maundumwingizi
Member
- Aug 1, 2016
- 7
- 17
KITANDA CHA KUWADI
LUCY aligonga mlango, na kabla hajajibiwa, akaingia moja kwa moja hadi ndani. Alipokwisha kuingia, ndipo macho yake yalipiga kwenye sofa. Akamwona Teddy akiendelea kusoma kitabu kilichokuwa mikononi mwake, akiwa amelijilaza kifuani pa Eddy, aliyekuwa akimchezea nywele zake kwa mkono mmoja, ilhali ule mwingine ukiendelea kubadili idhaa za runinga kwa rimoti.
“Wenyewe humu ndani,” Lucy alisema baada ya kukutanisha macho na Eddy, aliyekuwa ameugeuzia uso wake mlangoni kufuatia kuhisi mchakato wa miguu, “hamjambo?”
Eddy hapendezwi na kasumba ya Lucy kuingia ndani bila kukaribishwa, walakini alizidhibiti hisia zake; ghadhabu zilibaki moyoni, uungwana akauvaa usoni. Akamlaki, “Oh, Lucy!”
“Karibu shoga,” Teddy naye alimkaribisha huku akijiinua toka kwa Eddy.
“Ahsanteni wapendwa,” Lucy alijibu akitabasamu. Akaendelea, “na kumradhi kwa kukuvamieni ghafla!”
“Ah, usijali Lucy, hapa ni kwako!” Eddy alijafaragua kumtoa hofu. Siku zote Insafu na uadilifu, vimekuwa kama kwamba ni mavazi kwa Eddy. Kama kaburi lifichavyo maiti, vivyo hivyo, ukakasi wowote moyoni mwake, aliudhibiti kwa furaha ya usoni.
“Haya, karibu uketi mrembo!” Teddy alimwonesha kwa ishara ya kidole mahala pa kuketi.
“Hata nakaa basi,” Lucy alijibu, “nataka tu nikuudhi kidogo shemeji yangu!” alimalizia sentensi yake huku akimgeukia Eddy.
“Haki ya Mungu, mwaka huu nitakutoza faini, Lucy!” Eddy alitania na kufanya kicheko hafifu. Alikwishaelewa shida ya Lucy; kumchukua Teddy na kwenda naye kwake. “Haya, huyo hapo, kazi kwenu!”
“Ahsante mwaya shemeji yangu,” Lucy alijibu huku akiachia tabasamu. Alimgeukia Teddy akimwashiria watoke.
Teddy alijisogeza karibu ya Eddy. Akambusu juu ya paji la uso, akimwambia, “I love you!” kisha akainuka. Alitoka akifuatana na Lucy. Hakuwa na haja ya kujiandaa kwa libasi wala manukato, kwakuwa hawakuwa wakienda mbali. Dera lake nadhifu la rangi ya manjano, lilitosha kuyasitiri maungo yake.
Macho ya Eddy, yaliendelea kuwaangalia akina Lucy, hadi walipopotelea kwenye korido nyembamba, inayokwenda moja kwa moja hadi kwenye mlango wa nyuma. Huko ndiko inakoanzia sehemu ya pili ya upande anaoishi Lucy. Kisha, macho yalihamia kwenye picha iliyoning’inizwa juu ya mlango huo wa korido, ikimwonesha Eddy akiwa ametinga suti maridadi ya rangi ya kahawia. Teddy akiwa ndani ya shela aghali. Wote wakiwa na nyuso zenye bashasha. Nyuma yao, wakionekana wazazi na ndugu zao. Mwaka mmoja tu umepita, tangu picha ile ilipopigwa. Ilikuwa siku ya harusi yao.
Lucy Kingu, msichana wa Kizigua, mwenye kila sababu ya kuitwa mrembo kwa namna Muumba alivyokisanifisha vyema kiwiliwili chake. Ufupi usiochusha na mirindimo mithili ya Mjaluo, vilimfanya kila aliyekutana naye, ageuke mara mbilimbili kumtazama. Na hata lafudhi yake ni ya pwani, ambayo siku zote huitolea puani, kiasi cha kuweza kumfanya nyoka atoke pangoni. Ima kuhusu ucheshi wake, imedhihiri, ni wa kiwango cha kuweza hata kuingia ndani mwa watu bila kukaribishwa. Maisha yake ya fahari na anasa yalisadifu mwonekano wake. Ingawaje, vyanzo vya kipato chake viliendelea kuwa fumbo lililokosa mfumbuaji.
Lucy ni mpangaji mwenzao na akina Eddy, katika nyumba hiyo, ambapo Eddy na mkewe, walipanga upande wa mbele, ilhali yeye Lucy, akiwa amepanga upande wa sehemu ya nyuma, wa mjengo huo aghali na wa kisasa.
