Hadithi: Majaribu

Joined
Apr 12, 2025
Posts
31
Reaction score
60
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

UTANGULIZI: Ni hadithi inayomzungumzia kijana mdogo wa kuitwa majaribu. Wakati akijaribu kuyakimbia matatizo yake akakutana na majaribu menyewe Sasa Alijikuta akikabiliwa na kesi ya mauaji ambayo hakuyafanya ilipelekea kupelekwa gerezani je kijana Huyu atafanyaje ili kuthibitisha hana hatia. Ongozana nani Katika kigongo hili mwanzo mwisho. Mtunzi wa Hadithi hii anaitwa Mwaki Ze Done wasiliana naye Kwa whatsapp yake Kwa namba hizo hapo juu.

Sehemu: 1

Ni Majira Ya Usiku kwenye Moja ya Jengo la kifahari katikati ya Jiji ambalo lilikuwa limechangamka Haswa, kwenye Moja ya chumba ndani ya Jengo Hilo alionekana mdada wa Miaka kama 17 akiwa anaperuzi mtandao wa FB huku akiwa anakenua Meno Kwa furaha, Bila Shaka kile ambacho alikuwa anakifuatilia kilimfurahisha Sana.
Ila Mida hiyo ya Saa Saba za usiku akiwa bado kazama kwenye Mitandao kiasi kwamba usingizi uliogopa hata kumnyemelea Mara gafla Dada huyo alianza kusikia kukuru kakara upande wa pili ndani ya nyumba hiyo hiyo!.

Dada huyo taratibu aliweka Simu yake kitandani na kutoka kule chumbani ili kuona nini kinaendelea!.
Kwanza alienda mpaka sebuleni na kutulia ili kusikilizia zile kukuru kakara alizo zisikia ni wapi zimetokea.

"Msaadaaaa!! Nisaidieni......uuuuu!!!.." Dada Yule akiwa pale sebuleni alisikia Sauti Kwa mbaali ya mwanaume akiwa anaomba msaada! Haraka haraka Dada yule alipanda ngazi mpaka gorofa ya juu ambako Sauti hizo zilikuwa zinatokea! Kwa mwendo wa taratibu na umakini mkubwa Dada yule alisogea mpaka kwenye mlango ambao ulioneka upo wazi!.

"Mungu Wangu....!!" Dada Yule Kwa kile alicho kiona alijikuta anaropoka Kwa Sauti ya Chini huku akiwa anajiziba mdomo, Mapigo ya Moyo yalionekana kwenda Sipidi Muno Mwili mzima wa Dada Yule ulikuwa unatetemeka Kwa kile alicho kiona, Haraka haraka alitoka pale mlangoni na kukimbilia chumbani kwake!.
Dada Yule alianza kukusanya vitu vyake kule chumbani Kwa ajili ya kuondoka huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanamuenda sipidi, ila baada ya kukusanya na kufunga begi lake vyema, baada ya kufika mlangoni ni kama kuna akili ilimjia kwamba usiondoke!.

"Uuuuu!! Nikikimbia Hii kesi si itakuwa Yangu hii! Siendi kokote!" Dada yule alijiongelesha mwenyewe, baada ya kuwaza na kuwazua aliamua kurudi kitandani na kukaa!.
Simu Ya Dada huyo ilikuwa haishikiki tena yaani Moja ilikuwa haikai Mbili haikai Jasho tu ndo lilikuwa linamtoka Japo ilikuwa usiku.

Dada huyo akiwa katulia chumbani alisikia vishindo vya watu walionekana Sasa wanashuka ngazi kutokea gorofa ya juu! Dada yule ambaye bado hatujamjua ni nani, akiwa na Moyo wa kijasiri aliamua kutoka kule chumbani kwake taratibu na kwenda kuchungulia.
Dada Yule aliona Njemba kama Nne zikiwa zimebeba furushi zinatoka kule chumbani huku nyuma yao kukiwa na Mama Mtu mzima Miaka kama arobaini na kitu akiwa anafuata nyuma tena Kwa ujasiri!.

"Heeeee!! Mbona maajabu jamani! Wamefanana au ni Yeye!?? Mama Mchungaji si yupo India!?? aaaaaa hii haiwezekani!??" Dada yule baada ya kuona hali ile alijiuliza maswali ambayo hayana Majibu Huku akiwa anachungulia na Mwili mzima ukiwa unamtetemeka!.

Usiku huo huo kwenye Moja ya kijiji ambacho kilikuwa hakipo mbali Sana na Jiji lile ilikuwa ni kama mwendo wa masaa matatu na Kitu Hivi ukiwa na usafiri kutokea Mjini mpaka kwenye Kijiji hicho.
Ndani ya kijiji hicho Walionekana wanakijiji wakiwa wamechafukwa Haswa Usiku huo wa manane kwenye Moja ya nyumba ya nyasi ambayo alikuwa anaishi Bibi wa Miaka kama 70 na mjukuu wake wa kiume Miaka kama 16, wakiwa wamelala usiku huo Mara walisikia makelele ya wanakijiji wakiwa wanaonekana wanakuja pale nyumbani.

"Tumechoka!! Tumechoka!! Tumechoka!!" Hizo zilikuwa nyimbo za Mizuka kutoka Kwa wanakijiji, yaani nyimbo hizo zilifanya hata wale Ambao walikuwa wamelala usingizi wa pono waamuke na kwenda kuungana na wenzao katika kutimiza Jambo lao!.
Umati ule wa wanakijiji walifika mpaka kwenye nyumba ile ya nyasi ambayo alikuwa anaishi Bibi huyo kikongwe na mjukuu Wake!.

"Bibi Zoha Tumechoka! Tumekuchoka wewe na mjukuu wako! Wizi nyie! Uchawi nyiee! Kwa usalama wenu kabla hatujachoma hiki kinyumba chenu tokeni nje!" Basi umati ule baada ya kufika nyumbani Kwa Bibi yule kuna Jamaa aliongea Kwa mizuka na kweli watu waliripuka Kwa shangwe.
Upande wa ndani Bibi Yule na mjukuu wake walikuwa wanatazama huku wakiwa Hawaelewi kipi ni kipi!.

"Majaribu Hivi umeiba tena!? We mtoto upoje Lakini!?" Huku ndani Yule Bibi alianza kumlaumu mjukuu wake huku Moyo ukiwa unaenda mbio!.

"Bibi Mimi nimeiba Saa ngapi wakati tupo wote Muda wote, isitoshe hao wanasema uchawi siyo Wizi! Bibi wewe ni Mchawi na ndo wamekufuata!" Basi kijana yule naye akiwa na uoga alimjibu Bibi yake!.

"Majaribu acha ujuaji, sikiliza hapa hakuna usalama ebu tokea dirishani kimbia tena kimbia uende mbali, hata ukisikia nimekufa usirudi Hapa!" Bibi Yule akiwa anajiandaa kwenda kufungua mlango alimjibu mjukuu wake, lakini Kabla hata hajanyanyuka kwenda mlangoni Mara walianza kusikia mlango ukivunjwa Kwa kutumia vitu Vizito maana wanakijiji walikuwa wamevurugwa mpaka Siyo vizuri.

"Au kama Vipi tuchome nyumba mbona watatoka wenyewe!" Basi kuna jamaa aliongea Kwa mizuka na kufanya watu waanze Sasa kutafuta kiberiti, wale wa Karibu na pale Kwa Jinsi walivyo kuwa na Roho ngumu waliamua kufuata viberiti majumbani kwao!.
Huku ndani kijana wa kuitwa Majaribu baada ya kuona Sasa Maji yamezidi unga aliamua kuchomokea dirishani, Japo kuwa dirisha lilikuwa dogo ila alijilazimisha na alitosha na ilionekana ni mzoefu wa kupita Madirishani.

Baadhi ya Watu walimuona kijana Huyo akiwa anakimbia na waliamua kumuungia Kwa kumfukuza maana huyo ndo walikuwa na Shida naye zaidi kuliko hata Bibi yake!.
Kijana majaribu pamoja na umri wake alikuwa ni mwizi haijawahi kutokea, yaani alikuwa ni kama kasomea shahada ya Wizi, na tangia aanze kuiba alikuwa hajawahi kukamatwa, yaani Watu walikuwa hawambahatishi kwenye matukio Japo kuwa walikuwa wanajua ni Mwizi!.
Bahati mbaya Siku hiyo pale Kijijini kuna Mtu alikuwa kaibiwa mifugo yake Yote na baada ya wanakijiji kuamushana Usiku waliamua Sasa kuelekea nyumbani Kwa Bibi yake na Majaribu wakiwa na uhakika kwamba huwenda kijana huyo ndo mhusika kuhusu mifugo hiyo kupotea.

(Kwakuwa kijana Majaribu ndo mhusika mkuu bado kuna mengi tutayajua kumhusu mpaka Yeye kuwa kwenye mazingira yale Je ni ipi Historia Yake!? Tutajua tu!.)

Basi baada ya Watu kumuona Majaribu akikimbia waliamua kumuungia na kuanza kumfukuza, yaani Kwa Jinsi alivyo kuwa anakula unyoya ndo kabisaa watu waliamini Yeye ndo aliye husika na Wizi wa mifugo kushirikiana na anao wajua Yeye!.
Majaribu pona pona yake ilikuja baada ya kukimbilia kwenye pori kubwa ambalo lilikuwa linapakana na Kijiji hicho!.

Wanakijiji baada ya kumkosa Majaribu Sasa Hasira walizihamishia Kwa Bibi Yake, yaani Bibi wa Watu Siku hiyo alipigwa kipigo cha uhakika na nyumba Yake ilichomwa Moto kabisa.
Bibi Yule alifariki Usiku ule ule Bila hata kusema neno lolote, yaani wanakijiji walikuwa wamechafukwa Haswa, maana walikuwa wamechoka na Wizi wa Majaribu.

Majaribu alikuwa anakimbia huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanaenda sipidi, yaani alikuwa kachoka Lakini bado alikuwa anaendelea na mchaka mchaka maana alikuwa anajua akikamatwa basi Hana Bahati, alikuwa analikata pori lile huku akiwa hajui hata anako kimbilia!.

Ikiwa ni majira ya kama Saa Kumi za usiku Majaribu akiwa anaendelea kusonga mbele ndani ya pori lile! Mara alishituka kuna mwanga mkali unamurika Kwa mbali kuja maeneo aliko.

"Heeeee ni Majini au watu Gani!? Nani yupo Porini huku Usiku huu!" Majaribu akiwa kajibana kwenye Mti alijiongelesha Kwa uwoga!.
Majaribu alitulia kuangalia ule mwanga unaelekea wapi, basi akiwa kabana kwenye Mti aliona watu kama watano wakiwa wanasogea kwenye upande aliko huku wakiwa wamebeba furushi!.

Baada ya watu wale kuhakikisha kuna usalama lile furushi walilirusha huku wakiwa Makini!.

"Sasa Jamani! Mimi nasubiriwa na ndege maana nimekodi! Narudi India! Hakikisheni kila kitu kinakaa Sawa!" Hayo yalikuwa ni maneno ya mwanamke mmoja ambaye ndo alikuwa mwanamke pekee yake kwenye kundi lile, maneno Hayo pia kijana Majaribu aliyasikia Vyema akiwa kajibana kwenye Mti!.

Basi watu hao walianza kuondoka kuelekea njiani ambako walikuwa wameliacha Gari lao!.
Kijana Kwa uoga hakutaka hata kuangalia kwenye furushi lile lililo rushwa na Wale Jamaa kuna nini, mdogo mdogo alianza kuzipiga hatua kuondoka yale maeneo maana aliona ni nuksi!.
Ila baada ya kupiga hatua kama Tatu hivi Majaribu alisikia kikohozi kikiwa kinatoka kwenye furushi lile, yaani kikohozi kilikuwa kinatoka Kwa taabu kweli kweli

"Heeeee!! Nini tena!? Mtu!!!!??" Majaribu kwanza aliganda kama kanaswa na sumaku alafu alijiuliza ni nini tena hicho!
Majaribu Kwa ujasiri na kujiamini alisogea mpaka pale kwenye furushi, alifungua Huku mapigo ya Moyo yakiwa yanamuenda kasi, hakika Siku hiyo Majaribu aliamini Watu wana Roho mbaya!.

Ndani ya furushi lile alionekana mwanaume wa makamo kidogo Miaka kama 50 na kitu akiwa kachomwa vibaya muno na visu, yaani alikuwa amekatwa katwa hovyo kila sehemu ni dhahiri mwanaume huyo alikuwa anapambana na uhai wake wa mwisho, yaani kama ni Israel mtoa Roho alikuwa tayari kavunja kufuri imebakia tu kuingia ndani kuchukua kilicho chake!.

"Heee! Mzee upo hai! Kwani umetokea wapi na Kwa Nini wamekutupa hapa!?" Kijana Majaribu aliuliza maswali mfululizo huku akiwa mguu Sawa maana aliamini huwenda hata yule Mtu akawa ni Jini, maana Kwa visu ambavyo vilikuwa vimepita mwilini Mwake ilikuwa ni ngumu kuamini kama yupo hai!!.

"Aaaaaa!! Ehuuu! Kijana naomba nisaidie Vitu Viwili tu na Mungu atakubariki!" Baba Yule akiwa anakohoa Damu aliongea Kwa taabu kweli kweli!.

"Vitu gani hivyo!? " Majaribu akiwa anajua tu ataombwa msaada aliuliza huku kichwani akiwa anajijibu mwenyewe kwamba atawezeja kumbeba Mtu yule kumtoa kule porini!.

"Mimi ni mchungaji ila nakiri kwamba ni mkosefu mbele za Mungu! Naomba Hii Dhambi utanitubia mbele ya Watu wote, kitu Cha Pili ndani ya kanisa Langu Mazabahuni Chini ya Viti vya Mazabahuni kuna Siri Zangu, naomba kamtafute Mtu anaitwa Melisa ni katibu wa kanisa kampe Hii Siri na mwambie kila Kitu ampe mwanangu na ndo urithi Wangu wa Pekee kwake, chonde chonde naomba hizo Siri usimwambie Mtu yeyote zaidi ya Melisa, Kitu Cha mwisho Mke Wangu Siyo Mtu mzuri" Baba yule akiwa anaongea Kwa taabu huku pumzi zikiwa zinamuishia alitoa maelezo ambayo kijana majaribu hakuelewa Hata Moja!.

"Mzee ebu toa maelezo Vizuri nikuelewe basi, kanisa la wapi na Siri gani hizo mbona unaongea Mambo sielewi!??" Majaribu akiwa kama kapaniki aliuliza, Lakini hakuambulia Jibu lolote maana tayari Baba yule alikuwa kaaga dunia baada ya kutoa maelezo!.
"Heeeee! Kafariki!?? Jamani hili Jina ntabadilisha Sasa naona linaniletea majaribu ya kweli! Haya si majaribu Sasa!!? Haya hilo kanisa Mimi ntajua la wapi!?" Kijana majaribu alibaki anajilalamisha pale porini!.

Huu ni mwanzo mzuri wa Mkasa huu wa kusisimua Naami
ni hutojutia kuifuatilia hadithi hii, Je ipi safari ya Majaribu!.

Tukutane sehemu ya 2
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 2

"Heeeee! Kafariki!?? Jamani hili Jina ntabadilisha Sasa naona linaniletea majaribu ya kweli! Haya si majaribu Sasa!!? Haya hilo kanisa Mimi ntajua la wapi!?" Kijana majaribu alibaki anajilalamisha pale porini!.

Ulikuwa ni usiku mbalamwezi ikiwa inaangaza na kufanya kila sehemu ionekane vyema, kijana Majaribu Alisimama Huku Jasho jembamba likiwa limeanza kumtoka! Gafla radi nazo zilianza kupiga na wingu zito la mvua kutanda Juu!.

"Ujinga sitaki kila Mtu atabeba mizigo Yake!" Kijana Majaribu alijiongelesha mwenyewe na kuanza kuzipiga hatua, Huku manyunyu ya Mvua yakiwa yameanza kushuka! Majaribu alitembea mpaka aliikuta barabara ya Lami ambayo ilikuwa imekatiza katikati ya Msitu ule!.
Kijana Majaribu alijikuta Roho yake imeanza kuuma Muno, Yaani kuna akili ilikuwa inamwambia arudi porini tena aliko muacha Yule Baba!.

Baada ya Majaribu kuwaza na kuwazua aliamua kurudi porini tena, baada ya kufika kitu alicho kifanya aliamua kuukokota mwili ule mpaka Barabarani, Japo kuwa barabarani palikuwa mbali na pale ulipo tupwa ule mwili wa Yule Baba Lakini Majaribu alipambana na kuufikisha barabarani!.
Baada ya Majaribu kuhakikisha mwili kauweka sehemu ambayo aliamini ni salama aliangaza huku na Kule ili aone ni wapi aelekee, ilikuwa ni Majira ya Saa Kumi na moja alfajiri kuelekea Saa kumi na mbili kifupi kulikuwa kumeanza kupambazuka kabisa!.
Ila bahati mbaya kijana Majaribu akiwa anaukokota mwili na kuuweka pale barabarani kuna Gari ilipita maeneo Yale na ndani ya Gari lile alionekana Dada wa Miaka kama 30 Hivi akiwa anaendesha, kwanza baada ya kufika mbele kidogo Dada yule alisimama na kurudisha Gari kinyume nyume, Kisha alisimamisha na kushuka.

"We dogo Vipi unafanya Nini hapo!?" Yule Dada alimuuliza kijana Majaribu tena alionekana anaogopa Muno!.

"Aaaaaa! eeeeeee!! Nimemkuta kauawa katupwa porini!" Majaribu akiwa na kigugumizi alijibu
Yule Dada alirudi kwenye Gari lake, baada ya hapo alitoka na Simu yake alimpiga picha kama Tatu hivi Majaribu, na alimrekodi video fupi Majaribu, kijana Majaribu alikuwa haelewi hata kinacho fanyika, yaani alikuwa haelewi Dada yule anafanya nini Yeye alibaki kaganda pale pale huku Chini Mwili wa Yule Baba ukiwa umelala.

"Watu wengine bwana ndo nini Sasa! Aisee Mimi nishamaliza Kazi Yangu!" Majaribu akiwa na Hasira alijiongelesha na kuanza kuondoka Huku akiwa ameanza kula jaramba Kwa kukimbia!.
Dada yule naye baada ya kurudi kwenye Gari Moja Kwa Moja alipiga Simu kituoni kutoa taarifa ya tukio la Mauaji, maana alicho Amini ni kwamba Yule dogo huwenda ndo kaua.

Masaa yalizidi kusogea! Ikiwa ni kama Saa mbili kijua kikiwa kimeanza kuwaka Majaribu alionekana akiwa kanyosha barabara anaelekea Mjini, yaani alikuwa hataki kurudi Kijijini kwao Tena, ila akiwa anaelekea Mjini alipishana na Gari za Askari kama mbili zikiwa kasi kweli kweli kuelekea kule aliko tokea!.
Majaribu hakugundua haraka haraka kwamba Gari zile ni wapi zinaelekea yeye aliendelea kuzihesabu hatua tu kusonga mbele.
Baada ya kama lisaa Sijui Nini kilitokea huko ziliko elekea Gari za Askari, Majaribu alishangaa anasikia king'ora Cha Askari tena Gari zikiwa zinarudi Kwa Kasi, huku mbele ya Gari zile kukiwa na Gari nyeusi ambayo ilikuwa inaendeshwa na mdada yule yule aliye mpiga Majaribu picha!.

Gari zile zilipo fika pale alipo Majaribu zilisimama na Askari walishuka, Huku Majaribu akiwa kando ya Barabara anatumbua tu Macho.

"Dada vipi mbona tunasimama!??" Askari ambaye alikuwa kiongozi wa msafara alimfuata Yule Dada ambaye alikuwa yupo mbele na Gari yake!.

"Afande, kijana mwenyewe ndo huyo Hapo!?" Yule Dada akiwa anamnyoshea kidole Majaribu aliongea!.
Kwanza Majaribu alishangaa kumuona Yule Dada Kwa Mara nyingine, Macho yalikuwa yanamtoka huku akiwa haelewi kipi ni kipi!.

"Jamani mbona sielewi kuna nini!?" Kijana Majaribu aliuliza Kwa mshangao, lakini badala ya kupewa majibu alipigwa Bonge la Kofi mpaka mate yalimruka mdomoni pasina kupenda, ilibidi Majaribu atulie kama kamwagiwa maji.
Bila hata huruma alirushwa kwenye defenda kama gunia vile, yaani alidondokea Mkono vibaya Muno kiasi kwamba Mkono wake uliteguka na kuumia, Lakini Majaribu ilibidi abaki anagugumia maumivu ndani Kwa ndani!.

