Hadithi: Malaika Mweusi

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,638


HADITHI: MALAIKA MWEUSI
SEHEMU: 01
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

MALAIKA MWEUSI.

Alikuwa amepiga goti pembeni ya mwili wa mama yake ambaye alikuwa amefariki muda mfupi tu kutokana na kipigo cha mumewe, ambaye ni baba wa kufikia wa msichana Thereza. Huku akiwa analia kwa uchungu alimuahadi mama yake kuwa lazima atalipa kisasi kwa wale waliomtendea unyama. Kwa kusoma kwa bidii ili siku moja awe hakimu au mwanasheria awafunge wote wanaonyanyasa wanawake na kuwabaka. Lakini dhamira yake ilikatishwa kwa kuachishwa shule akiwa darasa la sita na kuuzwa kwa mtu ili awe mtumishi wa ndani! Je, msichana Thereza atatimiza ahadi yake aliyo ihaidi mbele ya mwili wa marehemu mama yake? Ungana na mtunzi mahiri Ally Mbetu katika riwaya hii ya kusisimua.

****
MLIO wa simu ulimshtua mkuu wa upelelezi aliyekuwa katikati ya usingizi. Aliyatupia macho yake kwenye saa ndogo iliyokuwa juu ya droo ya kitanda, ilimuonyesha kuwa ni saa 10:15 za usiku nusu saa tangu amsindikize rafiki yake wa kike aliyembatiza jina la Black Angel, yaani Malaika Mweusi.
Aliinyanyua simu yake iliyokuwepo pembeni ya mto aliokuwa ameulalia, alipoichukua simu ilimuonyesha ni simu maalumu kutoka ofisini. Mara nyingi simu hiyo hutumika kwa ajili ya dharura tu. Hasa pale panapotokea matatizo yasiyokuwa ya kawaida.
Alibofya kifute cha kupokelea simu na kuzungumza kwa sauti ya uchovu, kutokana na shughuli ya usiku haikuwa haba, ilimnyong’onyesha mwili.
Shughuli ya Malaika Mweusi ilimfanya atangaze ndoa na msichana huyo aliyetokea kumuamuni kupita kiasi, hasa kutokana na tabia yake ya upole, ucheshi na roho ya huruma. Vitu ambavyo wanawake wengi hawana zaidi ya kuwa na kimojakimoja, pia Malaika Mweusi alijaliwa sura na umbile la kuvutia.
Mwanaume yeyote asingeweza kujizuia kutangaza ndoa kwa binti huyo aliyeonekana kutoka kwenye familia ya kitajiri. Akizungumza kwa sauti ya kivivu, Mkuu huyo wa upelelezi bwana Anderson:
“Ndiyo nakupata, lete habari.”
“Afande, mambo yameharibika,” sauti ya upande wa pili ilisema.
“Wapi tena?” Aliuliza huku akiiweka sawa akili yake.
“Yule hakimu.”
“Ooh! Mungu wangu, hii sasa inatisha nakuja sasa hivi ofisini.”
Bwana Anderson alikwenda bafuni kuoga haraka haraka na kubadili nguo, wakati alitoka nje aliona mkoba wa Malaika Mweusi ukiwa juu ya kochi. Aliwaza sana kuhusu ule mkoba wa Malaika Mweusi na kusema kwa sauti ya chini:
“ Aah! Kumbe jana aliacha mkoba wake, siyo mbaya ataufuata jioni.”
Alikwenda hadi kwenye banda la gari na kulichukua tayari kwa safari ya ofisini. Saa yake ya mkononi ilimuonyesha kuwa ni saa 11:35. Akiwa njiani akiwaza mambo mengi kuhusu vifo vya kutisha vya mfululizo, vifo ambavyo vimemchanganya yeye na vijana wake. Alipofika ofisini alimkuta maofisa upelelezi na vijana wake wakiwa wameshafika ofisini. Alipoingia ofisini wote walinyanyuka, baada ya kukaa aliwaamuru nao wakae chini.
“Mnaweza kukaa,” baada ya kuketi alisema.
“Ndiyo, leteni habari,” alisema huku akitembeza macho kila kila mmoja aliyekuwemo mule ndani.
“Afande kama ulivyosikia yule hakimu ameuawa, inavyoonekana ameuawa si chini ya saa sita zilizopita.” Alisema afisa upelelezi.
“Saa sita! Ilikuwaje akachelewa kujulikana?”
“Inavyosemekana amekutwa amekufa katika gari lake ambalo lililokuwa limeegeshwa pembeni ya barabara.”
“Nani aliyegundua mwili wa marehemu kwenye gari?”
“Askari wa doria ambao walikuwa wanalipita kila mara ile gari, walipoamua kulichunguza ndipo walipogundua mwili wa hakimu.”
“Lazima tukubali tumefanya uzembe wa hali ya juu kutokana na kifo cha hakimu.”
“Bosi sidhani kama tumehusika, pamoja na muuaji kutoa vitisho miezi miwili iliyopita. Nina imani tulimpa Hakimu tahadhari na kumweleza sehemu na muda anaotakiwa kuwa nje ya nyumba yake. Kwa kukiuka masharti yetu kifo chake amekitengeneza yeye mwenyewe.”
“Mmh! Sasa muuaji ni nani, hivi vifo vinafanana? sidhani lakini la muhimu tuwahoji wale ndugu wa yule bwana aliyefungwa na kusababisha vitisho vya muuaji. Maelezo ya awali yalionesha Hakimu alipindisha sheria na mwisho wa siku ilimuhukumu mwenyewe.”
“Lakini si tuliwahoji mapema wao wakasema hawana uhusianao wowote wala taarifa yoyote kutoka kwa muuaji.”
“Unajua hii inatisha, eti muuaji anajiita mtetezi wa haki za binaadamu.”
“Kwani kwa mara ya mwisho hakimu alikuwa wapi?”
“Job Pub.”
“Okay, kuna umuhimu wa kuwahoji watu waliokuwepo pale Job Pub ili kujua kuwa aliondoka saa ngapi na aliongozana na nani.”
“Sawa bosi, tutaifaanya kazi hiyo.”
“Haya majibu niyapate kabla ya saa moja usiku, sawa jamani?”
Mkuu wa upelelezi Anderson aliagana na vijana wake na kuondoka kurudi nyumbani huku akiwa amejawa na mawazo mengi kuhusu mauaji ya kutisha yaliyokuwa yakiendelea huku muuaji akionekana ni mtaalamu wa hali ya juu. Alijiuliza muuaji ni nani? Kama kamuua hakimu kwa ajili ya kupindisha sheria na hao wengine vifo vyao vimetokana na nini? Kikiwepo cha mkewe na mwanaye kipenzi Gift?
Alijiapiza kuwa siku atakayomtia mikononi huyo muuaji ama zake au za muuaji. Alipofika nyumbani alikuwa amechoka akili na mwili, alijitupa kwenye kochi na usingizi mzito ukamchukua.
Anderson alishtuka usingizini majira ya jioni na kujiona amelala kipindi kirefu, muda uliobaki ilikuwa nusu saa akutane na vijana wake kumpa taarifa ya hakimu hiyo. Kama kawaida alikwenda kuoga na kubadili nguo tayari kwenda ofisini.
Wakati anataka kutoka mkoba mweusi wa Malaika Mweusi ulimgusa na kuhisi kuna kitu cha muhimu kukiangalia kwenye mkoba wa binti anayeonekana mtoto wa tajiri. Aliangalia saa yake ilimuonyesha bado dakika ishirini akijua ni muda wa dakika tano hivi kwa mwendo wa gari atawahi ofisini. Hamu ya kujua kuna nini katika mkoba ule ilimfanya kuupekua ili ajue kuna vitu gani. Aliamini huenda angegundua siri yoyote ya msichana huyo kutoka familia ya kitajiri. Kwa dakika kumi alijua zinatosha kufanya upekuzi wa haraka haraka.
Alipofungua pochi, ndani alikutana na cheni isiyopungua thamani ya shilingi milioni moja na nusu na simu ya mkononi aina ya Sum sung yenye thamani ya shilingi milioni moja na laki saba, lakini ilikuwa haina line. Katika mfuko mdogo wa ile pochi alikuta kijitabu kidogo “note book.”
Alikifungua na kuanza kukisoma karatasi moja baada ya nyingine, ilionyesha kuwa ni msichana mwenye miradi mingi ya mamilioni ya shilingi. Aliendelea kusoma karatasi za mbele alikutana na majina yameandikwa majina ya bluu.
Lakini asilimia kubwa ya majina hayo yalikuwa yamezungushiwa wino mwekundu na majina mawili tu ndiyo yalikuwa hayajazungushiwa wino mwekundu.
Majina yale yalimshtua moyo wake na kusababisha mwili kusisimka na jasho jembamba kumvuja juu ya paji la uso. Aliyarudia zaidi ya mara tano na jibu lilikuwa lilelile, alichokisoma machoni mwake kilikuwa sahihi.
Yalikuwa ni majina ya baadhi ya watu waliouawa katika matukio yaliyomchanganya akili na kushindwa kumtambua muuaji. Mbele ya majina yale yalikuwa na tarehe sahihi ya mauaji yaliyofanyika. Ndani ya majina yale lilikuwepo jina la marehemu mama yake mzazi, siku na tarehe aliyouawa, japo mama yake alijua amekufa kwa ajali ya gari.
Jina lingine lilikuwa la mdogo wake aliyeuawa kwenye mazingira ya kutatanisha. Mwili wake ulikutwa kwenye bwawa la mji machafu chuo kikuu. Pia tarehe ya kifo cha mkewe na mwanaye ilionekana siku moja na tarehe ilikuwa ileile. Kifo kilichomuuma sana na kumchanyanya akili.
Mkewe aliuawa kikatili kwa kuchunwa ngozi sehemu za siri na kisha kupigiliwa kipande cha mti. Kilikuwa kifo cha mateso makubwa, maiti yake ilikatwa ikiwa imelaliwa na mwanaye ikiwa inavuja damu mwili mzima.
Vifo vya mkewe na mwanaye vilimuuma sana hasa alipouona mwili wa mkewe livyoharibika vibaya hasa sehemu za siri. Aliapa mbele ya ya mwili wa mkewe na mwanaye siku ya kutoa heshima za mwisho kwamba atamfafuta muuaji na kumtia hatiani kwa mkono wake mwenyewe.
Alijikuta katika mawazo mengi kuhusu kile kitabu cha majina na Malaika Mweusi kina uhusiano gani? Alijiuliza kama atakuwa amehusika na vifo vile au la. Hakukubaliana na akili yake kuwa Malaika Mweusi ndiye muuaji.
Alimuamini na kumwona ndiye atakayeziba pengo la marehemu mkewe hadi akafikia hatua ya kumtambulisha kwa wazazi wake ambao nao wakawapa baraka zote ili wafunge ndoa.
Kile kitabu kilimchanganya sana akili yake, Mama yake kabla kifo chake alionyesha mapenzi mazito kwa Malaika Mweusi na alimsifia mwanaye kwa chaguo lake zuri la msichana mzuri mwenye tabia njema.
Alijikuta akisema kwa sauti:
“Hapana haiwezekani Malaika Mweusi kuwa muuaji, lazima atakuwa anamjua muuaji, lazima nipate ukweli kupitia kwake.”
Jasho lilikuwa linamvuja chapachapa kama aliyefungiwa kwenye chumba cheye joto kali. Aliendelea kusoma kitabu majina ya mwisho mawili yaliyobaki ambayo hayakuwa yamezungushiwa wino mwekundu. Katika majina hayo lilikuwepo jina la baba yake mzazi, yalizidi kumchanganya, alijikuta akibwatuka:
“Ha! Na babaa, nooo..nooo.”
Tarehe iliyokuwa mbele ya jina la baba yake ilikuwa ni siku ileile, alisema tena kwa sauti:
“Hapana haiwezekani na baba tena, hapana.”
Alitoa simu yake ya mkononi na kubofya namba ya baba yake ili kumjulisha awe makini kwani kifo kilikuwa kinamnyemelea. Lakini alipopiga ilikuwa inaita tu bila kupokelewa mpaka ikakatika. Alijikuta akitoka ndani kwa mwendo wa kuruka hadi katika gari lake na kuliondoa katika mwendo wa kasi mithili ya ndege za kivita kuwahi kwa baba yake.
Ndani ya dakika tano alikuwa anaelekea kwa baba yake, aliiacha barabara kuu na kuingia ndogo inayoelekea kwa baba yake, mbele yake kulikuwa na gari limeharibika.
Kwa haraka aliteremka kwenye gari bila ya kuchomoa funguo wala kufunga mlango na kuanza kukimbia kuelekea kwa baba yake.
Njiani alikutana na mwanamke kama Malaika Mweusi, lakini hakumjali zaidi ya kuwahi kuokoa maisha ya baba yake. Nyumba ya baba yake ilikuwa giza, aliingia ndani ya geti na kwenda moja kwa moja hadi ndani. Alimwita baba yake kwa sauti ya juu, lakini hakukukuwa na majibu lolote. Sebule ilikuwa kimya pia giza.
Alipowasha taa alishangaa kukuta ukumbi mtupu hakukuwa na mtu yeyote, alielekea chumbani kwa baba yake. Mlangoni alikutana na michirizi ya damu lakini chumbani kwa baba yake kulikuwa na giza. Ile damu ilimfanya aione hali ya hatari mbele yake
Alitoa bastola na kuingia kwa tahadhari kubwa alipapasa ukutani na kufanikiwa kuwasha taa.
Hakuamini macho yake, alishuhudia mwili wa baba yake ulikuwa umelazwa kitandani ukiwa mtupu kama alivyozaliwa. Sehemu zake za siri zilikuwa zimetenganishwa na kisu kilikuwa kimemchoma katikati ya moyo wake, macho yalikuwa yamemtoka akionyesha amekufa kwa mateso makali.
Damu ilikuwa mbichi na mwili wake ulikuwa bado una joto. Chumba chote kilikuwa kinanuka damu mbichi. Anderson aliuvamia mwili wa baba yake na kuukumbatia huku akiendelea kuapa atamshikisha adabu aliyetenda kosa lile.
Alitoka harakahara ili aanze msako wa Malaika Mweusi ili apate ukweli a vifo vyote. Lakini alikataa katakata muuaji anaweza kuwa Malaika Mweusi. Kwa vile nguo zake zilikuwa zimetapakaa damu ya baba yake alipapigia simu vijana wake waje kuchukua mwili wa marehemu baba yake kuupeleka hospitali.
Akiwa njiani aliwaza sana uhusu vifo vyote hasa vinavyoihusu familia yake kama wameuawa wote aliyebaki ni yeye na kama asipomuwahi muuaji basi atamuua yeye.
“Hivi Malaika Mweusi anaweza kuwa muuaji?.....inawezekana maana nimemuona eneo la tukio sasa hivi, kwani ana siri gani inayomfanya afanye hivyo?” Mr. Anderson alijikuta akizungumza peke yake. Hakuamini mtu aliyemuamini na kumbatiza jina la Malaika Mweusi awe muuaji, kama ni kweli alihusika hakuwa Malaika Mweusi bali Shetani Mweusi.

ITAENDELEA KESHO
 
HADITHI: MALAIKA MWEUSI
SEHEMU: 02
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500
ILIPOISHIA:
Akiwa njiani aliwaza sana uhusu vifo vyote hasa vinavyoihusu familia yake kama wameuawa wote aliyebaki ni yeye na kama asipomuwahi muuaji basi atamuua yeye.
“Hivi Malaika Mweusi anaweza kuwa muuaji?.....inawezekana maana nimemuona eneo la tukio sasa hivi, kwani ana siri gani inayomfanya afanye hivyo?” Mr. Anderson alijikuta akizungumza peke yake. Hakuamini mtu aliyemuamini na kumbatiza jina la Malaika Mweusi awe muuaji, kama ni kweli alihusika hakuwa Malaika Mweusi bali Shetani Mweusi.
SASAA ENDELEA...
*******
Alianza kukumbuka siku ya kwanza walipoanza kufahamiana na Malaika Mweusi ilikuwa ni siku ambayo alikuwa amechanganyikiwa kutokana na zaidi ya miezi miwili kutokutulia nyumbani kutokana na mfululizo wa matukio ya vifo vya watu kila kukicha watu waliuawa na muuaji hakuonekana.
Kwanza yalikuwa mauaji ya mzungu mmoja aliyekuwa msimamizi wa uchimbaji wa madini. Kabla hajajua kinachoendelea vikatokea vifo vya kutisha vya wazungu wengine sita ambao waliuawa kinyama kwa kupigwa risasi nyingi miilini. Hali ile ilitishia jiji na kufanya kikosi cha upelelezi na jeshi zima la polisi uwa katika wakati mgumu wa kuhangaika huku na huko kuwasaka wauaji wenye mbinu za kijasusi.
Kutokana na kuwa bize katika suala la kutafuta muuaji usiku na mchana bila mafanikio hali ilimfanya Anderson kutokuwa karibu na mkewe. Kitendo cha kutolala kila siku nyumbani na mkewe na kutopata muda wa kuzungumza, kwa muda mwingi, kuwa bize na shughuli za serikali. Hali iliyosababisha mkewe amjie juu na kumuomba achague moja kazi ama mke.
Pamoja na kumwambia mkewe umuhimu wake kwa taifa lake, kuwa yeye ni mtumishi wa watu. Lakini mkewe hakumuelewa na kutishia endapo ataendelea hivyo basi yeye atarudi nyumbani kwao.
Anderson alifikiri kuwa ni utani, siku moja aliporudi kutoka kwenye msako wa muuaji hakumkuta mkewe alikuwa amerudi kwao, alijikuta amechanganyikiwa. Muuaji hakumtia mkononi na mkewe ndio amekimbia na alipokwenda kwao alimkatalia katakata huku akimwuliza:
“Huyo muuaji ameshampata?”
“Bado.”
“ Kama bado unanifuatia nini?”
“Sikiliza mke wangu muuaji na ndoa yetu ni vitu viwili tofauti kila kitu kina nafasi yake.”
“Kwa hiyo muuaji amechukua nafasi zote au sio? Basi mimi nakuachia umsake huyo muuaji ni mtu mwenye mbinu za hali ya juu hivyo kumtia mikononi ni vigumu itachukua muda mrefu.”
“Mimi kurudi nyumbani sitaki chagua moja uachane na kazi hiyo ya kumsaka muuaji au la mimi niendelee kubaki nyumbani.”
“Mke wangu elewa kazi ndiyo inayotuweka mjini, sasa nikiacha unataka tukae tunatazamana, tutakula mawe?”
"Ina maana hiyo kazi nzito umeanza leo, tuna miaka minne sijaona kitu kama hicho basi watu wote walioolewa na watu kama ninyi hawafurahii maisha ya ndoa?”
“Hapana mambo haya hutokea kwa msimu hivyo nivumilie.”
“Siwezi, we endelea sijakuzuia, najiona sina tofauti na mlinzi wa nyumba, mara simu ililia Anderson alilipokea ilikuwa inamjulisha kifo cha meneja wa wa kampuni ya mafuta jijini ambaye amekutwa ofisini kwake.
Anderson alijikuta katika kipindi kigumu, alijiuliza atamwelezaje mke wake juu ya ujumbe alioupata muda ule.
“Unashangaa shangaa nini?” Mkewe alimuuliza.
“Aah! Kawaida.”
“Wee nenda,” mkewe alisema baada ya kuigundua simu ilikuwa ya kazi.
“Sawa….. sasa tutaongea vizuri nikirudi mpenzi.”
“Sawa, lakini hakikisha unampata muuaji ama sivyo uzi ni uleule, bai,” mkewe alimuaga huku akishikilia msimamo wake.
Anderson aliingia katika gari na kuelekea eneo la tukio, alijikuta katika kipindi kigumu maishani mwake toka atoke tumboni kwa mama yake. Kazi aliipenda ndiyo inamfanya aitwe mwanaume na mkewe vile vile anampenda ni zaidi ya kazi kwani ndiye pumbazo la moyo wake suruhisho la mawazo yake.
Ule usemi wa mwili mmoja wa mke na mume, mkewe Sarah aliudhinisha kwani alikuwa mshauri mwema wa mumewe. Alimlea kama mwanawe na mtoto wao wa kike Gift.
Hali ya mkewe kubadilika ilimchanganya, alikuwa na haki ya kulalamika, mwezi wa pili hajalala ndani kwa kusaka muuaji. Heri angempata kuliko kuwa kama anazurula bila mpango.
Anderson alifika kwenye eneo la tukio kwenye ofisi moja iliyopo katikati ya jiji, alikuta umati wa watu wengi. Alijipenyeza katikati yao na kukutana na kijana wake walipanda juu ya ghorofa ya tatu.
Waliingia na kumkuta mtu mmoja mwenye umbo kubwa aliyevaa kinadhifu akiwa amelalia meza akitokwa na povu lililochanganyika na damu. Walimnyanyua na lile povu liliochanganyika na matapishi yenye damu lilichuruzika chini ya meza.
Anderson baada ya kumchunguza yule mtu aliwaamuru vijana wake kumpeleka hospitali kwa ajili ya uchunguzi. Alimchukua secretari wa meneja aliyeuawa, na aliondoka naye kwa mahojiano zaidi.
Walipofika ofisini alikuwa na mahojiano mafupi na secretari.
“Binti una muda gani katika ofisi ambayo imetokea mauaji?”
“Ni mwaka na miezi mitano sasa.”
“Unazifahamu vizuri tabia za bosi wako?”
“Kuzifahamu kivipi?”
“Yaani muundo wa maisha yake kwa ujumla.”
“Si sana.”
“Nieleze unavyomfahamu.”
“Bosi ni mtu mpole, mcheshi na alikuwa anajali wafanyakazi wote tulio chini yake.”
“Unaweza kunieleza kifo cha bosi wako kimetokana na nini?”
“Kwa kweli sijui.”
“Ni nani aliyegundua bosi wako ameshafariki?”
“Mimi.”
“Uligundua kivipi?”
“Wakati nampelekea kahawa kama ilivyo kawaida yake, muda ukifika ni lazima nimpelekee. Nilishangaa kumkuta bosi kalalia meza na povu lililochanyanyika na damu lilimtoka mdomoni.”
“ Baada ya kuona hivyo ulifanya nini?”
“Nilipiga kelele ya woga iliyowafanya wafanyakazi wenzangu waje kuangalia kuna nini, ndipo ilipojulikana kuwa amefariki na kuamua kujulisha chombo cha usalama.”
“Ni nani aliyeingia ofisini kwake kwa mara ya mwisho?”
“Mmh! Sina uhakika sana…Aaaha, sawa ni msichana mmoja hivi.”
“Unamkumbuka sura yake?”
“Hapana alikuwa amevaa hijabu iliyomfunika uso na alikuwa akizungumza lafudhi ya Kiunguja.”
“Alichukua muda gani?”
“Mmh! Sina kumbukumbu sidhani kama alitoka, maana nina uhakika sikumuona akitoka. Hata muda wa kumpelekea kahawa nilijua bado yupo nilibeba vikombe viwili, ajabu sikumkuta na kukuta bosi katika hali kama vile nilivyoeleza.”
“Unadhani ni muda gani alipita toka yule msichana aingie na wewe kupeleka kahawa?”
“Zaidi ya saa tatu.”
“Saa tatu! Mazungumzo gani ambayo hukuyatilia wasi wasi?”
“Saa tatu mbona ni chache, huzungumza na wateja zaidi ya saa sita.”
“Sawa, unaweza kwenda lakini uwe tayari muda wowote tunakuhitaji.”
“Sawa muheshimiwa,” yule secretari aliruhusiwa kuondoka.
Anderson aliongozana na baadhi ya vijana wake kuelekea hospitali kwa ajili ya majibu ya kifo cha meneja. Alipofika alipata maelezo kuhusiana na kifo cha meneja wa kampuni ya mafuta. Dokta alimweleza kuwa kifo cha meneja kimetokana na kupuliziwa dawa ya sumu iliyoharibu mapafu na kifua.
Kwa mara ya kwanza Anderson aliona kazi ya upelelezi ni ngumu, kumtafuta mtu asiyemjua na mtu mwenyewe awe na ujuzi wa hali ya juu anayefanya mauaji yake kwa mpangilio wa hali ya juu. Wakati anatoka hospitali alikuwa ni mwingi wa mawazo juu ya mauaji yale alijiuliza maswali yasiyo na majibu.
“Kwa nini muuaji ameamua kufanya vile, lazima ipo sababu yake au ndiyo kiasasi? Na kama kisasi kwa nini asitoe taarifa kwenye vyombo husika ili wabaya wake wakamatwe na kufunguliwa mashtaka? Mbona mauaji yenyewe yanachanganya? Mmh! Kazi ya upelelezi ni ngumu kumtafuta mtu usiyemjua inawezekana kabisa anakufahamu na kula naye meza moja.
Mmh! Kweli huu ni mwaka wangu, muuaji ananichanganya na mke wangu aishi vituko vinavyotishia maisha ya ndoa yangu. Kitu kisichowezekana eti niamue kuacha kazi tutakula mawe?”
Anderson alijikuta anazidi kuchanganyikiwa, ili kutuliza mawazo aliamua kuingia katika ukumbi mmoja wa starehe wa Puzzo Hill Hotel na kutafuta meza moja ya pembeni mwa ukumbi uliokuwa umejaa watu. Lakini kuna meza moja ilikuwa tupu watu ndiyo kwanza walikuwa wamenyanyuka.
Alipoketi kitini alionekana mtu mwenye mawazo mengi, mikono ilikuwa shavuni. Hata mhudumu alipofika kumsikiliza mbele yake hakumuona.
“Samahani kaka nikusaidie nini?”
“Ooh! Samahani dada yangu nilikuwa mbali nisaidie safari mbili.”
”Sawa kaka yangu punguza mawazo, kama huna kampani mimi nipo kwa ajili yako.”
“Asante dada yangu nitakapohitaji nitakujulisha.”
Yule mhudumu alifuata bia huku sehemu zake za nyuma akizitingisha, naye hakuwa haba Mungu alimjalia. Anderson aliyekuwa katikati ya mawazo hakukiona alichokifanya muhudumu yule. Baada ya kumuagiza alizama tena ndani ya dimbwi la mawazo kwa kurudisha mikono yake shavuni.
“Samahani mpenzi kinywaji hiki,” mhudumu alishtuka zaidi ya mara mbili, Anderson alizipiga zote mbili kama tarumbeta kisha akaagiza nyingine mbili. Nazo alizipiga kama tarumbeta zilipofika sita aliagiza nyingine mbili ambazo alikunywa taratibu muda huo sasa ulikuwa majira ya saa moja usiku.
***
Anderson aliamka siku ya pili yake na kugundua sehemu alipolala si nyumbani kwake ilikuwa sehemu ngeni. Alipepesa macho yake, alishtuka kuona pembeni yake amelala binti mwenye urembo wa shani. Kama yule binti angekuwa mweupe na uzuri ule basi angejua ni jini.
Binti aliyelala pembeni yake alikuwa na uso wa kitoto yaani ‘baby face’. Alikuwa amepitiwa na usingizi wa fofofo, Anderson alianza kujiuliza:
“Hapa ni wapi?”
Alipepesa macho yake na kugundua pale ni nyumba ya wageni, alijiuliza amefikaje pale, kutoka alipofunga ndoa na mkewe hajawahi kulala nje, pasipokuwa na sababu za kikazi wala kuwa na uhusiano na mwanamke yeyote zaidi ya mkewe mama Gift.
Alijiuliza yule mwanamke ni nani mbona hamtambui ilibidi avute hisia za jana ilivyokuwa.
“Mmh! Jana nilipotoa hospitali nilikwenda Puzzo Hill Hoteli..Ehe nimekumbuka, niliagiza vinywaji.. eeh.. sawa.. aliingia msichana aliyeushtua moyo wangu aliyekuja moja kwa moja ahadi kwenye meza yangu na kuniambia nikae naye.
”Oooh sawa nilimkubalia na kuanza kunywa pamoja, mmh nina imani hapo ndipo mwisho wa kumbuumbu zangu. Lakini kilichoendelea sikujua cha kushangaza nimeshituka alfajili hii na kujikuta nipo hotelini na mtu nisiyemjua wala kuwa na uhusiano naye.
“Hizi pombe sasa zinanipeleka pabaya Mungu wangu! Sijui nimefanya nae ngono? Na kama nimefanya sijui kama nimetumia kinga huu ndiyo mwanzo wa kuambukizwa ukimwi.”
“Vipi umeamka zamani,” Sauti tamu mithili ya kinubi cha mtume Daudi alichotumia kumbembeleza mfalme Sauli, ilipenya wenye ngoma za masikio ya Anderson na kumfanya alishtuka kutoka kwenye lindi la mawazo.
“Eeeh!”
“Pole sana kaka yangu, inawezekana kuna jambo linakutatiza lililokuchanganya akili yako, tena si dogo ni kubwa,” alisema yule binti huku akitambaza mikono yake laini mgongoni kwa Anderson.
Habari zile zilizidi kumchanganya ilibidi amuulize yule binti kwa ukali.
“Hizi habari zangu umezijuaje? Wewe ni nani na hapa ni wapi na nimefikaje?”
“Aah! Kaka yangu unaniuliza kwa ukali hivyo au wema wangu kwako umekuwa mbaya? Basi nisamehe kwa wema wangu.”
Kauli tamu ya binti mrembo ilimfanya Anderson kuwa mpole.
“Samahani dada yangu, sikuwa na nia hiyo kauli yangu imekuwa kali naomba nisamehe kwa hili.”
“Basi kaka yangu jana nilipoingia ukumbini, sehemu zote zilikuwa zimejaa watu ila meza uliyokuwa umekaa peke yako ilikuwa na nafasi ndipo nilipokuja kukuuliza kama una mtu ulinijibu kuwa uko peke yako kwa sauti ambayo ilionyesha umeshaanza kulewa.
“Tulijumuika pamoja na tukaanza kunywa kwa pamoja huku ukinikataza nisilipe utalipa wewe. Tulipokuwa tukiendelea kunywa ulionekana ni mtu mwenye mawazo mengi. Ilikuwa haipiti dakika mbili lazima ujifyonye na kila nilipokuwa nikikuuliza, ulinijibu we acha tu.
“Sikujua una maswahibu gani kilichonishangaza zaidi ni unywaji wako wa pombe wa kupita kiasi. Hata nilipojaribu kukukataza ulinikaripia nikuache la sivyo utanifukuza.”
“Nilikuacha unywe utakavyo, ukinywa mpaka ukawa ujielewi na kulala juu ya meza, nikawa sina jinsi siwezi kukuacha peke yako unaweza kuiibiwa na vibaka vitu vyako si unajua jinsi vibaka wanavyo watamani walevi.
“Ilibidi nikunyanyue kwa shida mpaka nje kwenye gari lako, kwani nilikuwa nalijiua wakati unateremka garini nami nilikuwa naingia. Nilipokupapasa nilikukuta na funguo ya gari na pesa shilingi laki mbili na ishirini. Nilikukokota hadi kwenye gari na kukupeleka sehemu ambayo utapumzika kwa amani hadi asubuhi hii uendelee na shughuli zako.”
“Mmh! Siamini wewe ni msichana wa ajabu hii ni hoteli gani na gari langu liko wapi?”
“Hapa ni Biski Hill Hotel, Hoteli ya kitalii iliyo pembeni mwa bahari yenye ufukwe mwanana na gari lako lipo salama kwenye maogesho ya magari ya hoteli hii.”
“Siamini wewe ni kiumbe wa ajabu lazima nilipe fadhila zako.”
“Hapana sikukutendea wema ili unilipe fadhila, bali ni msaada kama msamaria mwema.”
“Sawa, suruali yangu ipo wapi?” Mr Anderson aliuliza.
Yule msichana alimletea, aliingiza mkono mfukoni na kuhesabu fedha zake na kuzikuta sawasawa pia simu yake ilikuwemo, alichukua laki moja na kumpa yule msichana kama asante.
“Hapana kaka yangu ukinipa siku nyingine nitachukua siyo leo.”
Wakati huo yule binti alikuwa akinyanyuka kutoka kitandani na kuelekea bafuni kuoga alipotoka bafuni alivaa nguo zake na kumuaga.
“Samahani kaka wacha nikuache uendelee kupumzika,” yule binti aliupitia mkoba wake ili aondoke, Anderson alitaka kumfahamu vizuri.
“Samahani mrembo, unaitwa nani?”
“Naitwa Teddy”.
“Ooh! Jina zuri kutokana na vitu ulivyonitendea sina budi kukubatiza jina lingine.”
“He! Lipi tena hilo?”
“Nakuomba nikuite ‘Black Angel’ Malaika Mweusi.”
“Sidhani kama ninalingana na hilo jina,” Teddy alisema huku akibinua midomo kike.
“Siku zote kioo cha kujifahamu ni yule aliye pembeni yako wewe mwenyewe hata siku moja huwezi kujijua,” Anderson alisema huku akimtamaza yule binti.
“Nakushukuru kwa jina hilo, langu umelijua sijui wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Anderson.”
“Nakushukuru kaka yangu kwa kulijua jina lako, nilikuwa na hamu ya kujua nini kilichokusibu lakini muda hauniruhusu ila siku yoyote Mungu akijalia tutaonana.”
”Hapana Malaika wangu, nina mengi ya kuzungumza kila nikikuangalia sipati jibu. Hivyo nakuomba jioni ya leo tukutane Puzzo hoteli.”
”Sawa basi tukutane saa 12:00 jioni tuwe na ahadi za uhakika japokuwa wengi wanakasumba kusema za kizungu, ina maana mzungu akichelewa atakuwa na ahadi za Kiswahili?”
“Inaonekana u muelewa sana, kwa kugundua kasumba iliyotutawala wengi.”
Anderson aliagana na Mailaka Mweusi, alipotaka kumsindikiza alitakataa.
“Kwa nini nisikusindikize?” Anderson alihoji.
“Hapana usisumbuke kuna usafiri hapo nje unanisubiri,” Malaika Mweusi aliondoka na kumwacha Anderson bado akiwa kitandani amejifunga shuka.
Baada ya Malaika Mweusi kuondoka Anderson alibakia na maswali mengi kichwani juu ya msichana yule aliyetoka muda mfupi na kukiacha chumba kikinukia manukato ya bei mbaya. Alimshangaa yule msichana alikuwa wa aina gani, wasichana wengi jijini hujiuza ili kujikimu na ugumu wa maisha. Lakini ilikuwa tofauti na tena kwa tofauti kubwa. Alikuwa na uwezo wa kuchukua kila kitu hata gari, lakini kila kitu amekikuta kipo katika hali nzuri, ilikuwa ajabu kubwa kwake.
Aliomba jioni ifike haraka ili aweze kuonana na binti wa ajabu aliyemfananisha na Malaika Mweusi. Aliona hakuna muda wa kuendelea kuwa pale alinyanyuka na kwenda bafuni kuoga ili akirudi nyumbani kubadili nguo ili aingie ofisini kumtafuta muuaji ambaye ameichanganya akili yake kila kukicha na bila ya kumsahau.
Mke wake aliyempa masharti ya kutorudi nyumbani mpaka awe amempata muuaji sharti lililompa wakati mgumu. Lakini vitu alivyofanyiwa na Malaika Mweusi vilimpunguzia mawazo yake aliyaelekeza kwake alimuona ni msichana wa ajabu.
Kutwa nzima alifanya kazi lakini akili yake yote ilikuwa kwa Malaika Mweusi msichana wa ajabu ambaye akuwahi kumuona katika maisha yake yote. Ilipotimu saa kumi jioni alirudi nyumbani alijiandaa kwa ajili ya kukutana na Malaika Mweusi.
Anderson alivalia nguo zenye hadhi ya juu na kujipulizia pafyumu ya bei mbaya ambayo huitumia mkewe ili aonekane mtu wa hali ya juu. Alijitazama kwenye kioo na kujiona amependeza kwani nguo zilikuwa zimemkaa vyema, alitazama saa yake ya ukutani iliyomuonyesha ni saa kumi na moja na robo alijua muda ule utamtosha kufika Puzzo Hoteli.
Alikwenda kwenye banda la gari na uchukua gari lake tayari kwenda Puzzo Hoteli kwa ajili ya kuonana na Malaika Mweusi binti wa ajabu ambaye alimfanya asiamini kama kweli aliyoyafanya yanatendeka katika dunia ya sasa ambayo asilimia kubwa ya akina dada wamekuwa na roho ya kinyama.
Kwa hali aliyomkuta angeibiwa kila kitu ikiwa pamoja na gari lake. Majira ya saa kumi na mbili kasoro dakika tano aliwasili eneo la Puzzo Hotel, alipepesa macho yake huku na kule ili atafute sehemu nzuri ya kuegesha gari lake na baada ya muda aliiona sehemu nzuri ya kuegesha gari lake.
Akiwa katika harakati za kupaki gari lake mara gari dogo aina ya Mitsubishi Pajero nyeusi ilipita na kwenda kusimama mbele yake, akiwa anasubiri lile gari limpishe aliteremka binti mrembo katika lile gari.
Anderson alijikuta anapigwa na bumbuwazi na woga wa kumtawala alijikuta akijisemea moyoni. Yule msichana alipiga hatua za alipiga hatua za taratibu kwenda alipo.
Ile ilimpa nafasi ya kumsoma vizuri yule mrembo sura na umbile lake alianza kumwangalia toka nywele zake za rasta ndogondogo zilizoishia mgongoni na usoni alivaa miwani ndogo ya mviringo iliyobebwa na pua ndogo ya kitusi, midomo yake midogo ambayo ilionekana kama iliumbwa kwa matumizi ya vitu laini na vinywaji baridi.
Akiwa bado anamkazia macho yule msichana aliyekuwa amemuelekea alikutana na tabasamu lililozidisha uzuri wa binti aliyekuja mbele yake ambaye alionesha kama anamfahamu lakini kwake alikuwa mgeni.
Lilikuwa tabasamu tamu lililonakshiwa na mwanya mwembamba lililopoteza mawasiliano katika ubongo wa Anderson. Yule msichana alikuwa amevalia brauzi cha rangi ya jani la mgomba iliyoishia juu ya kitovu na kuliacha tumbo lake dogo wazi kidogo, chini alivaa sketi yenye rangi kama kiblauzi iliyoishia kidogo juu ya makalio kutokana na kupasuliwa kwa nyuma na nyuma alikuja amejaaliwa kiasi hakika mwenyezi Mungu alimpendelea kwa kila kitu.
Shingoni alikuwa na cheni tatu za dhahabu hesabu ya haraka haraka zilikuwa na thamani ya milioni mbili kasoro, masikioni kila sikio lilitobolewa matundu matano na kila tundu lilikuwa na hereni ya dhahabu, vidoleni kila kidole kilikuwa na pete ya dhahabu ya miundo tofauti mkono mmoja ulikuwa na bangili ya dhahabu na mwingine ulikuwa na saa ndogo vilevile ya dhahabu, mdomo ulikuwa na meno mawili ya dhahabu.
Tabasamu ya yule binti nusra lisimamishe mapigo ya moyo katika mwili wa Anderson. Akiwa bado ameshangaa kama kaona meli barabarani yule binti mrembo alipita upande wa pili wa mlango wa gari la Anderson na kufungua mlango baada ya kuingia alifunga mlango.
Aliona kama yupo ndotoni baada ya kuona ule mlango unafunguliwa na yule msichana mwenye uzuri wa ajabu aliyevaa vitu vyenye mamilioni ya pesa.
“Eeeh…unataka lifti?’ Aliuliza huku akimtupia jicho la wizi.
“Anderson vipi?” yule msichana alisema kwa sauti tamu na laini. “Unasemaa….Umejuaje jina langu?” Anderson alimshangaa yule mrembo.
“Unanitania au unasema kweli?” binti mrembo aliuliza.
“Si utani, we nani na umejuaje jina langu?”
“We umekuja kukutana na nani hapa?”
“Swali lile lilimshtua Anderson alituliza akili na kumuangalia yule binti aliyekaa pembeni yake ambaye kipindi hicho alikuwa amevua miwani yake. Taratibu sura yake ilianza kumjia na kugundua ni Malaika Mweusi lakini huyu ni mzuri mara dufu lakini harufu ya manukato yalimfanya abahatishe.
“Ina maana wewe ni Malaika wangu?”
“Ndio mimi wala si mwingine,” Malaika alijibu huku akilegeza sauti.
“Umebadilika kwa asilimia mia.”
“Si kweli, sura na umbile lilelile kilichobadilika ni mavazi.”
“Malaika Mweusi umependeza sana, hongera sana unastahili pongezi zangu.”
“Nashukuru, sasa ni hivi geuza gari tuelekee tulipolala jana, ni sehemu inayofaa kwa mazungumzo,” Malaika alimweleza Anderson.
Anderson aligeuza gari na kwenda Biski Hoteli, waliposhuka Biski Hoteli walikwenda moja kwa moja hadi mapokezi. Chumba kimoja kilikuwa laki mbili na nusu moja za Kitanzania. Mr Anderson aliingiza mkono mfukoni ili atoe malipo ya chumba lakini Malaika Mweusi alimkataza.
“Hapana nitalipa mimi,” Malaika Mweusi alifungua mkoba wake na kutoa noti kumi za kumikumi na kulipa. Walipewa chumba kimoja chenye kila kitu, walipoingia chumbani Malaika Mweusi alikaa kitandani na Anderson alikaa kwenye sofa. Malaika Mweusi alihama kutoka kwenye kitanda na kumsogelea karibu na Anderson, wakati huo Anderson alionekana mtu mwenye mawazo mengi.
“Vipi Mr Anderson naona uko mbali?”
“Ha…ha..pana tuko pamoja.”
“Nina imani huu ni muda mzuri wa kuzungumza lililokusibu jana,” Malaika Mweusi alisema huku akitembeza kikono yake kwenye kifua cha Mr Anderson.
“Halina umuhimu sana tuachane nalo.”
“Hapana Anderson nipo hapa kwa ajili yako nimeacha kazi zangu naomba ujali muda wangu na pia ni muhimu mimi kuwa hapa,” Malaika Mweusi alisema kwa msisitizo. Anderson hakupenda mambo yake yatoke nje wala siri ya kazi yake. Akabaki katikati ya mawazo, Malaika Mweusi alimstua.
“Mr. Anderson naona huna la kuongea?” Malaika Mweusi alinyanyuka na kutaka kuondoka.
“Hapana usiondoke na nitakueleza,” Anderson alinyanyuka na kumshika mkono Malaika.
Wakati huo Malaika Mweusi alikuwa ameshachukua mkoba wake ili aondoke, Anderson alimshika mkono na kumrudisha kwenye sofa.
“Samahani Malaika wangu sina nia ya kukuudhi bali linataka maelezo ya kina.”
“Ndio maana nikaamua kuondoka kwa vile sina msaada kwako wala umuhimu wowote,” Malaika alijibu kwa hasira kidogo.
“Hapana Malaika wangu sina maana hiyo wewe ni mtu ninaye kuona una umuhimu wa kipekee kuliko hata hao niliokuwa nao muda mrefu. Wewe kwa ufupi inaonyesha jinsi gani unanijali sina budi nikueleze kilichonisibu.
“Usinieleze kwa kukulazimisha haitakuwa vizuri bali kwa hiari yako.”
“Nitakuelewa kwa hiyari yangu.”
“Haya nieleze.”
Anderson alimweleza masahibu yote yanayomzonga ubongo wake hadi hatua ya kuichukia dunia na kujuta kwa nini amezaliwa mwanaume. Alikuwa amechanganywa na mauaji yaliyokuwa yakitikisa jiji kwa takribani miezi miwili na nusu. Akiwa katika mtihani mzito wa kumsaka muuaji mkewe naye alimjia juu kwa kitendo cha kukosekana nyumbani usiku na mchana na muuaji haonekani kila moja lilimchanganya sana.
“Nashindwa Malaika wangu nifanye nini, muuaji amenichanganya akili nyumbani nako mke wangu anazidi kunichanganya ati niache kazi, unafikiri nitakuwa mgeni wa nani utaishi vipi bila kazi?” Anderson kwa mara ya kwanza alijikuta anitoa siri ya kazi yake kosa lilikuwa kubwa kumuamini usiyemjua.
Malaika Mweusi baada ya kumsikiliza kwa kina alimsogelea Anderson aliyekuwa ameweka mikono shavuni akionesha wazi kuwa amekosa ufumbuzi wa matatizo yaliyokuwa mbele yake.
Malaika Mweusi aliuweka mkono wake mgongoni kwa Anderson na kuongea kwa sauti yake tamu mithili ya kinubi cha mfalme Daudi, aliongea kwa sauti ya chini:
“Pole sana Anderson kweli mzigo uliokuwa mbele yako ni mzito sana unahitaji msaada mkubwa... sasa ni hivi….”

