HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,445
- 6,207
- Thread starter
- #281
BRUNO THE FISHERMAN
Episode 14
CIA watatu, Andrew Putt, Gilbert Michaebl na Richard Bull wakaianza kazi yao nchini Kenya kuhakikisha Sharifa anapatikana haraka iwezekanavyo.
Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kwenda Mombasa katika kijiji cha Goulduvai alipokuwa akiishi Sharifa kwa muda huku akiwahudumia wanakijiji kwa afya zao.
Walipofika huko, kila kona watu walikuwa wakilizungumzia tukio hilo. Hakukuwa na mtu aliyekuwa na furaha, kila mmoja alihuzunika kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea hawakukitegemea hata kidogo.
Hapo, wakazungumza na Bruno na kumuuliza maswali kadhaa. Aliwasimulia kila kitu alichokuwa akikifahamu kuhusu Wazungu wale na mwisho kabisa akawaambia kwamba lengo la watu hao ni kwamba hakutakiwa kwenda nchini Marekani kutoa ushahidi kwa yaliyokuwa yametokea kwa mzee Todd.
“Someone is behind this,” (kuna mtu yupo nyuma ya hili) alisema Bull huku akiwaangalia wenzake.
Wakahitaji simu ambayo Bruno aliwasiliana na Tim, walipopewa, wakachukua namba, wakasogea pembeni hidogo huku Putt akichukua tablet yake na kufungua sehemu ya ramani na kuanza kuangalia.
Bruno alitulia pembeni, alibaki akiwaangalia Wazungu hao walioonekana kuwa hatari katika kumtafuta mtu yeyote waliyekuwa wakimtaka. Walikaa huko kwa zaidi ya nusu saa huku wakizungumza na wakati mwingine wakiangalia tablet ile kwa lengo la kujua zaidi kuhusu watu hao walikuwa mahali gani.
“Hivi kweli wanaweza kwenda Nairobi?” aliuliza Putt huku.
“Sidhani! Haiwezekani mtu afanye tukio kama hili halafu akaelekea Nairobi,” alisema Bull huku akiwaonyeshea wenzake ramani katika table.
“Kwa maelezo ya mumewe alisema kwamba alipigiwa simu, lakini haikuwa ya kawaida, ilipigwa kwa mtandao wa WhatsApp, mnajua kwa nini mpigaji alifanya hivyo?” aliuliza Gilbert.
“Hapana!”
Gilbert alikuwa miongoni mwa maofisa wa CIA waliokuwa na utaalamu mkubwa wa kumtafuta mtuhumiwa yeyote yule. Alikuwa mtaalamu wa hisia ambaye kama kulikuwa na tukio limetokea ndani ya nyuma na mtuhumiwa kutoweka, aliweza kusimama na kukwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea ndani ya nyumba hiyo.
Alikuwa mtaalamu na makao makuu walimpeleka nchini Kenya kwa lengo la kuhakikisha kwamba Kundi la Al Shabaab linateketezwa haraka sana kwa kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Kwa akili yake, akagundua kwamba watu hao hawakuwa nchini Kenya, walikuwa wameondoka na kuelekea katika nchi nyingine na ndiyo maana waliamua kupiga simu kwa kutumia Mtandao wa WhatsApp.
“Kivipi?” aliuliza Bull.
“Ni kwa sababu hawakutaka kupatikana katika minara ya simu za mkononi. Kama wangetumia simu ya kawaida, tungejua wapo wapi, ila kwa WhatsApp, bila shaka watu hawa wameamua kuficha mawasiliano ili tusijue wapo wapi,” alisema Gilbert huku akionekana kumaanisha alichokuwa akikizungumza.
Alichokisema ndio ulikuwa ukweli wenyewe kwamba watu hao waliondoka na kuelekea nje ya Kenya. Hakukuwa na maswali mengi kwamba ni nchi gani walikuwa wameelekea, moja kwa moja wakagundua kwamba ilikuwa ni Tanzania na hivyo ilikuwa ni lazima waende huko.
“Kwa nini isiwe Somalia?”
“Ni kwa sababu kuna mapigano huko. Kwa akili ya kawaida tu, ungeweza kukimbilia Somalia?” aliuliza Gilbert.
“Haiwezekani!”
“Kama haiwezekani, basi watu hao watakuwa wamekimbilia Tanzania,” alisema.
Hawakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka na kuelekea nchini humo. Hawakuaga bali walimwambia Bruno kwamba watakaporudi watarudi wakiongozana na mpenzi wake hivyo alitakiwa kuwasubiri hapohapo Mombasa.
Njiani, walikuwa wakizungumza mambo mengi, kwao, kazi ile haikuonekana kuwa ngumu tena, waliamini kwamba kwa namna moja ama nyingine wangefanikiwa kwa kuwa tu walijiona kuwa na uwezo mkubwa kuliko hata hao watu waliokuwa wamemteka Sharifa.
Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika mpaka wa Horohoro kwa upande wa Kenya. Wakateremka na moja kwa moja kuelekea katika ofisi ya kiongozi wa maaskari hapo mpakani, mzee Hamidu na kumuuliza kuhusu watu hao waliokuwa wamepitia mahali hapo kuingia Tanzania.
“Hakuna watu waliopita,” alisema mzee Hamidu huku akimwangalia Bruno.
“Si kweli!”
“Huo ndiyo ukweli, au kama mmekuja na ukweli wenu mwingine,” alisema mzee Hamidu huku akisimama kwenye kiti, yote hayo ilikuwa ni kutaka kuwaonyeshea watu hao kwamba alikuwa mwanaume imara na kile alichokuwa akikisema ndicho kilikuwa sahihi.
“Hapana! Bado tunajua kwamba walipita hapa, ila walipitaje? Inawezekana wewe hufahamu lakini kuna mtu hapa atakuwa anafahamu,” alisema Gilbert.
“Kwa hiyo kuna mtu alichukua rushwa?”
“Huwezi kujua!”
“Hizo ni dharau,” alisema mzee huyo.
Gilbert hakutaka kubaki ndani ya ofisi hiyo, kwa jinsi mzee Hamidu alivyokuwa akiongea, alihisi moyo wake ukipatwa na hasira kali, na ili kuepusha matatizo, akaamua kutoka ndani ya ofisi ile.
Pale nje akasimama na kuanza kuangalia huku na kule, aliwaangalia jinsi ambavyo askari walivyokuwa wakipekua magari, alikuwa na uhakika kwamba watu hao walipita mahali hapo kwani hata upekuzi ambao ulikuwa ukifanyika, ulifanyika kizembe sana.
“Tuingieni nchini Tanzania, bado moyo wangu una uhakika kwamba watu hawa walipita mahali hapa,” alisema Gilbert, wakaingia ndani ya gari lao na kuingia nchini Tanzania, hapo wakaanza kuitafuta Tanga Mjini.
***
Kila kona katika Tanga Mjini kulikuwa na stori moja tu iliyokuwa ikianza kuzagaa kila kona. Wazungu watatu ambao walichukua chumba kimoja katika nyumba ya wageni iliwashangaza kila mtu aliyekuwa ameisikia.
Watu walijua kwamba Wazungu walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na pesa, watu ambao mara baada ya kufika barani Afrika basi wangekuwa wakiishi katika hoteli nzuri lakini Wazungu waliokuwa wameingia Tanga kwa siku hizo walionekana kuwa tofauti na wenzao kabisa.
Hali hiyo ikaanza kuwatia wasiwasi watu wa hapo Tanga kiasi kwamba wengi wakahisi kwamba kulikuwa na kitu cha siri kilichokuwa kikiendelea ambacho kingeweza kuwa hasara au hata kupoteza maisha kwa wakazi wa hapo.
Walichokifanya siku iliyofuata ni kuwasiliana na polisi. Waliwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea kwamba inawezekana kabisa Wazungu wale hawakuwa watu wazuri na ndiyo maana hawakutaka kupanga katika hoteli kubwa kwa kuogopa kukamatwa.
Polisi walipoambiwa, hawakutaka kusubiri, wakaondoka na kuelekea huko kwa lengo la kuwaona Wazungu hao. Walipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuzungumza na mmiliki wa gesti hiyo na kumuuliza maswali mengi.
Hakuwaficha, aliwaambia kila kitu kuhusu Wazungu hao na hivyo kuhitaji kuzungumza nao. Hilo halikuwa tatizo, alichokifanya ni kuwaita, wanaume hao, wakatoka chumbani, wakafunga mlango kwa ufunguo ili Sharifa asitoke, wakawafuata polisi na kuanza kuzungumza nao.
Waliwaambia kwamba walifika hapo Tanga kwa lengo la kuingia katika mapango ya Amboni lakini kabla ya kwenda huko walijikuta wakiibiwa kiasi cha pesa walichokuwanacho cha dola elfu themanini, laptop na saa zao za mikononi na vijana wa mitaani ambao waliwafuata na kuwatolea visu.