Askari wale walirudi Eneo la tukio walibeba mwili wa Yule Baba ambaye alikuwa kauawa baada ya hapo safari ya kuelekea kituoni ilianza!.
Ni ndani ya sekunde tu picha ya Baba Yule akiwa kakatwa katwa vibaya na visu ilianza kusambaa Mitandaoni na kufanya kila Mtu ambaye alikuwa anamjua Baba huyo kushika kichwa, haieleweki ni Mtu gani alikuwa kampiga picha zile Baba Yule na kusambaza mtandaoni.

Turudi ndani ya Jumba la kifahari ambako tulimuona Yule Dada akishuhudia tukio la kutisha usiku.

Asubuhi na mapema kabisa Dada yule aliamka Huku Bado Mwili wake ukiwa unatetemeka! Yaani kile alicho kiona usiku bado kilikuwa kinampa kiwewe!.
Dada Yule alishika Simu yake na kuwasha Dada, kwanza baada ya kuwasha tu data, ujumbe ulianza kutiririka kwenye Simu Yake Kwa upande wa Whatsapp! Dada Yule alifungua Whatsapp yake alikutana na SMS kama 10 mojawapo ilikuwa ni Video ambayo alikuwa katumiwa na Namba iliyo seviwa "Boss Mama mchungaji ".

Video hiyo Dada yule aliifungua, ilikuwa ni video ambayo alikuwa katumiwa na Boss wake ambaye Kwa muda huo alikuwa yupo India, na ilikuwa ni salamu tu za Asubuhi!.

"Revina Haiii, Hamjambo Huko Home!? Huku India Sisi tupo poa as You see!!" Hayo yalikuwa ni maneno ambayo Mama yule alikuwa kayazungumza kwenye video!.
Kwanza Dada yule Kwa Jina la Revina alishangaa Muno, yaani ilikuwa Mara ya kwanza Kwa Boss wake huyo kumtumia video ya kumtakia Hai, Boss wake huyo alikuwa ni Mtu wa Roho mbaya Muda wote Kwa upande wake na kila Siku ilikuwa ni kuoga matusi na kipigo japo kuwa mwanamke Huyo alikuwa Mke wa mchangaji!.

Basi Revina aliachana na ujumbe Ule huku akiwa anataka kusoma na ujumbe mwingine, ila kabla hajafungua ujumbe mwingine Mara alisikia ni kama kuna makelele getini!.
Revina alitoka mpaka nje alikutana na Nyomi ya watu pale nje!.

"Eheee Revina Bora umekuja!? Ni kweli Mchungaji Nemeke kauawa!! Na Jana alirudi nyumbani au hakurudi!?" Hilo lilikuwa ni swali kutoka Kwa Baba Mtu mzima ambalo Dada yule alikutana nalo baada ya kutoka nje!
Revina Macho tu yalikuwa yanamtoka alikuwa haelewi hata kinacho endelea, yaani kila alipo kumbuka kile alicho kiona usiku mwili wake ulibaki unasisimuka tu!.

Kabla Revina Hajajibu swali lile Mara kuna Gari ya Askari ilifika pale nyumbani! Na Muda huo idadi ya Watu ilikuwa inazidi kuongezeka, maana Bwana aliye uawa alikuwa ni Mtu maarufu pale Mjini, ukiachana na uchungaji Wake pia alikuwa mfanyabiashara mkubwa.

Revina alichukuliwa na askari waliingia mpaka ndani Kwa ajili ya kumhoji baadhi ya maswali!.

"Binti, mchungaji Nemeke Jana Usiku alilala Hapa nyumbani au hakulala!!?" Hilo lilikuwa ni Swali la kwanza ambalo Revina aliulizwa!.

"Alilala hapa nyumbani!?" Revina akiwa anatetemeka alijibu!.

"Eheee baada ya kulala nini kilitokea!?? Au usiku kuna Hali yoyote Isiyo ya kawaida ilitokea!??" Revina aliulizwa tena, Lakini Binti huyo mdomo wake Ulionekana kutetemeka yaani alikuwa haelewi ajibu Nini!.

"Okay afande Mika Huyu tunaondoka naye inaonekana kuna Vitu anajua!" Basi askari kiongozi wa msafara aliongea baada ya kuona Revina kashikwa na kigugumizi, baada ya hapo askari walielekea mpaka chumbani ambako ndo ilisadikika marehemu alikuwa analala yeye na Mkewe!.
Ndani ya chumba hicho palikuwa Safi kabisa na palikuwa pametandikwa vizuri kiasi kwamba hakuna kilicho tokea!.
Ila katika askari wanne walio ingia kule chumbani, kuna askari mmoja aliona madoa kama mawili ya Damu ukutani, Askari huyo aliamua kuvunga na wala hakuwashirikisha wenzake kitu alicho kiona!.

"Inaonekana Huyu Mtu hakulala hapa, Huyu Binti kuna Vitu kadanganya!" Baada ya ukaguzi basi askari kiongozi aliongea na kweli askari waliondoka pale nyumbani huku wakiwa wameambatana na Revina kuelekea naye kituoni.
Upande wa huku kituoni kijana Majaribu alikuwa anachezea kipigo cha maana huku akiwa anaulizwa maswali!.

"Kwa nini umemuua mchungaji Nemeke!?? Ulitumwa na Nani au ulishirikiana na nani!?" Hayo ni miongoni mwa maswali ambayo Majaribu alikuwa anaulizwa! Kijana Majaribu alijaribu kutoa maelezo Lakini swali zito lilikuwa ni kwamba alikuwa anafanya nini Porini Usiku ule!?.

"Kijijini kwetu walitaka kuniua wakidai Mimi ni Mwizi Kwa hiyo Katika Hali ya kukimbia Usiku ndo nilikutana na watu wanatupa Mwili Porini!" Majaribu alitoa maelezo Lakini badala ya kujiokoa ndo alijikuta anaongeza Matatizo!.

"Afande Gozi unaona, nimesema Huyu dogo anahusika! Ona anasema yeye ni Mwizi! Yaani huyu dogo muhuni kuna kitu anajua!" Basi kuna afande aliongea Kwa mizuka!.
Muda huo huo Revina naye alifikishwa pale kituoni Kwa ajili ya mahojiano zaidi!.

Lakini ilikuwa tofauti badala ya askari upelelezi kumhoji Revina kwenye chumba Cha upelelezi iliamuliwa kwamba Binti huyo apelekwe kwenye ofisi ya Mkuu wa kituo ndo akahojiwe huko tena na Mkuu!
Revina baada ya kufikishwa kule ofisini baada ya kutishiwa kidogo na Yule mkuu wa kituo, Revina alianza kuropoka kila kitu alicho shuhudia usiku! Yaani mpaka Yule mwanamke anaye fanana na Boss wake alimuelezea huku akiwa anahisi huwenda ni Boss wake.

"Binti Sikiliza ukitaka kuwa Salama hayo maelezo usije ukatoa sehemu yoyote utaenda kufia Jera au kufa kabisa, Nakuandikia maelezo Hapa chochote utakacho ulizwa hayo ndo Majibu itabidi uyatoe na huo ndo usalama wako!" Hayo yalikuwa maneno ya Mkuu wa kituo Cha polisi!.
Ni kweli Revina aliandikiwa maelezo kwenye karatasi na kuanza kuyameza kama yalivyo baada ya kama lisaa limoja alitolewa na kuruhusiwa arudi nyumbani!.

"Kwa maelezo ya Huyu Binti, kijana Huyu kuna Namna anahusika kwenye mauaji, maana Binti anasema kijana Huyu alikuja mchana pale nyumbani Kwa mchungaji!" Basi Mkuu wa kituo baada ya kutoka kumhoji Revina hayo ni maelezo ambayo alitoka nayo!.
Hapo kesi ilizidi kuwa kubwa na ngumu Kwa kijana Majaribu!.

Yule Dada ambaye alikuwa kampiga picha alikuwa kathibitisha kwamba alimuona Majaribu akikokota mwili na kuuleta barabarani! Hakika Majaribu alikuwa kapatikana yaani kila maelezo aliyo yatoa alionekana ni Muongo tu.

Mitaani taarifa ilikuwa ni Moja tu kuuawa kwa mchungaji Nemeke, yaani kila Mtu alikuwa anaongea lake!.

"Yaani nasikia mchungaji Nemeke alikuwa kwenye maombi huko milimani ndo alikutana na wauwaji!"

"Masikini Mke wake ndo kwanza yupo India nasikia anafanya matibabu ya mguu!"

"Nasikia muuaji ni Chali tu aisee! Hii noma!"

"Sema tuache yote kinacho niuma mwamba kafariki Bila hata kuwa na mtoto, yaani hajaacha chata yoyote kitaa"

"Hivi ni kweli Hana mtoto! Ujue kuna Kipindi nilisikiaga mchungaji kazaa na mwanamke wa Nje!?"

"Aaaaaa huo ulikuwa uvumi tu wa kumchafua Mchungaji, si unajua Mti wenye matunda ndo hupigwa Mawe!"
Hayo yalikuwa ni mazungumzo ya baadhi ya vijana kwenye vijiwe wakizungumzia Kifo Cha mchungaji Nemeke.
Ilikuwa ni Siku ya kuuaga mwili wa mchungaji Nemeke kwenye Moja ya kanisa kubwa ambalo lilikuwa lipo pale mjini, na ndo kanisani ambalo lilikuwa linaongozwa na mchungaji Huyo, kila muumini wa kanisa Hilo alikuwa analia kilio Cha Aina Yake!.
Na hiyo ndo Siku ambayo Mke wa mchungaji alikuwa anarudi kutokea India, na alirudi Huku akiwa kafungwa mhogo na bandeji za kutosha mguuni, yaani Kwa Jinsi ambavyo mwana Mama huyo alikuwa anajitirisha huruma kila Mtu alijikuta anamuonea huruma pale kanisani na ndo vilio vilizidi zaidi na zaidi.

Je Ipi hatima ya Kijana Majaribu!?? Je kijana Majaribu ni nani!? Na ipi Historia Yake!? Vipi kuhusu Mauaji ya Mchungaji itaku
aje? Na Sababu za kuuawa ni zipi!? Usipange kukosa miendelezo ya simulizi hii Tamu.

Tukutane Sehemu ya 3
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 3

Na hiyo ndo Siku ambayo Mke wa mchungaji alikuwa anarudi kutokea India, na alirudi Huku akiwa kafungwa mhogo na bandeji za kutosha mguuni, yaani Kwa Jinsi ambavyo mwana Mama huyo alikuwa ananitirisha huruma kila Mtu alijikuta anamuonea huruma pale kanisani na ndo vilio vilizidi zaidi na zaidi.

Pale kanisani vilikuwa ni vilio hata ibada haikufanyika ipasavyo, kitu ambacho kilikuwa kinawaliza wengi mchungaji Nemeke alikuwa ni Mtu anaye toa Muno na kusaidia watu maana alikuwa na Mali za kutosha, Pia alikuwa kajitolea kulea baadhi ya Watu wasio jiweza, kifupi Alikuwa anasaidia watu Muno Japo kuwa naye alikuwa na mapungufu Yake n madhambi yake ambayo ilikuwa Siri yake.
Basi baada ya Ibada Mwili wa mchungaji Nemeke ulipelekwa kwenye uwanja wa wazi , yaani hapo ilikuwa kama mafuriko Ya Watu walio jitokeza kumuaga!.

Siku Hiyo ilipita, Siku nyingine ilifika ikiwa ni Siku ya kupumzisha Mwili wa Nemeke! Yaani Mke Wake alikuwa analia anazimia na kuzinduka huku akiwa anashikiriwa na Watu!.
Binti Revina alikuwa anamkata Jicho Muno Boss Wake yaani yule Mke wa mchungaji, ni dhahiri Binti huyo alikuwa kaanza kubaini kitu!.

Revina akiwa Makaburini ambako Mwili wa marehemu ulikuwa unazikwa kuna Sura aliona pale makaburini, ilikuwa ni miongoni mwa Sura aliyo ishuhudia Usiku wa tukio pale nyumbani, Mtu huyo alionekana yupo mbele mbele kushugurikia maswala mbali mbali pale msibani!.

"Samahani Mama yule Baba aliyevaa suti ya Kijivu na tai nyekundu unamjua!?" Binti Revina aliamua kumuuliza Mama ambaye alikuwa kakaa naye Karibu!.

"Yes Yule ni katibu wa Jimbo Kwa hiyo ni mhusika mkubwa hapa maana mchungaji aliye fariki alikuwa kwenye Jimbo lake" Mama Yule alijibu kistaarabu, Revina hakuongeza Swali jingine lolote alitulia Huku akiwa na mawazo mengi Kweli kweli.
Binti Revina alikuwa ni mdada wa Kazi ambaye alikuwa kaajiliwa pale nyumbani Kwa Mchungaji, Binti Revina alikuwa hajawahi kuwajua wazazi wake maana alikuwa amekulia kwenye kituo Cha watoto Yatima na baada ya kufikisha Miaka 12 aliingia mtaani na kuwa mtoto wa mtaani mpaka pale alipo saidiwa na mchungaji Nemeke na kumfanya mtoto wa pale nyumbani anaye saidia kazi ndogo ndogo, mchungaji Nemeke alikuwa anamchukulia Revina kama mwanae tu, Lakini ilikuwa tofauti na Mke Wake ambaye alikuwa anamtesa Muno Revina, yaani ule upendo Ambao Revina alikuwa anaoneshwa na Mchungaji Nemeke ulikuwa unamkera Muno Mama mchungaji.

Basi Siku hiyo mazishi yalifanyika na Historia ilisomwa kwamba marehemu hajaacha mtoto yeyote! Ni watu wachache Sana Ambao walikuwa wanajua Siri ya mchungaji Nemeke na baada ya Historia kusomwa walibaki kucheka tu Chini kwa Chini.

Zilipita Siku kama mbili Huku kituoni Mambo yalikuwa yanazidi kuwa mazito Kwa kijana Majaribu, tayari kesi Yake ilikuwa imepelekwa mahakamani! Huku yeye akiwa ndo anaonekana kama muuaji!.

Baada ya Wiki Tatu kupita huku Majaribu akiwa ananyea debe Gerezani kama mtuhumiwa hatimaye Siku ya Kwanza kusikiliza kesi ilifika, Majaribu alikuwa haelewi chochote Kwanza alikuwa hana hata Mtu wa kumtetea! Alivyo fikishwa kizimbani na kuulizwa kama ana wakili yeyote Majaribu alibaki anatumbua Macho tu, maana alikuwa hajui hata wakili ni nani!.

"Jina Langu naitwa Majaribu, huyo wakili simjui" kijana Majaribu akiwa serious alitoa Jibu ambalo lilifanya Watu waanze kuchekea Chini ya meza, maana kucheka mahakamani ni mwiko, hata Hakimu alitamani kucheka!.

Baada ya kuonekana Majaribu hana Hata wakili Basi alianza kuulizwa maswali baada ya kusomewa mashtaka yake!.
Majaribu aligoma kabisa kuhusika na kifo Cha Mchungaji Nemeke, lakini Kwa Namna ambavyo alikuwa anaulizwa ni kama alikuwa analazimishwa kukubali makosa kwamba yeye ndo kaua.

Siku hiyo kesi iligairishwa, kijana Majaribu alirudishwa rumande, baada ya Siku kama mbili kuna askari alikuja kumtembelea Majaribu pale Gerezani!.
Alikuwa ni Askari ambaye Kwa Mara ya mwisho tulimuona kwenye upelelezi akificha Siri baada ya kushuhudia madoa ya Damu ukutani! Alikuwa anaitwa Afande Jedi!.

"Dogo nataka kukusaidia! Nambie ukweli kutoka moyoni wewe uliuwa au hukuuwa!?" Basi baada ya afande yule kukaa faraghaa na Majaribu alianza kumuuliza maswali!.

"Haki ya Mungu naapa, Mimi sijaua bro! Yule Mtu alitupwa na watu fulani usiku Porini na Mimi niliona!"

"Okay Vipi walivyo mtupa Wewe ulichukua hatua gani!? Na je uliwaona sura hao watu! Na walikuwa wangapi!?" Majaribu aliulizwa tena!.

"Kiukweli Mimi nilijificha mpaka walipo ondoka, Lakini nikiwa nataka kuondoka niligundua yule Baba bado hajafa nilienda kumfungua kwenye kile kiroba, ila kabla hajafa kuna Maneno aliniambia!" Majaribu alizidi kutoa maelezo!.

"Eheee! Alikwambiaje!??" Afande yule aliuliza, kijana Majaribu kwanza aliwaza alikumbuka Jinsi alivyo sisitiziwa na marehemu kwamba ile Siri asimwambie Mtu yeyote zaidi ya huyo aliyemtaja kwamba ni katibu wa kanisa!

"Aliniambia kwamba Mke wake Siyo Mtu mzuri!" Kijana Majaribu aliamua kuongea maneno machache miongoni mwa mengi aliyo ambiwa, mengine aliamua kuyaacha.

"Vipi walio utupa Mwili ukibahatika kuwatambua na ukiwaona unaweza kuwajua!?" Afande Yule aliuliza huku akionekana kuna Vitu ashaanza kuvijua!.

"Japo ulikuwa Usiku ila kutokana na mbalamwezi niliwaona vyema, walikuwa wanaumme wanne na Mwanamke mmoja, Tena nimekumbuka mwanamke yule nilismikia anasema anarudi India Kwa ndege ya kukodi!" Majaribu alitoa maelezo ambayo yalifanya afande yule atikise kichwa, kwanza alitoa Simu yake na kuingia Instagram alitafuta Jina la Rehema Nemeke, baada ya kuipata akaunti hiyo alitafuta picha mojawapo ambayo amewahi Post huyo Rehema!.

"Hii sura umewahi kuiona!?" Yule afande baada ya kufungua ile picha alimuonesha kijana Majaribu.

"Ndo Huyu Huyu mwanamke nilimuona Usiku ule, afande Mimi Macho Yangu yapo vizuri hata kuwe Usiku naona vyema ni Huyu huyu mwanamke tena alikuwa kavaa miwani!" Kijana Majaribu aliongea Kwa mizuka Huku akiwa anaona kama anaenda kupona hivi kwenye ile kesi!.
Ila mahojiano Yale yakiwa yanaendelea kuna askari magereza alionekana anasikiliza Kwa Siri, kifupi Alikuwa mkuda!.

"Sasa dogo sikiliza Hii kesi ni nzito kwako!? Hii Siri hatakiwa Mtu yeyote kuijua mpaka Siku ya kesi, na Siku hiyo Mimi ntakuletea mawakili, Wewe kazaa usimwambie Mtu yeyote sawa dogo!?" Afande Jedi aliongea Kwa msisitizo haswa, baada ya hapo aliondoka zake kurudi kituoni ambako alikuwa anafanyia Kazi!.
Afande Jedi baada ya kufika tu kituoni kabla hajaingia ndani alipo fika mapokezi tu alikutana na Barua ya kufukuzwa Kazi! Kwanza jicho lilimtoka huku akiwa haamini kama kibarua Cha uaskari kimeota nyasi!.

Afande Jedi akiwa na hasira alizama mpaka Kwa mkuu wa kituo hicho kuuliza sababu za yeye kufukuzwa Kazi!.

"Afande Jedi!?? Wewe umekuwa fukunyuku Muda mrefu Sana, yaani unapenda kufuatilia kesi ambazo hazikuhusu, Wewe Hii kesi ya kifo Cha mchangaji Nemeke haikuhusu hata kidogo na walio pewa kuipeleleza ni wengine, kinacho kuwasha na kuanza kuifuatilia ukaacha kesi zako ulizo pangiwa ni nini!!!?, Kwa mantiki Hiyo unadharau mamlaka inayo panga majukumu, mpaka hapo una Kosa la kudharau Mamlaka ambalo adhabu yake ni kufukuzwa kazi, kama ni onyo tushakupa Mara nyingi tu!" Hayo ni majibu ambayo afande Jedi alipewa na Mkuu wa kituo!.
Kwakuwa afande Jedi alikuwa anajua kinacho endelea aliamua kuondoka Kwa hasira, pamoja na hasira zake ndo hivyo kazi alikuwa hana tena!.