ITAENDELEA JUMANNE
 
HADITHI: MALAIKA MWEUSI
SEHEMU: 03
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500
ILIPOISHIA:

Malaika Mweusi baada ya kumsikiliza kwa kina alimsogelea Anderson aliyekuwa ameweka mikono shavuni akionesha wazi kuwa amekosa ufumbuzi wa matatizo yaliyokuwa mbele yake.
Malaika Mweusi aliuweka mkono wake mgongoni kwa Anderson na kuongea kwa sauti yake tamu mithili ya kinubi cha mfalme Daudi, aliongea kwa sauti ya chini:
“Pole sana Anderson kweli mzigo uliokuwa mbele yako ni mzito sana unahitaji msaada mkubwa... sasa ni hivi….”
SASA ENDELEA...

Malaika Mweusi alizungumza huku akimpapasa Mr Anderson shingoni na kumfanya asisimke huku aliendelea kuzungumza:
“Ni hivi suala moja nitajaribu kulitatua lakini jingine liko nje ya uwezo wangu.”
“Lipi hilo?”
“La mkeo.”
“Utanisaidiaje?” Anderson aliuliza huku akigeuka kumtazama Malaika aliyeonesha hana wasiwasi.
“Unajua siku zote kila kitu kina nafasi yake, kazi ina nafasi yake na mkeo ana nafasi yake vilevile, kwa hiyo unaweza kupanga muda wako vizuri tu. Utashangaa kazi inakwenda na huku ukifurahia maisha yako ya nyumbani kama kawaida.
“Lazima uelewe kutokana na ugumu wa kazi yako lazima mwezi wako awe pozeo la yote yanayokuchanganya siku nzima,” Malaika alisema kwa sauti ya upole.
“Ungekuwa wewe ungefanyaje?” Anderson aliuliza akitegemea msaada wa Malaika.
“Swali zuri, ningekuwa mimi tena una nafasi ya juu wewe ndio top kuanzia asubuhi unadili na kazi za serikali lakini jioni unakuwa na mamaa ili kupoteza akili kwa ajili ya kupanga mikakati kwa kazi inayofuata.
“Ni wazi inaichosha sana akili yako huna muda kuiacha akili yako ipumzike kwa kufurahi na mkeo na mwanao, kitu kitakacho kufanya usahau matatizo ya mbele.”
“Sawa kuna matatizo yanatokea usiku unafikiri nitaacha kwenda?”
“Matukio ya usiku ni siku moja moja lakini imekithiri na kuwa kero kwenye ndoa hata mimi nisingekubali miezi miwili na nusu unanusa nyumbani na kuondoka mkeo ana haki, ni kweli kabisa unaweza kuzipunguza kazi zisizo na umuhimu.
“Haya tangu tuanze kumtafuta muuaji hata fununu yake hujaipata zaidi ya kujigeuza walinzi wa sungusungu.’’ Malaika alisema kwa utulivu tofauti na umbile na umri wake.
“Nimesikia nitajaribu.’’
“Si kujaribu anza kutekeleza sasa, mfuate mkeo ikiwezekana ukitoka hapa mweleze kama nilivyokueleza nakutakia muafaka mwema. Ila suala la kumpata muuaji hilo lipo nje ya uwezo wangu, nina imani umenielewa?”
“Nimekuelewa Malaika wangu nitatekeleza yote uliyonieleza.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda, Anderson na Malaika Mweusi waliongozana na kutoka nje ya Hotel ili kurudi mjini.
“Naomba nikupeleke kwako.”
“Hapana we nenda tu, mimi nina usafiri wangu nitafika sasa hivi ila mwisho wa wiki tukutane nijue umeutumiaje ushauri wangu.”
Anderson na Malaika Mweusi waliagana ilikuwa ni majira ya saa mbili usiku. Aliamua apitilize moja kwa moja hadi Sinza kwa mkewe mama Gift ili warudi nyumbani.
Alipofika alimweleza mkewe jinsi atakavyoutenga muda wake wa kazi na muda wa kukaa na familia yake kama alivyoelezwa na Malaika Mweusi. Mkewe alimjibu:
“Kama itakuwa hivyo mimi sina kipingamizi ila ukienda kinyume na haya unayonieleza basi nikiondoka tena usinifuate, sawa umenielewa?”
“Ndiyo mke wangu.”
Alimchukua mke wake na kurudi naye nyumbani Mikocheni walipokuwa wakiishi na familia yake.
****
Anderson alijitahidi kupanga muda wake wa kazi na wa kukaa na familia yake, kitu kilichorudisha upendo katika nyumba yake kama zamani. Alizidi kumuona Malaika Mweusi kiumbe cha ajabu kutokana na uwezo mkubwa wa kutatua tatizo lililokosa ufumbuzi kwa watu aliowaamini wenye busara.
Hakuamini msichana mdogo kama yeye kuwa na moyo wa busara na huruma uliojaa upendo, alipanga siku atakayokutana naye tena lazima ampe zawadi kubwa.
Alipanga zawadi gani itakayolingana na wema wake ambayo amgeiona nzuri kwake. Kumpa pesa ingekuwa utani kutokana na yule mwanamke kuonesha ana uwezo mkubwa kuliko yeye pengine mara kumi yake, aliamua kumuuliza mwenyewe anahitaji zawadi gani toka kwake.
Ilikuwa siku ya jumapili walikutana pale Puzzo Hoteli na kuongozana wote hadi Biski Hoteli. Wakiwa njiani kuna kitu kilikuwa kinagonga kwenye gari kila lilivyokuwa likienda kitu ambacho kilimkera Malaika Mweusi akabidi aulize:
“Anderson nini kinachogonga chini ya gari?”
“Aah! kuna matatizo kwenye Propela shafti.”
“Kwa nini usipeleke gereji?”
“Ugonjwa wake ni pesa nyingi kidogo na sasa sina pesa nasubiri mwisho wa mwezi.”
“Kwani kiasi gani?”
“Ni pesa nyingi kwani kuna spea mpya inatakiwa kununuliwa na matengenezo yake ni kama laki nne kasoro.”
“Sawa,” Malaika Mweusi alimjibu na kukaa kimya hadi walipofika Biski Hoteli.
Anderson kwa kuwa aliona hakukuwa na kitu kingine zaidi ya mazungumzo tu ya kawaida hakutaka kupoteza pesa kwa kuchukua chumba alionelea bora waongelee palepale kwenye gari au waende kwenye mchanga na kuzungumza.
“Kwani tatizo ni nini kama ningekuwa sina uwezo wa kulipia chumba nisingekueleza tuje huku,” Malaika alipingana naye.
“Hapana pamoja na hayo mimi naona maongezi yetu hayana haja sana ya kuongelea chumbani bora kama tungekuwa wape..,” Anderson hakumalizia.
“Nimekuelewa vizuri sana pengine labda kukushinda wewe mwenyewe lazima uwe mwelewa siku zote, ila samahani kama kauli yangu itauudhi. Wewe ni mume wa mtu sipendi kutia dosari ndoa yako ndio maana nachukua chumba ili tuongee kwa mapana zaidi.”
“Huoni kuwa ni pesa nyingi unazitumia bila sababu?”
“Pesa kazi yake ni matumizi ndio maana zinatafutwa ili zitumiwe, pesa kwangu si tatizo au ushanichoka sema tu usipindishe pindishe maneno kama safari ya nyoka?” Malaika alimuuliza akiwa amemkazia macho.
“Malaika wangu sina maana hiyo bali lazima nami nionyeshe ni jinsi gani ninavyokujali hata katika matumizi yako au hupendi ushauri wangu?” Anderson alimuuliza kwa sauti ya upole.
“Hapana, nauhitaji sana kwani umenizidi vitu vingi sikupati hata kimoja moja lakini hili halina tatizo na suala kuwa wapenzi mbona sisi ni wapenzi, siku zote hakuna urafiki bila kupendana sisi ni marafiki na pia wapenzi au mmeshazoea wapendanao wote lazima wafanye ngono?” Malaika aliuliza kwa sauti ya upole.
Anderson alikubali na kufanya waongozane wote hadi Hotelini kama kawaida Malaika Mweusi alilipia chumba.
Walipofika chumbani Malaika alitaka kujua wamefikia wapi na mkewe.
“Eeh! Lete stori, mmefikia wapi na mkeo? Ulinieleza kuwa anaitwa mama Gift eeh?”
“Ndio mama Gift.”
Anderson alimshukuru kwa ushauri wake na nasaha alizompa zilizorudisha furaha katika nyumba yake.
“Ooh, siamini kumbe nami naweza kuokoa nyumba za watu basi muda si mrefu nitafungua kituo cha ushauri nasaha,” Malaika alisema huku akionesha aibu na kumfanya achanue kama tausi bustanini na kuuongeza uzuri wake mara dufu.
“Nami nitakitangaza kila kona,” Anderson aliongezea.
Mara simu ya Anderson ikaita, naye alipokea na kuongea mara akasema:
”Hebu subiri,” Anderson alitoa pochi yake na kuchambua baadhi ya vitu fulani na kutoa business card na kuanza kumsomea mtu wa upande wa pili.
Wakati anaitoa ile business card, picha yake ya kipande ilidondoka chini ambayo Malaika Mweusi aliokota na kuangalia wakati huo Anderson alimaliza kuzungumza na simu.
Malaika mweusi alitazama ile picha na kupiga kelele ya mshituko.
“Haa! Huyu ndio mkeo?”
“Eeh, mbona umestuka baada ya kumuona una mfahamu?”
“Hapana ni mzuri sana unajua kuchagua.”
“Hakushindi wewe.”
“Ananishinda tena kwa mbali ndio maana yeye ameolewa na mimi bado nazurula.”
“Naamini ulikuwa umejificha kama ningekuona wewe nisingethubutu kuoa mwanamke mwenye kiburi kama huyu.”
“Na huyu ndiye mtoto wenu?”
“Eeh, ndio Gifti mwenyewe huyo.”
Ilikuwa ni picha ndogo ya pamoja ya familia ya Mr. Anderson yeye na familia yake.
“Sasa lini nitamuona wifi?”
“ Kwa kuwa tupo pamoja tutapanga siku ya kumuona.”
“Sawa nitafurahi kumfahamu wifi pamoja na mtoto wetu.”
Baada ya mazungumzo, kabla ya kutoka Malaika Mweusi alimuliza Anderson kuwa anahitaji kiasi gani cha pesa kwa ajili ya matengenezo ya gari lake.
“Laki nne kasoro,” Malaika Mweusi alifungua mkoba na kutoa laki nne taslimu.
“Nina imani tutakapokutana gari likuwa zima?”
“Asante sana, sijui nikushukuru vipi, sina cha kukupaa,” Teddy alizidi kumchanganya Anderson.
“Vipo vingi,” Teddy alijibu huku akitabasamu.
“Kimojawapo?”
“Ipo siku nitakwambia ni kipi.”
“Kipi mpenzi?” Anderson alitaka kujua.
“Ooh! Mbona umefika mbali, wewe ni mume wa mtu, naheshimu ndoa yako sitaki ndoa yako ivunjike, tutaendelea kuwa marafiki tu na usidhani kutaka msaada kwako ni kutaka penzi kwako la hasha bali moyo wangu umekutunuku hilo wazo litoe mawazoni,” Teddy alimkatisha tamaa Anderson.
“Sasa ni lini utaniambia kitu hicho?”
“Nilishakwambia nitakujulisha lini tena kitu hicho hakina gharama.”
“Sawa ngoja nisubiri ingawa umeniachia fumbo zito.”
“Tena imekuwa vizuri nimekumbuka kuanzia kesho nitakuwa na safari ambayo itaniweka mbali kwa wiki mbili nitakaporudi nitakujulisha.”
“Sawa japo sipendi kujua unaenda wapi.”
“Nami natarajia kukuta ndoa yako inashamiri, sitaki kusikia mkeo amerudi nyumbani kwao.”
“Sidhani, wewe nenda salama Mungu akijali tutaonana sio siri umeshaniambukiza ugonjwa wa mazoea moyo wangu huwa taabani nisipokuona hata sijui kwa nini?”
“Umenishiba, hata mimi mgonjwa juu yako ungekuwa ujaoa sijui….” Hakumaliza na kujikuta walicheka kwa pamoja huku wakigonganishiana mikono. Waliagana na kama ilivyokuwa kawaida kwa kutangulia Anderson na kumuacha Malaika Mweusi.
******
Siku ya pili tangu walipoagana na rafiki yake wa karibu aliyemteka mawazo yake Malaika Mweusi, msichana mwenye fumbo la ajabu kwake. Anderson baada ya shughuli zake za kawaida za wiki nzima aliamua kutoka na familia yake kwenye ufukwe mwanana wa Biski Beach ili kupumzisha misukosuko ya wiki nzima ya kumtafuta muuajia ambaye kwa wiki mbili alikuwa ametulia na kuacha swali kwake safari ile angefanya mauaji wapi au kamaliza kampeni yake.
Akiwa na familia yake mkewe na mtoto wake Gift walijiandaa kutoka majira ya saa sita alasiri, wakati huo mkewe alikuwa akijipodoa kwenye meza ya kujipodoa. Mara simu yake iliita na alipoziangalia namba zilikuwa ngeni kwake alijiuliza kabla ya kupokea ni nani, wasiwasi wake huenda mambo yameharibika.
Kilichomshangaza namba zote zinazopigwa katika simu yake hutoa jina, namba ile wanaoijua ni wachache na majina yao yamo kwenye simu.
Alijiuliza sijui anatakuwa ni nani na anataka nini tena katika muda ambao anahitaji kupumzika na familia yake, aliamua kupokea kwa ukali kidogo akihoji:
“Haloo, nani? Na unataka nini?” aliuliza kwa ukali kidogo.
“Samahani wewe ni Mr Anderson?” sauti ya kike iliuliza.
“Wewe ni nani?” hakumjibu alimuuliza swali.
“Kabla ujajua mimi ni nani kwanza nijue wewe ni Mr, Anderson?”
“Hii namba kakupa nani?” Anderson hakujibu zaidi ya kuongeza swali lingine.
“Mzee huu muda si wakulizana maswali mengi kuchelewa kwako ni kuendelea kuharibu mambo,” kauli ilimtaadhalisha.
“Una maana gani kusema hivyo?” alishtuka kidogo.
“Mimi ni msamalia mwema si lazima ujue ni nani aliyenipa namba yako, ukija katika eneo la tukio tutaelewana vizuri,” kauli ya upande wa pili ilizungumza kwa taratibu na kujiamini.
“Tukio! Tukio gani tena hilo?” moyo ulimpasuka kwa kujua mambo yameiva.
“Mzee, kuna vijana watatu wameingia katika moja ya ofisi tumewatilia mashaka huenda ndio wauaji wenyewe wanaofanya mauaji jijini.”
“Ooh! Ni eneo gani hilo?”
“Ni maeneo ya Jengo la Ushirika, Mnazi Mmoja pembeni kuna jengo moja lenye ghorofa mbili. Wameingia humo ndani fanyeni haraka mkichelewa tu mtakuta watu wameuawa.”
“Ooh! Ishakuwa tabu, sasa hii ni kazi gani isiyokuwa na mapumziko?” Anderson alizungumza peke kwa sauti.
“Vipi tena mume wangu ?” mama Gift aliuliza.
“Kuna tukio limetokea mnazi mmoja karibu na jengo la ushirika. “
“Sasa ndio itakuwaje?”
“Hakuna kitakachoharibika nyie jiandaeni kama kawaida ngoja niwajulishe vijana wangu waende katika tukio ili tuedelee na safari yetu.”
Anderson aliwajulisha vijana wake kuwa wakutane katika eneo la Mnazi Mmoja kwenye jengo lililo pembeni na Ushirika tayari kulivamia. Alimwacha mkewe akiwa analalama hakusikiliza lawama za mkewe aliingia kwenye gari na safari ya kuelekea Mnazi mmoja ilianza.
Alikwenda kwa mwendo wa kasi ya kuruka alitumia dakika kumi na mbili kufika katika eneo la tukio na kuwakuta vijana wake wakiwa tayari wameshafika mara moja walilitafuta jengo lililoelezwa limevamiwa.
Hali katika eneo la Mnazi Mmoja ilikuwa shwali hakukuwa na dalili yoyote ya kuwepo tukio lolote la hatari. Ilibidi wawahoji baadhi ya watu waliokuwepo kwenye eneo lile lakini kila mmoja habari ile ilikuwa mpya kwake. Walijaribu kuzunguka katika eneo lote bila kuona dalili zozote za hatari.
“Bosi hebu mpigie basi huyo mtu atuelekeze vizuri.”
Alipojaribu kupiga namba ilikuwa haipatikani.
Anderson aliwachagua vijana wake zaidi ya watano waendelee kulinda katika eneo lile na yeye alirudi nyumbani kumwahi mkewe ambaye alijua lazima safari yenyewe ataisusa.
Ilikuwa imepita saa moja tangu aondoke nyumbani kwake kwenda kwenye tukio aliendesha gari kwa mwendo wa kasi ili kumuwahi mkewe alijua akifika tu hata ndani haiingii zaidi ya kumpigia honi na kuondoka.
Alifika nyumbani kwake majira saa kumi na robo hakuwa na haja ya kuingia ndani alipofika tu alipiga honi ili mkewe atoke na kuondoka. Alipiga honi zaidi ya mara kumi lakini mkewe hakutoka alijua amesusa ilibidi ateremke garini amfuate ndani, sio siri tabia mkewe zilimchosha, jambo ndogo lazima asuse na kuwa kubwa hata kama lina umuhimu.
Aliteremka kwenda ndani, mlango wa sebuleni ulikuwa umeegeshwa aliusukuma kuingia moja kwa moja ndani huku akimuita mkewe.
“Sweet ... Ma Sweet heart, Mama Gifti upo wapi mpenzi au ndio umesusa? Njoo mpenzi nimerudi mumeo sijachelewa najua umeshajiandaa twende basi mpenzi au umerudi ndani kulala?”
Sebuleni hapakuwepo mtu alijua wapo chumbani alikwenda moja kwa moja hadi chumbani, mlango wa chumbani nao ulikuwa umesindikwa aliusukuma na kuingia ndani. Picha aliyoiona machoni mwake hakutarajia kuiona maishani mwake mpaka anakufa. Alijiuliza yupo ndotoni au wapi, alijikuta akisema kwa sauti ya juu:
“Hapana…hapana...haiwezekani,” alisema huku akishika mikono kichwani. Kilichokuwa mbele yake kilikuwa ni kweli, mwili wa mke wake ulikuwa umelazwa kitandani ukiwa mtupu kama alivyozaliwa akiwa ameuawa kifo cha kinyama.
Kilikuwa kifo cha kinyama na cha ukatili wa hali ya juu alikuwa amelazwa chali mwili wote ukiwa umechanwachanwa na matumbo yote yakiwa yapo nje, sehemu za siri zikiwa zimeharibiwa vibaya zilikuwa zimechanwachanwa na sehemu za siri zilikuwa zimewekwa kipande cha mti.
Kilikuwa ni kifo cha unyama wa hali ya juu na pembeni yake alikuwa mwanae Gifti akiwa amelalia kifuani kwa mama yake naye alikuwa ameuwawa pia. Ilionyesha kuwa Gifti alikufa kwa kunyongwa kwa kamba au mshipi kwani alikuwa hana jeraha lolote mwilini Anderson alijikuta nguvu zikimwishia na kujibweteka chini pwaaa! Huku nguvu zikimuishia kabisa.
Alilia kama mtoto mdogo akiwalilia mke na mtoto wake Gitfi, lakini alijikuta akijisemea ni upumbavu kulia kama mwanamke kwani adui anaweza kuwa yumo humo ndani na anaweza kunimaliza kirahisi.
Alijikaza kiume na alichukua bastola yake mkononi, alinyanyuka kutoka pale chini alipokuwa amejibweteka na kuanza kuanza kumsaka mbaya wake kwa taadhari kubwa. Alizunguka kila kona bila kumuona mtu yeyote aliamua kurudi ndani kuifadhi miili ya marehemu mkewe na mtoto wake Gifti zilizokuwa zimejitandaza katika kitanda kizima huku akiwa ametapakaa damu nyingi na kuchuruzika kwenye sakafu.
Aliunyanyua mwili wa mtoto wake Gifti na kuulaza pembeni ya mama yake huku mwili wake ukimtetemeka na jasho likimvuja kama maji mwili mzima. Aliuchunguza mwili wa mtoto wake na kugundua kuwa ulikuwa na jeraha shingoni likionesha kuwa amenyongwa na mshipi.
Aliuchukua mwili wa mkewe na kuufunika vizuri alinyanyua simu na kuwajulisha vijana wake yaliyomsibu. Vijana wake waliwasili haraka kumpa msaada bosi wao, miili ya marehemu wote ilipeleka Hospitali ya taifa ya Muhimbili na vijana wengine walifanya usafi sehemu zote zenye damu.
Anderson alionyesha kuwa mtu mwenye mawazo mengi juu ya tukio lile zito la kutisha. Alijawa na mawazo juu ya mbinu za hali ya juu wanazotumia wauaji, ikiwemo kumuondoa nyumbani na kupata nafasi ya kuitelekeza familia yake.
Alijikuta akijiuliza muuaji ni nani na kwanini ameamua kuua familia yake au ni kwa sababu ameanza uzijua nyendo zake. Amefanya vile ili umtisha. Lakini alijiapiza kwa hali yoyote ile atahakikisha anamtia mikononi, iwe isiwe. Aliweka nadhiri kumsaka muuaji hadi tone la mwisho la damu yake.
 
SEHEMU: 04
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Alijikuta akijiuliza muuaji ni nani na kwanini ameamua kuua familia yake au ni kwa sababu ameanza uzijua nyendo zake. Amefanya vile ili umtisha. Lakini alijiapiza kwa hali yoyote ile atahakikisha anamtia mikononi, iwe isiwe. Aliweka nadhiri kumsaka muuaji hadi tone la mwisho la damu yake.
SASA ENDELEA...
****
Mazishi ya mkewe na mtoto wa mkuu wa upelelezi Anderson yalifanyika kwa heshima zote. Kabla ya maziko wakati wa kuaga miili ya marehemu Anderson alimuahidi mkewe kwa sauti kubwa mbele ya kadamnasi:
“Ewe mke wangu na mwanangu mpenzi nendeni mkiwa mmeniachia jeraha kubwa moyoni mwangu nakuahidi damu yenu aitapotea bure. Nakuhakikishia muuaji nitamtia mkononi na kulipiza mara dufu kwa hili alilowafanyia. Eeh! Mungu wapokee na uwape makazi mazuri ili siku moja tukutane
“Ooh! Maskini ni nini nilichomkosea huyu muuaji mpaka afanye unyama wa kikatili namna hii. Eeeh! Mke wangu….Ooh! Mwanangu kipenzi Gifti, zawadi nilizopewa na Mungu baba leo inapotea kama kibatari kilichozimika kwenye upepo mkali.”
Anderson nguvu zilimwisha na kujitupa juu ya majeneza na mke wake na mtoto wake. Alilia kama mtoto mdogo kila alipofikilia kifo cha mkewe alikuwa anajiuliza kama muuaji ameona ameanza kugundua mbinu zake. Kwa nini awaue mkewe na mtoto wake ni bora angemuua yeye mwenyewe kuliko unyama alioufanya.
Kuua familia yake anakuwa hajafanya kitu chochote kwani ni sawa na kumwaga mafuta kwenye moto si kuuzima bali ni kuzidisha moto uwake kwa nguvu.
***

Wiki moja baada ya kifo cha mkewe na mtoto wake akiwa ofisini alikuwa ni mwingi wa mawazo kuhusu mbinu za muuaji. Alifikiria ujumbe ambao hupenda kuwaachia wauaji. Maneno ambayo hupenda kuyatumia ni ‘Mtetezi wa Haki za Binaadamu, Mshahara wa Dhambi ni Mauti, Hukumu baada ya Hukumu, na alioachiwa kwa mkewe kuwa ALINIMULIKA MIMI NIMEMCHOMA.
Alijuliza haya maneno yana maana gani ni wazi inaonyesha si muda mrefu muuaji atamtia mikononi kitendo cha muuaji cha kuteketeza familia yake ni dalili za mfa maji ambaye ameanza kutapatapa.
Akiwa bado kwenye lindi la mawazo simu yake ililia, alichukua juu ya meza aliziangalia zile namba kwa makini kwani zilikuwa ni ngeni kwake namba zile zilimfanya aingiwe na hofu ilikuwa ni sawa na kutonesha kidonda kilichoanza kupona.
Simu kama ile wiki iliyopita ilipoteza familia yake, alipandisha pumzi juu na kuzishusha ili kujipa ujasiri na baadaye alibonyeza kitufe cha kupokea na kuongea kwa ukali:
“Haloo nani mwenzangu?”
“Aah! Anderson mbona kila wakati unakuwa mkali hivi hata wifi anapata nafasi ya kucheka na wewe?” Ilikuwa ni sauti tamu ya kinubi cha mtume Daudi ya rafiki wake wa karibu Malaika Mweusi ambaye walipotezana kwa takribani wiki mbili kwa kuwa alikuwa safari nje ya nchi.
“Aaah! Samahani Malaika wangu umerudi lini?”
“Leo hii nina hamu kubwa ya kukuona rafiki yangu mpenzi nina imani wifi hajambo na mtoto wenu kipenzi Gift pia, nina matumaini ndoa yenu inashamiri na kuleta furaha isiyo na kifani.”
Kauli ile iliuchoma moyo wa Anderson ilikuwa ni kama kutonesha donda lililokwishaanza kupona. Jibu lilikuwa zito sana kutoka mdomoni kwake, kitu kilichomshtua Malaika Mweusi upande wa pili.
“Vipi mbona kimya nasikia ukivuta pumzi na kuzishusha au hupendi kuonana na mimi, basi samahani,” Malaika Mweusi alikata simu Anderson alikurupuka kama anatoka usingizini.
“No..no..hapana Malaika wangu sikuwa na maana hiyo wakati huo simu ilikuwa imekatwa. Kwa haraka alimpigia simu Malaika Mweusi aliipokea upande wa pili.
“Eeh! Unasemaje?”
“Samahani Malaika wangu sina maana uifikiriayo.”
“Kufikiria nini Anderson?”
”Kuwa labda sipendi kuonana na wewe Malaika, ni mambo mazito yamenipata sina msaada wowote nina imani wewe ndiye tegemeo langu la pekee. Kwanza nina shukuru kukutana nawe nipo chini ya miguu yako Malaika wangu, ni mtu wa pekee duniani unayeweza angalau kwa asilimia tano kunipa faraja maana najiona nipo katikati ya dunia na mbingu,” Andarson alibembeleza.
“Anderson mbona unanitisha una nini?” Malaika alishtuka.
“Ni mengi ya kuzungumza na wewe tukikutana, nahitaji msaada wako mkubwa kwa muda huu.”
“Sawa basi tukutane palepale pa siku zote muda uleule tafadhali jali wakati, usijali kila kitu nitalipia mimi.”
“Sawa Malaika wangu usiache kuja nakutegemea kuliko kitu chochote duniani kwa sasa.”
“Sawa Anderson lazima nifike usihofu nipo kwa ajili yako,” Malaika alimtoa hofu.
“Nitafurahi kama utafika.”’
“Usihofu nisubiri au nitawahi ili kukuonyesha jinsi ninavyokujali.”
Kwa vile muda ulikuwa umeisha Anderson alitoka ofisini na kurudi nyumbani tayari kwa kujiandaa kukutana na Malaika Mweusi. Baada ya kujiandaa aliingia garini na kuelekea Biski hoteli, aliwasili robo saa kabla ya muda waliopangaa kukutana, alitafuta eneo zuri na kuegesha gari lake aliteremka na kuhakikisha gari lake lipo kwenye usalama alielekea hotelini.
Akiwa anaelekea mapokezi alishtukia anashikwa bega alipogeuka alikutana na harufu kali ya manukato apendayo ujipulizia Malaika Mweusi alipogeuza shingo alilakiwa na tabasamu lililonakshiwa na meno madogo meupe yenye mwanya mwembamba.
“Ooh! Vizuri, kumbe tumewahi pamoja karibu sana,” ilikuwa ni sauti tamu ya Malaika Mweusi.
“Jambo nililonalo ni zito hivyo linatakiwa umakini na kujali muda,” Aderson alisema akielekea mapokezi.
“Asante, twende zetu moja kwa moja nimeshalipia mapema na ufunguo ninao.”
Waliongozana moja kwa moja hadi kwenye chumba ambacho Malaika alikuwa amelipia.
Sura ya Anderson ilikuwa imezongwa na lindi la mawazo yaliyokosa ufumbuzi. Kama kawaida Malaika Mweusi alifikia kitandani na Anderson alikaa kwenye kochi.
Kabla hawajaanza chochote kilichowapelekea pale chumbani, mara mlango ulipogongwa, alikuwa ni mhudumu alileta vinywaji na Malaika alivipokea na kufunga mlango kwa ndani.
Aliruhdi hadi kochini akiwa na glasi mbili za vinywaji na kukaa pembeni ya Anderson.
“Karibu,” alimkabidhi glasi moja.
“Asante,” alijibu huku akiipokea na kugongesha glasi kutakiana afya njema.
Baada ya kimya kifupi Malaika kwa sauti ya upole aliuvunja ukimya ule.
“Ndiyo Mr. Anderson nipo hapa kwa ajili yako, nipo tayari kukusaidia kwa kadri ya uwezo wangu,” maneno ya Malaika yalimpa faraja Anderson.
Kwa ujasili mkubwa alianza kumhadithia kuanzia mwanzo hadi mwisho yaliyomsibu wiki moja iliyopita. Simulizi lile lilimshtua sana Malaika Mweusi na kuangua kilio kilichomshtua hata Anderson.
“Malaika mbona unanivunja nguvu? Wakati wewe ndiye niliyekutegemea unaonyesha udhaifu sasa unafikiri nani atanisaidia?”
“Anderson inauma ni unyama wa aina gani huo, mkeo amekosa nini mpaka apewe adhabu kubwa namna hiyo, inauma…inauma….mtoto Gift amekosa nini? Mtu kama huyu si wa kuhurumiwa hata kidogo,” wakati huo Malaika Mweusi alikuwa analia akiwa kajitupa chini.
Ilibidi Anderson afanye kazi ya ziada kumbembeleza:
“Malaika wangu wewe ndiye niliyekuwa nakutegemea, unalia hivyo nani atakaye nisaidia?”
“Inauma sana wacha nilie nikamue uchungu uliopo moyoni mwangu ili niweze kujua nini nitakachokusudia,” baada ya kimya ndipo Malaika Mweusi alipoanza kusema:
“Ni kweli inaniuma sana lakini cha kufanya kwanza kabisa kabla ya yote nakuahidi nitashirikiana na wewe katika kipindi chote cha majonzi nitakuliwaza na kukufariji,” Malaika alisema huku akinyanyuka alipokuwa amekaa.
“Hilo nashukuru sana, je, la huyu muuaji utanisaidia vipi?”
“Sipendi kukudanganya suala la polisi mimi sijui chochote lakini kuna umuhimu wa kuwatumia hata Interpool (polisi wa kimataifa) nina imani ninyi kazi iliyopo mbele yenu naona imewazidi na siku zinakatika na mauaji yanaongezeka kila kukicha. Ni vizuri kusema umeshindwa ili upate msaada.”
Malaika alitumia muda mwingi kuongea na Anderson baada ya kikao chao kilichowarudisha katika fikira nyingine ambazo ndizo zingekuwa suluhu ya matatizo ya Anderson.
Hata hivyo kila mmoja alikuwa na fikra tofauti ndani ya moyo wake kutokana na ukaribu wao waliokuwanao. Anderson hisia zake zilikuwa katika mapenzi yaani wako bibi na bwana.
Alijikuta akiongeza mapenzi kwa Malaika Mweusi na kumwona ndiye mwanamke anayefaa kuziba pengo la mkewe, kwani alionekana kuwa msichana aliyesimama kidete kumliwaza muda wote wa matatizo.
Kilichomshangaza ni tofauti ya mawazo yake, alihisi labda pamoja na kupenda lakini Malaika Mweusi alishindwa kumweleza kwa sababu alikuwa akijua kwamba yeye ni mume wa mtu.
Lakini alijua huo ndio ulikuwa muda mzuri wa Malaika Mweusi kulionyesha penzi kwake. Hata hivyo aliishia kuona penzi la kirafiki kama la dada na kaka.
***
Siku zote Anderson alipokuwa na Malaika Mweusi hasa sehemu za faghara, mikao na nguo alizovaa zilimfanya awe na matumaini kuwa Malaika Mweusi anamwonyesha alivyojirahisi kwake. Siku zilikatika bila mabadiliko yoyote katika uhusiano wao.

