Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 10,884
- 18,824
Na D. Kingdon.
Makao ya watu yalionekana kando ya vilima, na mbugani, chini ya mteremuko mkubwa unaoingia katika nchi. Makao yao yalikuwa ni jumla ya vibanda na ghala za vyakula ambazo zilizunguuka zizi la ng'ombe; na vyote vilizungukwa na 'milangali'. Katika nchi hii, palikuwa msichana mmoja aitwaye Robi, ambaye aliolewa na Chacha. Huyu Chacha alikuwa mzee, na aliyekwisha oa wake wawili. Mzee Chacha aliweza kumwoa Robi kwa sababu alikuwa tajiri kuliko vijana. Ingawa Robi alikuwa ni mke wa tatu, alistarehe, na aliridhika kumzalia mtoto wa kiume wa kwanza.
Vibanda vyote vilifanana, na viliunganishwa na ua wa miti minene. Kila kibanda kilikuwa na ukuta uliotenga wanyama wagonjwa na ndama mbali na watu. Katika chumba cha watu kulikuwa giza, na pembeni palikuwa kitanda kilichotandikwa ngozi; upande wa miguuni, palikuwa na mafiga.
Mwezi ulipokuwa kamili, wazee walimshauri mganga wa mvua. Alifanya matambiko mengi ya siri, lakini alishindwa.
Akasema, 'Baba zetu wamekasirika, wamezuia mvua.' Walimpa kondoo na mbuzi wawili. Ikaja mvua ya manyunyu, lakini binadamu na wanyama walisubiri kupata mvua ya kutosha ili iondoe dhiki ile. Mwishowe, yakaja mawingu mengi yaliyokusanyika pamoja, yakipita angani. Kulikuwa mvumo wa upepo na mungurumo wa radi.
Sauti za kengele za ngombe zilizidi kwa uziri wakati wipwa wa Chama wakiwarudisha ngombe kwa haraka nyumbani kutoka machungani. Kundi la ng'ombe lilipoingizwa zizini, watoto walifunga mlango kwa magogo mazito. Magogo haya yalifungwa pamoja na mti mrefu ambao ulipita katikati ya jengo la banda upande wa kulia, na kufuata kitanda ili uwape ishara, kama kuna mtu ye yote anayejaribu kufungua mlango usiku. Mvua ilinyesha sana mpaka asubuhi, lakini upepo ulitulia mapema. Robi siku ile alichelewa kuamka, na alipooza sana. Moto ulififia kidogo, na mtoto Mwita alikuwa akilia. Alikuwa mtoto wake wa kwanza kama jina lake lilivyoonyesha; kwa sababu mtoto ye yote wa kiume wa kwanza kuzaliwa huko Kuria, lazima aitwe Chacha, Mwita, au Marwa.
Kwa desturi yao, humwacha mtoto wa kwanza akae na bibi yake, anapotazamiwa wa pili; kwa hiyo, ilimlazimu Mwita amwache mama yake. Basi, kwa masikitiko mengi, Robi alimlisha akamlaza. Kisha aliongeza kuni motoni, na ulipowaka, akakaa kuotea. Hapakuwa mwanga mwingine zaidi ya ule wa moto kibandani, ila ule uliopenya katika nyufa za mlango wa fito kutoka nje. Mionzi mikali ya mwanga iliang'aza ndani ya heleni za shaba ambazo Robi alivaa kujijulisha kuwa ni mwanamke aliyeolewa. Heleni hizi zilipembea katika ndewe kubwa za masikio yake. Bangili zake nzito ziling'aa sana. Alikuwa amezivaa bangili hizi kwa miaka mingi hata zikakata katika mikono yake na kuvimbisha pande zote mbili. Robi alipotoka nje, jamaa zake walikwisha kuamka mapema, wakishughulika na kazi. Ng'ombe walikwisha kukamuliwa na mbegu zilikuwa zimetolewa ghalani. Miti na majani yenye umande yalimeta-meta kwa mwanga wa jua, na Robi alichangamka.