Aghalabu, siku za Jumamosi na Jumapili, Lucy humfuata Teddy na kwenda naye kwake kwa minajili ya kumsaidia mambo kadhaa ikiwemo, usafi wa nyumba pamoja upangaji wa samani za ndani. Siku nyingine, kupanga vyombo kabatini na ghasia za namna hiyo. Kama ilivyo kawaida ya mazoea, yakajenga tabia. Ikafikia kiasi, hata kama hapakuwa na cha kufanya, bado Lucy alimwendea Teddy kwa ajili ya kwenda kupiga naye soga tu.
Tabia hii haikumpendeza sana Eddy. Walakini aliipuuza, hakuyona madhara yake kwa nyakati zile. Ukizingatia, Lucy na Teddy hawakuwa na wasaa wa kutosha kuonana na kuwa pamoja mara kwa mara, zaidi ya mwishoni mwa wiki, tena kwa muda mchache tu. ‘Shemeji, nimekuja kumuiba bibiye kidogo!’ ama,‘Nataka nikuudhi kidogo shemeji yangu.’ Ndiyo yalikuwa maneno matamu toka kwa Lucy, akiyatumia kama utangulizi wa kumlainisha Eddy pindi amtakapo Teddy.
Upole wa Eddy uliosababishwa na uungwana wake, haukuweza kukabiliana na uchakaramu wa Lucy kila alipodiriki kumhitaji Teddy. Ingawaje, Teddy naye hakuonekana kuufurahia sana mchezo huo wa kuchukuliwa mara kwa mara, lakini hakuupinga.
____________
“MBONA kama leo umechangamka sana shosti. Kunani?” Teddy alimsaili Lucy hali usoni amekunja ndita kiudadisi.
“Kha! Ina maana umesahau?” Lucy alijibu akimgeukia Teddy. Taratibu, waliteremka kwenye ngazi za mlangoni. “Si nilikwambia leo ndiyo Frank anakuja!”
“Oh, No Lucy! Kama mambo yenyewe ndo hayo, hata huko kwako siingii tena!” Teddy aligomea nje ya mlango wa Lucy. “Haya mambo yataniletea matatizo-nilishakwambia.”
“Jamani Teddy, tafadhali usifanye hivyo. Jamaa alikuwa anaomba siku hii ifike haraka aje mkutane. Leo ghafla tu ubadilike kama tumbo la kuharisha!”
“Lucy, siku ile haikuwa serious kihivyo – viweje ukalibebea bango?” Teddy alimjia juu Lucy.
Ghadhabu zilimvaa Lucy. Macho yakambadilika. Alitamani hata amrarue Teddy. Lakini alijitahidi kujidhibiti. Akauvaa uso wa nyani anayesubiri kuuawa kutafuta huruma. Akasema, “Vyovyote iwavyo, nisamehe mimi shoga’angu. Tafadhali usiniangushe. Hebu fikiria, mtu na heshima zake ameacha majukumu yake kwa ajili yako, halafu ghafla tu iwe bure bileshi!”
Maneno ya Lucy yalimmaliza nguvu na kumlainisha kabisa Teddy.
Takribani mwezi sasa, tangu Lucy alipoanza kumkuwadia Frank kwa Teddy, bila ya kujali kuwa Teddy ni mke wa mtu. Vishawishi na maneno matamu vilimwisha Lucy bila dalili ya mafanikio. Wa aidha, Frank naye kupitia kwa Lucy, alijitahidi kumwagizia Teddy vijizawadi vya mara kwa mara, hadi kufikia siku hiyo ambapo, kwa mujibu wa Teddy ni kwamba haikuwa serious. Tangu awali, Lucy alishawishi ifanyike miadi baina yao hapo nyumbani kwake. Lengo likiwa kutokum-makinisha Eddy juu ya kinachoendelea. Na, kwakuwa Teddy hakupinga, Lucy alilichukulia kwa umuhimu huo, akiamini ule usemi wa Kiyunani, kwamba,‘kimya humaanisha ndiyo’.
Nikirudi kwangu muda huu, Eddy atahisi kuna jambo. Teddy alijifikiria. Haikuwa kawaida yake kutoka nyumbani kwake na kwenda kwa Lucy, kisha arudi ghafla namna ile. Hivyo, hofu ikawa, huenda angezua maswali toka kwa Eddy.
“Lakini ni maongezi tu Teddy!” Lucy alimtoa Teddy kwenye lindi la mawazo. Teddy alipouinua uso wake kumtazama, akapata mwanya wa kuendelea. “Kama utaogopa kuongelea naye hapo sitting room, mi’ nitakusabilieni chumba changu.”
Zikateketea sekunde kadhaa wakati Teddy akitafakari. Hatimaye, alilegeza msimamo. “Okay fine, kwa heshima yako Lucy. Ila, nitakaa naye dakika tano tu, si’ zaidi ya hapo.”
Shangwe ililipuka moyoni mwa Lucy. Alitamani ambebe Teddy mgongoni kwa furaha. Kufanikisha mpango huo wa ukuwadi, alijiongezea thamani kwa mfadhili wake, Frank.
“Hayo ni maamuzi yenu shosti. Wala sina pingamizi.” Lucy alijibu. Akaongezea, “kwahiyo chumbani au sitting room?”
Baada ya kukosekana jibu la haraka, Lucy alipendekeza. “Ila mimi nashauri tu, bora mkaongelee chumbani, maana sitting room anaweza kutokea mtu akaingia, akakuhamisheni kwenye mazungumzo – yote kwa yote, chaguo ni lako!”
Teddy aliafiki chumbani.
Walipanda ngazi. Wakaingia ndani. Teddy akawa wa kwanza kujitosa chumbani, kwakuwa chumba kilikuwa mwanzo kabisa kabla ya kuifikia sebule. Lucy akiwa amechanulisha tabasamu usoni, haraka alikwenda barazani kumwendea Frank.
Ambacho Teddy na Lucy hawakuking’amua ni kwamba, wakati wakiendelea kujibizana na kushawishiana pale nje, Eddy alikuwa akiwaona kupitia madirisha madogo ya msalani. Ilitokea kwa sadfa tu, Lucy na Teddy walipotoka kule kwake, Eddy aliinuka na kwenda msalani. Baada ya kukidhi haja yake na kusimama, ndipo aliwashuhudia wakilumbana.
____________
CHUMBA cha Lucy ni chenye kupendezesha macho na kuburudisha ubongo. Si tu kwa hewa mwanana iliyopozwa kwa kiyoyozi, bali pia kwa namna upangaji wa samani ulivofanywa kisanii; Kitanda kikubwa cha futi sita kwa sita, kiliegeshwa mashariki mwa chumba; Runinga kubwa na bapa ya Samsung iliyokuwa ikicheza nyimbo za Kihindi kwa sauti hafifu, ilibandikwa kiufundi ukutani huku nyaya zitokazo kwenye ungo ulioegeshwa juu ya paa la vigae, na zile zinazokwenda kwenye deki, zikiwa zimejaladiwa vema na tranki maalumu, ili kufanya mazingira kuwa nadhifu; Kaskazini mwa kitanda, paliwekwa viti viwili maridadi vilivyochongwa kwa mninga, katikati vilitenganishwa na meza ndogo ya kioo; Jokofu dogo lilikuwa dhiraa chache nyuma ya kabati kubwa la nguo lililopambwa kwa maua. Vyote hivyo, vikiwa juu ya zulia zito na laini mithili ya sufi.
Baada ya kuingia chumbani, Teddy alijibwaga kitandani kiasi cha kufanya miguu yake ipepee angani. Lakini ghafla, haikupita muda akiwa hapo kitandani, kama aliyejihadhari jambo, upesi aliinuka kitandani. Akahamia kwenye moja kati ya viti viwili. Bila shaka, hakutaka Frank amkute kitandani, kitu alichohisi kingemtengenezea fikara mbaya kichwani.
Haikuchukua walau dakika moja tangu Teddy alipoketi, mlango ukafunguliwa. Frank akaingia. Moyo wa Teddy ulipiga kwa kasi ya ajabu. Akajikuta akipoteza mhimili wa kujiamini, akawa mithili ya mbwa aliyemwona chatu. Hakuelewa ni kwanini hasa aliingiwa na hali ile ya kutojiamini. Pengine ni kwa sababu haikuwahi kutokea, hata siku moja, akakaa faragha ya mapenzi na mwanaume mwingine zaidi ya mumewe tangu alipoolewa. Ama pengine, ni nyota tu ya Frank iliizidi nguvu ile ya kwake.
Baada ya kufunga mlango, Frank aligeuka na kumwangalia Teddy. Uso wake ulichanulisha tababasamu. Alimsogelea na kumsabahi kwa bashasha. “Oh, mrembo – mambo!”
“Poa, karibu!” Teddy alijibu. Alijilazimisha kuiondosha hofu iliyokwishaanza kumnyima hali ya kujiamini kiasi cha kumkosesha uhuru.
Frank alijongea. Akaketi kwenye kiti kidogo kilichobaki jirani na alichokalia Teddy. Sasa, wakawa wanawajihiana uso kwa macho, wakitenganishwa na kile kijimeza kidogo cha kioo. Harufu ya marashi aliyojinyunyizia Frank, ilibadili kabisa reha ya chumba hicho kiasi cha kumnyanyasa Teddy kisaikolojia, baada kukiri kwamba yeye hakuwa akinukia.
“Teddy,” Frank aliita akimtazama Teddy, uso ungali ukichanua kwa tabasamu. Teddy alipoyagonganisha macho yake yaliyojaa junaa, akakosa pozi. Akamfanya Frank kuendelea. “Bahati iliyoje kukutana nawe leo hii. Nimefurahi sana.”
“Mimi pia.” Teddy alijibu akiyakwepesha macho yake yaliyokolea wanja wa chini.