MIEZI 6 BAADA YA VIFO VYA FAMILIA YA ANDERSON.
Siku moja wakiwa faragha Mr Anderson hakuamini masikio katika mazungumzo yake na Malaika Mweusi.
“ Anderson,” Malaika Mweusi alimwita akiwa amemchanulia tabasamu pana.
“Unasemaje Malaika wangu?”
“Utakaa hivi hadi lini?”
“Una maana gani?”
“Lazima uoe ili kuondoa mawazo ya matatizo yaliyonikuta, lazima uwe na mwenza ambaye atafungua ukurasa mpya.”
Anderson alijua sasa wazo lake la kumpenda Malaika Mweusi limepata jibu.
“Ni kweli kabisa Malaika wangu, sijui utanisaidiaje?”
“Tafuta mwanamke ili ufungue ukurasa mpya yaliyopita yamepita , imebaki historia.” Malaika alisema huku akimuangalia kwa jicho la huruma.
“Ni kweli Malaika wangu, na nina imani wewe unajua nani ni chaguo langu.”
“Ni vigumu, mimi si mnajimu wala hujawahi kunidokeza nani anaweza kuwa chaguo lako baada ya kifo cha kipenzi chako mama Gift.”
“Wamjua wazi ila hutaki kumweka bayana na…”
“Ni kweli simjui, hebu nifumbue macho nami nimjue wifi yangu atakayeziba pengo la wifi yangu mama Gift.”
“Ni kweli humjui?” Anderson alimuuliza akiwa amemkazia macho.
“Simjui, kwa nini nikukatalie?”
Anderson mdomo ulikuwa mzito kumtamka huyo mwenza mtarajiwa, Malaika Mweusi alipoona amepata kigiugumizi alimuliza.
“Vipi Anderson mbona umekuwa bubu ghafla?”
“Hapana, basi kesho tukikutana utamjua vizuri hata nikikueleza utashangaa.”
“Anderson… nikueleze mara ngapi kuwa mtu huyo simjui au kuna mtu ulimuonyesha ukafikiri kuwa ni mimi? Katu sijui.”
“Utamjua tu,” Mr Anderson alimtoa wasiwasi.
“Ni vizuri na mimi nimjue wifi yangu mtarajiwa ili nikupe maksi, lakini nakuamini mjuzi wa kuchagua wasichana warembo. Ina maana huna hata picha yake?” swali lile lilizidi kumchangaya sana Anderson roho ilimwambia kwani nini asimweleze ukweli kuliko kuyaficha maumivu yake.
Alipandisha pumzi na kuzishusha kitu kilichomfanya Malaika Mweusi amwangalie usoni na kupandisha macho yake kwenye uso wa Anderson ambaye alipopeleka macho yake kwenye uso wa Malaika yalikutana na kuona aibu. Ilibidi aangalie pembeni Malaika Mweusi alimsogelea karibu na umshika bega.
“Una nini, mbona umebadilika?”
“Aah! Wacha tu,” alipoteza ujasili wa kiume.
“Hapana nipo hapa kwa ajili yako kwa hiyo usihofu nieleze tu nipo tayari kukusaidia kwa vile wewe ni mtu muhimu sana maishani mwangu.”
“U…naaa…jua,” bado Mr Anderson alipata kigugumizi
“Simjui ndio maana nataka unieleze nimjue wifi yangu.”
“Kweli unanipenda?” aliuliza swali badala ya kujibu swali.
“Hilo si swali bali upendo wangu kwako upo wazi hauhitaji maswali,” Malaika alijibu kwa sauti tamu huku akimuangalia kwa jicho la huruma.
“Upo tayari kunisikiliza?”
“Nimekusikiliza mara ngapi hadi hili linishinde kusikiliza.”
“Malaika wangu,” Anderson alimwita kwa sauti ya upole.
“Unasemaje?”
“Nakupenda sana Malaika wangu.”
“Hata mimi naelewa ndio maana nipo pamoja nawe baada ya kuelewa ulivyo na umuhimu kwenye maisha yangu.”
“Sasa mbona unielewi?” aliongea kwa sauti nyonge sana.
“Kwa lipi?”
“Kuhusu upendo wa dhati juu yako, unafikiri ni nani atakayeziba pengo la mke wangu mama Gift kwa asilimia mia kama si wewe!”
Malaika Mweusi alivyosikia vile alishituka na kuuliza kama kwamba hajasikia.
“Eti unasemaje?”
“Ni kweli kabisa kuwa wewe ndiye chaguo langu sina mwingine zaidi ya hapo sitaoa tena mwingine maishani mwangu.”
“Mmh! Mbona unanipa mtihani mkubwa nisio uweza kujibu.”
“Mtihani gani huo, kwani umeolewa?”
“Hapana.”
“Una mchumba?”
“Hapana.”
“Rafiki wa kiume?”
“Sina.”
“Sasa Malaika wangu ugumu upo wapi?”
“Sikiliza Anderson chaguo lako lilikuwa zuri ambalo hata mimi ningeweza kulipokeakwa mikono miwili lakini…”
“Lakini nini tena Malaika wangu, elewa moyo wangu wote umeubeba wewe.”
“Anderson aliyoyasema ni sawa lakini kuna vitu vinanipa ugumu wa mimi kuwa mkeo.”
“Vitu gani?”
“Unaelewa vizuri kuwa uhusiano wetu umeanza muda mrefu kabla ya kifo cha mkeo.”
“Hilo naelewa sasa tatizo ni nini?”
“Kama ulivyonieleza kifo cha mkeo kilivyokuwa.”
“Naelewa lakini mbona unapindisha si useme kipingamizi kingine lakini nina imani hakuna kipingamizi ni wazi ulikuwa hunipendi bali unanidanganya tu, nafikiri hiki ndicho kipindi cha kudhihirisha mapenzi yetu bayana.”
“Unajua Anderson unaongea tu bila ya kufikiri unachokisema kimesimama upande gani.”
“Una maana gani?”
“Mimi kama nitaolewa na wewe watu watafikiri mambo mengi kuhusu kifo mkeo labda tumemuua ili tuishi pamoja.”
“Hivi nani duniani aliyewahi kuzuia mwanadamu asizunguze anayotaka kusema. Ukisikiliza maneno ya watu unachelewa maendeleo, kwanza nani anajua uhusiano wetu?”
“Ina maana katika dunia hii tupo wawili tu?”
“Hapana ila sidhani kama watafikiri hivyo, huo ni wasiwasi wako tu japo waswahili wanasema jino la pembe si dawa ya pengo lakini kwangu wewe si jino la pembe ni jino jipya linaloota na kuziba pengo.”
“Usemavyo sikatai lakini tatizo jingine huoni kama utanioa utakuwa umeniingiza kwenye matatizo?”
“Matatizo gani tena?”
“Nina imani bado muuaji atataka kuiteketeza familia yako, huoni kuwa uhai wangu utakuwa umeuweka sokoni?”
“Nakuhakikishia kuwa kosa nililofanya awali sitarudi tena nitakulinda kama mboni ya jicho langu sidhani kama muuaji atanisogelea tena.”
“Mmh! Sawa.”
“Sawa nini, mbona uniweki sawa?”
“Nimekubali.”
“Aah! Siamini…Siamini Malaika wangu, nimeamini kuwa wewe si mtu wa kawaida bali Malaika uliyeubwa kwa ajili yangu ili kunipa faraja,” Anderson alimkumbatia Malaika Mweusi na kumbeba juu juu hadi kitandani.
Alimuomba Malaika Mweusi siku ileile wakalale nyumbani kwake.
“Hapana mpenzi sina budi kulitamka neno mpenzi kutoka uvunguni mwa moyo wangu,” Malaika alisema kwa sauti ya kinanda.
“Kwa nini honey tusiende nyumbani kwako ili ukapazoee kabla ya harusi?”
“Ni haraka sana, lakini nimeshakukabidhi moyo wangu hivyo siku zote mambo mazuri hayataki haraka.”
“Hapana lazima niwe na haraka mimi kwako kama msafiri aliye jangwani aliyedondosha chupa ya maji na kuteswa na kiu kwa kipindi kirefu bila matumaini ya kupata maji. Ghafla anakiona kisima chenye maji sidhani kama atasubiri.”
“Maneno yako yana ukweli wa asilimia mia, lakini siku zote subira waswahili wanasema ni dhahabu.”
“Sawa nimekubali, basi wiki endi hii nitakupeleka kwa wazazi wangu nina imani ndio siku itakayokuwa maalum wa sherehe fupi ya kuvishana pete ya uchumba na mipango ya ndoa ianze mara moja.”
“Nina furaha sana tena sana kufahamiana na familia yako.”
Ilikuwa ni siku ya furaha kwa watu wawili Anderson pale alipopata tulizo la moyo wake lililokuwa likimpa kimuhemuhe usiku na mchana. Naye Malaika Mweusi alikuwa na furaha kubwa kumpata yule aliyemuota usiku na mchana kuwa siku moja atakuwa mumewe wa ndoa.
***
Ilikuwa ni siku maalum iliyoandaliwa kwa vitu viwili muhimu kwa wakati mmoja, moja kutambulishwa kwa Malaika Mweusi kwa wazazi wa Anderson pili kuvishwa pete ya uchumba. Malaika Mweusi alimpitia Mr Anderson kwake akiwa kwenye gari lake la kifahari aina ya Range Rover Vogue sport ya rangi nyeusi.
Hakuwa yule Malaika Mweusi aliyependa kuvaa mavazi yanayomweka nusu uchi na mapambo ya gharama, la hasha huyu alikuwa mwingine kabisa.
Alikuwa amevalia vazi refu la kitenge cha rangi ya njano na nyeusi kilichoshonwa kwa ustadi mkubwa na kilemba chake na mkoba wa ngozi ya pundamilia, hakika alipendeza sana. Ukimwangalia harakaharaka ungesema ameteremka kutoka Lagos Nigeria au DR Congo.
Vazi alilolivaa hupendelewa kuvaliwa na wanawake matajiri nchini Nigeria au wafanya biashara wa Kikongomani. Chini alivaa viatu virefu vya ngozi ya pundamilia vilivyofanana na rangi ya mkoba wake. Shingoni alivaa mkufu mpana wa dhahabu. Hakuvaa mingi kama kawaida yake na mkononi hakuvaa bangili ya dhahabu aliivaa saa yake ndogo ya dhahabu.
Hakika Malaika Mweusi alipendeza sana machoni mwa mtu yeyote alionekana msichana mrembo mwenye heshima anayefaa kupelekwa kwa wakwe. Anderson alipomwona Malaika Mweusi alichanganyikiwa kwani kila siku alimuona mwanamke mpya.
“Malaika Mweusi! Hakika mwenyezi Mungu lazima nimpe shukrani zangu kwa kumuumba mrembo asiye na mapungufu yeyote ya sura, umbo na hata tabia hongera sana umependeza,” Anderson alimsifia akiwa amechanganyikiwa na urembo wake.
“Asante kwa kunisifia lakini sikushindi wewe ulivyopendeza kwenye suti nzito, hali hii tunaenda kutambulishana je, itakuwaje siku ya harusi yetu, Anderson mpenzi na mimi sina budi kumshukuru mwenyezi Mungu kunichagulia mume bora, unajua nilichokupendea?”
“Sijui Malaika wangu hebu niondoe tongotongo zililotanda kwenye ubongo wangu.”
“Si tupo pamoja habari hizi zinataka kituo kwa vile tuna safari ambayo tunasubiriwa kwa hamu kubwa kama ulivyonieleza huu si wakati wake fanya twende tuwahi tusije onekana kama tuna ahadi za ubabaishaji na kuwafanya wazazi wako kupunguza maksi.”
“Sawa mpenzi wacha tuwahi japokuwa unaniweka roho juu kama kiuno cha mnazi juu sipo na chini pia sipo nipo katikati.”
“Ushaanza, tangu lini mnazi ukawa na kiuno? Ninyi ndio mnaosema eti nyoka ana kiuno.”
Walicheka kwa pamoja na kuingiaa ndani ya gari la Malaika Mweusi alikuwa anaendesha mwenyewe kuelekea nyumbani kwa wazazi wa Anderson. Walipofika walipokewa kwa shangwe na vifijo walifika sebuleni ambako palikuwa pamepambwa kwa maua ilionyesha kuwa ni siku maalum iliyoandaliwa kwa shughuli maalum.
Sebuleni kulikuwa na wageni wasiopungua kumi na mbili ila wazazi wa Anderson walikuwa ndani baada ya mgeni kufika na kutulia ndio walipokwenda kuitwa.
Baba na mama Anderson walitoka wakiwa wameongozana pamoja, wakati wanaingia Malaika mweusi alikuwa ameinama alinyanyua uso wake baada ya kusikia sauti ya mama mkwe wake mtarajiwa.
“Ooh! Karibu sana mwanangu!”
Macho ya Malaika Mweusi alikutana juu ya macho ya mama mkwe wake, wakati huo alikuwa ananyanyuka ili amlaki mama mkwe wake mtarajiwa. Alijikuta akipatwa na mshtuko wa ajabu na kupiga ukelele mdogo.
“Ooh! Mungu wangu!” alijikuta akirudi tena chini kwenye kochi wakati huo alikuwa ameshikilia kifua chake kuonyesha amepatwa na hofu, kitu kilichomfanya mama Anderson abaki amesimama kama sanamu.
Watu waliokuwepo pale walikuwa na mshangao Anderson naye alipigwa na butwaa asijue nini kilichotokea. Baba na mdogo wake ilibidi wamfuate Malaika Mweusi aliyekuwa akihema kwa shida. Walipofika pale alipokuwa amekaa na kumuuliza.
“Nini tatizo mama?”
Malaika kabla ya kujibu alinyanyua uso wake na na kukutana tena na sura za watu wawili baba na mkwe wake na shemeji yake mdogo wa Anderson. Alishtuka zaidi kitu kilichozidi kuwashangaza wote waliokuwa pale.
Ilionyesha kuna kitu kilimtisha pale ndani na kupatwa na mshtuko. Anderson ambaye alikuwa amesimama pembeni ya mlango walioingilia wazazi wake alishangazwa na hali aliyojitokeza kwa mchumba wake. Alitoka pale mlangoni na kwenda moja kwa moja kwa mchumba wake ambaye muda mchache angemvisha pete ya uchumba na kuwa mke wake mtarajiwa.
Alijipenyeza katikati alipokuwa mdogo wake na baba yake mdogo waliokuwa wamepigwa na butwaa kwa kile alichokionyesha Malaika Mweusi, alimshika mabega na kumwita:
“Malaika wangu kulikoni mbona hivyo?”
Baada ya kusikia sauti ya Anderson alinyanyua kichwa ili kuhakikisha kuwa ni yeye. Alipitisha mikono yake nyuma ya shingo ya Anderson na kumkumbatia na kilio cha kuvuta makamasi kwa ndani.

Itaendelea
 
SEHEMU: 05
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Alijipenyeza katikati alipokuwa mdogo wake na baba yake mdogo waliokuwa wamepigwa na butwaa kwa kile alichokionyesha Malaika Mweusi, alimshika mabega na kumwita:
“Malaika wangu kulikoni mbona hivyo?”
Baada ya kusikia sauti ya Anderson alinyanyua kichwa ili kuhakikisha kuwa ni yeye. Alipitisha mikono yake nyuma ya shingo ya Anderson na kumkumbatia na kilio cha kuvuta makamasi kwa ndani.
SASA ENDELEA...

“Malaika wangu hebu nitoe kizani nini kilichokusibu muda mfupi ulikuwa na furaha lakini ghafla umebadilika baada ya kuiona familia yangu?”
“Hapana mpenzi sivyo ufikiliavyo,” Malaika alisema kwa sauti ya kilio.
“Kama si hivyo ni nini kimekusibu?”
Alijitoa mikono ya Anderson, kwanza alimfuta machozi na kupangusa kamasi nyembamba kwa kitambaa cha mkononi. Kisha alikohoa ili kutengeneza sauti yake na kuzungumza kwa sauti ya chini kidogo inayomuwezesha mtu yeyote aliyekuwepo sebuleni kumsikia.
“Kwanza niombe radhi kwa hali niliyoionyesha kila mmoja ana shauku ya kutaka kujua kilichonisibu. Haikuwa nia yangu bali hali hii imejitokeza ghafla bila ya mimi kutarajia, Naweza kusema kweli dunia ni watu wawiliwawili.
“Yaani marehemu mama yangu anafanana sana na mama mkwe, si kwa umbile bali hata sauti utafikiri walizaliwa mapacha. Wakati nanyanyua macho nionane na mama mkwe wangu nilipigwa na mshituko wa ajabu na kuona kama mama yangu mzazi amefufuka na siyo siri katika vitu nilivyovipenda ni mama yangu mzazi. Nilimpenda zaidi ya kitu chochote hasa kwa malezi na mapenzi mazito aliyonileana.
“Alipofariki ilikuwa ni pigo ambalo liliniumiza siku hadi siku kila nimkumbukapo marehemu mama yangu majonzi hunianza upya huwa kama nachubua kidonda ambacho kilianza kupona. Kwa kweli nilipomuona mama mkwe ilikuwa ni jeraha jingine la moyo wangu kwa hilo naomba baba, mama na shemeji yangu na wote mliokusanyika mnisamehe sana haikuwa nia yangu.”
Malaika mweusi baada ya kusema sababu iliyomfanya atokewe na hali ile huku akilia. Alikwenda moja kwa moja hadi kwa mama mkwe wake na kumkumbatia. Mama mkwe naye alimpokea na kumkumbatia na kumpa pole.
“Pole sana mwanangu kazi ya Mungu haina makosa….je, baba yupo?”
“Hapana sina, kwani mpaka mama anafariki nilikuwa simjui baba yangu.”
“Ooh! Pole sana, nani aliyekulea mpaka ukafikia hatua hii?”
“Ni walimwengu tu.” Malaika Mweusi aliondoka kwa mama na kwenda kwa baba mkwe wake na kumtaka kumshika miguu.
“Baba naomba unisamehe.” lakini alimuwahi kabla ajainama na kumnyanyua.
“Hapana mama huna kosa lolote jisikie huru kwa lolote lile hapa ni kwenu.”
“Asante kwa hilo wazazi wangu”.
Aliwageukia wageni walikwa na kuwaomba msamaha ambao nao hawakuliona kosa lake na walimpa pole kwa mkasa wake mzito. Baada ya muda Malaika Mweusi alijitajidi kurudi katika hali yake ya kawaida na shughuli zote zilikwenda kama walivyopangwa.
Alitambulishwa kwa ndugu na jamaa na wazazi wake wa Anderson na kuhitimisha kwa sherehe fupi lakini iliyofana vilivyo ya kuvishana pete ya uchumba. Baada ya sherehe Anderson na mchumba wake, mkewe mtarajiwa walikaa kikao kabla ya kuondoka kuzungumzia masuala ya harusi.
Japokuwa Anderson alitaka harusi ifanyike ndani ya mwezi mmoja, lakini Malaika Mweusi alitaka iwe baada ya miezi mitatu ili naye apate muda wa maandalizi kwa kuwaalika marafiki wake walio nje ya nchi. Wazo la Malaika lilipitishwa na baada ya kikao waliondoka pamoja siku hiyo alilala kwa Anderson. Ilipofika saa kumi na nusu usiku aliondoka.
****
Tokea siku ile ikawa ni mazoea kwa Malaika Mweusi kulala na saa kumi na nusu huondoka. Kila alipotaka kusindikizwa alikataa kitu ambacho kilichoanza kumtilia wasiwasi Anderson.
“Malaika.”
“Unasemaje my sweet?”
“Unajua tabia yako ya kuondoka alfajiri kila unapokuja kulala hapa inanitia wasiwasi.”
“Wasiwasi wa nini?”
“Labda kuna mume mwenzangu.”
“Hilo ni wazo potofu, lakini siwezi kukukataza kuwaza hivyo lazima unionee wivu, kama ningekuwa na bwana kwako ningekuja kufanya nini. Nilitaka kuja kwako baada ya kunioa lakini nimekubali kwa sababu ya upendo wa dhati kwako. Umeniomba nije nilale kwako nimekubali tena kwa muda wa siku uipendayo kwa vile bado hatujaoana huu ni utaratibu wangu wa kuondoka alfajiri ili asubuhi unikute nipo nyumbani kwangu najua huwezi kuamini lakini huo ndio ukweli sina mwanaume yeyote zaidi yako ili ukweli utaupata utakapo nioa.”
“Mmh sawa,” alijibu Anderson kwa unyonge.
“Usihudhunike mpenzi hizi ni zako dhabibu utazila taratibu hakuna wa kukuibia.” Malaika Mweusi alimpiga busu Anderson na kuondoka na kumuacha akimkodolea macho.
*****
Mahusianao kati ya Malaika Mweusi na familia ya Anderson yalikuwa makubwa kitu kilichojenga mapenzi mazito kutoka ndani ya familia na kumsifu mtoto wao kwa kuchagu msichana mwenye upendo na huruma.
Kwa muda mfupi alitoa msaada mkubwa ikiwa ni pamoja kumaliza nyumba ya wakwe zake na kuwanunulia gari dogo la kutembelea kila mmoja aliomba siku ifike ili ndoa halali ifungwe.
Anderson alitaka kujua utajiri wa mchumba wake ameupata wapi wakati ni msichana mdogo tena yatima aliyelelewa na wasamalia wema. Hatua hiyo ilikuja baada ya kuonyeshwa mikataba.
“Najua utashangaa mpenzi baada ya kuona utajiri wangu wa kutisha nikiwa jijana mdogo na kuongoza vitu vyote hivi hili ni jambo linalotaka nafasi..si unakumbuka siku nilikueleza nilikupendea nini?”
“Ndio nakumbuka.”
“Basi vitu vyote navitafutia siku ili nikueleze kwa kituo, si haya tu kuna mengi yaliyo chini ya moyo wangu ambayo siku hadi siku yananiumiza akili yangu.
“Ni siku gani isiyokuwa na jina?”
“Ni baada ya ndoa yetu.. unajua bado ni muda gani tufunge pingu za maisha?”
“Mwezi mmoja na siku kama ishirini hivi.”
“Vizuri siku ya kesho nitakuwa na safari yangu ya mwisho ya kibiashara kabla ya harusi yetu vilevile nitatumia safari hiyo kufanya mambo makubwa wawili. Moja kumtambulisha mtu ambaye atakuwa anafuata bidhaa kwani baada ya ndoa sitatoka mbali nawe ili tuweze kuonja raha ya ndoa au sio dear?”
“Mimi sina cha kuongea.”
“Pili kufanya shoping kwa kwa ajili ya harusi yetu nataka nikakununulie bonge la suti ya gharama ilingane na harusi yetu itakayoacha kumbukumbu kwenye ubongo wa watu.”
“Sawa lakini usikae sana kuondoka kwako ni sawa na kunyang’anywa blanketi kwenye baridi kali.”
“Si wewe tu bali imebidi ndio maana baada ya harusi nitahakikisha sibanduki kwako nina imani wivu wangu ni maradufu zaidi ya marehemu mke wako mama Gift.”
Malaika Mweusi aliondoka kuelekea Uingereza, Marekani, Asia na Falme za Kiarabu, katika uwanja wa ndege aliagwa na mumewe mtarajiwa na familia nzima ya Anderson baba, mama na ndugu na jamaa zake.
Kabla ya kupanda ndege aliagana na kila mmoja wao kwa kukumbatiana naye na wa mwisho aliagana na mumewe mtarajiwa kwa kukumbatiana kwa muda huku kila mmoja machozi yakimtoka kwa sauti iliyojaa majonzi alisema:
“Japo moyo unaniuma kutengana kwa muda lakini imebidi kutokana na sababu maalum lakini cha muhimu ni kuniombea dua niende salama na nirudi salama ili tusheherekee harusi yetu na nanyi bakini salama mkiendelea na mipango ya harusi nina imani baada ya wiki mbili au tatu nitakuwa nimerudi kabla ya harusi au itanilazimu nikatize ziara yangu.”
Machozi yalimtoka Malaika Mweusi wakati akiagana na ndugu wa familia ya mumewe mtarajiwa, baada ya muda aliingia kwenye Gulf Air na kuondoka nchini alimuacha Anderson kama kinda la ndege lililoachwa kwenye kiota na mama yeke.
Wiki mbili baada ya Malaika Mweusi kuondoka kwenda kwenye ziara yake ya kibiashara Anderson aliendelea na mipango ya harusi yao wakati huo mauaji jijini yalikuwa yamepoa japokuwa uchunguzi haukufanikiwa kumtia mikononi muuaji.
Muda wote alikuwa akiwasiliana na kipenzi chake kipya Malaika Mweusi lakini wiki moja baada ya Malaika Mweusi kuondoka alimjulisha Anderson namba yake mpya kuwa amepoteza simu yake hivyo atamjulisha kwa namba mpya ili waendelee kuwasiliana.
Malaika kupoteza simu yake alikuwa akiwasiliana na mchumba wake kwa yeye kumpigia kila siku usiku. Siku zilikatika kama tatu bila ya mawasiliano kitu kilichomtia hofu Anderson na kujiuliza kulikoni mbona kimya cha ghafla ni kitu gani kimemsibu mchumba wake.
Alipokuwa ofisini kama kawaida yake alipokea simu ya baba yake mzee Chuma.
“Ndiyo baba, shikamoo.”
“Marahaba aisee njoo nyumbani haraka sana.”
“Kuna nini?”
Anderson habari zile zilimchanganya sana, aliingia kwenye gari akiwa na mawazo mengi juu ya simu ile ya baba yake. Aliendesha gari kwa mwendo wa kasi hadi Mbezi mwisho kwa wazazi wake alipofika alifungua geti na kuingia ndani moja kwa moja hadi ndani.
Ndani alilakiwa na vilio vilivyoonyesha kuna tukio lisilokuwa la kawaida wote walipomuona walimvamia kwa kilio.
“Jamani kulikoni?!”
“Ooh! Mama yako hatunaye,” aliambiwa na baba yake ambaye macho yake yalikuwa yamembadilikana kuwa mekundu kwa kulia na mkononi alishikilia kitambaa kwa ajili ya kujifutia machozi na kamasi.
“Eti unasema mama kafanyaje?” Anderson aliuliza kama hakusikia.
“Mama yako amefariki.”
“Amefanya nini, ameuawa?”
“Hapana amepata ajali amegonga mti wakati anakwenda shambani.”
“Una uhakika hajauawa?”
“Ni kweli taarifa zilitufikia na askari wa usalama barabarani.”
“Mwili wake upo wapi?”
“Muhimbili kwa uchunguzi zaidi.”
“Kuna umuhimu wa kwenda sasa hivi.”
Aliongozana na baba yake hadi hospitali muhimbili kuchukua majibu ya kifo cha mama yake. Majibu yalionyesha kuwa amekufa kwa ajili ya kupata presha wakati anaendesha gari iliyosababisha ashindwe kuliongoza gari vizuri na kwenda kugonga mti.
Wakati anatoka hospitali na baba yake mara simu yake iliita. Ilikuwa ni simu ya kiofisi ambayo alipokea huku roho ikimdunda.
“Ndiyo lete habari.”
“Mkuu kuna maiti moja imekutwa imekufa maji kwenye bwawa la maji machafu chuo kikuu. Marehemu kandika ujumbe kwenye kikaratasi kuwa amejiua kwa sababu amejigungua kuwa ameathirika, maelezo yake tumeyakuta kwenye mfuko wake yaliyozungushiwa na karatasi ya nailoni ili usilowane.
“Kwa sasa hivi mpo wapi?”
“Tunakaribia hospitali ya Muhimbili.”
“Vizuri hata mimi nipo hapahapa mama yangu amefariki kwa ajali ya gari.”
Vijana wa Anderson waliwasili katika hospitali ya muhimbili harakaharaka walichukua machela kwa ajili ya marehemu tayari kumpeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Wakati wanateremsha mwili wa marehemu na kuuweka kwenye machela Anderson alikuwa amefika eneo lile alikisogelea kitanda alipokifikia wakati huo vijana wake walikuwa tayari kukisukuma, aliamua kuifunua shuka ili aione sura ya marehemu.
Anderson alishtuka na kupiga ukulele:
“Aaah!” nguvu zilimuishia baada ya kuiona sura ya marehemu alianguka chini na kupoteza fahamu.

Itaendelea
 
SEHEMU: 06
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500
.ILIPOISHIA
Wakati wanateremsha mwili wa marehemu na kuuweka kwenye machela Anderson alikuwa amefika eneo lile alikisogelea kitanda alipokifikia wakati huo vijana wake walikuwa tayari kukisukuma, aliamua kuifunua shuka ili aione sura ya marehemu.
Anderson alishtuka na kupiga ukulele:
“Aaah!” nguvu zilimuishia baada ya kuiona sura ya marehemu alianguka chini na kupoteza fahamu.
SASA ENDELEA...