Babu zake Mwita waliishi umbali wa mwendo wa siku nzima, upande wa magharibi. Chacha alimwambia Robi kuwa baada ya kumaliza kupanda, aende huko. Basi, siku moja alfajiri, baada ya kumaliza kupanda, aliiteremsha ngozi yake ya arusi. Ilitundikwa kwa ukanda mkuukuu kwenye pao la nyumba, na ilivaliwa wakati wa sherehe ya kumpeleka mtoto kwa babu zake au wakati wa arusi ya wanawe.
Alimbeba Mwita pamoja na hirizi na dawa zake, ambazo zilikuwa vijiti vidogo, vifuko vidogo vya kamba vilivyofungwa pamoja, shanga za rangi, senti, na kibuyu kidogo kilichopambwa ambacho alipewa na mpenzi wake kabla ya harusi yake.
Alipokuwa akitembea njiani, hali ya nchi ikawa inabadilika kidogo kidogo. Njia yake ilipitia kwenye miinuko na miteremko hata akafikia uwanda wa juu; na ilipofika jioni akateremka kwenye nchi yenye miti mingi. Aliona vilima vidogo vidogo vyenye majabali yaliyochongoka. Pengine alipita mahame ya watu. Hapa ilibaki milangali iliyosongwa na majani na mimea mingine, ambayo ilikuwa makao ya wanyama wadogo wa porini na pengine mizimu ya watu waliokaa hapo. Wakati huu wote jua lilikuwa likichwa na mbingu ilibadilika rangi.
Robi alipofika nyumbani kwa wazazi na ndugu zake, kulikuwa kumetulia. Vibanda vilifungwa na ng'ombe walikuwa zizini. Alibisha hodi, na mara alisikia mlio wa mlango ukivutwa toka kwa ndani ya kibanda. Wasichana wawili walichungulia nje huku wakitafuna makande. Walikuwa wakingojea chakula cha jioni, lakini waliposikia kuwa ni Robi aliyebisha hodi, walitoka nje wote na kumkaribisha kwa furaha. Baada ya kupeana mikono na kuongea kwa muda mrefu, aliingia kibanda cha wazee na kushirikiana chakula chao cha jioni. Alilala usiku ule tu, na asubuhi akarejea nyumbani, akimwacha Mwita katika hali ya ugenini.
Msichana mmoja mwenye umri wa miaka kama tisa, aliyekuwa amevaa kiunoni majani yaliyosukwa, mara ile alichukua daraka ya kumlea. Alimkorogea uji na kumlisha, lakini punde kidogo alimkumbuka mama yake na alianza kumlilia. Bibi yao alishughulika na kupiga mtama. Alikaa huku ameinyosha miguu, na mtama ulijirundika katika ngozi iliyokuwa katikati ya miguu yake. Ufito wa kupigia mtama ulitoa mlio hafifu. Pengine alimfukuza kuku, na wakati fulani aliwatazama watoto. Mwishowe aliwaita, akainyosha mikono yake kumchukua Mwita, akambembeleza kidogo na kumkumbatia. Alipoburudika, alipendezwa na bangili zake za shaba hata akalala.
Babu yake aliyekuwa akisinzia kivulini, akaja kumchukua mtoto aliyelala, na kamlaza taratibu karibu yake. Baada ya kumfunika ngozi, naye akajifunika blanketi lake, wakalala kwa utamu wa sauti za wadudu wakiimba na mvumo wa mtama ukipetwa. Kwahiyo wakati ulipitishwa kwa kulala, kula na michezo kidogo.
Ilikuwa ni wakati wa masika; mimea ilisitawi sana, na mtama ukachanua na kukomaa.