Siku zilizidi kusogea hatimaye mwezi mmoja ulikatika, Siku ya kurudi mahakamani ilifika tena!.
Kijana Majaribu aliulizwa kama anaye wakili, Lakini kila Mtu akiwa anaamini Majaribu Hana wakili Mara kuna Mzee wa makamo kidogo alisimama na kudai Yeye ndo mwanasheria atakaye msimamia Majaribu!.

Kesi ilianza kusikilizwa, Kwanza baadhi ya mashahidi waliletwa akiwemo Revina na yule Binti aliye Ona Majaribu akikokota Mwili kule porini.
Binti Revina alitoa maelezo ambayo alikuwa kamezeshwa, yaani aliyatoa kama yalivyo!.

"Ndugu hakimu napinga Maelezo ya huyo Binti, Kwa Upelelezi nilio ufanya ni dhahiri Kifo Cha Mchungaji kilifanyika pale nyumbani, na Kwa ratiba ya Mchungaji Siku hiyo ilikuwa siyo Siku ya maombi kwake!! Je tunaomba Shahidi athibitishe wakati anaenda kulala marehemu alikuwa kaondoka au alikuwa bado hajaondoka!?" Mwanasheria ambaye anamuwakilisha Majaribu alikuwa ni mzoefu kweli kweli yaani alikuwa na maswali ya mtego isivyo kawaida.

"Eeeeeee!! aaaaaa! Ninavyo Enda kulala Baba alikuwa eeee eeee! Alikuwa ameondoka!" Binti Revina akiwa anatetemeka alijibu!.

"Okay Wewe ulilala Saa ngapi na mchungaji aliondoka Saa ngapi!!?" Revina alipigwa Swali tena!.

"Nililala Saa Nne Baba aliondoka Saa Mbili Usiku!" Revina alijibu huku Mapigo ya Moyo yakiwa yanaenda kasi!.

"Mheshimiwa hakimu Huyu Binti anadanganya, Kwa maelezo ya Mlinzi wa getini amesema mchungaji aliondoka Jioni, Kwa Nini yeye anasema aliondoka Usiku!??" Mwanasheria Yule akiwa anazidi kusokomeza maswali! Hakimu aliamua kuahirisha kesi gafla baada ya kuona Binti Revina kaanza kupaliwa na maswali!.
Kijana Majaribu alifurahi na alianza kuona dalili za yeye kuokoka kwenye ule Msala!.

Basi Majaribu alirudishwa rumande, upande wa Afande Jedi naye akiwa kafukuzwa Kazi alizidi kufanya upelelezi wake Chini Kwa Chini, na kila kitu anacho kibaini alikuwa anamshirikisha mwanasheria aliye mtafuta yaani Yule Mzee.
Mpaka Siku ya kesi inafika Mr Jedi na Yule mwanasheria walikuwa wamebahatika kujua vitu vingi Muno! Jedi alikuwa anajua kabisa Kwa ushahidi walio ukusanya lazima kijana Majaribu ataachiwa! Haieleweki Kwa Nini afande Jedi alikuwa kachagua kumsaidia Majaribu!.

Siku Zote Pesa inaweza kubadili hata welekeo wa Maji mtoni! Mr Jedi hakuamini macho yake Siku ya Kesi ilipo wadia, yule mwanasheria wake alimgeuka, yaani badala ya kuwa upande wa Majaribu yeye alikuwa anamsokomeza na kumfanya Majaribu aonekane ni mharifu zaidi!.

"Ndugu Hakimu, mteja Wangu alikiri mbele Yangu kuhusika na tukio hilo ila anacho dai mchungaji Nemeke ndo alikuwa mwanzilishi wa ugomvi Kwa Madai kwamba alienda kufanya maombi Porini kwao!" Hayo ni maelezo ya yule mwanasheria ambayo yalifanya Mr Jedi na Majaribu mwenyewe wabaki wameacha midomo wazi pale mahakamani!.

Je ipi ha
tima ya Majaribu ambaye anaonekana kuwa kwenye wakati mgumu!??

Tukutane sehemu ya 4
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 4


"Ndugu Hakimu, mteja Wangu alikiri mbele Yangu kuhusika na tukio hilo ila anacho dai mchungaji Nemeke ndo alikuwa mwanzilishi wa ugomvi Kwa Madai kwamba alienda kufanya maombi Porini kwao!" Hayo ni maelezo ya yule mwanasheria ambayo yalifanya Mr Jedi na Majaribu mwenyewe wabaki wameacha midomo wazi pale mahakamani!.

"Muongo! Muongo Mimi sijawahi kuzungumza naye anaongea uong, kwanza simjui" Kijana Majaribu akiwa kapaniki huku akiwa yupo kizimbani aliropoka Kwa Sauti ya juu tena bila utaratibu wala kuruhusiwa na Hakimu!.
Kwanza Hakimu alipiga nyundo kwenye meza na kufoka!.

"Wote tutulie ni Muda Sasa wa kutoa hukumu!" Hakimu akiwa na Sura ya Kazi aliongea,na Kwa Jinsi Hakimu alivyo kuwa anaendesha Kesi ile alionekana ni kama ana Maelezo kabisa, yaani baada ya maelezo ya Yule wakili hakutaka kusikiliza maneno mengine tena.

"Majaribu Majaribu! Amepatikana na kosa la kumuua Mchangaji Nemeke kimakusudi kabisa Kwa kutumia siraha! Adhabu yake ni kifungo Cha maisha Gerezani na Kazi ngumu!" Hakimu akiwa anamaanisha alitoa hukumu baada ya hapo aligonga nyundo na kusimama kisha aliondoka!.
Mr Jedi alibaki kaacha mdomo wazi akiwa haamini kama dogo ndo anaenda kunyea Debe, pia kijana Majaribu alikuwa anaona kama ndoto, yaani alikuwa anaona Dunia nzima inamzomea!.

"Mbona sielewi naota au ni laivu imekaaje kaaje mpaka tunafikia huku aisee!" Kijana Majaribu alikuwa anajiuliza maswali ambayo yalikuwa hayana Majibu.
Kijana Majaribu kabla ya kupelekwa Huko Gerezani kwenda kuanza kutumikia adhabu hiyo kwanza aliomba akutane na katibu wa kanisa ili kama anaweza amuelezee Siri ambayo alikuwa kaambiwa na marehemu!.
Basi Muda ule ule taarifa zilimfikia Katibu wa kanisa, alikuwa ni Mama Mtu mzima kidogo.

Majaribu alipelekwa pale Gerezani kwa ajili ya kuanza Sasa kutumikia kifungo Chake huku ikiwa imepangwa kwamba baada ya Wiki Moja ahamishwe Gereza na kupelekwa gereza analo stahili kutokana na makosa yake.
Ikiwa ni majira ya Jioni Katibu wa kanisa alionekana kaambatana na Baba Mtu mzima wakiwa ndani ya Gari na safari yao ilienda kuishia mpaka pale Gerezani!.

Majaribu aliitwa Kwa ajili ya kwenda kuzungumza na katibu wa kanisa kama alivyo agizwa na mchungaji! Kabla hajakata kauli!.
Baada ya Majaribu kufika kwenye chumba Cha mazungumzo alishangaa kumuona Mama Mtu mzima akiwa kaambatana na mwanaume ambaye Sura yake ilikuwa siyo ngeni machoni pake!.
Majaribu alivuta kumbukumbu vizuri, ile Sura aliikimbuka kwamba ni miongoni mwa Sura alizo ziona pale porini Siku ya tukio!.

"Samahani Mama Wewe ndo Katibu wa kanisa au Huyu Baba!?" Majaribu macho yakiwa yamemtoka Huku akiwa anajiuliza maswali mengi Muno aliuliza!.

"Mini ndo Katibu wa kanisa na nimepokea ujumbe kwamba kuna Siri unataka kunipa!"Yule Mama alijibu!

"Okay tunaweza tukabakia wawili kwani!?" Majaribu aliuliza!.

"Usiwe na wasiwasi Wewe ongea tu huyu ni Mume Wangu wala usiogope!?" Yule Mama aliongea maneno ambayo yalifanya kijana Majaribu ashituke Muno!.

"Kijana usiwe na wasiwasi Mimi ni Mtu mwema! Ongea tu kila Kitu!" Yule Baba ambaye alikuwa ni Katibu Mkuu wa Jimbo aliongea, na alikuwa ni Baba ambaye alikuwa na familia Lakini alikuwa na mchepuko na mchepuko wake alikuwa ni yule katibu wa kanisa ambaye alikuwa anajulikana Kwa Jina la Melisa.

"Okay kitu ambacho marehemu aliniambia kabla ya kufariki aliniambia nikupe ujumbe kwamba mtunze mtoto wake na pia Mali Zake zote umsaidie mtoto wake azipate!" Kijana Majaribu baada ya kuona huwenda kuna kitu kipo nyuma ya pazia kinaendelea aliamua kuficha Siri ambayo aliambiwa na Mchungaji, aliongea tu maneno ya juu juu, yaani Majaribu Roho tu iligoma kumpa Yule Mama Siri.

"Kwani Vipi ndo hicho tu alicho kwambia!? Hakuna kingine!?" Mama yule Kwa Jina la Melisa au Katibu wa kanisa aliuliza huku akionekana kukerwa na taarifa nyepesi kama zile!.

"Ndiyo Mama ndo hicho tu nilitaka nikwambie!" Majaribu alijibu!, Basi Mama Yule na bwana yule waliondoka pasina kuongea Neno lolote wala kutoa asante Kwa Majaribu Kwa ile taarifa!

"Inawezekana Vipi Mtu aliye husika na kifo yupo na Mtu niliye ambiwa nimpe Siri!? Au Huyu Mama ndo aliwatuma na yule Baba hakujua!?? Uuuuu!! Mbona sielewi hii Siri ntabaki nayo Mimi mwenyewe mpaka kufa Kwangu!" Kijana Majaribu alijikuta anapata mawazo mengi Muno!.

Basi Siku hiyo ilipita! Zilipita Siku nyingine kama Tatu hivi!, Mr Jedi alionekana ni Mtu anaye dhurura huku na kule kutafuta taarifa ili kujua ukweli kuhusu Kifo Cha Mchungaji Nemeke!.
Mr Jedi alikuwa ni Mtu mwenye kipaji Cha pekee linapo kuja swala la upelelezi kitu ambacho alikuwa hajajaliwa ni elimu kubwa ambayo alikuwa hajaipata, yaani alikuwa na Elimu ya kawaida kiasi kwamba hata pale kituoni alikuwa ni askari asiye na cheo Chochote mpaka anafukuzwa, ila Mr Jedi alikuwa ni Mtu mwenye kipaji Cha kupeleleza Jambo na akajua ukweli, yaani kuna Muda alikuwa anatumia mpaka hisia kwenye kupeleleza na hakosei!.

Haieleweki ni Kwa Nini Mr Jedi alikuwa kaamua kulivalia swala lile njuga na kulifuatilia kiundani.
Baada ya Mr Jedi kupeleleza Kwa Siku kadhaa kuna Vitu Vingi alivigundua na Siku hiyo aliamua kwenda Gerezani kuonana na kijana Majaribu ili aone Namna ya kumsaidia maana alikuwa na asilimia zote kwamba Majaribu hajauwa!.

Kijana Majaribu baada ya kuitwa na kuambiwa kwamba kuna mgeni wake alitembea haraka Muno kwenda kuona mgeni aliye mtembelea, ila baada ya kuiona Sura ya Mr Jedi Majaribu alinyong'onyea maana alikuwa anaamini Yule ni miongoni mwa watu walio fanya yeye awe pale!.

"Bro kuna Nini tena!?? Wewe na yule Mzee wako si mliamua kkkunichoma!? Eheee umefuata nini hapa!?" Majaribu akiwa na Hasira aliuliza!

"Hakuna Mtu atakaye kusaidia zaidi Yangu! Napambana usiku na mchana Wewe utoke, nilipambana hata mwanzo ila Yule Mzee pesa zilimpumbaza na hatimaye mahakamani alitugeuka" Mr Jedi alitoa maelezo ambayo yalifanya walau kijana Majaribu akae kusikiliza kile alicho itiwa!.

"Eheee kilicho kuleta ni kipi!?" Majaribu aliuliza!.

"Sikiliza kuna Vitu kadhaa nimevijua kuhusu marehemu, kwanza nimegundua mkewe wa Ndoa ndo aliye husika na kifo Chake kushirikiana na baadhi ya watu na sababu ya mkewe kumuua mchangaji Nemeke Sina uhakika nayo Saana ila nahisi ni baada ya kutambua mumewe ana mtoto Nje ya Ndoa! Japo bado nazidi kulifuatilia!" Mr Jedi aliongea maneno ambayo yalimgusa kidogo Majaribu na alikumbuka hata maneno ya mchungaji kwamba kuna Dhambi aliifanya!!

"Heeeee inamaana yule Baba, mtoto ambaye alikuwa anamzungumzia ni mtoto wa Nje ya Ndoa!!!??" Kijana Majaribu akiwa kajisahau alijikuta anaropoka!.

"Unasemaje!? Marehemu alizungumzia kuhusu mtoto!? Ebu dogo eleza kila kitu alicho kwambia marehemu kabla hajafarika ili tujue tunatatua vipi hili tatizo!"

"Aaaaaa!! eeee!! Hapana bro hakuniambia kitu chochote! " Majaribu baada ya kugundua kazingua aliamua kupotezea, ila Mr Jedi aligundua kwamba kuna Siri lazima kijana Majaribu anazijua kuhusu marehemu na huwenda aliambiwa na marehemu kabla ya Kifo Mambo mengi tu.

"Okay sikiliza Kijana ngoja nikupe maelezo kifupi nilicho kibaini kuhusu marehemu, na Wewe utaniambia unacho kijua kumhusu ili Lengo letu la wewe kuwa Huru litimie, marehemu Nemeke na Mke Wake anaye fahamika Kwa Jina la Rehema walifunga Ndoa Miaka kama ishirini na kitu iliyo pita,
Kwa maelezo niliyo yapata wawili hao walidumu kwenye Ndoa Karibu Miaka nane pasina kupata mtoto, na walipotembelea hospital iligundulika mwanamke hana uwezo wa kubeba ujauzito, hapo ndipo uvumilivu ulimshinda mchungaji Nemeke aliamua kuchepuka na kwenda kuzaa Nje!.

Ila swala la yeye kuzaa njee inasadikika ilikuwa ni Siri kubwa Muno Ambayo ni baadhi ya watu wachache tu ndo walikuwa wanaijua, mchungaji Nemeke inasemekana alikuwa anatuma matumizi Kwa Siri Kwa Mtu ambaye alikuwa anamlea mtoto wake, na baadhi ya Miaka kumi na kitu kupita baadhi ya watu walianza kuijua Siri ambayo mchungaji alikuwa hataki ijulikane Kwa kuhofia Sifa Yake Kuvunjika!.
Ila Kwa Upelelezi kidogo nilio ufanya inasadikika Hivi punde Siku za hapa Karibuni Mke wake Rehema aligundua Siri ya Mumewe kuwa na mtoto nje, kitu ambacho Bado sijakipatia Jibu ni je Kwa Nini Mke wa mchungaji aliamua kumuua mumewe! Na je huyo Mtu ambaye anamlea mtoto wa mchungaji ni nani!? Kifupi ipo hivyo, Sasa Kijana kama kuna Siri unajua naomba nambie!" Mr Jedi Kwa Upelelezi wake ulio Shiba Ambao alikuwa kaufanya Kwa njia anazo jua yeye hayo ni machache ambayo alikuwa kayabaini.
Kijana Majaribu hapo kuna kitu alikibaini kichwani Mwake japo hakutaka kumshirikisha Mr Jedi, maana ni dhahiri kwamba Bado alikuwa hamuamini hata kidogo!.

Kwanza Majaribu alimwangalia Mr Jedi Kwa makini machoni pake, aligundua Bwana huyo kuna uongo kaongea kuhusu yale maelezo yake!

"Kwanza brother Kwa Nini wewe unataka kunisaidia!?" Majaribu aliuliza

"Majaribu Siku zote Mimi napenda Haki, sipendi Mtu anaye onewa?" Mr Jedi alijibu!,basi Majaribu aliitikisa kichwa kuonesha kakubali Japo alikuwa hajamuamini Kwa asilimia zote Mr Jedi.

"Bro kuna Mtu Mama Mtu mzima kidogo ni Katibu wa kanisa la marehemu, mtafute Yule au mfanyie upelelezi Nadhani utajua kitu kuhusu mtoto wa marehemu, maana mchungaji kabla hajafa alimtaja huyo Mama kwamba amtunze mtoto wake vyema!!" Kijana Majaribu alitoa maelezo ambayo yalifanya Mr Jedi apate Kazi nyingine ya kufanya!.
Mr Jedi alitoka pale Huku kazi inayo fuata ikiwa ni kumpeleleza Katibu wa kanisa na kujua kila kitu kumhusu!, Yaani Lengo la Mr Jedi alikuwa anataka kabla ya kukataa rufaa ya Kesi ya Kijana Majaribu basi awe na ushahidi ulio shiba!.

Upande wa Huku nyumbani Kwa marehemu mchungaji Nemeke, Binti Revina alikuwa Siyo mfanyakazi wa ndani tena, yaani baada ya Mke wa Mchungaji kugundua kwamba kuna Siri Revina anazijua kumhusu basi alimfanya Binti huyo mfalme pale ndani kila anacho kitaka alikuwa anapata, na alianza kumtuma kwenye baadhi ya mambo yake ya Siri, yaani kifupi tunasema Revina aligeuka chawa wa Mama Mchungaji.
Siku Hiyo pale nyumbani Kwa mchungaji kikao kizito kilikuwa kinaendelea, Mabishano makubwa yalikuwa yameshika kasi, ni kundi la Watu kama Saba Hivi walikuwa wamekaa wanabishana!.

"Rehema huo ni uzembe Siku zote Hizo unashindwaje kupata nyaraka zilipo, haya Sasa utajuaje Mali zote za Mchungaji ikiwa Mali nyingi alikuwa anaziweka Siri!? Au kuna Namna unataka kutuzunguka tusipate share!?"

"Siyo hivyo jamani nimejaribu kutafuta nyaraka hapa nyumbani sijaona, nyaraka zote ambazo nilikuwa najua ni nyaraka kumbe ni kopi tu! Yaani mpaka sielewi Nemeke alikuwa kaficha wapi Siri Zake!

"Uuuuu!! Haya tunafanyaje Sasa bila kuwa na nyaraka!?"

"Jamani Labda mpigieni Simu Melisa muulize maana inasadikika yeye ndo alikuwa Mtu wa Siri anaye jua mtoto wa Nemeke anako lelewa!?"

"Mrisho unaona Ninavyo sema tunafichana Siri!? Kumbe nyie mlikuwa mnajua kwamba Nemeke ana mtoto!? Na huyo Melisa ndo mpanga mipango, Sasa naomba Melisa aje hapa ajibie huyo mtoto yuko wapi maana huwenda huyo ndo alipewa nyaraka zote na Mume Wangu" Mama mchungaji aliongea Kwa jaziba.

"Rehema tuliza jaziba kila kitu kitakaa Sawa!"

"Siwezi kutulia! Mume Wangu alikuwa anataka aache Uchungaji kisa huyo mtoto unahisi angeshindwa kumuachia kila kitu kama alivyo niropokea!?" Mama mchungaji alikuwa anazidi kuuwasha Moto kwenye kikao kile, yaani mabishano yalikuwa makubwa, inaonekana Bado kuna Siri zilikuwa zipo Chini kwa Chini.

Je Siri Gani zipo Chini Kwa Chini!? Kwa nini Nemeke aliuawa!? Ip
i hatima ya Kijana Majaribu!?? Mr Jedi Kwa nini anafuatilia Sana swala hili!?

Tukutane sehemu ya 5
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 5

"Siwezi kutulia! Mume Wangu alikuwa anataka aache Uchungaji kisa huyo mtoto unahisi angeshindwa kumuachia kila kitu kama alivyo niropokea!?" Mama mchungaji alikuwa anazidi kuuwasha Moto kwenye kikao kile, yaani mabishano yalikuwa makubwa, inaonekana Bado kuna Siri zilikuwa zipo Chini kwa Chini.