Vijana wa Anderson walistushwa na hali ilivyotokea kwa bosi wao ilibidi wauguzi wafanye kazi ya ziada kumuhudumia Mr Anderson kwani alikuwa amepoteza fahamu.
Wakati huo mzee chuma mr Anderson alikuwa anakuja mbio kumuwahi mtoto wake.
“Vipi jamani?” aliuliza mzee Chuma.
“Mzee, amepata na mshituko baada ya kuiona sura ya marehemu aliyelazwa hapo juu ya kitanda”.
“Kwani ni mwili wa nani?.
“Hata sisi hatujui!’
Mzee Chuma aliuendea ule mwili pembeni ya kitanda upande wa kichwani na kufunua shuka, alipoiona ile sura alipiga kelele mara moja naye alianguka chini na kuzirai.
Kitendo kile kilimshtua kila mmoja aliyekuwepo pale, walijiuliza yule marehemu ana uhusiano gani na wale watu wawili.
Baada ya kupata huduma ya kwanza Anderson alikuwa wa kwanza kupata fahamu kabla ya baba yake. Mmoja wa vijana wake walimuliza bosi wake.
“Vipi bosi kuna nini mboma mnazidi kutuacha njia panda?”
“Huu ni mwaka wetu.”
“Una maana gani?”
Kabla ya machungu kuishaya kufiwa na mke na mtoto nafiwa na mama yangu mzazi na kidonda kikiwa bado ni kibichi nafiwa na mdogo wangu kipenzi huu ni mkosi gani sijui?”
“Ina maana huyu ni mdogo wako?”
“Enhee huyu ni mdogo wangu anayenifuata kwa mara ya pili.”
“Ooh, pole sana.”
“Asante, mpelekeni kwa uchunguzi zaidi na taarifa zake mtaniletea, na pia wengine mjigawe kwa ajili ya maandalizi ya mazishi kwani swala hili lazima lifanywe upesi.”
Anderson na baba yake walirudishwa nyumbani tayari kwa matanga ya vifo vya ghafla vya mama na mdogo wake.
Lilikuwa ni pigo kubwa maishani mwake, watu aliowategemea kwa mengi likiwemo suala la kusimamia ndoa yake na Malaika Mweusi ndio walikuwa wamefariki.
Alijiuliza maswali mengi ya kumweleza Malaika Mweusi kuhusu kifo cha mama yake aliyempenda kupindukia. Hata alipoondoka alimuahidi mkwewe lazima amletee zawadi ambayo hataisahau maishani mwake.
Alizidi kujiulliza kama alivyomweleza vifo vya mkewe na mwanaye tena muda ulikuwa umepita nusura azirai itakuwaje ikiwa atamweleza vifo vya mama yake na mdogo wake.
Anderson akiwa katikati ya mawazo mara simu yake ya mkononi iliita aliichomoa mkononi na kuangalia namba na kugundua ni Malaika Mweusi. Ghafla mapigo ya moyo yalibadili mwelekeo na kwenda kasi. Kama ungekuwa karibu yake ungesikia mapigo yake ya moyo yalivyokuwa yakidunda.
Aliishika ile simu na kuanza kutetemeka, alijiuliza kuwa ataanzaje kumweleza misiba ile miwili. Simu iliita mpaka inakatika akiwa bado ameshikilia, baada ya simu kukatika ndipo akashtuka.
“Ohh shit,” alisema kwa hasira.
Mara iliita tena na safari hii aliipokea na kuzungumza.
“Hallo.”
“Ohh my sweet heart vipii? Mbona hupokei simu au una mtu mwingine? Usiache nikafa kwa presha bure hebu nieleze kwa nini hupokei simu au umeshanichoka… yaaa…ni..”
Malaika Mweusi hakumaliza alianza kulia upande wa pili kitu kilichozidi kumpa ugumu Anderson.
“Si…si hivyo nini najua unipeni.”
“Hapana Malaika wangu hakuna kitu ninachokipenda kama pendo lako nipo tayari kufa ili nisikupoteze wewe ua la moyo wangu, kato la kiu yangu, baridi la joto langu.”
“Sasa kama ni hivyo kwa nini umechelewa kupokea simu mpaka unanipa presha bure?”
“Kuna tatizo?”
“Tatizo tatizo gani tena Yahillah?”
“Mama amepatwa na ajali.”
“Mungu wangu nisaidie aja wako, ajali imetokana na nini na vipi hali yake inaendeleaje?”
“Presha ilimpata ghafla akaendesha moja kwa moja akagonga mti hali yake si nzuri na hajapata kauli mpaka sasa tangu apate ajali.”
“Ooh maskini nakufa mie…sasa mpaka muda huu mmempa msaada gani?”
“Yupo kwenye matibabu ya hali ya juu na madaktari wanahangaikia kuokoa maisha yake.. wewe kwa sasa upo wapi?”
“Nipo Dubai kesho asubuhi nitarejea ili nije kumuuguza mama. .ooh maskini kipenzi changu mama mkwe wangu. Mungu ampe afueni ili apone haraka mwambie mama nampenda sana,” maneno ya Malaika yalikuwa kama mkuki kwa Anderson lakini alijikaza kiume ili asijulikane.
“Kwa hiyo dear nikutegemee kesho?”
“Yaani ingekuwa ni uwezo wangu nisingekuja leo hiihii ila naomba uendelee kunijulisha maendeleo ya mama.”
“Sawa, ngoja nikuache ujiandae na safari.”
“Sawa mpenzi usiku mwema, samahani hapo kwani uko hospitali au nyumbani?”
“Mmh nipo nyumbani nimerudi muda sasa hivi.”
“Ok usiku mwema.”
“Nawe pia, bai.”
Baada ya ukata simu Anderson alishusha pumzi ndefu kama ameshusha mzigo mzito, alijiuliza kuwa akija akikuta kuna msiba sijui itakuwaje au naye ndio presha itampanda liwe pigo la tatu takatifu.
Usiku kucha akupata usingizi akipanga mipango ya kumpokea Malaika Mweusi na namna ya kumweleza kifo cha mkwewe na mdogo wake bila ya upata mshituko wowote ambao utaleta madhara yeyote. Mpaka kunakucha alikuwa macho akipanga hili na lile ambayo yote aliyaona hayafai.
Saa 12.00 alfajiri alikuwa kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere zamani Dar es Salaam International Air port kumsubiri kipenzi chake Malaika Mweusi.
Malaika Mweusi aliwasili hapo uwanjani saa moja na dakika kumi na kulakiwa na mumewe mtarajiwa Anderson.
Baada ya kukumbatiana na kupigana mabusu na kujuliana hali katika siku zile walizopoteana machoni, swali la Malaika lilimchanganya Anderson.
“Enhe, mpenzi vipi hali ya mama?”
“Mmh hajambo kidogo,” alijibu kwa sauti ya chini.
“Mbona una sita kuna mabadiliko yeyote ya hali yake tangu jana?”
“Aaah! kidogo afadhali.”
“Sasa mpenzi breki ya kwanza ni hospitali kwa mama mkwe.”
“Hapana mpenzi kwanza tuanzie nyumbani kisha hospitali.”
“Hapana, haiwezekani, kwani kuna nini tukienda moja kwa moja hospitalini?”
“Si unajua asubuhi kunakuwa na masuala ya usafi. hivyo haitakuwa vema ni bora tusubiri kidogo.”
“Bora usafi unikute palepale lakini siwezi kwenda nyumbani mpaka nikamuone mama, tafadhali nipeleke hospitali alipolazwa,” Malaika alikuwa mbishi.
Anderson hakuwa na ujanja ilibidi atafute njia nyingine ya kumdanganya ili warudi nyumbani na mambo yote atayajua akikapo huko.
“Ni hivi mpenzi mama yupo nyumbani ndipo anapopata matibabu.”
“Mbona sikuelewi, mara hospitali mara nyumbani nishike lipi sasa?”
“Nyumbani si unajua tena mpenzi nimechanganyikiwa.”
“Pole sana mama anauma sana siwezi kueleza jinsi nilivyoumia.”
Walikubaliana kwenda moja kwa moja hadi nyumbani ambapo ni ukweni. Wakiwa njiani Anderson alikuwa na mawazo ya hali ya Malaika Mweusi atakapogundua mkwewe si mgonjwa bali ni marehemu.
Gari lilisimamishwa mbele ya geti la nyumba wa wazazi wa Anderson na baada ya kufunguliwa waliingia na gari ndani. Mazingira ya pale yalimshangaza haikuwa hali ya ugonjwa bali ni msiba. Wakati wakiteremka kwenye gari Malaika alimuliza Anderson.
“Dear kuna nini kinaendelea mbona sielewi?”
“Uuu…unajua…mama..ma..mama”
“Mama kafanya nini tena mpenzi? Mbona sikuelewi?”
“A..a..me..me.”
“Niambie ukweli mama amefanya nini..mbona unielezi ukweli mama amefanya nini?”
“Samahani mpenzi …mama amefariki.”
“Aaa maskini roho yangu.”
Malaika mweusi alianguka chini na kuzirai, ilibidi ifanywe kazi ya kumwagia maji ya baridi ili kurudisha fahamu zake na baada ya kurudiwa na fahamu alianza kulia tena bila ya kujua msiba si wamama mkwe tu bali na shemeji yake. Taarifa za msiba zilisababishwa akimbizwe hospitali lakini hali yake ilikuwa nzuri kwa muda mfupi na kurudishwa msibani.
Malaika aliamua gharama zote za mazishi ziwe juu yake, yalikuwa ni majeneza yote mawili ya gharama kubwa ambapo kila moja lilikuwa milioni moja na nusu yalikuwa yamenakshiwa kwa dhahabu. Mazishi yalikwenda vizuri na yalifanyika kwenye ua wa nyumban.
Baada ya mazishi ya tofauti makaburi hayakufukiwa na badala yake, juu ya kaburi kiliwekwa kioo kikubwa, yalikuwa ni mazishi ya aina yake yaliyoachwa simulizi midomoni mwa watu.
“Baada ya mazishi Malaika Mweusi alitaka kujua kifo cha shemeji yake kimetokana na nini?”
“kutokana na maelezo aliyoyaacha mwenyewe aliamua kujiua baada ya kugunduakuwa ameatrhirika.”
“Si kweli,” Malaika alikataa.
“Una maana gani?” Anderson aliuliza.
“Kwa nini ukubali kirahisi namna hiyo?”
“Kwa nini usiamini?”
“Labda watu wamemuua na kushinikisha amekufa maji.”
“Maneno yako yanaweza kuwa na ukweli ndani yake lakini kuna ugumu kwani hati ya mwandiko ni wa mdogo wangu na mwandiko wake naufahamu vizuri.”
“Au mmemnyanya paa?”
“Waala, yaani jana ndio nimejua ameathirika.”
“Sasa mpenzi mipango yetu tuisimamishe mpaka hapo tutakapo panga baadaye.”
“Lakini tusichelewe si unajua majonzi juu ya majonzi sina mwingine wa kuniliwaza ila ni wewe?’
“Hilo nalielewa ndio maana nipo pamoja na wewe katika kipindi chote kigumu cha majonzi kwani lako ndio langu.”
“Ndiyo maana nikakuita Malaika Mweusi uliyeletwa duniani kwa ajili ya kunifariji mtu kama mimi.”
“My sweet hivi sasa sisafiri tena hadi nihakikishe upo katika hali yako ya kawaida.”
“Sawa mpenzi.”
Malaika Mweusi alikuwa karibu na Anderson safari ile alilala siku zote kwa mchumba wake lakini ilikuwa kama kawaida yake kuondoka saa kumi alfajiri. Anderson alipenda kujua shughuli za Malaika Mweusi.
“Ni kweli nakupenda na ni vizuri kuelewa utajiri wangu umetokana na nini, lakini ni haraka sana kwa kuwa tupo pamoja taratibu utanielewa tu.”
“Kwa nini usinieleze tatizo ni nini?”
“Utanipenda?”
“Hilo halina kificho.”
“Unaniamini?”
“Nakuamini kwa asilimia mia moja.”
“Hapana hunipendi.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Kwa nini tubishane kwanye jambo ambalo liko wazi?”
“Basi mpenzi nimekuelewa.”
“Si hivyo darling kama hatuaminiani au hauko tayari kunisikiliza kuna umuhimu gani wa kuwa pamoja?”
“Usifike huko mpenzi nimekuelewa naomba unisamehe sipendi kukudhi kwani itakuwa sawa na kuiudhi nafsi yangu.”
Anderson alijikuta hana kauli ya kuhoji chochote cha Malaika Mweusi kitu ambacho kilimtatiza. Japokuwa hakuna alichokikosa kutoka kwa Malaika Mweusi, alipata kila alichotaka huku akilelewa kama yai.
Malaika Mweusi alionyesha mapenzi ya dhati kwa Anderson na kuwa karibu naye katika kipindi chote cha majonzi alimpa ahadi nyingi tu watakapofunga ndoa yao ahadi zilizomtia wazimu Anderson.
Mara nyingi Malaika alipokuwa akienda kulala kwa Anderson alikwenda bila mkoba wake, kitu ambacho Anderson alikuwa amekizoea. Ilikuwa ni jambo la ajabu siku moja Malaika alipokwenda kulala akiwa na mkoba wake, kitu kilichomfanya Anderson kukosa usingizi kwa kutaka kuchunguza kulichokuwa ndani ya mkoba kwani haikuwa kawaida.
Alimtegea Malaika Mweusi alipokuwa amelala kwenye usingizi mzito, aliuchukua mkono wake aliokuwa ameuweka juu ya kifua chake aliuweka juu ya mto na kunyanyuka taratibu hadi kwenye mkoba uliokuwa juu ya droo ya kitanda.
Mawazo yake yalimtuma Malaika anajishughulisha na biashara haramu iliyompa fedha nyingi kwani ni vigumu kwa msichana mdogo kama yule kuwa na pesa kiasi kile ni kazi au biashara ya dawa za kulevya.
Kwa mafunzo yake ya kijeshi aliweza kujitoa kwa Malaika bila kujijua, aliuchukua ule mkoba na kuufunga taratibu kwa tahadhari kubwa.
Ndani ya mkoba ule kulikuwa na pesa nyingi packeti mbili za glovu, kichupa kidogo cha pafyumu kilichokuwa nusu kilichokuwa na marashi ya Kirusi, alijiuliza zile glovu za nini. Kabla hajafanya kitu Malaika alishtuka usingizini kwa haraka Anderson aliingia na ule mkoba chini ya uvungu wa kitanda.
Malaika mweusi alipoangalia pale kitandani alijiona yupo peke yake aliamua kumuita Anderson kwa sauti ya kati.
“Sweetie..”
Anderson alikaa kimya chini ya uvungu huku akijiuliza maswali mengi kuhusu vile vitu vina maana gani, aliona wazi kabisa Malaika anajihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya. Hofu ilimuingia endapo Malaika atagundua yupo uvunguni? Tena na mkoba wake atamuelewaje.

Itaendelea
 
SEHEMU: 07
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Anderson alikaa kimya chini ya uvungu huku akijiuliza maswali mengi kuhusu vile vitu vina maana gani, aliona wazi kabisa Malaika anajihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya. Hofu ilimuingia endapo Malaika atagundua yupo uvunguni? Tena na mkoba wake atamuelewaje.
SASA ENDELEA...

Malaika baada ya kushtuka usingizini alijiuliza mpenzi wake yupo wapi alimwita tena.
“Sweetie uko wapi?”
Hakuwa na jibu, aliangalia saa yake ndogo ya mkononi ilimuonyesha ni saa tisa na nusu usiku. Alijinyanyua na kujipekecha macho kutokana na usingizi alijua lazima Anderson atakuwa msalani alipitia taulo lake na kwenda msalani.
Anderson aliutumia muda ule kutoka uvunguni mwa kitanda na kurudisha mkoba ulipokuwa na kujilaza kitandani na kujifanya kukoroma.
Malaika alipotoka kuoga alishtuka kumuona Anderson kitandani akiwa katika usingizi mzito. Alijiuliza alipoamka alikuwa na usingizi mzito kichwani uliomfanya ashindwe kumuona. Alijikuta akishindana na mawazo yake kwani alikuwa na uhakika aliamka usingizini Anderson hakuwa kitandani.
Alijua yupo msalani vilevile alishangaa kutomkuta kama alivyotarajia na cha kushangaza zaidi alipotoka kuoga alimkuta kitandani tena kwa usingizi mzito.
Aliyapuuza mawazo yake kwani aliona yanampotezea wakati, hakuwa na haja ya uendelea kulala pale. Alikwenda hadi kitandani wakati huo Anderson alijifanya yupo kwenye usingizi mzito na kumshika mgongoni huku akimtingisha taratibu akimuita.
“Sweet….sweet,” Anderson hakushtuka mapema mpaka alipomuita zaidi ya mara sita na kujifanya anashtuka.
“Eeeh.” Aliitikia huku akijifanya kujigeuza kitandani.
“Sweet” Malaika Mweusi alirudi tena.
“Naam,” aliitika bila kufumbua macho.
“Mi’ ndio naondoka.”
“Kwani saa hizi ni saa ngapi?”
“Kumi kasoro.”
“Kumi kasoro mbona ni usiku sana?” aliuliza huku akifumbua macho na kujifanya kupiga miayo.
“Aah, nimeamua kuondoka tu.”
“Nikusindikize?”
“Hapana we endelea kulala tu.”
Malaika Mweusi alipitia mkoba wake bila kuchunguza alimbusu Anderson na kutoka nje. Nje alisikia sauti ya gari likiondoka. Anderson alikaa kitandani baada ya Malaika kuondoka akiwa na mawazo mengi juu ya vitu alivyovikuta kwenye mkoba. Chupa ya manukato, chupa ya dawa ya sindano yenye maji meupe, bomba la sindano na glovu.
“Hapana kuna haja ya kufuatilia nyendo zake lazima kesho niwape kazi vijana wangu kufuatilia miradi yote iliyo chini ya msichana mdogo lakini mwenye utajiri wa kutisha,” alijisemea kwa sauti ya chini.
Swali lingine lilikuwa ni kuhusu Malaika Mweusi kuondoka ghafla usiku huku akionyesha kitu kama hasira. Alijiuliza inawezekana amepekua mkoba wake na kugundua jambo? Alijua kama itakuwa hivyo basi uhusiano kati yao utaingia ufa au kufa kabisa kwani ni msichana aliyeonyesha msimamo wa hali ya juu.
Alfajiri ilimkuta akiwa macho alioga na kwenda ofisini kwake mapema, kitu kilichomshtua Secretari wake hata vijana wake pia. Hakupoteza muda aliwaita vijana wake na kuwapa jukumu la kufuatilia miradi yote iliyopo chini ya leseni ya TEMA na kuchunguza pia inashughulika na nini ikiwa ni pamoja na kuwahoji kwa siri baadhi ya wafanyakazi na majibu aliyataka jioni ile.
Vijana walitawanyika na kuanza kazi ile mara moja, wengine walianza kwenye miradi wote inayofahamika wengine kwenye ofisi ya kodi ya mapato huku wengine wakiingia kwenye mtandao ili kujua TEMA inashughulika na nini katika mtandao wa www.mate.com.tz.
***
Majira ya saa moja jioni Mr Anderson alikutana na vijana wake ili kumpa majibu ya kazi alizowatuma.
“Vipi jamani za kutwa?”
“Nzuri tu bosi.”
“Eeh mambo yamekwendaje?”
“Si mabaya sana tumepata baadhi ya dondoo nina imani unaweza kupata mwanga wa kitu unachokitaka.”
“Sawa mmefikia wapi?”
“Bosi baada ya kutugawa tumefanya uchunguzi wetu wa kina na kila mmoja akiwa na jukumu lake nina imani kila mmoja wetu mambo yake yamekwenda vizuri,” Alisema Aziz.
“Baada ya kila mmoja kupata alichokidodosa tulikutana pamoja kabla ya kukuletea jibu moja litakalokuwa limejitosheleza,” Aliongezea Suzana aliyekuwa kiongozi.
“Sawa nawasikiliza.”
Taarifa ilionyesha kuwa miradi iliyopo chini ya leseni ya TEMA ni mingi ambayo yote ipo chini ya msichana mmoja mdogo jina lake Tereza Maria Magdalena, anamiliki shule za kimataifa sita, nne zipo jiji la Arusha na moja Mwanza, pia anamiliki viwanda vitano viwili za dawa za binadamu na mifugo kimoja cha plastiki kwa ajili ya kutengenezea bidhaa za maji, biskuti na juisi ambavyo amevitenga mahsusi kwa ajili ya wanawake wajane wenye maisha magumu.
Pia ana hospitali mbili kubwa hapa jijini inayotoa huduma kwa gharama pia alitenga sehemu maalum kwa ajili ya magonjwa ya ukimwi ili afanye kazi nyepesi ambazo hazitawachosha sana. Amejenga vituo ishirini kwa ajili ya kulelea watoto yatima ambavyo vina shule ndani, ni msichana anayeishi katika mazingira ya kawaida hajaolewa.
“Mmedodosa vyanzo vyake vya pesa?”
“Inaonyesha pesa nyingi anapata kwa wafadhili, kuna mashirika zaidi ya ishirini yanatoa pesa zaidi ya dola milioni elfu moja ili kuboresha shughuli zote za kujitolea kama watoto yatima, kuanzisha mfuko wa kuwahudumia wagonjwa wa ukimwi ikiwa ni pamoja na kugawa dawa bure ambazo hununua kwa pesa zake.
“Siku zote NGO’s za nje zinatafuta watu au vikundi vyenye kutoa msaada kwa jamii na kuiongezea nguvu.”
“Miradi mingi ameiongeza baada ya kupata fedha kutoka kwa wafadhili nje kabla ya pesa za wafadhili hizo za kuanzia ametoa wapi?”
“Ukweli hapo hatukupata habari za pesa zake za kuanishia hiyo miradi aliipata wapi.”
“Ok kazi si mbaya ila kesho nataka kupata jibu kuwa pesa za kuanzia alizipata vipi.” “Asante nashukuru kwa kazi nzuri tutaonana kesho.”
Aliagana na vijana wake na kujirudisha nyumbani huku akiwa na mawazo kuhusu utajiri wa kutisha wa Malaika Mweusi. Ni msichana wa ajabu anayeonyesha ni jinsi gani anajali binadamu wenzake ukweli usiopingika kuwa msichana Tereza ni Malaika mwenye umbile la kibinaadamu.
Ni msichana mwenye huruma na mapenzi ya kweli lakini je, chanzo cha utajiri wake kimetokana na nini? Mara nyingi watu wengi wenye roho nzuri walio mstari wa mbele kusaidia jamii misaada yao huwa kama kinga ya kulinda maovu yao lakini nyuma yao ni uozo unaotapisha na kutotamani kuuona wala kusikia.
Anderson alijua kesho yake ni lazima atajua ukweli juu ya chemchemi ya utajiri wa Malaika Mweusi unatokana na nini pia vitu alivyoviona kwenye mkoba vilikuwa na maana gani. Alijikuta akijilaumu ni kwa nini asimulize lakini angeanzia wapi na ni nani aliyempa ruksa ya kupekua mkoba wake bila ya idhini ya mhusika.
Akiwa sebuleni alijikuta kila achokiwaza hakupata jibu kamili, hata usingizi ulivyomchukua hakujua alishtushwa usingizini na sauti ya Malaika Mweusi.
“Sweetie.. vipi ulalaji gani huo kama si askari?”
“Aah! Hivi umekuja muda mrefu, kwani sasa hivi ni saa ngapi?”
“Ni saa tatu kasoro.”
“Mungu wangu kumbe nimelala bila ya kujijua!”
”Pole sana shughuli ya leo ilikuwa nzito nini?”
“Si sana.”
“Ushakula?”
“Bado nilikuwa nakusubiri wewe.”
“Muongo ulijiua nakuja saa ngapi?”
Muda wote hata kama ingekuwa ni alfajiri ningekusubiri tu.”
Walijikuta wakiangua kicheko pamoja na kwenda kuoga, waliporudi walikwenda kwenye mgahawa wa karibu kupata chakula na waliporudi walilala.
Kama kawaida Anderson alipanga kuwa Malaika Mweusi atakapolala atafanya uchunguzi wa kina pamoja na kuandika majina ya chupa zile mbili ili awapelekee wataalam wa maswala ya kemikali.
Kama kawaida alijifanya amelala Malaika Mweusi alipitiwa na usingizi, muda mrefu aliangalia saa ya ukutani akisubiri ifike saa saba ya nusu au nane aamke. Alijitahidi kuwa macho hadi saa sita na nusu aliamua kujinyoosha kidogo na usingizi ukampitia. Aliposhituka macho yake yalikuwa juu ya saa kubwa ya ukutani ikimuonyesha ni kuwa saa nane na nusu saa moja zaidi ya muda aliopanga.
Kitandani alikuwa peke yake alijiuliza Malaika Mweusi amekwenda wapi au msalani. Alisubiri kwa robo saa hakumuona na na alipomuangalia msalani pia hakuwepo. Alijikuta akijiuliza atakuwa amekwenda wapi alizunguka nyumba nzima lakini hakumuona ufunguo ulikuwepo mlangoni na mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani.
Anderson aliingiwa na wasiwasi inawezekanaje mtu atoke ndani bila ya kufungua mlango au Malaika Mweusi si binadamu wa kawaida ni jinni. Akiwa kati kati ya mawazo, mara simu yake ililia alipofuata kwenye kitanda na kwenda kuichukua namba zilizokuwa za ofisi. Moyo ulimlipuka usiku kama ule simu ya nini tena na aliinyanyua na kuanza kuongea.
“Enhe lete habari?”
“Bosi habari ni mbaya.”
“John Masu na Mustachi wameuawa.”
“Wameuawa na nani na vifo vyao vimetokana na nini?”
“Bosi usiombe, vita iliyotokea saa moja na nusu iliyopita sijawahi kuiona toka nijiunge na kazi ya jeshi.”
“Ilikuwaje?”
“Tulifanikiwa kuwazingira wauaji waliokuwa wamevamia kanisa shida yao ubwa ilikuwa kumuua Mchungaji Marco Gin.”
“Kwa kuwa tuliwazingira vizuri tulijitahidi kupambana nao na kufanikiwa kuwatia mikononi sita kati ya kumi, tulijua ndio mwisho wao.
“Huwezi kuamini ni vijana wadogo sana hata umri miaka kumi na tano bado tena ni watoto wa kike wazuri lakini wote wana ujuzi wa hali ya juu wa kutumia siraha za aina zote.
“Tukiwa tunasheherekea ushindi mara kuna gari mbili zilifunga breki mbele yetu bila ya kutarajia walianza kutumimia risasi wakiongozwa na wanawake mmoja hatari sana kwa kuwa tulikuwa tumejisahau aliua watu wetu wawili palepale Mustach na John….Masu alimuwahi yule mwanamke alionyesha amevaa nguo nyeusi tupu ya kitambaa cha mpira mwili mzima.
Alimuwahi risasi ya begani ambayo nina uhakika atakuwa amemuua lakini mfuasi wa yule mwanamke alimuwahi risasi iliyohitimisha idadi ya wenzetu watatu.”
“Shughuli bado pevu na kanisani hawakudhuru mtu?”
“Wamekufa walinzi wanane pia wamemjeruhi mchungaji Marco Gin.”
“Vipi hali yake?”
“Bado mbaya.”
“Ok nakuja.”
Wakati anajiandaa mara simu iliita iliingia namba ngeni machoni mwake alipokea na kuongea.
“Haloo… haloo...eeh ndiyo mimi…eti unasema Malaika Mweusi amefanya nini? Hapana…hapana haiwezekani…lazima nije nishuhudie mwenyewe kama ni kweli itakuwa pigo la tatu takatifu,” taarifa zile zilimchanganya Anderson alichanganyikiwa alijikuta anapanda gari na taulo tena kifua wazi.
Taarifa za Malaika Mweusi zilimchanganya kwa kiasi kikubwa na kujiona kiumbe mwenye mkosi mapigo ya moyo yalimtingisha lakini mke wangu na mwanangu na sasa wamemuua kipenzi changu Malaika Mweusi nani sasa atakuwa amebaki kama si mimi mwenyewe?” Anderson alizungumza mwenyewe huku akiendesha gari kuelekea kwenye tukio.
Aliwaza mengi baada ya kupata taarifa za Malaika Mweusi. Akiwa njiani alijigundua kuwa yupo kifua wazi na amevaa taulo tu, hilo hakujali alisimamisha gari mbele ya mapokezi ya Muhimbili na kwenda moja kwa moja mapokezi huku akihema utafikiri alikuwa anatembea kwa miguu na wala hakupanda gari.
“Samahani ndugu kuna taarifa zozote za kipolisi zilizofikishwa hapa?”
“Ndio..ndio.. mzee.”
“Ya kwanza kuna maiti zimeletwa kutoka kwenye eneo la kanisa.”
“Na nyingine?”
“Maiti ya msichana iliyookotwa barabarani.”
“Ooh Mungu wangu ipo wapi?.... ni bora nikaishuhudia mimi mwenyewe.”
“Mzee maiti itakaa wapi zaidi ya monchwari?”
Mr Anderson aliishiwa na nguvu alijikuta anakaa chini, vijana waliokuwepo hospitali walianza kumshangaakumuona bosi wao katika hali ile.
“Vipi bosi mbona upo katika hali hii?”
“Nyie acheni tu mbona mwaka huu wangu?”
“Nini tena bosi?”
“Si shemeji yenu.”
“Nani? Malaika wako?”
“Kuna nani zaidi yake?”
“Kafanya nini?”
“Amekufa…..
Hakumalizia kusema mzee mzima alianza kulia mbele ya vijana wake.

Itaendelea
 
SEHEMU: 08
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
“Si shemeji yenu.”
“Nani? Malaika wako?”
“Kuna nani zaidi yake?”
“Kafanya nini?”
“Amekufa…..
Hakumalizia kusema mzee mzima alianza kulia mbele ya vijana wake.
SASA ENDELEA...

“Utani huo bosi muda si mrefu uliniambia kuwa upo na mamaa kabla ya lile sheshe la maeneo ya kanisani, vipi amevamiwa akiwa nyumbani?”
“Ni historia ya ajabu ngoja niende mochwari nikaishuhudie hiyo maiti kama ni ya Malaika Mweusi.”
Kutokana na kuishiwa nguvu vijana wake walimsaidia kuingia chumba cha maiti ili ashuhudie. Walikwenda hadi kwenye chumba cha kuhifadhia maiti, mhudumu baada ya kufika alipoulizwa kuhusu kupokea maiti ya mwanamke alisema:
“Kwa kweli nimepokea maiti nyingi sana leo za wanawake sasa sijui mnamhitaji nani labda tumtafute kwa pamoja.”
“Hamna tabu.”
Anderson alijibu huku wakiingia katika chumba cha maiti na kuanza kufungua dro moja hadi nyingine za kuhifadhi maiti zilizoigizwa siku hiyo. Maiti zote walizoziona zilizokuwa ndani ya chumba ajabu hawakuiona ya Malaika Mweusi.
Ilibidi wamuulize vizuri yule mhudumu wa mochwari.
“Mbona bado maiti moja?”
“Maiti gani hiyo?”
“Kati ya zilizoingia usiku huu.”
“Ni hizi tu hakuna nyingine.”
“Hapana bado moja.”
“Labda kama iliingia kabla yangu hebu tuangalie kwenye kitabu.”
Waliongozana moja kwa moja hadi kwenye kitabu cha maiti waliingia usiku ule lakini pia maiti ya Malaika Mweusi haikuwepo ili kumridhisha roho yake waliangalia maiti zote zilizokuwepo bila ya kujali maiti nyingine ambazo zilikuwa zinatisha sana kutokana na majeraha.
Lakini maiti ya Malaika Mweusi haikuwepo, ilibidi kijana wake amulize.
“Kwani bosi, taarifa za kifo ulizipata wapi na kutoka kwa nani?”
“Kuna mtu alinipigia simu akinijulisha kuwa mwili wa Malaika Mweusi umeokotwa ukiwa umelowa damu nyingi kifuani.”
“Alikueleza amepelekwa wapi?”
“Amesema hapahapa Muhimbili.”
“Sasa mbona haupo au yupo wodini?” alitoa wazo.
“Tangu lini maiti akawekwa wodini?” Anderson aliuliza.
“Una uhakika gani kama amekufa labda wingi wa damu tu inawezekana yupo hai au atakuwa amepoteza fahamu wakajua amefariki.”
“Kwa hiyo unaniambia twende wodini tukaulize?” Anderson aliuza swali kama mtoto mdogo.
“Ndio maana yake.”
Waliongozana pamoja hadi wodini na kuliza kama kuna majeruhi yeyote aliyeingizwa usku ule.
“Ni wengi waliovamiwa na majambazi, wapo waliopatwa na ajali pia kuna mwanamke mmoja aliyeokotwa inaonekana alijeruhiwa vibaya na risasi.”
“Eeh, ndiye huyo yupo wapi?” Anderson alirukia.
“Taratibu mzee yupo katika chumba cha wagonjwa mahututi huwezi kuonanana naye kwa sasa.”
“Lakini yupo katika hali gani?”
“Sikudanganyi yupo katika hali mbaya sana kupona kwake ni majaliwa ya Mungu.”
“Mungu wangu sijui itakuwaje!”
“Kwani mzee ni nani yako?”
“Mke wangu.”
“Ina maana haya yote yanatokea alikuwa anatoka wapi?”
“Si wakati wake sasa cha msingi ni kujua hali ya mgonjwa kwanza.”
“Kwa leo hatuna jibu njoo kesho utapata habari kamili za mgonjwa.”
“Jamani hata kumuona kidogo?”
“Sasa itasaidia nini?”
“Angalau nimuone kwa macho roho yangu iamini.”
Anderson aliongozwa na daktari hadi kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) na kushuhudia Malaika Mweusi akiwa amelala kitandani akipumua kwa msaada wa mashine maalum pia alikuwa ameongezewa damu.
Malaika alikuwa sawa na maiti kwani alikuwa hajui kinachoendelea, Anderson hakuwa na jinsi ilibidi aende nyumbani ili arejee kesho yake kufuatilia hali ya kipenzi chake.
****
Siku ya pili kabla ya kwenda hospitali ili kujua hali ya Malaika Mweusi hata hivyo jibu alilopewa halikuwa na tofauti na la jana kwani hali yake bado ilikuwa ni mbaya sana alikuwa bado anatumia mashine ya kupumulia.
Anderson alirudi ofisini alikuwa mnyonnge kutokana na hali ya kipenzi chake kuwa bado mbaya. Akiwa ofisini alijawa na mawazo mengi juu ya mkasa mzima na mazingira yaliyompata Malaika hadi kufikia kukumbwa na dhahama ile alijiuliza kwa nini aliondoka bila kuaga na gari lake lipo wapi. Baada ya muda mfupi simu yake iliita alinyanyua na kuongea.
“Habari za asubuhi bosi.”
“Nzuri tu.”
“Si kweli, pole sana.”
“Bado sijapoa, ulikuwa unasemaje?”
“Vijana wapo tayari kuonana na wewe.”
“Ooh, wambie waingie.”
Mara mlango uligongwa, vijana saba wa kazi waliingia ambao idadi yao walikuwa kumi lakini wenzao watatu walikufa kwenye mshikemshike wa usiku kuamkia jana yake.
“Habari za asubuhi,” aliwasabahi baada ya kuwaruhusu kukaa chini.
“Nzuri bosi sijui wewe?”
“Zangu ni mbaya kama mlivyosikia.”
“Pole sana inavyoonekana muuaji amepania.”
“Mimi wasiwasi wangu bado kidogo kumtia mikononi hivyo anajiamini ili kukutisha lakini nakuahidi sitaacha kumtafuta hadi damu ya mwisho”.
“Bosi usemayo ninakuunga mkono ni wasiwasi wake tu ndio maana anafanya vitu vya kukutisha,” kijana wake mmoja aliunga mkono.
“Sasa ni hivi, wanne nendeni mkafanye mipango ya mazishi, wawili mtakaa mmoja ndani ya hospitali na wengine nje ili kulinda Malaika wangu asipate shambulio jingine. Mimi na Lyasi tutaongozana hadi kanisani tukapate maelezo ya mchungaji Father Marco Gin labda tutapata picha yeyote.. haya tutawanyikeni tutaonana msibani.”
Anderson baada ya kugawa kazi kwa vijana wake alielekea kanisa kuu la WALIJITOA KWA AJILI YA MUNGU. Moja ya makanisa makubwa sana nchini japokuwa ni geni lilikuwa na tofauti na yanayotangulia kwa muda mfupi ilikusanya waumini wengi kutokana na mfumo mzima wa usambazaji wa neno la Mungu.
Ndiyo kanisa lililokuwa linaongoza kwa msaada na promotion kwa vijana wengi kwenda nje ya nchi kufanya kazi. Pia lilitoa misaada kwa vijana wengi wanawake wajane bila usahau waathirika wa ugonjwa wa ukimwi.
Kanisa lililoongozwa na mchungaji Marco Cin raia wa Marekani lakini aliishi sana nchini Italia ni mtu aliyekuwa na umaarufu mkubwa. Kwa muda wa miaka saba aliweza kufungua matawi mengi nchini mjini na vijijini makanisa ya WALIOJITOA KWA AJILI YA MUNGU yalisambaa nchi nzima.
Jina la Marco Cin lilikuwa kubwa ndani na nje ya nchi kwani alikuwa ni mtu mwenye huruma na mwenye kujali utu wa watu. Alikuwa ni mtu anayeheshimika serikalini.
Kila sehemu walipofungua kanisa sehemu hiyo ilipata maendelea kama huduma za maji, shule, hospitali na huduma za umeme wa jua la solar power.
Sehemu zote hizo vijana wote walipata nafasi za kufanya kazi nje ya nchi hata waliokuwa hawana elimu jambo lililowafanya vijana wengi kwenda katika kanisa hilo.
Mchungaji Marco Cin alifungua miradi mingi ya vijana ili kuwapunguzia ukali wa maisha. Akiwa njiani na kijana wake Anderson alibadilishana naye juu ya wimbi la mauaji yaliyogubika jiji.
“Hivi Lyasi unaweza kujua haya mauaji yanafanywa na mtu mmoja au kikundi cha watu?”
“Yoye mawili yanawezekana.”
“Sasa inamaana haya mauaji ni ya kisasi au?”
“Sidhani kama kuna kisasi cha aina gani hiyo.”
“Sasa unadhani ni nini?”
“Nina wasiwasi mauaji haya yanafanywa na watu tofauti na si mtu mmoja.”
“Unadhani ni kwa nini?”
“Hilo ni swali gumu mkuu ndio maana tunaangaika kutafuta tatizo ili tujue kiini cha matatizo yote.”
Mara simu ya Anderson ililia alipoangalia ilikuwa ya kiofisi aliipokea na kuongea.
“Haloo.. en’hee..lete habari.”
“Bosi gari la Malaika Mweusi limekutwa Kibaha likiwa na alama za risasi na michirizi ya damu maeneo ya mlango wa dereva.”
“Inawezekana wezi walimpora?”
“Ni kweli kabisa mkuu wazo lako halitofautiani na langu kwani inawezekana waliamua kuliacha baada ya upasukiwa na gurudumu moja.”
“Kwa sasa gari hilo lipo wapi?”
“Lipo Kibaha katika kituo cha polisi.”
“Sawa nitalifuata baadae baada ya kupata maelezo kwa mchungaji.”
“Sawa mkuu tunaendelea na uchunguzi zaidi.”
Anderon alikata simu na kumgeukia kijana wake.
“Hivi Lyasi suala la kutaka kuuawa kwa mtu kama Father Gin mtu aliyejitoa kwa ajili ya watu leo hii anataka kuuawa bila ya sababu mbona kama sielewi.”
“Mkuu hii ishu lazima kuna watu hawapendezwi na huduma anazozitoa kwa jamii, siku zote si watu wote wanaopenda maendeleo ya watu.”
“Ni kweli Lyasi lakini ukweli tutaupata kwa mchungaji.”
Wakati huo gari lao lilikuwa limesimama mbele ya lango la kuingilia katika kanisa la WAUMINI WALIOJITOA KWA MUNGU. Baada ya mahojiano na walinzi wa getini waliruhusiwa kuingia ndani. Walipaki gari lao kuelekea kwenye ofisi za kanisa, walipokewa na sister wa kizungu aliyekuwa mapokezi.
“Ooh, karibuni sana,” aliwakaribisha kwa unyenyekevu.
“Asante.”
“Niwasaidie nini?” Anderson alijitambulisha na yule sister alimueleza.
“Mr Anderson subirini kidogo kaeni hapo kwenye kochi..sijui mnatumia kinywaji gani cha moto au baridi?” Walikaribishwa kwenye makochi.
“Asante hatuhitaji kwa sasa.”
“Hapana hii ni kwa ajili yenu hiki ni kinywaji kwa ajili wageni wanaomsubiri Father.”
“Sawa sista tuletee chochote”.
Waliletewa kinywaji baridi, baada ya robo saa walielezwa na yule sister:
“Mchungaji yupo tayari nendeni kwenye chumba cha wageni.”
Alitokea sister mwingine na kuwaongoza hadi kwenye chumba cha maongezi.
Walipoingia ndani walimkuta Father akiwa kwenye kibaiskeli cha matairi manne.
“Ooh! Mr Anderson, karibuni sana.”
Kabla hajajibu simu yake iliita.
“En’heee ndiyo mimi….eti… acha utani Malaika amefanya nini?... ameibiwa hospitalini? Hii kali nakuja sasa hivi. Anderson ilibidi amuage mwenyeji wake Father Gin.
“Vipi ofisa kuna habari gani, naona kama zimekushitua sana?”
“Aaa..a. samahani Father ni habari za kikazi tu nitarudi baadaye.”
“Ooh! Bwana awafikishie salama ili tuonane tena.”
“Asante Father.”
Anderson aliondoka na kijana wake Lyasi kuwahi Muhimbili kupata taarifa rasmi za kutoweka kwa Malaika Mweusi katika mazingira tata.
“Lyasi sasa huu ni mchezo, ina waana watu wote walikuwa wapi mpaka aibiwe?”
“Ndiyo suala la kushangaza mkuu.”
“Unajua Lyasi naona kama utani vile yaani atoweke katika hali kama ile ina maana wale wauaji hawakuridhika baada ya kusikia hakufa?”
“Mkuu mbona kama kitendawili, inavyoonekana hawakutaka kumuibia gari bali nikumuua.”
“Unajua Lyasi kama Malaika Mweusi akiuawa mimi ndiye nitakuwa nimechangia kifo chake,” alisema Anderson.
“Kwa nini mkuu?”
“Baada ya kifo cha mke wangu na mwanangu nilipotaka kumuoa Malaika Mweusi alikataa kwa kuhofia naye anaweza kuuawa.”
“Sasa wewe unahusika kivipi?”
“Nimeshindwa kumlinda vijana wangu safari hii mmeniangusha,” Anderson alisema kwa masikitiko.
“Si hivyo tulijaribu kumlinda kwa karibu sana lakini kwa Malaika Mweusi ilikuwa vigumu kumlinda.”
“Kwa nini?”
“Kwani anaweza kuwapotoea katika mazingira ya ajabu mnabaki mnaulizana amepita wapi!”
“Kuwapotea kivipi?”
“Siku moja baada ya kutoka hapa kwako tulimfuatilia hadi kwenye maegesho ya magari Kinondoni lakini cha kushangaza ndani ya gari alitoka bibi kizee kikongwe ambaye aliingia kwenye gari lingine na kuondoka.”
“En’he ikawaje?”
“Basi mkuu tuliilinda lile gari ili kujua Malaika Mweusi ataenda wapi lakini cha kushangaza hakuonekana kutoka hadi kunakucha na tulipokwenda kwenye lile gari hatukumkuta!!”
“Mmh! Ipo shughuli.”
“Acha hiyo bosi kuna siku moja alituacha hoi watu wote.”
“Ilikuwaje?”
“Kama kawaida alipotoka kwako siku hiyo ilikuwa ni mchana kwa bahati mbaya gari lake liligongana na gari kwa nyuma tena eneo lenyewe lilikuwa na trafic ilibidi amtoe kwenye gari na kumpeleka kituoni.
“Mmh?”
“Tuliona si vyema mama mtarajiwa afikishwe kituoni ni lazima angetuuliza tunafanya kazi gani.”
“Mkamfanyaje sasa?”
“Tulilipita lile gari lilikuwa limembeba Malaika, tulisimamisha trafiki alituelewa na kumuachia, lakiini kilichotokea kilikuwa kama mazingaombwe.”
“Nini kilitokea?”
“Mkuu hakuwa Malaika Mweusi lakini wanafanana sana kwa umbo na sura kopi raiti. Hakuna kutofautisha.”
“Kwa nini msihoji yupo wapi?”
“Tulimhoji mkuu.”
“Akasemaje?”
“Akasema kuwa tumemuacha kwenye gari na tulipokwenda tulimkuta.”
“Hamuoni hapo mlifanya uzembe?”
“Najua utasema uzembe kumlinda Malika Mweusi ni kazi ngumu kwa kweli hatumuelewi vizuri.”
“Kivipi?”
“Anabadilika kama kinyonga.”
“Habadiliki chochote pupa yenu tu kutokuwa makini kwa yale mnayotumwa.”
Wakati huo alikuwa anasimamisha gari mbele ya hospitali ya Muhimbili. Aliteremka harakaharaka na kukimbilia wodini. Alikutana na dokta Bon Mandi ambaye alionekana hajatulia vizuri.
“Vipi Dokta?”
“Hili mzee ni tukio la kigaidi.”
“Una maana gani?”
“Yaani madaktari wote wameleweshwa kwa kupuliziwa dawa.”
“Na mgonjwa?”
“Mzee nikueleze mara ngapi hili ni tukio la kijasusi baada ya kuwalewesha wote na kumuiba mgojwa”
“Wewe ulikuwa wapi?”
“Nilikuwa nipo chumba cha upasuaji, dokta Mbilinyi aliponiletea taarifa kuwa mgonjwa ametoweka.”
“Yeye alijuaje?”
“Dokta Fanuel alikuwa anatoka alimtumia ujumbe kuwa akiingia aende kumjulia hali mgonjwa, alipokwenda wodini alishangaa kuwaona wauguzi wote wakiwa wamejilalia na mgonjwa hakuwepo ndipo aliponiita chumba cha upasuaji na kunieleza yaliyojitokeza.”
“Mpaka sasa mmechukua hatua gani?”
“Tumeitalifu polisi nao wamekuja kufanya uchunguzi wao na kuchukua maneno mawili matatu.”
“Hakuna aliyekufa?”
“Hakuna mheshimiwa.”
“Sawa nitarudi baadaye kupata taarifa zaidi.”
“ Anderson alirudi ofisini na kuanza kuwasema vijana wake.”
“Jamani naona wazi kazi imetushinda ni bora kila mtu akashike jembe akalime sioni umuhimu wa sisi kuwepo hapa zaidi ya kuitia hasara serikali.”
“Bosi hii ngoma ni nzito si ya kitoto kama tunavyofikiria adui tunayepambana naye ana utaalamu wa hali ya juu hivyo sasa hivi si muda wa kufanya kazi kwa kufuatana fuatana kila mtu ahangaike kivyake na kwa mbinu nyingine kabisa ni wazi adui yetu anatuelewa vizuri sana mpaka udhaifu wetu na ndio maana anatuzidi maarifa.
“Sasa kwa mawazo yangu kila mmoja atoweke kijijini na arudi baada ya mwezi mmoja ataleta taarifa kwa wakati wake atakaporudi …..sijui hapo mnasemaje?”
“Wazo lako ni zuri sana kesho baadhi ya watu nitawapa pesa ya kujikimu na kutoweka kijijini kila mtu aje kivyake na kuanza kazi mara moja.”
Anderson aliagana na vijana wake na kurudi nyumbani alipofika nyumbani alishangaa kukuta barua imebandikwa mlangoni kwake. Aliichukua na kuingia nayo ndani kabla hajaisoma ile barua aliyoingia nayo ndani ilikuwa imeandikwa:
Anderson ukaidi wako ndiyo umesababisha lkifo cha Malaikwa Mweusi sasa hili ni onyo usiingilie yasiyo kuhusu ukaidi wako utakufanya kila siku upoteze roho za watu na mwisho wake itakuwa roho yako. Bado tunaipenda hatupendi kuiona inapotea kwa jambo la kuacha kila yamkute basi yakazua mwenyewe siku zote akumulikae wewe mchome kabisa, wacha walinywe wamelikoroga wenyewe.
Ndimi apendaye maisha yako.
Anderson baada ya kuisoma ile barua alishusha pumzi na kujiona sawa na mtu aliye jangwani anayeonekana kwa uwazi. Aliona jinsi adui zake walivyo mzunguka kila kona kuliko yeye anavyowafuata usiku na mchana bila ya kuwaelewa wapo wapi.
Vita aliiona ni nzito aliifananisha na mpiganaji aliyefungwa kitambaa machoni na kupigana na mtu anayeona tena ana nguvu za ziada.
Lakini alijipa moyo kuwa anamtafuta muuaji wake hadi tone la mwisho la damu yake. Hakuona hasara kwani mama yake mdogo wake mkewe, mwanaye na kipenzi chake Malaika mweusi hawapo, akuona ubaya naye kuwafuata.

