Hadithi: Bruno the Fisherman

Hadithi: Bruno the Fisherman

BRUNO THE FISHERMAN

Episode 14


CIA watatu, Andrew Putt, Gilbert Michaebl na Richard Bull wakaianza kazi yao nchini Kenya kuhakikisha Sharifa anapatikana haraka iwezekanavyo.
Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kwenda Mombasa katika kijiji cha Goulduvai alipokuwa akiishi Sharifa kwa muda huku akiwahudumia wanakijiji kwa afya zao.
Walipofika huko, kila kona watu walikuwa wakilizungumzia tukio hilo. Hakukuwa na mtu aliyekuwa na furaha, kila mmoja alihuzunika kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea hawakukitegemea hata kidogo.
Hapo, wakazungumza na Bruno na kumuuliza maswali kadhaa. Aliwasimulia kila kitu alichokuwa akikifahamu kuhusu Wazungu wale na mwisho kabisa akawaambia kwamba lengo la watu hao ni kwamba hakutakiwa kwenda nchini Marekani kutoa ushahidi kwa yaliyokuwa yametokea kwa mzee Todd.
“Someone is behind this,” (kuna mtu yupo nyuma ya hili) alisema Bull huku akiwaangalia wenzake.
Wakahitaji simu ambayo Bruno aliwasiliana na Tim, walipopewa, wakachukua namba, wakasogea pembeni hidogo huku Putt akichukua tablet yake na kufungua sehemu ya ramani na kuanza kuangalia.
Bruno alitulia pembeni, alibaki akiwaangalia Wazungu hao walioonekana kuwa hatari katika kumtafuta mtu yeyote waliyekuwa wakimtaka. Walikaa huko kwa zaidi ya nusu saa huku wakizungumza na wakati mwingine wakiangalia tablet ile kwa lengo la kujua zaidi kuhusu watu hao walikuwa mahali gani.
“Hivi kweli wanaweza kwenda Nairobi?” aliuliza Putt huku.
“Sidhani! Haiwezekani mtu afanye tukio kama hili halafu akaelekea Nairobi,” alisema Bull huku akiwaonyeshea wenzake ramani katika table.
“Kwa maelezo ya mumewe alisema kwamba alipigiwa simu, lakini haikuwa ya kawaida, ilipigwa kwa mtandao wa WhatsApp, mnajua kwa nini mpigaji alifanya hivyo?” aliuliza Gilbert.
“Hapana!”
Gilbert alikuwa miongoni mwa maofisa wa CIA waliokuwa na utaalamu mkubwa wa kumtafuta mtuhumiwa yeyote yule. Alikuwa mtaalamu wa hisia ambaye kama kulikuwa na tukio limetokea ndani ya nyuma na mtuhumiwa kutoweka, aliweza kusimama na kukwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea ndani ya nyumba hiyo.
Alikuwa mtaalamu na makao makuu walimpeleka nchini Kenya kwa lengo la kuhakikisha kwamba Kundi la Al Shabaab linateketezwa haraka sana kwa kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Kwa akili yake, akagundua kwamba watu hao hawakuwa nchini Kenya, walikuwa wameondoka na kuelekea katika nchi nyingine na ndiyo maana waliamua kupiga simu kwa kutumia Mtandao wa WhatsApp.
“Kivipi?” aliuliza Bull.
“Ni kwa sababu hawakutaka kupatikana katika minara ya simu za mkononi. Kama wangetumia simu ya kawaida, tungejua wapo wapi, ila kwa WhatsApp, bila shaka watu hawa wameamua kuficha mawasiliano ili tusijue wapo wapi,” alisema Gilbert huku akionekana kumaanisha alichokuwa akikizungumza.
Alichokisema ndio ulikuwa ukweli wenyewe kwamba watu hao waliondoka na kuelekea nje ya Kenya. Hakukuwa na maswali mengi kwamba ni nchi gani walikuwa wameelekea, moja kwa moja wakagundua kwamba ilikuwa ni Tanzania na hivyo ilikuwa ni lazima waende huko.
“Kwa nini isiwe Somalia?”
“Ni kwa sababu kuna mapigano huko. Kwa akili ya kawaida tu, ungeweza kukimbilia Somalia?” aliuliza Gilbert.