"Ebu subirini Ngoja tumpigie Simu Melisa!" Mmoja wao aliongea, Basi ni kweli Muda ule ule Simu ilipigwa Kwa huyo Katibu wa kanisa ajulikanae Kwa Jina la Melisa na aliambiwa Aje Kwa mchungaji Muda ule ule!.
Ilipita kama Nusu Saa Mama Yule ambaye alikuwa Katibu wa kanisa alifika pale nyumbani kwa Mchungaji, baada ya kuingia ndani na kukuta watu wamekaa wamenuna alishituka kidogo!.

"Melisa ebu naomba nambie mtoto wa Nemeke yuko wapi!? Na unajua nini kuhusu nyaraka za Siri za marehemu Mume Wangu!?" Baada ya kufika tu Mama mchungaji aliuliza Kwa jaziba!.

"Haya ndo mambo sipendagi ndo maana nilikuwa sitaki kuja Mimi! " Mwanamama Melisa alijibu!

"Jamani tukae Kimya! Mbona ni Mambo madogo tu! tuende Hoja Kwa Hoja!" Basi Baba Mtu mzima ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Jimbo alizungumza, na Baba huyu naye alionekana ana mambo yake katika lile Swala!.

"Melisa ebu toa maelezo Yote kama marehemu alivyo kwambia hapa lazima tufikie muafaka!" Baba Yule alizungumza huku akionekana anamkonyeza Melisa Kwa Siri!.

"Okay, ni Kweli Nemeke alizaa mtoto na mwanamke mmoja hivi, ambapo mwanamke huyo alifariki Kwa ajali na mtoto alimuacha kwenye mazingira magumu, hapo ndipo mchungaji Nemeke aliamua kuniomba Mimi nisimamie malezi ya mtoto Yule, Basi ili nisitengeneze picha mbaya na kuendelea kuficha Siri Yule mtoto kuna sehemu ilibidi nimpeleke Kwa ajili ya malezi yake, Japo kika Siku nilikuwa namwangalia na mchungaji Nemeke alikuwa anatoa matumizi!.
Baada ya Miaka kadhaa kupita mtoto kuwa mkubwa mchungaji Nemeke alinipa maelezo kwamba mwanae inatakiwa ajulikanae rasmi maana ndo mrithi wake wa pekee na kama ni Uchungaji Bora aache kuliko mwanae aendelee kuishi kiyatima Wakati Yeye yupo.
Mchungaji alimtafuta mpaka mwanasheria na Sijui Vitu Gani aliongea na mwanasheria kuhusu mwanae! Mpaka mchungaji Nemeke anafariki hayo Ndo alikuwa kaniachia! Na juzi nilivyo enda Gerezani Yule mtoto aliye husika na kifo chake anasema kabla mchungaji hajafa alisema kila kitu chake ni Cha mwanae!." Mwanamama Melisa alitoa maelezo! Lakini maelezo yake asilimia kubwa yalionekana ni maelezo ya kutungwa!.

"Haiwezekani! Mr Luka unaona maelezo anayo toa Huyu Mwanamke! Yaani mtoto ambaye hajulikani eti ndo arithi Mali! Ebu kamlete mtoto huyo hapa!" Mama mchungaji aliongea Kwa kupaniki!.
"Jamani hapa inabidi tuyajenge Kwa Haki, Mtoto wa mchungaji Nemeke ana Haki Zake Pia Mke wake naye ana Haki Zake hatuwezi kumpuuzia mmoja! Hapa kilichopo ni ijulikane nyaraka ziko wapi then kila Mtu atapata asilimia zake!" Katibu wa Jimbo alitoa maelezo ambayo yalifanya Mama mchungaji agune Japo bado alikuwa hakubaliani na hilo ila aliona ni sawa tu Bora iwe hivyo!.
Basi kikao kile kilitamatika Kwa watu wale kukubaliana kumtafuta mwanasheria ambaye ilisadikika Mara ya mwisho aliachiwa maelezo na mchungaji Nemeke, pia wamlete na mtoto wa mchungaji Nemeke.

Basi Siku hiyo ilipita, Siku iliyo fuata kijana Mr Jedi alionekana nyumbani Kwa Melisa yule Katibu wa kanisa! Mama huyo alikua ni mjane, yaani tangia mumewe afariki miaka kadhaa iliyopita alikuwa hajawahi kuolewa tena!.
Mr Jedi baada ya kufika pale aliruka ukuta na kuingia ndani, ilikuwa ni Jioni Mida ya Saa Kumi na Moja, Mr Jedi alijua lazima Muda huo Mama huyo atakuwa yupo kanisani!.

Mr Jedi alikuwa na funguo za bandia, alifungua ndani na kuingia baada ya hapo alitegesha camera yake vizuri kabisa pape sebuleni, yaani ambayo ina rekodi Sauti na video na aliiweka sehemu ambayo alikuwa anajua hakuna Mtu anaweza kuona, baada ya kufanya hivyo aliondoka!.
Masaa yalisogea! Mida ya Saa Moja Jioni ndo Mida ambayo Melisa akiwa na mdogo wake pamoja na mdada wa Kazi walifika pale nyumbani!.

"Naya uache uzembe Sasa! Dili linaenda kufanikiwa wewe unaenda enda Shuleni Kwa Habir, unaenda kufanya nini Sasa!??"basi baada ya kufika pale nyumbani mwanamama Melisa alimuuliza mdogo wake!.

"Dada Melisa, Damu nzito kuliko Maji ujue, mwenzako najikuta tu nashindwa kuvumilia yaani namumiss mwanangu" Dada Yule Kwa Jina la Naya ambaye alikuwa mdogo wake na Melisa alijibu!.

"Sasa Wewe jishaue uje uharibu Dili wakati tupo mwishoni Mwishoni,na Luka akijua unaenda enda Shuleni Kwa mtoto Mara Kwa Mara sidhani kama atafurahi!"

"Eeeeeee Dada na wewe bwana na huyo Luka wako! Utafikiri sijui nani, Mtu mwenyewe Mume wa Mtu unavyo mpapatikia Sasa kama dhahabu!"

"We mtoto Wewe koma eee! Ulivyo kuwa unazaa naye hukujua kama Mume wa Mtu!"

"Eeeeeee Dada nawe! Haya yaishe basi!"
Hayo yalikuwa mazungumzo ya Melisa na Naya, na mazungumzo ya wawili hayo yalionekana yana Siri kubwa iliyo jificha ndani yake! Muda huo huo mlango uligongwa na Mtu aliye ingia alikua ni Mr Luka yule Katibu mkuu wa Jimbo!.
Basi Melisa na Luka walikumbatiana kimahaba na kupigana busu mbele ya Naya na Dada wa Kazi!.

"Eeeeeee!! Naya macho Gani hayo si muende Jikoni basi umbea tu!" Melisa aliongea Kwa Sauti ya wivu huku akiwa anamwangalia mdogo wake! Na inaonekana Naya kipindi Cha nyuma alikuwa Mtu wake na Luka mpaka wakazaa mtoto! Sasa nini kilitokea mpaka Melisa ndo yupo na Luka tutajua yote!.
Basi Naya akiwa anaumia ndani Kwa ndani alielekea chumbani kwake huku Dada wa Kazi akielekea Jikoni!.

"Uuuuu! Mr Luka ujue Jana ulinifurahisha Muno kipenzi!" Melisa aliongea!.

"Kuhusu nini Dear!"

"Si pale nyumbani Kwa Mama mchungaji! Yaani ulivyo mpangilia kuhusu mgao mpaka nilikuta ameanza kuregea! Ila Luka kipenzi kwenye hilo Dili nimekuamini! Kwenye mgao wa Habiri Nusu Yangu Nusu Yako! Isitoshe Wewe utapata Mara mbili maana hata Mama Mchungaji atakupa asilimia!" Melisa aliongea tena akionekana yupo serious!.

"Kuhusu hilo usijali! Ila wasiwasi Wangu ni huyu mdogo Wako Naya, ebu ongea naye atulize komwe lake asije akaharibu wakati Mambo yapo mwisho!"

"Dear kuhusu naya usijali hawezi fanya hivyo!"

"Basi kama ni hivyo vizuri! Kuhusu mwanasheria nimeongea naye kila kitu nimempangalia na amesema yupo vizuri katika Hilo ila amesema kabla ya Kazi lazima apewe kwanza laki mbili!"

"Okay haina Shida!"
Wawili hao waliongea mipango yao, baada ya hapo walitiana mabusu ya kiutu Uzima, baada ya kuona wamepandwa na midadi walibebana mpaka chumbani!.
Mr Jedi yeye alikuwa anaangalia tu kwenye laptop yake kile kinacho endelea nyumbani Kwa Melisa, yaani kila kitu ambacho kilikuwa kinatokea kilikuwa kinarekodiwa Haswa vinavyo fanyika pale sebuleni!.

Basi Siku zilizidi kusogea! Mwezi mmoja ulipita huku kijana Jedi akiwa Bado anafuatilia, na alionekana ana machungu kweli kweli Katika ile Kesi, Yaani alikuwa anafuatilia hatua Kwa hatua!
Basi Siku hiyo ikiwa ni usiku Mr Jedi akiwa mtaani alikutana na bango kubwa likiwa limebandikwa picha ya Mchungaji Nemeke yaani waumini waliamua kwenda kuiweka picha ya Mchungaji Nemeke kama kumbukumbu kwenye bango kubwa la barabarani!.
Mr Jedi aliangaza huku na kule baada ya kutoona Mtu, lile bango kubwa aliling'oa na kulivunja Kwa hasira!, Yaani alionekana ana hasira Haswa na Marehemu mchungaji Nemeke!.

Siku nyingine Iliyo fuata Mr Jedi alienda kwenye Moja ya shule za private pale mjini, na Kwa Namna alivyo ingia pale getini na kuchangamkiana na mlinzi ilionekana Siyo Mara ya kwanza kwenda pale!.
Ila Siku hiyo baada ya kufika pale Shuleni alishangaa anaiona sura ya Melisa na Mr Luka, kwanza ilibidi ajibane sehemu kuona kipi wamekifuata!.

Baada ya dakika chache aliwaona wawili wale wakitoka na kijana mmoja Kwa Jina la Habir, alikuwa ni mtoto anaye soma kidato Cha pili Katika Shule Hiyo!.

"Heeeee mbona bado sielewi! Huyu Habir ni mtoto wa mchungaji Nemeke au wa huyu Bwana!" Mr Jedi alijiuliza swali ambalo hata hivyo hakupata Majibu, Kwanza Siku hiyo aliamua kwenda mpaka ofisini pale Shuleni kuuliza Jina kamili la kijana Yule aliye toka pale!.

"Huyu anaitwa Habir Nemeke!" Mr Jedi alijibiwa hivyo na Mwalimu baada ya kuuliza!.
Muda huo Melisa na Luka walionekana wakifika pale nyumbani Kwa mchungaji Nemeke wakiwa na mtoto Habir! Huku na watu wengine kama watano wakifika pale Kwa mchungaji na ilionekana kuna kikao kizito kinaendelea! Lakin kijana Jedi alionekana hayupo Mbali na maeneo yale maana baada ya kutoka pale Shuleni na kuona wawili wale wametoka na mtoto aliamua kufuatilia nyuma, Mr Jedi alikuwa anapiga mahesabu ya kuingia Mule ndani baada ya kuona kundi la watu kadhaa wameingia.

Je ipi Siri ipo n
yuma ya pazia!? Habir ni mtoto wa Nemeke!!? Itakuwaje!?

Tukutane sehemu ya 6
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 6

Muda huo Melisa na Luka walionekana wakifika pale nyumbani Kwa mchungaji Nemeke wakiwa na mtoto Habir! Huku na watu wengine kama watano wakifika pale Kwa mchungaji na ilionekana kuna kikao kizito kinaendelea! Lakin kijana Jedi alionekana hayupo Mbali na maeneo yale maana baada ya kutoka pale Shuleni na kuona wawili wale wametoka na mtoto aliamua kufuatilia nyuma, Mr Jedi alikuwa anapiga mahesabu ya kuingia Mule ndani baada ya kuona kundi la watu kadhaa wameingia.

Basi baada ya Jedi kuhakikisha wote wameingia Mule ndani! Naye alisogea mpaka pale Getini na alimkuta Mlinzi akiwa kakauka koo mpaka Siyo vizuri!.

"Oya dingi kuna Laki Moja Hapa kuna Kazi nataka unisaidie!" Jedi alimshawishi yule mlinzi, kwanza mlinzi baada ya kusikia Laki Moja macho yalimtoka kama kaona dhahabu Chini imetelekezwa, maana mshahara wake wenyewe Kwa mwezi mzima ulikuwa haufiki hata hiyo Laki!.

"Kazi Gani hiyo mwanetu! Yaani hapa nina hamu na ugoro kuliko Kawaida ebu nipe niishi nayo Mimi napiga mishe yoyote!" Yule mlinzi aliongea Kwa mizuka!.
Basi Jedi alitoa kakifaa kadogo mithiri ya kifungo Cha sharti, Kalikuwa ni kadogo Lakini Kalikuwa na uwezo wa kunasa Sauti kuliko Kawaida!.

"Chuku hii kitu nenda mpaka ndani sebuleni pale walipo kaa hao Wageni walio ingia kadondoshe Chini au kaweke popote ambapo hakawezi kuonekana, yaani tumia njia yoyote ile!" Jedi aliongea baada ya kumkabidhi kale kakifaa!.
"Eheee dingilai baada ya hapo kingine nafanya nini!"
"Hakuna kingine, ukishafanya tu hivyo basi!"
"Heeeee masihara haya dingi! Yaani hivyo tu unanitia Laki!"
"Ndiyo!" Jedi alijibu
Basi yule mlinzi akiwa na mizuka na pesa aliyo ahidiwa alizama ndani kama hana akili vizuri!.

"We Yoctan! Umeanza lini kuingia ndani! Tena unaingia kama kirabuni, ebu toka nje umefuata nini humu!?"basi Mama mchungaji alifoka kweli kweli baada ya kumuona mlinzi kaingia ndani kichwa kichwa.

"Boss samahani kuna Jamaa yupo nje amekuja kuomba Kazi, nimemwambia ngoja nimuulize Boss Ndo maana nimekuja" Mlinzi yule aliongea uongo, ila tayari alikuwa kakiweka kile kifaa kwenye sofa!.

"Kwa Hiyo we huna akili ya kujiongeza, unataka ufukuzwe kazi yeye ndo aajiriwe Siyo! Ebu nitokee hapa kamwambie Kazi hamuna!" Mama mchungaji alimjibu Kwa hasira, na kweli mlinzi Yule alitoka huku akiwa haamini kama atapewa Hiyo Laki au laaa!.
"Daaaa akinipa hata Ten naishi nayo mbona!" Yule mlinzi akiwa fast kutoka nje alijiongelesha! Basi alifika pale getini alimkuta Jedi katulia!.

"Mwanangu tayari Kazi yako! Nigei Basi changu!" Mlinzi yule aliongea Kwa midadi! Basi Jedi aliweka earphone zake Masikioni huku akiwa kaunganisha kwenye Simu na kufungua program maalumu ambayo ilikuwa imeunganikana Moja Kwa Moja na kifaa kile, baada ya kuthibitisha mambo yapo vizuri alichomoa Pesa kama Laki mbili na kumkabidhi yule mlinzi!.

"Mwanangu ishi nayo Hiyo Laki mbili, kuanzia Leo utakuwa mwana kuna madili madogo madogo kama haya ntakuwa nakupa!" Jedi aliiongea baada ya hapo aliondoka!.
Yule mlinzi alikuwa anaona kama anaota kwanza alimwangalia Jedi Mara mbili mbili huku akiwa haamini!.

"Heeeee yule mwana Mwizi au jambazi, yaan kirahisi Hivi kanipa laki mbili, au lile ni bomu anataka kuripua hapa, au ni mtego!? "Yule mlinzi alibaki na maswali ambayo hata hivyo aliamua liwalo na liwe!.
Huku ndani mjadala ulikuwa ni mkubwa Muno! Mwanasheria alikuwa ameitwa atoe ufafanuzi ambao marehemu Nemeke alimuachia!!

"Jamani Mimi kiukweli mchungaji Nemeke hakuniambia mambo mengi! Kitu alicho nambia ni kwamba Mali Zake zote zitakuwa Mali za mtoto Wake, na alinionesha picha ya mwanake pia alinipa vipimo vya DNA endapo itatokea Mtu atapinga, na huyu ndo mtoto wake aliye nionesha ni hivyo tu" mwanasheria yule alitoa maelezo!.

"Haiwezekani jamani! Iweje museme alisema Mali zote za mtoto wake alafu mseme hati Miliki hakuacha, Mr Luka au Huyu Mwanamke kuna mchezo anataka kuufanya, alafu na Wewe unamtetea badala ya kuwa upande Wangu!"Mama mchungaji aliongea!.

"Jamani Mimi naona hakuna haja ya ugomvi tulikubaliana kwamba Mali zote hawezi kuchukua mtoto! Lazima agawane na Mama mchungaji! Kuhusu hati Miliki hiyo Siyo Shida Sana zitatengenezwa tu zingine kikubwa tuende kwenye Sheria mgawo ufanyike Sawa!" Mr Luka aliongea!.
Siku Hiyo walipanga mipango Mingi Muno na mwishowe walikubaliana kila Kitu.

Kijana Jedi alikuwa kakaa getoni kwake akiwa anasikiliza kila Kitu kilicho zungumziwa huku akiwa anarekodi.
Jedi alikuwa anaishi pekee yake kwenye geto la chumba kimoja na sebule, Na ilikuwa nyumba ya Kawaida. Jedi alikuwa na maisha ya kawaida Muno Haswa baada ya kufuzwa Kazi ndo kabisaa Maisha yalikuwa magumu! Pamoja na ugumu wa maisha alijikunja na kumpatia mlinzi Laki mbili kwa sababu alikuwa na maana Yake!.

Siku Nazo hazigandi, mwezi mwingine ulikatika! Upande wa Huku Kwa kijana Majaribu, kijana huyo alihamishwa gereza na kupelekwa gereza jingine ambalo waharifu wa Mauaji ndo walikuwa wanapelekwa! Japo kuwa Gereza hilo halikuwa mbali Sana na Mji, yaani ilikuwa ni Nje kidogo ya Mji!.
Maisha mapya Kwa Majaribu yalianza, mwanzo kijana Huyo alikuwa anaishi Kwa kuteseka Muno, yaani pale Gerezani Yeye ndo alikuwa mnyonge wa kila Mtu kutokana na udogo wake! Ila baada ya miezi kama mitatu kupita alijenga urafiki na mbabe mmoja wa pale Gerezani ambaye alikuwa anaitwa Nesto, mbabe huyo pale Gerezani alikuwa anaogopwa Haswa na alikuwa na vijana wake kama wawili.
Chanzo Cha urafiki ni pale kijana Majaribu alipo onesha kipaji Cha Wizi, yaani alikuwa anaibia wafungwa wenzake na kupeleka Kwa Nesto!.

Majaribu hakika alikuwa Mwizi, yaani ilifika kipindi alianza kuibia mpaka askari magereza! Yaani hata sehemu iwe nyembamba vipi Majaribu alikuwa anapita!, Pia pamoja na udogo wake Wote hakuna ukuta ulikuwa unamshinda kuruka!!
Siku Hiyo pale Gerezani kuna kiongozi mkubwa wa Serikali alikuwa anakuja kufanya ukaguzi na zaidi zaidi alikuwa anakuja kuwakagua askari magereza utendaji wao wa Kazi, na pia kuwakagua wafungwa kwamba wanaishije!!

Pale Gerezani kuna askari magereza alikuwa hapendwi na kila mfungwa, yaani alikuwa mnoko na pia alikuwa na Roho mbaya! Yaani alikuwa anachukiwa na wafungwa kuliko hata mavi, pia kutokana na unoko wake mpaka askari magereza wenzake walikuwa hawampendi!.
Basi Siku hiyo kiongozi huyo wa Serikali alifika pale Gerezani na Mkuu wa Gereza alimpokea Kwa heshima!.

Muda huo wafungwa wote pale Gerezani kila Mtu alikuwa anahaha kuficha kitu chake ambacho hakiruhusiwi kuwa nacho pale Gerezani! Haswa ilikuwa ni bangi! Lakini katika Hali ya kushangaza kila Mtu mzigo wake Haswa bangi zilikuwa hazipo pale anapo fichaga! Ilikuwa ni ndani ya sekunde mbili tu kila Mtu aliibiwa Bangi Zake!.

"Oya Wazee Mali Yangu mbona Sioni"

"Hata Mimi Sioni!"

"Kudadeki au yule afande mnoko kachukua!?"