“Hii ni bahati kubwa sana kwangu. Sina budi kukushukuru!” Frank alisema, sauti yake ikikosa haraka.
“Bahati kukutana tu?” Teddy alisaili. Akafuatisha kicheko hafifu ili kukabiliana na hofu iliyokuwa imemganda moyoni. Hakutaka kuonekana mshamba, asiyejiamini, au anayejirahisi.
Ambacho Teddy alianza kukisahau ni kwamba, zile dakika tano alizosisitiza kuzitumia bila kuzidisha japo sekunde, zilikwishakukatika.
“Naam.” Frank alisadikisha maneno yake. Huku akiendelea kumtazama Teddy, hakuwa haba wa maneno. “Ni bahati iliyoje kukutana kwa mara ya kwanza na mtu niliyempenda hata akafanikiwa kuichachafya akili yangu!”
“Mmh, wanaume kwa uongo! Vile ulivyo serious utadhani ni kweli unenayo!”
“Kha! Hivi huamini kweli, Teddy?” Frank alijiulizisha huku akiitoa ile meza ndogo katikati yao. Akaiweka pembeni. Akakiburuza kiti chake. Akamsogelea Teddy kwa karibu, hadi magoti yalipogoteana.
“Teddy,” Frank alisema, mikono yake akiipeleka na kuikutanisha na ile ya Teddy. Kwa sauti nzito, yenye kuutetemesha moyo wa Teddy, akasema, “Nakupenda sana. Sina hata chembe ya ulaghai. Na sijaanza leo kukupenda!”
Kikapita tena kimya kifupi, Teddy aliyahamisha tena macho yake. Akayazugisha runingani. Frank aliiinua mikono ya Teddy. Akaibusu.
Mapigo ya moyo ya Teddy yalibadilika. Joto la aina yake likampanda. Dakika tano zikawa kumi. Mara, kumi na tano. Akafunua kinywa, “Lakini Frank, ujue mi’ ni mke wa mtu!”
“I know Teddy. Ninakuahidi sitakubughudhi, wala kukuharibia ndoa yako,” Frank alijitetea. “Na nakuhakikishia, wewe ndiye utakuwa mratibu wa mipango yote katika mahusiano yetu!”
Waliangaliana.
Macho ya Frank yenye kiu na tamaa ya huba yalizidi kuimarika ilhali yale ya Teddy, yenye hofu na kutojiamini yakizidi kulainika. Teddy aliposhindwa kumtazama Frank, akakwepesha kwa aibu.
Frank aliinuka kwenye kiti. Akamsogelea Teddy na kumuinamia. Akambusu kwenye paji la uso. Kama haitoshi, akapiga magoti. Akamwambia kwa sauti ya kubembeleza, “Teddy, tafadhali niamini. Nakupenda! Nakupenda ile mbaya!”
Unajisikiaje kubembelezwa kwa kupigiwa magoti na tajiri, kijana mtanashati? Wazo lilimjia Teddy.
Frank, kijana mkwasi, anamiliki vituo kadhaa vya mafuta; petrol na diesel. Kama haitoshi, anamiliki jengo kubwa la biashara jijini Dar es Salaam, liitwalo Home of Shopping. Zaidi, ana utitiri wa nyumba na magari ya kifahari. Sehemu ndogo ya urithi wa marehemu baba yake, pamoja na biashara za haramu, vilimfanya aendelee kudumu kwenye orodha ya vijana wadogo wenye ukwasi wa kusaza.
Frank hachoshi kumtazama. Urefu kimo chake. Ucheshi haiba yake. Jamali sura yake. Utajiri tunu yake. Na, kama walivyo vijana wengi wakwasi, wanawake ugonjwa wake (ingawaje hili hakuna wa kulithibitisha hadharani kwakuwa lilifanyika faraghani).
Nani asiyeiota bahati ya kuliliwa na mtu huyu? Teddy aliendelea kutafakari, hata asitambue, muda huo tayari alikuwa amemkumbatia Frank.
Frank hakuruhusu kuipoteza nafasi hiyo ya kukumbatiwa. Akamsogezea Teddy mdomo wake. Milio mithili ya ile ya kasuku ilisikika baina yao. Taratibu, ulimi wa Frank uliaanza kutalii kinywani mwa Teddy. Joto nalo, halikufanya ajizi kuwachemka maungoni. Wakazoana msobemsobe. Wakajibwaga kitandani huku dera la Teddy likipeperushwa na upepo. Piga picha mwenyewe. Kama upepo tu umelipeperusha, vipi litamshinda Frank?
Bashasha na taadhima usoni, ni udhihirisho wa uungwana moyoni. Kwa hivi, kwa mwonekano wa Frank, Teddy alijihisi yu katika mikono salama. Hivyo, bila hiyana, alimsabilia Frank mwili wake. Akamsusia maungo yake.