“Haiwezekani!”
“Kama haiwezekani, basi watu hao watakuwa wamekimbilia Tanzania,” alisema.
Hawakutaka kupoteza muda, ilikuwa ni lazima kuondoka na kuelekea nchini humo. Hawakuaga bali walimwambia Bruno kwamba watakaporudi watarudi wakiongozana na mpenzi wake hivyo alitakiwa kuwasubiri hapohapo Mombasa.
Njiani, walikuwa wakizungumza mambo mengi, kwao, kazi ile haikuonekana kuwa ngumu tena, waliamini kwamba kwa namna moja ama nyingine wangefanikiwa kwa kuwa tu walijiona kuwa na uwezo mkubwa kuliko hata hao watu waliokuwa wamemteka Sharifa.
Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika mpaka wa Horohoro kwa upande wa Kenya. Wakateremka na moja kwa moja kuelekea katika ofisi ya kiongozi wa maaskari hapo mpakani, mzee Hamidu na kumuuliza kuhusu watu hao waliokuwa wamepitia mahali hapo kuingia Tanzania.
“Hakuna watu waliopita,” alisema mzee Hamidu huku akimwangalia Bruno.
“Si kweli!”
“Huo ndiyo ukweli, au kama mmekuja na ukweli wenu mwingine,” alisema mzee Hamidu huku akisimama kwenye kiti, yote hayo ilikuwa ni kutaka kuwaonyeshea watu hao kwamba alikuwa mwanaume imara na kile alichokuwa akikisema ndicho kilikuwa sahihi.
“Hapana! Bado tunajua kwamba walipita hapa, ila walipitaje? Inawezekana wewe hufahamu lakini kuna mtu hapa atakuwa anafahamu,” alisema Gilbert.
“Kwa hiyo kuna mtu alichukua rushwa?”
“Huwezi kujua!”
“Hizo ni dharau,” alisema mzee huyo.
Gilbert hakutaka kubaki ndani ya ofisi hiyo, kwa jinsi mzee Hamidu alivyokuwa akiongea, alihisi moyo wake ukipatwa na hasira kali, na ili kuepusha matatizo, akaamua kutoka ndani ya ofisi ile.
Pale nje akasimama na kuanza kuangalia huku na kule, aliwaangalia jinsi ambavyo askari walivyokuwa wakipekua magari, alikuwa na uhakika kwamba watu hao walipita mahali hapo kwani hata upekuzi ambao ulikuwa ukifanyika, ulifanyika kizembe sana.
“Tuingieni nchini Tanzania, bado moyo wangu una uhakika kwamba watu hawa walipita mahali hapa,” alisema Gilbert, wakaingia ndani ya gari lao na kuingia nchini Tanzania, hapo wakaanza kuitafuta Tanga Mjini.
***
Kila kona katika Tanga Mjini kulikuwa na stori moja tu iliyokuwa ikianza kuzagaa kila kona. Wazungu watatu ambao walichukua chumba kimoja katika nyumba ya wageni iliwashangaza kila mtu aliyekuwa ameisikia.
Watu walijua kwamba Wazungu walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na pesa, watu ambao mara baada ya kufika barani Afrika basi wangekuwa wakiishi katika hoteli nzuri lakini Wazungu waliokuwa wameingia Tanga kwa siku hizo walionekana kuwa tofauti na wenzao kabisa.
Hali hiyo ikaanza kuwatia wasiwasi watu wa hapo Tanga kiasi kwamba wengi wakahisi kwamba kulikuwa na kitu cha siri kilichokuwa kikiendelea ambacho kingeweza kuwa hasara au hata kupoteza maisha kwa wakazi wa hapo.
Walichokifanya siku iliyofuata ni kuwasiliana na polisi. Waliwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea kwamba inawezekana kabisa Wazungu wale hawakuwa watu wazuri na ndiyo maana hawakutaka kupanga katika hoteli kubwa kwa kuogopa kukamatwa.
Polisi walipoambiwa, hawakutaka kusubiri, wakaondoka na kuelekea huko kwa lengo la kuwaona Wazungu hao. Walipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuzungumza na mmiliki wa gesti hiyo na kumuuliza maswali mengi.
