo moyoni mwangu ipo siku nitakwambia. Tell me why kila dakika unanifanya niwe mwanafunzi wako wa kujifunza tabia za watu na kufuta dhana kuwa baadhi ya viumbe si wabaya ila kiumbe mmoja ndiye anayeweza kutia doa na kusababisha kuona wote ni wabaya....wewe ni mfano wa kuigwa."
"Kwa nini unasema hivyo?"
"Ni vigumu kuamini japo ni muda mrefu nashangaa kuona kama nilikuwa nawe siku zote na kujiona mpweke pale utakapo niaga na kujuta kwa nini nimekufahamu."
"Gift una maana gani?" Maneno ya Gift yalimchanganya kidogo Tell me.
"Ni vigumu kuwa wakili wa moyo wako, hasa sisi wanawake pale moyo unapoingia gerezani pasipo kosa wakati mtetezi yupo ambaye ni muoga kuutetea moyo ambao huteseka bila kosa."
"Ninaweza kuwa nimekuelewa lakini huenda vilevile sijakuelewa hebu niweke wazi una maana gani kama sivyo nifikiliavyo?" Maneno ya mafumbo yalizidi kumwweka njia panda.
"Sio siri kila muda kila dakika kila nikikufikiria nakosa jibu kuwa wewe ni kiumbe wa aina gani hata mama yangu mzazi alikusifia kwa yote uliyonitendea nashindwa nikilipe nini...ili isiweze kukupoteza ili nami uuone ukarimu wangu."
"Sihitaji malipo yoyote kutoka kwako...ilikuwa ni wajibu wangu kama mwanadamu kuonyesha ubinaadamu hasa pale unaposababisha maumivu kwa mwenzio japo ilikuwa bahati mbaya."
"Lakini elewa Tell me why siku zote hesabu huanzia moja, lakini kwa upande wangu naomba ifike kumi na moja nina imani unaijua hesabu hii hutumika hasa kanisani, moja na moja huwa moja kibinaadamu huwa kumi na moja naomba hesabu yetu iende kikanisa ili tupate moja."
"Nimekuelewa kuliko ulivyozungumza nipe muda."
"Umenielewa nini Tell me why?"
"Nina imani mzigo ulionipa umeufunga hukutaka kila mtu aujue kwa mimi muungwana nimekuelewa kwa hiyo wacha nikauangalie kama unapendeza hauna kipingamizi."
"Nitafurahi kama kile nilichokiota mchana kinakuwa kweli nimeamini unaweza kuota huku ukiwa macho."
"Umeota nini tena Gift?"
"Nimeota moja na moja ni moja wala si mbili wala kumi na moja."
"Mmmh kweli wewe msomi unayeongea kwa mifano isiyoonekana kwa macho wala kwa akili nyepesi bali kwa yule aliyezama chini ya maji ndiye hugusa mchanga mweupe."
"Hakika kila asimamae kwa ajili ya nafsi yake huiokoa nafsi yake."
Tell me why alimuaga Gift ambaye alimsindikiza hadi kwenye gari lake aliwaaga na kuondoka huku akimuacha Gift kwenye mtihani mzito wa moyo wake na kujiuliza ni kweli turufu aliyoitupa ni kubwa kuliko ya mpinzani wake au ndio imemezwa na kubwa zaidi kama samaki mdogo kuliwa na mkubwa.

Nini Kitaendelea?

Mambo yanazidi kunoga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom