Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,019
- 454,034
SEHEMU YA 42
Johnson hakutaka kubaki nchini Marekani, ilikuwa ni lazima arudi nchini Tanzania kwa lengo la kumtafuta msichana Bhoke ambaye aliamini angeifanya kazi yake kama alivyotaka.
Aliukumbuka uzuri wa msichana yule, mchanganyikio wake wa rangi ambao uliwaacha watu wengi midomo wazi. Hakujua alipokuwa akiishi ila kitu ambacho alikikumbuka ni kwamba alikuwa Magomeni alipokuwa akiishi na mama yake.
Alipofika nchini Tanzania, akaanza kuelekea huko ambapo nao walihama na kuhamia Mikocheni B. Alipofika huko akaanza kumuulizia msichana huyo, kila mmoja hakujua mahali alipokuwa, mama yake alipofariki, naye hakukaa sana akaondoka, alipoondoka, hakuna aliyepafahamu.
Hilo likamuhuzunisha mno, kwake, huyo Bhoke alikuwa mtu muhimu kuliko yeyote yule. Ilikuwa ni lazima apambane kadiri alivyoweza lakini mwisho wa siku afanikiwe kuonana naye.
Kwa kuwa alikumbuka msichana huyo alikuwa na rafiki mahali hapo aliyeitwa Happiness, akamtafuta, alipomuona akaanza kuongea naye.
Msichana huyo ndiye ambaye alimwambia ukweli kuhusu Bhoke, kwamba alikuwa akijiuza kwa kusafiri kwenda sehemu mbalimbali kama kutanua soko lake. Johnson alivyosikia hivyo, hakuamini masikio yake, aliumia moyoni mwake lakini pia alikumbuka maisha ambayo aliishi Bhoke.
Yalikuwa maisha magumu mno, hakuwa na pesa za kutosha, alimtegemea mama yake ambaye baada ya kufariki, hakujua ni kwa namna gani angeweza kuyaendesha maisha hayo.
Hakutaka kumlaumu, kwa mtoto wa kike kama yeye ilikuwa ni lazima kuishi maisha hayo hivyo akapotezea na kumwambia Happiness kwamba alihitaji kuonana na msichana huyo.
“Nitakupa namba yake!” alisema Happy.
“Sawa.”
Akapewa namba ya Bhoke na kuanza kuwasiliana naye. Siku hiyo ndiyo kwamba msichana huyo alimaliza kufanya mapenzi na rais Edmund usiku uliopita, kitendo cha kupigiwa simu na Johnson kilimshtua kupita kawaida.
Ilipita miaka mingio, tangu mama yake alipofariki, alimpenda mno kijana huyo, alikumbuka jinsi alivyomjali katika kipindi cha nyuma, japokuwa hakuwa ameutoa usichana wake lakini kwake alikuwa mtu mwenye thamani kuliko mtu yeyote yule.
Johnson hakutaka kubaki nchini Marekani, ilikuwa ni lazima arudi nchini Tanzania kwa lengo la kumtafuta msichana Bhoke ambaye aliamini angeifanya kazi yake kama alivyotaka.
Aliukumbuka uzuri wa msichana yule, mchanganyikio wake wa rangi ambao uliwaacha watu wengi midomo wazi. Hakujua alipokuwa akiishi ila kitu ambacho alikikumbuka ni kwamba alikuwa Magomeni alipokuwa akiishi na mama yake.
Alipofika nchini Tanzania, akaanza kuelekea huko ambapo nao walihama na kuhamia Mikocheni B. Alipofika huko akaanza kumuulizia msichana huyo, kila mmoja hakujua mahali alipokuwa, mama yake alipofariki, naye hakukaa sana akaondoka, alipoondoka, hakuna aliyepafahamu.
Hilo likamuhuzunisha mno, kwake, huyo Bhoke alikuwa mtu muhimu kuliko yeyote yule. Ilikuwa ni lazima apambane kadiri alivyoweza lakini mwisho wa siku afanikiwe kuonana naye.
Kwa kuwa alikumbuka msichana huyo alikuwa na rafiki mahali hapo aliyeitwa Happiness, akamtafuta, alipomuona akaanza kuongea naye.
Msichana huyo ndiye ambaye alimwambia ukweli kuhusu Bhoke, kwamba alikuwa akijiuza kwa kusafiri kwenda sehemu mbalimbali kama kutanua soko lake. Johnson alivyosikia hivyo, hakuamini masikio yake, aliumia moyoni mwake lakini pia alikumbuka maisha ambayo aliishi Bhoke.
Yalikuwa maisha magumu mno, hakuwa na pesa za kutosha, alimtegemea mama yake ambaye baada ya kufariki, hakujua ni kwa namna gani angeweza kuyaendesha maisha hayo.
Hakutaka kumlaumu, kwa mtoto wa kike kama yeye ilikuwa ni lazima kuishi maisha hayo hivyo akapotezea na kumwambia Happiness kwamba alihitaji kuonana na msichana huyo.
“Nitakupa namba yake!” alisema Happy.
“Sawa.”
Akapewa namba ya Bhoke na kuanza kuwasiliana naye. Siku hiyo ndiyo kwamba msichana huyo alimaliza kufanya mapenzi na rais Edmund usiku uliopita, kitendo cha kupigiwa simu na Johnson kilimshtua kupita kawaida.
Ilipita miaka mingio, tangu mama yake alipofariki, alimpenda mno kijana huyo, alikumbuka jinsi alivyomjali katika kipindi cha nyuma, japokuwa hakuwa ameutoa usichana wake lakini kwake alikuwa mtu mwenye thamani kuliko mtu yeyote yule.