Hakuwaficha, aliwaambia kila kitu kuhusu Wazungu hao na hivyo kuhitaji kuzungumza nao. Hilo halikuwa tatizo, alichokifanya ni kuwaita, wanaume hao, wakatoka chumbani, wakafunga mlango kwa ufunguo ili Sharifa asitoke, wakawafuata polisi na kuanza kuzungumza nao.
Waliwaambia kwamba walifika hapo Tanga kwa lengo la kuingia katika mapango ya Amboni lakini kabla ya kwenda huko walijikuta wakiibiwa kiasi cha pesa walichokuwanacho cha dola elfu themanini, laptop na saa zao za mikononi na vijana wa mitaani ambao waliwafuata na kuwatolea visu.
“Poleni sana! Kwa nini hamkutoa taarifa polisi?” aliuliza polisi mmoja, kwa jinsi Tim alivyokuwa akielezea, ilikuwa ni vigumu kuamini kwamba alikuwa akidanganya.
“Tulichanganyikiwa! Hatupo sawa, hata nauli ya ndege kurudi nyumbani hatujui tutaipataje, hapa mnapotuoni, tupo hivihivi pamoja na msichana wa nchini Ghana ambaye tumekuja naye, hatuna kitu,” alisema Tim.
Polisi wakaangaliana, kile alichokuwa amekisema kilionekana kuwagusa kupita kawaida hivyo kuwaambia kwamba wanaondoka na kurudi baadaye huku wakiwa tayari wamejua ni kitu gani walitakiwa kufanya kuwasaidia Wazungu hao.
Walipoona polisi wameondoka, hawakutaka kuendelea kukaa kwenye gesti hiyo, ilikuwa ni lazima waondoke kwani walihisi kwamba mara baada ya kuondoka, wangekwenda kupata ukweli wa wao kuwa hapo na kurudi huku wakiwa na sura nyingine.
Wakaufungua mlango na ufunguo, wakaingia ndani, kilichowashtua ni kwamba Sharifa hakuwemo chumbani humo. Hilo liliwatia hofu kwani walipokwenda nje kuzungumza na polisi walimuacha humo ndani na zaidi ni kwamba waliufunga mlango kwa ufunguo, sasa kama ameondoka, atakuwa amepitia wapi?
“Kwenye dari! Tuangalieni kwenye dari,” alisema Adson na kwa kuwa pale kulipokuwa na mlango wa dari kulikuwa na meza, wakajua kabisa msichana huyo alipanda juu ya meza hiyo na kuingia humo kwa lengo la kuwatoroka hotelini humo.
“Jamani! Ili tuwe salama, huyu msichana ni lazima apatikane,” alisema Kelly, wakautoa mlango wa dari na Tim kuingia huko kumtafuta Sharifa.

Je, nini kitaendelea?
Sharifa atapatikana?
 
Mbona Shunie analeta story mpaka zinaisha.Hawa kina Kulubime na the Banker vipi?
 
BRUNO THE FISHERMAN

Sharifa alikuwa ndani ya chumba kile huku akiwa n a wasiwasi tele, hakujua ni kitu gani kingeendelea kama tu watu hao wangeendelea kumshikilia kama ilivyokuwa.
Hakutaka kuona akiwa mikononi mwa watu hao, alitamani kuona akiondoka na kurudi kwa mpenzi wake. Kama kulia, alilia sana lakini muda huo haukuwa wa kulia tena, ilikuwa ni lazima kufanya kila liwezekanalo kuondoka ndani ya chumba hicho.
Alikuwa humo, Tim na wenzake walikwenda nje walipokuwa wakihitajika na polisi, yeye mule ndani ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anatoka ndani ya chumba hicho.
Akaufuata mlango, akakishika kitasa na taratibu kuanza kukitekenya kwa lengo la kukifungua. Mlango haukufunguka kuonyesha kwamba ulifungwa kwa nje.
Haraka sana akaacha. Akaangalia huku na kule, akafanikiwa kuuona mlango wa dari ukiwa umefungwa. Kichwa chake kikamwambia kwamba hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ya kuweza kuondoka ndani ya chumba hicho.
