Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,975
- 453,778
SEHEMU YA 34
“Basi ni lazima nifanye naye mapenzi!”
“Ila si lazima!”
“Hapana! Lazima nifanye naye. Napenda mno kufanya mapenzi,” alisema Bhoke, alimaanisha alichokuwa akikizungumza kwani kwake, kufanya mapenzi ndiyo ilikuwa starehe yake kubwa kuliko hata kula.
Mambili hakuwa na shida na hilo, alichohitaji ni msichana huyo kufanya kazi yake tu. Kwa kuanzia, akampa kiasi cha milioni tatu na kumwambia mahali ambapo mwanaume huyo angekuwepo kwa ajili ya kuzungumza na wadau mbalimbali kama njia mojawapo ya kuanza kampeni zake.
Bhoke alipoondoka, haraka sana akawapigia simu viongozi wake na kuwaambia kuhusu msichana huyo kwamba alikubali kufanya kazi yake kwa malipo yaleyale waliyokuwa wamepanga.
“Na ni mzuri?” aliuliza waziri mmoja kwenye simu.
“Sanaaaa! Yaani isingekuwa hapa nyumbani, nadhani leo ningevunja naye amri ya sita,” alisema Mambili na kuanza kucheka.
Haraka sana taarifa zikatumwa mpaka kwa Rais Edmund Golam na kuambiwa kuwa msichana huyo alipatikana na tayari alianza kujipanga kwa ajili ya kufanya kazi hiyo kubwa iliyokuwa mbele yake.
Naye alipoambiwa hivyo, kama ilivyokuwa kwa waziri akaulizia uzuri wa Bhoke, akaambiwa kwamba alikuwa mrembo mno hivyo walikuwa na uhakika wa kufanikiwa kwa kile walichokuwa wamekipanga.
Rais Edmund aliposikia hivyo ni kama akili yake ilichanganyikiwa, akamwambia waziri kwamba kabla ya kazi hiyo kufanyika ilikuwa ni lazima aonane na msichana huyo ili ampe mbinu za kufanya katika kutekeleza mpango huo.
Hilo halikuwa tatizo, haraka sana simu ikapigwa mpaka kwa Mambili na kuambiwa kile alichokisema rais hivyo kama iliwezekana ilikuwa ni lazima ampigie simu Bhoke na kumwambia kuhusu kile alichoambiwa.
Halikuwa tatizo, akampigia simu msichana huyo na kumwambia kila kitu. Bhoke aliposikia, hakuamini masikio yake, katika maisha yake yote hakuwahi kufikiria hata mara moja kwamba angeingia ikulu hata kwa bahati mbaya.
“Basi ni lazima nifanye naye mapenzi!”
“Ila si lazima!”
“Hapana! Lazima nifanye naye. Napenda mno kufanya mapenzi,” alisema Bhoke, alimaanisha alichokuwa akikizungumza kwani kwake, kufanya mapenzi ndiyo ilikuwa starehe yake kubwa kuliko hata kula.
Mambili hakuwa na shida na hilo, alichohitaji ni msichana huyo kufanya kazi yake tu. Kwa kuanzia, akampa kiasi cha milioni tatu na kumwambia mahali ambapo mwanaume huyo angekuwepo kwa ajili ya kuzungumza na wadau mbalimbali kama njia mojawapo ya kuanza kampeni zake.
Bhoke alipoondoka, haraka sana akawapigia simu viongozi wake na kuwaambia kuhusu msichana huyo kwamba alikubali kufanya kazi yake kwa malipo yaleyale waliyokuwa wamepanga.
“Na ni mzuri?” aliuliza waziri mmoja kwenye simu.
“Sanaaaa! Yaani isingekuwa hapa nyumbani, nadhani leo ningevunja naye amri ya sita,” alisema Mambili na kuanza kucheka.
Haraka sana taarifa zikatumwa mpaka kwa Rais Edmund Golam na kuambiwa kuwa msichana huyo alipatikana na tayari alianza kujipanga kwa ajili ya kufanya kazi hiyo kubwa iliyokuwa mbele yake.
Naye alipoambiwa hivyo, kama ilivyokuwa kwa waziri akaulizia uzuri wa Bhoke, akaambiwa kwamba alikuwa mrembo mno hivyo walikuwa na uhakika wa kufanikiwa kwa kile walichokuwa wamekipanga.
Rais Edmund aliposikia hivyo ni kama akili yake ilichanganyikiwa, akamwambia waziri kwamba kabla ya kazi hiyo kufanyika ilikuwa ni lazima aonane na msichana huyo ili ampe mbinu za kufanya katika kutekeleza mpango huo.
Hilo halikuwa tatizo, haraka sana simu ikapigwa mpaka kwa Mambili na kuambiwa kile alichokisema rais hivyo kama iliwezekana ilikuwa ni lazima ampigie simu Bhoke na kumwambia kuhusu kile alichoambiwa.
Halikuwa tatizo, akampigia simu msichana huyo na kumwambia kila kitu. Bhoke aliposikia, hakuamini masikio yake, katika maisha yake yote hakuwahi kufikiria hata mara moja kwamba angeingia ikulu hata kwa bahati mbaya.