Itaendelea Jumapili
 
SEHEMU: 09
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Lakini alijipa moyo kuwa anamtafuta muuaji wake hadi tone la mwisho la damu yake. Hakuona hasara kwani mama yake mdogo wake mkewe, mwanaye na kipenzi chake Malaika mweusi hawapo, akuona ubaya naye kuwafuata.
SASA ENDELEA...
***
Siku ya pili alikwenda kanisa la WALIOJITOLEA KWA AJILI YA MUNGU ili apate mawili matatu kwa Father Gin.
Kama kawaida alikaribishwa na sister wa Kiswahili na kuletewa kinywaji baridi, wakiwa katikati ya vinywaji alikuja sister mwingine na kuwaomba waongozane hadi chumba cha maongezi na baada ya salamu zilipita kama dakika ishirini hivi ndiyo Father Gin alitokea akiwa kwenye kiti chake cha magurudumu(wheel chair) alipowaona tu aliwakaribisha kwa furaha.
“Ooh! Wapendwa karibuni sana.”
“Asante Father.”
“Za tokea jana, safari yenu ilikuwa yenye amani?”
“Ndiyo Father Gin.”
“Ooh, karibu sana.”
“Asante samahani Father.”
“Bila ya samahani.”
“Tulikuwa tunaomba kupata maelezo yako kutokana na sakata la juzi.”
“Kwa kweli siwezi ulieleza kwa undani zaidi kwa kuwa mengine siyajui ninachokumbuka nilitoka kwenye gari ili niwaangalie vijana waliokuwa wamelewa lakini baadaye niligundua hawajalewa bali dhamira yao ilikuwa ni kufanya mauaji.”
“Unafikiri nani mlengwa wa mauaji hayo?”
“Sijui labda ni mimi.”
“Unakumbuka sura zao?”
“Ni vigumu kwani ilikuwa ni usiku wa giza.”
“Pole sana Father Mungu atakusaidia upone haraka.”
”Amen, nanyi pia ila nitawaombea wote waliofanya unyama huu Mungu awarudishe kwani awana tofauti na kipofu anayehitaji msaada wa kuongozwa hata bwana yetu Yesu Kristo amefundisha kusamehe kwani wengi wetu hatujui tutendalo.”
“Ni kweli lakini watu hawa wakikamatwa ni lazima wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.”
“Hiyo ndiyo hukumu ya sheria.”
“Unasema baada ya kukugundua watu hao si walevi ulifanya nini?”
“Kwa kweli nilichelewa nilihisi maumivu upande wa bega la kulia na kilichoendelea sikujua mpaka nilipojikuta nipo Hospitali.”
“Pole sana Father Gin ila tutakapokuwa na shida na wewe tutarudi tena.”
“Hakuna tatizo karibuni sana Bwana atawaongoza mfike salama.”
Anderson aliagana na Father Gin na kuelekea ofisini kwake akiwa hajapata mwanga wowote wa kumsaidia katika uchunguzi wake.
Njiani alijawa na mambo mengi na moja ni kifo cha Malaika Mweusi ilikuwa ni vigumu kukubaliana adui yake kuwa ndiye mhusika mkubwa wa mauaji yote. Lakini mauaji yalianza kabla ya kuanza upelelezi pia alijua kurudi nyuma ni sawasawa na kusaliti jeshi.
Mwezi ulikatika bila ya matukio yoyote ya mauaji, mji ulikuwa shwari lakini Anderson muda wote roho ilikuwa juu safari hii kuwa ni nani atakayefuata kufa. Vijana nao waliangaika huku na huko kutafuta taarifa zozote zitakazo wasaidia jeshi kuwatia mikononi watuhumiwa.
Kilichomshangaza juu ya taarifa za vitisho toka kwa mtu anayejiita mtetezi wa haki za binaadamu siri zote za vijana wake zilikuwa hadharani japo kila mmoja alirudi kwa wakati wake.
Alijiuliza ina maana muuaji amekuwa na uwezo gani wa kujua siri yao. Kidogo alianza kuuona ugumu wa kumtia mikononi muuaji, lakini hiyo haikumkatisha tamaa ya kuendelea na uchunguzi wake kwani hakuwa tayari kusalimu amri.
MWAKA MMOJA BAADAYE
Anderson akiwa amekwisha kata tama ya kumkamata muuaji wake, kipindi chote cha mwaka mzima kilikuwa shwari amani ilijirudia hapakuwa na taarifa za mauaji kitu kilichomfanya Anderson na vijana wake kulala usingizi. Siku zote alijipa matumaini adui yake amesitisha mauaji baada ya kuona yupo mbioni kutiwa nguvuni na askari wa upelelezi.
Taarifa zilizomfikia zilimtibua akili yake kuwa nyumba zote na vituo vya mafuta vinavyomilikiwa na tajiri mmoja wa kiarabu vimelipuliwa na mabomu na kusabaabisha hasara kubwa pamoja na kupoteza maisha ya watu zaidi ya mia moja akiwemo tajiri na familia yake.
Kazi aliiona ni nzito mbele yake kweli kimya kingi kilikuwa na mshindo mkubwa.
Kama kawaida vijana wake waliendelea na upelelezi wao naye alichukua maelezo muhimu ambayo aliyafanyia kazi.
Aliamua kurudi nyumbani kwani tukio lile lilimshtua sana hakutegemea, aliendesha gari lake hadi kwenye baa na kuagiza kinywaji baridi ili kutuliza akili yake ambayo nusura ipasue kichwa kutokana na mawazo.
Baada ya kuridhika na kinywaji chake aliingia ndani ya gari lake na kuondoka kuelekea nyumbani kujipumzisha akijua wazi kuwa hana ujanja wowote wa kumkwepa muuaji anayemfahamu kama kiganja cha mkono.
Alifika kwake majira ya saa tatu na nusu usiku alishangaa kukuta taa ndani inawaka huku kukiwa na sauti ya muziki ukilia. Alijiuliza ina maana wakati anaondoka asubuhi alisahau kuzima taa na bila kuzima redio.
Lakini hata hivyo akili yake ilishindana na mawazo yake kwani alikuwa na uhakika kuwa alipoondoka asubuhi alizima taa na kuzima redio. Baada ya kupaki gari lake alikwenda hadi mlangoni alitoa ufunguo na kufungua. Alipoingia sebuleni alishangaa hali aliyoikuta, ilikuwa na usafi wa hali ya juu alijiuliza ni nani aliyefanya usafi ule.
Kilichomshangaza zaidi ni kuwa funguo za nyumba alikuwa nazo yeye na marehemu Malaika Mweusi. Alijiuliza maswali mengi atakuwa nani, muziki wa taratibu uliendelea kulia chumbani mlango ulikuwa umeegeshwa tu aliusukuma na kuingia ndani.
Alishtuka kumkuta mwanamke amelala kitandani akiwa amevaa night dress alikuwa amempa mgongo amelala kifudifudi huku akiwa ameukumbatia mto alijiuliza kuwa huyu mwanamke atakuwa nani, tangu afariki Malaika Mweusi hakuwa na uhusiano na kiumbe chochote cha kike.
“Mmh!… atakuwa nani….mbona kama a..a..ana..fa..fanana…. hapana….. haiwezekani kuwa yeye sasa ni nani au jini nipige kelele…mmh! Ngoja,” alijikuta akiwaza vitu vingi.
Kwa ujasiri mkubwa alisogea kitandani kwa mwendo wa kunyata, alisimama pembeni ya kitanda huku akitetemeka na kumshika bega aliyelala ili amuulize. Pombe zote zilimtoka.
Anderson alipotaka kumgusa yule mwanamke aliyekuwa amelala kitandani roho ilisita. Alimwangalia kwanza usoni ili ajue ni nani hasa, huku akihema kwa hofu ya kutaka kujua ni nani, alizunguka upande wa pili wa kitanda yule mwanamke alipokuwa ameelekeza uso wake, baada ya kumuona alijikuta akipingana na mawazo yake.
''Mmmh haiwezekani...haiwezekani hawezi kuwa ni yeye huu lazima utakuwa ni mzimu wake...sijui nifanyaje.''
Akiwa katikati ya mawazo mara yule mwanamke alijigeuza na kufumbua macho yake yalikutana sawia na ya Anderson.
"Ooh! My sweet! Umerudi?! Karibu sana mpenzi wangu my husband to be'',alisema yule mwanamke ambaye hakuwa mwingine bali ni Malaika Mweusi.
''Hapana si wewe,'Anderson aling`aka.
''Kusema sio mimi una maana gani?''
''Wewe ni mzimu!''
''My sweet Ander mbona sikuelewi? Kwa nini unanifananisha na mzimu?''
''Wewe ni kivuli cha mzimu wa mpenzi wangu Malaika Mweusi!''
''Ni nani amekueleza kuwa nimekufa?''
''Hao waliokuua''
''Anderon mimi sijafa kama hao watu wanavyonizushia.”
''Kama hujafa ulikuwa wapi?!''
''Ni historia ndefu inahitaji nafasi zaidi ya kuzungumza, maadam tuko pamoja utanielewa vizuri na utajua baada ya kupigwa risasi na kutoroshwa hospitali nilikuwa wapi katika kipindi cha mwaka mzima.”
''Pamoja na maelezo yako yanalingana na ukweli lakini mimi bado sikuamini.”
''Naomba uniamini mimi si mzimu bali ni yule Malaika wako aliye hai na wala si kivuli cha mfu,” Malaika kwa sauti tamu.
Malaika Mweusi alinyanyuka kitandani alipokuwa amekaa na kumfuataAnderson amkumbatie lakini Anderson aliruka nyuma kwa hofu.
''Mpenzi usiniogope mimi ni yuleyule malaika wako.'' Alizungumza huku akimshika mabega Anderson na mkono mmoja akiuzungusha shingoni ili amkumbatie.
''Mpenzi hawakuwahi kuniua niliokolewa, onyesha furaha kuniona au ulipenda nife? Haya basi nitakunywa sumu mbele yako ili ushuhudie kifo changu na wala hutaona mzimu wangu.''
''Nina imani hutaona huo mzimu wangu unaoufikiria, nifanye nini ili unielewe? Mimi mzima,naona sina budi kuiaminisha akili yako kuwa mimi si mfu hadi utakapoiona maiti yangu mbele yako.”
Kauli ile ilimshitua Anderson, wakati huo Malaika Mweusi alikuwa akijitoa kifuani kwake. Kwa muda mfupi machozi yalilowesha shati la Anderson.
Hali ya Malaika Mweusi ilimchanganya ilibidi awe mpole kwani hali aliyoionyesha ilimtisha.
“Si hivyo Malaika wangu lilikuwa ni jambo la ajabu kwa mtu aliyejua umekufa kisha baada ya mwaka nikuone ukiwa hai.”
''Ni kweli kama ulielezwa hivyo lazima uwe na wasiwasi, ni kweli nilinusa mauti baada ya kupigwa risasi begani na watu walionipora gari yangu lakini Mungu mkubwa ameokoa maisha yangu.”
''Basi yameisha mpenzi wangu karibu sana jisikie kama uko kwako kwa mara nyingine tena,” Anderson aliyasema huku akimkumbatia Malaika Mweusi aliyejilaza kifuani.
***
Malaika Mweusi akiwa amerudi tena kwa mara nyingine baada ya mapumziko Anderson alitaka kujua ilikuwaje mpaka tukio lile likamkuta baada ya kuondoka bila ya kuaga tena katikati ya usiku mkubwa kama ule.
''Unajua mpenzi mapenzi yangu mazito kwako ndiyo yaliyosababisha yanikute yaliyonikuta.”
''Una maana gani kusema hivyo?”
''Nilikuwa nimelala nilipigiwa simu kuwa kama nitaendelea kulala humu ndani basi tutakufa wote nyumba ilikuwa imetegwa kwa bomu.”
''Ni nani aliyekupigia simu?''
“Kwa kweli simjui.”
“Wewe uliamini vipi na kwanini hukunieleza.”
''Alinitisha kuwa kama nitachelewa bomu lingelipuka muda uleule.”
“Uliamini vipi?”
''Kutokana na matukio yanayoendelea kutokea upande wako.”
''Kwa nini hukunieleza?”
“Lazima pangetokea ubishi kati ya mimi na wewe hivyo ingefanya tupoteze muda na kufanya nyumba yetu ilipuliwe na kupoteza maisha yetu hatuna ujanja zaidi ya mimi kuondoka.”
''Ee’he baada ya kuondoka nini lilitokea?”
''Inavyoonesha muuaji hataki kukudhuru bali kuiteketeza familia yako na watu waliokuzunguka shida yake ni kunitoa pale na kuniua.”
“Ikawaje baada ya kutoka kwangu.”
“Nikiwa naelekea kwangu mara gari mbili zilinipita na kusimama mbele yangu kitu kilichonifanya na mimi nisimame kwani hapakuwa na njia ya kupita.”
" Mara nilisikia milio ya risasi ikipigwa kwenye gari langu kabla sijaamua nini cha kufanya nilipigwa risasi ya bega. Kutokana na kuvuja damu nyingi pamoja na jeraha walijua nimeua ndipo waliponitoa garini na kunitupa chini na kuondoka na gari langu zaidi ya hapo sikujua nini kilichoendelea mpaka miezi miwili ndipo nilipopata fahamu na kujua hapa ni wapi.
“Nilijua nipo hospitali lakini sikujua ni wapi wakati huo nilikuwa napata huduma ya hali ya juu. Nilirudishwa kwenye hospital ya dini inayomilikiwa na shirika moja la kidini. Nilielezwa kuwa pale ni nchini Kenya niliokotwa kwenye gari lililokuwa lipo kama gari la wagonjwa baada ya lile gari kupata ajali na wahusika kukimbia.
“Baada ya kupona nilirudishwa Tanzania nilipofika tu niliamua kwenda kuishi nchini Marekani nilikuwa na mawazo mengi juu yako nilijua kuwa nilikuacha kwenye hali mbaya na maswali mengi kichwani mwangu.
“Kwa kweli niliamua kurudi nchini nakuamua kama kufa bora tufa wote ndio maana nimeamua kurudi mikononi mwako sitaogopa vitisho vyovyote nakuahidi mpenzi kwanzia leo hii nitakuwa kifuani kwako sitaachana na wewe hadi kifo,” Malaika alisema kwa hisia kali.
''Mpenzi kwanza pole kwa yote yaliyokukuta nina imani Mugu yuko ndani yako hivyo hutapungukiwa na kitu na maisha yako bado ni marefu Mungu atuhepushe na mabaya yote.”
Penzi la Anderson na Malaika Mweusi lizaliwa upya, tabia ya Malaika Mweusi ilikuwa ile ile ya kuondoka usiku wa manane. Baada ya muda walikwenda kumtembelea baba mzaa chema akiwa na kipenzi chake Malaika Mweusi.
Siku hiyo aliongea mengi pamoja na mipango ya harusi yao ambayo walipanga kufanya miezi mitatu ijayo. Pia siku ile ilihitimmishwa usiku na Malaika kumpa penzi zito Anderson lililomrusha akili na kujiuliza alikuwa wapi siku zote kumpa penzi tamu kama lile.
Hata asubuhi Malaika alipoamka ili amuage sauti yake ilitoka kivivu kwani mwili wake ulikuwa umechoka kwa patashika ya usiku. Baada ya Malaika kuondoka aliendelea kujilaza kwa uchovu.
***
MlLIO wa simu ulimshtua mkuu wa upelelezi aliyekuwa katikati ya usingizi, alipotupa macho yake kwenye saa ndogo iliyokuwa juu ya droo ya kitanda ilimuonyesha kuwa ni saa tisa na robo usiku ikiwa ni nusu saa tangu amsindikize Malaika Mweusi.
Aliinyanyua simu yake iliyokuwa pembeni ya mto aliokuwa ameulalia, ilimuonesha ni simu maalumu kutoka ofisini, mara nyingi simu hiyo hutumika kwa ajili ya dharura hasa pale panapotokea matatizo yasiyokuwa ya kawaida.
Alibofya kitufe cha kupokelea simu na kuzungumza kwa sauti ya uchovu kwani shughuli ya usiku haikuwa ya kitoto iliyongonyesha mwili. Mwanaume yeyote asingeweza kujizuia kutangaza ndoa kwa binti anayetoka katika familia ya kitajiri. Akizungumza kwa sauti ya kivivu :
“Ndiyo nakupata leta habari.”
“Afande mambo yameharibika .“
“Wapi tena?”

Itaendelea
 
SEHEMU: 10
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500
ILIPOISHIA:
Mlio wa simu ulimshtua mkuu wa upelelezi aliyekuwa katikati ya usingizi, alipotupa macho yake kwe nye saa ndogo iliyo kuwa juu ya droo ya kitanda ilimuonyesha kuwa ni saa kumi na robo usiku ikiwa ni nusu saa tangu amsindikize Malaika Mweusi.
Aliinyanyua saa yake iliyokuwa pembeni ya mto alio kuwa ameulalia, aliichukuwa simu ilimuonesha inatoka kwa mmoja wa vijana wake. Simu ile ilimshtua sana na kujiuliza kuna habari gani tena.
Alibofya cha kupokelea na kuzungumza kwa sauti ya uch ovu kwani shughuli ya usiku haikuwa ya kitoto ilimnyongonyesha mwili wote.
Mwanaume yeyote asingeweza kujizuia kutangaza ndoa kwa binti huyo aliye onekana kutoka katika familia ya kitajiri. Akizungumza kwa sauti ya kivivu :
" Ndiyo nakupata leta habari."
"Mkuu mambo yameharibika. "
" Nani tena?"
SASA ENDELEA...

" Hakimu ."
"Ooh Mungu wangu!.. hii sasa inatisha ! tukutane ofisini sasa hivi."
Anderson alikwenda bafuni kuoga haraka haraka na kubadili nguo, wakati akitoka nje aliuona mkoba wa Malaika Mweusi ukiwa juu ya kochi.
Wakati akitoka aliwaza sana kuhusu ile pochi ya Malaika Mweusi.
" Aah kumbe jana alisahau pochi yake sio mbaya ataukuta jioni. "
Alikwenda hadi kwenye banda la gari yake na kulichukua tayari kwa safari ya ofisini. Saa yake ya mkononi ilimuonyesha kuwa ni 11:35 alfajiri. Akiwa njiani aliwaza mambo mengi kuhusu vifo vya kutisha vya mfululizo ni vifo ambavyo vinamchanganya yeye na vijana wake.
Alipofika ofisini alimkuta ofisa mpelelezi na vijana wake wakiwa wameashafika ofisini. Alipoingia wote walisimama baada ya kukaa aliwaamuru nao wakae chini.
"Ndio jamani leteni habari."
" Mkuu kama uliovyosikia yule hakimu ameuwawa si chini ya saa sita zilizopita. "
" Saa sita ina maana ilikuwaje hadi ikachelewa kujulikana?"
"Inavyo semekana amekutwa amekutwa amekufa katika gari lake ambalo lilkuwa limeegeshwa pembeni mwa barabara."
"Ni nani aliyegundua mwili wa marehemu kwenye gari?"
"Ni askari wa dori ambao walikuwa wanakipita kila mara lile gari, walipoamua kulichunguza ndipo walipogundua ni mwili wa hakimu.”
"Lakini ni lazima tukubali kuwa tumefanya uzembe wa hali ya juu kutokana na kifo cha hakimu."
" Kwa kweli bosi sidhani kama tumehusika pamoja na muuaji kutoa vitisho miezi miwili iliyopita nina imani tulimpa tahadhari na kumwelekeza sehemu na muda anaotakiwa kuwa nje ya nyumba yake nina imani kifo chake amekitengeneza yeye mwenyewe."
“Sawa lakini muuaji ni nani? hivi vifo vinahusiana na nini?"
" Sidhani lakini la muhimu tuwahoji wale ndugu wa yule bwana, inasemekana hakuwatendewa haki na muuaji alihidi pindi hakimu akipandisha , basi sheria itamuhukumu yeye."
“'Lakini si tuliwahoji mapema wao wakasema hawana uhusiano wowote wala tarifa yoyote kutoka kwa muuaji?"
" Kwani mara ya mwisho hakimu alikuwa wapi?"
"Job Pub"
"Sawa, kuna umuhimu wa kuwahoji watu waliokuwepo pale JobPub ili kujua kuwa aliondoka saa ngapi na aliongozana na nani."
" Sawa mkuu tutaifanya kazi hiyo."
" Haya majibu nayataka kabla ya saa moja usiku sawa jamani?"
Mkuu wa upelelezi Anderson aliagana na vijiana wake na kuondoka kurudi nyumbani huku akiwa amejawa na mawazo mengi kuhusu mauaji ya kutisha, alijiuliza muuaji ni nani.
“Kama kamuua hakimu kwa ajili ya kupandisha sheria na hao wengine vifo vyao vimet okana na nini, kikiwemo cha mkewe na mwanaye mpenzi Gift.”
Alijiapiza kuwa siku atakayo mtia mikononi muuaji huyo ama zake au za muaji. Alipofika nyumbani alikuwa amechoka akili na mwili, alijitupa kwenye kochi na usingizi mzito ukamchukua. Alishtuka usingizini majira ya jioni na kujiona amelala muda mrefu na ilikuwa imebaki nusu saa tu akutane na vijana wake kumpa taarifa za hakimu aliyeuwawa usiku wa kuamkia siku hiyo.
Kama kawaida alikwenda kuoga na kubadili nguo tayari kwenda ofisini, kilichiomvutia wakati anataka kutoka ni mkoba wa Malaika Mweusi. Aliangalia saa yake ilimuonyesha bado dakika ishirini, alijua ni muda wa dakika kama tano hivi kwa mwendo wa gari angefika ofisini.
Aliamua kuipekua ile pochi ili ajue kuna vitu gani pengine angegundua siri yoyote kuhusu msichana yule kutokana na siku moja kukutana na vitu vilivyo mchanganya kwenye pochi ya Malaika. Alijua kuwa ule ndio wakati wa kufanya uchunguzi wa kina .
Dakika kumi zingemtosha kufanya upekuzi wa harakaharaka , ndani ya lile pochi alikuta na cheni isiyopungua thamani ya shilingi milioni mbili na nusu simu ya mkononi aina ya samsung yenye thamani ya shilingi milioni moja na nusu lakini ilikuwa haina laini.
Katika kimfuko kidogo alikuta kijitabu kidogo (note book) alikifungua nakuanza kukisoma karatasi moja baada ya jingine. Ilionyesha namna ya miradi yake mingi yenye thamani ya mamilioni ya shilingi. Aliendelea kusoma kalatasi za mbele alikut5ana na majina ya watu yaliyoandikwa na wino wa bluu.
Lakini asilimia kubwa ya majina hayo yalikuwa yamezungushiwa wino mwekundu na majina mawili tu ndiyo yaliyo kuwa hayajazungushiwa wino mwekundu.
Majina yale yaliushtua moyo wake na kusababisha mwili wote kusisimka na jasho jembamba likimvuja juu ya paji la uso. Aliyarudia yale majina zaidi ya mara tano na jibu likuwa lilelile alichokisoma machoni mwake kilikuwa sahihi.
Yalikuwa ni majina baadhi ya wale wote waliouwawa na kumchanganya na kushindwa kumtambua muuaji na mbele ya majina yale kulikuwa na tarehe na siku mauaji yaliyofanyika. Ndani ya majina yale kulikuwepo jina la marehemu mama yake, siku na tarehe aliyouwawa , japo alijuwa mama yake alikufa kwa ajali ya gari.
Jina jingine lilikuwa la mdogo wake aliyeuwawa katika mazingira ya kutatanisha. Mwili wake ulikutwa kwenye bwawa la maji machafu.
Pia tarehe ya vifo vya mkewe na mwanaye vilivyotokea siku moja ambavyo vilimuuma sana na kumchanganya akili kwani mkewe aliuawa kikatili kupasuliwa matumbo na sehemu za siri na kisha kupigiliwa kipande cha mti.
Alikumbuka alivyouapia mwili wa mkewe na mwanaye siku za kuuaga kwamba atamtafuta muuaji na kutia hatiani kwa mkono wake mwenyewe.
Alijikuta katika mawazo mengi juu ya kile kitabu cha majina na Malaika Mweusi vina uhusiano gani.
Ajiuiiza kama atakuwa amehusika na vifo vile au la, hakukubaliana na akili yakekuwa Malaika Mweusi anahusika kwa vile alikuwa ni msichana aliyemuamini na kumuona kuwa ndiye aliyeziba pengo la marehemu mkewe hadi akafikia hatua ya kumtambulisha kwa wazazi wake ambao nao waliwapa baraka zote ili wafunge ndoa.
Kile kitabu kiliichanganya a kili yake, kwani hata mama yake kabla ya kifo chake alionyesha mapenzi mazito kwa Malaika Mweusi na alimsifia mwanaye kwa chaguo lake zuri la msichana mzuri mwenye tabia njema.
Alijikuta akisema kwa sauti :
"Hapana haiwezekani Malaika Mweusi akafanya hivi ila nina imani atakuwa anamjua muuaji lazima nipate ukweli kupitia kwake."
Jasho lilikuwa linamtoka chapachapa kama alifungiwa katika chumba chenye joto kali aliendelea kusoma kile kitabu na majina ya mwisho mawili yaliyobaki ambayo hayakuwa yamezungushiwa wino mwekundu, lilikuwepo jina la baba yake mzazi alijikuta akibwatuka.
“Ha! Na baba?" Tarehe iliyopo mbele ya jina la baba yake ilikuwa ni siku ileile alisema tena kwa sauti:
"Hapana haiwezekani na baba tena hapana."
Alitoa simu yake ya mkononi na kubonyeza namba za baba yake ili kumjulisha awe makini kwani kifo kilikuwa kinamnyemelea. Alipopiga iliita bila kupokelewa mpaka ikakatika. Alijikuta akitoka kwa mwendo wa kuruka hadi katika gari lake na kuliondoa katika mwendo wa kasi mithili ya ndege za kivita ili kuwahi kuokoa maisha ya baba yake.
Ndani ya dakika ishirini alikuwa anaelekea kwa baba yake, aliachana na njia kuu na kufuata njia ndogo kuelekea kwa wazazi wake. Kwa vile njia ilikuwa ni ya kupita gari moja mbele yake kulikuwa na gari limeharibika.
Hata bila ya kuchomoa funguo ya gari aliteremka na kuanza kukimbia kuelekea kwa baba yake, njiani alikutana na mwanamke kama Malaika Mweusi, lakini hakumjali zaidi ya kuwahi kuokoa maisha ya baba yake. Nyumba ya baba yake ilikuwa giza aliingia ndani ya geti na kwenda moja kwa moja hadi ndani, alimuita baba yake lakini hakukukuwa na majibu.
Alikwenda hadi sebuleni na kuwasha taa ilikuwa tupu na hakukuwa na mtu yeyote, alielekea chumbani kwa baba yake.
Mlangoni alikutana na michirizi ya damu lakini chumbani kwa baba yake kulikuwa na giza. Ile damu ilimfanya aione hali ya hatari mbele yake
Alitoa bastola na kuingia kwa tahadhari kubwa alipapasa ukutani na kufanikiwa kuwasha taa hakuamini macho yake palepale alishuhudia mwili wa baba yake ulikuwa umelazwa kitandani ukiwa mtupu kama alivyozaliwa.
Sehemu zake za siri zilikuwa zimetenganishwa na kisu kilikuwa kimemchoma katikati ya moyo wake, macho yalikuwa yamemtoka akionyesha kuwa amekufa kwa mateso makali. Damu ilikuwa mbichi na mwili wake ulikuwa bado una joto. Chumba chote kilikuwa kinanuka damu mbichi.
Anderson aliuvamia mwili wa baba yake na kulalia na huku akiendelea kuapa atamshikisha adabu aliyetenda kosa hilo. Alitoka harakahara ili aanze msako wa Malaika Mweusi ili apate ukweli wa vifo vyote. Lakini alikataa katakata muuaji anaweza kuwa mpenzi wake.
Kwa vile nguo zake zilikuwa zimetapakaa damu ya baba yake aliwapigia simu vijana wake waje kuchukua mwili wa marehemu baba yake kuupeleka hospitali.

****
Anderson alipokuwa njiani anarudi nyumbani alijawa na mawazo mengi juu ya ile note book ya Malaika Mweusi ina uhusiano gani na mauuaji yaliyotokea. Akili na mawazo vilishindana na alichokuwa anafikiria, aliwaza:
“Hivi kile kitabu kina maana gani? Inawezekana Malaika Mweusi akawa ni muuaji? …. Hapana …..Si Malaika atakuwa ni mtu mwingine ….. lakini muuaji anamjua sina budi kuyaweka mapenzi pembeni nimbane anieleze muaji ni nani.”
Alisimamisha gari mbele ya nyumba yake na kuwahi kile kitabu ili apate ushaidi… kama kawaida mlango ulikuwa umerudishwa na taa ilikuwa ikiwaka huku muziki mwororo ukilindima kwa mbali.
Hakuwa na swali la kujiuliza kuwa ni nani, alijua atakuwa ni Malaika. Harakaharaka aliwahi mezani kile kitabu lakini hakikuwepo. Alijilaumu kwa kuacha ushidi na kukimbilia eneo la tukio. Akiwa ameshika kiuno na nguvu zimemwishia baada ya kufanya uzembe wa hali ya juu kuacha ushaidi ambao ungemsaidia kumbana Malaika.
Mara alitokea Malaika Mweusi akiwa amejifunga taulo akionyesha anatoka kuoga.
“Ooh! My husband to be huyooo,” akiwa anamfuata kumkumbatia alishtuka kuona nguo za mpenzi wake zina damu.
“ Ha! Sweet nini tena hiki?” Malaika alikuliza kwa mshangao.
“Unamuuliza nani, hujui?”
“Kama ningekuwa najua nisingekuuliza hebu nijulishe nini kimekusibu mume wangu? “
“Naomba kile kitabu kilichokuwa juu ya meza.”
“kitabu gani?”
“Ulichokichukuwa .“
“Mbona sikijui sweet”
“Utanieleza majina yaliyokuwemo kwenye kitabu chako yanahusiana vipi na mauaji yote ya raia wasio na hatia na familia yangu yote.”
“Sweet upo sawa mbona naona kama umelewa mbona maneno yako siyaelewi? “
“Eti? “
Kofi zito lilitua kwenye shavu la kushoto la Malaika Mweusi lililompeleka chini.
“ Nataka kitabu na maelezo ya mauaji yote yaliyotokea la sivyo wewe utawafuata hao waliotangulia.”
“Mpenzi mimi sijui lolote utaniumiza bure. “
“Aha unafanya masihara eeh na damu za watu basi leo utanijua mimi ni nani ?”
Alimfuta pale chini Malaika Mweusi alipokuwa amelala na kumnyanyua juu na kumuuliza kwa ukali.
“Utanipa kitabu hunipi?”
“Kitabu kipi na nikitoe wapi?” Malaika bado aliendelea kukataa.
Anderson alimuongeza kofi jingine lililomtoa damu puani na mdomoni. Siku zote unapotaka kumuua nyani usimuangalie usoni. Alimfuata tena pale chini na kumnyanyua.
“Nieleze nani kamuua baba yangu?”
“Sijui.”
“Teddy nitakuumiza sema ukweli,” Anderson mapenzi yote kwa Malaika yaliisha.
“Sijui lolote wewe fanya upendavyo hata ukitaka kuniua niuue.“
Kauli ile ilimzidi kumuongezea hasira Anderson alimtikisa kwa nguvu na kumsukumia ukutani Malaika Mweusi alijigonga kichwani na kupasuka.
Damu nyingi zilimtoka akiwa mtupu na kumlaza kwenye zulia wakati huo alikuwa amelegea na kuhema kwa mbali.
Aliwapigia simu vijana wake waje kumchukua, mara ghafla umeme ulikatika kwa dakika moja na uliporudi Malaika Mweusi hakuwepo.

Itaendelea
 
SEHEMU: 11
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Kauli ile ilimzidi kumuongezea hasira Anderson alimtikisa kwa nguvu na kumsukumia ukutani Malaika Mweusi alijigonga kichwani na kupasuka.
Damu nyingi zilimtoka akiwa mtupu na kumlaza kwenye zulia wakati huo alikuwa amelegea na kuhema kwa mbali.
Aliwapigia simu vijana wake waje kumchukua, mara ghafla umeme ulikatika kwa dakika moja na uliporudi Malaika Mweusi hakuwepo.
SASA ENDELEA...