Baada ya mavuno, Robi akamzalia Chacha mtoto wa kike. Alfajiri ile baada ya mtoto kuzaliwa, mzee mzalishaji alitoka na kapu la unga na kijiko cha uji. Akasimama juu ya kisuguu nje ya kibanda, akaumwaga hewani, huku akiita kwa sauti kali mara nne. Jirani waliposikia, waliambizana' 'Robi mke wa Chacha amezaa Shoka na Kuni,' maana yake mtoto wa kike. Kama angeliita mara tano, wangejua kwamba ni mtoto wa kiume, na wangesema, 'Amezaa Ngao na Mkuki'. Robi alikaa ndani siku nne, kama ilivyo kawaida baada ya kuzaa mtoto wa kike. Kisha alimnyoa na kumwita Boke, kwani kila mtoto wa kwanza wa kike huitwa Boke, Robi, au Gati.
Mara baada ya haya, mtoto akaugua. Robi akamtafutia hirizi na madawa. Alishuku kuwa babu zake walikasirika. Ili kutaka kujua mzimu uliokasirika, alipiga bao. Aliyataja majina kadhaa ya mizimu ya ukoo wao, huku akisimamisha bangili yake juu ya jiwe dogo la mviringo ambalo lilitumika kwa kusagia mtama. Alipolitaja jina la Mirimo, bangili ilisimama sawa sawa juu ya jiwe, na toka pale Mirimo likawa jina la pili la mtoto. Kwa mastaajabu makubwa, homa ilimtoka, na alipoacha kunyonya, Mwita alirudishwa nyumbani kwa baba yake.
Alipokuwa na umri wa miaka mitatu, alivaa kipande cheupe cha ngozi ya mbuzi, na alikwenda kuchunga na ndugu zake. Hivi miaka ilipita, na Mwita alipata makamo na akawa mwenye nguvu.
Aliangushana mieleka na watoto wakubwa na kuwinda nao sungura kwa makundi ya mbwa wao. Wakati mwingine alitumwa kwenda kwa babu zake na huko alikaa muda kidogo kabla ya kurudi. Alipokwisha kuwa mtu mzima, alizikumbuka zaidi safari zake kuliko mambo mengine yote ya utotoni mwake.
Itaendelea. . . .
HADITHI YA WAKURYA WA TANGANYIKA
WAKATI ule mvua ilikwishaanza; lakini majani yalikuwa yangali makavu, ingawa sehemu zingine zilikuwa na majani mabichi. Vivuli vya mawingu vilitanda juu ya miinuko ya nchi, na ukiangalia kwa mbali, utaona milima kama imefunikwa na moshi, kwa ajili watu hawajamaliza kuchoma mabua.
Makao ya watu yalionekana kando ya vilima, na mbugani, chini ya mteremuko mkubwa unaoingia katika nchi. Makao yao yalikuwa ni jumla ya vibanda na ghala za vyakula ambazo zilizunguuka zizi la ng'ombe; na vyote vilizungukwa na 'milangali'. Katika nchi hii, palikuwa msichana mmoja aitwaye Robi, ambaye aliolewa na Chacha. Huyu Chacha alikuwa mzee, na aliyekwisha oa wake wawili. Mzee Chacha aliweza kumwoa Robi kwa sababu alikuwa tajiri kuliko vijana. Ingawa Robi alikuwa ni mke wa tatu, alistarehe, na aliridhika kumzalia mtoto wa kiume wa kwanza.
Vibanda vyote vilifanana, na viliunganishwa na ua wa miti minene. Kila kibanda kilikuwa na ukuta uliotenga wanyama wagonjwa na ndama mbali na watu. Katika chumba cha watu kulikuwa giza, na pembeni palikuwa kitanda kilichotandikwa ngozi; upande wa miguuni, palikuwa na mafiga.
Mwezi ulipokuwa kamili, wazee walimshauri mganga wa mvua. Alifanya matambiko mengi ya siri, lakini alishindwa.
Akasema, 'Baba zetu wamekasirika, wamezuia mvua.' Walimpa kondoo na mbuzi wawili. Ikaja mvua ya manyunyu, lakini binadamu na wanyama walisubiri kupata mvua ya kutosha ili iondoe dhiki ile. Mwishowe, yakaja mawingu mengi yaliyokusanyika pamoja, yakipita angani. Kulikuwa mvumo wa upepo na mungurumo wa radi.
