The Story Vault
Member
- Apr 12, 2025
- 31
- 60
Hadithi: MAJARIBU
Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)
UTANGULIZI: Ni hadithi inayomzungumzia kijana mdogo wa kuitwa majaribu. Wakati akijaribu kuyakimbia matatizo yake akakutana na majaribu menyewe Sasa Alijikuta akikabiliwa na kesi ya mauaji ambayo hakuyafanya ilipelekea kupelekwa gerezani je kijana Huyu atafanyaje ili kuthibitisha hana hatia. Ongozana nani Katika kigongo hili mwanzo mwisho. Mtunzi wa Hadithi hii anaitwa Mwaki Ze Done wasiliana naye Kwa whatsapp yake Kwa namba hizo hapo juu.
Sehemu: 1
Ni Majira Ya Usiku kwenye Moja ya Jengo la kifahari katikati ya Jiji ambalo lilikuwa limechangamka Haswa, kwenye Moja ya chumba ndani ya Jengo Hilo alionekana mdada wa Miaka kama 17 akiwa anaperuzi mtandao wa FB huku akiwa anakenua Meno Kwa furaha, Bila Shaka kile ambacho alikuwa anakifuatilia kilimfurahisha Sana.
Ila Mida hiyo ya Saa Saba za usiku akiwa bado kazama kwenye Mitandao kiasi kwamba usingizi uliogopa hata kumnyemelea Mara gafla Dada huyo alianza kusikia kukuru kakara upande wa pili ndani ya nyumba hiyo hiyo!.
Dada huyo taratibu aliweka Simu yake kitandani na kutoka kule chumbani ili kuona nini kinaendelea!.
Kwanza alienda mpaka sebuleni na kutulia ili kusikilizia zile kukuru kakara alizo zisikia ni wapi zimetokea.
"Msaadaaaa!! Nisaidieni......uuuuu!!!.." Dada Yule akiwa pale sebuleni alisikia Sauti Kwa mbaali ya mwanaume akiwa anaomba msaada! Haraka haraka Dada yule alipanda ngazi mpaka gorofa ya juu ambako Sauti hizo zilikuwa zinatokea! Kwa mwendo wa taratibu na umakini mkubwa Dada yule alisogea mpaka kwenye mlango ambao ulioneka upo wazi!.
"Mungu Wangu....!!" Dada Yule Kwa kile alicho kiona alijikuta anaropoka Kwa Sauti ya Chini huku akiwa anajiziba mdomo, Mapigo ya Moyo yalionekana kwenda Sipidi Muno Mwili mzima wa Dada Yule ulikuwa unatetemeka Kwa kile alicho kiona, Haraka haraka alitoka pale mlangoni na kukimbilia chumbani kwake!.
Dada Yule alianza kukusanya vitu vyake kule chumbani Kwa ajili ya kuondoka huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanamuenda sipidi, ila baada ya kukusanya na kufunga begi lake vyema, baada ya kufika mlangoni ni kama kuna akili ilimjia kwamba usiondoke!.
"Uuuuu!! Nikikimbia Hii kesi si itakuwa Yangu hii! Siendi kokote!" Dada yule alijiongelesha mwenyewe, baada ya kuwaza na kuwazua aliamua kurudi kitandani na kukaa!.
Simu Ya Dada huyo ilikuwa haishikiki tena yaani Moja ilikuwa haikai Mbili haikai Jasho tu ndo lilikuwa linamtoka Japo ilikuwa usiku.
Dada huyo akiwa katulia chumbani alisikia vishindo vya watu walionekana Sasa wanashuka ngazi kutokea gorofa ya juu! Dada yule ambaye bado hatujamjua ni nani, akiwa na Moyo wa kijasiri aliamua kutoka kule chumbani kwake taratibu na kwenda kuchungulia.
Dada Yule aliona Njemba kama Nne zikiwa zimebeba furushi zinatoka kule chumbani huku nyuma yao kukiwa na Mama Mtu mzima Miaka kama arobaini na kitu akiwa anafuata nyuma tena Kwa ujasiri!.
"Heeeee!! Mbona maajabu jamani! Wamefanana au ni Yeye!?? Mama Mchungaji si yupo India!?? aaaaaa hii haiwezekani!??" Dada yule baada ya kuona hali ile alijiuliza maswali ambayo hayana Majibu Huku akiwa anachungulia na Mwili mzima ukiwa unamtetemeka!.
Usiku huo huo kwenye Moja ya kijiji ambacho kilikuwa hakipo mbali Sana na Jiji lile ilikuwa ni kama mwendo wa masaa matatu na Kitu Hivi ukiwa na usafiri kutokea Mjini mpaka kwenye Kijiji hicho.
Ndani ya kijiji hicho Walionekana wanakijiji wakiwa wamechafukwa Haswa Usiku huo wa manane kwenye Moja ya nyumba ya nyasi ambayo alikuwa anaishi Bibi wa Miaka kama 70 na mjukuu wake wa kiume Miaka kama 16, wakiwa wamelala usiku huo Mara walisikia makelele ya wanakijiji wakiwa wanaonekana wanakuja pale nyumbani.
"Tumechoka!! Tumechoka!! Tumechoka!!" Hizo zilikuwa nyimbo za Mizuka kutoka Kwa wanakijiji, yaani nyimbo hizo zilifanya hata wale Ambao walikuwa wamelala usingizi wa pono waamuke na kwenda kuungana na wenzao katika kutimiza Jambo lao!.
Umati ule wa wanakijiji walifika mpaka kwenye nyumba ile ya nyasi ambayo alikuwa anaishi Bibi huyo kikongwe na mjukuu Wake!.
"Bibi Zoha Tumechoka! Tumekuchoka wewe na mjukuu wako! Wizi nyie! Uchawi nyiee! Kwa usalama wenu kabla hatujachoma hiki kinyumba chenu tokeni nje!" Basi umati ule baada ya kufika nyumbani Kwa Bibi yule kuna Jamaa aliongea Kwa mizuka na kweli watu waliripuka Kwa shangwe.
Upande wa ndani Bibi Yule na mjukuu wake walikuwa wanatazama huku wakiwa Hawaelewi kipi ni kipi!.
"Majaribu Hivi umeiba tena!? We mtoto upoje Lakini!?" Huku ndani Yule Bibi alianza kumlaumu mjukuu wake huku Moyo ukiwa unaenda mbio!.
"Bibi Mimi nimeiba Saa ngapi wakati tupo wote Muda wote, isitoshe hao wanasema uchawi siyo Wizi! Bibi wewe ni Mchawi na ndo wamekufuata!" Basi kijana yule naye akiwa na uoga alimjibu Bibi yake!.
"Majaribu acha ujuaji, sikiliza hapa hakuna usalama ebu tokea dirishani kimbia tena kimbia uende mbali, hata ukisikia nimekufa usirudi Hapa!" Bibi Yule akiwa anajiandaa kwenda kufungua mlango alimjibu mjukuu wake, lakini Kabla hata hajanyanyuka kwenda mlangoni Mara walianza kusikia mlango ukivunjwa Kwa kutumia vitu Vizito maana wanakijiji walikuwa wamevurugwa mpaka Siyo vizuri.
"Au kama Vipi tuchome nyumba mbona watatoka wenyewe!" Basi kuna jamaa aliongea Kwa mizuka na kufanya watu waanze Sasa kutafuta kiberiti, wale wa Karibu na pale Kwa Jinsi walivyo kuwa na Roho ngumu waliamua kufuata viberiti majumbani kwao!.
Huku ndani kijana wa kuitwa Majaribu baada ya kuona Sasa Maji yamezidi unga aliamua kuchomokea dirishani, Japo kuwa dirisha lilikuwa dogo ila alijilazimisha na alitosha na ilionekana ni mzoefu wa kupita Madirishani.