Hali ile ilimshtua Anderson na kuhofia kuwa watu wanamfuatilia hata kumuua wangeweza. Mara vijana wake walitokea.
“Vipi mzee hata bado ulikuwa hujabadili hata nguo?”
“Aaa… basi endeleeni na shughuli zenu ila vijana watatu wabaki kwa ajili ya kulinda nyumba yangu,” Anderson alianza kuingiwa na woga.
Lakini alilala salama mpaka asubuhi bila ya hatari yoyote aliyofikilia kumtokea. Asubuhi kama kawaida alishughulikia mazishi ya baba yake na baada ya mazishi alirejea nyumbani. Ndugu na jamaa walienda nyumbani kwake kumpa pole kwa misiba ya mfululizo iliyomuandama.
***
Baada ya msiba alianzisha operesheni ya kuichunguza miradi yote ya Malaika Mweusi. Wakurugenzi wake wote waliwekwa ndani ili waeleze Malaika Mweusi amekwenda wapi.
Jambo lile ilikuwa ni geni kwao, walikuwa hawajui taarifa zozote za Malaika pia walikuwa wameonana naye mara moja tangu waajiriwe na wengine ni mara chache sana. Alikuwa akifika mara mojamoja tena bila taarifa na kuangalia shughuli zinaendaje na kisha kuondoka zake zaidi ya hapo huwasiliana kwa simu.
Kutokana na ukali wake kwenye kazi zake kila aliyepewa jukumu lake alitekeleze kwa umakini mkubwa aliisha watishia atakayefanya mchezo katika kazi zake atamuua hadharani. Ile ilisababisha kila moja kuwa makini hata kama yeye hayupo.
Siku zote kazi zake zilikwenda vizuri hivyo hakuna mtu yoyote aliyejua nyendo zake kwa vile hakuwa na ukaribu na mtu. Pamoja na kujitetea waliendelea kuwekwa ndani ili kumshinikiza Malaika Mweusi ajitokeze la sivyo wakuruenzi wote wangeendelea kusota mahabusu. Wiki zilikatika bila kujitokeza .
Anderson aliendelea na msako mkali kuhakikisha anamtia mkononi bila ya kuogopa hatari yoyote kwa vile hakuna alichokuwa akikiogopa tena hasa baada ya familia yake yote kupotea.
Akiwa ofisini akisubiri ripoti za vijana wake kuhusu Malaika Mweusi mara alijulishwa na sekretari wake kuwa kuna kikongwe kimoja kinataka kumuona. Alimruhusu aingie ndani mara aliingia bibi kizee mmoja mwenye mvi kichwa kizima akiwa anatembea kwa kuinama akitumia mkongojo wake, alipomuona alimkaribisha huku akiwa amesimama.
“Ooh, karibu sana bibi.”
“Ahsante mjukuu wangu .”
“Shikamoo, sijui nikusaidie nini?”
Ghafla bibi alibadili sauti toka ya kizee na kuwa ya kijana iliyokuwa tofauti na umri wake.
“Anderson,” yule bibi alimwita.
Akiwa bado anashangaa kubadilika kwa sauti ya yule bibi, ghafla mgeni wake alinyanyuka na na kuondoa zile nywele nyeupe na plastiki yenye uso wa bibi kizee. Hakuwa mwingine ila Malaika Mweusi aliyekuwa mbele yake.
Anderson akiwa kwenye mshangao mkubwa alishtuliwa na sauti ya Malaika Mweusi.
“Anderson nasikia unanitafuta kwa udi na uvumba mpaka umewaweka ndani watu wasio na hatia, sasa nimekuja sijui ulikuwa unasemaje?”
Kabla Anderson hajajibu kitu Malaika Mweusi akatoa kitabu na kumtupia juu ya meza:
“Nina imani kilichofanya unipige na kutaka kuniua ni hiki kitabu nimekuletea ukisome halafu niulize swali ambalo nitakujibu leo nipo tayari kwa lolote utakalo,” Malaika alizungumza kwa sauti ya upole aliyoizoea Anderson.
Anderson alikichukua kitabu huku mikono ikitetemeka alikirudia kukisoma kilikuwa vilevile kilikuwa hakijaongezwa kitu wala kufutwa.Baada ya kukisoma jasho jembamba lilimtoka lakini alijikaza kiume na kumuuliza swali kwa sauti ya kitetemeshi.
“ Haya majina ni ya nani?”
“Ni ya wafu kasoro jina moja tu la father Gin.”
“ Nani aliyewauwa?”
“ Mimi.”
“Ooh! Mungu wangu, “ Anderson alishika kichwa.
“ Uliza swali jingine nina muda mfupi wa kuendelea kukaa hapa,” Malaika alimwambia huku akiangalia saa yake ya mkononi.
“Wapo walionimulika mimi nikawachoma siku zote akuanzae mmalize.”
“Hapana ….hapana…..siamini kama wewe ni muuaji ila muuaji unamjua tafadhali mtaje ili tumtie hatiani ili afunguliwe mashitaka na kupata adhabu kubwa.“
“Ni mimi.”
“ Kama ni wewe siamini sijawahi kukuona unaua siamini.”
“Ni kweli siwezi kuua hata sisimizi ukiona hivyo ujue kuna sababu.”
“Ni kweli ulimuua mama?”
“Ndiyo .”
“Kwa sababu gani?”
“ Ipo sababu.”
‘ Ina maana mke wangu na mwanangu uliwaua wewe?”
“Ndiyo.”
“Malaika acha utani huu si wakati wa utani nieleze ukweli muuaji ni nani?”
“Muuaji ni mimi,” bado alishikilia kauli yake.
“kama ni wewe kwa nini umewauwa watu wote hawa?”
“Hii si sehemu ya kuujua ukweli, sasa hivi utaongozana na mimi usiulize nakupeleka wapi? Upole wako ndio utakaokusaidi usifanye ujanja wowote kwa usalama wako.“
Anderson alikubali, Malaika Mweusi aliuvaa ule ubibi kizee na kuongozana na Anderson hadi nje. Wote waliwaona walijua ameongozana na kikongwe, wakiwa wameelekea barabarani mara gari aina ya Land Cruiser V8 yenye vioo vyeusi ilisimama mbele yao aliamliwa kuingia ndani ya gari naye alifanya vile bila ubishi liling’oa nanga.

*****
Gari lilipoondoka, Malaika Mweusi alijirudisha akiwa katika hali yake ya kawaida.
Anderson alitulia tuli kama mtu aliyefungwa akitafakari Malaika ni mwanamke wa aina gani? Alikumbuka tabia ya kubadilika mara kwa mara aliyoelezwa na vijana wake pale walipokuwa wakimfuatilia.
Ndani ya gari kulikuwa na vijana wanne waliokuwa wamevalia fulana nyeusi za kubana huku miili yao ikionekana wazi kuwa ni watu wa mazoezi, walioonekana ni walinzi wa Malaika Mweusi.
Kwenye gari watu wote walikuwa kimya isipokuwa Malaika mweusi aliyekuwa akijiangalia kwenye kioo kidogo akiutengeneza vizuri mwili wake. Gari liliingia kwenye moja ya makampuni yake ambayo haikuwa ngeni machoni kwa Anderson kwani alishawahi kufika alipotembezwa na Malaika Mweusi.
Gari ilikwenda moja kwa moja hadi kwenye chumba kimoja ambapo gari liliteremshwa kwa kutumia 'lift' hadi chini na mara baada ya kufika chini aliamuliwa ateremke.
"Samahani mzee tafadhali teremka."
Anderson alitii amri na kuteremka, aliamuliwa aingie kwenye gari jingine aina ya Range Rover Sports Car jeusi, alitii amri na kuteremka kwenye gari moja na kuhamia jingine aliloelezwa,
Ndani ya gari lile ilikuea ni vigumu kuona nje, vioo vyake vilikuwa ni vyeusi tii visivyo ruhusu aliye nje kuona ndani hata wa ndani kuona nje. Gari liliondoka kupitia njia nyingine. Anderson hakujua anapelekwa wapi alitualia tuli kusubiri nini alichokusudia kikukifanya Maliaika Mweusi alikuwa tayari kwa lolote hata kufa.
Baada ya mwendo wa dakika ishirini gari lilipiga honi kwenye geti la mlango wa jumba kubwa la kifahari.
Baada ya gari kusimama wale vijana wanne waliteremka pamoja na Malaika Mweusi na kisha Malaika alimkaribisha Anderson ambaye muda wote alikuwa kimya.
"Karibu mheshimiwa karibu ujisikie kuwa mtu huru,” Malaika alisema kwa sauti tamu.
Jumba lililokuwa mbele yake hakuwahi kuliona kwa macho zaidi ya kuliona kwenye TV.
Akiwa bado ameshangaa Malaika alimshika mkono na kumkaribisha ndani kwenye sebule la kifahari.
"Karibu ujisikie kuwa upo kwako..ooh sorry si kama vile uko ugenini, hapa ni kwako japo makaribisho yenyewe hayakuwa mazuri lakini kutokana na kazi yako hutashangaa."
Anderson hakujibu kitu zaidi ya kuzidi kushangaa alikuwa akijiuliza kuwa lile jumba la nani, alitembeza macho yake kwa chati kulisanifu lile jengo lenye thamani mule ndani. Macho yake yalitua kwenye picha kubwa iliyomuonyesha yeye akiwa amekumbatiana na Malaika Mweusi na picha yake na nyingine ya Malaika kubwa ya paspoti zikiwa zimepamba sebule ile.
Kitu kilichozidi kumchanganya kilikuwa ukubwa wa jumba lile la Malaika Mweusi, akiwa katikati ya mawazo alishtushwa na sauti ya Malaika alipokuwa akiwaamuru walinzi wake watoke nje.
"Haya jamani endeleeni na shughuli zenu."
Walinzi bila ya kujibu waligeuka na kuondoka, Malaika alimgeukia Anderson ambaye bado alikuwa amesimama kama sanamu.
"Ooh, mpenzi karibu sana, japo najua moyo wako umejaa kisasi juu ya yote nina imani moyoni mwako mimi si Malaika wako Mweusi tena bali ni shetani Mweusi. Muda si mrefu utanielewa tafadhali ondoa hofu hakuna baya lolote litakalokupata," alimtoa hofu.
Wakati huo Malaika Mweusi alikuwa amejisogeza karibu kabisa na Anderson na kumshika begani.
"Mbona umegeuka kuwa bubu? Onyesha angalau furaha bila woga."
"Lakini kwa nini umefanya hivi?” Anderson aliuliza swali la kukurupuka.
"Utanielewa maadamu tupo pamoja na sehemu yenye usalama na utulivu wa hali ya juu hapa hata wanajeshi wa Bush waliomshika Sadamu hawawezi kufika."
"Yaani siamini..siamini tena naona kama njozi akili yangu haikubali kama muuaji ni wewe, kwa nini usimseme au ndiye aliyetaka kukuua ili usitoe siri..nakuhakikishia ukimtaja utapata ulinzi kama wa rais.
"Basi ondoa hofu mpenzi utamjua sasa hivi..."
Malaika Mweusi alisema yale huku akimpapasa mgongoni kwa mikono yake laini.
"Sasa mpenzi twende kwanza ukaoge ili utoe uchovu maana naona kila muda nikikuona unatoka jasho."
"Sasa mpenzi twende kwanza ukaoge ili utoe uchovu maana naona kila muda nikikuona unatoka jasho."
"Usiwe na hofu taarifa za muuaji ni muhimu kuliko hata huko kuoga".
"Sasa mpenzi unataka kuniudhi umetaka nikueleze muuaji wa kweli nimekubali sasa haraka ya nini habari zake si za kubabaisha inahitaji muda na utulivu, naomba unisikilize twende."
"Sawa,” Anderson kama kawaida yake hakuwa na ubishi mbele ya kauli ya Malaika mweusi.
Waliongozana hadi ghorofa ya juu katika jumba lile lililokuwa na ghorofa moja, Malaika Mweusi alimuingiza hadi kwenye chumba cha kulala chenye kitanda kipana sana na sofa za nguvu za kukalia kilikuwa ni chumba cha gharama sana.
Anderson alikaa kwenye sofa na Malaika Mweusi alikwenda hadi kwenye kabati alivua nguo alizokuwa amevaa na kuvaa upande mmoja wa kanga nyepesi bila ya kitu chochote ndani.
Alichukua taulo hadi kwenye kiti alichokuwa amekaa Anderson na kumvua zile nguo alizokuwa amevaa na kumfunga taulo, waliongozana wote hadi bafuni kuonga. Walipotoka kuoga Malaika Mweusi alimpa bukta Mr Anderson ambayo ilionekana ni mpya na fulana ya mikanda ambayo iliuweka mwili wazi ili upate baridi.
Akiwa amevalia kigauni chepesi cha kulalia alimuongoza hadi kwenye chumba kimoja kilichokuwa na computer na makochi madogo mawili. Alimuacha Anderson akiwa amekaa kwenye kiti alitoka na baada ya muda alirudi na chupa kubwa ya pombe na glasi mbili zenye shingo ndefu.
Aliziweka kwenye stuli aliyoichukua sebuleni alimimina whisky katika glasi zote mbili na kumkaribisha Anderson aliipokea na kuigonganisha na ile ya Malaika Mweusi kwa lengo la kutakiana heri kinywaji chao.
Wakiwa wamekaa kila mtu na kiti chake wakitazamana, muda wote akili ya Anderson haikuwa sawa kwani alitaka kumjua muuaji halisi.
"Thereza nakusikiliza," Anderson alivunja ukimya.
Anderson kwa mara ya pili alimuita jina lake halisi ambalo lilimganda kichwani mwake kwa muda mrefu.
"Hakuna tatizo nitakueleze."
"Thereza.”
"Abee".
"Nani muuaji?"
"Mimi".
"Thereza huu si muda wa utani wewe si muuaji, muuaji yupo nieleze ukweli nani muuaji?"
"Anderson shida yako ni kumjua muuaji au unataka nini kingine?"
"Nataka kumjua muuaji wa kweli."
"Mimi ndiye muuaji."
"Kwani ukimtaja kuna nini?"
"Wewe umegunguaje kuwa mimi namjua muuaji?"
"Kwenye kitabu."
"Ule mwandiko ni wa nani?"
"Wako."
"Sasa kwa nini hutaki kuniamini au kuuliza nini chanzo cha mauaji, nafikiri hili ni muhimu kuliko kung'ang'ania kitu kisicho kuwepo."
"Sawa, kama ni wewe kwanini umefanya mauaji yale na ulifanya kwa kushirikiana na nani?"
"Kwa kweli mauaji yote niliyofanya ni kisasi yaani ni malipizo ya yote niliyotendewa ila kwenye kitabu changu kila jina lililokuwepo kwenye kile kitabu nimemuua kwa mkono wangu."
"Sawa hao wakubwa walikukosea na Gift alikukosea nini?"
"Kwa wepesi hivyo huwezi kuelewa tulia utalewa vizuri kisha ruksa kunifikisha kwenye vyombo vya sheria. Nipo radhi kwa hukumu yoyote itakayotolewa juu yangu tena safari hii sitapotea kama nilivyofanya awali."
Malaika alipiga funda moja la whiski na kuendelea kuzungumza, aliinama kama dakika mbili bila ya kuongea kitu alipoinuka tayari macho yake yalikuwa yamebadilika kuwa mekunduna kamasi nyembamba zilimtoka huku mishipa ya kichwa ikiwa imesimama kitu kilichomshtua Anderson.
Alijawa na mawazo na kujiuliza maswali yaliyokosa majibu kwani alimuona ni kiumbe kilichobadilika kila wakati, alizungumza kwa sauti yenye kitetemeshi iliyojaa machungu iliyochanganyika na kilio kitu kilichomfanya Anderson kuhoji:
"Thereza mbona unaniangulia kilio badala ya kunieleza sababu za wewe kutoa roho za watu ambao mimi nina imani hawana hatia."
"Anderson inaniuma sana lakini sijui nilichokifanya ni kwa sababu ya kufanya hivyo japokuwa marehemu mama alinikataza nisilipe kisasi. Ni historia ili unielewe lazima nianze kutoka chimbuko langu.
"Nikiwa na umri wa miaka sita akili yangu ilipembua zuri na baya nilishuhudia maisha ya manyanyaso na mateso aliyopata mama kutoka kwa baba ambaye kila siku alikuwa akimpa kipigo kila akirudi kutoka kwenye pombe.
Mpaka napata akili yangu nilimkuta mama akiwa hana baadhi ya meno mdomoni lakini baba hakujali hilo zaidi ya kuendelea kumpa kipigo cha mbwa mwezi. Kila nilipomwa mama amshitaki baba lakini alikataa na kusema anamuachia Mungu kila nikimuangalia mama roho iliniuma sana nilikuwa sina jinsi.
Kuna wakati nilishindwa kuvumilia manyanyaso ya baba nilikwenda kwa wazee ambao ni jirani lakini nao waliogopa kutokana na ukirofi wa baba. Maisha ya manyanyaso na kipigo yaliendelea na hali ile mama aliizoea siku ikipita bila ya mzozo wowote au mama kupigwa ilikuwa kwa bahati mbaya.
Nikiwa darasa la nne siku moja nilirudi nyumbani na kumkuta mama yangu akiwa mwenye wasiwasi mwingi kitu kilichonitia hofu ilibidi nimuulize mama.
"Mama vipi mbona haupo katika hali yako ya kawaida kulikoni?"
"Mwangu leo mbona kasheshe ," alinijibu.
"Kasheshe ya nini tena mama?".
"Sijui kama leo nitalala baba yako alitaka nimpikie bata lakini wakati nimefuata maji kisimani huku nyuma sijui kaja mbwa au paka amechukua baadhi ya nyama."
"Sasa mama si umueleze ukweli," nilimshauri mama.
"Wewe si unamjua vizuri baba yako anaelewa neno?".
"Mmh! Sasa utafanyaje?"
"Nasubiri kipigo sina kingine."
Kauli ya mama iliniumiza roho na kujiapia siku hiyo nisingelala, nitakaa macho mpaka baba atakaporudi."
Usiku ulipoingia niliingia chumbani kwangu na kujilaza lakini masikio yote niliyaelekeza chumbani kwa wazazi wangu, majiri ya saa tano baba alirudi kwa bahati nzuri nilimsikia mlango ukifunguliwa na mama.
Niliwasikia wakizungumza japo maneno yao sikuyasikia vizuri, baada ya muda kidogo nilisikia kilio cha mama hapo nikajua shughuli imeanza. Nilikurupuka kutoka chumbani kwangu na kwenda chumbani kwa wazazi wangu, nilimkuta mama amelala chini huku baba akimshindilia miguu ya kichwa.
Mama alimuomba msamaha huku akimweleza baba kuwa anamuua lakini baba hakusikia kilio cha mama kilichochanganyika na maumivu makali...masikini mama yangu alikuwa kwenye mateso makali. Kufika hapo Malaika Mweusi alianza kulia. Alifuta machozi yake kwa kutumia lile gauni lake, kisha aliendelea.
Kuona vile ilibidi niingilie kati kwa kumvamia baba japo kwa nguvu wala mwili simuwezi lakini nguvu niliyoingia nayo ilimfanya baba apepesuke na kuangukia upande wa pili kwa ukali alinifokea.
"Wewe mtoto unaweza kuingilia ugomvi wetu huna adabu eeeh."
"We Thereza hebu ondoka," mama alisema kwa sauti ya chini iliyoonesha kuwa ana maumivu makali ya kipigo, sikukubali nilipomfuata baba aliyekuwa anamrudia mama kutaka kumpiga, alinisukuma hadi ukutani ambako niligonga kichwa na kupasuka wakati huo baba aliendelea kumsurubu mama. Nami sikukubali nilijitupa juu ya mama ili atuue wote wakati huo mama alikuwa amekata kauli.
Baba aliendeleza kipigo pale aliponikanyaga mgongoni na kunipiga kwa mateke ya mbavuni mpaka nikapoteza fahamu. Nilizunduliwa na maji yaliyokuwa yakinidondokea kwani nyumba yetu ilikuwa ya miti kutokana hali yetu ya umaskini tuliyokuwa nayo.
Nilizinduka na kujizoa pale chini huku mwili wangu wote ukiwa unaniuma kwa maumivu ya kipigo cha baba. Mama alikuwa amejilaza pembeni yangu huku akikoroma nilimgeukia na kumuita.
"Mama..mama..”
" Mwanangu Tereza nichemshie maji ya moto unikande mwili," aliitikia kwa tabu sana wakati huo baba alikuwa ameondoka. Niliwasha moto wa kuni kwa shida na kumchemshia maji ya moto mama. Maji yalipopata moto nilimkanda mwili mzima kidogo alianza kujisikia nafuu.
Siku hiyo baba alirudi mapema ambapo alimletea mama dawa za maumivu aina ya panadol na kisha kuondoka. Kwa kweli hali ya mama haikua nzuri muda wote alishinda amelala hata kujigeuza kwake ilikua ni shida ilikuwa lazima akipiga kelele za maumivu hata mimi pia mwili wangu ulikuwa na maumivu hasa nyonga na sehemu za mbavu nilizokanyagwa na baba na jeraha la kichwani lililopasuka.
lakini kutokana na hali ya mama ilibidi maumivu yangu niyaweke kando ili nimhudumie hata shule ilinibidi nisitishe kwa muda kwa ajili ya mama yangu, siyo siri mama yangu nilimpenda sana.
Baada ya siku chache za kumhudumia kidogo mama alipopata nafuu ilibidi nianze kwenda shule lakini hata hivyo ilinilazimu niwahi kurudi nyumbani kumjulia hali kwa kuwa alikuwa hawezi kufanya kazi yeyote.
Siku moja niliporudi nyumbani kumjulia mama hali yake nilimkuta katika hali mbaya sana akiugulia maumivu nilimkimbilia chumbani kwake ambapo alikuwa amelala kwenye kitanda na kumuita.
''Mama...mama.''
''Ooh...ooh Mungu wangu..nakufa mie..''
''Mama..nini tena mama yangu..mbona unanitisha?”
''Aaha..nani..mwanangu Thereza?” mama aliniuliza.
''Abee mama, ndio mimi.''
''Ooh, vizuri njoo unigeuze upande huu.”
Nilimshika na kumgeuza ambapo alipiga kelele kutokana na maumivu. Maskini mama yangu aliteseka..sijui wanadamu wengine kwa nini Mungu aliwaumba katika hali ya ubinadamu kwa nini asiwaumbe wanyama nilimchukia sana baba sijui nimfananishe na kitu gani,” Malaika alisema kwa uchungu mkubwa huku machozi na makamasi yakimtoka japo jambo lile lilitokea muda mrefu.

Itaendelea
 
Safi sana...

Hapo inawezekana malaika mweusi akawa na undugu na Anderson...

Au Malaika Mweusi ndiyo huyo muuwaji mwenyewe...

Ngoja tuone...


Cc: mahondaw
 
SEHEMU: 12
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Nilimshika na kumgeuza ambapo alipiga kelele kutokana na maumivu. Maskini mama yangu aliteseka..sijui wanadamu wengine kwa nini Mungu aliwaumba katika hali ya ubinadamu kwa nini asiwaumbe wanyama nilimchukia sana baba sijui nimfananishe na kitu gani,” Malaika alisema kwa uchungu mkubwa japo jambo lile lilitokea muda mrefu.
SASA ENDELEA...

Aliendelea kuhadithi kisa kilichokuwa sawa na kuchubua ndonda lilipona. Baada kumgeuza huku moyo wangu ukiwa katika maumivu makali nilimpa moyo mama yangu.
''Ooh pole sana mama yangu taratibu.”
Nilimgeuza mama alilalia mgongo kisha akaniita tena
“Mwanangu Tereza.”
''Abee mama''
“Kila nikikuangalia moyo wangu unaniuma.''
''Una maana gani mama?’
“ Mwanangu najua utapata shida utaishi maisha ya tabu hata ile dhamira yako siamini kama itatimia''
“ Mama...mbona leo sikuelewi, una maanisha nini?”
''Ni vigumu kunielewa kwa vile bado mdogo akili yako ni changa ndiyo maana nakuonea huruma”
“ Unanionea huruma kwa lipi?”
“Mwanangu nakuacha kama kinda la ndege ambalo mama yake amekufa kutokana na mvua kubwa yenye upepo mkali iliyozoa kiota chake na kuua wazazi wote na kubaki kinda lisilojua lolote.”
“ Mama unataka kwenda wapi kama mateso ya baba yamekushinda basi tuondoke wote sitakubali kubaki kuendelea kupigwa na baba. “
Kauli yangu ilimfanya mama acheke kicheko ambacho sikukielewa kilikuwa ni kicheko cha mtu aliye jikatia tamaa ya kuendelea kuishi.
''Tereza mwanangu.''
''Abee mama.”
“Leo nataka kukupa siri moja sipendi kufa nayo moyoni nina imani Mungu atanihukumu.”
''Siri gani mama yangu?”
Mama aliushika mkono wangu na kuunyanyua kisha alianza kunisimulia.
“Miaka 15 iliyopita mimi mama yako nilikuwa mtawa kwenye kanisa kuu mjini nimekuwa pale kwa zaidi ya miaka mitano nikimtumikia Mungu.
Siku moja niliporudi nyumbani kumjulia hali bibi yako ambaye ni mama yangu, kwa kuwa vijijini kuna shida ya maji niliamua kufuata maji kisimani. Kisima hikihiki tulichokitumia miaka ya nyuma kabla ya kujengwa baadhi ya nyumba kulikuwa na pori.
Wakati natoka kisimani kuchota maji ile navuka tu lile pori walitokea wanaume watatu ambao ni vijana wa pale kijijini ambao nilikuwa nimesoma nao na kucheza nao lakini siku hiyo walikuwa na roho ya kishetani kwa kunivamia na kunivuta kichakani ambapo walinibaka kwa zamu.”
“Aah! Mamaa!” Nilishtuka sana kusikia habari ile japo moyo uliniuma nilitulia nijue mwisho wake.
“Kitendo kile kwa kweli kilinidhalilisha sana na kunitia dosari katika maisha yangu ya utawa lakini sikutaka kumweleza mtu na wale wote walionitendea kitendo kile niliwasamehe, kwani sisi tumefundishwa kusamehe saba mara sabini kwa kuwa walionibaka hawakujua walitendalo.
“Nilirudi hadi nyumbani nikiwa na siri yangu moyoni niliogopa kumwambia mtu kwani niliona aibu. Baada ya kumaliza mapumziko yangu nilirudi Parokiani kuendelea na huduma na siri yangu moyoni. Siku zilibadilika na hali yangu ya kimaumbile nayo ilibadilika ilibidi nipelekwe hospitali ambapo nilipopimwa niligundulika ni mjamzito.
“Hapakuwa na jinsi, kanisa ilibidi linitenge na kuondolewa baada ya kuonekana nilivunja masharti kufanya ngono nje ya utaratibu za utawa. Nirudi tena kijijini kuanza maisha mapya, hiyo mimba ndio uliyozaliwa wewe,” habari hizi zilinishitua sana na kujua kumbe sina baba ujauzito wangu uliingia baada ya mama yangu kubakwa.
“Waliokubaka kwani bado wapo hapa kijijini?” nilimuuliza mama.
'"'Eehe wapo mbona huwa naongea nao walishakuja kuniomba msamaha nami niliwasamehe.”
“Aah! Mama hao si watu wa kuwasamehe ningekuwa na uwezo ningewaulia mbali,” nilisema kwa hasira japo nilikuwa binti mdogo.
”Aah, mwanangu jifunze kusamehe ili hata bwana Mungu naye akusamehe usipende kulipiza kisasi.”
“'Ni ngumu, ni akina nani hao?”
Mama alinitajia kwa majina, kumbe ni watu ambao nilikuwa nawaheshimu sana kumbe ni mashetani ipo siku yao,” nilijikuta nikisema kwa hasira.
“Mama kwa nini mungu aliumba wanaume si bora angeumba dunia na jinsia moja. Mama wanaume wote angewageuza wanyama kama nyati, kiboko na hata fisi.” ''Hapana sio wote wanaume wana roho mbaya wapo wenye roho nzuri na pia wapo wanawake wenye roho mbaya kuliko hata wanaume.”
''Hapana...hapana...hakuna mwanaume mwenye roho nzuri yaani mama naapa sitawapenda wanaume mpaka nimeingia makaburini nina imani ni kundi la mashetani yaliyohasi ingekuwa amri yangu ingekuwa dunia ya jinsia moja...na huyo shetani mwingine alikujuaje?”
“Mwanangu lekebishe kauli yako, baba yako usimwite shetani,” mama alinionya.
“Tena mkubwa wa mashetani binadamu gani asiyekuwa na huruma ndio maana nilikuwa najiuliza muda mrefu baba gani asiyekuwa na mapenzi ya familia yake?”
''Yule baba yako tulikutana nae hapahapa kijijini kwa kweli katika siku za mwanzo alikuwa ni mtu mzuri sana, lakini kumbe upole wake ulikuwa wa kuniteka kimawazo kumbe ni chui aliyevaa ngozi ya kondoo...alianza kubadilika na kunipiga hasa baada ya bibi yako kufariki, ulevi ukawa ndio sehemu ya maisha yake.”
“Alizidi kubadilika na kunipiga, yeye ndio aliyenitia ubovu huu wa mwili kwa kipigo hata meno yeye ndiye aliyeningoa kutokana na kipigo.”
“Sasa mama bado mtu huyo unamtetea labda sio mimi nitakapokua mkubwa nimkute amekufa la sivyo lazima nitalipa kisasi,” nilisema kwa uchungu.
“'Hapana mwanangu usifanye hivyo, la muhimu ni kuomba kwa Mungu usome kwa bidii kwani huo ndio mtaji wako utaokutoa kwenye dimbwi la umaskini.”
“Mama ninakuahidi nitasoma kwa bidii ili siku moja niwe hakimu au polisi ili niwashikishe adabu wote wenye tabia ya kuwanyanyasa wanawake'.”
“Mungu atasikia maombi yako lakini chonde usilipe kisasi,” mama alizidi kunionya, alitulia kidogo kisha alianza kuhema kama mwenye pumu, kitu kilichonitisha.” ''Tereza...mwanangu nipe...maji,” mama alisema kwa shida, nilimletea maji wakati huo alikuwa akiongea kwa sauti iliyoanza kufifia.
''Maskini mwanangu...Mungu nilindie mwanangu,” hakuendelea tena alinyamaza kimya,nilimuita:
''Mama...mama.” hakunijibu zaidi ya kunitazama, alitabasamu lakini tabasamu lake liliishia kati alitulia tuli, nilimuita lakini hakunijibu.
Ile hali ilinitisha ilinibidi nitoke nje niombe msaada wa majirani, nilishangaa wakati natoka nje baada ya muda ndipo nilipotambua mama yangu alikuwa amekufa. Siku hiyo nililia sana hadi nikapoteza fahamu. Sio siri mama yangu nilikuwa nampenda sana lilikuwa pigo zito maishani mwangu.
Baada ya mazishi ya mama niliendelea kukaa na baba ambaye nilifahamu kuwa si baba yangu mzazi ila ni wakufikia, nilikuwa sina jinsi lakini ukweli nilimchukia sijui nimfananishe na kitu gani. Si yeye tu hata wanaume wote duniani niliwachukia sana licha ya mama kunikataza nisilipe kisasi. Kisasi changu ni kusoma kwa bidii ili siku moja niwe askari wa cheo cha juu au hakimu ambaye nitawashikisha adabu wote wanaonyanyasa wanawake.
Baada ya msiba wa mama kidogo nyumbani alirudi katika hali ya utulivu, niliendelea kusoma kwa bidii na darasani nilifanya vizuri mtihani wangu wa darasa la tano. Nikiwa darasa la tano mwaka mmoja baada ya kifo cha mama alikuja mama mmoja hivi.
Nilimsikia baba yangu akisema:
“Tena huyo ndio anarudi,” nilipofika niliwasalimia na kisha kuingia ndani, nikiwa nabadili nguo baba aliniita.
"Thereza."
”Abee baba, nabadili nguo."
"Fanya haraka kidogo.”
Baada ya kubadili nguo nilitoka nje.
"Abee baba."
"Thereza mwangu huyu mama hapa anataka akuchukue akupeleke mjini.”
“Na shule baba?”
“Aah! Utasomea huko huko.”
Nilishindwa kukataa hata nguo za kubadili sikubeba niliingia ndani ya gari na kuletwa jijini kwa mara ya kwanza. Mawazo yangu nilijua nakuja kusoma kumbe kufanywa mfanyakazi wa ndani nilipomuuliza mama alinijibu kuhusu kusoma jibu alilonipa ndio lilinimaliza kabisa ndoto yangu ya kuwa afisa wa jeshi au hakimu ilizimika.
Alijibu kuwa yule baba wangu wa kambo amemuuzia kwani alipofika pale kijijni kutafuta mtumishi wa ndani alinitoa mimi, roho iliniuma nilipojua nimeuzwa kama mbuzi.
Kuanzi hapo nikawa mtumishi wa ndani ya nyumba hiyo kwa kweli nilifanyishwa kazi kama mbwa sikuwa na mapumziko. Kitu kilichonifanya nimshangae mama huyu ambaye hakuonyesha hata huruma kwanza umri wangu haukuwa wa kufanya kazi pili kazi zilikuwa nzito ambazo zilinizidi uwezo.
Miaka miwili ilikatika nami nikazoea kazi za sulubu siku moja nilivamiwa chumbani kwangu na baba ambaye alinibaka na kunitishia endapo nitasema nitajuta kuzaliwa. Japo aliniumiza ilibidi niwe mpole sikumweleza mtu nilikumbuka yale yote ambayo yalimtokea mama yangu.
Roho iliniuma nilimkumbuka mama yangu siku hiyo nililia sana kitu kilichomshtua mama mwenye nyumba. Usiku wa siku iliyofuata ilikuwa kama wameambizana mtoto wa mwenye nyumba naye alinibaka, Mchezo ule ukawa wa kila siku kunibaka. Mwisho hali ile niliizoea nikawa sigomi tena akifika baba sawa au mtoto wa mwenye nyumba walinikuta tayari nawasubiri.
Nafikiri walikuwa hawajuani siku zote penzi halina siri siku moja tulifumaniwa na mama mwenye nyumba mbona siku hiyo ilikuwa kasheshe. Pamoja na kujitetea kuwa nililazimishwa lakini hawakunielewa siku hiyo alichonifanya mama yule nina imani akitanitoka akilini mwangu.
Alinifunga kwa kamba na kunichoma katika mapaja yangu kwa pasi na kunipaka pili pili sehemu za siri kisha kunipa kipigo cha mbwa.
******
Baada ya mateso makali nilifukuzwa pale nyumbani tena ukiwa ni usiku huku mvua kubwa ikinyesha. Yaani ulikuwa ukatili wa hali ya juu, kubakwa nibakwe niteswe na kipigo juu.
Nililala kwenye jumba moja bovu hadi asubuhi ambapo niliokotwa na wasamali wema na kupelekwa hospital ambapo sehemu zangu za siri zilikuwa hazitamaniki, mapaja na ngozi yote ilikuwa imebanduka. Kabla ya matibabu kwanza nilipelekwa kituo cha polisi na kupewa PF3 ndipo nilipopata matibabu.
Nilimshukuru Mungu nilipata msamalia mwema mmoja ambaye alisema atanisimamia kuhakikisha wahusika wote wanatiwa hatihani. Katika muda wote niliokuwa pale hospitali alinihudumia kama mdogo wake na baada ya kupata nafuu alinichukua hadi nyumbani kwake.
Kisha aliifungulia mashtaka ile familia kwa unyanyasaji wa kijinsia na ubakaiji. Siku moja wakati anarudi nyumbani yule dada ambaye kitaaluma alikuwa mwanasheria wa kujitegemea alinieleza kuwa ameamua kujitoa katika kesi yangu kwa kuhofia usalama wa maisha yake.
Alinipa nauli ili nirudi nyumbani kwetu iringa katika wilaya ya Makete kwani kama ningeendelea kukaa pale basi maisha yake yangekuwa hatarini. Kutokana na vitisho ilibidi niondoke siku ileile usiku na kulala kwenye nyumba ya wageni karibu na stendi ya mabasi Ubungo.
Kama kawaida asubuhi nilidamkia kituo cha basi, lakini mwaka wa mkosi ni mkosi tu nikiwa nataka kukata tiketi nilipogundua pesa yangu ya nauli ilikuwa nimeibiwa. Niliangua kilio pale kituo cha basi lakini hakuna mtu hata mtu mmoja aliyenijali.
Wapo walionisaidia pesa ya chakula tu na hata jioni ilipoingia ilibidi nilale palepale kituoni hadi asubuhi. Nilijifikiria sana nirudi tena kwa yule dada ili nimweleze masahibu yaliyonikuta, lakini aliyonieleza jana yake yaliniogopesha kuhofia usalama wa maisha yake.
Niliamua kuingia mjini na kuomba msaada kwa wasamalia wema, siku hiyo Mungu aliniangazia kwani mpaka jioni nilikuwa nimepata laki moja na arobaini elfu. Hapo tamaa ikanipata nikaona nisifanye haraka kuondoka niendelee kuombaomba hata nikirudi nyumbani niwe na pesa nyingi za kufungulia miradi ya kujiendeleza kimaisha.
Jioni ile nilipanga chumba cha gesti moja ya uswahilini na kulipokucha nikaendelea kuchangisha mchango wa hiyari. Siku hiyo mambo hayakuwa mazuri sana nilipata elfu sitini. Kama kawaida yangu jioni nilirudi kwenye chumba changu na kulala hadi asubuhi.
Kulipo pambazuka kama kawaida yangu kiguu na njia, nakumbuka siku moja nilikutana na mtu mmoja ambaye nilimuomba pesa zaidi ya mara tatu. Hapo sasa niliona naanza kuchanganya mambo niliamua kukaa kona moja sehemu ya Mtaa ya barabarani maeneo ya Faya nakufanya hapo ni makazi yangu ya kudumu.
Niliamua kutafuta nguo zilizochakaa ili nionekane kweli ni chokoraa na shukuru kipindi kile cha mzee ruksa watu walikuwa wakitoa pesa zao bila ya ubahiri. Ndani ya mwezi mmoja nilipata pesa nyingi kiasi cha kufuta wazo la kurudi nyumbani sikuwa na neno niliamua kupanga chumba na kununua vitu vya ndani.
Kuanzia hapo ikawa ni kawaida yangu ifikapo jioni kujichanganya katika majumba ya starehe ilikuwa ni vigumu kunitambua kwani mchana nilikuwa chokoraa niliyenyoa upara wenye kuonyesha kidonda kikubwa lakini usiku hubadili nguo na kuvaa nguo nusu uchi za kichangudoa na kichwani nilivaa wigi la nguvu. Nashukuru Mungu aliniumba nikiwa na umbo la kuvutia ndio maana hata baba na mtoto wake walishindwa kujizuia na kuamua kunibaka.
Nikiwa viwanjani nilipata marafiki waliosifia figa yangu kuwa endapo nitafuatana nao lazima wazungu wajichanganye siwezi kukosa dola mia tano mpaka elfu kwa mara moja. Kutokana na malengo yangu nilikubali kuifanya kazi ile kwa muda kisha niachane nayo.
Kuanzia hapo nikawa na kazi mbili asubuhi nakuwa ombaomba na usiku naruka viwanjani kama kawaida. Utafikiri nilikuwa nimejifukiza dawa wanaume walikuwa wakinifuata kama malkia wa nyuki hoteli zangu zilikuwa za kitalii tu sio za uswahilini.
Kutokana na kitendo cha mimi kuwazidi kete baadhi ya rafiki zangu kiliwaudhi na walifanya kunifanyia njama. Shoga yangu mmoja alinipeleka kwa rafiki yake mmoja anayekuwa akisoma chuo kikuu ili tukamtembelee kumbe walikuwa wamepanga nibakwe na wanafunzi zaidi ya kumi ili wanikomoe .
Bila ya kujua niliongozana na rafiki yangu yule tulipofika chuo kikuuu niliingia katika chumba kimoja cha yule shoga yake mara aliniomba nimsubiri kumbe walikuwa wamewafuata wale wanafunzi wa kiume mara waliingia vijana wa kiume kama kumi walinishika kwa nguvu na kunibaka. Kutokana kuwa sijawahi kufanya mapenzi zaidi ya mwanume mmoja nilizidiwa nguvu na kupoteza fahamu nilipozinduka nilijikuta nipo hospitali nikiwa katika hali mbaya.
Wanieleza kuwa walinikuta ufukweni nikiwa mtupu kama nilivyozaliwa baada ya kuokotwa na askari wa doria ambao walinileta hospitali. Kila nilivyowaeleza hawakukubali walidai kuwa mimi ni changudoa uliyataka mwenyewe. Niliruhusiwa kutoka hospital baada ya wiki tatu.
Nilipotoka hospitali hali yangu haikuwa nzuri sehemu zangu za siri zilikuwa zimeharibika vibaya na zilikuwa zikitoa harufu mbaya kama mzoga uliokufa kwa ajali.
Kwa vile nilikuwa na pesa za kutosha nilikwenda kwenye hospitali ya Mjerumani ambaye huduma zake zinasifika.
Hospitali yenyewe ipo Kibaha, Pwani, nilikutana na yule mzungu ambaye alinichukua vipimo baada ya muda alinijulisha kuwa vipimo tayari nakuniita kwenye chumba ambacho kilikuwa na mitambo ya kisasa.
Alinilaza kitandani ambapo aliniambia nipanue miguu yangu, alikuwa amevaa gloves na kunichunguza sehemu zangu za siri na kisha aliandika kwenye karatasi kabla hajaniruhusu kuvaa nguo zangu. Tulirudi hadi ofisini kwake na kunihoji sababu zilipelekea nipate ugonjwa huo.
Nilimweleza yote bila ya kumficha kitu, alitikisa kichwa na kusema:
“Ugonjwa huu auhusiani na kubakwa bali ni vimelea ambavyo vimepandikizwa. Katika hospitali za kawaida usingepona kwani sehemu zako za siri zingeoza kabisa na hatimaye utumbo pia mwisho wake ungekufa.”
 