Sauti za kengele za ngombe zilizidi kwa uziri wakati wipwa wa Chama wakiwarudisha ngombe kwa haraka nyumbani kutoka machungani. Kundi la ng'ombe lilipoingizwa zizini, watoto walifunga mlango kwa magogo mazito. Magogo haya yalifungwa pamoja na mti mrefu ambao ulipita katikati ya jengo la banda upande wa kulia, na kufuata kitanda ili uwape ishara, kama kuna mtu ye yote anayejaribu kufungua mlango usiku. Mvua ilinyesha sana mpaka asubuhi, lakini upepo ulitulia mapema. Robi siku ile alichelewa kuamka, na alipooza sana. Moto ulififia kidogo, na mtoto Mwita alikuwa akilia. Alikuwa mtoto wake wa kwanza kama jina lake lilivyoonyesha; kwa sababu mtoto ye yote wa kiume wa kwanza kuzaliwa huko Kuria, lazima aitwe Chacha, Mwita, au Marwa.
Kwa desturi yao, humwacha mtoto wa kwanza akae na bibi yake, anapotazamiwa wa pili; kwa hiyo, ilimlazimu Mwita amwache mama yake. Basi, kwa masikitiko mengi, Robi alimlisha akamlaza. Kisha aliongeza kuni motoni, na ulipowaka, akakaa kuotea. Hapakuwa mwanga mwingine zaidi ya ule wa moto kibandani, ila ule uliopenya katika nyufa za mlango wa fito kutoka nje. Mionzi mikali ya mwanga iliang'aza ndani ya heleni za shaba ambazo Robi alivaa kujijulisha kuwa ni mwanamke aliyeolewa. Heleni hizi zilipembea katika ndewe kubwa za masikio yake. Bangili zake nzito ziling'aa sana. Alikuwa amezivaa bangili hizi kwa miaka mingi hata zikakata katika mikono yake na kuvimbisha pande zote mbili. Robi alipotoka nje, jamaa zake walikwisha kuamka mapema, wakishughulika na kazi. Ng'ombe walikwisha kukamuliwa na mbegu zilikuwa zimetolewa ghalani. Miti na majani yenye umande yalimeta-meta kwa mwanga wa jua, na Robi alichangamka.
Babu zake Mwita waliishi umbali wa mwendo wa siku nzima, upande wa magharibi. Chacha alimwambia Robi kuwa baada ya kumaliza kupanda, aende huko. Basi, siku moja alfajiri, baada ya kumaliza kupanda, aliiteremsha ngozi yake ya arusi. Ilitundikwa kwa ukanda mkuukuu kwenye pao la nyumba, na ilivaliwa wakati wa sherehe ya kumpeleka mtoto kwa babu zake au wakati wa arusi ya wanawe.
Alimbeba Mwita pamoja na hirizi na dawa zake, ambazo zilikuwa vijiti vidogo, vifuko vidogo vya kamba vilivyofungwa pamoja, shanga za rangi, senti, na kibuyu kidogo kilichopambwa ambacho alipewa na mpenzi wake kabla ya harusi yake.
Alipokuwa akitembea njiani, hali ya nchi ikawa inabadilika kidogo kidogo. Njia yake ilipitia kwenye miinuko na miteremko hata akafikia uwanda wa juu; na ilipofika jioni akateremka kwenye nchi yenye miti mingi. Aliona vilima vidogo vidogo vyenye majabali yaliyochongoka. Pengine alipita mahame ya watu. Hapa ilibaki milangali iliyosongwa na majani na mimea mingine, ambayo ilikuwa makao ya wanyama wadogo wa porini na pengine mizimu ya watu waliokaa hapo. Wakati huu wote jua lilikuwa likichwa na mbingu ilibadilika rangi.