Baadhi ya Watu walimuona kijana Huyo akiwa anakimbia na waliamua kumuungia Kwa kumfukuza maana huyo ndo walikuwa na Shida naye zaidi kuliko hata Bibi yake!.
Kijana majaribu pamoja na umri wake alikuwa ni mwizi haijawahi kutokea, yaani alikuwa ni kama kasomea shahada ya Wizi, na tangia aanze kuiba alikuwa hajawahi kukamatwa, yaani Watu walikuwa hawambahatishi kwenye matukio Japo kuwa walikuwa wanajua ni Mwizi!.
Bahati mbaya Siku hiyo pale Kijijini kuna Mtu alikuwa kaibiwa mifugo yake Yote na baada ya wanakijiji kuamushana Usiku waliamua Sasa kuelekea nyumbani Kwa Bibi yake na Majaribu wakiwa na uhakika kwamba huwenda kijana huyo ndo mhusika kuhusu mifugo hiyo kupotea.
(Kwakuwa kijana Majaribu ndo mhusika mkuu bado kuna mengi tutayajua kumhusu mpaka Yeye kuwa kwenye mazingira yale Je ni ipi Historia Yake!? Tutajua tu!.)
Basi baada ya Watu kumuona Majaribu akikimbia waliamua kumuungia na kuanza kumfukuza, yaani Kwa Jinsi alivyo kuwa anakula unyoya ndo kabisaa watu waliamini Yeye ndo aliye husika na Wizi wa mifugo kushirikiana na anao wajua Yeye!.
Majaribu pona pona yake ilikuja baada ya kukimbilia kwenye pori kubwa ambalo lilikuwa linapakana na Kijiji hicho!.
Wanakijiji baada ya kumkosa Majaribu Sasa Hasira walizihamishia Kwa Bibi Yake, yaani Bibi wa Watu Siku hiyo alipigwa kipigo cha uhakika na nyumba Yake ilichomwa Moto kabisa.
Bibi Yule alifariki Usiku ule ule Bila hata kusema neno lolote, yaani wanakijiji walikuwa wamechafukwa Haswa, maana walikuwa wamechoka na Wizi wa Majaribu.
Majaribu alikuwa anakimbia huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanaenda sipidi, yaani alikuwa kachoka Lakini bado alikuwa anaendelea na mchaka mchaka maana alikuwa anajua akikamatwa basi Hana Bahati, alikuwa analikata pori lile huku akiwa hajui hata anako kimbilia!.
Ikiwa ni majira ya kama Saa Kumi za usiku Majaribu akiwa anaendelea kusonga mbele ndani ya pori lile! Mara alishituka kuna mwanga mkali unamurika Kwa mbali kuja maeneo aliko.
"Heeeee ni Majini au watu Gani!? Nani yupo Porini huku Usiku huu!" Majaribu akiwa kajibana kwenye Mti alijiongelesha Kwa uwoga!.
Majaribu alitulia kuangalia ule mwanga unaelekea wapi, basi akiwa kabana kwenye Mti aliona watu kama watano wakiwa wanasogea kwenye upande aliko huku wakiwa wamebeba furushi!.
Baada ya watu wale kuhakikisha kuna usalama lile furushi walilirusha huku wakiwa Makini!.
"Sasa Jamani! Mimi nasubiriwa na ndege maana nimekodi! Narudi India! Hakikisheni kila kitu kinakaa Sawa!" Hayo yalikuwa ni maneno ya mwanamke mmoja ambaye ndo alikuwa mwanamke pekee yake kwenye kundi lile, maneno Hayo pia kijana Majaribu aliyasikia Vyema akiwa kajibana kwenye Mti!.
Basi watu hao walianza kuondoka kuelekea njiani ambako walikuwa wameliacha Gari lao!.