"Sema poa tu hata hivi katusaidia! Wakija kuuliza ni kumkataa!"
Hayo yalikuwa mazungumzo baadhi ya wafungwa mule Gereza!, Muda huo kijana Majaribu alikuja akiwa anahema haswa!!.

"Oya dogo au Wewe ndo umeiba Mali!? Maana dogo Kwa Wizi hujambo!" Basi kuna Jamaa aliuliza!.

"Oya nyie tulieni Afande Pablo mtapata habari Zake!" Kijana Majaribu aliongea huku akiwa anahema, Na kweli hazikupita dakika hata Tatu wafungwa wote waliitwa kwenye paredi!.
Baada ya kufika paredi walikuta yule afande magereza mnoko yupo Chini ya ulinzi huku mifuko ya Bangi ikiwa pembeni yake!.

"Okay! Jamani tunataka kuuliza, huyu afande anadai kuna Mtu kamuwekea Hizi bangi, je mnakubaliana na Hilo!? Na je kuna taarifa yoyote mnaijua kuhusu huyu askari!" Basi kiongozi aliye kuja kufanya ukaguzi aliuliza!.
Ukisikia watu kumsagia Mtu kunguni , hakika Siku hiyo yule afande mnoko alichomekewa yaani alisagiwa kunguni kweli kweli! Na wafungwa wote waliropoka kwamba ndo huwaga anawauzia Bangi!.
Basi askari yule mnoko Siku hiyo hiyo kazi iliisha na alienda kupewa hukumu kama muuza bangi!.

Pale Gerezani kuanzia Siku hiyo kijana Majaribu aligeuka shujaa, yaani alikuwa anaishi kama yupo nyumbani, Siyo wafungwa wala askari magereza ambao walikuwa wanamkubali Kwa ushujaa alio ufanya!.
Baada ya miezi kadhaa kupita baadhi ya askari magereza wale wanao penda kufanikiwa kupitia njia za mkato walianza kumtumia Majaribu kwenye madili yao haswa ya Wizi! Yaani walikuwa wanamtoa Majaribu usiku Kwa njia za panya akifika mtaani wanamcholea Raman anaenda kuiba, alafu anarudishwa tena Gerezani!.

Majaribu alikuwa Master wa Wizi! Yaani mtoto alikuwa balaa zito kwenye Wizi!
Upande wa huku mtaani Mr Jedi alizidi kukusanya taarifa Zake kuhusu ukweli, na inaonekana Siyo tu kufungwa Kwa Majaribu ambako alikuwa anafuatilia Bali kulikuwepo na Vitu Vingine ambavyo alikuwa anafuatilia!.

Mwaka mzima ulipita! Siku Hiyo Mr Jedi akiwa mtaani Majira ya Saa Saba Usiku, Huku akiwa katokea kwenye upelelezi wake ambao alikuwa anafanya kila Siku! Mara alishangaa kuna pikipiki ilipita kasi, na pikipiki ile ilienda kusimama mbele.
Jedi ilibidi aisogelee ile pikipiki haraka haraka na kujibana sehemu!.

"Dogo unasikia! Unaona ile nyumba pale kama kawaida utazama ndani! Pale getini kuna Gari zimepita utafanya kama tulivyo kuelekeza ukishafanikiwa utatukuta Eneo lile lile" hayo yalikuwa ni maelezo ambayo Jedi aliyasikia Vyema Mtu akiwa anaelekezwa!.
Lakini Mr Jedi alipo chungulia vizuri aligundua Mtu anaye pewa yale maelezo ni dogo Majaribu!!.

"Heeeee! Huyu dogo vipi si yupo Gerezani!? Hapa tena imekuwaje!?" Jedi alijiuliza maswali ambayo hata hivyo hakuwa na majibu ya haraka haraka!.
Kwanza alijipa subiri ya kusubiria ili aone nini kitatokea.
Basi Watu wawili Ambao walionekana ndo wamemleta pale Majaribu, baada ya kumpa maelezo waliwasha pikipiki na kuondoka!, Kijana Majaribu aliangaza Huku na kule baada ya kutoona Mtu aliruka Fensi Kwa ufundi mkubwa na kuzama ndani!.

Kwanza Mr Jedi alibaki kaacha mdomo wazi, Kwa Namna Majaribu alivyo ruka ule ukuta na kuzama ndani!.
Bahati mbaya kuliko zote maelezo ambayo Majaribu alikuwa kapewa na wale walio mtuma yalikuwa siyo! Bila kujua lile Eneo kumbe ulinzi ulikuwa umeongezeka zaidi.

"Mwizi!! Jamani Mwizi! Mwizi!" Nduru za Mtu kuitiwa Wizi zilisikika upande wa ndani Huku Muda huo Jedi akiwa upande wa Nje, na zile nduru alizisikia vyema kabisa!.
Majaribu aliruka ukuta haraka na kuanza kukimbia Huku Jedi akiwa bado kakodoa macho anashangaa pale nje na alijithibitishia kwamba yule ni Majaribu baada ya kumuona Kwa Karibu zaidi!.
Walinzi wa Maeneo yale ambayo yalionekana ni parking ya Magari walitoka getini wakiwa wanapiga nduru za Wizi, bahati mbaya pale nje Mr Jedi alikuwa yupo na alikuwa anatumbua tu Macho huku ak
iwa anajiuliza maswali Yasiyo na majibu!.

Je kipi kilimkuta bwana huyu!?

Tukutane sehemu ya 7
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 7

Walinzi wa Maeneo yale ambayo yalionekana ni parking ya Magari walitoka getini wakiwa wanapiga nduru za Wizi, bahati mbaya pale nje mr Jedi alikuwa yupo na alikuwa anatumbua tu Macho huku akiwa anajiuliza maswali Yasiyo na majibu!.

"Kamata Mwizi huyo! Mwizi huyo!" Jedi akiwa haelewi hili wala lile alikoswa na Rungu, mpaka hapo alijua akizembea kinamdondokea!.
Mbio Kwa bwana huyo zilianza na alikuwa anaelekea kule kule aliko kimbilia Majaribu! Bahati nzuri Eneo hilo watu walikuwa wavivu kujitokeza Usiku pindi wasikiapo kelele za Mwizi na hiyo ndo ilikuwa pona pona ya Mr Jedi maana wale Walinzi watatu ambao walikuwa wanamfukuza waliamua kukata tamaa baada ya kuona Jamaa anakipimbia kama ana mota miguuni.

Mr Jedi akiwa anakimbia Kwa mbali alimuona dogo Majaribu akiwa naye anakimbia huku akiwa hoi, yaani ilikuwa Siyo kawaida Majaribu kufukuzwa kwenye matukio au kushitukiwa!.
Mr Jedi alimfuata Majaribu nyuma Kwa nyuma! Mpaka Eneo la uwanja wa shule! Ambapo aliona kuna pikipiki imepaki!.

Basi Majaribu alifika mpaka pale ilipo pikipiki, walikuwa ni askari magereza wawili wanamsubiri!.

"Wote tulieni hapo hapo lasivyo nauwa Mtu!" Mr Jedi gafla alifika pale, Wale askari wakiwa wanataka kuondoka zao na Majaribu Mara walisikia Sauti Kavu kutoka Kwa Mtu wasiye mjua!.
Askari magereza Wale walijaribu bahati yao Kwa kumpiga Jedi, Lakini kidogo Jedi alikuwa kabarikiwa uwezo wa kupigana kuliko wao, dakika mbili nyingi kila Mtu alikuwa anaugulia maumivu Chini!.

"Majaribu Kwa Hiyo Siku hizi umeanza kutumika kwenye Wizi!? Huoni kama unaingia kwenye Matatizo zaidi!?" Jedi alimuuliza Majaribu, Basi Majaribu baada ya kugundua na kumfahamu bwana huyo walau alipumua kidogo!.

"Daaaa! Bro Kumbe Wewe ujue umenishitua unapiga kama kwenye video nikajua Mtu gani! Sema bro potezea tu!" Majaribu alijielezea Lakini Jedi userious uliongezeka alipo gundua kwamba wale ni maaskari Gereza.

"Sikilizeni! Nawapeleka kituoni Muda huu, haiwezekani askari ndo mnafanya huo ujinga!" Jedi aliwapiga mkwara.
Basi wale Jamaa walibembeleza kuliko Kawaida.
Kitu ambacho Jedi alikifanya ile pikipiki yao alichukua na ndo ilikuwa kusamehewa kwao! Baada ya hapo walianza kukanyaga Mguu mpaka gereza liliko, ilikuwa ni mbali kabisa nje ya Mji ila walitembea mpaka walifika! Huku kijana Jedi akijipatia pikipiki, na aliwaahidi kabisa itakapo fika Kesho yake anaenda kuchukua bluu kadi!.

Baada ya tukio hilo! Kijana Majaribu hakupewa tena yale madili ya kwenda kuiba mtaani Japo pale Gerezani kila Mtu alikuwa anamnyoshea Mkono Kwa kipaji Cha Wizi ambacho alikuwa nacho!.
Baada ya miezi miwili mingine mbele Mr Jedi alipata vithibitisho ambavyo aliamini vinaweza kumsaidia kwenye ile Kesi!.
Na kweli Mr Jedi alitafuta mwanasheria na walifanikiwa kukata rufaa ya Kesi ya Kijana Majaribu!

Siku iliyo fuata Mr Jedi alienda Gerezani kumtembelea Majaribu na kumpa taarifa ya ile rufa waliyo ikata!.

"Bro una uhakika Lakini kwamba tutashinda hii kesi!?" Majaribu aliuliza!.

"Kuhusu kushinda hilo tumwachie Mungu ila ushahidi wote ninao!"

"Samahani Lakini bro Hivi Kwa nini umeamua kunisaidia Mimi!!? Na sikujui hunijui!?"

"Najisaidia Mimi mwenyewe! Ila wewe umeingia tu kwenye njia Zangu Katika hali ya kujisaidia ndo maana unaona kama nakusaidia!"

"Njia Zako kivipi tena bro!?"

"Mchungaji Nemeke yule marehemu alikuwa ni adui Yangu na nilikuwa namfuatilia Mguu Kwa mguu na kuna Vitu nilikuwa nataka kuvijua toka kwake, bahati mbaya akawa amekufa ndo maana ikawa rahisi hata kufuatilia kifo Chake!"

"Hee bro mbona sikuelewi! Kwamba ulikuwa na ugomvi naye!? Mbona ni kama alikuwa Mtu poa Sana Kwa Nilivyo muona Mara ya mwisho!"

"Majaribu ujue wema wa Mtu hauonekani Kwa Macho!!.
"Heeeee haya Bwana kwamba alikufanyia vibaya hivyo mpaka ukawa unamufuatilia!!!??"
"Siku ikifika utajua! Ila mchungaji Nemeke alimuua Dada Yangu na kumdhurumu baadhi ya Mali"
"Heeeee Kweli!!? Ilikuwaje bro!?"
"Mchungaji Nemeke alizaa na Dada Yangu Kwa Siri mtoto, ila baada ya kuona Sasa Dada Yangu anataka kuitoa Siri ili kila Mtu aijue, kwakuwa alikuwa mchungaji hakutaka kuharibu Sifa zake na hicho ndo chanzo Cha kumuua Dada Yangu akishirikiana na baadhi ya watu!"
"Heeeee Jamani Kumbe yule bwana naye alikufa kihalali! Sema brother nikitoka Hapa kuna Siri ya mchungaji Nemeke aliyo niambia kabla hajafa ntakwambia!" Majaribu aliongea maneno ambayo yalifanya Mr Jedi awe na mizuka ya kujua ni Siri ipi, japo kuwa alikuwa anakisia tu!.

"Ebu nidokezee kidogo!"

"Kuna sehemu mchungaji Nemeke aliniambia alificha Siri zake na nyaraka na kuna Mtu aliniambia ndo nimwambie hiyo Siri, ila kabla sijamwambia niligundua yule Mtu niliye ambiwa nimpe Siri Siyo Mtu mzuri, maana kuna Siku alikuja kuniona akiwa na Mtu niliye muona kwenye mauaji!" Kijana Majaribu alizidi kuelezea, bahati mbaya wakati anatoa maelezo yale kumbe kulikuwa na askari magereza mnoko ambaye alikuwa ashapewa kazi ya kumchunga Majaribu na endapo kuna mgeni atakuja kumuona Basi ijulikane ni mgeni wa aina Gani na wanazungumzia kuhusu nini!.

"Mtu Gani Huyo uliambiwa umpe Siri" Jedi aliuliza!.

"Kuna Mama mmoja Hivi mrefu mweupe ni Katibu wa kanisa!" Majaribu alielezea!.

"Shiitiiii!! Dogo sikiliza tulia hivyo hivyo hao ndo wabaya wenyewe! Kibaya zaidi nilicho gundua wanazungukana wao Kwa wao kuna mchezo unafanyika! Ila subiri Muda Siyo mrefu naenda kugusanisha waya mbona watapigana wao Kwa wao, ila sikiliza kitu kimoja ni kwamba.....!!" Jedi aliongea ila wakati anazidi kutoa maelezo kabla hajamalizia aligundua kuna mpuuzi anasikiliza yale maelezo! na baada ya kugundulika kama anasikiliza aliamua kuondoka!

"Okay Majaribu zingatia kila kitu nilicho kwambia Siku Siyo nyingi utaenda kupandishwa mahakamani Kwa Mara nyingine!." Jedi aliongea baada ya hapo aliondoka!.
Siku Hiyo ilipita! Ikiwa ni Siku nyingine Majira ya usiku kama Saa nne Hivi Jedi akiwa getoni kwake anapangilia baadhi ya ushahidi Kwa ajili ya kesho yake kupeleka Kwa mwanasheria aliye mtafuta, Mara alisikia mlango unagongwa.

"Uuuuu!! Nani tena usiku huu" kwanza Jedi alijiuliza maana ilikuwa ni adimu Sana kugongewa usiku, kwanza alikuwa hana rafiki wa hivyo mpaka kuja kugongewa usiku, Pili alikuwa hana hata demu Labda kwamba atasema demu wake kaja!.
Kijana Jedi alisimama na kusogea mlango! Kisha alitulia kama dakika Moja bila kufungua!, Mara gafla alisikia minong'ono mlangoni, mpaka hapo alijua kimeumana!.

Jedi alitamani apige kelele za kuomba msaada Lakini aligundua hakuna msaada atakao pata! Maana mitaa hiyo ushirikiano ulikuwa sifuri, yaani ukivamiwa hata upige Kelele vipi watu walikuwa hawajitokezi kabisa!.
Jedi aliangaza huku na kule aliona Mule ndani kuna paint Spray ambayo ilibakia Mara baada ya kuwa amepulizia kwenye pikipiki ile aliyo jipatia kutoka Kwa askari magereza.
Kwanza Jedi alikusanya ushahidi wake wote zikiwemo flash disk ambazo zilikuwa na video pamoja na ushahidi mwingine, baada ya hapo alielekea sehemu ambayo palikuwa Kama ukuta!tu alisogeza kidogo, Basi kuna kashimo kalionekana pale ukutani alificha ule ushahidi wake, na alirudisha kama palivyo kuwa awali! Ilikuwa ni ngumu Muno kugundua kama pale ukutani kuna shimo linafunguka!.

baada ya hapo Kitu Alicho kifanya alichukua nondo ambayo alikuwa nayo mule ndani na hiyo spray!.

Jedi alisogea mlango na kufungua taratibu taratibu! Baada ya kufungua pale mlangoni aliona vijana wanne walio Shiba Huku mmoja wa mbele akiwa kashika Bastola!.
"Chini ya ulinzi! Ukifanya chochote Cha kipuuzi nakufyatua Risasi!" Basi Jamaa aliye shika bastola aliongea!.
Jedi wala hakuogopa bastola haraka aliwapulizia ile spray usoni, wakiwa wanahaha Jedi alitembeza nondo kama mbili baada ya hapo alitoka baruti!, Yaani Jamaa mmoja baada ya kupigwa nondo na Jedi alidondoka Chini na kuzima pale pape!.

Basi wenzake ilibidi wambebe haraka haraka na kuondoka naye.
Siku Hiyo ilipita ikiwa ni asubuhi ndo Jedi alirudi pale Getoni kwake, lakini wakati anafika tu nao askari ndo walikuwa wanafika pale kwake!.

"Jedi unashitakiwa Kwa kumvamia Mtu Usiku na kumpiga na nondo!" Hayo ni maneno ambayo Jedi aliambiwa na pale pale alikamatwa na kupelekwa kituoni!.

Siku Hiyo Hiyo upande wa Gerezani aliko fungwa kijana Majaribu! Alionekana mwanamama Melisa akifika pale Gerezani akiwa na wapambe wake wawili, basi kama Kawaida waliomba wazungumze na Majaribu na walitoa kitu kidogo!.
Yaani pale Gerezani ili uzungumze na Mtu wako mazungumzo ya Siri ilikuwa lazima utoe rushwa, lasivyo inabidi yawe ya wazi ambayo askari wanasikia!.

Kijana Majaribu aliletwa na baada ya kumuona mwanamama Melisa, Majaribu alibaki katumbua tu macho!.

"Okay kijana sitaki kupindisha maneno! Najua marehemu mchungaji Nemeke alikwambia Siri ya zilipo nyaraka zake zote, na alikwambia unambie mimi Hiyo Siri! Sasa nimekuja hapa Siyo kukuomba nataka uniambie Hizo nyaraka ziko wapi!?" Melisa akiwa na Sura ya ukauzu aliuliza!.

"Nyaraka Gani unazizungumzia!?"! Majaribu aliuliza kana kwamba haelewi kinacho zungumziwa!.

"Kijana usifikirie kwamba utaachiwa hapa kirahisi! Huyo uliye kuwa unamtegemea tayari kakamatwa Kwa kosa la kuuwa, Siku Siyo nyingi utakuwa naye hapa Gerezani!."Melisa aliongea maneno ambayo yalifanya Majaribu atokwe na Jasho, yaani matumaini Yote yalipotea tena Kwa Mara nyingine!.
Wakati huo huo upande wa hospital aliko pelekwa yule Jamaa aliye pigwa na nondo usiku na kijana Jedi alifariki, ila kuna daktari wa field ambaye alikuwa yupo pale hospital Kwa ajili ya mafunzo alijaribu kupima kifo Cha yule bwana aligundua kilicho muua Siyo kupigwa na nondo bali alikuwa amekufa Kwa Sumu Kali!, Inaonekana kuna Mtu alikuwa kamchoma sindano ya Sumu kwa makusudi ili afe Japo kuwa daktari huyo aligundua hilo Lakini aliamua kukaa kimya tu.

Yaani hapo Kesi ndo ilizidi kuwa ngumu Kwa kijana Jedi! Maana pale kituoni taarifa zilifika kwamba Jamaa aliye pigwa na nondo na Jedi usiku amefariki dunia, kwanza kijana Jedi zile taarifa zilimshangaza Kwa sababu hata nondo yenyewe alivyo piga alikuwa hajakaza Mkono Sana!.
Pia wale wenzake na marehemu nao walishangaa mwenzao kafaje kafaje maana alikuwa hajaumia kihivyo kufikia hatua ya kufa!!.

Wakati yote Hayo yakitokea huku Gerezani kijana Majaribu alikuwa kagoma kutoa Siri! Yaani alikuwa katishiwa Lakini kijana alimjibu Melisa kwamba hajui lolote, mwishowe Melisa alianza kutumia maneno mazuri kama ya kumtoa Gerezani na kumpa maisha mazuri Lakini napo Bado Majaribu alisimama kwenye mstari kwamba hana Siri yoyote aliyo ambiwa na marehemu!.
Siku Hiyo Melisa aliondoka kichwa kikiwa kinawasha, yaani ilibakia kidogo hata wigi alilovaa limtoke!.

Basi Siku kadhaa zilipita bwana Jedi alipandishwa mahakamani Kwa kosa la kuuwa! Yaani ushahidi na mashahidi wa uongo walikuwa wametengenezwa! Bahati mbaya Jedi alijichanganya pale alipo sema alimpiga jamaa huyo baada ya kuwa wamemvamia kwake na alikuwa
anajihami.

Je Mr Jedi atafungwa Gerezani!? Baada ya kufungwa kipi kitatokea!??

Tukutane sehemu ya 8
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 8

Basi Siku kadhaa zilipita bwana Jedi alipandishwa mahakamani Kwa kosa la kuuwa! Yaani ushahidi na mashahidi wa uongo walikuwa wametengezwa! Bahati mbaya Jedi alijichanganya pale alipo sema alimpiga jamaa huyo baada ya kuwa wamemvamia kwake na alikuwa anajihami.