____________
HADITHI: Kitanda cha Kuwadi
MTUNZI: Maundu Mwingizi
***ITAENDELEA kesho papa hapa!
LUCY aligonga mlango, na kabla hajajibiwa, akaingia moja kwa moja hadi ndani. Alipokwisha kuingia, ndipo macho yake yalipiga kwenye sofa. Akamwona Teddy akiendelea kusoma kitabu kilichokuwa mikononi mwake, akiwa amelijilaza kifuani pa Eddy, aliyekuwa akimchezea nywele zake kwa mkono mmoja, ilhali ule mwingine ukiendelea kubadili idhaa za runinga kwa rimoti.
“Wenyewe humu ndani,” Lucy alisema baada ya kukutanisha macho na Eddy, aliyekuwa ameugeuzia uso wake mlangoni kufuatia kuhisi mchakato wa miguu, “hamjambo?”
Eddy hapendezwi na kasumba ya Lucy kuingia ndani bila kukaribishwa, walakini alizidhibiti hisia zake; ghadhabu zilibaki moyoni, uungwana akauvaa usoni. Akamlaki, “Oh, Lucy!”
“Karibu shoga,” Teddy naye alimkaribisha huku akijiinua toka kwa Eddy.
“Ahsanteni wapendwa,” Lucy alijibu akitabasamu. Akaendelea, “na kumradhi kwa kukuvamieni ghafla!”
“Ah, usijali Lucy, hapa ni kwako!” Eddy alijafaragua kumtoa hofu. Siku zote Insafu na uadilifu, vimekuwa kama kwamba ni mavazi kwa Eddy. Kama kaburi lifichavyo maiti, vivyo hivyo, ukakasi wowote moyoni mwake, aliudhibiti kwa furaha ya usoni.
“Haya, karibu uketi mrembo!” Teddy alimwonesha kwa ishara ya kidole mahala pa kuketi.
“Hata nakaa basi,” Lucy alijibu, “nataka tu nikuudhi kidogo shemeji yangu!” alimalizia sentensi yake huku akimgeukia Eddy.
“Haki ya Mungu, mwaka huu nitakutoza faini, Lucy!” Eddy alitania na kufanya kicheko hafifu. Alikwishaelewa shida ya Lucy; kumchukua Teddy na kwenda naye kwake. “Haya, huyo hapo, kazi kwenu!”
“Ahsante mwaya shemeji yangu,” Lucy alijibu huku akiachia tabasamu. Alimgeukia Teddy akimwashiria watoke.
Teddy alijisogeza karibu ya Eddy. Akambusu juu ya paji la uso, akimwambia, “I love you!” kisha akainuka. Alitoka akifuatana na Lucy. Hakuwa na haja ya kujiandaa kwa libasi wala manukato, kwakuwa hawakuwa wakienda mbali. Dera lake nadhifu la rangi ya manjano, lilitosha kuyasitiri maungo yake.
Macho ya Eddy, yaliendelea kuwaangalia akina Lucy, hadi walipopotelea kwenye korido nyembamba, inayokwenda moja kwa moja hadi kwenye mlango wa nyuma. Huko ndiko inakoanzia sehemu ya pili ya upande anaoishi Lucy. Kisha, macho yalihamia kwenye picha iliyoning’inizwa juu ya mlango huo wa korido, ikimwonesha Eddy akiwa ametinga suti maridadi ya rangi ya kahawia. Teddy akiwa ndani ya shela aghali. Wote wakiwa na nyuso zenye bashasha. Nyuma yao, wakionekana wazazi na ndugu zao. Mwaka mmoja tu umepita, tangu picha ile ilipopigwa. Ilikuwa siku ya harusi yao.
Lucy Kingu, msichana wa Kizigua, mwenye kila sababu ya kuitwa mrembo kwa namna Muumba alivyokisanifisha vyema kiwiliwili chake. Ufupi usiochusha na mirindimo mithili ya Mjaluo, vilimfanya kila aliyekutana naye, ageuke mara mbilimbili kumtazama. Na hata lafudhi yake ni ya pwani, ambayo siku zote huitolea puani, kiasi cha kuweza kumfanya nyoka atoke pangoni. Ima kuhusu ucheshi wake, imedhihiri, ni wa kiwango cha kuweza hata kuingia ndani mwa watu bila kukaribishwa. Maisha yake ya fahari na anasa yalisadifu mwonekano wake. Ingawaje, vyanzo vya kipato chake viliendelea kuwa fumbo lililokosa mfumbuaji.
Lucy ni mpangaji mwenzao na akina Eddy, katika nyumba hiyo, ambapo Eddy na mkewe, walipanga upande wa mbele, ilhali yeye Lucy, akiwa amepanga upande wa sehemu ya nyuma, wa mjengo huo aghali na wa kisasa.