Kijana Kwa uoga hakutaka hata kuangalia kwenye furushi lile lililo rushwa na Wale Jamaa kuna nini, mdogo mdogo alianza kuzipiga hatua kuondoka yale maeneo maana aliona ni nuksi!.
Ila baada ya kupiga hatua kama Tatu hivi Majaribu alisikia kikohozi kikiwa kinatoka kwenye furushi lile, yaani kikohozi kilikuwa kinatoka Kwa taabu kweli kweli
"Heeeee!! Nini tena!? Mtu!!!!??" Majaribu kwanza aliganda kama kanaswa na sumaku alafu alijiuliza ni nini tena hicho!
Majaribu Kwa ujasiri na kujiamini alisogea mpaka pale kwenye furushi, alifungua Huku mapigo ya Moyo yakiwa yanamuenda kasi, hakika Siku hiyo Majaribu aliamini Watu wana Roho mbaya!.
Ndani ya furushi lile alionekana mwanaume wa makamo kidogo Miaka kama 50 na kitu akiwa kachomwa vibaya muno na visu, yaani alikuwa amekatwa katwa hovyo kila sehemu ni dhahiri mwanaume huyo alikuwa anapambana na uhai wake wa mwisho, yaani kama ni Israel mtoa Roho alikuwa tayari kavunja kufuri imebakia tu kuingia ndani kuchukua kilicho chake!.
"Heee! Mzee upo hai! Kwani umetokea wapi na Kwa Nini wamekutupa hapa!?" Kijana Majaribu aliuliza maswali mfululizo huku akiwa mguu Sawa maana aliamini huwenda hata yule Mtu akawa ni Jini, maana Kwa visu ambavyo vilikuwa vimepita mwilini Mwake ilikuwa ni ngumu kuamini kama yupo hai!!.
"Aaaaaa!! Ehuuu! Kijana naomba nisaidie Vitu Viwili tu na Mungu atakubariki!" Baba Yule akiwa anakohoa Damu aliongea Kwa taabu kweli kweli!.
"Vitu gani hivyo!? " Majaribu akiwa anajua tu ataombwa msaada aliuliza huku kichwani akiwa anajijibu mwenyewe kwamba atawezeja kumbeba Mtu yule kumtoa kule porini!.
"Mimi ni mchungaji ila nakiri kwamba ni mkosefu mbele za Mungu! Naomba Hii Dhambi utanitubia mbele ya Watu wote, kitu Cha Pili ndani ya kanisa Langu Mazabahuni Chini ya Viti vya Mazabahuni kuna Siri Zangu, naomba kamtafute Mtu anaitwa Melisa ni katibu wa kanisa kampe Hii Siri na mwambie kila Kitu ampe mwanangu na ndo urithi Wangu wa Pekee kwake, chonde chonde naomba hizo Siri usimwambie Mtu yeyote zaidi ya Melisa, Kitu Cha mwisho Mke Wangu Siyo Mtu mzuri" Baba yule akiwa anaongea Kwa taabu huku pumzi zikiwa zinamuishia alitoa maelezo ambayo kijana majaribu hakuelewa Hata Moja!.
"Mzee ebu toa maelezo Vizuri nikuelewe basi, kanisa la wapi na Siri gani hizo mbona unaongea Mambo sielewi!??" Majaribu akiwa kama kapaniki aliuliza, Lakini hakuambulia Jibu lolote maana tayari Baba yule alikuwa kaaga dunia baada ya kutoa maelezo!.
"Heeeee! Kafariki!?? Jamani hili Jina ntabadilisha Sasa naona linaniletea majaribu ya kweli! Haya si majaribu Sasa!!? Haya hilo kanisa Mimi ntajua la wapi!?" Kijana majaribu alibaki anajilalamisha pale porini!.
Huu ni mwanzo mzuri wa Mkasa huu wa kusisimua Naami
ni hutojutia kuifuatilia hadithi hii, Je ipi safari ya Majaribu!.
Tukutane sehemu ya 2
Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)
UTANGULIZI: Ni hadithi inayomzungumzia kijana mdogo wa kuitwa majaribu. Wakati akijaribu kuyakimbia matatizo yake akakutana na majaribu menyewe Sasa Alijikuta akikabiliwa na kesi ya mauaji ambayo hakuyafanya ilipelekea kupelekwa gerezani je kijana Huyu atafanyaje ili kuthibitisha hana hatia. Ongozana nani Katika kigongo hili mwanzo mwisho. Mtunzi wa Hadithi hii anaitwa Mwaki Ze Done wasiliana naye Kwa whatsapp yake Kwa namba hizo hapo juu.
Sehemu: 1
Ni Majira Ya Usiku kwenye Moja ya Jengo la kifahari katikati ya Jiji ambalo lilikuwa limechangamka Haswa, kwenye Moja ya chumba ndani ya Jengo Hilo alionekana mdada wa Miaka kama 17 akiwa anaperuzi mtandao wa FB huku akiwa anakenua Meno Kwa furaha, Bila Shaka kile ambacho alikuwa anakifuatilia kilimfurahisha Sana.
Ila Mida hiyo ya Saa Saba za usiku akiwa bado kazama kwenye Mitandao kiasi kwamba usingizi uliogopa hata kumnyemelea Mara gafla Dada huyo alianza kusikia kukuru kakara upande wa pili ndani ya nyumba hiyo hiyo!.
Dada huyo taratibu aliweka Simu yake kitandani na kutoka kule chumbani ili kuona nini kinaendelea!.
Kwanza alienda mpaka sebuleni na kutulia ili kusikilizia zile kukuru kakara alizo zisikia ni wapi zimetokea.
"Msaadaaaa!! Nisaidieni......uuuuu!!!.." Dada Yule akiwa pale sebuleni alisikia Sauti Kwa mbaali ya mwanaume akiwa anaomba msaada! Haraka haraka Dada yule alipanda ngazi mpaka gorofa ya juu ambako Sauti hizo zilikuwa zinatokea! Kwa mwendo wa taratibu na umakini mkubwa Dada yule alisogea mpaka kwenye mlango ambao ulioneka upo wazi!.
"Mungu Wangu....!!" Dada Yule Kwa kile alicho kiona alijikuta anaropoka Kwa Sauti ya Chini huku akiwa anajiziba mdomo, Mapigo ya Moyo yalionekana kwenda Sipidi Muno Mwili mzima wa Dada Yule ulikuwa unatetemeka Kwa kile alicho kiona, Haraka haraka alitoka pale mlangoni na kukimbilia chumbani kwake!.
Dada Yule alianza kukusanya vitu vyake kule chumbani Kwa ajili ya kuondoka huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanamuenda sipidi, ila baada ya kukusanya na kufunga begi lake vyema, baada ya kufika mlangoni ni kama kuna akili ilimjia kwamba usiondoke!.
"Uuuuu!! Nikikimbia Hii kesi si itakuwa Yangu hii! Siendi kokote!" Dada yule alijiongelesha mwenyewe, baada ya kuwaza na kuwazua aliamua kurudi kitandani na kukaa!.
Simu Ya Dada huyo ilikuwa haishikiki tena yaani Moja ilikuwa haikai Mbili haikai Jasho tu ndo lilikuwa linamtoka Japo ilikuwa usiku.
Dada huyo akiwa katulia chumbani alisikia vishindo vya watu walionekana Sasa wanashuka ngazi kutokea gorofa ya juu! Dada yule ambaye bado hatujamjua ni nani, akiwa na Moyo wa kijasiri aliamua kutoka kule chumbani kwake taratibu na kwenda kuchungulia.
Dada Yule aliona Njemba kama Nne zikiwa zimebeba furushi zinatoka kule chumbani huku nyuma yao kukiwa na Mama Mtu mzima Miaka kama arobaini na kitu akiwa anafuata nyuma tena Kwa ujasiri!.