"Kwa Hiyo Kijana baada ya kuvamiwa ndo ukaona Sasa una Haki ya kuuwa ukaamua kuua kabisa!!?" Wakili wa Serikali alimuuliza Jedi swali!.

"Mimi Sikuuwa na nilimpiga kidogo tu, sidhani kama kumpiga Kwangu ndo kumepelekea kifo Chake naomba kifo chake kichunguzwe upya!" Jedi alitoa maelezo na wasiwasi wake juu ya Kifo kile lakini alizidi kushindiliwa maswali mfululizo!.
Siku Hiyo kesi iligairishwa na Jedi akirudishwa tena rumande! Yaani Mambo yalikuwa yamegeuka gafla badala ya Jedi kufuatilia kesi ya Majaribu Sasa alikuwa anaparangana na Kesi yake!.

Wiki Tatu zilipita Tarehe nyingine ya kurejea mahakamani iliwadia! Siku Hiyo ndo ilikuwa Moto zaidi Kwa Jedi maana mashahidi kama wote walijitokeza pale mahakamani na wote walikuwa karibia na maelezo yanayo fanana wakiwa wanasema Jedi wala hakuvamiwa bali alimpiga Mtu huyo Njiani na Siyo kwake!.
Na kibaya walio kuwa wanatoa ushahidi walikuwa Siyo wale vijana ambao walikuwa na marehemu usiku, bali walikuwa ni watu wengi tu Ambao hawakuwepo hata Siku ya tukio!.

Mpaka hapo Kesi ilikuwa ngumu Kwa upande wa Jedi na Mwishowe Hakimu aliamua kusoma Hukumu!.
Kijana Jedi alihukumiwa Miaka 30 Gerezani kwa Kosa la kuuwa Kwa makusudi kabisa! Yaani Jedi alijaribu kujikanyaga Lakini ilishindikana!!.
Hakika kijana Huyo alikuwa anaziona Ndoto zinapotea taratibu taratibu, yaani kutoka kuwa askari mpaka kuja kuwa mfungwa!!.

"Dada Yangu Nisamehe! Nilijiunga na uaskari ili niweze kufichua maovu ya watu walio kusababishia kifo, Lakini Leo hii naishia Gerezani bila kulipiza kisasi chako!" Akiwa kwenye karandinga anapelekwa Gerezani kijana Jedi alikuwa analia huku akiwa anajiongelesha maneno ya huzuni!.

Siku Hiyo ilikuwa jmatatu wafungwa wakiwa wametoka kugonga Mawe huku wakiwa hoi bin taabani Mara kuna mfungwa mpya alionekana akiletwa!.
Majaribu alibakia kaacha mdomo wazi baada ya kumuona Jedi naye kaletwa Mule Gerezani, hapo ndo alianza kuamini maneno ya Melisa kwamba Yeye na Huyo Jedi wake watafia Gerezani!.
Maisha Mapya Kwa Jedi yalianza huku rafiki yake mkubwa akiwa ni Majaribu! Kutokana na umaarufu wa Majaribu pale Gerezani hiyo ilisaidia hata Jedi kutopelekeshwa Sana na Wahuni, pia Jedi mwenyewe naye alikuwa anajiweze kwenye upande wa kupigana!.

Siku nazo hazigandi hatimaye Mwaka mzima ulipita, huku mtaani Mama Mchungaji aligawana Mali Nusu Kwa Nusu na mtoto Habir ambaye ilisadikika ni mtoto wa marehemu mchungaji Nemeke! Mali zingine ambazo zilikuwa zimejificha ambazo hawakuweza kuzitambua zilipotea kimya kimya!.
Ila pamoja na kwamba Mama mchungaji alikuwa kagawana na yule mtoto Mali zote Lakini bado Mama mchungaji Yule alikuwa na wasiwasi kweli kweli kwamba yule ndo mtoto wa mchungaji kweli au kuna mchezo! Maana mtoto huyo na marehemu mchungaji Nemeke walikuwa hawafanani hata kidogo!!.

Upande wa huku Gerezani kijana Jedi aliona Siyo kweli kwamba yeye aendelee kusota Gerezani wakati kesi Siyo yake! Na Hiyo ilitokana na kwamba kuna Mtu alikuwa amekuja kumletea taarifa kwamba marehemu aliye fariki alipewa Sumu!.

"Ndugu Yangu Kwa saizi Mimi nimeajiliwa hospital ya mkoa, ila nimeona Siyo busara kukaa na Siri! Kipindi kile nafanya field kwenye ile hospital aliyo fia yule kijana! Kiukweli kila kitu nilishuhudia! Yule kijana alikuwa amepona kabisa! Ila kuna daktari pale hospital alimchoma sindano ya Sumu! Na ushahidi ninao! Pia vipimo vyote na aina ya Sumu Ninavyo! Kwa Hiyo ndo hivyo kaa ukijua ulisingiziwa!" Hayo ni maelezo ambayo Jedi aliletewa na yalifanya apate mizuka ya kutoka pale Gerezani!.
Jedi alikuwa anajua Kutoka Kwa njia ya kihalali ni ngumu bali lazima atoke Kwa njia za kiwizi Wizi!.
Kijana Jedi alianza kutengeneza mipango kushirikiana na baadhi ya askari wenye tamaa!.

"Hivi huo mpango una uhakika nao!? Na umewahi shuhudia wapi mpango kama huo? isije ikawa unaleta Mambo ya kwenye video!"

"Mimi si ndo nakwambia ndugu Yangu mbona simpo tu! Nyie kazi yenu ndogo itakuwa kutukimbiza hospital Mimi na Majaribu!"

"Uuuuu! Na ikithibitika hamjafa itakuwaje!?"

"Haiwezi kutokea, yaani tukitoka hapa tunapotea Mjini moja Kwa Moja!"

"Una uhakika Lakini Pesa uliyo isema baada ya kutoka tutapata!?"

"Aaaaaa million 100 kitu gani afande msijali hiyo mtapata!"
Jedi alikuwa anazidi kuwashawishi askari magereza pale Gerezani!.
Mpango wa Jedi alikuwa ameongea na Yule Daktari ambaye alimletea taarifa, na Lengo alikuwa anataka yeye na Majaribu wanywe Dawa, na zilikuwa ni Dawa maalumu ambazo zinasimamisha Mapigo ya Moyo Kwa Muda.
Baada ya kunywa hiyo Dawa ithibitishwe kwamba wamekufa na wafutwe kwenye faili la pale Gerezani Kisha wapotelee mitaani, yaani kifupi Jedi alikuwa anataka kutoroka Gerezani kwa njia ya kuwa kama mfu!.

Basi baada ya askari kupangiliwa vyema nao walipangika vizuri kabisa na walikubaliana kila kitu na Jedi, kijana Majaribu alipo pewa ule mpango yeye aliona noma tu maana alikuwa hana tumaini lingine lolote la maisha mbele yake!.
Basi Siku kadhaa zilipita Siku Hiyo Majira ya mchana Mara gafla Majaribu aliumwa ugonjwa wa ajabu, yaani alikuwa anatetemeka hovyo, wale wale askari walio kula dili na Jedi walimbeba haraka haraka dogo na kumkimbiza hospital ya mkoa na daktari aliye wapokea alikuwa ni yule Yule aliyepangana na Jedi!.
Siku inayo fuata asubuhi Jedi naye alipatwa na Hali kama aliyo patwa nayo Majaribu Jana yake! Pia naye alikimbizwa hospital!.

Baadhi ya askari magereza Ambao walikuwa hawaelewi mchezo unao endelea walihofia kwamba huwenda kuna ugonjwa wa mripuko umezuka pale Gerezani! Basi haraka haraka wataalamu wa kupuliza Dawa za kuuwa vidudu waliitwa na gereza zima Dawa zilipulizwa!.
Yaani Dili lile lilikuwa linapita Chini Kwa Chini kiasi kwamba hata mkuu wa gereza alikuwa hajui kinacho endelea aliamini ni ugonjwa tu!.

Basi Jedi na Majaribu walijikuta wapo hospital Kwa pamoja!.
Siku Moja ilipita! Yule Daktari aliye julikana Kwa Jina la Lameck aliamua Sasa kuwapa vile vidonge maalumu vya kusimamisha mapigo ya Moyo Kwa Muda na Daktari huyo tangu aajiriwe alikuwa na miezi mitatu tu kazini.
Jioni ilipo Fika ilithibitika wale wagonjwa wamefariki, taarifa zilifika mpaka Gerezani! Mpaka mkuu wa kituo taarifa zilimfikia kwamba wafungwa wawili wamefariki!.
Daktari mkuu wa hospital ya mkoa naye alithibitisha kwamba ni kweli wafungwa wale wamefariki, madaktari wazoefu nao walipima vipimo vyao waligundua wale watu wamefariki! Ila kuna Mzee mmoja alikuwa mzoefu aligundua kitu maana hata miili ya wawili wale ilikuwa ya Moto, Japo kuwa daktari huyo aligundua ila aliamua kuuchuna tu na kupotezea!.

Basi wawili wale Majaribu na Jedi walipelekwa mochwari ikiwa ni kama maiti!.
Majira ya Saa Kumi na Moja alfajiri bahati mbaya Majaribu na Jedi walizinduka maana vile vidonge Sasa vilikuwa vimeisha Kazi yake! Bahati nzuri doctor Lameck alikuwa analijua hilo mapema, alfajiri ile ile alifika pale mochwari! Alimhonga mlinzi wa mochwari Pesa ya pombe aliingia Mule ndani! Basi alifanya kile kilicho mpeleka alitoka tena!.

Majira ya Saa mbili asubuhi Mkuu wa Gereza na baadhi ya askari Walifika pale hospital kuthibitisha ni kweli Majaribu na Jedi walikuwa wamepoteza maisha, na Sijui doctor Lameck alikuwa kawamwagia Vitu Gani, maana walikuwa wananuka kama maiti kweli!.

Taarifa za vifo vya Watu hao zilifika mpaka mtaani! Watu walipata taarifa kwamba kijana aliye husika na Kifo Cha Mchungaji Nemeke amefia Gerezani kwa ugonjwa wa mripuko! Maana taarifa zilitangazwa mpaka kwenye vyombo vya habari!.
Bwana Luka na Melisa walishituka ila hawakuzingatia Sana wala kufuatilia kabisa Swala hilo kwamba inawezekana vipi Majaribu na Jedi wafe Kwa pamoja, Upande wa Mama mchungaji Yeye Ndo alionekana ameshituka Sana kuliko Hata kina Melisa, yaani hakuamini kabisa mpaka Mama Huyo alipo enda kujionea na kuthibitisha walau ndo aliamini Japo kuwa alikuwa anajiuliza maswali mengi Muno kwamba imekuwaje wafe wawili tu tena wanao Juana!.

Kwa Macho yake alijonea kabisa maiti ya Jedi na Majaribu tena zikiwa zinatoa harufu vibaya Muno ikiwa ni dalili ya kwamba zimeanza kuharibika!.
Basi ilitangazwa kwamba ndugu wa wawili hao wajitokeze wakabiziwe miili ya wapendwa wao wakaizike!.

Kuna vijana wawili, Baba mmoja na wamama wawili walijitokeza kama wao ndo wahusika Huku kila Mtu akiwa anataja ndugu yake! Na Watu hao Kwa maelezo yao walionekana wamepangwa.
Basi ndugu walienda mpaka Gerezani walisaini sehemu zinazo takiwa na walienda hospital kukabiziwa miili ya wapendwa wao tena walinunuliwa na majeneza kabisa!.

Hakika Njia ile aliyo ibuni Jedi ilikuwa ngumu Muno! Akiwa ndani ya Jeneza kijana Majaribu alizinduka Lakini baada ya kusikia maneno nje Watu wakiwa wanaongea kuhusu vifo hivyo huku wengine wakiwa wanalia aliamua kuvunga!.
Kwa mbwembwe kabisa na vilio juu Gari ya kubeba maiti ilikodiwa huku ikiwa inasemekana maiti Inasafilishwa kwenda mkoani, pia maiti ya Majaribu ilisadikia inapelekwa kijijini!.
Wafiwa bahati mbaya walikuwa hawataki kusindikizwa na Mtu yaani, lakini mkuu wa gereza alisema lazima atume vijana wake wakathibitishe kwamba Watu hao wanazikwa!.

Bahati nzuri Kwa Jedi na Majaribu wale wale askari walio kula nao Dili ndo walijipendekeza Kwa mkubwa na walitumwa wasindikize misafara!.

Basi yaliyo tokea yalitokea na askari magereza wale walirudisha ripoti kwamba wameshuhudia mazishi tena walikuja na picha za msibani kabisa, Sijui walikuwa wamezitoa wapi!.
Askari magereza wale kazi yao ilikuwa imeisha walicho kuwa wanasubiri ni million 100 Kutoka Kwa Jedi kama walivyo ahidiwa! Na Kwa mahesabu yao kila Mtu alikuwa anapita na million 25 maana walikuwa wanne!.
Siku zilizidi kukatika miezi kama mitatu ilipita huku Jedi na Majaribu wakiwa hawajaonekana kabisa! Kiasi kwamba hata wale askari magereza walianza kujiuliza watampatia wapi Jedi awape Pesa zao!.

"Daaaa Sema na Sisi Wazembe kweli! Yaani tulikubali Dili la hatari vile bila hata kujua tutakabidhiwa Pesa Kwa mfumo upi, Ona Sasa huyu msenge hatujui hata pa kumkutia!" Basi Siku hiyo wakiwa wanajadili askari mmoja aliongea Kwa malalamiko kweli kweli!

"Ndugu Yangu usijali hii dunia ndogo Muno! Ipo Siku tutamnasa ndo atajua kwamba Pesa ina maana Gani! Maana tutauza hata Figo yake Moja!" Basi askari mwingine akionekana ana hasira aliongea!!.

Je watafanikiwa kumpata Jedi!!
? Na Je upi mpango wa Jedi na Majaribu baada ya kutoroka Gerezani!?

Tukutane sehemu ya 9
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 9

"Ndugu Yangu usijali hii dunia ndogo Muno! Ipo Siku tutamnasa ndo atajua kwamba Pesa ina maana Gani! Maana tutauza hata Figo yake Moja!" Basi askari mwingine akionekana ana hasira aliongea!!.

"Sema dogo hawezi kuzingua, tutulize mizuka maana Kwa Hali ilivyo kaa Sidhani kama dogo anaweza onekana kitaa haraka hivyo!" Basi askari mwingine aliongea kuwatoa shaka wenzake!.
Muda huo Jedi na Majaribu walionekana nyumbani Kwa doctor Lameck wakiwa mezani wanapata chakula Cha usiku!.

"Daaaa! Lameck Sijui usingekuwa wewe tungefanyaje ndugu Yangu, yaani nakushukuru Sana!"

"Jedi usijali ndugu Yangu! Ujue historia yako uliyo nisimulia pale Gerezani ilinigusa Muno Kwa sababu hata Mimi nimepitia kama uliyo pitia wewe, tena Mimi Mtu aliye nifanyia ubaya alikuwa Baba Yangu mzazi!"

"Uuuuu!! Pole ndugu Yangu walimwengu waache kama walivyo, zamani nikiwa mtoto nilikuwa naaminigi viongozi wa Dini hawanaga Dhambi lakini kumbe nilikuwa najidanganya!" Jedi aliongea!.

"Alafu ujue Jedi hukunifafanulia vizuri, unasema mchungaji Nemeke alimuua Dada yako yaani Ilikuwaje na chanzo haswa ni kipi!?"doctor Lameck aliuliza!.

"Ujue Mimi na Dada Yangu tuliachwa na wazazi wetu tukiwa wadogo! Wazazi wetu wote wawili Kwa pamoja walipata ajari na kufariki papo hapo!, Kiukweli lilikuwa ni pigo kubwa kwetu, Kwa kipindi kile hatukuteseka Sana Kwa sababu wazazi wetu waliacha Mali za kutosha! Kampuni na biashara kubwa kubwa! Na biashara zote bahati nzuri Baba alikuwa kaandika Majina yetu!.
Basi baada ya vifo vile tulianza kulelewa na Shangazi Yetu pale nyumbani ambaye ndo alikuwa ndugu yetu pekee aliye Salia, na Shangazi ilibidi ahamie na Mume wake pale nyumbani!.

Baada ya Miaka kama Mitatu kiukweli hatukuamini Shangazi na Mumewe waliiba baadhi ya hati zetu na waliuza karibia Nusu ya Mali zetu, baada ya hapo walikimbilia Sijui Nchi gani!.
Mimi na Dada Yangu tuliabaki tukiishi pekee yetu, uzuri Dada alikuwa kawa Mtu mzima anaye jitambua kidogo!.

Baada ya Miaka miwili biashara zetu zilikuwa zinaenda vizuri Japo Siyo Sana, Sijui Dada alidanganywa vipi na mchungaji Nemeke! Dada alijikuta anamwamini Sana mchungaji Huyo mpaka kumshirikisha kwenye biashara zetu na kuomba atusaidie baadhi ya Mambo, na Hiyo ilifanya mchungaji Nemeke kuzama kwenye mahusiano na Dada Yangu ambapo mwishowe ilipelekea wao kupata mtoto!.
Kipindi hicho Mimi nilikuwa kidato Cha kwanza na nilikuwa nakaa Shuleni, Kwa hiyo nilikuwa sielewi yale yanayo endelea!.
Mchungaji Nemeke Sijui alimlaghai vipi Dada Yangu! Yaani alimdanganya kwamba atampa taraka mkewe alafu atamuoa yeye! Na hiyo ilifanya Dada kumuamini Nemeke kupita kiasi mpaka ikapelekea kumpa hati zetu za Mali zote atunze Yeye!.

Mwishowe Dada alikuja kugundua hati zote Nemeke kabadili Jina na kuweka Jina lake badala ya kuweka Jina la mtoto kama walivyo kubaliana!, Hali Hiyo ilifanya Dada apate hasira na Lengo la Dada ilikuwa ni kutangazia kila Mtu Siri kwamba Yeye kazaa na mchungaji Nemeke, na mchungaji Huyo kamdhurumu Mali!.
Baada ya mchungaji Nemeke kuona Sasa ni kama anaenda kuumbuka aliamua kumuua Dada Yangu Kwa kushirikiana na baadhi ya watu, na Mtoto alimchukua na kumpeleka kusiko julikana!.

Kiukweli baada ya hapo niliishi Kwa kuteseka Muno, yaani niliishi kama Digi Digi, japo nilifanikiwa kumaliza kidato Cha Nne, Lakini Kwa taabu na misaada ya baadhi ya watu!.
Kwa hasira tu niliamua kuanza kupambana kutafuta nafasi ya Jeshi, bahati mbaya nilikosa na nilijijuta nimebahatika kupata uaskari Lengo Langu likiwa ni kulipa kisasi Kwa mchungaji Nemeke!.

Bahati mbaya Wakati sijalipa kisasi mchungaji Nemeke aliuawa kwenye mazingira ambayo Hata hayaeleweki, na hapo ndipo nilipo Anza kufanya uchunguzi!.
Hakika nimepata kujua mengi, kwanza niligundua Mtoto wa Dada Yangu Shule anayo Soma na nilianza kumfuatilia, ila mwishowe niligundua yule Siyo mtoto wa Dada Yangu bali kuna mchezo unafanyika wa kutaka kujipatia Mali za marehemu, Ambapo Mali nyingi za marehemu huyo zimetokana na Mali zetu!, Kwa kifupi ndo hivyo " Mr Jedi alimaliza kuelezea historia Yake ambayo ilifanya atilie mkazo Sana ile Kesi ambayo ilikuwa inamkabili Majaribu!.

"Bwana Jedi pole Sana! Kwa Hiyo mpaka saizi hujui mtoto wa Dada yako alipo!?"

"Hilo ntalifanya baada ya kuwa waharifu wapo mahali wanapo takiwa kuwepo!".

"Kwa hiyo inakuwaje! Yaani mchakato unaanzia wapi Mimi nipo tayari kuwasaidia kila hatua!" Lameck aliuliza,na kijana Lameck alionekana ni Mtu mpole na mwenye Moyo!.