“Poleni sana! Kwa nini hamkutoa taarifa polisi?” aliuliza polisi mmoja, kwa jinsi Tim alivyokuwa akielezea, ilikuwa ni vigumu kuamini kwamba alikuwa akidanganya.
“Tulichanganyikiwa! Hatupo sawa, hata nauli ya ndege kurudi nyumbani hatujui tutaipataje, hapa mnapotuoni, tupo hivihivi pamoja na msichana wa nchini Ghana ambaye tumekuja naye, hatuna kitu,” alisema Tim.
Polisi wakaangaliana, kile alichokuwa amekisema kilionekana kuwagusa kupita kawaida hivyo kuwaambia kwamba wanaondoka na kurudi baadaye huku wakiwa tayari wamejua ni kitu gani walitakiwa kufanya kuwasaidia Wazungu hao.
Walipoona polisi wameondoka, hawakutaka kuendelea kukaa kwenye gesti hiyo, ilikuwa ni lazima waondoke kwani walihisi kwamba mara baada ya kuondoka, wangekwenda kupata ukweli wa wao kuwa hapo na kurudi huku wakiwa na sura nyingine.
Wakaufungua mlango na ufunguo, wakaingia ndani, kilichowashtua ni kwamba Sharifa hakuwemo chumbani humo. Hilo liliwatia hofu kwani walipokwenda nje kuzungumza na polisi walimuacha humo ndani na zaidi ni kwamba waliufunga mlango kwa ufunguo, sasa kama ameondoka, atakuwa amepitia wapi?
“Kwenye dari! Tuangalieni kwenye dari,” alisema Adson na kwa kuwa pale kulipokuwa na mlango wa dari kulikuwa na meza, wakajua kabisa msichana huyo alipanda juu ya meza hiyo na kuingia humo kwa lengo la kuwatoroka hotelini humo.
“Jamani! Ili tuwe salama, huyu msichana ni lazima apatikane,” alisema Kelly, wakautoa mlango wa dari na Tim kuingia huko kumtafuta Sharifa.
Je, nini kitaendelea?
Sharifa atapatikana?
Episode 14
CIA watatu, Andrew Putt, Gilbert Michaebl na Richard Bull wakaianza kazi yao nchini Kenya kuhakikisha Sharifa anapatikana haraka iwezekanavyo.
Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kwenda Mombasa katika kijiji cha Goulduvai alipokuwa akiishi Sharifa kwa muda huku akiwahudumia wanakijiji kwa afya zao.
Walipofika huko, kila kona watu walikuwa wakilizungumzia tukio hilo. Hakukuwa na mtu aliyekuwa na furaha, kila mmoja alihuzunika kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea hawakukitegemea hata kidogo.
Hapo, wakazungumza na Bruno na kumuuliza maswali kadhaa. Aliwasimulia kila kitu alichokuwa akikifahamu kuhusu Wazungu wale na mwisho kabisa akawaambia kwamba lengo la watu hao ni kwamba hakutakiwa kwenda nchini Marekani kutoa ushahidi kwa yaliyokuwa yametokea kwa mzee Todd.
“Someone is behind this,” (kuna mtu yupo nyuma ya hili) alisema Bull huku akiwaangalia wenzake.
Wakahitaji simu ambayo Bruno aliwasiliana na Tim, walipopewa, wakachukua namba, wakasogea pembeni hidogo huku Putt akichukua tablet yake na kufungua sehemu ya ramani na kuanza kuangalia.
Bruno alitulia pembeni, alibaki akiwaangalia Wazungu hao walioonekana kuwa hatari katika kumtafuta mtu yeyote waliyekuwa wakimtaka. Walikaa huko kwa zaidi ya nusu saa huku wakizungumza na wakati mwingine wakiangalia tablet ile kwa lengo la kujua zaidi kuhusu watu hao walikuwa mahali gani.
“Hivi kweli wanaweza kwenda Nairobi?” aliuliza Putt huku.
“Sidhani! Haiwezekani mtu afanye tukio kama hili halafu akaelekea Nairobi,” alisema Bull huku akiwaonyeshea wenzake ramani katika table.
“Kwa maelezo ya mumewe alisema kwamba alipigiwa simu, lakini haikuwa ya kawaida, ilipigwa kwa mtandao wa WhatsApp, mnajua kwa nini mpigaji alifanya hivyo?” aliuliza Gilbert.