"Heeeee!! Mbona maajabu jamani! Wamefanana au ni Yeye!?? Mama Mchungaji si yupo India!?? aaaaaa hii haiwezekani!??" Dada yule baada ya kuona hali ile alijiuliza maswali ambayo hayana Majibu Huku akiwa anachungulia na Mwili mzima ukiwa unamtetemeka!.
Usiku huo huo kwenye Moja ya kijiji ambacho kilikuwa hakipo mbali Sana na Jiji lile ilikuwa ni kama mwendo wa masaa matatu na Kitu Hivi ukiwa na usafiri kutokea Mjini mpaka kwenye Kijiji hicho.
Ndani ya kijiji hicho Walionekana wanakijiji wakiwa wamechafukwa Haswa Usiku huo wa manane kwenye Moja ya nyumba ya nyasi ambayo alikuwa anaishi Bibi wa Miaka kama 70 na mjukuu wake wa kiume Miaka kama 16, wakiwa wamelala usiku huo Mara walisikia makelele ya wanakijiji wakiwa wanaonekana wanakuja pale nyumbani.
"Tumechoka!! Tumechoka!! Tumechoka!!" Hizo zilikuwa nyimbo za Mizuka kutoka Kwa wanakijiji, yaani nyimbo hizo zilifanya hata wale Ambao walikuwa wamelala usingizi wa pono waamuke na kwenda kuungana na wenzao katika kutimiza Jambo lao!.
Umati ule wa wanakijiji walifika mpaka kwenye nyumba ile ya nyasi ambayo alikuwa anaishi Bibi huyo kikongwe na mjukuu Wake!.
"Bibi Zoha Tumechoka! Tumekuchoka wewe na mjukuu wako! Wizi nyie! Uchawi nyiee! Kwa usalama wenu kabla hatujachoma hiki kinyumba chenu tokeni nje!" Basi umati ule baada ya kufika nyumbani Kwa Bibi yule kuna Jamaa aliongea Kwa mizuka na kweli watu waliripuka Kwa shangwe.
Upande wa ndani Bibi Yule na mjukuu wake walikuwa wanatazama huku wakiwa Hawaelewi kipi ni kipi!.
"Majaribu Hivi umeiba tena!? We mtoto upoje Lakini!?" Huku ndani Yule Bibi alianza kumlaumu mjukuu wake huku Moyo ukiwa unaenda mbio!.
"Bibi Mimi nimeiba Saa ngapi wakati tupo wote Muda wote, isitoshe hao wanasema uchawi siyo Wizi! Bibi wewe ni Mchawi na ndo wamekufuata!" Basi kijana yule naye akiwa na uoga alimjibu Bibi yake!.
"Majaribu acha ujuaji, sikiliza hapa hakuna usalama ebu tokea dirishani kimbia tena kimbia uende mbali, hata ukisikia nimekufa usirudi Hapa!" Bibi Yule akiwa anajiandaa kwenda kufungua mlango alimjibu mjukuu wake, lakini Kabla hata hajanyanyuka kwenda mlangoni Mara walianza kusikia mlango ukivunjwa Kwa kutumia vitu Vizito maana wanakijiji walikuwa wamevurugwa mpaka Siyo vizuri.
"Au kama Vipi tuchome nyumba mbona watatoka wenyewe!" Basi kuna jamaa aliongea Kwa mizuka na kufanya watu waanze Sasa kutafuta kiberiti, wale wa Karibu na pale Kwa Jinsi walivyo kuwa na Roho ngumu waliamua kufuata viberiti majumbani kwao!.
Huku ndani kijana wa kuitwa Majaribu baada ya kuona Sasa Maji yamezidi unga aliamua kuchomokea dirishani, Japo kuwa dirisha lilikuwa dogo ila alijilazimisha na alitosha na ilionekana ni mzoefu wa kupita Madirishani.