"Hapa ndugu Yangu naomba nitafutie mwanasheria mzuri ambaye ana msimamo nimkabidhi ushahidi, maana kila kitu ninacho!" Mr Jedi alitoa maelezo!.
"Basi kuhusu hilo usijali na hiyo itakuwa njema, na Vipi kuhusu huyu dogo yeye ilikuwaje akaingizwa kwenye Kesi za mauaji!" Lameck aliuliza!.

"Uuuuu ni Stori ndefu! Ila Huyu dogo alisingiziwa! Na bahati nzuri aliwaona wauwaji na marehemu alimtaja kabisa kwamba Mkewe ndo Mtu mbaya!"

"Heeeee! Inaamana yeye ndo alishuhudia kifo Cha marehemu Nemeke, inaamana Nemeke hakumuelezea sababu za mkewe kumuua!" Lameck alizidi kuuliza!!

"Kwa Hali ambayo alikuwa nayo hakufanikiwa kuniambia yote hayo!" Kijana Majaribu ilibidi adakie na kujibu!.
"Uuuuu Mara nyingi Watu wakiwa wanakata Moto huwaga wanaropoka kila Kitu Kwa Jinsi Ninavyo jua katika taaluma Yangu, unataka uniambie hakuropoka kitu chochote Ambacho kinaweza kikafanya tukashinda hii kesi!?" Lameck aliuliza tena!.

"Kuna Siri aliniambia tu kuhusu maficho yake ya Siri yaani alipo ficha nyaraka zake na Siri zingine, ila tatizo niliye ambiwa nimpe taarifa niligundua ndo mhusika wa kifo Chake!" Majaribu alitoa Maelezo Kwa ufupi.

"Sasa hapo tunaweza shinda kirahisi hii Kesi! Yaani itakuwa rahisi maana ushahidi utakuwa wazi kwamba wewe hukuuwa mpaka anakupa Siri zake! Vipi umewahi fika hiyo sehemu aliyo kwambia na ni wapi!?" Lameck aliuliza!.
Kijana Majaribu kwanza machale yalimcheza, yaani alijikuta tu Moyo wake unakuwa mzito kuendelea kuropoka! Na Siku zote hakuna Mtu mwenye machale kama Mwizi!, Kwa Hiyo Majaribu alikuwa na machale ambayo Siyo ya Dunia hii!.

"Nadhani Majaribu huu ni Muda wa kufunguka kila kitu alicho kwambia marehemu Nemeke kabla ya kufariki, usimuogope Lameck ni Mtu mwema tu!" Mr Jedi alimsihi Majaribu atoe maelezo!.

"Jamani msijali Mimi ntawaambia tu ila Siyo saizi Nadhani inatakiwa tuanze na Mambo ya msingi kwanza!" Majaribu aligoma kutoa Siri Kwa Muda ule!.
Basi Lameck na Jedi walichukulia kawaida na walikuwa wanaamini Muda wowote Majaribu atawaambia!.
Siku Iliyo fuata Dr Lameck alitafuta mwanasheria, na alikuwa mwanasheria mzuri tena kijana Damu inachemka!.
Mwanasheria Yule alijinadi vyema kwamba yeye hajawahi feli kwenye Kesi na alinogesha maongezi vizuri Muno.

Basi baada ya makubaliano na Jedi kukubali kwamba atampa ushahidi, Lameck na yule mwanasheria waliondoka pale nyumbani huku Lameck akimsindikiza yule mwanasheria Kwa kutumia pikipiki yake.

"Bro Jedi hivi unamuamini Huyu brother! Mimi naona ni kama wale wale tu!" Majaribu aliongea point ambayo Jedi aliona ni ya kitoto!.
"Majaribu kama huna Hoja tulia, Mtu katusaidia kutoroka Gerezani, katupa hifadhi, katusaidia Kwa mengi na pia wazo la kutoroka Gerezani alinipa yeye alafu saizi eti humuamini, angekuwa Mtu mbaya si angetupa Sumu tufe Muda ambao tulikuwa tunazuga tumekufa pale hospital!" Basi Jedi aliongea Kwa kupaniki mpaka Majaribu aliogopa!.

"Kama kumuamini ni Wewe! Mimi simuamini na siwezi kumpa Siri za marehemu, isitoshe Mtu mbaya hapimwi Kwa wema alio fanya, na wala Sura! Anaweza akafanya wema kumbe ni chambo tu ya kuwanasa!" Majaribu aliongea Kwa hasira na kutoka nje!.
Mr Jedi alikuwa ni mtaalamu wa upelelezi na pia alikuwa na kipaji Cha kupeleleza, na Sifa ya mpelelezi mzuri ni kwamba usiamini kila kitu Kwa Macho na maneno!.

Siyo Kwamba Jedi alikuwa kamuamini Lameck Moja Kwa Moja ila alikuwa anafanya uchunguzi wake kimya kimya tena Kwa Siri Muno, ili kujua Bwana Huyo anawasaidia kutoka moyoni au ana jambo lake!.
Basi ilifika usiku Lameck alirudi, walipika vyema na kula, na Siku hiyo Jedi alikuwa amepanga kwamba ikifika usiku lazima aelekee kwenye geto lake la zamani kwenye kuchukua zile Siri zake ambazo alifichaga, na bwana Jedi alikuwa haelewi kama atakuta Mtu au laaa!.
Basi yakiwa ni Majira ya Saa Sita usiku Jedi alimshitua Majaribu ili waongozane! Maana alikuwa anajua Majaribu ni mtaalamu wa kupita Madirishani!.

Ila Wakati wanatoka walishangaa kuona milango ipo wazi, walitoka mpaka nje geti nalo lilikuwa lipo wazi na walisikia nje ya geti kama Gari inaunguruma Hivi!.
Jedi alichungulia taratibu pale getini, ili aone nje kuna nini!.

Je Jedi aliona Nini!??

Tukutane sehemu ya 10




Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 10

Ila Wakati wanatoka walishangaa kuona milango ipo wazi, walitoka mpaka nje geti nalo lilikuwa lipo wazi na walisikia nje ya geti kama Gari inaunguruma Hivi!.
Jedi alichungulia taratibu pale getini, ili aone nje kuna nini!.

Jedi alibaki katumbua Macho baada ya kumuona Lameck akiwa kasimama na Melisa yule Katibu wa kanisa, pamoja na bwana Luka yule Katibu wa Jimbo ambaye ni mchepuko wa Melisa, tena walikuwa wamesimama mbele ya Gari huku wakiwa wanajadiliana majambo, na taa ambayo ilikuwa ipo pale getini Kwa upande wa nje ilimsaidia Jedi kuona vyema kinacho endelea pale nje!.

"Machale mabaya yamenicheza ebu twende ndani dogo huko tutaenda Kesho!" Jedi ilibidi amzuge Majaribu na kweli walirudi ndani kimya kimya.
Majaribu hakuelewa kitu chochote, Lakini Jedi alikuwa ashajua doctor Lameck Siyo, alianza kuhisi Kwamba huwenda hata yule Bwana aliyefia hospital aliye daiwa kwamba kauawa na Jedi basi ni Lameck alimtia Sumu!.
Masaa yalisogea hatimaye palikucha na kuwa asubuhi, Kama kawaida Lameck alikuwa anawachangamkia Jedi na Majaribu! Pia nao hawakusita kuonesha ushirikiano walimchangamkia!.

"Jedi vipi ushahidi mwanasheria ameniuliza Muda Gani utamkabidhi akafungue Kesi!?"Lameck aliuliza, basi Jedi alimjibu kwamba ataenda kuuchukua na atamkabidhi!.
Kutokana na kwamba ilikuwa imesadikika kwamba wawili wale wamepoteza maisha, ilikuwa ni ngumu Kwa Jedi na Majaribu kutembea mchana!.

Usiku ulipo fika Jedi na Majaribu walienda mpaka pale Jedi alipo kuwa anakaa! Bahati mbaya sehemu Hiyo kuna Dada alikuwa kapanga na alikuwa anakaa hapo!.
Kama kawaida Majaribu alipitia dirishani, Japo kuwa dirisha lilikuwa na nondo Lakini Majaribu alipita kibishi, baada ya kuingia ndani alifungua mlango ili Jedi aingie!.

Wawili wale walisukuma mlango wa chumbani, walikuta mdada wa watu akiwa na Mtoto wake mdogo wamelala huku wamejiachia, yaani Dada huyo alikuwa kazalia nyumbani, baada ya kujipatia kimtaji ndo akaamua kwenda kupanga geto!.

"Weeee...." Dada Yule alikurupuka usiku ku na kutaka kupiga makelele ya kuitia Wizi! Lakini Jedi alimziba mdomo!.

"Dada Sisi Siyo watu wabaya! Mimi ndo nilikuwa nakaa humu kabla yako, kuna Vitu vyangu humu niliacha nimevifuata!" Jedi aliongea kistaarabu, basi yule Dada alitikisa kichwa Kwa uoga!!
Jedi alisogea ukutani, kuna Namna alibinua pale ukutani tobo lilionekana, baada ya hapo alichukua vitu vyake na waliondoka na Majaribu!.
Yule Dada alibaki kaacha mdomo wazi huku akiwa haamini kama ukutani pale palikuwa na tobo mpaka la kuweka Vitu!.

Basi Siku Hiyo ilipita! Ikiwa ni majira ya Saa Nne asubuhi Jedi alivaa vizuri alipiga na kepu yake mpaka puani, baada ya hapo alielekea kitaa.
Jedi katika ile sehemu yake aliyo kuwa kaficha ushahidi pia alikuwa anaficha Pesa zake za akiba,Kwa hiyo alichukua na zile pesa!.
Basi Siku Hiyo alielekea mpaka Library alinunua flash disk nyingine mpya kama mbili! Yake mafaili Yote aliyakopi kwenye flashi Mpya, maana alikuwa anajua akiwapa ushahidi lazima tu wataupoteza!.

Ilipo Fika Jioni mwanasheria yule alikuja pale nyumbani Kwa Lameck, alikabidhiwa ushahidi, alijaribu kuchomeka kwenye laptop yake! Hakika alibaki kaacha mdomo wazi! Yaani zilikuwa ni video za kutosha na Sauti za kutosha za wahusika, zikiwa zinaonesha mipango yao, mpaka mazungumzo yao Jinsi walivyo husika na kifo Cha Nemeke!.

"Ndugu Yangu hapa umeuwa! Kwani hizi video na audio wewe ulipataje, maana ni adimu Mtu kuwa na ushahidi wa maana kama huu, yaani Mtu hapa hawezi kukwepa!" Manasheria alimuuliza Jedi, basi Jedi alijibu kijanja tu kwamba kuna Mtu alimpatia ambaye ni miongoni mwa wale wale wahusika, maana yake anawasaliti wenzake!.

"Heeeee!! Vipi ndugu Yangu kwani kuna kopi zingine za ushahidi unazo au ndo hizi hizi!?" Mwanasheria yule aliuliza tena!.

"Sina kopi yoyote ndugu Yangu, na inatakiwa uwe Makini maana ukipoteza huo ushahidi ndo utakuwa umefelisha kila kitu!" Jedi alijibu, Muda huo Majaribu alikuwa anamkata Jedi Macho mabaya Muno huku Moyoni akiwa anajisemea kwamba Jamaa huyo mjinga kuwaamini watu hao na kuwakabidhi kila kitu kirahisi!.
"Yaani naona kabisa hawa Siyo watu wema Lakini brother Jedi anavyo waamini Sasa, Sijui huo anao sema upelelezi alisomea wapi!" Hayo yalikuwa mawazo Ambao Majaribu alikuwa akijiwazia!.

Mwanasheria yule aliondoka akiwa anakenua Meno njia nzima! Kwanza baada ya Kutoka pale alienda mpaka kwenye Hoteli Moja ya kifahari!.
Halikupita hata Nusu Saa Luka na Melisa walionekana kufika pale!

"Eheee! Jofu nambie umefanikiwa kupata huo ushahidi!?" Melisa akiwa na kimuhe muhe baada ya kufika pale Hotelin na kumkuta mwanasheria yule amekaa aliuliza Kwa pupa!.

"Boss nimefanikiwa na bahati iliyoje yaani wameniamini Moja kwa Moja, pia Lameck naye wamemuamini vibaya Muno! " Mwanasheria Yule akiwa anakenua Meno alikabidhi flash disk mbili Kwa Melisa!.
"Safi Sana jofu! Sàsa imebakia Kazi ya Lameck kumpeleleza Yule dogo mpaka tujue Nemeke alificha wapi nyaraka zote na vitabu vya benki!" Melisa akiwa na mizuka aliongea.
Basi waliagana na kuondoka Huku wakiwa wanajiona washindi!.

Huku upande wa kina Jedi! Majaribu muda wote alikuwa anazitupa lawama kwa Jedi Kwa kuwaamini wawili wale.
Ila Jedi alikuwa anatumia akili yaani alikuwa anatumia ule usemi wa mnafiki ishi naye Kwa akili na ukila na kipofu usimshike Mkono!.

"Majaribu Mimi naelewa kuliko wewe! Kitu ulicho nizidi wewe ni Mbinu za Wizi tu, ila Mambo mengi yote nimekuzidi!" Jedi Siku hiyo aliamua kumjibu Kwa akili!.

"Hata kama bro ndo uwaamini watu kirahisi hivyo!"

"Majaribu nikuulize Swali!?"

"Swali gani hilo!?"

"Okay Sisi tunaishi kama tumekufa, haya Lameck akasema atufukuze hapa kwake tutaenda wapi!?"

"Maswali Gani hayo bro anatufukuzaje Sasa!?"

"Umeona eee! Sasa unavyo sema tusimuamini unamanisha nini! Si unamaanisha tumkatae na hapa kwake tuondoke! Muda mwingine tumia akili" Jedi aliongea Kwa mafumbo, ila bado Majaribu yeye alikuwa haelewi na alimwambia kabisa Jedi kwamba Siri yake hawezi kuizungumza!.
Basi Siku zilizidi kusogea huku ile rufaa ya Kesi inayo mhusu Majaribu ikiwa bado haijakatwa! , Yaani yule mwanasheria alianza kuzungusha!.

"Lameck Jamaa yako mbona haeleweki, ujue huu mwezi unapita naona bado tu hajakata rufaa ya kesi na Pesa kidogo nilimpatia pamoja na ushahidi? "Basi Siku Hiyo Jedi aliamua kumuuliza Lameck!.
"Sema usijali, Jamaa juzi juzi alikuwa nje za Nchi Kwa hiyo kuna mambo anayaweka sawa! Ila Jamaa kapendekeza kwamba Ingekuwa vizuri Majaribu angeelezea kila kitu alicho ambiwa na Nemeke kabla hajafa ili kazi iwe nyepesi" Lameck aliongea!.

"Okay kuhusu hilo ntazungumza na Majaribu! Ila msisitizie Mtu wako afanye hima basi!" Jedi aliongea, basi Lameck alijibu kwamba Sawa!.
Ikiwa ni usiku Lameck aliamua kuanza kumpekenyua Majaribu tena kuhusu Siri alizo ambiwa na Nemeke kabla hajaaga dunia!.

"Ngoja niongee ukweli! Marehemu aliniambia nyuma ya nyumba yake kuna box la Kijivu alishalifukia hilo ndo lina kila kitu chake" kijana Majaribu akiwa serious aliongea, na inaonekana huo ni uongo ambao alikuwa kaelekezwa na Jedi kwamba auseme!.

"Kweli!!! Una uhakika alisema hivyo!!?" Lameck Macho yakiwa yanamtoka aliuliza mara mbili mbili!, Baada ya kuthibitishiwa na Majaribu kwamba ni kweli Muda ule ule aliamua kutoka huku Simu ikiwa mkononi, yaani taarifa zile zilikuwa za moto kwake mpaka zilikuwa zinamuunguza alitamani azifikishe sehemu nyingine Muda ule ule!.
Basi Siku hiyo ilipita ikiwa ni Siku nyingine, nyumbani Kwa marehemu mchungaji Nemeke, Mama mchungaji akiwa kakaa mchana kwenye bustani na shoga yake mmoja ambaye walikuwa wanaivana Haswa, alishangaa vijana kama wanne wakiwa wanaongozwa na Bwana Luka wanafika pale kwake tena wakiwa na mashine ya kuchimbi!..

"Katibu kulikoni mbona mnakuja na dhana za kuchimbia Kwangu kuna Nini!?" Mama mchungaji aliuliza Kwa mshangao maana alikuwa hajui lolote linalo endelea, kumbe harakati zote ambazo zilikuwa zinaendelea Mama mchungaji alikuwa hahusishwi!.
Jedi alikuwa anajua kwamba Melisa na Luka kuna Namna wanamuzunguka Mama mchungaji ndo maana aliamua kumpa plani Majaribu kwamba ataje pale pape nyumbani ili kuumanisha Mambo, maana alijua kitawaka!.

Mr Luka baada ya kuulizwa vile na Mama mchungaji, ilibidi amuite pembeni kumuelezea kile kinacho endelea!.

"Unasemaje Mr Luka! Kwa Hiyo nyie na huyo Melisa sijui na kina nani, munaona wajanja Sana eee, Mimi najua tupo pamoja kumbe nyie mnaendelea na mpango wa kutafuta nyaraka Chini Kwa Chini! Sasa nasemaje nyumbani Kwangu hachimbi Mtu! Labda niwe marehemu!" Mama mchungaji Siku Hiyo alikuwa anaongea mpaka mate yanamtoka, yaani alikuwa anaona naye ile ndo fursa yake ya kujipatia kila kitu, maana ilikuwa inasadikika kwamba kwenye hizo Siri ndo huko bwana Huyo alikuwa anaficha mpaka vitabu vya Benki!.
Yaani Kwa Namna ambavyo Mama mchungaji alikuwa anawaka na kuongea kwa kufoka, mpaka yule shoga yake ambaye ali
kuwa yupo pale nyumbani alibaki anashangaa kwamba Shida nini!.

Je Ipi hatima!? Mama mchungaji atakubali na je baada ya kuchimba nini kitatokea!??

Tukutane sehemu ya 11
 
Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 11

Yaani Kwa Namna ambavyo Mama mchungaji alikuwa anawaka na kuongea kwa kufoka, mpaka yule shoga yake ambaye alikuwa yupo pale nyumbani alibaki anashangaa kwamba Shida nini!.
Mr Luka alijaribu kumshawishi Mama mchungaji Kwa utaratibu lakini Mama huyo wala alikuwa haelewi, yaani aliwaka isivyo kawaida! Na Lengo lake alitaka achimbe mwenyewe!.

Basi Mr Luka na watu wake waliondoka huku wakiwa wanapiga mahesabu Namna ya kufanikiwa Jambo lao!.

"Shiitiiii yaani hapa pilau limeingia mchanga! Yule mpuuzi kajua kwamba Nyaraka zimefukiwa nyuma ya nyumba yaani hapa Sijui itakuwaje!" Baada ya Luka kufika nyumbani alijiongelesha Kwa hasira huku Melisa naye akiwa anakuna kichwa kivyake!.
Ilipo Fika usiku Mama mchungaji wala hakutaka kulaza Damu! Alitafuta vijana na baada ya hapo walianza kuchimba nyuma ya nyumba maeneo ambayo waliamini watapata kitu!.

Walianza kuchimba Saa Tatu Usiku mpaka inafika Saa Saba hakuna kitu walikuwa wamekipata, na walikuwa wanatumia mashine! Yaani walichimba kila sehemu Lakini ilikuwa hola, baada ya kuona hamna Kitu ilibidi waaanze kufukia mashimo yote!.
Mama mchungaji alikuwa na hasira isiyo ya kawaida, yaani alikuwa katumia gharama kuchimba Lakini hakupata kitu, kwanza wale vijana aliwalipa, Pili zile mashine alikuwa kakodi na kuweka mafuta ya Kutosha!.

Kufukia walimaliza alfajiri baada ya hapo wale vijana waliondoka, Mama mchungaji aliamua kulala huku akiwa na hasira!.
Siku hiyo ilipita palikucha na Kuwa asubuhi, Mida ya Saa nne asubuhi Mr Luka akiwa na Melisa na vijana wa kuchimba walifika pale nyumbani Kwa Mama mchungaji tena, Siku hiyo walikuja na Mbinu nyingine Mpya ambayo waliamini lazima Mama mchungaji atakubali wachimbue kule nyuma!.

Pale Nje walimkuta Binti Revina akiwa anaotea Jua la asubuhi huku anachati mtandaoni, maana Binti huyo tangia azijue Siri za Mama mchungaji alikuwa anaishi kiboss kabisa!.