Akachukua meza, akaiweka chini ya mlango wa dari na kupanda, akaanza kuufungua mlango huo kwa kuusukuma, ukafanikiwa kufunguka.
Kazi kubwa ilikuwa ni kupanda juu ya dari. Ilikuwa ni kazi ngumu ambayo aliamini kwamba asingeweza kuifanya hata kidogo lakini kitu cha kushangaza kabisa ambacho hata yeye kilimwachia maswali ni kwa namna ambavyo alipanda na kuingia darini, akaurudishia mlango ule wa dari.
Ndani kulikuwa na giza, hakuwa na simu, hakuwa na kitu chochote kile ambacho kingemfanya kumulika mule ndani lakini hilo halikumfanya kubaki mahali pale, kwa kutumia magoti yake akaanza kusonga mbele, sehemu ambayo aliamini kulikuwa na mlango mwingine.
Humo darini, alisikia milio ya panya, hakuoga hata kidogo, kitu alichokuwa akikimbia kilikuwa ni hatari hata zaidi ya panya aliokuwa akiwasikia. Baada ya dakika mbili akafika katika mlango mwingine wa dari na kuufungua.
“Mungu nisaidie,” alisema huku akiangalia ndani ya chumba hicho.
Alisikia sauti za watu wakiongea bafuni kwa furaha, hakutaka kujiuliza kuhusu watu hao, akahisi kabisa kwamba walikuwa wapenzi waliokwenda kuyafurahia maisha yao na muda huo walikuwa wakioga tayari kwa kuondoka.
Bahati ilikuwa upande wake kwani pale kulipokuwa na mlango wa dari kulikuwa na kitanda, haraka sana akaruka mpaka juu ya kitanda.
Akaondoka na kuufuata mlango, akaufungua na kuanza kuangalia nje. Alipoona koridoni hakuna mtu, hakutaka kusubiri, hara sana akatoka na kuelekea nyuma ya gesti hiyo na kuanza kukimbia.
Mule ndani, Tim aliendelea kutambaa ndani ya dari na kufanikiwa kuuona mlango wa kushukua katika chumba kingine. Haraka sana akaufuata, haukuwa umefungwa hivyo akarukia ndani ya chumba hicho.
“She was passing through this room,” (amepitia chumba hiki) alisema Tim na kuufungua mlango na kutoka ndani.
Kichwa chake kilimwambia kwamba msichana huyo alikuwa ameondoka kupitia katika mlango wa nyuma na hivyo kuanza kukimbilia huko.
Alichanganyikiwa, msichana huyo alikuwa mtu muhimu mno, aliwafanya kufika nchini Kenya, wakatoroka mpaka Tanzania na walikuwa wamelipwa kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya kuhakikisha mpenzi wa msichana huyo, Bruno haondoki kuelekea nchini Marekani.
Kule nje aliwakuta watu wakiwa wamepigwa na taharuki, kilichokuja kichwani mwake ni kwamba walimuona Sharifa akiwa amekimbia na hawakujua sababu iliyomfanya kukimbia na ndiyo maana walikuwa kwenye hali hiyo.
Akaanza kuelekea katika njia iliyokuwa na watu wengi waliokuwa wamesimama kwa kuamini kwamba msichana huyo alipitia njia hiyo. Watu wote wakaanza kumwangalia na yeye, ni kweli walimuona msichana mmoja akiwa amekimbia lakini ghafla, baada ya sekunde kadhaa wakamuona mwanaume wa Kizungu naye akikimbia kuelekea kule alipokimbilia mwanamke yule.
“Jamani! Kuna nini tena?” aliuliza jamaa mmoja aliyekuwa amevaa msuli kama mtu aliyekuwa na busha.
“Hata mimi nashangaa! Hawa watoto wetu siku hizi wana visa sana, utakuta huyo Mzungu kamtoa Instagram halafu anamkimbia,” alisema mzee mwingine.
Tim alikimbia mpaka katika barabara kuu kabisa lakini hakuweza kumuona Sharifa. Alichanganyikiwa, kwa wakati huo msichana huyo alikuwa muhimu kuliko kitu chochote kile.