Baadhi ya Watu walimuona kijana Huyo akiwa anakimbia na waliamua kumuungia Kwa kumfukuza maana huyo ndo walikuwa na Shida naye zaidi kuliko hata Bibi yake!.
Kijana majaribu pamoja na umri wake alikuwa ni mwizi haijawahi kutokea, yaani alikuwa ni kama kasomea shahada ya Wizi, na tangia aanze kuiba alikuwa hajawahi kukamatwa, yaani Watu walikuwa hawambahatishi kwenye matukio Japo kuwa walikuwa wanajua ni Mwizi!.
Bahati mbaya Siku hiyo pale Kijijini kuna Mtu alikuwa kaibiwa mifugo yake Yote na baada ya wanakijiji kuamushana Usiku waliamua Sasa kuelekea nyumbani Kwa Bibi yake na Majaribu wakiwa na uhakika kwamba huwenda kijana huyo ndo mhusika kuhusu mifugo hiyo kupotea.
(Kwakuwa kijana Majaribu ndo mhusika mkuu bado kuna mengi tutayajua kumhusu mpaka Yeye kuwa kwenye mazingira yale Je ni ipi Historia Yake!? Tutajua tu!.)
Basi baada ya Watu kumuona Majaribu akikimbia waliamua kumuungia na kuanza kumfukuza, yaani Kwa Jinsi alivyo kuwa anakula unyoya ndo kabisaa watu waliamini Yeye ndo aliye husika na Wizi wa mifugo kushirikiana na anao wajua Yeye!.
Majaribu pona pona yake ilikuja baada ya kukimbilia kwenye pori kubwa ambalo lilikuwa linapakana na Kijiji hicho!.
Wanakijiji baada ya kumkosa Majaribu Sasa Hasira walizihamishia Kwa Bibi Yake, yaani Bibi wa Watu Siku hiyo alipigwa kipigo cha uhakika na nyumba Yake ilichomwa Moto kabisa.
Bibi Yule alifariki Usiku ule ule Bila hata kusema neno lolote, yaani wanakijiji walikuwa wamechafukwa Haswa, maana walikuwa wamechoka na Wizi wa Majaribu.
Majaribu alikuwa anakimbia huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanaenda sipidi, yaani alikuwa kachoka Lakini bado alikuwa anaendelea na mchaka mchaka maana alikuwa anajua akikamatwa basi Hana Bahati, alikuwa analikata pori lile huku akiwa hajui hata anako kimbilia!.
Ikiwa ni majira ya kama Saa Kumi za usiku Majaribu akiwa anaendelea kusonga mbele ndani ya pori lile! Mara alishituka kuna mwanga mkali unamurika Kwa mbali kuja maeneo aliko.
"Heeeee ni Majini au watu Gani!? Nani yupo Porini huku Usiku huu!" Majaribu akiwa kajibana kwenye Mti alijiongelesha Kwa uwoga!.
Majaribu alitulia kuangalia ule mwanga unaelekea wapi, basi akiwa kabana kwenye Mti aliona watu kama watano wakiwa wanasogea kwenye upande aliko huku wakiwa wamebeba furushi!.
Baada ya watu wale kuhakikisha kuna usalama lile furushi walilirusha huku wakiwa Makini!.
"Sasa Jamani! Mimi nasubiriwa na ndege maana nimekodi! Narudi India! Hakikisheni kila kitu kinakaa Sawa!" Hayo yalikuwa ni maneno ya mwanamke mmoja ambaye ndo alikuwa mwanamke pekee yake kwenye kundi lile, maneno Hayo pia kijana Majaribu aliyasikia Vyema akiwa kajibana kwenye Mti!.
Basi watu hao walianza kuondoka kuelekea njiani ambako walikuwa wameliacha Gari lao!.