"Revina vipi Mama mchungaji yuko wapi, ebu muite basi" Mr Luka aliongea!.

"Duuuuuu!! Mama mchungaji kalala alfajiri! Usiku kucha walikuwa wanachimba huko nyuma hata sielewi walikuwa wanachimba nini, Kwa hiyo kumuamusha saizi atanifokea Labda mpaka aamke mwenyewe!" Revina alijibu.
Kwanza Mr Luka Macho yalimtoka baada ya kusikia kwamba eti Mama mchungaji alikuwa anachimba usiku kule nyuma!.

Mr Luka na Melisa Macho yakiwa juu juu, walizunguka mpaka nyuma ya mjengo ule na kweli walikuta kila sehemu imechimbwa na kufukiwa vyema!.

"Shiitiiii Huyu Mwanamke hanijui eee!! Yaani Sisi tumefanya Kazi kubwa ya kupeleleza na kujua hizo nyaraka ziko wapi, yeye kirahisi tu anakuja kuzichukua! Hakika patachimbika!." Mr Luka aliongea Kwa hasira, baada ya hapo alizunguka na kuingia ndani Kwa hasira!.

"Mr Luka ndo Nini hivyo unaingia ndani Kwa vurugu, yaani kama kwako! Wewe una mamlaka kanisani Siyo kwenye majumba ya Watu!" Revina alimkimbilia Mr Luka na kuongea kwa hasira!.
Muda huo hayo Yote yanaendelea kumbe Mama mchungaji alikuwa kaamka Muda na alikuwa kaweka earphones 🎧 Masikioni mwake kuna video alikuwa katumiwa kutoka kwenye namba ngeni!
Baada ya Mama mchungaji kufungua video ile nusura azimie alibaki anatetemeka Kwa hasira, ilikuwa ni video ambayo ilikuwa inaonesha nyumbani Kwa Melisa na mazungumzo Yote!.

Mama mchungaji alijaribu kupiga ile Namba iliyo mtumia ilikuwa haipatikani!.

"Shiitiiii kumbe Luka na Yule mwanamke lao Moja wananizunguka eee! Hata yule mtoto Siyo mtoto wa Nemeke, huu ujinga Gani! Na Bado wanaona haitoshi wanataka wapate nyaraka zote!" Mama mchungaji akiwa kajilaza kitandani huku anarudia rudia kuangalia ile video alikuwa anajiongelesha Kwa hasira isiyo ya kawaida, kwanza alichomoa earphones masikioni huku akitamani kumeza Mtu!.
Akiwa na mawazo na hasira za kujaza Dunia nzima, Mara alisikia makelele sebuleni, ilikuwa ni mabishano Kati ya Revina na Mr Luka, maana Mr Luka alikuwa kaingia ndani bila utaratibu tena Kwa kupiga teke mlango!.

Mama mchungaji ilibidi atoke kwenda kujionea kinacho endelea!.

"Bora umetoka mwenyewe! Hizo nyaraka ulizo chimba huko nyuma zilete hapa, haiwezekani tutumie nguvu na gharama alafu wewe uje uchimbe kirahisi tu!" Mr Luka mishipa ikiwa inamtoka aliongea Kwa jaziba!.

"Hahaaaaaa!! Ebu nicheke mie! Hivi Mr Luka ujasiri wa kunifokea unaupata wapi!? Unazidai hizo nyaraka kama nani!? Kwa mamlaka ipi!? Au huo ukatibu wa Jimbo ndo umeamua kuuhamishia nyumbani Kwangu!?" Mama mchungaji aliongea Kwa nyodo na kujiamini huku naye akiwa na hasira za ndani Kwa ndani!.
Yaani kauli ya Mama huyo ilifanya Mr Luka na Melisa waamini kwamba Mama mchungaji alifukua na kupata Nyaraka!.

"Kama hutaki tuharibu mambo lete Hizo nyaraka lazima share ifanyike, mtoto wa Nemeke kwanza ndo mwenye Haki kuliko hata wewe, unafikiri tukimpelekea Hizi taarifa itakuwaje!?" Mr Luka alizungumza Kwa msisitizo!.

"Hahaaaaaa eti mtoto wa Nemeke! Kwa Hiyo mnanifanya Mimi mjinga Siyo!?" Mama mchungaji alizungumza huku akiwa anapekua kwenye Simu yake, aliingia Whatsapp na kufungua ile video Kisha aliwapatia wajionee!.
Mr Luka na Melisa baada ya kuona ile video kwanza walibaki wanatazamana Kwa aibu huku wakiwa hawaelewi hata wazungumze nini!, Walipo angalia pale juu namba ya Mtu aliye tuma ilikuwa haijaseviwa, ila Mr Luka Hata Melisa mwenyewe waliitambua vyema ile Namba!.

"Shiitiiii!! Jofu ! Jofu huyu mtoto kumbe mpuuzi! Hivi!" Mr Luka akiwa na hasira alijiongelesha Kwa hasira, huyo Jofu alikuwa ni yule mwanasheria ambaye Jedi alimpatia ushahidi wote!!.

"Haya ongeeni mniambie kwamba huyo mtoto ni wa Nemeke! Na najua mmenidanganya kwamba Nyaraka zimefukiwa nyuma ya nyumba huwenda hata mshazipata! Kwa taarifa yenu huko nyuma zijakuta kitu!" Mama mchungaji aliongea Lakini hakuna aliye Amini kwamba hajakuta kitu, wote walijua amezipata nyaraka ila sababu ni Kwa Vile kagundua kwamba yule Habir Siyo mtoto wa Nemeke.

Mr Luka na Melisa pamoja na Vijana walio kuja nao waliondoka Kwa aibu maana tayari Siri zao Mama mchungaji alikuwa kazijua! Yaani Mr Luka alikuwa na hasira isivyo kawaida huku akiwa na uhakika kwamba mwanasheria Yule ndo kamtumia video Mama mchungaji!.

"Huu ujinga! Madogo wengine wehu kabisa, yaani alitupatia zile flash disk kumbe amebaki na kopi! Mjinga Sana yule ona Sasa!" Mr Luka wakiwa njiani alikuwa analalamika Njia nzima!.

"Mr Luka Kwa Nini tusimtumie Yule Revina kuiba nyaraka pale nyumbani kwa Mama mchungaji, ujue Yule Binti ana Tamaa ya Pesa!?"

"Hilo nalo wazo! Ila Kwa saizi ngoja tumalizane na Jofu kwanza haiwezekani tunafanya mipango tunampa Pesa ya kutosha yeye anatusaliti!" Mr Luka aliongea Kwa hasira!.
Muda huo Jedi na Majaribu Bado walikuwa wanaendelea kukaa Kwa Lameck, japo kuwa walikuwa wanakaa Mguu pande!.

"Heeeee bro Jedi! Ile video bado haijamfikia mlengwa Nini, mbona mwanasheria hajaja!"wakiwa wametulia pale nyumbani kwenye varanda Majaribu alimuuliza Lameck!.

"Majaribu we subiri tu si anatukwepa!!? Jana Lameck si alitwambia rafiki yake yupo Dubai kikiwaka huko lazima atakuja tu hapa!" Jedi alijibu, na hilo ni ushahidi tosha kwamba Jedi na Majaribu ndo walituma ile video iliyo mfikia Mama mchungaji, njia Gani waliitumia Mimi na Wewe hatujui.

Upande wa Pili kijana anaye itwa Jofu akiwa kwenye ofisi yake ya wanasheria ambayo alikuwa ameifungua Mara alishangaa pale ofisini kwake Mr Luka na Melisa wanafika tena wakiwa wamefula hasira isivyo kawaida!.

"Jofu Kwa Hiyo umeamua Sasa kutusaliti na kushirikiana na Mama mchungaji! Yaani mjinga wewe ndo wakutuharibia kiasi hiki!?" Mr Luka baada ya kufika ofisini alimkunja Jofu huku akiwa anaongea Kwa Hasira!.
Kwanza kijana Jofu alibaki katumbua Macho huku akiwa haelewi, maana yeye alikuwa hajafanya kitu!.

"Boss Mimi mbona sijafanya chochote, alafu hata huyo Mama mchungaji sina mazoea naye!" Jofu alijitetea!.
"We mpuuzi unafikiri kuna kitu utadanganya Kwa taarifa yako tumeona Kwa Macho yetu hatujaambiwa na Mtu ebu lete Simu yako hapa, toa password!" Mr Luka aliongea.
Kwakuwa Jofu alikuwa anajiamini na alikuwa anajua hajafanya kitu alitoa Simu na kumpatia Luka!.

"Hiki nini! Huyu uliye mtumia hii video nani alafu eti humjui, na umemsevu Boss Namba 1, yaani Alex Wewe wa kufanya hivi!?" Mr Luka baada ya kuingia kwenye upande wa Whatsapp ya Jofu alikuta ni kweli Bwana huyo alituma video, Majira ya Saa Tisa za usiku! Hata kwenyewe Simu yake alipo angalia mafaili ushahidi wote ulikuwa upo kwenye Simu!.

"Jamani mbona Mimi sijatuma! Yaani....." Jofu akiwa anajitetea alikula Bonge la Kofi zito kutoka Kwa Luka!.

"Mpuuzi wewe, yaani unaniuza, Wewe si ulisema hakuna kopi yoyote uliyo nayo Kumbe umesevu kila kitu kwenye Simu, kijana mbaya wewe! Sasa subiri ntakuonesha nguvu Yangu ilipo si unajifanya ndumila kuwili!" Mr Luka alichimba mkwara, baada ya hapo alichukua na Simu ya Jofu, Yeye na Melisa waliondoka!.
Jofu Moja ilikuwa haikai Mbili haiki, yaani alikuwa kachanganyikiwa isivyo kawaida, alihisi kabisa ule mchezo lazima Jamaa yake Lameck anahusika maana alijaribu kufikiria kama watakuwa ni kina Jedi aliona hapana, maana ni tangia apewe ushahidi alikuwa anawazungusha na alikuwa hajawahi kutana nao!.

Masaa yalisogea! Majira ya Jioni kijana Jofu aliona we usinichezee, aliamua kumfuata Lameck huko huko kwake, maana kama ni kumpigia Simu alikuwa hawezi tena maana simu yake alikuwa kapokonywa!.
Muda huo Lameck alikuwa kakaa nyumbani kwake na kina Jedi wanacheza karata pale sebuleni! Mara gafla walishituka Mtu anasukuma mlango na kuingia kama mvamizi!.

Je Kipi kiliendelea!? Majaribu na Jedi walifanyaje fanyaje mpaka video ikaenda na Namba ya Jofu.

Tukutane sehemu ya 12



Hadithi: MAJARIBU

Mtunzi:Mwaki Ze Done (0653814440)

Sehemu: 12

Muda huo Lameck alikuwa kakaa nyumbani kwake na kina Jedi wanacheza karata pale sebuleni! Mara gafla walishituka Mtu anasukuma mlango na kuingia kama mvamizi!.

"Oya Jofu mwanangu pigo Gani hizo Sasa unaingia ndani kama mvamizi, je ningekuwa nipo na Shemeji Yako nafanya Yangu je!" Lameck aliuliza Kwa kupaniki maana Jofu aliingia Kwa vurugu Kwanza aliwashitua!.

"Oya mwanangu Lameck usenge ulio ufanya najua, Kwa Hiyo unataka wewe ndo uonekane unapiga kazi Sana Siyo!?" Akiwa na jaziba Jofu aliuliza!.

"Mbona hueleweki Mzee! Umevuta Bangi au kitu gani!? Mambo gani nimefanya!" Lameck akiwa anashangaa aliuliza!.

"Au Siyo unajifanya hamnazo eeee! Au na Wewe unataka Siri Zako niwachane Hawa madogo!" Jofu aliuliza!.

"Jamani kuna nini!? Jofu ebu Njoo kwanza nje tuzungumze" Lameck ilibidi kwanza amvutie Jofu nje ili akina Majaribu wasiendelee kusikia!.
Basi Jedi na Majaribu walitazamana Kisha walichekeleana, maana walikuwa wanajua kimeumana!.

Huku nje ilikuwa ni balaa! Jofu alikuwa haamini kama Lameck hajafanya kama alivyo jitetea!.

"Sasa Lameck mwanangu kama Siyo Wewe ni nani, kama ni Hawa madogo Mimi sijawahi kutana nao, hata ninapo kaa hawapajui, Simu Yangu hawajawahi gusa Hiyo inaingia Vipi akilini!" Jofu Bado alikuwa haamini!!.

"Mwanangu Haki ya Mungu Mimi siwezi kufanya huo upuuzi!! Mimi na wewe tumetoka mbali tangia enzi hizo skuli, isitoshe Mimi ndo niliye kuunganisha Kwa Mr Luka ningewezaje kufanya hivyo Sasa!?"Lameck alijitetea Kwa hisia mpaka Jofu alishusha Hasira japo kuwa Bado alikuwa haamini kama Lameck hajafanya huo mchezo!!.
Lameck alianza kuwahisi kina Jedi Japo ilikuwa Siyo Sana! Basi Jofu aliondoka na Lameck alirudi ndani!.

"Oya Lameck Jamaa kaondoka! Mimi nikajua amekuja kwenye maswala ya Kesi unajua sikuelewi huyo jamaa yako, juzi tu mlisena yupo Dubai! Kama kashindwa Kazi basi arudishe ushahidi tutafute mwanasheria mwingine, maana ushahidi wenyewe ndo ule ule nao niliupata Kwa shida kweli!" Jedi akiwa serious aliongea Kwa Kufoka!.

"Mwanangu usijisahaulishe hapa upo nyumbani Kwangu, Kwa Hiyo punguza Sauti usinikoromee! Naweza nikwatimua na mkakosa pa kwenda! Isitoshe naweza kwenda kuwachoma Kwa wale askari magereza maana wanakusaka Sana wanataka Pesa zao ulizo waahidi!" Lameck alifoka na aliongea Kwa jaziba! Kifupi rangi yake ilianza kuonekana!.
Jedi ilibidi awe mpole wala hakuongeza neno! Pia Majaribu naye alitulia kama Hana mdomo!.

Masaa yalisogea ikiwa ni majira ya usiku wa Saa Sita Jedi akiwa na Majaribu, Bwana Jedi alitoa Simu ambayo alikuwa anaitumia kisiri na kuficha Lameck asije akaiona!.
Baada ya hapo Jedi aliingia kwenye Simu ile alichagua baadhi ya video na audio alafu alizituma Kwenye namba ambayo alikuwa kasevu Mrs Nemeke, na alisindikiza na ujumbe mrefu!.

Upande wa Pili Mama mchungaji akiwa kalala huku ana mawazo tele haswa baada ya kugundua kwamba Mr Luka na Melisa wanamzunguka Mara alisikia ujumbe unaingia, na alipo angalia ilikuwa ni upande wa Whatsapp, Basi Mama huyo alifungua ili aone kitu Gani katumiwa!.
Hakika Jasho lilianza kumtoka Mama Yule kule chumbani usiku ule, mapigo ya Moyo yalikuwa yanaenda Kasi isivyo kawaida, yaani mwili mzima ulikuwa unatetemeka!.

Ilikuwa ni video ambayo ilikuwa imerekodiwa pale kwake, Yeye na kundi Zima wakiwa wanajadiliana tena wakiwa wanahusisha na Jinsi walivyo shirikiana kumuua mchungaji Nemeke!, Pia Audio ambazo alikuwa katumiwa zilikuwa ni Sauti zake tena zikiwa zinadhihirisha laivu kwamba Mama huyo alihusika kwenye Kifo Cha mumewe!.
Alafu Chini yake baada ya zile video kulikuwa na ujumbe!.

"Kama hutaki hizo video ziende Mitandaoni naomba tukutane saizi Eneo la uwanja wa shule ya Azimio, na uje pekee yako Mimi ni Mtu mwema kwako, na kingine ambacho hukijui Mr Luka ana mpango wa kukuuwa Wewe!" Huo ni ujumbe ambao ulikuwa upo pale Chini!.
Kwa Jinsi mama mchungaji ambavyo alikuwa kachanganyikiwa, wala hakuhofia kama unaweza kuwa mtego, yaani aliamuka na kuvaa gauni lake bila hata kumuaga Mtu aliwasha Gari na kuelekea huko aliko ambiwa wakutane na Mtu huyo ambaye hata hamjui!.

Mama mchungaji aliendesha Gari Kwa vurugu usiku ule huku akiwa kapaniki! Na kichwani mwake alikuwa anajuta kumuua Mumewe! Na swala la Mama huyo kumuua mumewe ilikuwa ni ushawishi na uchochezi wa Mr Luka!.

Muda huo huo Jedi akiwa na Majaribu walionekana wapo uwanjani kwenye kona huku wakiwa wamejibana kuona kama Mama mchungaji atafika, maana wao ndo walikuwa wamemtumia zile video!.
Wakiwa wapo pale waliona kuna Gari inafika pale uwanjani Kwa vurugu na ilienda kusimama Katikati ya uwanja wa shule! Baada ya hapo Mama mchungaji alishuka huku mwili mzima ukiwa unatetemeka, alikuwa anaangaza huku na kule!.

Basi Jedi akiwa kavaa Kofia mpaka kwenye pua huku akiwa kajifunika uso baada ya kuthibitisha kwamba Mama Yule amekuja pekee yake naye alisogea pale Huku Majaribu akiwa anafuata nyuma!.
Mama mchungaji kwanza alipo muona Majaribu ilibakia kidogo akimbie maana aliamini ni mzimu, Jedi hakutambulika kwa sababu alikuwa kaziba uso!.

"Heeeee we mtoto si walisema umekufa na nilishuhudia kabisa mwili wako wewe nani kwanza!?"Mama mchungaji akiwa anatetemeka aliuliza!.

"Hicho sicho tulicho kuitia hapa Mama! Kitu tulicho kuitia ni Wewe kwenda mbele ya vyombo vya habari kusafisha Jina la Majaribu! Hicho ndo kitu kikubwa!" Jedi aliongea maneno ambayo yalifanya Mama mchungaji Macho yamtoke na aone kama Dunia inazunguka!.

"Heeeee kivipi mbona sikuelewi!?" Mama mchungaji akiwa na kigugumizi aliuliza!.

"Mama najua unajua kwamba Huyu mtoto hakumuua Nemeke, pia unajua nyie na wenzako ndo mlio husika na Kifo, Kwa taarifa Yako wenzako Wana mipango mibaya na Wewe wanataka wahakikishe kila kitu wanakichukua wao, Sasa Sisi tupo Tayari kusaidiana na Wewe na kuwaangusha akina Mr Luka, kikubwa inabidi uende mbele ya vyombo vya habari uelezee kwamba Majaribu hakuhusika na chochote Bali ni kina Mr Luka ndo walihusika! Wewe funguka kila kitu!" Jedi aliongea Kwa msisitizo!.

"Heeeee mbona Hiyo ngumu Kwangu! Kwanza Wewe Kwa Nini unataka nifanye hivyo!?" Mama mchungaji aliuliza!.
Kwanza ilibidi Jedi amsimulie Mama mchungaji kila kitu ambacho Nemeke alimfanyia Dada yake na pia alivyo wapora Mali, yaani alielezea kila kitu Mpaka kuhusu yule mtoto Habir!.

"Heeeee!! Kweli dunia kubwa jamani! Nimeishi na Nemeke zaidi ya Miaka ishirini na kitu sijawahi jua kama ana tabia za hovyo hivyo! Ila pamoja na Yote Mimi siwezi kufanya hicho unacho taka Kwa sababu Mr Luka akikamatwa hata Mimi ntakamatwa, maana huo ushahidi unanionesha na Mimi" Mama mchungaji alijibu!.

"Mama mchungaji hili Siyo ombi ni lazima, kama unataka Basi Wewe mwaga ugali Sisi tumwage mboga na Kesho ikifika Jioni hujatekeleza nilicho kwambia kila kitu kinaenda mtandaoni na Jina la Majaribu litajisafisha lenyewe maana watu wataona ukweli!" Jedi ilibidi Sasa aongee serious kama mwanaume!.
"Baba usifanye hivyo, Siyo Kwamba Mimi simuonei huruma huyo mtoto ila Sasa ushahidi huo mlio nitumia unatufunga wote! Ntawezaje kuwakataa!!?" Mama mchungaji alikuw
a anaongea Huku anatetemeka, Kama ni Maji yalikuwa yamefika shingoni!.

Je Ipi hatima ya Mama mchungaji atakubali au liwalo na liwe!??

Tukutane sehemu ya 13
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…