Akamtafuta na alipoona hajafanikiwa, akarudi kule gesti na kuwaambia wenzake kile kilichotokea. Kila mmoja alichanganyikiwa, kitendo cha kumkosa msichana huyo kilimaanisha kwamba Bruno angekwenda nchini Marekani na kuweka ushahidi juu ya kile kilichokuwa kimetokea.
“Ni lazima tuondoke kurudi Marekani haraka sana,” alisema Tim huku akiwaangalia wenzake, yeye alionyesha kuchanganyikiwa zaidi ya wenzake.
“Tukiulizwa?”
“Tunakwenda kimyakimya!”
“Halafu?”
“Huyu mtu tutamvizia uwanja wa ndege, najua tutajua siku ambayo atakwenda nchini Marekani, nadhani hapo ndipo tutakapofanya utekaji hukohuko mbele ya safari! Mnaonaje?” alisema na kuuliza.
“Linaingia akilini! Hakuna kuchelewa, kama vipi kesho tuondokeni,” alisema Kelly.
Hivyo ndivyo walivyokubaliana, hakukuwa na sababu ya kuendelea kubaki nchini Kenya na wakati kulikuwa na kazi kubwa ambayo walitakiwa kuifanya haraka iwezekanavyo.
Usiku huohuo wakaondoka na kuelekea katika hoteli ya kifahari ya Jumanji iliyokuwa Tanga Mjini na kuchukua vyumba hapo. Siku iliyofuata, wakapanda ndege na kuelekea Dar es Salaam ambapo huko wakaunganisha mpaka nchini Marekani.
Ndani ya ndege kila mmoja alikuwa akifikiria lake, mbele yao kulionekana kuwa na kazi kubwa lakini ilikuwa ni lazima kuhakikisha wanaikamilisha kwa haraka sana.
Hawakutaka kuzungumza mambo mengi kuhusu jambo hilo ila walipanga kuzungumzia zaidi mara baada ya kufika nchini humo.
Baada ya saa ishirini na tano, wakaingia nchini humo. Wakafikia hotelini, hawakutaka kuwasiliana na Maxwell, walitaka kukamilisha kila kitu haraka sana pasipo mwanaume huyo kufahamu jambo lolote lile.
Wakajipanga na baada ya siku tatu tangu wafike nchini Marekani wakapata taarifa kwamba Bruno alikuwa njiani akielekea nchini Marekani. Kwa kuwa walitakiwa kukamilisha mpango wao haraka sana, wakajipanga kwa kwenda uwanja wa ndege na kufanya uchunguzi ili wagundue ni ndege ipi ambayo ingemfikisha hapo nchini Marekani.
Wakapewa taarifa kwamba Bruno alipanda ndege ya Shirika la American Airlines na angeingia mahali hapo majira ya saa 05:43 usiku, hivyo walitakiwa kusubiri.
***
Gilbert na wenzake waliingia nchini Tanzania katika jiji la Tanga na kuanza kufanya upelelezi kugundua kile kilichokuwa kikiendelea. Walianza kuzunguka katika vituo vya polisi kwa lengo la kupata ukweli juu ya kile kilichokuwa kikiendelea.
Huko, wakaambiwa kwamba hakukuwa na taarifa yoyote ile juu ya mtu waliyekuwa wakimtafuta lakini kama wangewapa muda, basi bila shaka wangejua kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Japokuwa walikuwa katika kituo kikuu cha Tanga, wakaondoka na kuelekea katika vituo vingine vidogo, walikuwa na uhakika kwamba kama Sharifa alikuwa amepelekwa nchini humo basi ilikuwa ni lazima kupatikana hata kama kungetokea jambo gani.
Huko, wakapewa taarifa kuhusu Wazungu waliokuwa wamefika hapo Tanga na kuchukua chumba katika gesti moja ya uchochoroni ambapo huko walionekana wakiwa na mwanamke mmoja kutoka nchini Ghana.
“Mwanamke kutoka nchini Ghana?” aliuliza Gilbert.
“Ndiyo!”
“Ulimuona huyo mwanamke?”
“Hapana! Ila tuliambiwa na mwenye gesti kwamba walikuwa watalii,” alisema polisi aliyekuwa akijibu maswali kwa niaba ya mkuu wa kituo ambaye hakuwa mahali hapo.