“Hapana!”
Gilbert alikuwa miongoni mwa maofisa wa CIA waliokuwa na utaalamu mkubwa wa kumtafuta mtuhumiwa yeyote yule. Alikuwa mtaalamu wa hisia ambaye kama kulikuwa na tukio limetokea ndani ya nyuma na mtuhumiwa kutoweka, aliweza kusimama na kukwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea ndani ya nyumba hiyo.
Alikuwa mtaalamu na makao makuu walimpeleka nchini Kenya kwa lengo la kuhakikisha kwamba Kundi la Al Shabaab linateketezwa haraka sana kwa kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Kwa akili yake, akagundua kwamba watu hao hawakuwa nchini Kenya, walikuwa wameondoka na kuelekea katika nchi nyingine na ndiyo maana waliamua kupiga simu kwa kutumia Mtandao wa WhatsApp.
“Kivipi?” aliuliza Bull.
“Ni kwa sababu hawakutaka kupatikana katika minara ya simu za mkononi. Kama wangetumia simu ya kawaida, tungejua wapo wapi, ila kwa WhatsApp, bila shaka watu hawa wameamua kuficha mawasiliano ili tusijue wapo wapi,” alisema Gilbert huku akionekana kumaanisha alichokuwa akikizungumza.
Alichokisema ndio ulikuwa ukweli wenyewe kwamba watu hao waliondoka na kuelekea nje ya Kenya. Hakukuwa na maswali mengi kwamba ni nchi gani walikuwa wameelekea, moja kwa moja wakagundua kwamba ilikuwa ni Tanzania na hivyo ilikuwa ni lazima waende huko.
“Kwa nini isiwe Somalia?”
“Ni kwa sababu kuna mapigano huko. Kwa akili ya kawaida tu, ungeweza kukimbilia Somalia?” aliuliza Gilbert.
“Haiwezekani!”
“Kama haiwezekani, basi watu hao watakuwa wamekimbilia Tanzania,” alisema.
Hawakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka na kuelekea nchini humo. Hawakuaga bali walimwambia Bruno kwamba watakaporudi watarudi wakiongozana na mpenzi wake hivyo alitakiwa kuwasubiri hapohapo Mombasa.
Njiani, walikuwa wakizungumza mambo mengi, kwao, kazi ile haikuonekana kuwa ngumu tena, waliamini kwamba kwa namna moja ama nyingine wangefanikiwa kwa kuwa tu walijiona kuwa na uwezo mkubwa kuliko hata hao watu waliokuwa wamemteka Sharifa.
Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika mpaka wa Horohoro kwa upande wa Kenya. Wakateremka na moja kwa moja kuelekea katika ofisi ya kiongozi wa maaskari hapo mpakani, mzee Hamidu na kumuuliza kuhusu watu hao waliokuwa wamepitia mahali hapo kuingia Tanzania.
“Hakuna watu waliopita,” alisema mzee Hamidu huku akimwangalia Bruno.
“Si kweli!”
“Huo ndiyo ukweli, au kama mmekuja na ukweli wenu mwingine,” alisema mzee Hamidu huku akisimama kwenye kiti, yote hayo ilikuwa ni kutaka kuwaonyeshea watu hao kwamba alikuwa mwanaume imara na kile alichokuwa akikisema ndicho kilikuwa sahihi.
“Hapana! Bado tunajua kwamba walipita hapa, ila walipitaje? Inawezekana wewe hufahamu lakini kuna mtu hapa atakuwa anafahamu,” alisema Gilbert.
“Kwa hiyo kuna mtu alichukua rushwa?”
“Huwezi kujua!”
“Hizo ni dharau,” alisema mzee huyo.
Gilbert hakutaka kubaki ndani ya ofisi hiyo, kwa jinsi mzee Hamidu alivyokuwa akiongea, alihisi moyo wake ukipatwa na hasira kali, na ili kuepusha matatizo, akaamua kutoka ndani ya ofisi ile.
Pale nje akasimama na kuanza kuangalia huku na kule, aliwaangalia jinsi ambavyo askari walivyokuwa wakipekua magari, alikuwa na uhakika kwamba watu hao walipita mahali hapo kwani hata upekuzi ambao ulikuwa ukifanyika, ulifanyika kizembe sana.