Kijana Kwa uoga hakutaka hata kuangalia kwenye furushi lile lililo rushwa na Wale Jamaa kuna nini, mdogo mdogo alianza kuzipiga hatua kuondoka yale maeneo maana aliona ni nuksi!.
Ila baada ya kupiga hatua kama Tatu hivi Majaribu alisikia kikohozi kikiwa kinatoka kwenye furushi lile, yaani kikohozi kilikuwa kinatoka Kwa taabu kweli kweli
"Heeeee!! Nini tena!? Mtu!!!!??" Majaribu kwanza aliganda kama kanaswa na sumaku alafu alijiuliza ni nini tena hicho!
Majaribu Kwa ujasiri na kujiamini alisogea mpaka pale kwenye furushi, alifungua Huku mapigo ya Moyo yakiwa yanamuenda kasi, hakika Siku hiyo Majaribu aliamini Watu wana Roho mbaya!.
Ndani ya furushi lile alionekana mwanaume wa makamo kidogo Miaka kama 50 na kitu akiwa kachomwa vibaya muno na visu, yaani alikuwa amekatwa katwa hovyo kila sehemu ni dhahiri mwanaume huyo alikuwa anapambana na uhai wake wa mwisho, yaani kama ni Israel mtoa Roho alikuwa tayari kavunja kufuri imebakia tu kuingia ndani kuchukua kilicho chake!.
"Heee! Mzee upo hai! Kwani umetokea wapi na Kwa Nini wamekutupa hapa!?" Kijana Majaribu aliuliza maswali mfululizo huku akiwa mguu Sawa maana aliamini huwenda hata yule Mtu akawa ni Jini, maana Kwa visu ambavyo vilikuwa vimepita mwilini Mwake ilikuwa ni ngumu kuamini kama yupo hai!!.
"Aaaaaa!! Ehuuu! Kijana naomba nisaidie Vitu Viwili tu na Mungu atakubariki!" Baba Yule akiwa anakohoa Damu aliongea Kwa taabu kweli kweli!.
"Vitu gani hivyo!? " Majaribu akiwa anajua tu ataombwa msaada aliuliza huku kichwani akiwa anajijibu mwenyewe kwamba atawezeja kumbeba Mtu yule kumtoa kule porini!.
"Mimi ni mchungaji ila nakiri kwamba ni mkosefu mbele za Mungu! Naomba Hii Dhambi utanitubia mbele ya Watu wote, kitu Cha Pili ndani ya kanisa Langu Mazabahuni Chini ya Viti vya Mazabahuni kuna Siri Zangu, naomba kamtafute Mtu anaitwa Melisa ni katibu wa kanisa kampe Hii Siri na mwambie kila Kitu ampe mwanangu na ndo urithi Wangu wa Pekee kwake, chonde chonde naomba hizo Siri usimwambie Mtu yeyote zaidi ya Melisa, Kitu Cha mwisho Mke Wangu Siyo Mtu mzuri" Baba yule akiwa anaongea Kwa taabu huku pumzi zikiwa zinamuishia alitoa maelezo ambayo kijana majaribu hakuelewa Hata Moja!.
"Mzee ebu toa maelezo Vizuri nikuelewe basi, kanisa la wapi na Siri gani hizo mbona unaongea Mambo sielewi!??" Majaribu akiwa kama kapaniki aliuliza, Lakini hakuambulia Jibu lolote maana tayari Baba yule alikuwa kaaga dunia baada ya kutoa maelezo!.
"Heeeee! Kafariki!?? Jamani hili Jina ntabadilisha Sasa naona linaniletea majaribu ya kweli! Haya si majaribu Sasa!!? Haya hilo kanisa Mimi ntajua la wapi!?" Kijana majaribu alibaki anajilalamisha pale porini!.
Huu ni mwanzo mzuri wa Mkasa huu wa kusisimua Naami
ni hutojutia kuifuatilia hadithi hii, Je ipi safari ya Majaribu!.
Tukutane sehemu ya 2