Aghalabu, siku za Jumamosi na Jumapili, Lucy humfuata Teddy na kwenda naye kwake kwa minajili ya kumsaidia mambo kadhaa ikiwemo, usafi wa nyumba pamoja upangaji wa samani za ndani. Siku nyingine, kupanga vyombo kabatini na ghasia za namna hiyo. Kama ilivyo kawaida ya mazoea, yakajenga tabia. Ikafikia kiasi, hata kama hapakuwa na cha kufanya, bado Lucy alimwendea Teddy kwa ajili ya kwenda kupiga naye soga tu.
Tabia hii haikumpendeza sana Eddy. Walakini aliipuuza, hakuyona madhara yake kwa nyakati zile. Ukizingatia, Lucy na Teddy hawakuwa na wasaa wa kutosha kuonana na kuwa pamoja mara kwa mara, zaidi ya mwishoni mwa wiki, tena kwa muda mchache tu. ‘Shemeji, nimekuja kumuiba bibiye kidogo!’ ama,‘Nataka nikuudhi kidogo shemeji yangu.’ Ndiyo yalikuwa maneno matamu toka kwa Lucy, akiyatumia kama utangulizi wa kumlainisha Eddy pindi amtakapo Teddy.
Upole wa Eddy uliosababishwa na uungwana wake, haukuweza kukabiliana na uchakaramu wa Lucy kila alipodiriki kumhitaji Teddy. Ingawaje, Teddy naye hakuonekana kuufurahia sana mchezo huo wa kuchukuliwa mara kwa mara, lakini hakuupinga.
____________
“MBONA kama leo umechangamka sana shosti. Kunani?” Teddy alimsaili Lucy hali usoni amekunja ndita kiudadisi.
“Kha! Ina maana umesahau?” Lucy alijibu akimgeukia Teddy. Taratibu, waliteremka kwenye ngazi za mlangoni. “Si nilikwambia leo ndiyo Frank anakuja!”
“Oh, No Lucy! Kama mambo yenyewe ndo hayo, hata huko kwako siingii tena!” Teddy aligomea nje ya mlango wa Lucy. “Haya mambo yataniletea matatizo-nilishakwambia.”
“Jamani Teddy, tafadhali usifanye hivyo. Jamaa alikuwa anaomba siku hii ifike haraka aje mkutane. Leo ghafla tu ubadilike kama tumbo la kuharisha!”
“Lucy, siku ile haikuwa serious kihivyo – viweje ukalibebea bango?” Teddy alimjia juu Lucy.
Ghadhabu zilimvaa Lucy. Macho yakambadilika. Alitamani hata amrarue Teddy. Lakini alijitahidi kujidhibiti. Akauvaa uso wa nyani anayesubiri kuuawa kutafuta huruma. Akasema, “Vyovyote iwavyo, nisamehe mimi shoga’angu. Tafadhali usiniangushe. Hebu fikiria, mtu na heshima zake ameacha majukumu yake kwa ajili yako, halafu ghafla tu iwe bure bileshi!”
Maneno ya Lucy yalimmaliza nguvu na kumlainisha kabisa Teddy.
Takribani mwezi sasa, tangu Lucy alipoanza kumkuwadia Frank kwa Teddy, bila ya kujali kuwa Teddy ni mke wa mtu. Vishawishi na maneno matamu vilimwisha Lucy bila dalili ya mafanikio. Wa aidha, Frank naye kupitia kwa Lucy, alijitahidi kumwagizia Teddy vijizawadi vya mara kwa mara, hadi kufikia siku hiyo ambapo, kwa mujibu wa Teddy ni kwamba haikuwa serious. Tangu awali, Lucy alishawishi ifanyike miadi baina yao hapo nyumbani kwake. Lengo likiwa kutokum-makinisha Eddy juu ya kinachoendelea. Na, kwakuwa Teddy hakupinga, Lucy alilichukulia kwa umuhimu huo, akiamini ule usemi wa Kiyunani, kwamba,‘kimya humaanisha ndiyo’.
Nikirudi kwangu muda huu, Eddy atahisi kuna jambo. Teddy alijifikiria. Haikuwa kawaida yake kutoka nyumbani kwake na kwenda kwa Lucy, kisha arudi ghafla namna ile. Hivyo, hofu ikawa, huenda angezua maswali toka kwa Eddy.
“Lakini ni maongezi tu Teddy!” Lucy alimtoa Teddy kwenye lindi la mawazo. Teddy alipouinua uso wake kumtazama, akapata mwanya wa kuendelea. “Kama utaogopa kuongelea naye hapo sitting room, mi’ nitakusabilieni chumba changu.”
Zikateketea sekunde kadhaa wakati Teddy akitafakari. Hatimaye, alilegeza msimamo. “Okay fine, kwa heshima yako Lucy. Ila, nitakaa naye dakika tano tu, si’ zaidi ya hapo.”
Shangwe ililipuka moyoni mwa Lucy. Alitamani ambebe Teddy mgongoni kwa furaha. Kufanikisha mpango huo wa ukuwadi, alijiongezea thamani kwa mfadhili wake, Frank.
“Hayo ni maamuzi yenu shosti. Wala sina pingamizi.” Lucy alijibu. Akaongezea, “kwahiyo chumbani au sitting room?”
Baada ya kukosekana jibu la haraka, Lucy alipendekeza. “Ila mimi nashauri tu, bora mkaongelee chumbani, maana sitting room anaweza kutokea mtu akaingia, akakuhamisheni kwenye mazungumzo – yote kwa yote, chaguo ni lako!”
Teddy aliafiki chumbani.
Walipanda ngazi. Wakaingia ndani. Teddy akawa wa kwanza kujitosa chumbani, kwakuwa chumba kilikuwa mwanzo kabisa kabla ya kuifikia sebule. Lucy akiwa amechanulisha tabasamu usoni, haraka alikwenda barazani kumwendea Frank.
Ambacho Teddy na Lucy hawakuking’amua ni kwamba, wakati wakiendelea kujibizana na kushawishiana pale nje, Eddy alikuwa akiwaona kupitia madirisha madogo ya msalani. Ilitokea kwa sadfa tu, Lucy na Teddy walipotoka kule kwake, Eddy aliinuka na kwenda msalani. Baada ya kukidhi haja yake na kusimama, ndipo aliwashuhudia wakilumbana.
____________
CHUMBA cha Lucy ni chenye kupendezesha macho na kuburudisha ubongo. Si tu kwa hewa mwanana iliyopozwa kwa kiyoyozi, bali pia kwa namna upangaji wa samani ulivofanywa kisanii; Kitanda kikubwa cha futi sita kwa sita, kiliegeshwa mashariki mwa chumba; Runinga kubwa na bapa ya Samsung iliyokuwa ikicheza nyimbo za Kihindi kwa sauti hafifu, ilibandikwa kiufundi ukutani huku nyaya zitokazo kwenye ungo ulioegeshwa juu ya paa la vigae, na zile zinazokwenda kwenye deki, zikiwa zimejaladiwa vema na tranki maalumu, ili kufanya mazingira kuwa nadhifu; Kaskazini mwa kitanda, paliwekwa viti viwili maridadi vilivyochongwa kwa mninga, katikati vilitenganishwa na meza ndogo ya kioo; Jokofu dogo lilikuwa dhiraa chache nyuma ya kabati kubwa la nguo lililopambwa kwa maua. Vyote hivyo, vikiwa juu ya zulia zito na laini mithili ya sufi.
Baada ya kuingia chumbani, Teddy alijibwaga kitandani kiasi cha kufanya miguu yake ipepee angani. Lakini ghafla, haikupita muda akiwa hapo kitandani, kama aliyejihadhari jambo, upesi aliinuka kitandani. Akahamia kwenye moja kati ya viti viwili. Bila shaka, hakutaka Frank amkute kitandani, kitu alichohisi kingemtengenezea fikara mbaya kichwani.
Haikuchukua walau dakika moja tangu Teddy alipoketi, mlango ukafunguliwa. Frank akaingia. Moyo wa Teddy ulipiga kwa kasi ya ajabu. Akajikuta akipoteza mhimili wa kujiamini, akawa mithili ya mbwa aliyemwona chatu. Hakuelewa ni kwanini hasa aliingiwa na hali ile ya kutojiamini. Pengine ni kwa sababu haikuwahi kutokea, hata siku moja, akakaa faragha ya mapenzi na mwanaume mwingine zaidi ya mumewe tangu alipoolewa. Ama pengine, ni nyota tu ya Frank iliizidi nguvu ile ya kwake.
Baada ya kufunga mlango, Frank aligeuka na kumwangalia Teddy. Uso wake ulichanulisha tababasamu. Alimsogelea na kumsabahi kwa bashasha. “Oh, mrembo – mambo!”
“Poa, karibu!” Teddy alijibu. Alijilazimisha kuiondosha hofu iliyokwishaanza kumnyima hali ya kujiamini kiasi cha kumkosesha uhuru.
Frank alijongea. Akaketi kwenye kiti kidogo kilichobaki jirani na alichokalia Teddy. Sasa, wakawa wanawajihiana uso kwa macho, wakitenganishwa na kile kijimeza kidogo cha kioo. Harufu ya marashi aliyojinyunyizia Frank, ilibadili kabisa reha ya chumba hicho kiasi cha kumnyanyasa Teddy kisaikolojia, baada kukiri kwamba yeye hakuwa akinukia.
“Teddy,” Frank aliita akimtazama Teddy, uso ungali ukichanua kwa tabasamu. Teddy alipoyagonganisha macho yake yaliyojaa junaa, akakosa pozi. Akamfanya Frank kuendelea. “Bahati iliyoje kukutana nawe leo hii. Nimefurahi sana.”
“Mimi pia.” Teddy alijibu akiyakwepesha macho yake yaliyokolea wanja wa chini.
“Hii ni bahati kubwa sana kwangu. Sina budi kukushukuru!” Frank alisema, sauti yake ikikosa haraka.