Hapo hakukuonekana kuwa msaada tena, wakahisi kabisa kwamba watu hao ambao waliambiwa kuhusu stori zao na kwamba walikuwa na mwanamke kutoka nchini Ghana iliwezekana kabisa wakawa watu waliokuwa wakiwatafuta, wakaelekea katika gesti hiyo huku wakisindikizwa na polisi, walipofika, wakaingia ndani.
Wakakutana na mhudumu na kumuuliza kuhusu Wazungu hao, aliwaambia kwamba walikuwa ndani hivyo kwenda katika chumba walichokuwa wamechukua huku Gilbert na wenzake wakiwa na bastola mikononi mwao kwa ajili ya jambo lolote baya lile ambalo lingetokea huko.
Walipokifikia chumba, wakaufungua mlango na kuingia ndani huku wakiwa na bastola zao. Walipofika, hakukuwa na mtu yeyote yule, Wazungu wale ambao waliambiwa kwamba walikuwa humo na mwanamke mmoja, hakukuwa na yeyote yule, chumba kilikuwa kitupu kabisa.
“Wapo wapi?” aliuliza polisi.
“Mmh! Walikuwa humu! Sijui wapo wapi!” alisema jamaa mwenye gesti.
Wakatoka kwa kuhisi kwamba watu hao walikuwa wamekwenda sehemu fulani hivyo walitakiwa kuwawahi. Nje, kila kona hawakufanikiwa kuwaona watu hao zaidi ya wananchi kuwashangaa tu kwani kwa tukio lililokuwa likitokea siku hiyo kila mtu lilimshangaza kwani haikuwa na kawaida kwa Wazungu kuwa katika hali kama waliyokuwa wale wa mwanzo na hata hao wa kipindi hicho.
“Wametoroka! Wamekwenda naye wapi?” aliuliza Gilbert, kwa kumwangalia tu usoni alionekana kuwa na hasira kupita kawaida.

Je, nini kitaendelea?
 
BRUNO THE FISHERMAN


Sharifa alikuwa akikimbia huku akiangalia nyuma, kila mtu aliyekuwa akipishana naye alimshangaa, hawakujua kitu kilichokuwa kimetokea mpaka msichana huyo kukimbia huku akionekana kuwa na hofu kubwa.
Alikimbia mpaka alipofika mahali kulipokuwa na nyumba nyingi zilizokuwa milango wazi, hakutaka kuendelea kukimbia tu kwa kuona kwamba angekamatwa kwa kuwa hakuwa na kasi, hivyo akaingia ndani ya nyumba moja na kuomba msaada.
Watu walikuwa vyumbani mwake, wakatoka na kumwangalia Sharifa aliyekuwa ukumbini, aliwaambia watu hao kwamba alihitaji msaada kwa kuwa alikuwa akikimbizwa.
Wakati akiwa hapo ukumbini, akamuona Tim akipita nje kwa kasi huku akikimbia, Sharifa akajificha kwani hakutaka kuonekana na mwanaume huyo. Watu wote wakabaki wakimshangaa, kwao, alionekana kama mtu aliyekuwa na matatizo fulani, yaani kama changudoa aliyemkimbia mteja gesti.
“Bibie vipi?” aliuliza mwanamke mmoja.
“Kuna mtu ananikimbiza anataka kuniua,” alisema Sharifa huku akiangalia huku na kule, kwa kifupi alikuwa na wasiwasi.
Kwa lafudhi yake tu, kwa jinsi alivyokiongea Kiswahili chake hakukuwa na swali kwamba msichana huyo alikuwa Mkenya. Mwanamke mmoja akamchukua na kumuingiza chumbani mwake na kumuuliza tatizo alilokuwanalo ambapo akaanza kumwambia kila kitu kilichotokea.
Alishangaa, hakuamini kama kweli kungekuwa na watu ambao wangetoka nchini Marekani mpaka Kenya kwa lengo la kumteka mtu fulani, haikumuingia akilini, wakati mwingine aliona kama alikuwa akidanganywa na msichana huyo lakini akaamua kukubaliana naye.
“Nikusaidie nini?” aliuliza mwanamke huyo baada ya kusikiliza maneno ya Sharifa.