SEHEMU: 13
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Nilimweleza yote bila ya kumficha kitu, alitikisa kichwa na kusema:
“Ugonjwa huu auhusiani na kubakwa bali ni vimelea ambavyo vimepandikizwa. Katika hospitali za kawaida usingepona kwani sehemu zako za siri zingeoza kabisa na hatimaye utumbo pia mwisho wake ungekufa.”
SASA ENDELEA...
“Walinipandikizia kivipi?"
" Hii ni dawa hatari sana sijui aliyekupaka sehemu za siri ameitoa wapi pia inaonekana aliyefanya hivi alikuwa amedhamiria kukuua."
Kusikia vile moyo wangu ulinilipuka na kujiuliza hivi hawa nimewakosea nini hasa mpaka wafike hatua ya kutaka kuniua.
“je, gharama zake utaziweza?" aliniuliza.
‘Kwani ni shilingi ngapi?"
"Mmh! Sijui kama utaiweza hasa kutokana na kazi yako ya uchangudoa."
'We nieleze nikishindwa si basi siyo kazi yangu.”
"Milioni mmoja na laki saba tena nimekupunguzia kutokana na hali yako ya ugonjwa huu, dawa zake ni lazima uchanganye na dawa zaidi ya saba na matibabu yake halisi ni shilingi milioni mbili na laki mbili."
Baada ya kuniambia vile nilishusha pumzi japokuwa hela nilikuwa nayo lakini matibabu ni bora zaidi ya pesa ambazo zinatafutwa.
“Ndiyo nitalipa.”
“Sasa lini utaanza matibabu?"
"Hata sasa hivi niko tayari."
"Pesa unayo hapa?"
“Hapa nina laki tano nyingine nitaleta."
"Sasa sikiliza binti nataka nikusaidie na wewe unisaidie," alisema daktari.
"Unisaidie kivipi na mimi nikusaidie kivipi?"
"Nitakutibu bure tena ndani ya wiki moja hali yako itakuwa nzuri."
"Eeh na wewe nikusaidie nini?" Wazo langu kunitaka kimapenzi japokuwa sikuamini sana kwa vile sehemu zangu za siri zilikuwa hazitamaniki.
“ Kuna kazi moja ndogo ambayo nitakupa nina imani haitakuwa nzito kwako lakini yenye ujira mkubwa."
“Kazi! Kazi ipi hiyo?”
“ Kutokana na maelezo yako utanifaa sana tena sana kwani ulipokuwa ukikutana na mwanaume ulilipwa kiasi gani?"
“Kwa wazungu ilikuwa dola mia hamsini mpaka mia mbili kwa waswahili ilikuwa elfu hamsini mpaka laki na nusu lakini mimi nilikuwa siwataki waswahili."
"Basi kuna kazi yangu nitakulipa dola elfu mmoja kwa kila kichwa."
"Kwa kichwa una maana gani?"
"Utajua subiri upone kwanza, mbona hii kazi imewanufaisha wasichana wengi kama tungejuana mapema wala usingekumbwa na matatizo yote haya."
Nilianza matibabu mara moja kwa kweli nilipata matibabu ya hali ya juu ndani ya siku mbili hali ilianza kuwa vizuri na ndani ya wiki mbili nilipona kabisa. Baada ya kupona nilikutana rasmi na Mr Rymond au kama anavyopenda kuitwa Mr Ray ndani ya ile hospital yake ambavyo tulikutana under ground kulikuwa na sebule kubwa yenye samani za kifahari.
Aliniuliza natumia kinywaji gani, nilimweleza kuwa natumia pombe kali ambazo nilizoea kuzitumia .Alileta chupa kubwa kama mtungi aina ya whiski ikiwa kwenye kitololi kidogo alimimina kwenye glasi mbili kisha alinipa ya kwangu na yeye akabaki na yake.
" Karibu sana," Dk Rey alinikaribisha.
"Ahsante.”
Tuligonganisha glasi zetu ili kuonesha upendo na kutakiana baraka ya kinywaji chetu.
"Ndiyo binti kwa umbile lako na uzoefu wako kuna kazi mmoja nitakupa, nina imani itakupa pesa nyingi kwa muda mfupi itategemea bidii yako."
"Kazi ipi hiyo?"
Kabla ya kunijibu kililia kitu kama alama ya kuashiria kuna jambo.
"Samahani nakuja," alinitaka radhi na kuelekea chini ambapo aliniacha peke yangu nikiwa na mawazo mengi juu ya hiyo kazi aliyotaka kunipa.
Malipo manono kiasi kile na ule usemi wa kila kichwa kimoja dola 1000 alikuwa na maana gani. Nilitulia huku nikikata maji taratibu kama mamba mzee . Baada ya dakika kama tano alirudi na kunitaka radhi tena.
"Ooh ,samahani kwa kukatisha mazungumzo."
"Bila ya samahani najua una majukumu mengi."
"Ni hivi kwa kuwa unauzoefu mkubwa na kazi yako ya uchangudoa na ni msichana mwenye mvuto wa sumaku nina imani kazi yangu utaifanya vizuri."
"Ni kazi ipi hiyo?"
"Ni hivi, kazi mpya haina utofauti na kazi ya uchangudoa lakini tofauti yake hautokuwa ukifanya mapenzi."
"Unafikiri kuna mwanaume atakaye kubali kukulipa pesaa yake bila ya tendo la ndoa?"
'Swali lako ni zuri, shida yangu ni yule mtu ukishapatana naye usikubali akupeleke anapopataka yeye mwambie gharama ya chumba utalipa wewe kwa hiyo yeye ataona amepata mchekea, chakufanya utaenda naye hadi chumbani na kumuacha. Utamuachaje? Mkishaingia usipokee kwanza pesa yake mweleze akusubiri na wewe toka nje wala usirudi.
Ndani ya gari utamkuta mtu atakulipa pesa yako muda uleule kazi itakuwa imemalizika kwako sasa itakuwa ni juu yako kutafuta mtu mwingine."
"Sasa huyo mwanume atabaki huko chumbani akiwa anfanya nini?" nilitaka kujua.
"Ndio maana nikakueleza kuwa utakuwa milionea kwa muda mfupi sana, maswali mengi hayana umuhimu nia imani tumeelewana sawa?"
"Kwa kuwa una maadui sipendi upate matatizo kama yale unajua vizuri akumulikae mchana usiku atakuchoma nitakufanyia plastic surgery ili kutengeneza uso wako vizuri uvutie mara dufu ."
Sikuwa na kipingamizi nilifanyiwa utengenezaji wa uso ndani ya miezi miwili nilikuwa mtu tofauti sana sikuwa tena yule Thereza unayemjua nilitengenezwa umbo la kimalaika kweli.
Pua yangu ya asili ilikuwa ni pana lakini ilipunguzwa na kuwa nyembamba ya kisomali hata mama yangu mzazi kama angefufuka asingenitambua uso wangu ulichongoka. Baada ya kuwa sawa mara moja nilingia viwanja na safari hii sio kusimama barabarani bali kuagiza kinywaji cha gharama ni kwenye mahoteli makubwa .
Haikuchukua muda mtu mmoja mwenye wadhifa alijipendekeza masharti yalikuwa yaleyale ya kumpeleka nitakapo mimi alikubali bila pingamizi niliongozana naye.
Sharti nililompa atangulie nje nikiwa na sababu asijulikane ametoka na mimi ni moja ya masharti niliyopewa na Dokta Ray.
Yule kibopa alitangulia nje baada ya dakika kama tano hivi nilimfuata na kumweleza aingie kwenye yeksi iliyokuwa nje kwa ajili ya kazi maalumu. Nilikwenda naye moja kwa moja hadi kwenye ile nyumba ya wageni ya Royal Light. Nilikodisha chumba na kupewa funguo niliongozana na kibopa yule hadi chumbani.
Tulikaa wote kitandani akiniangalia kwa macho ya mahaba, nilimuomba radhi anisubiri nakuja baada ya muda si mrefu.
"Basi usichelewe bibie."
"Ondoa shaka mpenzi."
Nilimuacha ndani na kutoka zangu nje, nilirudi ndani na ile teksi iliyotuleta ambayo ilikuwa bado inaningojea nje. Dereva alinipa dola 1000 kisha akaniuliza anipeleke wapi kwa vile muda ulikuwa bado unaruhusu. Alinihamishia katika hoteli ya Sea Cliff napo hata robo saa haikufika nilichukuliwa na kijana wa kiarabu akajipendekeza nikaondoka naye japo mwanzo aling’ang’ania sana tutumie gari yake lakini
nilimdanganya kwamba nisingependa watu wajue nimeongozana naye alikubali kilimpeleka katika hoteli nyingine tofauti ambayo ipo karibu na maeneo ya White Cruse.
Mpaka saa saba za usiku nilikuwa tayari nimelamba watu wanne nilirudishwa nyumbani kulala wakati huo nilikuwa nimepanga maeneo ya Magomeni Chemchem kwa walima mchicha.
Niliona kama maajabu vile yaani kazi ya saa tano nilikuwa nimeingiza dola za Kimarekani elfu nne. Kazi ile nilipangiwa kuifanya mara tatu kwa wiki, ijumaa, jumamosi na jumapili. Siku nyingine nilishinda nyumbani kujipumzisha.
Nilipewa maelekezo kuwa nisijihusishe na kazi ya aina yoyote zaidi ya kupumzika lakini kila jioni ilikuwa ni lazima tukutane.
Tulikuwa zaidi ya wasichana kumi hapo ndipo nilipojuana na mkeo mama Gift ambaye alitokea kuwa rafiki yangu mkubwa. Kwa kweli kazi yetu ilikuwa ni nzuri ndani ya miezi sita nilikuwa na pesa nyingi lakini hata hivyo siku zote nilikuwa najiuliza maswali yasiyokuwa na majibu juu ya wale wanaume tuliokuwa tukiwapeleka kwenye nyumba za wageni walikuwa wanafanya nini?

Siku moja nilimdodosa Dokta Ray juu ya wale watu ndipo aliponipa siri hiyo lakini mwanzoni nilijua ni kweli kumbe ni uongo eti wao wanadili na wauzaji wa madawa ya kulevya hivyo wale wanaowapeleka ni wateja wao wanatujua wanakuja kwa njia ya kututongoza na tunapowapeleka kwenye nyumba za wageni na kuwaacha kuna watu ambao wakwenda kuwauzia yale madawa ya kulevya.
Pesa nyingi nilizozipata nilijenga nyumba kubwa maeneo ya Kunduchi na kununua magari mawili ya kutembelea na pesa nyingine niliweka benki. Siku moja nilipita katika maeneo ya kijiweni kwangu kwa zamani niliwakuta washirika wangu hakuna hata mmoja aliyenitambua.
Sio siri roho iliniuma kwa jinsi nilivyowakuta niliwapa pesa za kutosha na niliporudi nyumbani nilichukua nusu ya pesa zangu na kununua maeneo sehemu mbal mbali na kuamua kujenga vituo kwa ajili ya watoto wa mitaani . Ndoto yangu ilikuwa mara wamalizapo masomo yao wakute nimeshajenga viwanda ili wafanye kazi.
Wakati huo nilikuwa naendelea kazi yangu ya kusaka wateja wa madawa ya kulevya kwa muda mfupi jina langu lilikuwa kubwa ndani na nje ya nchi kutokana na kutoa misaada mbalimbali kwa watoto wa mitaani. Nilipata wageni wengi kutoka katika mashirika yasiyo ya kiserikali ya nchi za nje na kutaka kujua shughuli zangu naziendeshaje.
Niliwaeleza na hapo misaada mingi ilipofumuka na ndipo nilipozidi kujiendeleza ikiwa pamoja na kupata mikopo iliyonisaidi kujenga viwanda vidogo vidogo. Kwa mwaka mmoja NGO'S za nje zilikuwa zikinitumia dolla za kimarekani laki tano hizi zilinisaidia kuboresha miradi yangu na kupanua shughuli zangu.
Wakati huo rafiki yangu mama Gift alikuwa na mpenzi wake ambaye walifikia
hatua ya kutaka kuoana lakini mara ilitokea kutoelewana na yule mpenzi wake ilionesha mkeo alikuwa amepunguza mapenzi.
Kwa kuwa tulikuwa mashoga ilibidi anitumie mimi ili nimueleze tatizo linalofanya mpaka penzi lao kuyumba nilijitahidi kwa kadri ya uwezo wangu kuwapatanisha lakini mkeo alinieleza kuwa niachane nae.
Nilikuwa namuonea huruma sana yule kijana nilijaribu kumliwaza, alinieleza nimweleze nini anachotaka chochote kile atampatia ili tu arudishe penzi lao kama zamani.
Nilipomweleza mkeo mama Gift kwa kuwa alikuwa shoga yangu mkubwa, ilibidi anieleze kuwa yeye ni mchumba wa mtu na mchumba wake ni ofisa wa jeshi la polisi upande wa upelelezi ambaye alikuwa msomoni Russia amerudi.
Alinieleza hata hii kazi ya kukusanya wateja itamuwia vigumu kwani wakati wowote atakuwa mke wa mtu. Kuwa ule urafiki wake na yule kijana anayeitwa Mac Donald alikuwa anafanya nae kwa wizi tu lakini mhusika mwenyewe alikuwa nje ya nchi.
Ilibidi nimweleze ukweli Mac Donald juu ya penzi lao kulega, nilishangaa aliponiuliza kama nina mpenzi nilimjibu kuwa sina.
Basi yule kijana akaniahidi vitu vingi endapo nitamkubalia kuolewa naye ili kumuonesha mama Gift. Kwa kuwa mimi nilijali msirahi nilimkubalia ndipo aliponinunulia lile gari langu la Lexus pamoja na kuniporomeshea jumba hii la kifahari.
Mipango ya harusi iliendelea kama kawaida, siku mmoja nilikutana na mkeo mama Gift sikumficha nilimweleza ukweli juu ya uamuzi wangu na Mc Donald wa kunioa pia nilimweleza vitu alivyonipa ambapo nilimuona akionyesha hali ya unyonge fulani niliaga nae.
Ndoa yangu iliwahi kufanyika kuliko ya kwao nilimtumia kadi ya harusi .Usiku wa siku ile nilipokea simu kutoka kwa mkeo ambapo niliongea naye
"Ted vipi?"
"Safi tu lete stori shemu hajambo?"
"Hakuhusu."
" Mmh! Unasemaje?"
"Sikiliza Ted, elewa wazi Mac Donald ni mpenzi wangu na tulikuwa hatujaachana hivyo shoga kwa usalama wako achana naye."
"Mbona sikuelewi? "
"Huwezi kunielewa, umalaya tu, ina maana wanaume wameisha hadi umfuate bwana wangu?"
"Wewe si mke wa mtu mtarajiwa?"
"Kama hivyo? “
"Subiri ndoa yako."
"Ted huu si wakati wa mzaha, ama sivyo utajuta kuzaliwa hiyo ndoa yenu mtaifunga kwa Mungu .
"Usinitishe.”
''Tutaona.'.
''Tutaona.'' alikata simu.
Siku nne kabla ya kufunga ndoa nilitekwa kutoka nyumbani na watu wasiojulikana niliteremshwa kwenye gari na kufungwa kitambaa cheusi usoni.
Nilipelekwa sehemu nisiyojulikana na kuteremshwa garini niliingizwa kwenye jumba moja na kufunguliwa kitambaa usoni, mbele yangu kulikuwa wanamume wenye miili iliyoshiba.
Nilishangaa kuwepo sehemu ile nilijiuliza nimepelekwa pale kwa kosa gani kabla ya kupata jibu nilikatishwa na makofi yaliyotoka nyuma yangu.
''Shoga kiko wapi sasa tusilaumiane nilikueleza ukafikiri ni utani sasa ndoa yako utaifungia kwa Mungu,” ilikuwa ni sauti ya mkeo mama Gift aliyekuwa amevalia trak sut nyekundu na raba nyeupe.
''Kwani shoga tatizo ni nini kama ni Mac Donald mchukue na mimi uniachie uhai wangu,” mwanzo nilidhani utani lakini mpaka kufikia pale niliona kuna dalili mbaya mbele yangu.
''Mmh! Ndio unalijua hilo, ushachelewa.”
Aliwaamuru wale vijana wa kazi wanivue nguo zote na kulazwa chali juu ya meza.Waliniweka kama vile mtu anayetaka kujifungua japokuwa sijawahi kujifungua.
Wakiwa wamenishika barabara mama Gift alikuja hadi karibu yangu akiwa ameshika kisu kikubwa chenye ukali wa kutisha nilimsikia akisema huku akinishika sehemu zangu za siri.
''Hizi ndio sehemu zinazo kutia kiburi'', mara nilianza kusikia maumivu ya kuchokonolewa na kitu chenye ncha kali maumivu yalizidi kwani kisu kilizidi kuingizwa ndani zaidi katika sehemu zangu za siri, maumivu yalikuwa ni makali sana na sehemu zangu za mapaja nazo walizichanachana na kisu. Baada ya kumaliza unyama wake walichukua kipande cha mti na kunishindilia nacho damu zilinitoka kama ng`ombe aliyechinjwa.
Maumivu yalikuwa makali nilimsikia mama Gift akiwaamuru wale vijana wake wanipige hadi niage dunia. Kipigo kiliendelea mpaka nikapoteza fahamu sikujua kilichokuwa kinaendelea.

Itaendelea Alhamisi
 
SEHEMU: 14
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Maumivu yalikuwa makali nilimsikia mama Gift akiwaamuru wale vijana wake wanipige hadi niage dunia. Kipigo kiliendelea mpaka nikapoteza fahamu sikujua kilichokuwa kinaendelea.
SASA ENDELEA...

Nilipozinduka nilijikuta nipo kwenye nyumba moja mbovu mbovu ya miti ambayo aliyekuwa nje anakuona waziwazi juu iliezekwa na majani, nilijishangaa sana pale nilipo ni wapi nilipotaka kujigeuza nilihisi maumivu makali sana mwili mzima nilikuwa nimelazwa kwenye kitanda cha kamba nilitulia kidogo na kuvuta hisia kuwa pale ni wapi na nimefikaje na mara ya mwisho nilikuwa wapi.
Nikiwa katikati ya mawazo mara alitokea mzee mmoja wa makamo akiwa amembeba mtoto mdogo kama wa miezi saba mgongoni na kanga chakavu.
''Unajisikiaje mjukuu wangu?”
''Wewe ni nani na hapa nilipo ni wapi?” nilimuuliza yule babu ambaye kichwani alikuwa na nywele nyingi nyeupe.
''Mjukuu wangu hapa ni kijiji cha Nyato au kama wenyeji wanavyopenda kukiita Hatanijua nani, na mimi mjukuu wangu naitwa Nitakufa lini siku zenyewe hazisogei.” “Mmh jina hili kiboko,” niliguna kimoyomoyo.
''Samahani babu utakufa lini hapa kwako nimefikaje?”
''Ni historia ndefu la muhimu kwanza ni kushughulikia afya yako, Mungu mkubwa sikutegemea kama ungeongea tena.”
“Kwani babu ilikuwaje?”
“Taratibu mjukuu wangu labda nikuulize wewe ulikumbwa na masahibu gani?” Kabla ya kujibu nilitulia kwanza kurudisha kumbukumbu mara ya mwisho kipi kilichonisibu Taratibu nilianza kuvuta kumbukumbu na kukumbuka mara ya mwisho, nilikumbuka vizuri aliyonifanyia mkeo mama Gift ilionyesha wazi kuwa alidhamilia kuniua. Nilipotaka kumweleza babu nilianza kusikia maumivu ya kifua na mbavu.
''Babu...babu kifua kinaniuma.”
“Basi pumzika, hata hivyo hali yako bado taratibu itakaa vizuri mjukuu wangu.”
Babu alininywesha majani yenye ukakasi uliochanganyikana na uchungu, kisha alinipa maji mengine mekundu yenye harufu fulani ambayo sio nzuri kidogo nitapike.
''Hii dawa ndio iliyokusaidia kurudisha damu yako ulikuwa huna damu kabisa baada ya kunywa dawa babu alitoka na aliporudi alikuja na debe lililoonyesha halijui maji kwa nje na lilikuwa likifuka mvuke kuonesha maji yaliyomo ni ya moto.
Yule mzee alianza kunikanda mwili mzima pale nilipokuwa nimelazwa kwenye kitanda cha kamba alinivua nguo zote na kubaki kama nilivyozaliwa. Alinikanda mwili mzima maji yalikuwa ya moto na wakati mwingine nilipiga kelele za maumivu na kufikia hatua ya kutukana ili aniachie kwani haikuwa lazima kama maumivu ni yangu lakini hata hivyo babu hakusikia maneno yangu alinieleza.
“Binti huruma yangu ndio kifo chako.”
Alinigeuza na kunikanda sehemu za mgongoni kisha alinichua na mafuta yenye harufu mbaya ambayo alijipaka mikononi na kubanika kwenye moto na kuanza kunikanda mwili mzima kisha hunipa uji wa muhogo mweusi na viazi. Nilikuwa najiuliza yule mzee ni nani na pale ni wapi kama kwa mganga nani kanipeleka.
****
Siku zilizidi kukatika hali yangu iliendelea vizuri, kidogo nilianza kukaa chini angalau kwa nusu saa. Nilishindwa kuelewa kama pale ni kwa mganga wa kienyeji mbona sioni wagonjwa wengine zaidi ya yule mtoto aliyekuwa naye bila mama yake. Siku mmoja ilinibidi nimuulize:
"Hivi babu Utakufalini huyu ni mtoto wa nani na bibi yupo wapi maana siku zote nakuona uko peke yako?”
"Mjukuu wangu duniani kuishi kwingi si kuzeeka bali ni kuona mengi wahenga walisema kuwa uyaone ."
"Una maana gani babu?” nilimuuliza.
"Historia ya huyu mtoto ni ndefu inahitaji nafasi la muhimu kwanza ni kuangalia afya yako inatengemaa ili siku moja urudi ulipotoka."
Sikutaka kumdadisi zaidi nilitulia na kuendelea na shughuli zangu za matibabu ya kiasili ambayo sasa si mageni kwangu. Baada ya muda niliweza kusimama na kuanza kutembea lakini kuna wakati nilitembea kwa kuinama kutokana na maumivu ya mgongo.
Babu aliendelea kunihudumia kuhakikisha afya yangu inaimalika , vyakula nilivyokula havikuwa vigeni sana kwani hata kijijini nilikotoka ndivyo vilikuwa vyakula vyetu vikuu. Afya yangu baada ya muda iliimalika kiasi yalibaki madoa na maumivu madogomadogo japokuwa sehemu zangu za siri zilikuwa bado zina makovu kama nimekatwa na panga.
Babu Utakufalini baada ya kuridhika na hali yangu siku moja tulikuwa tumekaa baada ya kumaliza kula chakula cha usiku, tukiwa tumewasha majani kama taa yetu ya asili alianza kunipa mikasa mizito.
Kuwa sehemu kama ile kama una roho ndogo huwezi kukaa muda wote huo kwani ilikuwa inatisha usiku kulikuwa na wanyama wakali kama simba ambao walikuwa wanapita karibu na eneo la nyumba yetu. Lakini babu Utakufalini alikuwa ni mjuzi alisema yote mwenye nia mbaya pale hawezi kupaona alianza kunieleza jinsi alivyonipata mimi.
"Mjukuu wangu siku moja wakati nikitoka shambani nilipovuka bonde moja mbele yangu niliona gunia. Nililisogelea ili nijue kuna nini niliposogelea ndipo nilipogundua lilikuwa na damu. Nilijiuliza kuna nini ilinibidi nifungue nijue kilichomo nilishtuka kuona mwili wa binadamu japo nilishangaa lakini sikushtuka wala kuogopa kwani hali ile nilikuwa nimeshaizoea.
“Mwanzo nilikuwa nashtuka na kuogopa pale nilipokuta maiti za watu, mjukuu wangu katika pori hili kama una moyo mwepesi huwezi kukaa kuna miujiza na matukio ya kutisha. Katika kila mwezi ni lazima niokote maiti moja au zaidi.”
“ Eti ulikuwa unasema unaokota maiti moja kila mwezi hizo maiti zilikuwa zinatoka wapi?” nilimuuliza.
“Ukweli sijui lakini inavyoonekana huu msitu watu wengi wanautumia kutupia maiti za watu. “
“Kwa nini babu usipeleke taarifa polisi?”
“Mjukuu wangu we acha tu, vuta subira utaelewa tu kwa nini sikupeleka taarifa polisi?"
"Ee’he tuendelee babu ndio ikawaje?”
“Kama nilivyokueleza kuwa msitu huu hasa pale bondeni ndipo jalala la kutupia maiti za watu, kuna kipindi huwa naokota maiti mpaka tatu kwa mwezi. Basi mjukuu wangu baada ya kuona mwili wako kwenye gunia na kuulaza nje ili niuchimbie. Kilichonishangaza mwili wako ulikuwa umejaa damu sehemu moja mapajani na sehemu za siri. Lakini mwili wako ulikuwa na joto tofauti na miili mingine niliyowahi kuiokota kabla ilikuwa imesha poa. Kutokana na uzoefu wangu nikagundua hujafa bali ulikuwa umepoteza fahamu.
“ Sikuwa na jinsi ilinibidi niubebe mwili wako hadi nyumbani kwangu na kuuchunguza ambao niligundua kuwa sehemu zako za siri kulikuwa na majeraha makubwa. Kutokana na uwezo wangu wa kujua dawa za magonjwa ya siri nilianza mara moja kukutibu majeraha hayo makubwa. Ilichukua muda kurudiwa na fahamu zako ndipo siku ile nilishtuka kukuona katika hali ile nilimshukuru Mungu.
“Ndio nikaendelea na matibabu mpaka hivi leo hali yako kidogo inaridhisha nina imani siku zinavyozidi kwenda ndipo nitakapokuruhusu urudi ulipotoka."
“ Babu nashukuru sana sijui nikulipe zawadi gani ya kuokoa maisha yangu, lakini ninakuahidi utaishi maisha mazuri nusu ya peponi pale nitakapotoka kwenye msitu huu na kurudi nyumbani, " nilimuahidi mzee Utakufalini.
“Tumuombe Mungu hebu leo naomba unipe kisa cha wewe kilichokuweka kwenye hali ile ambayo kama Mungu asingenionesha mwili wako basi jina lako ulimwenguni lingepotea."
Kutokana na jinsi babu alivyonifanyia sikuwa na sababu ya kuuficha ukweli nilimweleza yote tangu mambo yaliyomsibu marehemu mama yangu kipenzi na jinsi mimba yangu ilivyopatikana na mlolongo mzima wa maisha yangu mpaka hatua iliyofikia ya kuwa pale kwake.
Babu aliniangalia na kutikisa kichwa chake kisha alinipa pole.
" Pole sana mjukuu wangu yote hiyo ni mitihani ya maisha lakini usife moyo, mama yangu alinikataza nuisilie kisasi naamini kama nitamfuata yeye mwishowe nami nitakufa kama yeye, kwa nini mama yangu hakuniruhusu kulipa kisasi?...Kwa nini mama umeniacha mwanao kwenye dunia yenye viumbe wenye roho mbaya walio tayari kuyapoteza maisha ya mwanadamu mwenzake.
Kufika hapo nilianza kulia ilibidi babu afanye kazi ya ziada kunibembeleza.
“Babu inauma sana ona sasa mama yangu ameona hali hii ya kinyama niliyofanyiwa unafikiri kuna usalama tena wa maisha yangu akiniona tena atanibakisha kama sio safari hii atanikata kichwa kabisa ili uokote kiwiwili kilichotengana na kichwa.
“ Ni kweli usemayo lakini Mungu yupo kama alikulinda na hili basi atakulinda na lingine.”
“ Babu kutokulipa kisasi ni donda ambalo litaendelea kunitesa, nina imani donda moyoni linaweza kuniua kuliko kipigo.”
“ Tujifunze kusamehe, japo tuna machungu moyoni mwetu bwana atatupa farijiko na kuyasahau maumivu yote ya mioyo yetu.”
“ Babu nitajitahidi, lakini, sijui..hasa shoga yangu sijui..sijui..sijui.”
“ Naheshimu wosia wa mama yako nina imani mzimu wake ndio unaochangia sehemu kubwa ya kuokoa maisha yako.”
“ Sina budi kufuata wosia mama sina budi kumuenzi mama yangu, mama yangu nilimpenda kuliko kitu chochote duniani ..eenhe Mungu mpe mama yangu makazi yaliyo mema kwenye pepo ya milele.”
“Najua mjukuu wangu una machungu sana yasiyoelezeka moyoni mwako muombe Mungu atakupa farajiko lenye kukufanya uyasahau.

“ Ameni..ee Mungu hebu nipe nguvu ili niweze kukujua wewe na kutimiza wosia wa mama yangu na kushinda nguvu za shetani,” pamoja na machungu nilijikabidhisha katika mikononi mwa Mungu.
“ Nina imani dua lako limesikilizwa njia pekee ni kuwa karibu na Bwana.”
Huku nikifuta machozi nilimuuliza babu Utakufalini:
“ Babu hebu nielize kwa nini umeamua kuishi katikati ya pori la kutisha namna hii tena peke yako huku ukiwa na mtoto mdogo, bibi yuko wapi kwani tangu nifike hapa sijaone mtu mwingine tofauti zaidi yetu. Vilevile Kalekwa ni mdogo sana anahitaji malezi ya mama yake.”
“Ndio maana mjukuu wangu nilikueleza awali kuwa kuishi kwingi si kuzeeka bali ni kuona mengi. Mjukuu wangu mimi nilikuwa ni mganga wa jadi miaka sita iliyopita.” “Ina maana kuna wagonjwa huwa wanafika hapa?”
“ Hapana nilikuwa naifanya kazi hiyo huko mjini ambayo ilinipatia kipato kidogo kilichonisaidia kupata mahitaji ya kila siku na familia yangu. Kazi hiyo ya kutibu watu ilinisaidia kujenga nyumba moja ya vyumba vinne ya tofali na mabati na mabanda madogo madogo ya udongo na nyasi.
“Mjukuu wangu kama ujuavyo waganya wa jadii tulivyo na tamaa kila mteja wa kike mzuri unamtaka nilijikuta naoa wanawake watano. Ndani ya miaka minane ya uganga nilikuwa na watoto kumi na tano. Siku hadi siku maisha yalianza kubadilika na kazi ya uganga ikawa ngumu wateja walipungua na maisha yakawa magumu sana na baadhi ya wanawake wakanikimbia kwa njaa nikabaki na wake wawili na watoto kumi na tano.
Kazi ya uganga niliona itaniua njaa ilibidi nitafute njia nyingine ya kupambana na maisha itakayonipatia riziki tofauti na uganga. Mungu alijalia nilipata kazi katika kanisa la palepale mjini, wengi hawakuamini mganga wa jadii aliyekuwa akiabudu mizimu kumrudia Bwana.
Nilipata kazi ya kufanya usafi na kutunza bustani eneo lote la kanisa mimi ndiye nilikuwa msimamizi mkuu. Nilizidi kumshukuru Mungu kipato nilichopata kilipunguza makali ya maisha pia wanangu waliweza kusoma. Hata hali yangu ya maisha ilikuwa nafuu kidogo nilijikuta najilaumu kwa kupoteza muda wangu mwingi kwa kutumikia nguvu za giza zilizopeleka kumuasi Mungu.
“Nilifanya ile kazi kwa miaka mitatu, muda huo niliongeza nyumba nyingine ya matofali na bati, kidogo kitambi kilianza kutoka usiseme mjukuu wangu madaraka matamu nilichaguliwa kuwa mkuu wa walinzi kanisani pale.
“Siku moja nikiwa katika ukaguzi wa bustani nyuma ya jengo la kanisa nilisikia watu wakiongea kwenye dirisha moja lililokuwa wazi nilimsikia mmoja akisema.
” Aisee usifanye kazi funga dirisha,”
Nilijiuliza chumba kile kuna kazi gani mpaka watu kuogopa kuchunguliwa, niliwasikia wakisema: tufanye chapchap ili tufanye kazi nyingine si unajua kuna damu inatakiwa kupakiwa kwa ajili ya safari ya kesho.”
“Umeshaangalia vipimo vya damu yake?” mwingine aliuliza.
“Ipo freshi.”
“Basi fanyeni kazi.”
Maneno yale yalinishitua ilibidi ninyate hadi kwenye dirisha na kuchungulia ndani sikuamini kama pale ni kanisani sehemu ya ibada kuna mambo machafu yanatendeka! Mjukuu wangu nilishuhudia kwa macho yangu mtu akinyonywa damu kwa mitambo inayotumia umeme. Nilijikuta naingiwa na woga nilijipa moyo kuwa ni lazima niujue mwisho wake. Mara taa iliwaka kwenye ile mashine ya kunyonyea damu imemaliza kunyonya.
Nilimsikia mtu akisema:
“Eeeh, bwana kazi tumeshamaliza mwiteni bosi basi.”
Alitoka kijana mmoja kumfuta bosi, mara alirudi na bosi aliyeongozana naye ndiye Pasta anayetusalisha kila siku. Mtu mwenye huruma na upendo kwa watu wote nilizivuta punzi zangu kwa taratibu sana ili zisitoe sauti nimuone Pasta atasemaje.
“ Vipi kazi mmemaliza?’
Wale vijana waliokuwa sita waliitika wote kwa pamoja, machoni ni watu wazuri ambao nawatambua vizuri
“Tayari bosi.” yeye akasema: “Ok, hii damu changanyeni na ile iliyopungua kwa ajili ya kusafirishwa kesho.”
“Sikuamini mjukuu wangu watu niliokuwa nawaona ndio mfano wa kuigwa nami kujifunza tabia zao za upole na ukarimu kumbe ni masubiani wanyonyaji, Ule mwili wa yule mtu ambaye walimnyonya damu ulichukuliwa na kuwekwa kwenye chombo kama droo ya majokofu ya monchwari.
“ Nilisikia akiuliza: “Zile ngozi zimetimia hesabu yake?”
“Ndio bosi tumekamilisha hesabu zake nina imani mzigo wa damu utaondoka na ngozi.” Yule bosi aliwajibu: Ok kazi nzuri, vijana nao walijibu: Asante, nilichokiona kingine mjukuu wangu nilijikuta napiga kelele za mshituko ni pale niliposhuhudia miili ya watu ikichunwa ngozi utafikiri nyama inayo pelekwa buchani, kelele zangu ziliwashitua.
Nilisikia wakishituka na kuuliza: "Nani tena huyo? mara nilisikia: "Mkamateni huyo haraka," Nilijua sasa pale hakuna usalama nilitimua mbio mjukuu wangu japo mwili wangu ulikuwa mkubwa na kitambi nilijikuta naruka ukuta bila ya kutegemea na kuangukia nje ya uzio.
Hivi leo mjukuu wangu ukiniuliza niliwezaje kuruka ukuta siwezi kukujibu, maisha matamu kwa vile nimetambua siri zao lazima wataniua. Hata sielewi hali iliyonikuta siku ile nilisikia haja ndogo ikinitoka na nguvu kuniishia. Namshukuru Mungu walianzia nyumba nyingine mimi nilipata upepo na kutoroka kwa kupitia dirishani. Nilijificha kwenye mti wa jirani nilishuhudia kupitia juu ya mti msako mkubwa ukifanywa uliondelea kila sehemu kwa muda wa takribani robo saa na baada ya kuridhika kuwa sipo waliondoka. Sehemu niliyokuwa nimejificha ilikuwa si rahisi mtu kuniona. Kuna dawa huitumia pale ninipokuwa na matatizo basi hiki kizizi, (huku akinionyesha na kuendelea kunihadithia matatizo yake). Basi mjukuu wangu hiki kizizi unapokuwa na matatizo yenye hatari unakiweka chini ya ulimi mtu hakuoni au anayekutafuta anakata tamaa.
Sikurudi nyumbani upesi nilisubiri kama saa moja hivi ndipo niliporudi, wake zangu na watoto wangu walishangaa na kutaka kujua kulikoni. Niliwasimulia yote niliyoyaona na hawakuamini. Niliwaeleza maisha yangu yapo mashakani ni lazima wataniua ili nisitoe siri na pia najua watanitafuta kwa udi na uvumba wakinishika ni lazima watanichune ngozi au kuninyonya damu.
“Habari zile ziliitia hofu familia yangu ambayo ilinishauri nisilale pale lazima usiku wangekuja kunifuata nilikubaliana nao na kwenda kulala msituni. Mjukuu wangu waliyonifanya Mungu anajua huwezi kuamini kwa kuelezewa tu mpaka ushuhudie mwenyewe.
Asubuhi nilirudi nyumbani ili nijue kuna nini na kupeleka taarifa polisi kwa ajili ya usalama na pia watu wale wakamatwe. Nilichokikuta mjukuu wangu eneo la nyumba zote zilikuwa zimeteketezwa kwa moto familia yangu ya wake zangu na watoto wangu kumi na tano na wajukuu zangu wawili wote walipotelea pale.”
Habari ile zilinishitua na kuufanya mwili wangu kunisisimka huku damu yangu ikichemka na nywele kunisimama. Sauti ya mzee Utakufalini ilibadilika na kuwa ya kilio na majonzi.
"Pole sana babu msiba mzito, unafikiri walifinya vile ili kuhakikisha hata kama nimejificha nifie ndani."
" Baada ya kuona tukio lile babu ulifanya nini? Mmh hapo babu ni lazima uwe mwendawazimu kufa watu 20 kwa wakati mmoja si mchezo lilikuwa ni pigo kubwa tena takatifu sijui kwa nini Mungu amewapa uwezo watu madhalimu kama yale," nilimuuliza huku macho yangu yamejaa macho na moyo kuiuma kama kidonda.

Itaendelea
 
SEHEMU: 15
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
" Baada ya kuona tukio lile babu ulifanya nini? Mmh hapo babu ni lazima uwe mwendawazimu kufa watu 20 kwa wakati mmoja si mchezo lilikuwa ni pigo kubwa tena takatifu sijui kwa nini Mungu amewapa uwezo watu madhalimu kama yale," nilimuuliza huku macho yangu yamejaa macho na moyo kuiuma kama kidonda.
SASA ENDELEA...

"Mjukuu wangu ndio maana waswahili walisema ukishangaa ya Musa utaona ya firauni na si kwamba Mungu amewapa uwezo ili watunyanyase sisi wanyonge bali amewaacha ili siku ya hukumu wayakute maovu yao na malipo yao ni moto wa milele.
"En’he baada ya kushuhudia mauaji yale ambayo kama yangetokea enzi hizo wangeyaita sunami ulifanya nini?" nilimuuliza swali huku nilifuta machozi na kupenga kamasi nyembamba ambazo mara nyingi zilikuwa zikiambatana na machozi.
Kabla ya kujibu alinyanyuka ili akamlaze Kalekwa aliyekuwa amempakata kwa kipindi kirefu tangu tuanze mazungumzo yetu. Baada ya kumlaza ndani alirudi tena ili tuendelee na mazungumzo yetu na baada ya kukaa aliongeza majani makavu kwenye moto na kuongeza mwanga.
"En’he babu lete bahari."
"Mjukuu wangu uchungu nilioupata nilijikuta naangua kilio mzee mzima watu walinizinguka na kunipa pole ambazo zilikuwa kama zimechokonoa kidonda. Mara walitokea askari na kunipeleka kituoni kwa ajili ya mahojiano juu ya vifo vya familia yangu.
“Nilikutana na mkuu wa kituo na kunihoji nawafahamu vipi wauaji wa janga lile. Mjukuu wangu nilimweleza yote niliyoyaona jana yake kanisani na jinsi nilivyotafutwa na asubuhi niliyoyakuta.Walitumwa askari kwenda kufanya uchunguzi huku mimi nikibaki ofisini kusubiri majibu ya uchunguzi wao.
“Nilikaa kama dakika kumi hivi mara mkuu wa lile kanisa Pasta Jonasan aliingia. Alinipita na kuingia ofisini kwa mkuu wa kituo na baada ya dakika mbili walikuja vijana na kunibeba juujuu bila kuelewa nini kinaendelea.
“ Nilitupwa mahabusu bila ya kufahamu kosa langu, nikiwa katikati ya mawazo nilifuatwa na kubebwa juujuu na kuingizwa kwenye chumba kilichokuwa na giza mara taa ziliwashwa na kujikuta nimekalishwa kwenye kiti na mbele yangu kuna meza na kiti kingine.
“Ndani nilikuwa peke yangu mara mlango ulifunguliwa na mkuu wa kituo aliingia na kuniita jina langu:
"Mzee Jacob."
"Jina langu."
"Kwa nini unalidanganya jeshi la polisi?"
"Sikuelewi mkuu."
"Unaidanganya serikali kuwa kanisa lililojitolea kwa ajili ya Mungu ni wauaji, wanyonya damu na pia wachuna ngozi.”
"Sidanganyi nisemayo yana ukweli kabisa na nina ushahidi nayo,” nilisimamia kauli yangu
"Haa..ha..ha,”alicheka kidogo kisha akasema:
"Hivi huo upuuzi wako utamuuingia nani? Ni nani atakubaliana na uzushi wako yaani kanisa na watumishi wake eti ni wauaji pia ni wanyonya damu na kuchuna ngozi," mkuu wa kituo alinigeuka.
"Mkuu hata mimi ninayoongea mbele yako ningehadithiwa na mtu nisingekubali hata ningekuwa radhi kupinga uhai wangu."
"Una maana gani?”
“Watumishi wa kanisa lile wapo sawa na jeneza lililopandwa kwa nje na maua mazuri lakini ndani ni mzoga uliooza tena unaotoa harufu kali."
"Mzee JJ."
"Naam mkuu."
"Kwa nini umeiua familia yako?"
“ Ati unasemaje?” niliuliza swali kama vile sikusikia.
"Nauliza kwa nini umeiua familia yako?"
"Siwezi na hata siku moja nisingeweza kufanya hivyo hata siku moja."
"Mzee JJ acha kujitoa akili narudia tena kwa nini umeiua familia yako?”
"Mkuu huo ni utani kama huna swali bora uniache niende zangu."
“ Ulisikia wapi muuaji anaachiwa huru."
“Nani muuaji?"
“Wewe, sasa naomba unieleze kisa na mkasa uliokufanya uiue familia yako?”
“'Sikujibu niliona sasa huu ni upumbavu na uonevu yaani familia yangu iteketezwe halafu kesi inirudie mimi. Ama kweli asiyekujua siku zote hakuthamini. Sikumjibu nilibaki kimya, kimya kilipozidi aliniuliza.
''Utajibu au hujibu,” mimi nilikaa kimya.
“ Moja ' kimya ' mbili ' kimya aliwaita vijana wake walionipa kipigo kitakatifu eti niseme kwa nini nimeiua familia yangu. Nilijigeuza bubu kila walivyokuwa wakiniuliza nilipata kipigo kitakatifu kilichonitoa damu mdomoni puani na kichwani nilikuwa nimepasuka, damu zilikuwa zinanitoka sana.
Nilichukuliwa na kwenda kutupwa kwenye chumba chenye baridi kali mjukuu wangu usiombe uchungu wa kupoteza familia yangu na bado mbichi kabisa na bado nimepewa mateso mazito. Mateso na vipigo viliendelea kwa siku tatu mfululizo bila kupata majibu wanalotaka.
“Nilirudishwa rumande na kufunguliwa mashtaka ya mauaji, siku ya kwanza mjukuu wangu niliposimamishwa kizimbani sikujibu neno lolote si siri watu wote walikuwa wakinililia kuwa nimeonewa lakini hakuna aliyejali vilio vyao. Mara ya pili sikujibu kitu zaidi ya kusomewa shitaka la kuiteketeza familia yangu kutokana na hali ilivyokuwa inaendelea kwa vile nilikuwa sina wakunitetea zaidi ya wananionea huruma kuwa naonewa.
“Siku moja wakati tunatoka mahakamani katika gari tuliokuwa kumi na mbili, gari letu lilipata ajali iliyosababisha lipinduke na mlango wa nyuma kufunguka. Tuliona kama ndio wokovu wetu. Hapo mjukuu wangu sikulaza damu nilitimua mbio moja kwa moja na baadhi ya wafungwa wengine waliokuwa na majeraha makubwa walishindwa kukimbia.
“Hata mimi nilikuwa na jeraha mguuni sikujua nilikimbia vipi kuingia porini, amini usiamini nilikimbia kwa wiki nzima usiku na mchana hadi kwenye pori hili nilikuwa nina imani kama wangenitafuta kwangu watachemsha, Katika pori hili nilifika nilikuta hakuna kitu chochote ndipo nilipoanzisha maskani yangu mpaka leo hii naishi peke yangu huu ni mwaka wa nane nipo huku."
Zilikuwa habari nzito zilizonifanya mwili wangu uingie baridi na kugundua pesa siku zote zinapindisha haki na kuwa batili nilimsongelea babu Utakufalini nilimshika mgongoni nakumpigapiga kidogo wakati huo alionyesha ni mtu mwenye majonzi sana. "Pole babu nina imani Mungu kayaona yote haki ya mtu haipotei lazima itapatikana na ukweli utajulikana."
" Ni vigumu, wenye pesa wamehodhi sehemu zote ambazo wanyonge tunapokimbilia."
"Hata pesa izibe vipi ipo siku amini mwanya utaonekana, sasa hebu ona jinsi ulivyofanyiwa halafu usilipize kisasi?”
“Katu sitalipiza Mungu atanilipia."
“Kauli hizo ndizo zinazowapa vichwa wazidi kutukandamiza, babu umenieleza mengi juu ya maisha yako inavyoonekana umekuja peke yako vilevile katika maongezi yako yote sikusikia taarifa za mama wa mtoto huyu?"
"Mjukuu wangu kama nilivyolibatiza jina hili pori kuwa la mauti, Siku moja narudi kutoka shambani kwangu, nilipopita sehemu moja nilishangaa kuona kitoto kidogo kikimnyonya mama yake ambaye ulalaji wake ulinitia mashaka. Nilisogea hadi pale wakati huo kitoto kiliendelea kumnyonya mama yake.
“Hali ya yule mama ilinishtua haikuwa ya uzima, kweli nilipomsogelea karibu niligundua yule mama niseme ni msichana alikuwa amefariki. Nilijiuliza amefikaje pale na yupo na nani nililichunguza eneo lile kwa muda lakini sikuona mtu yeyote. Niliamua kumchimbia kaburi na kumzika na kumchukua huyu mtoto na kuja nae hapa kwangu.
“Japo mwanzo ilikuwa vigumu kuishi naye, kama ujuavyo mtoto mchanga aliyezoea kunyonya kwa mama yake. Lakini kuna mti mmoja ambao ukiuchemsha maji yake hayawi tofauti na maziwa ya mama yake.
“Si rahisi mara moja kuyazoea ilimchukua wiki mbili mpaka kuyazoea. Ndipo nilipoanza maisha mapya kwenye pori hili la kutisha lenye wanyama wakali na lenye vibweka kama roho yako ni nyepesi unaweza kukimbia.
“Kuna siku wakati natoka shamba niliona viungo vya binadamu kila ninavyokwenda ndivyo nakiona kimoja kimoja. Mwanzo niliokota mguu wa kushoto, mbele nikaokota mguu wa kulia mbele kidogo kichwa nusura nikimbie lakini nilijipa moyo kwani bora nifie huku kuliko kuchunwa ngozi. Mara ya mwisho kabisa niliokota kiwiliwili, kama kawaida yangu nilivizika.”
“Yaani nashngaa ina maana serikali hawajui haya?" niliuliza huku nimeshikilia kifuani.
"Basi mjukuu hii ndio historia ya maisha yangu na Kalekwa."
"Jina la Kalekwa ulilitoa wapi wakati ulikuta mama yake ameshakufa?"
"Ndio maana nikamuita kalekwa yaani kaachwa nina imani alikuja bila kitu."
“Siku zote Mungu humpa unafuu kiumbe wake, katikati ya pori hili nilikuta mabaki ya ndege yaliyoanguka zamani kutokana na hali yake nina imani waliyaacha."
“Sasa babu nazidi kukuhaidi utaishi maisha mazuri nusu ya peponi."
"Nitashukuru mjukuu wangu na nimechoka kuishi maisha ya porini kama mnyama sina wa kuongea naye zaidi ya mjukuu wangu Kalekwa na wanyama wakali yaani nikitoka nje kidogo najiona kama binadamu kamili ninayeweza kuongea na binadamu wenzangu.”
"Babu poza moyo naona usiyahesabu kuwa ni matatizo muda si mrefu yatafika ukingoni, “nilimuyajidi babu maisha mazuri baada ya kurudi mjini,
"Nitashukuru mjukuu wangu nakuombea kwa Mungu upone kwa haraka."
Kwa vile usiku ulikuwa mkubwa tuliingi kulala. Siku zilivyozidi kwenda ndivyo hali yangu ilivyozidi kuwa kuimalika. Babu Utakufalini aliporidhika na hali yangu alinipangia siku ya kuondoka. Nilikubaliana na babu niondoke peke yangu ili kama nikirudi nirudi na gari kuwachukua wote. Yaani kwa muda ule sikujua nimekaa porini kwa muda gani.
Usiombe yaani lile pori kweli ndio maana mzee Utakufalini alijibatiza jina Atamjua nani, kweli unaweza kuzaliwa pori lile ukazeekea kule na watu huwajui wala kuonana na mtu zaidi ya wanyama na ndege.
Unaambiwa kutoka pale porini hadi kuishika barabara ni mwendo wasaa 36 na ukiwa legelege siku tatu hadi kufika barabarani. Siku niliyopanga na babu Utakufalini ilipowadia . Niliamka alfajiri kwenda kumuaga , ili nianze safari ya alfajiri nilipanga lazima nifike barabarani jioni ya siku ya pili.
Nilipokwenda chumba cha babu Utakufalini nilimsikia akikoroma tena mkoromo mzito. Ile hali sikuwahi kumuona nayo kipindi chote nilichokuwepo pale. Nilizidi kumwita lakini sikupata jibu lolote zaidi ya mkoromo kuendelea. Niliamua kuingia chumbani kwake nilimkuta macho yamemtoka pima.
Ile hali ilinitisha wakati huo Kalekwa naye alikuwa ameamka, nilimtenga akajisaidia kisha nikarudi kwa babu utakufalini. Hali yake ilinisikitisha kwa vile na mimi nianza kuwa mjuzi wa miti shamba, mara moja nilikoka dawa yaliyoweka moshi mwigi baada ya dakika tano babu Utakufalini alitoka jasho jingi kidogo hali yake ikawa afadhali.
Ilibidi nivunje safari ili nimhudumie babu na Kalekwa.
Pamoja na babu kupata nafuu lakini alikuwa hawezi kazi kwa kipindi kile. Ilinibidi shughuli zote nizifanye mimi. Suala la safari nililisitisha kwa muda , mtoto wa kike nikavaa rasmi kazi ya babu Utakufalini.
Ikawa asubuhi naingia kutafuta kuni na kushughulikia kilimo kilichoachwa na babu. Nilijikuta namaliza miezi mitatu bila kutegemea. Siku moja niliporudi shamba nilikuta mwili wa mtu aliyekufa. Nilikimbia mbio hadi nyumbani babu alishangaa na kuniuliza kulikoni nilimuelezea nilivyoona.

ITAENDELEA
 
SEHEMU: 16
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DrAmbe’
SIMU: 0713 646500
ILIPOISHIA:
Ikawa asubuhi naingia kutafuta kuni na kushughulikia kilimo kilichoachwa na babu. Nilijikuta namaliza miezi mitatu bila kutegemea. Siku moja niliporudi shamba nilikuta mwili wa mtu aliyekufa. Nilikimbia mbio hadi nyumbani babu alishangaa na kuniuliza kulikoni nilimuelezea nilivyoona.
SASA ENDELEA...

“Basi mjukuu wangu hayo ya kawaida la muhimu uufukie ule mwili .“
“Hapana babu wanaweza kuniua.”
“Kama kufa ningekufa mimi huu ni mwaka wa nne nipo huku na nishazika watu si chini ya mia mbili rudi ukazike mjukuu wangu.”
“ Hapana babu sirudi,” nilikataa.
“Usiogope kumbuka usipouzika utajiletea matatizo.“
“Matatizo! Matatizo gani?”
“Ule mwili ukioza patakuwa hapakaliki harufu ya mwanadamu ni kali sana.“
Nilijipa moyo nikarudi kuuzika mwili wa yule mtu alikuwa msichana, nilishangaa alikuwa amevaa hereni na mkufu wa bei mbaya nilijiuliza ina maana waliomuua shida yao ilikuwa ni nini? Nilichimba na kuufukia ule mwili .
Tangu hapo nikaanza kuwa na moyo wa ujasiri nilishangaa woga ulinitoka hata nilipokuta mwili mwingine niliufukia bila hofu yoyote. Siku moja nilirudi kutoka kwenye kilimo chetu, tena siku hiyo nilikuwa nimekamata kware nilijua babu Utakufalini atafurahia na kuona nimeanza kumrithi katika uwindaji.
Nilimkuta Kalekwa analia babu alikuwa amelala tu, si kawaida yake kumuacha Kalekwa alie kiasi kile. Nilipofika nilimnyanyua na kumbembeleza, baada ya kunyamaza nilimfuata babu Utakufalin. Nilishangaa kumkuta amelala wakati mjukuu wake alikuwa analia. Nilimuamsha alifumbua macho lakini macho yake yalikuwa mazito.
“Babu vipi?”
“Ha…a…a…a….apa..na,” aliongea kwa shida .
“Babu nimerudi, tena leo nimekuletea kitoweo.“
“Thereza,“ babu aliniita kwa sauti ya chini.
“Abee babu,” niliitaka huku nilimuinamia ili nimsikilize vizuri.
“Mtu …nze..Ka..le..kwa.”
“Ba..bu..vipi?”
Babu alinyoosha mkono aliokuwa ameukunja ngumi na kunipa kitu nilipokea hakikuwa kingine zaidi ya kile alichonionyesha na matumizi yake. Nilipokipokea tu swali la jina jina lake kuwa atakufa lini ilitimia, baada ya kupokea kile kizizi babu alikata roho.
Nilishindwa kulia japo roho iliniuma ,yaani dhamira yangu ya kulipa fadhila iliyeyuka kama donge la mafuta kwenye kikaango cha moto. Nilitamani kulia lakini nilijikaza, najua udhaifu ninapolia hasa msiba uwe unanihusu. Kwa kiasi gani babu Utakufalini alivyookoa maisha yangu nilijua kilio changu cha kawaida lazima nitapoteza fahamu kitu kitakachomfanya Kalekwa apate shida.
Nilijikaza kiume na kuchimba kaburi kisha niliuzika mwili wa shujaa wangu mzee Jacob au maarufu kama Utakufalini mtu aliyekufa kifo kama mnyama kutokana na roho mbaya za watu wanaoonekana nje kondoo lakini ndani ni wanyama wakali kushinda mbwa mwitu.
Niliuzika mwili wa mtu muhimu maishani mwangu, roho iliniuma lakini ndio hivyo Mungu amemuita. Mimi nilimpenda lakini yeye alimpenda zaidi. Baada ya mazishi siku ya pili alfajiri nilianza safari kurudi mjini njia ya pori na pori kutafuta barabara. Ungeniangalia ungesema labda ni mzuka jinsi nilivyokuwa na Kalekwa, tulikuwa na nywele ndefu utafikiri mizimu iliyofufuka, miili yetu ilikuwa imepauka na vumbi jingi. Nguo zetu chafu na zilizochanika zilituweka nusu uchi, nilianza safari ambayo kidogo ilikuwa ngumu.
Nilimbeba Kalekwa mgongoni kuanza safari nisiyojua naelekea wapi. Pori lilikuwa linatisha niliweza kupishana na wanyama wakali kama Simba, Chui, Tembo hata Vifaru. Kizizi nilichopewa na babu ndicho kilichonisaidia kusafiri salama, nilisafiri saa kumi na mbili nilipumzika na mdogo wangu Kalekwa kupata chakula na kujilaza hadi siku ya pili.
Siku iliyofuata alfajiri niliianza safari yangu, nilitembea kwa muda wa siku tatu hadi kukutana na barabara kuu ya magari. Tulipokuwa tunakaribia barabarani nilisikia watu wakiongea.
" Eeeh bwana jisaidie haraka tunataka Dar tufike saa nne usiku."
Nilibadili njia na kutokea upande mwingine lakini si mbali nao, mbele nilikuta lori la mizigo. Nilimshukuru Mungu kimoyomoyo nilitaka kuwaomba lakini hali yetu kama mizimu iliyofufuka nani angetukubalia au wangetaka kutuhoji na kutufikisha polisi niliona mambo yanaweza kuwa kama ya mzee Utakufalini afanyiwe ukatili ategemee polisi wamsaidie ndio kwanza wanamkandamiza na kumbambikia kesi nzito ya mauaji.
Niliamua kutumia ukomandoo wangu kama ndani ya sinema, nilinyata taratibu na kuwazunguka na kwenda kupanda nyuma kwenye mizigo. Muda si mrefu safari ilianza. Nilimuomba Mungu anifikishe salama. Dua yangu ilisikiliozwa tulisafiri bila tatizo gari liliingia Dar saa 4.30 usiku.
Kama kawaida yangu niliruka kwenye gari lilipokuwa limesimama taa za barabarani za maeneo ya Ubungo. Nilianza safari ya kuelekea kwangu, nilifika kwangu majira ya saa kumi alfajiri. Niligonga geti mlinzi alihoji kabla ya kufungua, nilimweleza ni mimi. Alipofungua alishangaa hali niliyokuwa nayo kwanza alinikatalia katakata kuwa si mimi. Baada ya kumuelewesha aliniruhusu kuingia ndani.
Alitaka kujua nini kilichomsibu hadi kuwa kwenye hali ile nilimweleza aniache nipumzike kwanza. Niliingia hadi ndani cha kwanza niliyesimama mbele ya kioo nilikuwa sina tofauti na mabush man. Kabla ya yote nilijipiga picha mimi na Kalekwa ili niweke kumbukumbu kwenye maisha yangu.
Nimekubali maneno ya babu Utakufalini kuwa tembea uone na kuishi kwingi kuona mengi. Baada ya kupiga picha kadhaa za ukumbusho ambazo ni hizi,” Malaika Mweusi alivuta droo na kutoa bahasha ambayo alimpa Anderson ambaye alizitazama na jinsi walivyokuwa kama wanyama.
Baada ya kuzitazama kwa muda alimrudishia bila kusema neno, Malaika Mweusi akaendelea:
“ Basi niliingia bafuni kuoga na kumwosha Kalekwa kisha tulijitupa kitandani na usingizi mzigo ulitupitia. Kutokana na uchovu niliamka siku ya pili saa kumi jioni kwa msaada wa Kalekwa aliyehi kuamka. Niliamka mwili ukiwa umechoka na njaa ilikuwa unauma kama kidonda, nilipiga simu Shoprite watuletee chakula.
Vilevile niligundua akili ya Kalekwa ilikuwa ya kiporipori kama angeendelea kuishi porini angekuwa kama mnyama. Kila kitu kilikuwa kigeni wakati huo alikuwa na miaka miwili. Umri wa Kalekwa ulinijulisha kumbe nilikaa kule porini kwa miaka miwili.
Baada ya kujirudisha hali ya ubinadamu, Sikutaka kupoteza muda lilikwenda moja kwa moja kwa Doctor Ray. Aliponiona hakuamini alinikumbatia kwa furaha. Hakuficha furaha yake na kuniuliza.
"Ulipotelea wapi Mr embo afadhali umeonekana kuna kazi inawaumiza akili watu, nina imani ufumbuzi ni wewe kama utaifanya vizuri malipo yake nina imani ni makubwa si chini ya bilioni moja."
"Kazi gani hiyo yenye pesa nyingi hivyo?”
Habari hizi zilinishtua ni kazi gani tena hivyo yenye malipo mazito pesa ambazo sikuwaza kuzipata maishani bilioni mia moja, mmh hapana ni kazi gani hii ambayo imesababisha moyo upasuke kwa mshtuko.
"Ray ni kazi gani hiyo yenye malipo kama hayo ambayo naona kama ndoto, au umekosea kusema?" nilishtuka.
"Hapana Thereza malipo ya kazi ni bilioni 100 kama utakubali advance shilingi bilioni 60 pale utakapo kuwa tayari kuifanya."
"Mmh! Mbona unanitisha ni kazi gani?"
"Utaelewa tu, vipi ulisafiri?"
“We acha niliyonikuta Mungu anajua nahitaji msaada wako mwingine,” nilimwambia Dokta Ray.
"Unashinda gani? Sema tu nipo tayari kukusaidia kwa hali na mali."
"Twende ofisini kwako," niliongozana na Dokta Ray japo yeye anapenda nimwite Mr Ray hadi ofisini mwake.
Nikiwa ofisini mwake aliniletea glasi iliyo jaa whisky ilikuwa miaka miwili imepita bila kutumia kilevi chochote. Sikuwa na haja tena ya kuendelea kunywa pombe kali.
Nilijua ule ndio wakati muafaka wa kuacha pombe kali ikiwezekana kuacha kabisa unywaji wa pombe. Nilimtaka radhi Mr Ray.
"Samahani Mr Ray situmii pombe."
"Hata bia?"
"Pombe ya aina yoyote."
“Ooh! Sasa itakuwaje na kwenye friji yangu kuna maji tu."
"Maji yanatosha sana," alinijazia maji kwenye glasi baada ya kukaa na kuitengeneza sauti yake alisema:
"Ehe...Thereza kwanza habari za siku?"
"Mbaya."
"Mbaya! Una maana gani?"
"Ndio maana nimerudi tena kwako.”
“Nina imani unakumbuka vizuri sababu iliyonileta hapa mara ya kwanza?"
"Ndio nakumbuka vizuri, kama sikosei ni tukio la kubakwa."
"Sawasawa kabisa."
"Vipi umebakwa tena?"
"Bora ningebakwa nikajua moja.”
“Sasa umepata masahibu gani?”
Nilianza kumwelezea kisa chote kilichonitokea mwanzo hadi siku ile nipokuwa mbele yake kama golikipa aliye okoa penati za Ziraili.
Habari zile zilinisisimua Dl Ray mpaka rangi yake nyeupe kuwa nyekundu. Aliniangalia mara mbili mbili kisha alishusha pumzi na kusema:
“Pole sana Thereza, wewe ni mwanamkae wa shoka, nina imani kwa hatua zote ulizopitia hautasita kuifanya kazi yetu.”
"Dk Ray niweke wazi ni kazi gani? Mbona moyo wangu unalipuka."
"Kwanza kabla sijakueleza ni kazi gani la muhimu kuishughulikia afya yako."
Niliongozana na Dk Ray hadi chumba cha uchunguzi na kuyachunguza makovu yangu sehemu za siri yaliyoniweka kwenye shepu mbaya.
Baada ya uchunguzi tulirudi ofisini kwake, aliniacha kidogo na kuingia kwenye chumba kimoja. Baada ya dakika kama tano alirudi na bahasha kubwa kidogo pamoja na kitabu kikubwa na kuviweka mezani.
Alinieleza nizunguke upande wake, baada ya kufanya hivyo alinifungulia kile kitabu kilichokuwa na picha za watu wenye majeraha na makovu ya kutisha na picha zingine wale watu wakiwa wamepona.
Kisha alinitolea picha za kawaida na kunionyesha watu waliopata matibabu kwenye hospitali yake walioungua moto lakini baada ya matibabu ya ngozi zao hurudi kwenye hali ya kawaida.
Vilevile watu wenye makovu ya kutisha waliofanyiwa upasuaji pale na hali zao zilivyo kuwa nzuri, huwezi kuamini kama hapo awali alikuwa na jeraha au kovu.
"Sasa Ther eza kazi yako ni ndogo nitaifanya kwa wiki tatu utakuwa mzima kabisa, kwa maelezo yako yule mzee aliyeokoa maisha yako dawa zake zilifanya kazi kubwa bila hivyo lazima ungekufa au kuoza kizazi mpaka utumbo kazi yangu ni upasuaji mdogo kuna dawa za kuponyesha kidonda kwa wiki kunakuwa kumepona vilevile kuna dawa za sindano zinazo kausha kidonda kabla ya kupakwa dawa juu ya kidonda ambayo hugeuka ngozi, ninajua utashangaa jinsi utakavyopona."
"Nitashukuru sana, sijui gharama zake ni shilingi ngapi?”
"Hapana sihitaji pesa yako zaidi ya kunikubalia kuifanya hiyo kazi."
"Usiwe na wasiwasi sitakuangusha kwa vile wewe ni mtu muhimu sana kwangu nina imani nitaifanya hiyo kazi bila pingamizi," nilijikuta nakubali bila kujua ni kazi gani.
"Waawoo Thereza katika siku uliyonifurahisha ni leo na mimi nakuahidi kukupa ushirikiano wa kutosha," Dk Ray alifurahi sana bila kujua sababu ya furaha yake na kazi anayotaka kunipa.
"Nitashukuru."
"Sasa sijui matibabu tutaanza lini?"
"Nilipendelea hata leo lakini kwa vile nina mdogo wangu ambaye hajuani na mtu yeyote lazima nimtengenezee mazingira mazuri kesho kutwa nitarudi kwa ajili ya matibabu.
Niliamua kuagana na Dk Ray ili nizungukie miradi yangu kujua maendeleo yake baada ya kutoweka kwa miaka miwili na ushee si mchezo unaweza kukuta mabadiliko makubwa.
Kabla ya kuagana Dk Ray alinieleza nisubiri kidogo alinyanyua simu moja, machoni kwangu ndio mara yangu ya kwanza kuiona. Ipo kama radio call, lakini ni ndogo sawa na simu za kawaida.
"Haloo mkuu yule mtu ameonekana.”
“Nani huyo?” kwa vile ilikuwa sauti inayosikika nilisikia maongezi yao.
“Thereza."
“Thereza ndio nani?"
"Yule msichana wa kazi ya PT."
"Ooh. samahani si unajua mambo mengi vipi amekubali?”
"Ndio amekubali.”
"Vizuri sana yupo tayari kuianza kazi?"
"Ndio nimekutana naye, vilevile ana matatizo anahitaji msaada wetu japo yeye mwenyewe yupo tayari kujilipia."
"Vizuri, anatatizo gani?"
Dk Ray alimweleza mtu wa upande wa pili tatizo langu.
“Ooh, siyo tatizo hakikisha anapata matibabu ya hali ya juu ya yatayomponyesha vizuri, nina imani unaelewa umuhimu wake?”
"Ndiyo bosi."
“Sasa, kwanza hata sijui niseme nini yaani kupatikana kwa binti huyo kumenipa matuini ya ajabu najishangaa hata furaha imemjaa ghafla nina imani binti ataifanikisha vizuri na mhakikishia akiifanya vizuri nitamuongezea bilioni 30 kama asante, matibabu anaanza lini?"
"Kesho kutwa bosi."
"Vizuri mpe shilingi 150 ili zimsaidie kipindi cha matibabu yake."
“Sawa bosi."
“Hakikisha vitu muhimu vinakuwa tayari ili amalizapo matibabu aanze kazi mara moja.''
“Hamna tatizo bosi."
“Ok bai kazi njema."
Baada ya maongezi Dk Ray alishusha pumzi nzito kisha alisema:
"Thereza subiri," aliingia tena kwenye kile chumba na kurudi na mfuko mkononi aliuweka juu ya meza na kuufungua.
Ulikuwa na maburungutu ya pesa zilizokuwa zimefungwa mafungu matano.
"Hizi ni milioni 150 unaweza kuzihesabu."
"Za nini zote hizi?"
“Nina imani miaka miwili uliyoipoteza umepoteza na kipato chako hivyo zitakusaidia wakati wa matibabu."
"Sawa, lakini ni nyingi sana wakati kazi yenyewe bado sijaifanya," pesa zile zilinitisha.”
"Sawa, wacha nikapumzike ili nihakikishe namtengenezea mdogo wangu mazingira mazuri kipindi chote nikiwa katika matibabu yangu," nilisema huku nikizirudisha zile pesa kwenye mfuko ili niondoke zangu.
“Zihesabu ili uzihakikishe.”
“Sina wasi wasi nawe nakuamini," niliubeba mzigo wangu na kuagana na Dk Ray.
Nikiwa narudi Dar nilijawa na mawazo mengi juu ya kazi nitayopewa, nilijiuliza ni kazi gani hiyo ambayo wanamwaga mamilion hata bila wasiwasi wowote.
Niliamua kuachana na mawazo juu ya kazi hiyo kwani kuwaza sana niliona ni kuiumiza akili yangu kwa kitu nisicho kijua.
Niliamua kuachana na kazi ya kuiwaza kazi hiyo ili kusubiri mpaka hapo nitapo elezwa ni kazi gani. Lakini ajabu kila nilipoiwaza kazi hiyo moyo ulinilipuka na kujawa na hofu moyoni. Lilibakia swali kichwani juu ya kazi ninayotaka kupewa.
Malipo billioni 100 advance bilioni 60 pesa za matumizi nje ya malipo milioni150.
Kwa upande mwingine nilijilaumu kukubali bila kuijua, nilijiuliza kama nikiikataa je itakuwaje. Wasiwasi wangu ulikuwa katika kukosa matibabu ambayo yalikuwa muhimu kwangu kuliko kitu chochote.
Nilijiuliza kwa nini niendelee kuumiza akili yangu na kuisubiri kazi hiyo watakayonipa. Wakati huo nilikuwa naaingia kwenye geti la moja ya makampuni yangu.
Siku hiyo nilizungurukia miradi yangu yote , nilimshukuru Mungu kukuta maendeleo vizuri vilevile niliwatembelea washirika wenzangu niliokuwa nao wakati wa uchokoraa.
Nao waliendelea vizuri waliponiona walifurahi sana kuniona nami vilevile nilifurahi. Siyo siri kila ninapowaona washirika wenzangu nlikumbuka mengi kweli maisha yanabadilika.
Tabu za kushinda juani ndizo zinazo niumiza roho sikuwa tayari kuona ombaomba au watoto wanaozurura mitaani. Nazidi kumshukuru Mungu hali ilikuwa inaridhisha japo ripoti ya mikoani ilinifanya niongeze vituo vingi vya watoto.
Nilipanga pesa nitayoipata kwa ajili ya kazi ambayo siijui robo ya pesa hizo ambazo ni bilioni 25 billioni 10 kuongeza vituo na shule pamoja na billioni 15 kujenga kiwanda kitachoongeza ajira kwa vijana.
Baada ya ziara yangu iliyoonyesha mafanikio makubwa pamoja na ongezeko la misaada ya wahisani iliyofikia dola millioni moja. Nilimkabidhisha Kalekwa kwa mlezi ambaye atamlea kipindi chote nitakuwa katika matibabu.
Matibabu yangu yalikwenda vizuri, ndani ya wiki tatu nilikuwa mzima wa afya njema kabisa sikuwa na kovu lolote mwilini kwangu. Kweli nimeamini dawa zipo.
Baada ya matibabu na mapumziko ya wiki mbili zingine, niliitwa ofisini kwa Dk Ray ambaye alinijulisha kuwa nijiandae safari ambayo ingekuwa baada ya wiki.
Ilikuwa kwa ajili ya mazoezi ya mwaka mzima kabla ya kuianza kazi ambayo ilihitaji mafunzo ya hali ya juu.
Nilikabidhiwa milioni 500 kwa ajili ya kuacha nyumbani kama kuna mtu anamtegemea. Sio siri kila muda na dakika nilijiuliza ni kazi gani yenye mafunzo ya mwaka mzima.
Baada ya kurekebisha mambo yangu niliwasili Kibaha kwa ajili ya safari ya mwaka mzima nisiyo jua na kwenda wapi. Majira ya saa moja usiku nilipakiwa ndani ya gari aina ya Toyota Land Cruser V8 na safari ilianza. Ilikuwa safari ya kurudi Dar.
Lakini kabla ya kuingia Dar nilifungwa kitambaa usoni nilipouliza niliambiwa ni mwanzo wa mazoezi. Nilipandishwa ndege nikiwa nimefungwa kitambaa usoni. Ndani ya Ndege wakati ikiwa angani nilifunguliwa kitambaa usoni.
Ndani ya ndege kulikuwa na watu zaidi ya hamsini kila mmoja alikuwa kimya.
Tulisafiri kwa muda wa siku mbili. Siku ya pili ndege ilitua ilikuwa ni usiku wa manane, tuliteremka sikujua ule ni mji gani hata nilipo wauliza wenzangu nao walisema hawajui lakini ni moja ya nchi za Ulaya.

Itaendelea
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…