Robi alipofika nyumbani kwa wazazi na ndugu zake, kulikuwa kumetulia. Vibanda vilifungwa na ng'ombe walikuwa zizini. Alibisha hodi, na mara alisikia mlio wa mlango ukivutwa toka kwa ndani ya kibanda. Wasichana wawili walichungulia nje huku wakitafuna makande. Walikuwa wakingojea chakula cha jioni, lakini waliposikia kuwa ni Robi aliyebisha hodi, walitoka nje wote na kumkaribisha kwa furaha. Baada ya kupeana mikono na kuongea kwa muda mrefu, aliingia kibanda cha wazee na kushirikiana chakula chao cha jioni. Alilala usiku ule tu, na asubuhi akarejea nyumbani, akimwacha Mwita katika hali ya ugenini.
Msichana mmoja mwenye umri wa miaka kama tisa, aliyekuwa amevaa kiunoni majani yaliyosukwa, mara ile alichukua daraka ya kumlea. Alimkorogea uji na kumlisha, lakini punde kidogo alimkumbuka mama yake na alianza kumlilia. Bibi yao alishughulika na kupiga mtama. Alikaa huku ameinyosha miguu, na mtama ulijirundika katika ngozi iliyokuwa katikati ya miguu yake. Ufito wa kupigia mtama ulitoa mlio hafifu. Pengine alimfukuza kuku, na wakati fulani aliwatazama watoto. Mwishowe aliwaita, akainyosha mikono yake kumchukua Mwita, akambembeleza kidogo na kumkumbatia. Alipoburudika, alipendezwa na bangili zake za shaba hata akalala.
Babu yake aliyekuwa akisinzia kivulini, akaja kumchukua mtoto aliyelala, na kamlaza taratibu karibu yake. Baada ya kumfunika ngozi, naye akajifunika blanketi lake, wakalala kwa utamu wa sauti za wadudu wakiimba na mvumo wa mtama ukipetwa. Kwahiyo wakati ulipitishwa kwa kulala, kula na michezo kidogo.
Ilikuwa ni wakati wa masika; mimea ilisitawi sana, na mtama ukachanua na kukomaa.
Baada ya mavuno, Robi akamzalia Chacha mtoto wa kike. Alfajiri ile baada ya mtoto kuzaliwa, mzee mzalishaji alitoka na kapu la unga na kijiko cha uji. Akasimama juu ya kisuguu nje ya kibanda, akaumwaga hewani, huku akiita kwa sauti kali mara nne. Jirani waliposikia, waliambizana' 'Robi mke wa Chacha amezaa Shoka na Kuni,' maana yake mtoto wa kike. Kama angeliita mara tano, wangejua kwamba ni mtoto wa kiume, na wangesema, 'Amezaa Ngao na Mkuki'. Robi alikaa ndani siku nne, kama ilivyo kawaida baada ya kuzaa mtoto wa kike. Kisha alimnyoa na kumwita Boke, kwani kila mtoto wa kwanza wa kike huitwa Boke, Robi, au Gati.
Mara baada ya haya, mtoto akaugua. Robi akamtafutia hirizi na madawa. Alishuku kuwa babu zake walikasirika. Ili kutaka kujua mzimu uliokasirika, alipiga bao. Aliyataja majina kadhaa ya mizimu ya ukoo wao, huku akisimamisha bangili yake juu ya jiwe dogo la mviringo ambalo lilitumika kwa kusagia mtama. Alipolitaja jina la Mirimo, bangili ilisimama sawa sawa juu ya jiwe, na toka pale Mirimo likawa jina la pili la mtoto. Kwa mastaajabu makubwa, homa ilimtoka, na alipoacha kunyonya, Mwita alirudishwa nyumbani kwa baba yake.
Alipokuwa na umri wa miaka mitatu, alivaa kipande cheupe cha ngozi ya mbuzi, na alikwenda kuchunga na ndugu zake. Hivi miaka ilipita, na Mwita alipata makamo na akawa mwenye nguvu.
Aliangushana mieleka na watoto wakubwa na kuwinda nao sungura kwa makundi ya mbwa wao. Wakati mwingine alitumwa kwenda kwa babu zake na huko alikaa muda kidogo kabla ya kurudi. Alipokwisha kuwa mtu mzima, alizikumbuka zaidi safari zake kuliko mambo mengine yote ya utotoni mwake.
Itaendelea. . . .