“Nataka kuwasiliana na mume wangu! Naomba unisaidie,” alisema.
Hilo halikuwa tatizo hata kidogo, akampa simu na msichana huyo kumpigia Bruno aliyekuwa nchini Kenya, baada ya sekunde kadhaa alikuwa akiongea naye.
Alimwambia mahali alipokuwa, Bruno aliposikia hivyo, alichanganyikiwa, hakuamini kama mpenzi wake alitoroka mikononi mwa watu hao na hivyo kuanza safari ya kuelekea Tanga.
Hakuwa akienda peke yake, aliwasiliana na polisi na kuwaambia kila kitu kilichotokea kwamba mpenzi wake alikuwa salama kabisa nchini Kenya hivyo alitakiwa kwenda huko na kumchukua.
Njiani, Bruno alikuwa na presha kubwa, moyo wake ulikuwa umekwishakata tamaa na alihisi kabisa kwamba huo ungekuwa mwisho wa kumuona mpenzi wake huyo akiwa mzima, kitendo cha kumwambia kwamba aliwatoroka watu wale kilimfanya kuwa na furaha kupita kawaida.
“Ila kawatoroka kweli au wanamtumia ili kunipata mimi?” alijiuliza Bruno, upande wake mwingine ulionekana kuwa na wasiwasi.
“Haiwezekani! Kama ingekuwa wanamtumia, wangemwambia aniambie niende peke yangu,” alijijibu.
Polisi hao wa Kenya walichokifanya ni kuwasiliana na polisi wa Tanzania kupitia Interpol na kuwaambia kile kilichokuwa kikiendelea.
Wao, yaani polisi wa Tanzania walitakiwa kwenda mahali alipokuwa Sharifa na kumchukua lakini baada ya Bruno kuambiwa hivyo, hakutaka kabisa hilo litokee, alichohitaji ni kwenda yeye mwenye mpaka alipokuwa mpenzi wake na kumchukua.
Baada ya saa kadhaa, wakafika Tanga. Akampigia simu Sharifa ambaye alimpa mwenyeji na kumuelekeza mahali nyumba yake ilipokuwa. Kutoka hapo walipokuwa mpaka kulipokuwa na nyumba hiyo hakukuwa mbali sana kwani ni mwendo wa dakika ishirini kwa gari wakawa wamekwishafika.
Wakamkuta mwenye nyumba nje, wakamfuata na yeye kuanza kuwapeleka ndani ambapo huko Bruno akakutana na Sharifa, kwa furaha aliyokuwanayo, akamsogelea na kumkumbatia.
“Walitaka kuniua,” alisema Sharifa huku akilia, alikuwa amekumbatiana na Bruno tu.
“Wasingeweza. Nipo pamoja na wewe, kukumaliza wewe inamaanisha walihitaji vita na mimi,” alisema Bruno huku akiwa amemkumbatia mpenzi wake huyo.
Wakamchukua na kuanza safari ya kurudi Mombasa. Njiani, kila mmoja alionekana kuwa na furaha, mioyo yao ilifurahia kuungana tena kwa mara nyingine tena.
Baada ya saa kadhaa wakafika Mombasa ambapo huko, kitu cha kwanza kilikuwa ni kwa Bruno kuwasiliana na akina Gilbert na kuwaambia kile kilichotokea na hivyo kukutana na kuzungumza.
Wao wenyewe walifurahi lakini bado walionekana kuwa na hofu na usalama wa maisha ya Bruno. Walijua kabisa kwamba kama lengo la kumteka Sharifa lilikuwa ni kuhakikisha kwamba Bruno haendi nchini Marekani basi ingekuwa ni lazima watu hao wafanye jambo lolote lile kuhakikisha mwanaume huyo hatoi ushahidi katika kesi hiyo.
“This is not the end,” (huu si mwisho) alisema Gilbert huku akimwangalia Bruno.
“What do you mean,” (unamaanisha nini?)
“They are going to look for you,” (watakutafuta)
“And kill me?” (na kuniua?)
“That what they want. Bruno, we have to take you to USA by ourselves,” (Hicho ndicho wanachokitaka. Bruno, tutakupeleka Marekani sisi wenyewe) alisema Gilbert.