“Tuingieni nchini Tanzania, bado moyo wangu una uhakika kwamba watu hawa walipita mahali hapa,” alisema Gilbert, wakaingia ndani ya gari lao na kuingia nchini Tanzania, hapo wakaanza kuitafuta Tanga Mjini.
***
Kila kona katika Tanga Mjini kulikuwa na stori moja tu iliyokuwa ikianza kuzagaa kila kona. Wazungu watatu ambao walichukua chumba kimoja katika nyumba ya wageni iliwashangaza kila mtu aliyekuwa ameisikia.
Watu walijua kwamba Wazungu walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na pesa, watu ambao mara baada ya kufika barani Afrika basi wangekuwa wakiishi katika hoteli nzuri lakini Wazungu waliokuwa wameingia Tanga kwa siku hizo walionekana kuwa tofauti na wenzao kabisa.
Hali hiyo ikaanza kuwatia wasiwasi watu wa hapo Tanga kiasi kwamba wengi wakahisi kwamba kulikuwa na kitu cha siri kilichokuwa kikiendelea ambacho kingeweza kuwa hasara au hata kupoteza maisha kwa wakazi wa hapo.
Walichokifanya siku iliyofuata ni kuwasiliana na polisi. Waliwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea kwamba inawezekana kabisa Wazungu wale hawakuwa watu wazuri na ndiyo maana hawakutaka kupanga katika hoteli kubwa kwa kuogopa kukamatwa.
Polisi walipoambiwa, hawakutaka kusubiri, wakaondoka na kuelekea huko kwa lengo la kuwaona Wazungu hao. Walipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuzungumza na mmiliki wa gesti hiyo na kumuuliza maswali mengi.
Hakuwaficha, aliwaambia kila kitu kuhusu Wazungu hao na hivyo kuhitaji kuzungumza nao. Hilo halikuwa tatizo, alichokifanya ni kuwaita, wanaume hao, wakatoka chumbani, wakafunga mlango kwa ufunguo ili Sharifa asitoke, wakawafuata polisi na kuanza kuzungumza nao.
Waliwaambia kwamba walifika hapo Tanga kwa lengo la kuingia katika mapango ya Amboni lakini kabla ya kwenda huko walijikuta wakiibiwa kiasi cha pesa walichokuwanacho cha dola elfu themanini, laptop na saa zao za mikononi na vijana wa mitaani ambao waliwafuata na kuwatolea visu.
“Poleni sana! Kwa nini hamkutoa taarifa polisi?” aliuliza polisi mmoja, kwa jinsi Tim alivyokuwa akielezea, ilikuwa ni vigumu kuamini kwamba alikuwa akidanganya.
“Tulichanganyikiwa! Hatupo sawa, hata nauli ya ndege kurudi nyumbani hatujui tutaipataje, hapa mnapotuoni, tupo hivihivi pamoja na msichana wa nchini Ghana ambaye tumekuja naye, hatuna kitu,” alisema Tim.
Polisi wakaangaliana, kile alichokuwa amekisema kilionekana kuwagusa kupita kawaida hivyo kuwaambia kwamba wanaondoka na kurudi baadaye huku wakiwa tayari wamejua ni kitu gani walitakiwa kufanya kuwasaidia Wazungu hao.
Walipoona polisi wameondoka, hawakutaka kuendelea kukaa kwenye gesti hiyo, ilikuwa ni lazima waondoke kwani walihisi kwamba mara baada ya kuondoka, wangekwenda kupata ukweli wa wao kuwa hapo na kurudi huku wakiwa na sura nyingine.
Wakaufungua mlango na ufunguo, wakaingia ndani, kilichowashtua ni kwamba Sharifa hakuwemo chumbani humo. Hilo liliwatia hofu kwani walipokwenda nje kuzungumza na polisi walimuacha humo ndani na zaidi ni kwamba waliufunga mlango kwa ufunguo, sasa kama ameondoka, atakuwa amepitia wapi?
“Kwenye dari! Tuangalieni kwenye dari,” alisema Adson na kwa kuwa pale kulipokuwa na mlango wa dari kulikuwa na meza, wakajua kabisa msichana huyo alipanda juu ya meza hiyo na kuingia humo kwa lengo la kuwatoroka hotelini humo.
“Jamani! Ili tuwe salama, huyu msichana ni lazima apatikane,” alisema Kelly, wakautoa mlango wa dari na Tim kuingia huko kumtafuta Sharifa.
Je, nini kitaendelea?
Sharifa atapatikana?