“Bahati kukutana tu?” Teddy alisaili. Akafuatisha kicheko hafifu ili kukabiliana na hofu iliyokuwa imemganda moyoni. Hakutaka kuonekana mshamba, asiyejiamini, au anayejirahisi.
Ambacho Teddy alianza kukisahau ni kwamba, zile dakika tano alizosisitiza kuzitumia bila kuzidisha japo sekunde, zilikwishakukatika.
“Naam.” Frank alisadikisha maneno yake. Huku akiendelea kumtazama Teddy, hakuwa haba wa maneno. “Ni bahati iliyoje kukutana kwa mara ya kwanza na mtu niliyempenda hata akafanikiwa kuichachafya akili yangu!”
“Mmh, wanaume kwa uongo! Vile ulivyo serious utadhani ni kweli unenayo!”
“Kha! Hivi huamini kweli, Teddy?” Frank alijiulizisha huku akiitoa ile meza ndogo katikati yao. Akaiweka pembeni. Akakiburuza kiti chake. Akamsogelea Teddy kwa karibu, hadi magoti yalipogoteana.
“Teddy,” Frank alisema, mikono yake akiipeleka na kuikutanisha na ile ya Teddy. Kwa sauti nzito, yenye kuutetemesha moyo wa Teddy, akasema, “Nakupenda sana. Sina hata chembe ya ulaghai. Na sijaanza leo kukupenda!”
Kikapita tena kimya kifupi, Teddy aliyahamisha tena macho yake. Akayazugisha runingani. Frank aliiinua mikono ya Teddy. Akaibusu.
Mapigo ya moyo ya Teddy yalibadilika. Joto la aina yake likampanda. Dakika tano zikawa kumi. Mara, kumi na tano. Akafunua kinywa, “Lakini Frank, ujue mi’ ni mke wa mtu!”
“I know Teddy. Ninakuahidi sitakubughudhi, wala kukuharibia ndoa yako,” Frank alijitetea. “Na nakuhakikishia, wewe ndiye utakuwa mratibu wa mipango yote katika mahusiano yetu!”
Waliangaliana.
Macho ya Frank yenye kiu na tamaa ya huba yalizidi kuimarika ilhali yale ya Teddy, yenye hofu na kutojiamini yakizidi kulainika. Teddy aliposhindwa kumtazama Frank, akakwepesha kwa aibu.
Frank aliinuka kwenye kiti. Akamsogelea Teddy na kumuinamia. Akambusu kwenye paji la uso. Kama haitoshi, akapiga magoti. Akamwambia kwa sauti ya kubembeleza, “Teddy, tafadhali niamini. Nakupenda! Nakupenda ile mbaya!”
Unajisikiaje kubembelezwa kwa kupigiwa magoti na tajiri, kijana mtanashati? Wazo lilimjia Teddy.
Frank, kijana mkwasi, anamiliki vituo kadhaa vya mafuta; petrol na diesel. Kama haitoshi, anamiliki jengo kubwa la biashara jijini Dar es Salaam, liitwalo Home of Shopping. Zaidi, ana utitiri wa nyumba na magari ya kifahari. Sehemu ndogo ya urithi wa marehemu baba yake, pamoja na biashara za haramu, vilimfanya aendelee kudumu kwenye orodha ya vijana wadogo wenye ukwasi wa kusaza.
Frank hachoshi kumtazama. Urefu kimo chake. Ucheshi haiba yake. Jamali sura yake. Utajiri tunu yake. Na, kama walivyo vijana wengi wakwasi, wanawake ugonjwa wake (ingawaje hili hakuna wa kulithibitisha hadharani kwakuwa lilifanyika faraghani).
Nani asiyeiota bahati ya kuliliwa na mtu huyu? Teddy aliendelea kutafakari, hata asitambue, muda huo tayari alikuwa amemkumbatia Frank.
Frank hakuruhusu kuipoteza nafasi hiyo ya kukumbatiwa. Akamsogezea Teddy mdomo wake. Milio mithili ya ile ya kasuku ilisikika baina yao. Taratibu, ulimi wa Frank uliaanza kutalii kinywani mwa Teddy. Joto nalo, halikufanya ajizi kuwachemka maungoni. Wakazoana msobemsobe. Wakajibwaga kitandani huku dera la Teddy likipeperushwa na upepo. Piga picha mwenyewe. Kama upepo tu umelipeperusha, vipi litamshinda Frank?
Bashasha na taadhima usoni, ni udhihirisho wa uungwana moyoni. Kwa hivi, kwa mwonekano wa Frank, Teddy alijihisi yu katika mikono salama. Hivyo, bila hiyana, alimsabilia Frank mwili wake. Akamsusia maungo yake.
____________
HADITHI: Kitanda cha Kuwadi
MTUNZI: Maundu Mwingizi
***ITAENDELEA kesho papa hapa!