Hicho walichokifanya, baada ya siku mbili wakaanza safari ya kuelekea nchini Marekani. Kwa kuwa walikuwa na uhitaji wa kuwapata watu hao, hawakutaka kujionyesha, ilikuwa ni lazima na wao wajifanye abiria ili iwe rahisi kwao kufanikiwa kwa kile walichokuwa wakikitaka.
Ndege ilichukua saa zaidi ya ishirini angani na ndipo ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK. Abiria wakaanza kuteremka akiwemo Bruno. Walitembea kwa mwendo wa taratibu kuufuata mlango uliokuwa ukielekea katika jengo la uwanja huo.
Hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, alijiamini mpaka alipochukua begi lake lililokuwa limechunguzwa na kuanza kutoka nje ya jengo lile.
Alipofika, harakaharaka mwanaume mmoja akamfuata na kumwambia kwamba alikuwa dereva teksi ambaye alitumwa na mwanaume aliyeitwa Todd kwa lengo la kumpokea.
“Alikuagiza?” aliuliza Bruno.
“Ndiyo! Au nimekuchanganya?”
“Ni mimi! Nilidhani ungekuwa na bango lililokuwa na jina langu,” alisema Bruno huku akiachia tabasamu pana.
“Hapana! Alinionyeshea picha yako. Karibu,” alisema mwanaume huyo huku akimpa mkono, wakaanza kuifuata teksi iliyokuwa maeneo hayo.
Bruno akaingia ndani ya teksi ile, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, aliamini maneno aliyoongea mwanaume yule kwamba alitumwa na mzee Todd kwenda kumchukua hapo uwanjani.
“Ni mara yako ya kwanza kufika hapa?” aliuliza mwanaume huyo.
“Ndiyo! Ni mara yangu ya kwanza, nimekuja kutoa ushahidi kwenye kesi yake kisha nitarudi Kenya,” alijibu huku tabasamu likiwa usoni mwake.
“Ooh! Sawasawa! Nadhani atafurahi sana akisikia umefika salama,” alisema dereva, safari ikawa inaendelea kama kawaida.
***
Tim na wenzake wakajipanga vilivyo, ilikuwa ni lazima Bruno atekwe uwanjani na kupelekwa sehemu kwa lengo la kuuawa na kisha mwili wao kuutupa.
Hilo likapangwa na hivyo kuanza kumtafuta dereva ambaye walimwambia kuwa ingekuwa vizuri kama angekwenda uwanjani hapo na kumchukua Bruno na kujifanya kwamba alikuwa ametumwa.
Siku ilipofika, Tim akaenda na dereva huyo mpaka uwanja wa ndege, akachukua namba yake ya simu na wakati abiria wanatoka ndani ya jengo la uwanja huo, alikuwa akizungumza naye na alipomuona Bruno, akamwambia kwamba alikuwa mwenyewe na ndipo dereva huyo alipoanza kumfuata.
Alifuatilia kila hatua mpaka alipoingia ndani ya teksi na kuanza safari ya kuondoka mahali hapo. Mipango yao ilikuwa ni kwenda katika jengo moja lililokuwa hapohapo New York.
Hawakuchukua muda mrefu, wakafika, dereva akasimamisha gari, hapohapo akateremka na Kelly na mwenzake, Adson kutokea na kuanza kuifuata teksi ile, walipoifikia, wakaufungua mlango na kumtoa kwenye gari.
“What is going on?” (nini kinaendelea?) aliuliza Bruno huku akionekana kushangaa.
“Shiiiiiiiiii!” alimnyamazisha Kelly huku akiwa na kipande cha nondo mkononi mwake.
Wakambeba na kuondoka naye, wakamuingiza ndani ya jumba hilo, kitu kilichokuwa kikitakiwa kufanywa haraka ni kumuua na kisha kuuacha mwili wake hapohapo na wao kuondoka.
“Don’t kill me, mplease,” (tafadhai, msiniue) alisema Bruno lakini hakukuwa na mtu aliyejali, kila mmoja alichokuwa akikihitaji mahali hapo ni kuona mwanaume huyo akifa haraka sana.

Je, nini kitaendelea?
tUKUTANE jUMAMOSI hAPAHAPA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom